Simulizi: Nyuma ya mlango wa adui

Simulizi: Nyuma ya mlango wa adui

Kuhusu yajayo, kule kwa mapacha hamna jipyaaaa, tuliosoma ile KAZI ya "Asali haitiwi kidole" tayari Kuna mwanga tunapataa.
Kipengele ni kwa wanafamilia UMD๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚Mungu saidia chama langu.
๐Ÿ˜…๐Ÿ˜… Team songoro wapo wapi maana zamu yao sasa
 
๐Ÿ˜…๐Ÿ˜… Team songoro wapo wapi maana zamu yao sasa
Achana na Sangoro๐Ÿ˜ƒ,
UMD ndyo habari ya mjini, yaani tumewavuruga polisi mjini,
Sasahivi tunatamani kusipambazuke maana siyo kwa huo msako unaoendelea๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ majamaa hawataniwi ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿคฃ
 
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA SITA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA TANO:- Wakati hayo yanaendelea mara Deus akasikia simu yake inaita, ni ile ambayo anawasiliana na baba yake, akaitazama toka mezani akaona kuwa mpigaji ni baba yake, akaipotezea na kurudisha macho kwa Veronica, ambae hakutamani hata kidogo Deus aache kile alichokuwa anakifanya kwenye mwili wake, mara kwa bahati mbaya au mzuri macho ya Deus yanapita kwenye screen ndogo ya nchi 32 yenye kujigawa mara nne, ambayo katika kipande kilichoandikwa cam 1 kilionyesha mwanga wa magari yaliyokuwa yanakuja upande ule. โ€ฆโ€ฆ. ENDELEAโ€ฆ


Deus alitazama kwa umakini camera namba moja, akagundua kuwa yalikuwa magari mawili, lakini sio ya polisi wala sio ya UMD ambayo aliyakuta pale Makabe, yalikuwa ni mengine kabisa, ambayo ni Toyota prado na Nissan, yaliyokuwa yanakuja taratibu upande iliko nyumba yake, na kwa kawaida camera za ulinzi zilizofungwa katika nyumba hii hasa zile za nje, zina uwezo wa kuona mita mia nane kwa mchana na usiku mita mia nne, japo kwa mita hizo usingeweza kutambua kitu halisi, sasa basi kwa muonekano wa magari yale na jinsi alivyo yatambua, ni kwamba yalikuwa ndani ya mita mia moja, โ€œwakifika mita hamsini hawana bahatiโ€ alisema Deus, huku anamuweka sawa Veronica na kumshika ile nguo ya chini kisha akaanza kuishusha taratibu, โ€œjamani mchoraji usiwe na haraka, si uniambie kama utanioaโ€ alisema Veronica kwa sauti ya ulegevu huku anashindwa kuzuia mkono wa Deus uliokuwa unaendelea kushusha ile truck aliyoivaa, ambayo sasa ilisha kata nusu ya mapaja na kuacha wazi viungo muhimu, japo kitumbua kilikuwa kimehifadhiwa ndani ya bikini iliyo lowa chepe chepe usawa wa kitumbua, โ€œumesahau kama tuliweka ahadi kuwa endapo JJ atazingua nitakuoa mimiโ€ alikumbusha Deus huku anaacha kushusha ile truck na kulaza mkono kwenye bumunda na kurudia tena kamchezo kama kale kamwanzo.


Veronica akajikuta anaachia kicheko cha kivivu halafu kitamu, โ€œsawa lakini mchoraj inabidi unifundishe taratibu, mwenzakoโ€ฆโ€ฆ mwenzio โ€ฆโ€ฆ. Sijawahiโ€ alisema Veronica kwa sauti ambayo sio tu kuzidiwa na hamu ya dudu iliyosababishwa na mitekenyo kwenye kunde, Deus alitabasamu kidogo, โ€œusiogope pacha, nakuahidi utafurahiโ€ alisema Deus kwa sauti nzito huku anaendelea kuchezea eneo la shambani kwa bibi, Wakati huo simu bado ilikuwa inaendelea kuita na mpigaji akiwa ni baba yake, je alikuwa anataka kumueleza chochote juu ya ujio wa watu hawa, au?, lakini kijana huyu mwenye kuelemewa na kiu kali ya kitumbua, anaachana na simu nakuendelea kupekecha sehemu ile yemye shamba la kunde, huku mkono mmoja ukiendelea kushusha ile nguo ya mwadada huyu mrembo, ambae alizidi kujiweka vizuri ili kumpa nafasi kijana huyu, aweze kuitoa nguo hiyo.


Nadhani haitokuwa vyema kama tukiendelea kubakia nao wakati wakiwa katika hali hii, hebu tuwapishe kidogo tutarudi baadae.*********


Naaam, king Elvis akiwa amekosa usingizi kabisa, akiwaza juu ya hiki kinacho endelea, ni swala la uasi ndani ya nchi yake, jambo ambalo halikuwahi kutokea enzi za utawala wa baba yake, na hata utawala wa babu yake lilikuwa katika tetesi, sasa utawala wake ndio kipindi ambacho waasi, wamepanga kutimiza uasi wao, na kitu cha kuhuzunisha zaidi ni kwamba, zoezi la kukomesha uasi lililofanywa miaka ya nyuma, alikuzaa matunda, baada yake ni kama liliimarisha ngome ya waasi.


