Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #401
SEHEMU YA 355
Mama Angel alijikuta akijiwa na moyo wa huruma tu, kwani huwa akisikia mtoto anaumwa anasikia kuteseka sana moyoni, basi akahitaji kwenda kumuona.
Ikabidi yeye na Tumaini huku wakiongozana na Siku wakaenda hadi chumbani kwa Sarah na kumkuta amekaa huku akilalamika tumbo, walipoingia tu alianza kutapika, wakati wanamuhamisha ili wamfute yale matapishi walikuta kuna damu nyingi sana zinamtoka.
Hapo wakaona kuwa huyu mtoto anahitaji tiba ya haraka sana, kwahiyo ilibidi mama Angel aanze kumuandaa kwaajili ya kwenda nae hospitali, yani Sarah hata hakuwa na maelezo yanayoeleweka juu ya hali yake.
Wakatoka nae na moja kwa moja kuanza nae safari ya kwenda hospitali, Siku alibaki nyumbani huku akiwaangalia tu maana alihitaji kubaki na kuangalia nyumba kwani alijua wazi kama mama yao angerudi na kutokuwakuta wote ingekuwa balaa.
Baada tu ya wale kuondoka, ndipo Elly aliporudi nyumbani na kumkuta Siku yupo nje anafua, alienda ndani kumuangalia Sarah aliyemuacha mgonjwa ila hakumkuta, ikabidi arudi nje kumuuliza Siku aliyekuwa anafua,
“Yuko wapi Sarah?”
“Oooh Sarah ni mgonjwa, yani anaumwa sana kwahiyo walikuja hapa wale wakina mama Erick ndio wamempeleka hospitali”
“Alizidiwa sana au?”
“Aaaah si unajua wale wana viherehere sana, mama si ameondoka kamuacha Sarah anaumwa hapa wala hakuwa na tatizo kwani alijua lazima atapona tu, ila wao sasa na viherehere vyao yani wamemchukua na kumpeleka hospitali”
“Sasa hata hujui ni hospitali gani wamempeleka, wasiporudi nae je?”
“Kwani kwao hapafahamiki? Tutaenda nyumbani kwao, waache wahangaike nae huko, watamrudisha tu”
Basi Elly akatamani kujua kuwa Sarah alikuwa akisumbuliwa na nini, ila kwa muda huo njaa nayo ilikuwa ikimsumbua maana aliondoka bila ya kula chochote, akamwambia Siku,
“Si chai ipo eeeh! Ngoja nikakoroge ninywe”
Muda huo huo Siku aliacha kufua na kumwambia Elly kuwa anaenda kumuandalia chai, basi moja kwa moja aliingia nae ndani, na kumuandalia chai kweli ambapo Elly alikunywa na kujihisi vizuri, baada ya hapo Siku alimletea Elly juisi na kumtaka ashushie kwa ile chai aliyokunywa,
“Mmmh nimeshiba sana”
“Aaaah kwetu kukataa mtu kitu alichokuandalia ni vibaya kabisa, naomba unywe hata kidogo”
Basi Elly alichukua ile glasi na kunywa kidogo ila baada ya kunywa tu alijihisi kulewa yani kama mtu aliyekunywa pombe, basi Siku alifunga milango na kumchukua Elly kwenda nae chumbani kwake, na kuanza kumpapasa, na kuweza kulala nae sababu tu Elly hakujielewa na ile hali ya kuwa kama amelewa.
Yani Elly alivyokuja kurejewa na fahamu zake aliumia sana kwenye moyo wake kwani hakutegemea kufanya kile kitu na Siku,
“Kwanini umenifanyia hivi dada?”
“Nilikuwa nakutamani sana Elly kwa muda wote, yani kila siku nilikuwa nakutamani sana. Nashukuru leo nimepata nafasi, huu ni mwanzo najua sasa utakubali kwa hiyari yako”
Elly alichukia sana, na kutoka mule chumbani kwa Siku na kwenda chumbani kwake huku akiwa amechukia sana.
Wakina mama Angel walifika hospitali wakiwa na Sarah na moja kwa moja alipelekwa kwenye matibabu, basi walitulia huku wakisikilizia kuwa itakuwaje. Mama Angel aliamua kumpigia simu mama Sarah ila ile simu iliita sana hadi kukatika yani hakuna cha maana alichokipata.
Baba Angel akasema,
“Haya mambo ndio huwa siyapendi, kweli mama wa mtoto anaondoka na kuacha mtoto wake anaumwa jamani”
“Labda alijua anaumwa kidogo”
“Kidogo, hakumuangalia vizuri, kwa zile damu zilizomtoka inaonyesha ni muda mrefu tatizo lilianza”
Waliongea kidogo pale huku baba Angel akifatilia hali ya yule mtoto Sarah, badae daktari alikuja na kuhitaji mzazi wa yule mtoto, sababu wale ndio walimpeleka na kudai kuwa ni ndugu wanaoishi na yule mtoto ilibidi tu awaambie kinachomsumbua yule mtoto,
“Ni hivi jamani, inaonekana mtoto alikuwa na mimba changa sasa imetoka”
Wote wakashangaa sana, mama Angel aliuliza,
“Jamani, mtoto mdogo kama Sarah anatoa wapi mimba?”
Tumaini akadakia na kusema,
“Kila siku huwa nasema sana kuhusu malezi mabovu, kwani Daima kapata vipi ile mimba aliyoipata? Watoto wa siku hizi wana mambo sana”
Basi daktari akaondoka kuendelea na huduma kwa yule mtoto kwani ilibidi wamsafishe, kwakweli baba Angel aliwaambia,
“Jamani, mimi naondoka mtaniambia yatakayojiri. Sitaki habari za watoto wasiojielewa kama huyo”
Baba Angel aliondoka zake na kumuacha pale Tumanini na mama Angel, ila muda kidogo Tumaini nae aliondoka zake na kumuacha pale mama Angel, yani mama Angel alishindwa kuondoka bila ya kuruhusiwa kuondoka na Sarah, kwahiyo hakutaka kuondoka kabisa.
Tumaini akiwa njiani akielekea nyumbani kwake, ndipo alipokutana na mama Sarah, alimsimamisha na kuanza kuongea nae,
“Kheee unajua nilikuwa sikujui kabisa mambo yako, kumbe wewe mwanamke ni mbaya kiasi hiki”
“Kwani nimefanyeje?”
“Unawezaje kuondoka na kumuacha mwanao mgonjwa ndani au ulikuwa ukijua ni kitu gani kinamsumbua mwanao?”
“Kwahiyo ulikuwa nyumbani kwangu?”
