Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,870
- Thread starter
- #441
SEHEMU YA 63
Nikacheka sana, mimi huwa siamini kama kuna mwanamke anakuwa hatari kama mwanaume, na kama yeye alitamba sana kwamba alikuwa hatari, nilitakiwa kumuachia nione ukali wake ulikuwa wapi.
Nawajua watoto wa kike, huwa hawana pumzi za kutosha. Wapo hivyo, tena wote duniani. Katika kipindi cha dakika kumi za mwanzo, wanaanza kucheza kwa kasi sana ila baada ya hapo pumzi inakata na kukwambia nimechoka.
Hapo ndipo zamu yako inapokuja na kumwambia kwamba hutakiwi kuchoka, humu hujaja kulala, umekuja kufanya kazi tu.
“Hivi una pumzi kweli?” niliamua kumuuliza kwa meseji.
“Kwa nini umeniuliza hivyo?”
“Ninataka kujua. Una pumzi?” nilimuuliza.
“Utaona kesho. Nataka kukuonyesha kwamba kungwi wangu hakufanya kazi ya bure,” aliniandikia.
Huwa sinaga presha kabisa, baada ya kuniambia hivyo, nikachukua cd yangu ya Kamasutra na kuanza kuangalia, unajua alinitisha sana, nilihisi kwamba alikuwa mtu hatari.
Nilichukua mafunzo kabisa, sikutaka kupitwa na chochote kile, baada ya kumaliza kutazama, nikanywa maziwa na karanga nyingi nikijiandaa kwa ajili ya siku inayofuata.
Kweli bwana, siku hiyo ilipofika, Halima mwenyewe akanipigia simu na kuniambia nipange tuonanie wapi.
Sijui alikuwa akinitega! Nina kwangu, nimenunua nyumba, inakuwaje twende kwenye nyumba ya wageni?
Aje humuhumu, kwanza ndipo kwenye vifaa vyangu.
“Njoo kwangu!” nilimwambia.”
“Kwako?”
“Yaap! Wewe njoo, usiogope, timu nzuri inacheza uwanja wowote ule,” nilimwambia.
“Sawa! Ngoja nijiandae.”
Hii ni kwa wanaume wote. Kitu cha msingi ni kutafuta pesa. Achana na kunyanyua vyuma, haisaidii hata kidogo, utaonekana kama mlinzi tu lakini pesa ndiyo kila kitu.
Wanawake wanapenda pesa, wanapenda kutunzwa, wanapenda kununuliwa zawadi za kila aina na ndiyo maana kwa mtu kama Halima hakuwa akinisumbua hata kidogo kwa kuwa alijua kabisa nilikuwa na pesa.
Nikafungua friji na kuangalia vinywaji, vilikuwa vimepungua sana na hivyo nilitakiwa kuongeza kidogo.
Nikatoka na kwenda kwenye duka moja la vinywaji lililokuwa Sinza Kijiweni.
Nikacheka sana, mimi huwa siamini kama kuna mwanamke anakuwa hatari kama mwanaume, na kama yeye alitamba sana kwamba alikuwa hatari, nilitakiwa kumuachia nione ukali wake ulikuwa wapi.
Nawajua watoto wa kike, huwa hawana pumzi za kutosha. Wapo hivyo, tena wote duniani. Katika kipindi cha dakika kumi za mwanzo, wanaanza kucheza kwa kasi sana ila baada ya hapo pumzi inakata na kukwambia nimechoka.
Hapo ndipo zamu yako inapokuja na kumwambia kwamba hutakiwi kuchoka, humu hujaja kulala, umekuja kufanya kazi tu.
“Hivi una pumzi kweli?” niliamua kumuuliza kwa meseji.
“Kwa nini umeniuliza hivyo?”
“Ninataka kujua. Una pumzi?” nilimuuliza.
“Utaona kesho. Nataka kukuonyesha kwamba kungwi wangu hakufanya kazi ya bure,” aliniandikia.
Huwa sinaga presha kabisa, baada ya kuniambia hivyo, nikachukua cd yangu ya Kamasutra na kuanza kuangalia, unajua alinitisha sana, nilihisi kwamba alikuwa mtu hatari.
Nilichukua mafunzo kabisa, sikutaka kupitwa na chochote kile, baada ya kumaliza kutazama, nikanywa maziwa na karanga nyingi nikijiandaa kwa ajili ya siku inayofuata.
Kweli bwana, siku hiyo ilipofika, Halima mwenyewe akanipigia simu na kuniambia nipange tuonanie wapi.
Sijui alikuwa akinitega! Nina kwangu, nimenunua nyumba, inakuwaje twende kwenye nyumba ya wageni?
Aje humuhumu, kwanza ndipo kwenye vifaa vyangu.
“Njoo kwangu!” nilimwambia.”
“Kwako?”
“Yaap! Wewe njoo, usiogope, timu nzuri inacheza uwanja wowote ule,” nilimwambia.
“Sawa! Ngoja nijiandae.”
Hii ni kwa wanaume wote. Kitu cha msingi ni kutafuta pesa. Achana na kunyanyua vyuma, haisaidii hata kidogo, utaonekana kama mlinzi tu lakini pesa ndiyo kila kitu.
Wanawake wanapenda pesa, wanapenda kutunzwa, wanapenda kununuliwa zawadi za kila aina na ndiyo maana kwa mtu kama Halima hakuwa akinisumbua hata kidogo kwa kuwa alijua kabisa nilikuwa na pesa.
Nikafungua friji na kuangalia vinywaji, vilikuwa vimepungua sana na hivyo nilitakiwa kuongeza kidogo.
Nikatoka na kwenda kwenye duka moja la vinywaji lililokuwa Sinza Kijiweni.