Wakati anawaza hayo, mara simu yake inaita, nae anaitazama na kuona kuwa mpigaji ni Major General Sixmund, anaipokea haraka, โ€œvipi Six, unahabari yoyote?โ€ aliuliza King Elvis kwa sauti iliyojaa shauku, โ€œmtukufu mfalme, kazi inaendelea vizuri na sasa tunaanza kutafuta watu walioshiriki katika kikosi maalumu cha kusaka waasi ndani ya serikali, maana kuna uwezekano kuwa baadhi yao walikiuka amri ya mfalme na kusababisha kile ambacho kilipelekea lawama kwa king Eugenโ€ ilisikika sauti ya Six akiongea kwa busara na unyeyekevu, โ€œinamaana mmeshindwa kuipata katika maktaba za kijeshi?โ€ aliuliza King Elvis kwa sauti ya mshangao, โ€œmtukufu, sehemu zote za kuhifadhia nyaraka muhimu hakuna hata nakala moja iliyosalia, inaonekana kuna mtu amefuta na kupoteza orodha hiyo kwalengo la kuondoa kumbukumbu ya watu walioshiriki msako huleโ€ alijibu Sixmund.


Hiyo ilimshtua kidogo King Elvis wa kwanza, โ€œlakini lazima kuna vyanzo vya watu ambao mnaweza kuanza nao, mfano aliekuwa kiongozi wa operation ile bwana Chitopelaโ€ alisema King Elvis, ndio mtukufu, lakini tumeona tuitafute orodha kwa njia yetu, kwasababu hatutaki kumshirikisha Chitopela kama ulivyosema tufanye uchunguzi kwa siriโ€ alisema Sixmund, na hapo King Elvis akaonekana kuelewa, โ€œsawa General, nakutumia kwenye email yako, lakini Six kumbuka hili swala ni muhimu liende sambamba na kule dar es salaam, maana mara tutakapo pata ushaidi wa wahusika moja kwa moja wakamatwe kabla silaha hazijaingia nchini na kuleta madharaโ€ alisisitiza king Elvis, ambae sasa alikuwa anainuka toka kitandani na kusogea sehemu ambayo kuna ofisi yake ya pale ndani.**********


Naaam saa sita za usiku, vyombo vya ulinzi na usalama vipo kazini, hakuna dalili ya kumaliza kazi na kwenda kulala majumbani mwao, hofu zime tanda miongoni mwa askari, hasa baada ya wenzao kushambuliwa na watu wanao hisiwa kuwa ni UMD, hakuna dalili ya kumpata Deus Nyati, ambae imesemwa ndie aliemteka Veroca James na ndie dereva wa BMW nyeusi ambae alifanya mauwaji jijini Arusha, japo nayo ilikuwa ni hofu ya pili kwa wanausalama hao, maana kupambana na kijana huyu ni sawa na kupambana na kikosi cha makomandoo.


Tukiangazia katika msako huu wa Deus Nyati, magari ya polisi yanaonekana kuzagaa kwenye barabara ya misegese kuelekea kwenye makutano ya barabara ya kisarawe na manero mango, katika msafari huu gari la akina Cheleji lilikuwa kilomita kama sita kabla ya kufika njia panda, wakiwa na magari yao matatu, wakati huo gari la mbele kabisa lilikuwa limeshafika njia panda na kusimama hapo wakiwa hawajuwli upande wa kuelekea, nao wakasimamisha magari na kuanza kuuliza kwa raia wachache ambao hukaa barabarani usiku kucha wakivizia wateja wa mkaa na bidhaa nyingine za matunda kama mafenesi na mapasheni, (passion) kwa bahati walikuwepo kama wanne hivi.


โ€œHabari zenu vijanaโ€ alisalimia Asistant inspector, aliekuwa kiongozi wa msafara ule, nzuri kamanda, poleni kwa majukumuโ€ alisema kijana mmoja alieonekana kuchangamka kidogo, โ€œasante bwana ndio majukumu yetu ya kila sikuโ€ alijibu yule polisi mwenye nyota moja, kabla hajauliza swali, โ€œeti kuna magari mawili yanayo fanana na land roverโ€ฆ.โ€ Kabla hajamaliza yule kijana mchangamfu akadakia, โ€œyale madefender mapya mapya hivi?โ€ aliuliza kijana yule, โ€œhaswaaaaa hayo hayo, yameelekea upande upi?โ€ aliuliza yule Asistant inspector, โ€œyameelekea huko Kazimzumbwiโ€ alisema yule kijana huku akionyesha upande wa manero mango.