“Ndio, tulikuwa na kikao na wewe kwani tulikuwa tukihitaji kujua ukweli kuhusu mtoto Sarah, ila hatujakukuta na kumkuta mtoto akiumwa vile nyumbani kwako”
“Kheee jamani, Sarah alikuwa anaumwa tumbo tu wakati naondoka. Siwaelewi imekuwaje?”
“Imekuwaje kuhusu nini? Mwanao katoa mimba huko”
“Katoa mimba? Hiyo mimba Sarah aitoe wapi? Mbona mnataka kuchekesha walionuna”
“Ndio hivyo, nenda hospitali huko kamfate mwanao. Umemkuta Erica hana roho mbaya na ndio kabaki na mwanao hospitali, nenda kamuangalie huko. Nilikusema sana kwa malezi mabaya unayompa Sarah, nadhani umeona matunda yake sasa”
Tumaini akamuelekeza tu hospitali aliyolazwa Sarah na kuachana nae pale.
Walipomaliza kumuhudumia Sarah na kila kitu ndio wakampa ruhusa mama Angel aweze kurudi nae nyumbani, daktari aliongea tu na mama Angel kiasi kidogo pale,
“Mpeni mtoto elimu stahiki, kumbe alikuwa mjamzito halafu akaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango, imeenda kuharibu ile mimba na ndiomana kaumwa sana, hebu muwe makini sana na hawa watoto wenu, mtawapoteza mjue.”
Basi akapewa na dawa zitakazoweza kumsaidia kwa kipindi hiko, mama Angel akaondoka sasa na Sarah yani alikuwa akimuangalia bila ya kummaliza kwakeli, basi akawa anaondoka nae huku akiendesha gari na kumuuliza baadhi ya maswali,
“Kwanza Sarah ulipata vipi hiyo mimba?”
Sarah alikuwa kimya tu huku akiinama chini, mama Angel alipumua kidogo na kumuuliza tena,
“Na ilikuwaje hadi ukaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango?”
Bado Sarah alikuwa kimya tu, basi mama Angel akamwambia,
“Utaniambia vizuri ukiwa vizuri, nakuhurumia sana, wewe Sarah bado ni mtoto mdogo sana”
Basi walifika nyumbani kwakina Sarah na Sarah kuingia ndani na moja kwa moja mama Angel alimpeleka Sarah chumbani ili aweze kupumzika, ila wakati anatoka tu chumbani kwake alikutana na mama Sarah ambaye ndio alikuwa ametoka kufika,
“Yani nimetoka hadi kwenye ile hospitali mliyoenda nikaambiwa kuwa mmetoka, kwanza nakushukuru kwa hili ulilolifanya kwani mwanangu anaumwa nini?”
“Yani unakaa na mwanao kweli hujui tatizo lake? Mwanao alikuwa ni majamzito, kaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango sijui basi ile sindano imeenda kuharibu ile mimba na kumfanya aumwe sana, na hiyo hali imefanya apoteze damu nyingi sana. Anatakiwa kula vizuri na kuna dawa nimemuachia hapo ambazo walimuandikia”
“Oooh nashukuru sana, sikutegemea kama ungefanya kitu cha namna hii, asante sana Erica”
“Usijali, watoto hawa ni wa kwetu sote. Ila dokta kasisitiza sana juu ya malezi tunayowapa watoto, tunatakiwa kuwa makini sana”
“Asante”
Basi mama Angel alimuaga na kuondoka zake, kwakweli hata yeye alishangaa mno kuona jinsi mama Sarah alivyokuwa mpole kwa siku hiyo.
Moja kwa moja mama Sarah alienda chumbani kwa mwanae na kumuangalia, basi alikaa karibu yake na kumuuliza,
“Mwanangu kwani hiyo mimba umepataje?”
“Sijui hata nimepataje”
“Nani alikupeleka kwenda kuchoma hiyo sindano ya uzazi wa mpango?”
“Sijui mama, nimechoka sana. Hali yangu sio nzuri kabisa, kwasasa nahitaji kupumzika”
“Pole sana mwanangu, Mungu atakusaidia utapona tu”
Kisha mama Sarah alitoka na kumtaka Siku amuandalie chakula Sarah ili aweze kwenda kumlisha kikiwa tayari. Siku hii mama Sarah hata hakujua kama ataweza kutoka kwa ile hali ya mtoto wake.
Mama Angel alirudi nyumbani kwake wakati hata giza limeanza kuingia na kumkuta mumewe akiwa amejilaza tu kwa muda huo, basi alienda kuoga na kurudi kuongea na mume wake,
“Ila mume wangu jamani, ndio kuniacha mwenyewe hospitali”
“Kiukweli huwa sipendi ujinga wa watoto wa kike kamavile kwakweli, mtoto anabeba mimba kwa umri mdogo vile! Na kwanini imetoka sasa?”
“Sijui alikuwa na mimba halafu akaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango”
“Aaaargh katoto kana tabia mbaya hadi kamewaza kwenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango jamani!! Si umri wakina Erica yule aarrgh!”
“Unajua watoto tusiwalaumu sana vitu vingine hawajui”
“Hawajui wapi? Mtoto anajua kabisa nitapata mimba ndio kaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango ili asipate na aendelee kufanya kwa raha zake, naye ni mtoto huyo? Hata sitaki tena awe karibu na watoto wangu maana atawafundisha tabia mbaya”
“Aaaah usiseme hivyo mume wangu, mimi nina uhakika Sarah hajapata mtu wa kuongea nae na kumuelewesha vizuri kwani nina hakika angeeleweshwa vizuri basi yote haya yasingetokea”
“Aeleweshwe nini na mtoto kashapata utamu wa tunda?”
Mama Angel alicheka tu, kisha baba Angel akauliza tena,
“Je umemuuliza nani muhusika wa hiyo mimba iliyotoka? Umemuuliza ni nani aliyempeleka kwenda kuchoma hiyo sindano ya uzazi wa mpango?”
“Nimemuuliza kabaki kimya tu, anaona aibu ila nasubiri apone vizuri nitamuuliza”
“Utamuuliza nini sasa? Si ndio wakina Daima hao? Toto limefata tabia mbaya ya mama yake lile aaargh”
Baba Angel alionekana kutokupenda kabisa lile jambo ambalo Sarah amelitenda kwahiyo kwa muda huo aliamua kulala tu wala hakutaka matatizo mengine.
Kulipokucha, Baba Angel alijiandaa na kwenda kazini kama kawaida na wakina Erica walienda shuleni kwahiyo pale nyumbani alibaki tu mama Angel, Vaileth na Ester kama kawaida.
Basi mama Angel alianza kumsimulia Vaileth kitu ambacho kimejiri kwa Sarah,
“Yani nimeumia sana kwa mtoto mdogo kama Sarah kupata ujauzito loh! Halafu kaenda kutumia sindano ya uzazi wa mpango jamani”
“Sasa nani kampa Sarah mimba?”
