SEHEMU YA 49
Tukaondoka na kuelekea hotelini. Nilijiona Mfalme Mswati. Niliona hotelini mbali, wakati mwingine nilitamani hata kupiga picha na kuwaonyeshea Watanzania wote kwamba si mnaona sasa nilivyo? Si mnaona jinsi ninavyoondoka na watoto wawili?
Tulipofika hotelini tukaingia, sikutaka kuchelewa, mambo yakaanza mara moja huku nikionekana kuwa na kasi kama Hussein Bolt.
Nilitaka kuwaonyeshea kwamba hela ya mwanaume haiendi bure, ilikuwa ni lazima wailipie na ndicho kilichotokea. Ilichukua masaa matatu, wote wakawa hoi.
“Wewe mtu balaa!” aliniambia Doreen huku akiniangalia kwa mshangao, pamoja na mambo yake machafu lakini alikiri kwamba hakuwahi kukutana na mimi.
“Balaa langu lipi sasa?”
“Utadhani siyo mwanaume wa Dar!” alidakia Amanda.
“Kwa hiyo mnaniambiaje? Mmeshakula laki moja yangu na huduma mliyonipa ni ya shilingi elfu sitini tu, kuna ya arobaini imebaki huko kwenu,” nilimwambia.
“We kaka utatuua!”
“Basi nawaongezeni, mimi mpaka niridhike!”
“Kwani hujaridhika tu?”
“Bado hata kidogo!” niliwaambia.
Niliongea kama masihara lakini nilimaanisha, ni masaa matatu lakini ilionekana kama nusu saa kwangu. Filimbi ikapigwa tena na wachezaji kuingia uwanjani.
Watu walikuwa wakihema kama mbwa, mpira wa siku hiyo ilikuwa balaa, viungo walikuwa wakimiliki mpira kwa kasi kubwa, kila ulipokuwa ukitoka, mpira mwingine ulirushwa ndani kuonyesha kwamba siku hiyo ilikuwa ni ya kazi tu, wachezaji wasiokuwa na uwezo wa kumaliza dakika tisini hawakutakiwa kucheza mechi hiyo.
Nakumbuka tuliingia majira ya saa kumi jioni na waliondoka pale saa tano usiku, niliwang’ang’aniza walale, wakakataa kabisa.
“Nitawapeni milioni moja kila mtu!”
“Hapana! Hata ukinipa milioni hamsini silali! Mwanaume gani hutosheki!” aliniambia Doreen.
“Jamaniiiiiiii....”
“Aku! Tena usiniguse,” aliniambia Doreen manake alishaona mkono wangu ulianza kumletea shobo.
Nikaachana nao, wakaondoka na mimi kulala hotelini.
Asubuhi ilipofika, baba yake na Zamaradi akaniambia kwamba siku hiyo ndiyo walitaka kuhama hivyo nilitakiwa kuonana naye.