Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,962
Mtunzi
Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01
Ukimya ulitawala ndani ya Jiji la Dar es Salaam, yale magari yaliyokuwa yakipita kwa kasi katika barabara nyingi jiji humu yalikata kabisa.
Watu wengi waliokuwa wakienda huku na kule hawakuwa wakionekana kama nyakati za mchana.
Kila kitu kilibadilika usiku huo, katika mitaa mingi ya Kariakoo hakukuwa na watu kabisa, ilikuwa ni vigumu kuamini kama nyakati za mchana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakipita huku na kule.
Katika muda huo, nilikuwa katika Mtaa wa Kongo. Hapo, ndipo kulipokuwa na maisha yangu, niliyaendesha humo, si kama mfanyabiashara bali nilifanya kazi hapo katika kusafisha barabara kila siku usiku.
Kwa jina ninaitwa Edward Francis. Nimeamua kukusimulia maisha yangu yalivyokuwa, najua kuna watu wanamuona mtu fulani amefanikiwa halafu wakahisi kabisa alitoka kwenye familia ya kitajiri, leo watu wanavyoniona nina nyumba kubwa, magari ya kifahari na hata biashara nyingi wanadhani kwamba nilizaliwa kwenye familia ya kitajiri, ndugu yangu, nilizaliwa kwenye familia ya kimasikini tena inawezekana zaidi ya hiyo yako, nilihangaika mno mpaka kufika hapa nilipo.
Maisha yangu ni simulizi nzuri kwako, kuna mambo mengi mazuri niliyoyafanya, ila kumbuka kwamba kuna mengi mabaya ambayo niliyafanya pia. Mabilionea wengi wa leo wakikusimulia maisha yao, watachambua, watakwambia yale mazuri lakini mabaya yatabaki moyoni mwao.
Ninaamua kuyafungukia maisha yangu leo, nitakwambia kila kitu, najua kuna watu wengi watajifunza kupitia maisha yangu.
Kuna mafunzo machache sana yanapatikana katika yale mambo mazuri uliyowahi kuyafanya ila kuna mafunzo makubwa yanayopatikana kwenye magumu na dhambi nyingi ulizopitia.
Mishemishe zangu zilikuwa Kariakoo, sikuwa na mahali pa kuishi, wazazi wangu walifariki miaka mingi iliyopita, sikuwahi kuziona sura zao, walifananaje?
Walikuwa wembambamba ama wanene? Weusi ama weupe? Kwa kweli sijui kitu chochote kile kuhusu wao.
Hapo Kariakoo nilikuwa mkimya, sikuwa muongeaji sana, nilijua kufanya kazi zangu nyingine kama kawaida.
Nakumbuka kila siku nilipokea kiasi cha shilingi elfu tano kila nilipokuwa nikimaliza kufanya usafi.
Nyemo Chilongani
Sehemu ya 01
Ukimya ulitawala ndani ya Jiji la Dar es Salaam, yale magari yaliyokuwa yakipita kwa kasi katika barabara nyingi jiji humu yalikata kabisa.
Watu wengi waliokuwa wakienda huku na kule hawakuwa wakionekana kama nyakati za mchana.
Kila kitu kilibadilika usiku huo, katika mitaa mingi ya Kariakoo hakukuwa na watu kabisa, ilikuwa ni vigumu kuamini kama nyakati za mchana kulikuwa na watu wengi waliokuwa wakipita huku na kule.
Katika muda huo, nilikuwa katika Mtaa wa Kongo. Hapo, ndipo kulipokuwa na maisha yangu, niliyaendesha humo, si kama mfanyabiashara bali nilifanya kazi hapo katika kusafisha barabara kila siku usiku.
Kwa jina ninaitwa Edward Francis. Nimeamua kukusimulia maisha yangu yalivyokuwa, najua kuna watu wanamuona mtu fulani amefanikiwa halafu wakahisi kabisa alitoka kwenye familia ya kitajiri, leo watu wanavyoniona nina nyumba kubwa, magari ya kifahari na hata biashara nyingi wanadhani kwamba nilizaliwa kwenye familia ya kitajiri, ndugu yangu, nilizaliwa kwenye familia ya kimasikini tena inawezekana zaidi ya hiyo yako, nilihangaika mno mpaka kufika hapa nilipo.
Maisha yangu ni simulizi nzuri kwako, kuna mambo mengi mazuri niliyoyafanya, ila kumbuka kwamba kuna mengi mabaya ambayo niliyafanya pia. Mabilionea wengi wa leo wakikusimulia maisha yao, watachambua, watakwambia yale mazuri lakini mabaya yatabaki moyoni mwao.
Ninaamua kuyafungukia maisha yangu leo, nitakwambia kila kitu, najua kuna watu wengi watajifunza kupitia maisha yangu.
Kuna mafunzo machache sana yanapatikana katika yale mambo mazuri uliyowahi kuyafanya ila kuna mafunzo makubwa yanayopatikana kwenye magumu na dhambi nyingi ulizopitia.
Mishemishe zangu zilikuwa Kariakoo, sikuwa na mahali pa kuishi, wazazi wangu walifariki miaka mingi iliyopita, sikuwahi kuziona sura zao, walifananaje?
Walikuwa wembambamba ama wanene? Weusi ama weupe? Kwa kweli sijui kitu chochote kile kuhusu wao.
Hapo Kariakoo nilikuwa mkimya, sikuwa muongeaji sana, nilijua kufanya kazi zangu nyingine kama kawaida.
Nakumbuka kila siku nilipokea kiasi cha shilingi elfu tano kila nilipokuwa nikimaliza kufanya usafi.