“Anataka kusema basi!! Sijui imekuwaje, yani mimi nina wasiwasi sana yasije kuwa mambo kama ya Daima”
“Jamani”
“Roho imeniuma sana, huwa namuona Sarah kama mtoto wangu, huwa namuona Sarah kama ninavyomuona Erica tu. Nimeumia sana”
“Kweli ni mdogo sana, kaanza mapenzi basi ndiomana akapata hiyo mimba, hadi imetoka dah!”
Mara mlango ulifunguliwa na aliyefungua mlango alikuwa ni Erica, basi mama yake alimuuliza kilichomfanya arudi mapema vile,
“Tumbo mama linaniuma sana”
Mama Angel akashtuka maana hofu ikamjaa kuwa isijekuwa mambo yale yale ya Sarah, basi alienda nae mwanae chumbani na kumuuliza vizuri,
“Ni tumbo gani linakuuma mwanangu”
“Tumbo la kikubwa mama”
Hapo mama Angel alielewa vizuri kabisa kitu kinachomsumbua mtoto wake.
Baada ya muda Erica alimfata Vaileth ambae kwa muda huu alikuwa chumbani kwake na kuanza kumuuliza,
“Ni nani mliyekuwa mnamzungumzia kuwa katoa mimba?”
“Ni Sarah huyo, yani kumbe mtoto mdogo ana mambo ya ajabu”
“Kheee Sarah kaanza mambo ya wanaume!! KWahiyo naye kapata mimba kama Daima?”
“Ndio ila imetoka, yani Sarah kafanya mchezo wa ajabu sana”
“Kheee kumbe!!”
Basi Erica aliridhika kwa muda kuipata habari hiyo maana alishindwa hata kupumzika kidogo bila kujua kilichokuwa kikizungumziwa na mama yake pamoja na Vaileth pale sebleni, kwahiyo alivyojua aliweza kuridhika na moyo wake sasa.
Baba Angel akiwa ofisini kwake leo alitembelewa na Sia, na kushangaa ila alimkaribisha na kumuuliza,
“Ndio ushapata jibu la utafiti wako juu ya aliniwekea sumu?”
Kidogo Sia alijiuma uma na kusema,
“Hiko sio kilichonileta ila kilichonileta ni swala lingine kabisa”
“Swala gani?”
“Hivi kwanza unajua kama Erica amewahi kuwa na mahusiano na Derrick? Ni ndugu yake ila amewahi kuwa na mahusiano nae”
“Hayo hayanihusu kabisa, kinachonihusu sasa ni kuwa Erica ni mke wangu halafu Derrick ni shemeji yangu”
“Duh!! Yani wewe Erick ni wa ajabu sana”
“Sema lingine ulilokuja nalo”
“Ni kuhusu mtoto Elly”
“Eeeeh una story mpya kuhusu Elly au kitu gani? Hebu sema ukweli kuwa Elly ni mtoto uliyezaa na Derrick”
“Hapana, mimi sijazaa na Derrick. Ngoja leo nikwambie ukweli”
“Haya, niambie nakusikiliza”
“Mimi kiukweli kabisa nilizaa na Steve yani huo ndio ukweli halisi”
Baba Angel alicheka kwanza na kusema,
“Ila wewe mwanamke jamani dah!! Nakusikiliza vizuri sana, na ulivyokuwa umekazana kuwa umezaa na mimi ni nini?”
“Sikiliza basi, ni hivi mimi siku nimeenda kujifungua nilienda kabla hata ya muda ila mwanangu alikuwa vizuri tu, sema hakuzaliwa kwa uzito ule uliotakiwa, basi ikapewa yule mtoto ila alikuwa akilia sanaalipokuwa kwangu. Baba yako mzee Jimmy alikuja kuongea nami, yani aliongea na mimi kabla sijajifungua na akaongea na mimi baada ya kujifungua, alipanga nami mpango wa kubadilisha mtoto wangu na mtoto wa Erica, nilikubali sababu ya shida yangu ya hela, mtoto alipofika miezi mitatu kasoro ndipo mzee Jimmy alipowabadilisha, kwamaana hiyo Elly ni mtoto wa Erica halafu Erick ni mtoto wangu ndiomana nilikuwa nakukazania kuwa nimezaa na wewe kwani nilijua hata mwanangu akipimwa damu atakutwa ni mwanao kweli yani Elly. Ila baada ya sokomoko hili la kusema kuwa Elly ni mtoto wa Derrick basi kuna uhakika kabisa kuwa Erica aliendelea na Derrick kwahiyo Elly na Erica mdogo wote ni watoto wa Derrick maana mtoto wangu mimi ni Elly”
“Uwiii sijakuelewa hata jambo moja ulilonieleza Sia”
“Hujanielewa kivipi? Ushahidi pia ninao kuwa mimi na baba yako tulibadilisha watoto”
“Mlibadilisha wakiwa na umri gani?”
“Miezi mitatu kasoro”
“Mbona wanangu walipomaliza mwezi tu niliondoka nao na mama yao tukaenda Afrika kusini na tulirudi huko baada ya miaka mitatu, unajua sikuelewi kabisa”
“Nitakuletea ushahidi basi, mimi sio chizi kusema kila siku kuwa Erick ni mtoto wangu. Ila ndio hivyo mkeo alikusaliti huyo ndiomana imekuwa hivyo”
“Nenda tu Sia, ila mke wangu awe alinisaliti au hakunisaliti bado nitampenda hadi mwisho wa maisha yangu”
“Duh!! Ni mzima kweli wewe?”
“Ni mzima kabisa, nilishasema hata nimfumanie hapo mke wangu basi nitamsamehe maana nampenda sana”
“Mmmmh!! Shukuru Mungu mkeo hana hayo mambo siku hizi”
“Ndiomana nimemuoa kwnai najua sio mwanamke wa kutangatanga tangu zamani”
“Sio wa kutangatanga wapi, angetembea na ukoo mzima huyo! Unamtetea tu”
“Alikuwa akitafuta penzi la kweli ila mke wangu katulia sana na nina mpenda sana, hakuna kinachoweza kututengenisha”
“Ngoja nikapekue vizuri ule ushahidi nikuletee”
Sia aliamua kuondoka zake maana aliona hakuna ushirikiano wowote kwa baba Angel ila alimuahidi kumletea ushahidi kwa yale aliyoyasema.
Baba Angel siku hii baada ya maneno ya Sia, aliamua kupitia dukani kumnunulia mkewe zawadi, kwnai yale maneno ya Sia yalimuingia sikio la kushoto na kutokea sikio la kulia, alienda moja kwa moja kwenye duka ambalo huwa ananunua na leo alimkuta baba Emma na kufurahi kwani alijua kuwa atamchagulia kitu ambacho mke wake atakipenda sana.