Na hapo yule polisi akawashukuru wote kwa ujumla, kisha akarudi yalipo magari yao na kuanza kuongea kwa radio call yake, โ€œhallow vituo vyote, mimi ni 25, kuna ujumbe, mnanipataโ€ alisema yule kamanda, na hapo zikaanza kusika sauti nyingine kwenye radio zikikubali kuwa wanamsikia, โ€œueleko wa farasi wapya ni Kazi mzumbwi, narudia uelekeo wa farasi wapya ni Kazi mzumbwiโ€ hapo hapo zikaanza kusikika sauti za wengine wakisema kuwa wapo njiani wanaelekea huko waliko wao lakini ya mwisho ilikuwa ni ya amri, โ€œhallow vituo vyote, mimi Alpha, tukutane njia panda ya manero mango, narudia tukutane njia panda ya manero mango, jibu kama mumenielewaโ€ ilisema ile call ya Alpha, ambayo katika alama ya miito ni kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam, yani CP Nyambibo


Wakati huo huo, maeneo ya misegese relini, mita kama mia mbili toka barabara ya vumbi yanaonekana magari mawili ya wakina Uled Songoro wakiwa wamesimamisha magari yao kwenye njia hii ambayo licha ya uhafifu wake, lakini ni wazi kuna watu wanaitumia tena kupitisha gari, โ€œinaonyesha huku kama sio kuna watu wanaishi, basi kuna shughuri fulani zinaendeleaโ€ alisema Songoro huku wakiwa wanatazama ile njia upande ilikoelekea, kabla hawajageuza macho yao kutazama upande wa barabarani, yani walikotoka, โ€œtuwasikilizie wapite, maana lazima wengine watakuwa mbeleโ€ alisema Songoro huku yeye na mwenzake wakitazama kule barabarani ambako kutokana na giza lililokuwa limetanda ungeweza kuona taa za magari zilizokuwa zimeongozana kuelekea upande wa njia panda ya manero mango, โ€œila boss kwa uwingi huu wa magari ya polisi sidhani kama tutaweza kumsaka yule dogo bila kukutana naoโ€ alisema mmoja kati ya vijana wa Songoro.


Japo ilikuwa ni ukweli alichoongea kijana huyo, lakini Songoro aligeuza uso wake na kumkata jicho la hasira, โ€œsipendi kusikia huo ujinga tena, kwa hiyo unataka tuache kumtafuta huyu mjinga na turudhishe makalio nyumbani?โ€ aliuliza Songoro kwa sauti iliyojaa hasira, โ€œsahamani boss, sikumaanishaโ€ alisema yule kijana kwa sauti iliyojaa uoga, ni wazi anaijua tabia ya Songoro pale anapohitaji kufanya jambo lake, hataki kuonekana dhaifu kwa mtu au kitu chochote.


Yap! wakati askari polisi wengine wakiwa njia panda ya manero mango, mpaka Kazimzumbwi, huku Kibamba chama, Kamanda wa kanda maalumu ya dar es salaam, CP Nyambibo, anakutana na makamanda watatu wa mikoa ya kipolisi ya kanda maalumu ya dar es salaam, mmoja wapo akiwepo kamanda wa ilala bwana ACP Ulenje Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalumu Ilala, wanakutana njia panda ya mloganzira pale kibamba chama, huku wakiwa na magari manne yenye askari ambao walikuwa na silaha zao tayari kuwalinda kwa chochote, โ€œjamani uelekeo mpaka sasa ni njia panda ya Manero mango, huko ndiko tutaanzia msako wetuโ€ alisema kamanda Nyambibo, kisha safari ikaanza kuelekea huko, โ€œhawa mabwege sijui wapo wapi kwa sasa, ngoja niwasiliane nao, wajue kinachokuja kuwa tokeaโ€ alisema Ulenje, huku anatoa simu yake toka mfukoni,


Upande wa magharibi mwa Kisarawe, sasa tuna zungumzia misitu ya Kazi mzumbwi, kilomita chache toka kijiji cha manero mango, mita kama mia mbili toka barabarani kwenye uwanda fulani wa chini wa bonde, lenye mto wenye maji mengi, panaonekana magari mawili aina ya Land rover puma yakiwa yamegeshwa, huku mita kama hamsini toka sehemu hiyo ikionekana miili ya watu zaidi ya kumi iliyokuwa imerundikwa sehemu moja kama mifuko ya taka, vijana wanaonekana wakiosha ndani ya magari yale yaliyokuwa yanachuruzika damu kama gari la kubebea ngombe toka machinjoni, pembeni kidogo toka yalipo yale magari anaokena kanali wa zamani wa MLA Erasto Kadumya, ambae anajiita General akiwa anaongea na simu huku pembeni yake akiwa amesimama, Luten wa zamani wa MLA Enock Kafulu, waliokuwa wamesimama pembeni kidogo na yalipokuwepo magari yale