Alipofika pale tu baba Emma alimuonyesha zawadi ya kumpelekea mke wake,
“Leo mpelekee tu hiki kikoi nina uhakika atakipenda sana”
“Mmmh atapenda kikoi mke wangu kweli!”
“Kweli atakipenda sana, ni kizuri hiki hakuna mwanamke ambaye atakiona na kukichukia”
Basi baba Angel alimchukulia mkewe kile kikoi na moja kwa moja kurudi zake nyumbani kwa mke wake.
Leo alipofika tu ndani moja kwa moja alimuonyesha mke wake ile zawadi aliyomchukulia, kwakweli mama Angel alifurahi sana na kumwambia mume wake,
“Ulijuaje kama nataka kikoi jamani mume wangu? Kweli wewe ni kiboko yangu. Nimependa sana hiki kikoi mume wangu, asante sana.”
Muda wote mama Angel alikuwa akikitazama tu kile kikoi ilionyesha ni jinsi gani amekipenda kile kikoi.
Usiku wa siku hii, Erica alienda moja kwa moja chumbani kwa kaka yake Erick na kuanza kuongea nae kuhusu kile alichosikia kuhusu Sarah,
“Umesikia hayo yaliyopo huko”
“Mmmh umeanza Erica, mambo gani hayo?”
“Kumbe Sarah alikuwa na mimba kwahiyo imetoka”
“Mmmh alikuwa na mimba!! Jamani, Sarah kapata wapi mimba?”
“Kapata wapi? Kwani wewe hujui mimba inapatikanaje?”
Erick alimuangalia nduguye bila ya kumjibu kitu na kuamua kuanza kumueleza mambo mengine,
“Hivi zile karata siku hizi unacheza mwenyewe? Leo nije tucheze wote?”
“Hapana, leo sichezi karata”
“Kwanini?”
“Subiri baada ya siku tatu ndio nitacheza karata”
“Kwanini?”
“Siri yangu, usiku mwema”
Kisha Erica aliondoka zake na kumuacha Erick pale akimshangaa tu na kujiuliza kwanini Erica kasema vile kuhusu kucheza karata mpaka baada ya siku tatu, hakumuelewa kwakweli.
Leo Erick alipokuwa shuleni aliamua kumuuliza Elly kuhusu Sarah kwani ni kweli hakuonekana shuleni, basi alikaa nae na kuanza kumuuliza,
“Vipi Sarah anaendeleaje?”
“Kheee mbona umeniuliza mimi!”
“Nasikia anaumwa, na wewe ulisema kuwa upo nae karibu”
“Ndio anaumwa, ila twende ukamuone sio kuniuliza uliza maana hilo sio jukumu langu”
“Duh!! Basi tutaenda badae baada ya masomo”
Walirudi darasani na kuendelea na masomo kama kawaida, ila vipindi vilivyoisha, Elly alimkumbusha tena Erick swala la kwenda kumuona Sarah, ni kweli Erick alikubali na moja kwa moja kuondoka na Elly kuelekea nyumbani kwakina Sarah.
Walipofika, walimkuta Sarah yupo chumbani, basi Siku alienda kumuita na kumwamnbia kuwa,
“Erick kaja kukuona”
“Oooh mwambie aje kuniona chumbani”
Ikabidi Siku ampelekee ujumbe ule Erick, na muda ule Erick na Elly waliingia pamoja chumbani kwa Sarah ila Sarah aliomba kuzungumza na Erick kwahiyo alihitaji Elly asubirie kwanza, na Elly alifanya vile basi Erick alianza kuzungumza nae,
“Kwani ni kitu gani kinakusumbua Sarah?”
“Najua mama yako ameshakwambia”
“Kaniambia kuhusu nini?”
“Kuwa nilikuwa na mimba na hiyo mimba imetoka”
Erick akashtuka kidogo maana hizi habari alizipata kwa Erica ila hakuziamini moja kwa moja, ila muhusika alipomuhakikishia alishangaa sana na kumuuliza kwa makini,
“Sarah unazungumzia nini?”
“Kwani hujanisikia au hujanielewa? Ndio kama ulivyoambiwa kuwa nilipata mimba na imetoka”
“Ulipataje mimba Sarah?”
“Kwani mimba inapatikanaje?”
Sarah alianza kucheka tena alicheka sana na kusema,
“Erick usiniambie hujui hata mimba inapatikanaje?”
“Wewe ni mtoto mdogo sana Sarah! Unajua kama ulichokifanya sio sawa kabisa”
“Sio sawa kitu gani, kuna mtu ambaye huwa hafanyi mapenzi?”
Erick aliona ni vyema abadilishe mada na kuanza mada zingine kwahiyo alianza kumpa pole tu maana aliona kama angeendelea na mada ile basi ingekuwa ni ngumu sana kuelewana na Sarah,
“Pole sana Sarah”
“Ila haya yote umeyataka wewe Erick”
“Kivipi sasa?”
“Wewe ndio chanzo cha mimi kupata mimba na wewe ndio chanzo cha mimi kuchoma sindano na mwisho wa siku ile mimba ikatoka kabisa”
“Unaongelea nini wewe? Unadhani mimi naweza kufanya huo upuuzi? Kwanza hiyo kwangu ni dhambi”
“Dhambi unaijua wewe! Yani hata usijitetee kwa lolote, maana wewe ndio chanzo cha kila kitu”
“Duh!! Kwaheri”
Erick hakuweza kukaa zaidi, basi aliinuka na kutoka kabisa, aliwaaga na kuondoka zake kwani hata hakumuelewa Sarah na wala hakutaka kumuelewa. Muda huu aliingia Elly chumbani kwa Sarah na kuanza kuongea nae,
“Ulikuwa unaongea nini na Erick?”
“Nilikuwa namwambia ukweli kuwa mimi nilikuwa na mimba na imetoka ndio alikuwa akishangaa kuwa mimba nimeitoa wapi, yani huyu Erick huwa anaongea kama sio mwanaume vile”
“Mmmh usiseme hivyo, mimi naogopa mama akijua ukweli maana atanifukuza hapa”
“Kwa usalama wako nishakwambia usiondoke kabisa mahali hapa yani endelea kuishi hapa hapa sababu ukiondoka tu basi niotasema ukweli wa mambo ulivyo”
“Mmmmh hata nikiwepo, ukikazaniwa na mama yako hutonitaja!”
“Subiri wakikazana kuniuliza kuna kitu nitakifanya, tulia tu”
“Mmmh kitu gani Sarah?”
“Wewe tulia tu, utaona itakavyokuwa”
Basi Elly alimuangalia tu Sarah bila ya kusema kitu kingine chochote kile.
Mama Angel alijikuta akijiwa na moyo wa huruma tu, kwani huwa akisikia mtoto anaumwa anasikia kuteseka sana moyoni, basi akahitaji kwenda kumuona.
Ikabidi yeye na Tumaini huku wakiongozana na Siku wakaenda hadi chumbani kwa Sarah na kumkuta amekaa huku akilalamika tumbo, walipoingia tu alianza kutapika, wakati wanamuhamisha ili wamfute yale matapishi walikuta kuna damu nyingi sana zinamtoka.
Hapo wakaona kuwa huyu mtoto anahitaji tiba ya haraka sana, kwahiyo ilibidi mama Angel aanze kumuandaa kwaajili ya kwenda nae hospitali, yani Sarah hata hakuwa na maelezo yanayoeleweka juu ya hali yake.
Wakatoka nae na moja kwa moja kuanza nae safari ya kwenda hospitali, Siku alibaki nyumbani huku akiwaangalia tu maana alihitaji kubaki na kuangalia nyumba kwani alijua wazi kama mama yao angerudi na kutokuwakuta wote ingekuwa balaa.
Baada tu ya wale kuondoka, ndipo Elly aliporudi nyumbani na kumkuta Siku yupo nje anafua, alienda ndani kumuangalia Sarah aliyemuacha mgonjwa ila hakumkuta, ikabidi arudi nje kumuuliza Siku aliyekuwa anafua,
“Yuko wapi Sarah?”
“Oooh Sarah ni mgonjwa, yani anaumwa sana kwahiyo walikuja hapa wale wakina mama Erick ndio wamempeleka hospitali”
“Alizidiwa sana au?”
“Aaaah si unajua wale wana viherehere sana, mama si ameondoka kamuacha Sarah anaumwa hapa wala hakuwa na tatizo kwani alijua lazima atapona tu, ila wao sasa na viherehere vyao yani wamemchukua na kumpeleka hospitali”
“Sasa hata hujui ni hospitali gani wamempeleka, wasiporudi nae je?”
“Kwani kwao hapafahamiki? Tutaenda nyumbani kwao, waache wahangaike nae huko, watamrudisha tu”
Basi Elly akatamani kujua kuwa Sarah alikuwa akisumbuliwa na nini, ila kwa muda huo njaa nayo ilikuwa ikimsumbua maana aliondoka bila ya kula chochote, akamwambia Siku,
“Si chai ipo eeeh! Ngoja nikakoroge ninywe”
Muda huo huo Siku aliacha kufua na kumwambia Elly kuwa anaenda kumuandalia chai, basi moja kwa moja aliingia nae ndani, na kumuandalia chai kweli ambapo Elly alikunywa na kujihisi vizuri, baada ya hapo Siku alimletea Elly juisi na kumtaka ashushie kwa ile chai aliyokunywa,
“Mmmh nimeshiba sana”
“Aaaah kwetu kukataa mtu kitu alichokuandalia ni vibaya kabisa, naomba unywe hata kidogo”
Basi Elly alichukua ile glasi na kunywa kidogo ila baada ya kunywa tu alijihisi kulewa yani kama mtu aliyekunywa pombe, basi Siku alifunga milango na kumchukua Elly kwenda nae chumbani kwake, na kuanza kumpapasa, na kuweza kulala nae sababu tu Elly hakujielewa na ile hali ya kuwa kama amelewa.
Yani Elly alivyokuja kurejewa na fahamu zake aliumia sana kwenye moyo wake kwani hakutegemea kufanya kile kitu na Siku,
“Kwanini umenifanyia hivi dada?”
“Nilikuwa nakutamani sana Elly kwa muda wote, yani kila siku nilikuwa nakutamani sana. Nashukuru leo nimepata nafasi, huu ni mwanzo najua sasa utakubali kwa hiyari yako”
Elly alichukia sana, na kutoka mule chumbani kwa Siku na kwenda chumbani kwake huku akiwa amechukia sana.
Wakina mama Angel walifika hospitali wakiwa na Sarah na moja kwa moja alipelekwa kwenye matibabu, basi walitulia huku wakisikilizia kuwa itakuwaje. Mama Angel aliamua kumpigia simu mama Sarah ila ile simu iliita sana hadi kukatika yani hakuna cha maana alichokipata.
Baba Angel akasema,
“Haya mambo ndio huwa siyapendi, kweli mama wa mtoto anaondoka na kuacha mtoto wake anaumwa jamani”
“Labda alijua anaumwa kidogo”
“Kidogo, hakumuangalia vizuri, kwa zile damu zilizomtoka inaonyesha ni muda mrefu tatizo lilianza”
Waliongea kidogo pale huku baba Angel akifatilia hali ya yule mtoto Sarah, badae daktari alikuja na kuhitaji mzazi wa yule mtoto, sababu wale ndio walimpeleka na kudai kuwa ni ndugu wanaoishi na yule mtoto ilibidi tu awaambie kinachomsumbua yule mtoto,
“Ni hivi jamani, inaonekana mtoto alikuwa na mimba changa sasa imetoka”
Wote wakashangaa sana, mama Angel aliuliza,
“Jamani, mtoto mdogo kama Sarah anatoa wapi mimba?”
Tumaini akadakia na kusema,
“Kila siku huwa nasema sana kuhusu malezi mabovu, kwani Daima kapata vipi ile mimba aliyoipata? Watoto wa siku hizi wana mambo sana”
Basi daktari akaondoka kuendelea na huduma kwa yule mtoto kwani ilibidi wamsafishe, kwakweli baba Angel aliwaambia,
“Jamani, mimi naondoka mtaniambia yatakayojiri. Sitaki habari za watoto wasiojielewa kama huyo”
Baba Angel aliondoka zake na kumuacha pale Tumanini na mama Angel, ila muda kidogo Tumaini nae aliondoka zake na kumuacha pale mama Angel, yani mama Angel alishindwa kuondoka bila ya kuruhusiwa kuondoka na Sarah, kwahiyo hakutaka kuondoka kabisa.
Tumaini akiwa njiani akielekea nyumbani kwake, ndipo alipokutana na mama Sarah, alimsimamisha na kuanza kuongea nae,
“Kheee unajua nilikuwa sikujui kabisa mambo yako, kumbe wewe mwanamke ni mbaya kiasi hiki”
“Kwani nimefanyeje?”
“Unawezaje kuondoka na kumuacha mwanao mgonjwa ndani au ulikuwa ukijua ni kitu gani kinamsumbua mwanao?”
“Kwahiyo ulikuwa nyumbani kwangu?”
“Ndio, tulikuwa na kikao na wewe kwani tulikuwa tukihitaji kujua ukweli kuhusu mtoto Sarah, ila hatujakukuta na kumkuta mtoto akiumwa vile nyumbani kwako”
“Kheee jamani, Sarah alikuwa anaumwa tumbo tu wakati naondoka. Siwaelewi imekuwaje?”