โ€œKobwe, nyie mmefika wapi, munajua kama kila kitu kimesimama tunawasubiri nyie?โ€ aliuliza Kadumya ambae ni kama aliona kikosi kina chelewa sana kufika, โ€œmkuu tunakaribia Rufiji, tuna kimbia kadiri tunavyoweza, nadhani baada ya masaa mawili tutakuwa dar es salaamโ€ ilisikika sauti ya kobwe, โ€œsikia wewe nani alikuambia mtaingia dar es salaam bila kujulikana kwamba kuna majeshi yasiyoeleweka yanaingia jijini, dar es salaam watu hawalali bwana, sasa sikiliza toka kwangu, mukifika karibu na mpakani mwisho wa soko kuna barabara inaingia upande wa kushoto, japo ni ya vumbi lakini munaweza kutembea kwa dakika arobaini na tano mpaka lisaa limoja mukawa mume shafika hapa, fanyeni hivyo tuna wasubiria nyie, na ninacho jua polisi wanatutafuta kwa shambulio tulilolifanya hapo nyumaโ€ alisistiza Kadumya, ambae kabla haja endelea akasikia simu yake inatoa mlio fulani wa kuashiria kuwa kuna simu ilikuwa inatarajia kuingia, akaitoa sikioni na kutazama, akaona ni Ulenje anapiga simu.


Moja kwa moja Kadumya akajua kuwa, kuna taarifa zinakuja na anatakiwa kuzipokea, โ€œhebu kata simu nipokee simu nyingine muhimu zaidiโ€ alisema Kadumya na upande wa pili wakakata simu na yeye akaipokea simu ya Ulenje, โ€œni kweli mupo kazimzumbwi?โ€ hilo ndilo swali la kwanza kuulizwa, โ€œndio umejuaje maana polisi tumewaacha mbali sana?โ€ aliuliza Kadumya kwa mshangao, maana aliona kuwa Ile ndiyo ilikuwa sehemu nzuri kwaajili ya kupanga majeshi yake na pengine kuweka kambi ya muda, kwa muda ambao watakuwa wakiendeleza msako, โ€œsio muhimu kuhusu nimejuaje, chamsingi ni kwamba, ondokeni haraka na muzidi kujificha, nadhani lisaa limoja baadae tutakuwa hapoโ€ alisema Ulenje na kukata simu.


Hapo kama amechanganyikiwa, Kadumya akageuka haraka yaliko yale magari, โ€œharaka sana ingieni kwenye magari, sio sehemu salama kwetuโ€ alisema Kadumya huku yeye na Kafulu wanakimbnilia kwenye magari ambayo tayari yalikuwa yamesha washwa tayari kwa kuondoka, kitendo cha kuondoka kilichukua dakika moja, tayari magari yalishaanza kuondoka kuifuata barabara kuu ya manero mango, huku wengine wakiwa wameshikilia bunduki zao kwa umakini mkubwa tayari kushambulia chochote watakacho kiona mbele yao.*******


Naaam ile bwana Six anamaliza kuongea na mfalme wa #mbogo_land, hazikupita hata sekunde tano, akaona simu yake inaanza kuita, alipoitazama alikuwa ni Captain Amos Makey, ni yule aliempatia askari na kumtuma kwenda Tanzania, akaipokea haraka na kuweka simu sikioni, โ€œAmos kuna jipya lolote?โ€ aliuliza major General Sixmund, ndiyo mkuu, kuna habari mpya za kiutendajiโ€ alijibu captain Makey, โ€œok! Unaweza kuniambiaโ€ alisema Sixmund na kutega sikio kusikiliza taarifa hiyo mpya, โ€œafande tukiwa hapa kwa bwana James Kelvin, tumegundua kuwa licha ya kwamba mtoto wa kanali Frank, yani private Deus Nyati kumuokoa bwana James, pia ndie aliemuokoa binti yake yani doctor Veronica, ambae kupatikana kwake ndio kuondoka kwetu, pia taarifa nyingine ni kwamba, Deus Nyati mpaka sasa ameshauwa UMD kadhaa, ambao idadi kamili hatujaipata, na kiingine ni kwamba, kama unamkumbuka afisa mmoja alieitwa Enock Kafulu alietoweka ghafla na kuandikwa kama mtoro jeshini, yupo huku kama UMD, na ndie alie ongoza utekaji nyara wa Veronicaโ€ captain Amos alimaliza kutoa maelezo yake.


Naaam hapo bwana Six anaachia tabasamu kidogo, โ€œkazi inazidi kuwa rahisi, sawa kama kuna taarifa nyingine itufikie harakaโ€ alisema Sixmund, kabla hajakatasimu na kufungua email ambayo ilikuwa imeingia, nayo ilikuwa inaorodha ya askari wa MLA na mawala wa MLSA, walioshiriki operation ya kuondoa waasi ndani ya serikali, ambayo ilianza na jina la kanal Dickson Chitopelah, ambae kwa sasa ni waziri wa ulinzi na usalama nchini #mbogo_land, na hapo akaendelea kuyasoma majina yaliyo fuatia.*******


Turudi nyumbani kwa Deus, ambako sasa pale sebuleni hatuoni mtu zaidi ya nguo zilizozagaa pale chini, nguo ambazo muda uliopita zilikuwa zime valiwa na Deus mwenyewe na mwanadada Veronica, hebu twendeni chumbani kwa Deus, labda walihamia huko, tunapiga hatua za taratibu kukifuata chumba cha Deus, ambacho kwa bahati kipo wazi, tunapoingia ndani ya chumba nako hakuna mtu, lakini wakati tunajiuliza wapo wapi, โ€ฆโ€ฆ. ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
 
Kwamba Bado wanatusaka, mpaka huku "KIZIMZUMBWI"?
Mamaaaaa!!! Twafwaa UMD๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
NYUMA YA MLANGO WA ADUI
SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA SITA
MTUNZI: Mbogo EDGAR
WHATSAPP: 0743632247 (KWAMATUMIZI YA OFISI TU)
TULIPOISHIA SEHEMU YA MIA MOJA NA ISHILINI NA TANO:- Wakati hayo yanaendelea mara Deus akasikia simu yake inaita, ni ile ambayo anawasiliana na baba yake, akaitazama toka mezani akaona kuwa mpigaji ni baba yake, akaipotezea na kurudisha macho kwa Veronica, ambae hakutamani hata kidogo Deus aache kile alichokuwa anakifanya kwenye mwili wake, mara kwa bahati mbaya au mzuri macho ya Deus yanapita kwenye screen ndogo ya nchi 32 yenye kujigawa mara nne, ambayo katika kipande kilichoandikwa cam 1 kilionyesha mwanga wa magari yaliyokuwa yanakuja upande ule. โ€ฆโ€ฆ. ENDELEAโ€ฆ


Deus alitazama kwa umakini camera namba moja, akagundua kuwa yalikuwa magari mawili, lakini sio ya polisi wala sio ya UMD ambayo aliyakuta pale Makabe, yalikuwa ni mengine kabisa, ambayo ni Toyota prado na Nissan, yaliyokuwa yanakuja taratibu upande iliko nyumba yake, na kwa kawaida camera za ulinzi zilizofungwa katika nyumba hii hasa zile za nje, zina uwezo wa kuona mita mia nane kwa mchana na usiku mita mia nne, japo kwa mita hizo usingeweza kutambua kitu halisi, sasa basi kwa muonekano wa magari yale na jinsi alivyo yatambua, ni kwamba yalikuwa ndani ya mita mia moja, โ€œwakifika mita hamsini hawana bahatiโ€ alisema Deus, huku anamuweka sawa Veronica na kumshika ile nguo ya chini kisha akaanza kuishusha taratibu, โ€œjamani mchoraji usiwe na haraka, si uniambie kama utanioaโ€ alisema Veronica kwa sauti ya ulegevu huku anashindwa kuzuia mkono wa Deus uliokuwa unaendelea kushusha ile truck aliyoivaa, ambayo sasa ilisha kata nusu ya mapaja na kuacha wazi viungo muhimu, japo kitumbua kilikuwa kimehifadhiwa ndani ya bikini iliyo lowa chepe chepe usawa wa kitumbua, โ€œumesahau kama tuliweka ahadi kuwa endapo JJ atazingua nitakuoa mimiโ€ alikumbusha Deus huku anaacha kushusha ile truck na kulaza mkono kwenye bumunda na kurudia tena kamchezo kama kale kamwanzo.


Veronica akajikuta anaachia kicheko cha kivivu halafu kitamu, โ€œsawa lakini mchoraj inabidi unifundishe taratibu, mwenzakoโ€ฆโ€ฆ mwenzio โ€ฆโ€ฆ. Sijawahiโ€ alisema Veronica kwa sauti ambayo sio tu kuzidiwa na hamu ya dudu iliyosababishwa na mitekenyo kwenye kunde, Deus alitabasamu kidogo, โ€œusiogope pacha, nakuahidi utafurahiโ€ alisema Deus kwa sauti nzito huku anaendelea kuchezea eneo la shambani kwa bibi, Wakati huo simu bado ilikuwa inaendelea kuita na mpigaji akiwa ni baba yake, je alikuwa anataka kumueleza chochote juu ya ujio wa watu hawa, au?, lakini kijana huyu mwenye kuelemewa na kiu kali ya kitumbua, anaachana na simu nakuendelea kupekecha sehemu ile yemye shamba la kunde, huku mkono mmoja ukiendelea kushusha ile nguo ya mwadada huyu mrembo, ambae alizidi kujiweka vizuri ili kumpa nafasi kijana huyu, aweze kuitoa nguo hiyo.


Nadhani haitokuwa vyema kama tukiendelea kubakia nao wakati wakiwa katika hali hii, hebu tuwapishe kidogo tutarudi baadae.*********


Naaam, king Elvis akiwa amekosa usingizi kabisa, akiwaza juu ya hiki kinacho endelea, ni swala la uasi ndani ya nchi yake, jambo ambalo halikuwahi kutokea enzi za utawala wa baba yake, na hata utawala wa babu yake lilikuwa katika tetesi, sasa utawala wake ndio kipindi ambacho waasi, wamepanga kutimiza uasi wao, na kitu cha kuhuzunisha zaidi ni kwamba, zoezi la kukomesha uasi lililofanywa miaka ya nyuma, alikuzaa matunda, baada yake ni kama liliimarisha ngome ya waasi.