“Imekuwaje kuhusu nini? Mwanao katoa mimba huko”
“Katoa mimba? Hiyo mimba Sarah aitoe wapi? Mbona mnataka kuchekesha walionuna”
“Ndio hivyo, nenda hospitali huko kamfate mwanao. Umemkuta Erica hana roho mbaya na ndio kabaki na mwanao hospitali, nenda kamuangalie huko. Nilikusema sana kwa malezi mabaya unayompa Sarah, nadhani umeona matunda yake sasa”
Tumaini akamuelekeza tu hospitali aliyolazwa Sarah na kuachana nae pale.
Walipomaliza kumuhudumia Sarah na kila kitu ndio wakampa ruhusa mama Angel aweze kurudi nae nyumbani, daktari aliongea tu na mama Angel kiasi kidogo pale,
“Mpeni mtoto elimu stahiki, kumbe alikuwa mjamzito halafu akaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango, imeenda kuharibu ile mimba na ndiomana kaumwa sana, hebu muwe makini sana na hawa watoto wenu, mtawapoteza mjue.”
Basi akapewa na dawa zitakazoweza kumsaidia kwa kipindi hiko, mama Angel akaondoka sasa na Sarah yani alikuwa akimuangalia bila ya kummaliza kwakeli, basi akawa anaondoka nae huku akiendesha gari na kumuuliza baadhi ya maswali,
“Kwanza Sarah ulipata vipi hiyo mimba?”
Sarah alikuwa kimya tu huku akiinama chini, mama Angel alipumua kidogo na kumuuliza tena,
“Na ilikuwaje hadi ukaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango?”
Bado Sarah alikuwa kimya tu, basi mama Angel akamwambia,
“Utaniambia vizuri ukiwa vizuri, nakuhurumia sana, wewe Sarah bado ni mtoto mdogo sana”
Basi walifika nyumbani kwakina Sarah na Sarah kuingia ndani na moja kwa moja mama Angel alimpeleka Sarah chumbani ili aweze kupumzika, ila wakati anatoka tu chumbani kwake alikutana na mama Sarah ambaye ndio alikuwa ametoka kufika,
“Yani nimetoka hadi kwenye ile hospitali mliyoenda nikaambiwa kuwa mmetoka, kwanza nakushukuru kwa hili ulilolifanya kwani mwanangu anaumwa nini?”
“Yani unakaa na mwanao kweli hujui tatizo lake? Mwanao alikuwa ni majamzito, kaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango sijui basi ile sindano imeenda kuharibu ile mimba na kumfanya aumwe sana, na hiyo hali imefanya apoteze damu nyingi sana. Anatakiwa kula vizuri na kuna dawa nimemuachia hapo ambazo walimuandikia”
“Oooh nashukuru sana, sikutegemea kama ungefanya kitu cha namna hii, asante sana Erica”
“Usijali, watoto hawa ni wa kwetu sote. Ila dokta kasisitiza sana juu ya malezi tunayowapa watoto, tunatakiwa kuwa makini sana”
“Asante”
Basi mama Angel alimuaga na kuondoka zake, kwakweli hata yeye alishangaa mno kuona jinsi mama Sarah alivyokuwa mpole kwa siku hiyo.
Moja kwa moja mama Sarah alienda chumbani kwa mwanae na kumuangalia, basi alikaa karibu yake na kumuuliza,
“Mwanangu kwani hiyo mimba umepataje?”
“Sijui hata nimepataje”
“Nani alikupeleka kwenda kuchoma hiyo sindano ya uzazi wa mpango?”
“Sijui mama, nimechoka sana. Hali yangu sio nzuri kabisa, kwasasa nahitaji kupumzika”
“Pole sana mwanangu, Mungu atakusaidia utapona tu”
Kisha mama Sarah alitoka na kumtaka Siku amuandalie chakula Sarah ili aweze kwenda kumlisha kikiwa tayari. Siku hii mama Sarah hata hakujua kama ataweza kutoka kwa ile hali ya mtoto wake.
Mama Angel alirudi nyumbani kwake wakati hata giza limeanza kuingia na kumkuta mumewe akiwa amejilaza tu kwa muda huo, basi alienda kuoga na kurudi kuongea na mume wake,
“Ila mume wangu jamani, ndio kuniacha mwenyewe hospitali”
“Kiukweli huwa sipendi ujinga wa watoto wa kike kamavile kwakweli, mtoto anabeba mimba kwa umri mdogo vile! Na kwanini imetoka sasa?”
“Sijui alikuwa na mimba halafu akaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango”
“Aaaargh katoto kana tabia mbaya hadi kamewaza kwenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango jamani!! Si umri wakina Erica yule aarrgh!”
“Unajua watoto tusiwalaumu sana vitu vingine hawajui”
“Hawajui wapi? Mtoto anajua kabisa nitapata mimba ndio kaenda kuchoma sindano ya uzazi wa mpango ili asipate na aendelee kufanya kwa raha zake, naye ni mtoto huyo? Hata sitaki tena awe karibu na watoto wangu maana atawafundisha tabia mbaya”
“Aaaah usiseme hivyo mume wangu, mimi nina uhakika Sarah hajapata mtu wa kuongea nae na kumuelewesha vizuri kwani nina hakika angeeleweshwa vizuri basi yote haya yasingetokea”
“Aeleweshwe nini na mtoto kashapata utamu wa tunda?”
Mama Angel alicheka tu, kisha baba Angel akauliza tena,
“Je umemuuliza nani muhusika wa hiyo mimba iliyotoka? Umemuuliza ni nani aliyempeleka kwenda kuchoma hiyo sindano ya uzazi wa mpango?”
“Nimemuuliza kabaki kimya tu, anaona aibu ila nasubiri apone vizuri nitamuuliza”
“Utamuuliza nini sasa? Si ndio wakina Daima hao? Toto limefata tabia mbaya ya mama yake lile aaargh”
Baba Angel alionekana kutokupenda kabisa lile jambo ambalo Sarah amelitenda kwahiyo kwa muda huo aliamua kulala tu wala hakutaka matatizo mengine.
Kulipokucha, Baba Angel alijiandaa na kwenda kazini kama kawaida na wakina Erica walienda shuleni kwahiyo pale nyumbani alibaki tu mama Angel, Vaileth na Ester kama kawaida.
Basi mama Angel alianza kumsimulia Vaileth kitu ambacho kimejiri kwa Sarah,
“Yani nimeumia sana kwa mtoto mdogo kama Sarah kupata ujauzito loh! Halafu kaenda kutumia sindano ya uzazi wa mpango jamani”
“Sasa nani kampa Sarah mimba?”
“Anataka kusema basi!! Sijui imekuwaje, yani mimi nina wasiwasi sana yasije kuwa mambo kama ya Daima”
“Jamani”
“Roho imeniuma sana, huwa namuona Sarah kama mtoto wangu, huwa namuona Sarah kama ninavyomuona Erica tu. Nimeumia sana”
“Kweli ni mdogo sana, kaanza mapenzi basi ndiomana akapata hiyo mimba, hadi imetoka dah!”
Mara mlango ulifunguliwa na aliyefungua mlango alikuwa ni Erica, basi mama yake alimuuliza kilichomfanya arudi mapema vile,
“Tumbo mama linaniuma sana”
Mama Angel akashtuka maana hofu ikamjaa kuwa isijekuwa mambo yale yale ya Sarah, basi alienda nae mwanae chumbani na kumuuliza vizuri,
“Ni tumbo gani linakuuma mwanangu”
“Tumbo la kikubwa mama”
Hapo mama Angel alielewa vizuri kabisa kitu kinachomsumbua mtoto wake.
Baada ya muda Erica alimfata Vaileth ambae kwa muda huu alikuwa chumbani kwake na kuanza kumuuliza,
“Ni nani mliyekuwa mnamzungumzia kuwa katoa mimba?”
“Ni Sarah huyo, yani kumbe mtoto mdogo ana mambo ya ajabu”
“Kheee Sarah kaanza mambo ya wanaume!! KWahiyo naye kapata mimba kama Daima?”
“Ndio ila imetoka, yani Sarah kafanya mchezo wa ajabu sana”
“Kheee kumbe!!”
Basi Erica aliridhika kwa muda kuipata habari hiyo maana alishindwa hata kupumzika kidogo bila kujua kilichokuwa kikizungumziwa na mama yake pamoja na Vaileth pale sebleni, kwahiyo alivyojua aliweza kuridhika na moyo wake sasa.
Baba Angel akiwa ofisini kwake leo alitembelewa na Sia, na kushangaa ila alimkaribisha na kumuuliza,
“Ndio ushapata jibu la utafiti wako juu ya aliniwekea sumu?”
Kidogo Sia alijiuma uma na kusema,
“Hiko sio kilichonileta ila kilichonileta ni swala lingine kabisa”
“Swala gani?”
“Hivi kwanza unajua kama Erica amewahi kuwa na mahusiano na Derrick? Ni ndugu yake ila amewahi kuwa na mahusiano nae”
“Hayo hayanihusu kabisa, kinachonihusu sasa ni kuwa Erica ni mke wangu halafu Derrick ni shemeji yangu”
“Duh!! Yani wewe Erick ni wa ajabu sana”
“Sema lingine ulilokuja nalo”
“Ni kuhusu mtoto Elly”
“Eeeeh una story mpya kuhusu Elly au kitu gani? Hebu sema ukweli kuwa Elly ni mtoto uliyezaa na Derrick”
“Hapana, mimi sijazaa na Derrick. Ngoja leo nikwambie ukweli”
“Haya, niambie nakusikiliza”
“Mimi kiukweli kabisa nilizaa na Steve yani huo ndio ukweli halisi”
Baba Angel alicheka kwanza na kusema,
“Ila wewe mwanamke jamani dah!! Nakusikiliza vizuri sana, na ulivyokuwa umekazana kuwa umezaa na mimi ni nini?”
“Sikiliza basi, ni hivi mimi siku nimeenda kujifungua nilienda kabla hata ya muda ila mwanangu alikuwa vizuri tu, sema hakuzaliwa kwa uzito ule uliotakiwa, basi ikapewa yule mtoto ila alikuwa akilia sanaalipokuwa kwangu. Baba yako mzee Jimmy alikuja kuongea nami, yani aliongea na mimi kabla sijajifungua na akaongea na mimi baada ya kujifungua, alipanga nami mpango wa kubadilisha mtoto wangu na mtoto wa Erica, nilikubali sababu ya shida yangu ya hela, mtoto alipofika miezi mitatu kasoro ndipo mzee Jimmy alipowabadilisha, kwamaana hiyo Elly ni mtoto wa Erica halafu Erick ni mtoto wangu ndiomana nilikuwa nakukazania kuwa nimezaa na wewe kwani nilijua hata mwanangu akipimwa damu atakutwa ni mwanao kweli yani Elly. Ila baada ya sokomoko hili la kusema kuwa Elly ni mtoto wa Derrick basi kuna uhakika kabisa kuwa Erica aliendelea na Derrick kwahiyo Elly na Erica mdogo wote ni watoto wa Derrick maana mtoto wangu mimi ni Elly”
“Uwiii sijakuelewa hata jambo moja ulilonieleza Sia”
“Hujanielewa kivipi? Ushahidi pia ninao kuwa mimi na baba yako tulibadilisha watoto”
“Mlibadilisha wakiwa na umri gani?”
“Miezi mitatu kasoro”
“Mbona wanangu walipomaliza mwezi tu niliondoka nao na mama yao tukaenda Afrika kusini na tulirudi huko baada ya miaka mitatu, unajua sikuelewi kabisa”
“Nitakuletea ushahidi basi, mimi sio chizi kusema kila siku kuwa Erick ni mtoto wangu. Ila ndio hivyo mkeo alikusaliti huyo ndiomana imekuwa hivyo”
“Nenda tu Sia, ila mke wangu awe alinisaliti au hakunisaliti bado nitampenda hadi mwisho wa maisha yangu”
“Duh!! Ni mzima kweli wewe?”
“Ni mzima kabisa, nilishasema hata nimfumanie hapo mke wangu basi nitamsamehe maana nampenda sana”
“Mmmmh!! Shukuru Mungu mkeo hana hayo mambo siku hizi”
“Ndiomana nimemuoa kwnai najua sio mwanamke wa kutangatanga tangu zamani”
“Sio wa kutangatanga wapi, angetembea na ukoo mzima huyo! Unamtetea tu”
“Alikuwa akitafuta penzi la kweli ila mke wangu katulia sana na nina mpenda sana, hakuna kinachoweza kututengenisha”
“Ngoja nikapekue vizuri ule ushahidi nikuletee”
Sia aliamua kuondoka zake maana aliona hakuna ushirikiano wowote kwa baba Angel ila alimuahidi kumletea ushahidi kwa yale aliyoyasema.
Baba Angel siku hii baada ya maneno ya Sia, aliamua kupitia dukani kumnunulia mkewe zawadi, kwnai yale maneno ya Sia yalimuingia sikio la kushoto na kutokea sikio la kulia, alienda moja kwa moja kwenye duka ambalo huwa ananunua na leo alimkuta baba Emma na kufurahi kwani alijua kuwa atamchagulia kitu ambacho mke wake atakipenda sana.