Wakati anawaza hayo, mara simu yake inaita, nae anaitazama na kuona kuwa mpigaji ni Major General Sixmund, anaipokea haraka, โ€œvipi Six, unahabari yoyote?โ€ aliuliza King Elvis kwa sauti iliyojaa shauku, โ€œmtukufu mfalme, kazi inaendelea vizuri na sasa tunaanza kutafuta watu walioshiriki katika kikosi maalumu cha kusaka waasi ndani ya serikali, maana kuna uwezekano kuwa baadhi yao walikiuka amri ya mfalme na kusababisha kile ambacho kilipelekea lawama kwa king Eugenโ€ ilisikika sauti ya Six akiongea kwa busara na unyeyekevu, โ€œinamaana mmeshindwa kuipata katika maktaba za kijeshi?โ€ aliuliza King Elvis kwa sauti ya mshangao, โ€œmtukufu, sehemu zote za kuhifadhia nyaraka muhimu hakuna hata nakala moja iliyosalia, inaonekana kuna mtu amefuta na kupoteza orodha hiyo kwalengo la kuondoa kumbukumbu ya watu walioshiriki msako huleโ€ alijibu Sixmund.


Hiyo ilimshtua kidogo King Elvis wa kwanza, โ€œlakini lazima kuna vyanzo vya watu ambao mnaweza kuanza nao, mfano aliekuwa kiongozi wa operation ile bwana Chitopelaโ€ alisema King Elvis, ndio mtukufu, lakini tumeona tuitafute orodha kwa njia yetu, kwasababu hatutaki kumshirikisha Chitopela kama ulivyosema tufanye uchunguzi kwa siriโ€ alisema Sixmund, na hapo King Elvis akaonekana kuelewa, โ€œsawa General, nakutumia kwenye email yako, lakini Six kumbuka hili swala ni muhimu liende sambamba na kule dar es salaam, maana mara tutakapo pata ushaidi wa wahusika moja kwa moja wakamatwe kabla silaha hazijaingia nchini na kuleta madharaโ€ alisisitiza king Elvis, ambae sasa alikuwa anainuka toka kitandani na kusogea sehemu ambayo kuna ofisi yake ya pale ndani.**********


Naaam saa sita za usiku, vyombo vya ulinzi na usalama vipo kazini, hakuna dalili ya kumaliza kazi na kwenda kulala majumbani mwao, hofu zime tanda miongoni mwa askari, hasa baada ya wenzao kushambuliwa na watu wanao hisiwa kuwa ni UMD, hakuna dalili ya kumpata Deus Nyati, ambae imesemwa ndie aliemteka Veroca James na ndie dereva wa BMW nyeusi ambae alifanya mauwaji jijini Arusha, japo nayo ilikuwa ni hofu ya pili kwa wanausalama hao, maana kupambana na kijana huyu ni sawa na kupambana na kikosi cha makomandoo.


Tukiangazia katika msako huu wa Deus Nyati, magari ya polisi yanaonekana kuzagaa kwenye barabara ya misegese kuelekea kwenye makutano ya barabara ya kisarawe na manero mango, katika msafari huu gari la akina Cheleji lilikuwa kilomita kama sita kabla ya kufika njia panda, wakiwa na magari yao matatu, wakati huo gari la mbele kabisa lilikuwa limeshafika njia panda na kusimama hapo wakiwa hawajuwli upande wa kuelekea, nao wakasimamisha magari na kuanza kuuliza kwa raia wachache ambao hukaa barabarani usiku kucha wakivizia wateja wa mkaa na bidhaa nyingine za matunda kama mafenesi na mapasheni, (passion) kwa bahati walikuwepo kama wanne hivi.


โ€œHabari zenu vijanaโ€ alisalimia Asistant inspector, aliekuwa kiongozi wa msafara ule, nzuri kamanda, poleni kwa majukumuโ€ alisema kijana mmoja alieonekana kuchangamka kidogo, โ€œasante bwana ndio majukumu yetu ya kila sikuโ€ alijibu yule polisi mwenye nyota moja, kabla hajauliza swali, โ€œeti kuna magari mawili yanayo fanana na land roverโ€ฆ.โ€ Kabla hajamaliza yule kijana mchangamfu akadakia, โ€œyale madefender mapya mapya hivi?โ€ aliuliza kijana yule, โ€œhaswaaaaa hayo hayo, yameelekea upande upi?โ€ aliuliza yule Asistant inspector, โ€œyameelekea huko Kazimzumbwiโ€ alisema yule kijana huku akionyesha upande wa manero mango.