Alipofika pale tu baba Emma alimuonyesha zawadi ya kumpelekea mke wake,
“Leo mpelekee tu hiki kikoi nina uhakika atakipenda sana”
“Mmmh atapenda kikoi mke wangu kweli!”
“Kweli atakipenda sana, ni kizuri hiki hakuna mwanamke ambaye atakiona na kukichukia”
Basi baba Angel alimchukulia mkewe kile kikoi na moja kwa moja kurudi zake nyumbani kwa mke wake.
Leo alipofika tu ndani moja kwa moja alimuonyesha mke wake ile zawadi aliyomchukulia, kwakweli mama Angel alifurahi sana na kumwambia mume wake,
“Ulijuaje kama nataka kikoi jamani mume wangu? Kweli wewe ni kiboko yangu. Nimependa sana hiki kikoi mume wangu, asante sana.”
Muda wote mama Angel alikuwa akikitazama tu kile kikoi ilionyesha ni jinsi gani amekipenda kile kikoi.
Usiku wa siku hii, Erica alienda moja kwa moja chumbani kwa kaka yake Erick na kuanza kuongea nae kuhusu kile alichosikia kuhusu Sarah,
“Umesikia hayo yaliyopo huko”
“Mmmh umeanza Erica, mambo gani hayo?”
“Kumbe Sarah alikuwa na mimba kwahiyo imetoka”
“Mmmh alikuwa na mimba!! Jamani, Sarah kapata wapi mimba?”
“Kapata wapi? Kwani wewe hujui mimba inapatikanaje?”
Erick alimuangalia nduguye bila ya kumjibu kitu na kuamua kuanza kumueleza mambo mengine,
“Hivi zile karata siku hizi unacheza mwenyewe? Leo nije tucheze wote?”
“Hapana, leo sichezi karata”
“Kwanini?”
“Subiri baada ya siku tatu ndio nitacheza karata”
“Kwanini?”
“Siri yangu, usiku mwema”
Kisha Erica aliondoka zake na kumuacha Erick pale akimshangaa tu na kujiuliza kwanini Erica kasema vile kuhusu kucheza karata mpaka baada ya siku tatu, hakumuelewa kwakweli.
Leo Erick alipokuwa shuleni aliamua kumuuliza Elly kuhusu Sarah kwani ni kweli hakuonekana shuleni, basi alikaa nae na kuanza kumuuliza,
“Vipi Sarah anaendeleaje?”
“Kheee mbona umeniuliza mimi!”
“Nasikia anaumwa, na wewe ulisema kuwa upo nae karibu”
“Ndio anaumwa, ila twende ukamuone sio kuniuliza uliza maana hilo sio jukumu langu”
“Duh!! Basi tutaenda badae baada ya masomo”
Walirudi darasani na kuendelea na masomo kama kawaida, ila vipindi vilivyoisha, Elly alimkumbusha tena Erick swala la kwenda kumuona Sarah, ni kweli Erick alikubali na moja kwa moja kuondoka na Elly kuelekea nyumbani kwakina Sarah.
Walipofika, walimkuta Sarah yupo chumbani, basi Siku alienda kumuita na kumwamnbia kuwa,
“Erick kaja kukuona”
“Oooh mwambie aje kuniona chumbani”
Ikabidi Siku ampelekee ujumbe ule Erick, na muda ule Erick na Elly waliingia pamoja chumbani kwa Sarah ila Sarah aliomba kuzungumza na Erick kwahiyo alihitaji Elly asubirie kwanza, na Elly alifanya vile basi Erick alianza kuzungumza nae,
“Kwani ni kitu gani kinakusumbua Sarah?”
“Najua mama yako ameshakwambia”
“Kaniambia kuhusu nini?”
“Kuwa nilikuwa na mimba na hiyo mimba imetoka”
Erick akashtuka kidogo maana hizi habari alizipata kwa Erica ila hakuziamini moja kwa moja, ila muhusika alipomuhakikishia alishangaa sana na kumuuliza kwa makini,
“Sarah unazungumzia nini?”
“Kwani hujanisikia au hujanielewa? Ndio kama ulivyoambiwa kuwa nilipata mimba na imetoka”
“Ulipataje mimba Sarah?”
“Kwani mimba inapatikanaje?”
Sarah alianza kucheka tena alicheka sana na kusema,
“Erick usiniambie hujui hata mimba inapatikanaje?”
“Wewe ni mtoto mdogo sana Sarah! Unajua kama ulichokifanya sio sawa kabisa”
“Sio sawa kitu gani, kuna mtu ambaye huwa hafanyi mapenzi?”
Erick aliona ni vyema abadilishe mada na kuanza mada zingine kwahiyo alianza kumpa pole tu maana aliona kama angeendelea na mada ile basi ingekuwa ni ngumu sana kuelewana na Sarah,
“Pole sana Sarah”
“Ila haya yote umeyataka wewe Erick”
“Kivipi sasa?”
“Wewe ndio chanzo cha mimi kupata mimba na wewe ndio chanzo cha mimi kuchoma sindano na mwisho wa siku ile mimba ikatoka kabisa”
“Unaongelea nini wewe? Unadhani mimi naweza kufanya huo upuuzi? Kwanza hiyo kwangu ni dhambi”
“Dhambi unaijua wewe! Yani hata usijitetee kwa lolote, maana wewe ndio chanzo cha kila kitu”
“Duh!! Kwaheri”
Erick hakuweza kukaa zaidi, basi aliinuka na kutoka kabisa, aliwaaga na kuondoka zake kwani hata hakumuelewa Sarah na wala hakutaka kumuelewa. Muda huu aliingia Elly chumbani kwa Sarah na kuanza kuongea nae,
“Ulikuwa unaongea nini na Erick?”
“Nilikuwa namwambia ukweli kuwa mimi nilikuwa na mimba na imetoka ndio alikuwa akishangaa kuwa mimba nimeitoa wapi, yani huyu Erick huwa anaongea kama sio mwanaume vile”
“Mmmh usiseme hivyo, mimi naogopa mama akijua ukweli maana atanifukuza hapa”
“Kwa usalama wako nishakwambia usiondoke kabisa mahali hapa yani endelea kuishi hapa hapa sababu ukiondoka tu basi niotasema ukweli wa mambo ulivyo”
“Mmmmh hata nikiwepo, ukikazaniwa na mama yako hutonitaja!”
“Subiri wakikazana kuniuliza kuna kitu nitakifanya, tulia tu”
“Mmmh kitu gani Sarah?”
“Wewe tulia tu, utaona itakavyokuwa”
Basi Elly alimuangalia tu Sarah bila ya kusema kitu kingine chochote kile.