Na hapo yule polisi akawashukuru wote kwa ujumla, kisha akarudi yalipo magari yao na kuanza kuongea kwa radio call yake, โ€œhallow vituo vyote, mimi ni 25, kuna ujumbe, mnanipataโ€ alisema yule kamanda, na hapo zikaanza kusika sauti nyingine kwenye radio zikikubali kuwa wanamsikia, โ€œueleko wa farasi wapya ni Kazi mzumbwi, narudia uelekeo wa farasi wapya ni Kazi mzumbwiโ€ hapo hapo zikaanza kusikika sauti za wengine wakisema kuwa wapo njiani wanaelekea huko waliko wao lakini ya mwisho ilikuwa ni ya amri, โ€œhallow vituo vyote, mimi Alpha, tukutane njia panda ya manero mango, narudia tukutane njia panda ya manero mango, jibu kama mumenielewaโ€ ilisema ile call ya Alpha, ambayo katika alama ya miito ni kamanda wa polisi kanda maalumu ya Dar es salaam, yani CP Nyambibo


Wakati huo huo, maeneo ya misegese relini, mita kama mia mbili toka barabara ya vumbi yanaonekana magari mawili ya wakina Uled Songoro wakiwa wamesimamisha magari yao kwenye njia hii ambayo licha ya uhafifu wake, lakini ni wazi kuna watu wanaitumia tena kupitisha gari, โ€œinaonyesha huku kama sio kuna watu wanaishi, basi kuna shughuri fulani zinaendeleaโ€ alisema Songoro huku wakiwa wanatazama ile njia upande ilikoelekea, kabla hawajageuza macho yao kutazama upande wa barabarani, yani walikotoka, โ€œtuwasikilizie wapite, maana lazima wengine watakuwa mbeleโ€ alisema Songoro huku yeye na mwenzake wakitazama kule barabarani ambako kutokana na giza lililokuwa limetanda ungeweza kuona taa za magari zilizokuwa zimeongozana kuelekea upande wa njia panda ya manero mango, โ€œila boss kwa uwingi huu wa magari ya polisi sidhani kama tutaweza kumsaka yule dogo bila kukutana naoโ€ alisema mmoja kati ya vijana wa Songoro.


Japo ilikuwa ni ukweli alichoongea kijana huyo, lakini Songoro aligeuza uso wake na kumkata jicho la hasira, โ€œsipendi kusikia huo ujinga tena, kwa hiyo unataka tuache kumtafuta huyu mjinga na turudhishe makalio nyumbani?โ€ aliuliza Songoro kwa sauti iliyojaa hasira, โ€œsahamani boss, sikumaanishaโ€ alisema yule kijana kwa sauti iliyojaa uoga, ni wazi anaijua tabia ya Songoro pale anapohitaji kufanya jambo lake, hataki kuonekana dhaifu kwa mtu au kitu chochote.


Yap! wakati askari polisi wengine wakiwa njia panda ya manero mango, mpaka Kazimzumbwi, huku Kibamba chama, Kamanda wa kanda maalumu ya dar es salaam, CP Nyambibo, anakutana na makamanda watatu wa mikoa ya kipolisi ya kanda maalumu ya dar es salaam, mmoja wapo akiwepo kamanda wa ilala bwana ACP Ulenje Kamanda wa jeshi la polisi kanda maalumu Ilala, wanakutana njia panda ya mloganzira pale kibamba chama, huku wakiwa na magari manne yenye askari ambao walikuwa na silaha zao tayari kuwalinda kwa chochote, โ€œjamani uelekeo mpaka sasa ni njia panda ya Manero mango, huko ndiko tutaanzia msako wetuโ€ alisema kamanda Nyambibo, kisha safari ikaanza kuelekea huko, โ€œhawa mabwege sijui wapo wapi kwa sasa, ngoja niwasiliane nao, wajue kinachokuja kuwa tokeaโ€ alisema Ulenje, huku anatoa simu yake toka mfukoni,


Upande wa magharibi mwa Kisarawe, sasa tuna zungumzia misitu ya Kazi mzumbwi, kilomita chache toka kijiji cha manero mango, mita kama mia mbili toka barabarani kwenye uwanda fulani wa chini wa bonde, lenye mto wenye maji mengi, panaonekana magari mawili aina ya Land rover puma yakiwa yamegeshwa, huku mita kama hamsini toka sehemu hiyo ikionekana miili ya watu zaidi ya kumi iliyokuwa imerundikwa sehemu moja kama mifuko ya taka, vijana wanaonekana wakiosha ndani ya magari yale yaliyokuwa yanachuruzika damu kama gari la kubebea ngombe toka machinjoni, pembeni kidogo toka yalipo yale magari anaokena kanali wa zamani wa MLA Erasto Kadumya, ambae anajiita General akiwa anaongea na simu huku pembeni yake akiwa amesimama, Luten wa zamani wa MLA Enock Kafulu, waliokuwa wamesimama pembeni kidogo na yalipokuwepo magari yale


โ€œKobwe, nyie mmefika wapi, munajua kama kila kitu kimesimama tunawasubiri nyie?โ€ aliuliza Kadumya ambae ni kama aliona kikosi kina chelewa sana kufika, โ€œmkuu tunakaribia Rufiji, tuna kimbia kadiri tunavyoweza, nadhani baada ya masaa mawili tutakuwa dar es salaamโ€ ilisikika sauti ya kobwe, โ€œsikia wewe nani alikuambia mtaingia dar es salaam bila kujulikana kwamba kuna majeshi yasiyoeleweka yanaingia jijini, dar es salaam watu hawalali bwana, sasa sikiliza toka kwangu, mukifika karibu na mpakani mwisho wa soko kuna barabara inaingia upande wa kushoto, japo ni ya vumbi lakini munaweza kutembea kwa dakika arobaini na tano mpaka lisaa limoja mukawa mume shafika hapa, fanyeni hivyo tuna wasubiria nyie, na ninacho jua polisi wanatutafuta kwa shambulio tulilolifanya hapo nyumaโ€ alisistiza Kadumya, ambae kabla haja endelea akasikia simu yake inatoa mlio fulani wa kuashiria kuwa kuna simu ilikuwa inatarajia kuingia, akaitoa sikioni na kutazama, akaona ni Ulenje anapiga simu.


Moja kwa moja Kadumya akajua kuwa, kuna taarifa zinakuja na anatakiwa kuzipokea, โ€œhebu kata simu nipokee simu nyingine muhimu zaidiโ€ alisema Kadumya na upande wa pili wakakata simu na yeye akaipokea simu ya Ulenje, โ€œni kweli mupo kazimzumbwi?โ€ hilo ndilo swali la kwanza kuulizwa, โ€œndio umejuaje maana polisi tumewaacha mbali sana?โ€ aliuliza Kadumya kwa mshangao, maana aliona kuwa Ile ndiyo ilikuwa sehemu nzuri kwaajili ya kupanga majeshi yake na pengine kuweka kambi ya muda, kwa muda ambao watakuwa wakiendeleza msako, โ€œsio muhimu kuhusu nimejuaje, chamsingi ni kwamba, ondokeni haraka na muzidi kujificha, nadhani lisaa limoja baadae tutakuwa hapoโ€ alisema Ulenje na kukata simu.


Hapo kama amechanganyikiwa, Kadumya akageuka haraka yaliko yale magari, โ€œharaka sana ingieni kwenye magari, sio sehemu salama kwetuโ€ alisema Kadumya huku yeye na Kafulu wanakimbnilia kwenye magari ambayo tayari yalikuwa yamesha washwa tayari kwa kuondoka, kitendo cha kuondoka kilichukua dakika moja, tayari magari yalishaanza kuondoka kuifuata barabara kuu ya manero mango, huku wengine wakiwa wameshikilia bunduki zao kwa umakini mkubwa tayari kushambulia chochote watakacho kiona mbele yao.*******


Naaam ile bwana Six anamaliza kuongea na mfalme wa #mbogo_land, hazikupita hata sekunde tano, akaona simu yake inaanza kuita, alipoitazama alikuwa ni Captain Amos Makey, ni yule aliempatia askari na kumtuma kwenda Tanzania, akaipokea haraka na kuweka simu sikioni, โ€œAmos kuna jipya lolote?โ€ aliuliza major General Sixmund, ndiyo mkuu, kuna habari mpya za kiutendajiโ€ alijibu captain Makey, โ€œok! Unaweza kuniambiaโ€ alisema Sixmund na kutega sikio kusikiliza taarifa hiyo mpya, โ€œafande tukiwa hapa kwa bwana James Kelvin, tumegundua kuwa licha ya kwamba mtoto wa kanali Frank, yani private Deus Nyati kumuokoa bwana James, pia ndie aliemuokoa binti yake yani doctor Veronica, ambae kupatikana kwake ndio kuondoka kwetu, pia taarifa nyingine ni kwamba, Deus Nyati mpaka sasa ameshauwa UMD kadhaa, ambao idadi kamili hatujaipata, na kiingine ni kwamba, kama unamkumbuka afisa mmoja alieitwa Enock Kafulu alietoweka ghafla na kuandikwa kama mtoro jeshini, yupo huku kama UMD, na ndie alie ongoza utekaji nyara wa Veronicaโ€ captain Amos alimaliza kutoa maelezo yake.


Naaam hapo bwana Six anaachia tabasamu kidogo, โ€œkazi inazidi kuwa rahisi, sawa kama kuna taarifa nyingine itufikie harakaโ€ alisema Sixmund, kabla hajakatasimu na kufungua email ambayo ilikuwa imeingia, nayo ilikuwa inaorodha ya askari wa MLA na mawala wa MLSA, walioshiriki operation ya kuondoa waasi ndani ya serikali, ambayo ilianza na jina la kanal Dickson Chitopelah, ambae kwa sasa ni waziri wa ulinzi na usalama nchini #mbogo_land, na hapo akaendelea kuyasoma majina yaliyo fuatia.*******


Turudi nyumbani kwa Deus, ambako sasa pale sebuleni hatuoni mtu zaidi ya nguo zilizozagaa pale chini, nguo ambazo muda uliopita zilikuwa zime valiwa na Deus mwenyewe na mwanadada Veronica, hebu twendeni chumbani kwa Deus, labda walihamia huko, tunapiga hatua za taratibu kukifuata chumba cha Deus, ambacho kwa bahati kipo wazi, tunapoingia ndani ya chumba nako hakuna mtu, lakini wakati tunajiuliza wapo wapi, โ€ฆโ€ฆ. ENDELEA Kufuatilia mkasa huu wa NYUMA YA MLANGO WA ADUI unao kujia hapa hapa jamii forums
Ungetutumia hata picha ya Carolina, huenda tukamfahamu๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚๐Ÿคฃ๐Ÿ˜‚UMD
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom