Simulizi : Nguvu ya Mapenzi

SEHEMU YA 388

Rahim alimkaribisha baba Angel kwenye ile ofisi ambapo walikuwa wawili tu na kuanza kuongea nae alichotaka kuongea nae, ila kabla ya yote baba Angel alimshukuru kwanza kwaajili ya kumtambulisha baba yake kwenye biashara yake,
“Nashukuru sana Rahim, sikujua kama ungefanya kitu kama hiki”
“Sina ugomvi na wewe, najua ugomvi wetu mkubwa huwa upo kwenye mapenzi sababu wote tumempenda mwanamke mmoja ila bado sio sababu ya mimi kugombana na wewe kila mara. Mara nyingi huwa nipo na pombe kichwani ndiomana nakujibu vibaya na kugombana na wewe ila sio kwa akili zangu timamu. Usijali kuhusu hilo, kumbuka kabla ya yote tumewahi kuwa marafiki wazuri sana, na tukiambiana kila kitu, kwahiyo bado nakumbuka mazuri tuliyotenda pamoja”
“Oooh sawa, ni vizuri sana”
“Sasa nilichokuitia ni kuhusu Angel”
Baba Angel akashtuka kidogo na kumsikiliza Rahim ambapo Rahim aliendelea kuongea,
“Yule binti kawa mkubwa kwasasa, nakumbuka pale shuleni hata nilivyomfata kumsalimia alinikwepa. Kama mzazi iliniuma sana ile kitu, na jinsi Angel alivyokaribu na wewe nikaumia zaidi, nakuomba jambo moja mwanaume mwenzangu, naomba Angel atambue ukweli, naomba Angel anitambue baba yake halisi na anipokee kama baba yake halisi, yani Angel ajue kama mimi ni mwanae”
Baba Angel akapumua kidogo na kusema,
“Dah, ila hilo swala ni gumu sana kuongea mimi”
“Najua ni ngumu sababu Angel amekuzoea sana, siku zote anajua kuwa wewe ni baba yake, hana wazo kuwa kuna kiumbe sijui baba mwingine wa kuitwa Rahim, naomba fanya lolote ili Angel atambue uwepo wangu”
“Labda niongee na mama yake ndio amwambie”
“Sijui kama atakubali ila najua wewe ni mwanaume pekee unayeweza kumshawishi Erica kuongea na mwanae ukweli wa mambo yote”
“Ila Rahim, unajua una makosa sana, kipindi kile niliweka utaratibu mzuri tu wa mtoto kuweza kukutambua wewe kama baba yake ila wewe ukataka kufanya mambo mengine”
“Sikatai, ni kweli nilifanya makosa yani hilo nakiri kabisa, nisamehe na Mungu anisamehe. Kweli ni mara nyingi sana nilitaka kumbaka Erica, sababu bado nilikuwa na mapenzi nae, nilijilaumu sana kuoa mwanamke ambaye hakuwa chaguo langu sababu yule alikuwa chaguo la baba, na mimi nilikubali tu kwa kutumiwa picha zake, niliporudi nikawa nae yeye, huwa najiona mjinga sana kumuacha mwanamke kama Erica ambaye kwa kipindi kile alikuwa tayari kwa chochote kile kwaajili ya mtoto ila mimi nilikuwa mjinga sana. Naomba hayo yaishe, ila naomba ongea na Erica amwambie ukweli Angel, amueleze kuwa mimi ni baba yake halisi ili Angel anithamini na kuniamini”
“Sawa, nitajaribu kuongea nae kuhusu hilo kwani Angel kawa mkubwa kwasasa anatakiwa kujua ukweli”
“Asante sana Erick, nashukuru sana kwa hilo yani utakuwa umenisaidia kwa kiasi kikubwa sana, natamani sana mtoto wangu anifahamu”
Basi baba Angel aliagana na Rahim kisha yeye kuondoka zake na kurudi nyumbani kwake huku kichwa chake kikiwa na mawazo mengi sana.

Usiku wa leo, wakati baba Angel yupo chumbani na mke wangu akaamua kumueleza lile swala la kukutana na mwarabu ya kuwa Rahim ni mtoto wa yule mwarabu na kitu ambacho Rahim kakifanya kumjulisha yule mwarabu kuhusu bidhaa zao,
“Mmmh Rahim huyo ndio kamfahamisha yule mwarabu kiwanda chetu!”
“Ndio, ni yeye. Mwarabu mwenyewe kasema hilo”
“Basi Rahim huwa anajichetua tu, kumbe mara nyingine anajielewa. Tunamshukuru kwa hilo”
“Ila kuna jambo lingine”
“Lipi hilo?”
Baba Angel aliamua kumwambia mama Angel kuhusu kile ambacho Rahim amekisema kuhusu kutambulishwa kwa Angel, basi mama Angel akasema,
“Kheee ndiomana kumbe kumtambulisha baba yake kiwanda chetu ili tuweze kumfahamisha kuhusu Angel! Aaaargh alivyokuwa akifanya ujinga hakujua kama kuna siku itabidi amfahamu Angel kwa undani zaidi?”
“Kaomba msamaha, ila mke wangu ni kweli ana haki ya kufahamiana na mtoto wake”
“Mimi simtambui Rahim, ninachojua ni kuwa Angel ni mtoto wako”
“Ila mama Angel twende mbele na kurudi nyuma, wakati unamwambia Rahim kuwa una ujauzito wake alikataa?”
“Hapana”
“Kipindi cha mimba alikuwa hakuhudumii?”
“Hapana, alikuwa akinihudumia vizuri tu hata akanipangia chumba maana niliogopa kurudi nyumbani na mimba, mama algundua siku ya mwisho mimi kwenda kujifungua”
“Ila unajua kuwa kuna mabinti wanabeba mimba na kukataliwa pindi anapomwambia mwanaume tu kuwa nina ujauzito wako?”
“Najua”
“Wewe chanzo cha Rahim kuacha kuhudumia mtoto na mengine ni kitu gani?”
“Kwakweli sijui, ila nakumbuka kila nikimwambia njoo kwetu anasema nitakuja nitakuja, halafu toka nilipojifungua ndipo Rahim alipoanza kupunguza matumizi kwangu kanakwamba hakumtaka tena mtoto. Hata nimwambie kitu gani hakuwa na muda wa kunisaidia kabisa, nakumbuka niliongea na dada zangu wakaniambia kama mwanaume ana pesa, muombe basi hela ya mtaji ili angalau upate cha kujishikisha uweze kulea mtoto wako, kwakweli hela Rahim alikuwa nayo wala sio hela ya kubabaisha, nikamuomba hela ya mtaji. Nakiri kwamba nilimuomba hela kubwa ila hakutakiwa kunijibu kitu ambacho alinijibu”
“Ulimuomba pesa ngapi?”
“Nakumbuka wazi, nilimuomba milioni kumi na tano ili nifungue biashara ya kuuza vitu vya watoto. Ni bora Rahim angenijibu kiustaarabu kuwa sina hiyo pesa au mimi nina kiasi kadhaa kwahiyo fikiria biashara nyingine, ila hapana alianza kunikejeli alinitusi sana, niliumia sana moyo wangu hadi akasema nimemfanya yeye ndio tegemeo langu na familia yangu kwasababu sisi ni masikini, akaniambia badala nimuombe elfu kumi ya mtaji eti namuomba milioni kumi na tano, nafikiri pesa inaokotwa, yani alinijibu kwa kejeli sana. Toka hapo ikawa ndio kama nimemfukuza kwani hakutaka tena kuwasiliana na mimi, hakutaka kujua habari za mtoto wala kumsaidia mtoto. Nilikuwa nalia tu, kumbuka ndio nilitoka kumaliza chuo, sikuwa na kazi wala chochote cha kuniingizia pesa, niliona maisha mabaya sana, nikikaa kidogo mama ananisema sana kuwa mimi ni mjinga kwa kuzaa mtoto asiye na baba. Yote aliyoyafanya Rahim sikuhesabia kama ni kosa ila swala la kutokutaka kumuona mtoto liliniuma sana, hakuwa na mpango wa kuja kujionyesha kwetu na wala kusema kuwa Angel ni mwanae. Nakumbuka hadi nilimwambia Rahim kama kikwazo ni dini basi mimi nipo radhi kubadilisha dini ili tulee mtoto pamoja, ila Rahim alinikataa kabisa. Unadhani ningefanya nini? Kumpeleka mtoto kwa baba asiyemtaka kweli?”
Baba Angel alipumua kidogo na kuongea tena na mke wake,
“Hilo kweli ni kosa, tena kosa kubwa tu alilolifanya ila nadhani ni upepo mchafu ambao ulimpitia kiasi cha kukataa kufahamishwa vizuri kwa mtoto aliyemuhudumia toka tumboni. Ila mimi kama mwanaume najua ni jinsi gani wanaume tulivyo na makosa, nakuomba mke wangu shusha moyo na upunguze presha, mwambie Angel ukweli wa mambo ili amjue baba yake halisi”
“Kwani umechoka kumlea Angel?”
“Hapana sijasema hivyo ila Angel ana haki pia ya kujua ukweli, yani yeye ndio atakuwa na maamuzi ya mwisho ila muweke wazi aufahamu ukweli”
“Dah!! Hiyo kitu naiona ni ngumu sana kwangu”
“Jitahidi mke wangu”
“Nitajaribu, ila sijui kama nitaweza kwakweli”
Kwa siku hiyo mama Angel alijihisi hata kutokupata usingizi kabisa, alikuwa akigeuka huku na huko akiwaza jinsi ambavyo Angel atachukulia hilo swala la kuambiwa ukweli halisi wa maisha yake.

Siku hii, mama Angel baada ya kazi za hapa na pale alimwambia Angel kuwa anahitaji kutoka nae sababu ana maongezi nae, hakufikiria kama lile jambo anaweza kuongea na Angel pale nyumbani.
Basi alitoka na Angel moja kwa moja alienda nae ufukweni na kuanza kuongea nae,
“Mwanangu Angel, leo nataka kukwambia ukweli”
“Ukweli gani huo mama?”
“Nisikilize kwa makini”
Angel alitulia na kumskiliza mama yake,
“Katika maisha yangu, kuna mwanaume mmoja nilikutana nae, niliamini ananipenda sana kwani alikuwa akionyesha mapenzi ya kweli kwangu na hata pesa alikuwa akinipatia, ila nikaja kupata ujauzito wake hapo ndio palianza kuwa na utata. Baada ya kujifungua alikataa kabisa kuja nyumbani kwetu na kufanya nitukanwe sana, nidharauliwe na kuitwa malaya kuwa niliyezaa nae simfahamu, nililia sana ila ni kosa kweli nilifanya kukubali kuzaa na mwanaume ambaye sifahamu hata nyumbani kwao. Nilikuwa nawasiliana nae na ananijibu vibaya sana, na mwisho wa siku alikata kabisa mawasiliano na mimi. Kwakweli niliona dunia ikinishurutisha sana na kunikosesha furaha kabisa kwani muda mwingi nilikuwa nikilia na kumshika mwanangu aliyekuwa akijaa machozi yangu, ila Mungu mwema akatokea mwanaume mwingine na kunipenda sana, huyu mwanaume akasema kuwa yupo tayari kumlea mtoto wangu na kumpa jina lake ni kweli kamlea kwa mapenzi yote, ila sasa kajitokeza yule mwanaume wa kwanza anamtaka mtoto wake”
Hapo mama Angel alinyamaza kwanza na kuinama chini huku machozi yakimtoka, Angel alimuangalia mama yake na kumuuliza,
“Unamaanisha huyo mtoto ni mimi? Unamaanisha baba sio baba yangu?”
Mama Angel alikuwa akilia na kusema,
“Nina uchungu mwanangu Angel nina uchungu sana, sikujua kama kuna siku kama ya leo itatokea katika maisha yangu. Nilifanya makosa sana, naomba unisamehe mwanangu”
“Sijakuelewa mama, naomba unieleweshe”
“Mwanangu, Erick sio baba yao mzazi. Baba yako mzazi anaitwa Rahim”
“Hapana mama, sitaki kusikia jambo kama hilo”
“Huo ndio ukweli mwanangu”
“Yani baba sio baba yangu! Hapana mama sitaki, sitaki kusikia hivyo”
Angel aliinuka na kuziba masikio kwa mkono halafu alianz akukimbilia baharini, hapo mama Angel akaona ni jambo lingine linataka kutokea, yani aliinuka na kumkimbia Angel, alipotaka kufika kwenye maji alimdaka kwa nguvu na kurudi nae nyuma ila Angel alisema,
“Ni heri nife kuliko kuniambia kuwa baba sio baba yangu”
“Jamani Angel mwanangu kwanini lakini, nisikilize kwanza”
Kwa muda huu mama Angel hakutaka kumuacha Angel mwenyewe, zaidi zaidi alimchukua hadi kwenye gari na kumpandisha huko, kisha naye akapanda na kumwambia,
“Mwanangu Angel jamani hebu jaribu kunielewa mama yako, nina maana thabiti kukueleza sasa”
“Sitaki kukuelewa na sitakaa nikuelewe juu ya hilo, ninachojua mimi ni kuwa baba ni baba yangu na si vinginevyo”
Mama Angel alijaribu kuongea ila kwa muda huu Angel hakumjibu chochote kile mama yake, yani alikaa kimya tu ilibidi mama Angel arudi nyumbani tu na mtoto wake.
 
SEHEMU YA 389

Walipofika nyumbani, moja kwa moja Angel alienda chumbani kwake na kujifungia, kwakweli mama Angel hakujua cha kusema, aliingia chumbani kwake pia na kuchukua simu yake kisha akampigia dada yake mkubwa aitwaye Mage,
“Dada, leo nimemwambia Angel ukweli kuhusu uwepo wa baba yake”
“Oooh wow, hapo ndio umeonyesha ukomavu wa akili maana mtoto ana haki ya kumjua baba yake mzazi haijalishi ni kipi kilitokea kati yako na baba yake ila kumtambua baba yake ni haki yake”
“Ila Angel amechukia sana na hataki kukubali ukweli, muda huu kajifungia tu chumbani”
“Muache tu hata usiwe na mashaka nae, muache atulize akili yake maana huko chumbani atafikiria na kujua umuhimu wa kitu ulichomwambia. Unajua Angel anaelekea pabaya kweli maana nishawahi kumkuta mara kadhaa tu na kaka zake, maana nawatambua wale watoto kuwa ni watoto wa Rahim, si picha nzuri kwa dada na kaka kutembeleana, umefanya jambo zuri mdogo wangu”
“Kwahiyo nimuache tu kwasasa?”
“Ndio, muache mwenyewe maana hapo ndio mawazo yake yatakuwa kwa upana zaidi”
Basi mama Angel aliongea ongea na dada yake na kukata simu, hata mumewe aliporudi usiku hakumwambia kama amemwambia Angel ukweli halisi wa maisha yake badala yake alianza kuongea nae mambo mengine kabisa.

Asubuhi ya leo wakati Sia akielekea kwenye biashara yake, njiani alikutana na Rahim na kuanza kusalimiana nae huku wakiongea machache,
“Unajua Erica hakutaka kabisa kukutana nami wala kuongea nami kuhusu jambo lolote lile ila nilikuwa na mambo ya maana sana kumuambia”
“Mambo gani hayo maana ulinidokeza ila hukuniambia”
“Nilitaka kumueleza kuhusu wale mapacha wake yani Erick na Erica”
“Ni kitu gani?”
“Kwa kifupi wale watoto wanapendana tena wanapendana sana”
“Mmmh kivipi? Ni mapacha wale kwahiyo wana haki ya kupendana”
“Ni kweli wana haki ya kupendana ila wanavyopendana wale ni kwa namna tofauti”
“Kivipi?”
“Wale watoto ni mapacha ila wanatamani kuwa wapenzi”
“Mmmh kwanini sasa?”
“Ndio hiko nilitaka kuzungumza na Erica ila hajataka kunisikiliza kabisa nadhani alishauriana ujinga na mume wake, ila watajutia badae. Nilikutana na Erick ila sikumwambia haya sababu pia hata mimi nina yangu kuhusu mtoto wangu”
“Yapi hayo?”
“Nataka Angel afahamu ukweli kuwa mimi ni baba yake mzazi, anipende na kuniheshimu kama anavyompenda na kumuheshimu Erick”
“Ni kweli ila hilo jambo linahitaji muda, sio rahisi kwa mtoto kuhamisha mapenzi yake toka kwa mtu anayependa na aliyemzoea kuja kwa mtu ambaye ni mgeni kwake”
“Ila mimi ni baba yake, basi anipende kama anavyompenda Erick”
“Pia si rahisi kukupa wewe na Erick upendo sawa, kumbuka Erick anampenda sana yule mtoto na amemfanya kama mtoto wake, kwahiyo ni ngumu sana kwa Angel kuhamisha majeshi yake ya upendo kuja kwako kwa urahisi namna hiyo”
“Kwahiyo nini kifanyike?”
“Unatakiwa kuwa mpole tu kwa mtoto, huo upendo hauwezi kuja kwa haraka. Mtoto lazima wewe umuonyeshe upendo na ukaribu kwanza ndipo na yeye atajifunza kukupenda hata kwa kidogo, kwakweli Erick yule ni wa viwango vingine, anajua sana kucheza nafasi yake kama mwanaume. Kwahiyo na wewe cheza nafasi yako vizuri”
Rahim aliona aagane tu na Sia na kuondoka zake kwa muda ule.

Mama Angel alitaka kuwasiliana na mtu kwa muda ule, ila aligundua kuwa hakuwa na muda wa maongezi hivyobasi akaamua kumtuma Erica kwenda kumnunulie vocha, kama kawaida Erica aliondoka na kwenda dukani kununua vocha ila njiani wakati anarudi alikutana na Sia, basi Sia alisalimiana nae na kuanza kuongea nae pale,
“Erica, bora nimekuona leo. Naomba nikuulize maswali machache tu, upo tayari?”
“Ndio niulize”
“Eti unampenda vipi Erick?”
“Kivipi?”
“Yani nasikia unampenda Erick kama mpenzi wako”
Erica alishtuka kidogo baada ya ile kauli ya Sia na alikaa kimya kwa muda, kisha Sia alimwambia tena,
“Mbona upo kimya Erica? Hebu niambie ili nijue jinsi ya kukusaidia”
“Sio nipo kimya ila nakushangaa tu, mimi nimpende kimapenzi kaka yangu kweli! Unachoniuliza umeambiwa na nani? Hujui kama yule ni pacha wangu? Kwahiyo watu kuongozana pamoja mara zote ndio wanapendana kimapenzi? Kwenye dunia hii wenye haki ya kupendana ni wapenzi tu? Ndugu hawawezi kupendana?”
“Sijui kama umenielewa Erica, hata mimi sikuelewa wakati naambiwa hivyo mwanzoni ila nilitaka kukusaidia ndiomana nimekuuliza”
“Aliyekwambia ni mbea, maana hiko kitu hakipo. Mimi na kaka yangu hatuwezi kupendana kwa namna hiyo maana sisi ni ndugu, aliyekwambia mwamabie kuwa mimi nina mchumba wangu anaitwa Emmanuel na Erick ana mchumba wake anaitwa Emmanah, nimemaliza”
Hapo Sia aliamua kukaa kimya tu na kuagana na Erica kisha Erica akarudi kwao na kumpa mama yake ile vocha ili aweze kuwasiliana.
Mama Angel muda huo aliamua kupiga ile simu sababu alikuwa akitaka kuwasiliana na mama Junior, basi alimpigia simu muda huo na kuanza kuongea nae,
“Dada, nitakuita ili tuweze kukutana sababu watoto hawa tunataka kuwapeleka kwao”
“Kivipi? Umewapangia nyumba kwani?”
“Sasa dada unafikiri hawa nitaishi nao milele? Ni mke na mume hawa kumbuka, yani wewe na shemeji huko hata hamjifikirii kuhusu hawa watoto?”
“Mimi sijui, unajua sina kazi ndiomana nipo nipo tu ila ningekuwa na kazi labda ningejua jinsi ya kuwasaidia watoto wangu”
“Usijali, jiandae mwisho wa wiki hii tuwapeleke watoto sehemu watakayoenda kuanzisha maisha yao. Kwahiyo usijali”
Mama Junior alikubali tu kwa hali ile na kuanza kufikiria mambo mengine.

Erica alimfata Erick chumbani kwake ili kuweza kumwambia habari aliyoambiwa na Sia alivyokutana nae njiani, basi alimweleza kila kitu na kumfanya Erick ashangae pia,
“Kaambiwa na nani maneno hayo?”
“Sijui ila nimemziba kidomodomo kwa kumwambia kuwa mimi nina mchumba wangu wa kuitwa Emmanuel na wewe unae wa kuitwa Emmanah”
“Khaaa inamaana wewe unampenda kweli Emmanuel?”
“Hapana, nimesema tu ili kumkata yule mwanamke kidomodomo maana mimi nakupenda wewe”
“Ila mimi na wewe ni ndugu si ndio msemo wako huo? Tutawezaje kuwa pamoja Erica?”
“Sijui ila ninachojua ni kuwa tunapendana tu, ila kwani uongo? Mimi na wewe ni ndugu kweli”
“Ndio tena ni mapacha, ila kwanini tunapendana?”
“Sijui Erick, yani mimi ukiniuliza swali la namna hiyo kwakweli sina jibu la kukujibu kabisa kwani naona tu tunapendana na sijui kwanini tunapendana”
“Unaweza kuhisi hali hii itaisha lini?”
“Sijui”
“Ila mimi najua hii hali itaishije?”
“Mmmh niambie sasa?”
“Kesho, muda wa kulala njoo chumbani kwangu halafu nitaongea na wewe jinsi ya kumaliza hii hali”
“Mmmh Erick!! Si uniambie tu”
“Nitakwambia kesho. Hivi Sarah kwasasa analala chumbani kwake eeeh!!”
“Ndio, siku nyingine analala chumbani kwake na siku nyingine analala chumbani kwangu”
Basi Erica alimuaga kaka yake kisha yeye aliondoka zake na kwenda chumbani kwake kulala ambapo kwa siku hiyo Sarah alikuwa kalala chumbani kwa Erica.
Kulipokucha tu, Sarah alianza kuongea na Erica,
“Unajua dada Angel sijamuona toka juzi akitoka na kula au kuongea nasi, hivi tatizo litakuwa ni nini?”
“Ila kweli usemayo, sijui ana tatizo gani. Ngoja niende kumwambia mama usikute hajui”
Erica aliondoka na moja kwa moja kwenda chumbani kwa mama yake.

Muda huu Erica alimkuta baba yake ndio anataka kutoka ila muda ule ule alimwambia mama yake,
“Mama, unajua dada Angel toka juzi hatoki nje kula!”
Hapo mama Angel alishtuka kidogo na kumtaka Erica kuondoka ili aongee na mume wake, halafu mama Angel alianza kumwambia baba Angel,
“Chonde chonde naomba ukaongee na Angel, nilimwambia ukweli na amechukia sana”
“Kivipi?”
“Nilimwambia ukweli kuwa baba yake ni Rahim”
“Lini hiyo mbona hukunishirikisha?”
“Nisamehe mume wangu, toka siku uliyosema, basi nilifikiria na juzi kumwambia ukweli Angel. Naomba unisamehe, sasa kusikia kuwa hatoki nje kabisa nimeogopa sana, nakuomba mume wangu nenda kaongee na Angel”
“Ila mama Angel una masikhara ujue, yani mtoto jana nzima hajatoka hata hujaulizia?”
“Nilijua katoka, yani sijafatilia swala hilo hata kidogo”
Basi baba Angel akatoka chumbani kwake na moja kwa moja alifika chumbani kwa Angel na kugonga maana Angel alikuwa kafunga malngo, aligonga sana bila kufunguliwa, ilibidi aseme,
“Angel mwanangu, naomba unifungulie, mimi ni baba yako”
Muda mfupi Angel alifungua ule mlango na kumkumbatia baba yake huku akibubujikwa na machozi, basi baba Angel alimbembeleza pale na kwenda kukaa nae humo chumbani ili kuongea nae,
“Mwanangu umejifungia mlango, huli chakula tatizo ni nini?”
“Naomba kwanza niambie ukweli, wewe ni baba yangu au sio baba yangu?”
Baba Angel alipumua kidogo na kusema,
“Mimi ni baba yako Angel, kwani tatizo ni nini?”
“Kwahiyo mama alikuwa akinidanganya eeeh!”
“Sikia Angel mwanangu, naomba kwanza utulivu wako halafu tutaongea vizuri”
“Sitaki cha kusikia kuwa wewe sio baba yangu”
“Mimi ni baba yako, hakuna mahali niliposema mimi sio baba yako. Umewahi kusikia hilo toka kwangu?”
“Hapana baba”
“Basi tulia, inuka hapo twende wote tukale. Leo sitoenda hata kazini ili nikae na wewe siku nzima”
Angel alifurahi sana, kisha aliinuka na baba yake, na kwenda nae mezani kula chakula.
Kwakweli siku hii baba Angel hakwenda tena popote maana alikuwa na binti yake tu huku akiongea nae mambo mbalimbali na sio swala la baba tena.
 
SEHEMU YA 390

Usiku wa leo, karibia na muda wa kulala, Erica alitoka chumbani kwake na kwenda cumbani kwa Erick kama ambavyo walipanga jana yake.
Alivyoingia tu alifunga mlango ila muda huo huo Erick alitoka bafuni kuoga na alipomuona Erica alifungua taulo lake na kuanza kujifuta maji, kile kitendo kilimfanya Erica atake kukimbia ila Erick alimsogelea na kumshika mkono.

Alivyoingia tu alifunga mlango ila muda huo huo Erick alitoka bafuni kuoga na alipomuona Erica alifungua taulo lake na kuanza kujifuta maji, kile kitendo kilimfanya Erica atake kukimbia ila Erick alimsogelea na kumshika mkono.
Erick alimuuliza Erica,
“Unakimbilia wapi sasa Erica?”
“Nataka kutoka humu chumbani”
“Kwani unafikiria ni kitu gani?”
“Sijui, kwani ni nini?”
“Hebu vua nguo kwanza halafu uone ni nini”
Erica akamshangaa sana Erick na kumwambia,
“Kheee nivue nguo? Erick unataka kufanya kitu gani?”
“Hapana, sitaki kufanya chochote ila nimekumbuka wakati wadogo tulikuwa tukioga pamoja na tukivaa pamoja, wala hakuna mtu aliyekuwa akimuogopa menzie”
“Hebu vaa taulo kwanza halafu ndio tuendelee kuongea”
Erick alichukua taulo na kujifunga, kisha Erica akamwambia,
“Vaa na kaptula ndio tuongee vizuri”
Erick alivaa ile kaptula na kumuangalia Erica ambaye alisema,
“Usiniangalie hivyo, haya niambie sasa ulikuwa ukitaka nini kati yangu na yako?”
“Sikia Erica, hata mimi sijui ni kwanini hakupenda au ni kwanini tunapendana, nilitaka mimi nibaki mtupu na wewe ubaki mtupu halafu tulale pamoja tuone nini kitatokea kati yetu”
Hapo Erica kidogo alinyamaza kimya kwa muda mpaka Erick alipomshtua tena,
“Erica, kwani vipi?”
“Sijui”
“Umekubali? Tuvue nguo halafu usiku wa leo tulale wote tuone nini kitatokea”
“Unahisi kitatokea nini?”
“Sijui, kwani kila siku tukilala pamoja kinatokea nini?”
“Hakitokei kitu”
“Ndio, nahisi hakitatokea kitu. Tulale tu pamoja halafu asubuhi kila mmoja atavaa nguo zake”
“Mfano kikitokea kitu je?”
“Kitu gani?”
Erica alikuwa kimya tena, basi Erick alimsogelea karibu na kumuuliza,
“Upo tayari tujaribu kufanya hivi tuone kitatokea nini? Ngoja nifunge mlango na funguo ili mama asije kutufata kama kawaida yake”
Basi Erick akasogea mlangoni, ila wakati akitaka kufunga mlango kuna mtu akaingia na huyo mtu alikuwa ni Sarah, ambaye moja kwa moja alimfata Erica alipokuwa amesimama na kumwambia,
“Erica, naomba tukalale wote, nashindwa kulala peke yangu”
Erica alikuwa kimya tu akimuangalia, kisha Sarah alimuuliza Erica,
“Mbona moyo wako unaenda mbio kiasi hiko?”
Sarah hakuongea tena ila alimshika mkono Erica na moja kwa moja kwenda nae chumbani kwao kwaajili ya kulala, halafu alipokaa nae alimuuliza tena,
“Erica kuna nini? Sijamuelewa Erick wala wewe sijakuelewa kwani kuna nini?”
“Hamna kitu”
Erica alijilaza tu pale kitandani ila siku hii ilikuwa tofauti sana kwa Erica kwani usiku wote alijikuta akifikiria tu maumbile ya Erick.

Kulipokucha tu, Sarah alitoka chumbani na moja kwa moja kwenda chumbani kwa Angel na kuanza kuongea nae,
“Sijui kwanini huwa sina mtindo wa kuja kuongea nawe, labda sababu muda mwingi nakuona unapenda kuwa peke yako peke yako”
“Usijali, unakaribishwa tu muda wote kuja kuongea na mimi”
“Mimi huwa napenda sana kuongea na Erica, mara nyingi nakuwa nae hata kulala huwa nalala nae. Ila kilichotokea jana sasa”
“Kitu gani?”
“Mara nyingi, huwa kama sijamuona Erica kwa muda mrefu shumbani najua lazima yupo kwa Erick na kweli nikienda namkuta huko, sasa jana nimemkuta tena”
“Aaah, ikawaje sasa?”
“Nimewakuta katika hali sio ya kawaida”
“Hali gani?”
“Kwanza Erick alishtuka sana kuniona, halafu Erica alikuwa akihema kwa haraka sana nadhani walitaka kufanya kitu kibaya”
“Kitu gani?”
“Sijui ila nimewashangaa tu”
“Nikuulize kitu?”
“Niulize dada”
“Ushawahi kupata sifa ya umbea yani ushawahi kukutana na watu wakakwambia kuwa wewe ni mbea?”
“Mmmmh!! Hapana kwakweli, sijawahi kuitwa mbea mimi”
“Basi kwa mara ya kwanza mimi ndio nitakuita mbea maana ulichokuja kunieleza ni umbea, sasa Erick na Erica wapange kufanya kitu gani? Na kuhusu kuwa pamoja, wale toka watoto ndio wapo vile, hata kuwatenganisha vyumba ni mama ndio alifanya kazi ya ziada maana hawakutaka kutengana, walikuwa wakipenda kula pamoja, kuoga pamoja na kulala pamoja kwahiyo mimi hata sishangai kuhusu hiko ulichokisema, wale ni kawaida yao kuwa sana karibu”
“Oooh basi yaishe dada”
“Yameisha ndio ila acha umbea, umbea sio mzuri na umbea haufai mtoto wa kike”
Basi Sarah aliamua kuondoka kwani kwa muda huo alihisi aibu ukizingatia aliyekuwa akimsalimia ndio huyo kajifanya ahusiki.

Kisha moja kwa moja Sarah alimfata mama Angel, aliamua kuongea nae kuhusu simu yake kwani hakutaka tena kumpa hiyo habari ya Erica na Erick ukizingatia ameshashushuliwa na Angel,
“Mama samahani, nilikuwa na uhitaji na simu yangu”
“Naona umeugua kwa kukosa simu yako kwa muda?”
“Kiukweli sina raha kabisa yani, natamani sana kuipata simu yangu ili niweze kuwasiliana na watu mbalimbali kama ambavyo nilikuwa nikifanya”
“Sawa nitakuletea ila kuwa makini, yale mavideo yako usiyaangalie”
“Sawa mama”
Baada ya muda mama Angel alienda kumkabidhi Sarah ile simu na kumfanya Sarah afurahi sana, moja kwa moja alienda nayo chumbani na kumpigia Elly sababu ndio mtu aliyetaka kuwasiliana nae kwa muda mrefu sana, alimsalimia na kuongea nae,
“Mama yangu hakuja huko kwenu kuniulizia?”
“Kwakweli mama yako kanitafutia balaa”
“Mmmh balaa gani hilo?”
“Anasema kuwa ninayeishi nae sio mama yangu mzazi, kwakweli nimeshangaa sana. Kulikuwa na balaa hapa Sarah, uko wapi kwani?”
“Mimi nipo kwakina Erick”
“Bado una mpango wako ule wa kumtaka Erick?”
“Hapana, halafu huwezi amini, siku hizi wala simtaki Erick kama mwanzoni, toka nimeambiwa kuwa ni ndugu yangu basi simtaki tena, hivi huwa unanikumbuka kweli?”
“Kwanini nisikukumbuke wakati wewe ni dada yangu jamani!! Halafu kitu kingine ni kuhusu yule baba, anaomba uje kumtembelea hata kidogo tu ili aongee na wewe”
“Baba yupi huyo?”
“Yule wa siku ile ambaye tuliambiwa mimi na wewe kuwa ni baba yetu”
“Ila dunia hii jamani loh!! Mtu kila siku unabadilishiwa wazazi tu, mimi namjua baba yangu aliyekufa tu, huyo mwingine simtambui ila nitakuja kumtembelea”
“Basi kesho twende”
Sarah alikubaliana na Elly sehemu ya kukutana ili kesho yake waweze kwenda kumtembelea Derrick ambaye inasemekana kuwa ni baba yao mzazi.

Usiku wa leo, Sarah akiwa chumbani na Erica akainuka na kufunga mlango kabisa halafu anamwambia Erica,
“Sasa nataka kukuonyesha zile video maana mama ameshanipa simu yangu”
Erica alitamani sana kuziona, basi akamsubiria Sarah azifungue, ila Sarah aligundua kuwa mama Angel alifuta zile video zote na kusema,
“Aaaah kafuta zote, ila nina rafiki yangu huyo ngoja nimpigie anitumie”
Sarah alipiga simu na kumwambia huyo rafiki yake amtumie, kisha alikuwa akingoja amtumie huku akiongea na Erica,
“Yani huyu ni noma, yeye lazima awe na hizo video”
“Nani huyo?”
“Ni rafiki yangu anaitwa Abdi”
“Abdi? Unamjua?”
“Na wewe unamjua? Mimi Andi ni rafiki yangu sana”
Sarah alimuelezea Erica kuhusu Abdi anayemfahamu yeye na hapo Erica akatambua wazi kuwa ndio Abdi yule yule ambaye yeye anamfahamu, basi muda kidogo Abdi alikuwa ametuma zile video ambapo Sarah alifungua ya kwanza na kumuonyesha Erica, kwakweli Erica alishtuka na kuuliza,
“Ndio manini wanafanya haya?”
Sarah alicheka sana na kusema,
“Acha ushamba Erica, hayo ndio mapenzi. Ndio chanzo cha mimi kupata mimba ya Elly”
“Duh!!”
“Ila usiogope, njia za kuzuia mimba zipo nyingi tu ukitaka nitakuelekeza”
“Mmmh hapana, Sarah usinionyeshe tena hizi video naogopa mimi”
Erica aliweka simu ya Sarah pembeni na kuamua kulala, ila siku hiyo ndio mawazo yalimzidi zaidi kwani kila muda alihisi zile video zikimjia kichwani na alihisi maumbile ya Erick yakimjia kichwani pia.

Leo Sia, moja kwa moja anaenda ofisinbi kwa baba Angel kwani alijikuta akitamani sana kumwambia baba Angel kuhusu ujumbe aliopewa na Rahim kuhusu wale mapacha wa baba Angel, ila aliona ni lazima aonekane ni mbea zaidi.
Alifika hadi ofisini kwa baba Angel na kumkuta na kazi zake, basi alimsalimia na kuanz akuongea nae,
“Kuna kitu nataka kukwambia”
“Kitu gani hiko?”
“Mmmh!! Wachunguze vizuri watoto wako”
“Kivipi? Niwachunguze watoto wangu gani?”
“Erick na Erica naomba uwachunguze”
“Kivipi? Ushakuja na umbea wako tena eeeh!! Unataka kusema wale watoto sio damu yangu au kitu gani maana wewe kuna muda huwa unajianzia tu, sijui unapata faida gani ukisema maneno kama hayo. Haya niwachunguze nini?”
“Umefika mbali Erick maana mimi nilitaka kuongelea kitu kingine kabisa”
“Kitu cha kuongelea, ushaanza na mada ya kusema nichunguze watoto wangu, unataka kuongelea nini? Unataka kusema wale mapacha sio wangfu, haya, watoto wangu wako wapi kama wale sio wangu? Semeni lingine ila kuhusu watoto sio wangu hapo nitaanza kuwa mswahili”
“Jamani Erick dah!! Sijui hata kama umejua nataka kuzungumzia nini, ngoja niondoke maana hutaki kunisikiliza”
“Ondoka ndio”
Kwakweli Sia hata alishindwa kuongea chochote baada ya kumuona baba Angel kabadilika hata sura juu ya watoto wake, hakuwa na namna yoyote zaidi ya kuondoka tu kwa muda huo.
Sia akiwa njiani, alikutana tena na Rahim, ambaye alimsimamisha Sia na kuanza kuongea nae, Rahim alianza kusema,
“Unajua kadri ninavyokuwa karibu na Manka, napata upenyo wa kuwa karibu na yule dokta wenu dokta Jimmy, kwakweli Erica hataki tu kunisikiliza sababu yeye anawaza mambo mengine ila angenisikiliza angeweza kuokoa mambo mengi sana”
“Kwahiyo umeshindwa njia yoyote ya kuzungumza nae?”
“Njia gani sasa? Kwasasa nikimpigia simu yangu anakata, nimeenda hadi kwao siku hiyo hawajataka kuonana na mimi. Jamani wale watoto wao wanatakana, hayo mambo yamefika pagumu kwasasa, watalia jamani, huyo Erick na Erica watalia, halafu watasema kumbe Rahim alitaka kutuambia toka mwanzo, ila watakuwa wamechelewa”
“Sasa ni kitu gani kinafanya wale watoto watakane”
“Kila kitu ni mchezo wa babu yao, huyo baba mzazi wa Erick. Ila mimi napenda sana kuwasema nyie mabinti, huo mtindo wenu wa kuvamia vamia maukoo na kuolewa nayo mtakuja kulia na kusaga meno. Yani hii kitu hawawezi kuiepuka kama hao wazazi hawajaamka kwasasa, watoto wanatakana wale, wanapenda kufa mtu, yani kila mmoja yupo tayari kufa kwaajili ya mwenzie, upendo wao ni mkubwa sana. Siku ukikutana na yule Erick au Erica muulize tu swali la mtego kuwa nani afe kati yao ikitokea hivyo kama hawajakujibu wanataka wote wawili wafe, yani hawawezi hata kuwa na mahusiano tufauti na wao sababu wanapendana sana”
“Duh!!”
“Endelea kushangaa tu, ila wewe tulia tulia na uangalie jinsi mchezo unavyoenda, yule binti akishajaa tumbo ndio wale wazazi akili zitawakaa sawa”
Kwa hapo Rahim aliachana tena na Sia na kuondoka zake.
 
SEHEMU YA 391

Elly alifika na Sarah nyumbani kwakina Derrick na yeye aliwapokea vizuri sana na kuwakaribisha kisha alianza kuongea nao, ambapo Sarah alimuuliza,
“Ila unasema kuwa mimi ni mwanao, je ni mwanao kivipi? Maana mimi nina baba yangu ambaye alishakufa”
“Sarah ulidanganywa kuhusu baba yako ila baba yako mzazi ni mimi”
“Hapana, siamini kuwa wewe ni baba yangu mzazi maana mama hajawahi kuniambia hilo”
“Hajawahi ndio, ila mimi ni baba yako mzazi”
“Hapana kwakweli, hiko kitu nitapinga hadi naingia kaburini. Wewe sio baba yangu mzazi, hivi unajua jinsi baba alivyokuwa akinipenda? Yani mali zote ambazo mama anajivunia ni mimi nimepewa na baba yangu”
“Ni kweli ila mama yako alifanya hivyo sababu ya mali na si vinginevyo, mimi ni baba yako Sarah”
Pale Derrick alijaribu kumshawishi Sarah sana ila bado ilikuwa ngumu kwa Sarah kushawishika kuwa yule ni baba yake, basi wakaongea ongea kidogo na kuamua kuondoka ambapo Sarah aliongozana tena na Elly na kumuuliza maswali Elly,
“Kwani huyu mbaba ana undugu gani na mamake Erick?”
“Huyu na yule mama ni mtu na kaka yake kabisa, wamechangia baba kasoro mama tofauti”
“Kwa maana hiyo hata mimi na wewe tumechangia baba kasoro mama?”
“Aaaah Sarah dunia ina mambo sana hii, unajua kama yule ninayeishi nae sio mama yangu halisi?”
Sarah alishtuka na kumuuliza tena Elly,
“Kwahiyo mama yako ni nani?”
“Nikikwambia waliyeniambia nadhani utachoka na huwezi kukubali kama ambavyo mimi sijaweza kukubali”
Mara kidogo kuna mtu alitokea na kuwasalimia, alikuwa ni mama wa makamo ambaye anaenda kama kwenye ubibi basi aliwauliza,
“Samahanini, kuna mwanamke mmoja niliwahi kuonana nae zamani sana, nadhani kwasasa atakuwa ni mama mtu mzima tu. ANaitwa Erica, mtakuwa na undugu nae eeeh!!”
Elly na Sarah walitazama na kuitikia kuwa wanamfahamu, kisha yule bibi akasema tena,
“Yani kama wewe binti ndio umefanana nae balaa, ila hata huyu kijana kafanana nae pia. Msalimieni sana”
“Sawa, tumwambie nani anamsalimia?”
“Mwambieni mama mkwe wake wa zamani anamsalimia sana”
Elly na Sarah waliangaliana tena ila waliitikia tu na kuendelea na safari yao, ila Sarah akasema,
“Unajua naanza kuamini kuwa mimi nina undugu na mama Erick maana huyu sio wa kwanza, ni wengi nikikutana nao huwa wananifananisha mimi na mama Erick, nina hakika kuwa yule mama kwa namna yoyote ile lazima atakuwa ni ndugu yangu tu ndiomana nampenda sana”
“Basi ndio ujue kuwa yule kweli ni baba yetu”
“Mmmh kwa hapo nina mashaka kidogo, ila mmmh sijui labda siku mama anihakikishie”
Waliongozana na moja kwa moja Elly alimfikisha Sarah na kuagana nae maana yeye hata hakuingia kabisa ndani.

Mama Angel leo jioni aliwasiliana na dada yake ili aweze kukutana nae, kisha aliongea na wakina Junior kuhusu swala la kutoka nao kesho na kuwapeleka kwenye makazi yao, kwahiyo walifurahi ingawa kwa upande mwingine waliumia kidogo sababu walishazoea kuishi hapo nyumbani. Mama Angel aliwataka mapema kabisa wajiandae kwaajili ya kuondoka naye kuelekea huko kwao.
Basi siku hiyo, kwa pamoja walikula wote chakula cha usiku kwaajili ya kuwaaga wakina Junior maana tayari alishawaambia kuwa kesho yake atawapeleka huko.
Basi walikula na kufurahi huku wakiongea mambo mengi sana na usiku ulipoingia wote waliamua kwenda tu kulala.
Kulipokucha, kama ambavyo mama Angel alihitaji wajiandae, basi aliwachukua na mizigi yao kisha kuanza safari ya kwenda alipowaambia kuwa wanaenda kwa siku hiyo.
Moja kwa moja, walimpitia kwanza mama Junior na kuondoka nae kuelekea ambapo walipokuwa wakielekea.
Kufika kule, walimkuta Dora ameshafika na walishuka pale, kwakweli mama Junior alishangaa sana, yani mpaka wanaingia ndani ya nyumba ile bado alikuwa akishangaa kwakweli, kisha wakina Junior walikabidhiwa pale huku Dora akimwambia Junior,
“Karibu hapa ni nyumbani kwako, hii ni nyumba ambayo wewe Junior ulizaliwa humu, baba yako mzazi na mama yako walikuwa wakiishi humu”
Junior alikuwa akishangaa tu, yani mama Junior alijikuta akianza kulia maana hakuelewa kabisa kile kitu, ilibidi mama Angel akae nae na kumuelekeza dhumuni la Dora kufanya vile, kwakwlei alifurahi sana kwa mwanae Junior kurudi kwenye nyumba ambayo alizaliwa humo,
“Kwahiyo umewapangia tena hii nyumba?”
“Hapana, James aliinunua kabisa hii nyumba. Nilichokifanya mimi ni kuikarabati na kuirudisha kwa muhusika”
“Oooh asante sana Dora, yani sikufikiria kabisa jambo kama hili, nashukuru sana”
Mama Juior alimkumbatia Dora na hapo walianza kuongea mengi kwani ilikuwa ni furaha kubwa sana kwa mama Junior, hata Junior nba Vaileth walibaki kustaajabu tu huku wakionyeshwa mazingira ya nyumba ile huku Junior akiambiwa vitu mbalimbali kuhusu uwepo wa nyumba ile ambao hakuujua sababu kipindi kile alikuwa ni mtoto mdogo.

Angel aliona siku hii ni siku nzuri kwa yeye kuweza kuonana na Samir ukizingatia wote kwenye familia yake hawakuwepo, basi aliomba simu kwa Sarah na kumpigia simu Samir kuwa aende kwao, na kweli muda sio mrefu Samir alifika, na muda ule walibaki tu Angel, Erica, Sarah na Ester maana wengine wote walitoka kutokana na majukumu ya siku hiyo.
Angel alimkaribisha Samir na kwenda kukaa nae kwenye bustani yao huku wakiongea ongea,
“Mfano wazazi wako wakija je itakuwaje?”
“Sipendi kujificha ujue, yani wazazi wangu wajue wazi ni jinsi gani nakupenda na huwa nawaambia wazi kuwa nakupenda sana”
“Kweli Angel umeamua ila nadhani tungekaa chumbani na kuongea ingekuwa vizuri zaidi kuliko hapa nje”
“Mmmh kwahiyo twende chumbani?”
“Ndio, twende tukaongee chumbani ndio vizuri”
“Sawa, ila ngoja nikuulize kitu. Kwa mfano ukaja kuambiwa kuwa baba unayeishi nae sio baba yako utafanyaje?”
“Mmmh mimi jamani sijui ila baba yangu nagombana nae kila siku, sipatani nae kwa matendo yake anayomfanyia mama, najua hata mama anamvumilia tu sababu yetu, ila isingekuwa sisi basi mama hata asingeweza kumvumilia baba maana baba yetu ana mambo ya ajabu sana”
“Na wewe badae utakuwa kama hivyo?”
“Hapana, mimi nitakuwa kama baba yako sababu huwa naambiwa sifa zake na yule mdogo wangu Samia, nasikia baba yenu anampenda sana mama yenu, nasikia anawapenda sana watoto wake, na mimi nahitaji kuwa kama baba yako”
“Wow, baba yangu kweli ana upendo sana”
“Sawa, Angel twende chumbani tukaongee vizuri, ni mengi nataka kuongea na wewe ila nashindwa kuongea nawe hapa nje. Halafu nafasi kama hii juu yetu ni nadra sana kupatikana Angel”
Angel alipofikiria aliona ni kweli kuwa nafasi ya yeye kuongea na Samir na ndogo sana, basi aliamua kwenda nae chumbani kwake huku akipanga siku ya kwenda kwa bibi yake ili kuchukua simu yake ambayo upo huko kwa bibi yake.

Baba Angel akiwa anakaribia kutoka ofisini kwake, siku ya leo akafatwa na rafiki yake Juma kwahiyo alitoka na kwenda nae nje ili kuzungumza nae mawili matatu, ila kuna jambo Juma alimueleza baba Angel ambalo lilimshangaza kidogo,
“Yani nimeamua kukutafuta ili niongee na wewe”
“Kitu gani hiko?”
“Uliwezaje kulea vyema mtoto wa mke wako hadi akajua kuwa wewe ndiye baba yake?”
Baba Angel alicheka na kumuuliza,
“Wewe umejuaje kama yule si mwanangu?”
“Dunia haina siri, mtu anatakunyima chakula na sio maneno ndugu yangu. Kuna mtu alimtonya mke wangu, hata hivyo mtoto hafanani na wewe Erick hata kidogo yule, ila mwenzetu upo katika viwango vingine, ndiomana nimekuuliza umewezaje kulea mtoto wa mke wako hadi kujulikana kuwa ni mtoto wako?”
“Nilimpenda mke wangu, nikapenda na uzao wake, toka siku ya kwanza nilimchukulia yule mtoto kama mtoto wangu wa damu, kwahiyo hakuna kitu kilichonifanya nimlee mtoto yule vizuri kama swala la kumchukulia kama mtoto wangu wa damu”
“Hongera sana kwa hilo, maana sisi wengine sijui vipi hatukuweza jambo hilo. Mke wangu alikuwa mapepe sana, unalea mtoto huku na majukumu yote unafanya halafu yeye anaenda kukutana na baba wa mtoto wake, nikamwambia mke wangu, tumpeleke mtoto kwa baba yake, ndio hapo mtoto akaenda kwa baba yake na mimi na mke wangu tukaanza maisha mengine”
“Oooh, kwanini umeniambia yote hayo?”
“Jamani, kale katoto kalipata mimba sijui kalipewa na nani huko, kakatimuliwa na baba yake na kuja kukimbilia kwa mama yake yani pale ninapoishi na mama yake, kwakweli nilikaonea huruma na tukalea hiyo mimba hadi kakajifungua vizuri kabisa, mtoto ni mkubwa sasa ana miaka minne, huwa sisemi tu jambo hili. Ila leo nimemuuliza kama baba mwenye mtoto ni nani yani mwanaume aliyempa mimba ni nani! Jamani katoto kale kamenitusi hadi nimehisi kizunguzungu, nimeona nikikapiga nitakaumiza, kwakweli nimekosa hata raha ndiomana nikaja kwako rafiki yangu ili unipe ushauri juu ya hili”
“Duh pole sana ndugu yangu, kumbe una mitihani kiasi hiko!”
“Yani acha tu, nina mitihani hadi nahisi kuchanganyikiwa hapa. Naomba unishauri chochote tu ili nami niridhike jamani.”
“Ngoja kwanza, niongee na mke wangu ili ashauriane na mwenzie na mjue cha kufanya na mtoto wenu huyo. Kwasasa sina ushauri kwakweli”
“Sawa, nadhani hata kupitia kwa mkeo napo sio jambo baya, itanisaidia kwakweli, labda aongee na mwenzie yani mimi nimeshindwa maana chochote nitakachofanya yule mtoto ataona nambagua”
Basi waliongea kidogo na kisha kila mmoja kuondoka zake na kuelekea nyumbani kwake.
 
SEHEMU YA 392

Usiku wa leo, baba Angel alikuwa akimueleze mkewe kuhusu alichoongea na Juma, mkewe alikubali kumtafuta rafiki yake ili aongee nae maana aliona kuna umuhimu wa yeye kufanya hivyo,
“Nitaongea nae tu hakuna tatizo, ila habari njema ni kuwa wakina Junior wamefurahi sana kwenye makazi yao mapya”
“Na mamake kasemaje?”
“Amefurahi sana kwakweli, nadhani alikuwa akiwaza sana maisha ya mwanae ila kwasasa kafurahi, mimi nitakuwa naenda kuwatembelea mara kwa mara ili kujua maendeleo yao. Halafu kuna mahali nimemtafutia Vaileth atakuwa anaenda kujifunza maswala ya ushonaji, ngoja kwanza mtoto akue kue”
“Oooh hapo sawa mke wangu”
Mara simu ya baba Angel ilianza kuita, alipoiangalia aliona namba ya yule mwarabu, alishangaa sana na kusema,
“Huyu mwarabu ananipigia leo usiku kuna nini?”
“Pokea umsikie”
baba Angel alipokea ile simu na kuanza kuongea nayo,
“Mr.Erick, kesho nitakuja kwako hapo mapema kabisa kumchukua Erick mdogo, kuna mahali nahitaji kwenda nae, kwenye kile kiwanda nilichokwambia”
“Oooh sawa nimekuelewa hakuna tatizo”
Basi yule mwarabu alikata simu kisha mama Angel akamuuliza mume wake,
“Kwani huyo mwarabu na Erick huwa wanafanya kazi gani? Maana naona kama wiki yote hii Erick alikuwa akienda kwenye kazi ya huyo mwarabu”
“Aaaah huyu mwarabu kuna biashara zake alipenda Erick amuelekeze, halafu pia kuna kiwanda chake kimoja hivi niliongea nae, aliniomba Erick afike pale kwa siku moja ili amuelekeze baadhi ya mambo”
“Ila mume wangu unaona ni sawa kwa watu kumtumia hivi mtoto wetu? Hivi huyu Erick atakumbuka masomo kweli? Naona kama itaenda enda hela zitaanza kumtawala, lini nimemuona Sarah kavaa viatu vya gharama sana, nimemuuliza kavitoa wapi, kasema kanunuliwa na Erick, naona kama Erick ameanza kutawaliwa na hela”
“Hapana mke wangu, Erick ni kijana mwenye akili sana na anajitambua sana, kwahiyo hata tusiwe na hofu naye, shule ikifunguliwa basi atakazana na masomo na bila shaka atamaliza vizuri maana ana akili”
Waliongea kiasi ila mama Angel anaonekana hakuridhika kabisa na lile swala la Erick kufanya kazi na mwarabu.

Asubuhi na mapema, Angel alitoka nje na kuanza kufanya usafi, kisha Erica na Sarah nao walitoka pia ila wakiwa sebleni pale kuna mtu aligonga mlango na Angel ndio alienda kufungua na kumkaribisha, mtu huyu alikuwa ni yule mfanyabiashara maarufu wa kuitwa mwarabu, basi walimsalimia pale ila huyu mfanya biashara hakuitikia kwanza zile salamu za wale mabinti.
Kwa muda kidogo yule mwarabu alimtazama Angel na kusema,
“Bila shaka wewe ni mjukuu wangu! Bila shaka wala kupepesa macho, wewe ni mtu wa ukoo wangu”
Baba Angel nao na mama Angel walikuwa wametoka ndani ila hii kauli iliwafanya wajikute wamesimama gafla.
Kwa muda kidogo yule mwarabu alimtazama Angel na kusema,
“Bila shaka wewe ni mjukuu wangu! Bila shaka wala kupepesa macho, wewe ni mtu wa ukoo wangu”
Baba Angel nao na mama Angel walikuwa wametoka ndani ila hii kauli iliwafanya wajikute wamesimama gafla.
Yule mwarabu aliendelea kusisitiza pale kuwa Angel ni mjukuu wake, akasema,
“Mbona mnanishangaa? Wewe binti ni mjukuu wangu kabisa yani, sijawahi kuwagundua wajukuu wangu haraka kama nilivyokugundua wewe”
Baba Angel aliamua kusogea maana aliona huyu mwarabu anaharibu tu kwa muda huo, Angel alitoka pale na kukimbilia chumbani kwake, basi baba Angel alitoka kidogo nje na mwarabu ili kuongea nae ila mwarabu ndiye aliyeongea,
“Erick, kwakweli nahitaji kuongea na wewe kwa upana zaidi kuhusu huyo binti, nahisi kabisa ni damu yangu. Huyo binti ni mjukuu wangu”
“Sawa sawa, tutaongea vizuri hakuna tatizo juu ya hilo”
“Kwa muda huu naomba niitie Erick mdogo niende nae huko maana inatakiwa tuwahi ndiomana nimemfata mwenyewe”
Basi baba Angel anamuita Erick mdogo na Erick anatoka akiwa kajiandaa sababu baba yake alimwambia juu ya hilo, kwahiyo moja kwa moja Erick anaondoka na yule mwarabu.
Baada ya kuondoka tu, mama Angel alimfata baba Angel na kuongea nae,
“Mmmmh kaongee na binti yako huko, si unajua alivyo kisirani basi atakuwa kashachukia kuambiwa na huyu mwarabu kuwa ni babu yake ndiomana kaenda kujifungia chumbani kwake”
“Ngoja nikaongee nae”
Baba Angel aliondoka zake na kuekea chumbani kwa binti yake ambapo aligonga na kuamua tu kufungua mlango ambapo Angel hakuwa ameufunga kwa funguo, alimkuta Angel akilia, basi alimsogelea na kuanza kuongea nae,
“Angel mwanangu tatizo ni nini?”
“Najua babu zangu wote walishakufa, huyu simtambui naomba baba uniambie kuwa si babu yangu”
“Hebu Angel tulia kwanza, tulia nikwambie. Kwani tatizo lako haswa ni nini?”
“Mimi nakujua wewe tu baba, wewe ndio baba yangu sitaki kusikia kuwa mimi nina bab mwingine”
“Sasa kwani ukiwa na baba mwingine Angel ni tatizo?”
“Kwani baba hunipendi?”
“Hapana, nakupenda sana binti yangu”
“Sasa kwanini uruhusu mimi niwe na baba mwingine? Kwanini baba mwingine aje katika maisha yangu? Mimi nakutambua wewe tu”
Baba Angel akapumua kidogo na kuona wazi kuwa lile ni tatizo, ila je nani wa kulaumiwa kwa lile tatizo? Ni mama Angel, baba Angel au Rahim? Hapo hakujua kwakweli yani alijikuta akikosa hata jibu la kusema kuhusu kumsaidia Angel, aliishia tu kumbembeleza na kumuhakikishia kuwa yeye ndiye baba yake halisi,
“Kwani baba si uliniambia hizi nywele nimefanana na bibi yako?”
“Ndio, bibi yangu alikuwa na nywele ndefu hata baadhi ya watu walimuita mwarabu”
Hapo Angel alitulia kidogo kuona kuwa kuna mtu kafanana nae kwenye ukoo wa baba yake, na hiko ndio kitu pekee ambacho huwa kinamfanya Angel afarijike maana huwa akiambiwa tu kafanana na huyo bibi alikuwa akijihisi amani sana.

Mwarabu alifika kwenye kiwanda chake na Erick, ambapo alianza kumuonyesha baadhi ya sehemu na vitu ambavyo kile kiwanda kinatengeneza, kuna mahali kwenye kile kiwanda kipo chini ya usimamizi ya mwanamke ambapo huyu mwanamke Erick alikuwa hapendi kukutana nae sababu alimsumbua hata walipokuwa dukani kwa yule mwarabu ila alimkuta tena kwenye hiko kiwanda akiwa ndio msimamizi wa sehemu hiyo,
“Unamkumbuka huyu eeeh!! Huyu wa kuitwa Zaby”
“Namkumbuka ndio”
“Haya, kwasasa nitakuacha nae hapa ili umuelekeze baadhi ya vitu halafu mimi nitaondoka na kurudi badae, nitakuchukua mimi mwenyewe na kukurudisha kwenu”
Erick aliitikia tu, na yule mwarabu kweli aliondoka kwa muda ule, na sehemu ile kumuacha Erick pamoja na yule Zaby, basi Zaby alianza kumuelekeza,
“Hii sehemu tunatengeneza haswaa nguo za ndani za wanawake za kuvaa kwenye tupu yao”
Zaby alianza kumuonyesha Erick baadhi ya nguo za ndani na jinsi ya kutengeneza, huku akimwambia kuwa wameambiwa yeye atawaonyesha cha kufanya zaidi, basi waliwatembelea wote wanaotengeneza pale kwenye mashine, kisha Zaby alienda ofisini na Erick ili Erick aweze kuandika baadi ya mambo, na kweli Erick alikaa na kuanza kuandika andika, yule Zaby alizunguka kwa nyuma ya Erick na kumshika mabega na kuwa kama akimkanda kanda yale mabega,
“Niache bhana”
“Erick una nini lakini? Mbona ni mshamba hivyo wewe”
“Ndio, niache na ushamba wangu”
“Sawa, ila ngoja nikuonyeshe kitu”
Mara Zaby alienda mbele ya Erick na kumwambia,
“Unafahamu tupu ya mwanamke?”
Erick alinyamaza tu, na muda ule ule yule Zaby alifungua nguo yake na kumwambia Erick,
“Hii nguo ya ndani pia imetengenezwa hapa, ngoja niivue uone tupu ya mwanamke”
Erick aliinama chini na kujilaza kwenye meza kabisa kwani hakutaka kuonyeshwa alichotaka kuonyeshwa na Zaby, mwishowe aliona hata kuinama haitasaidia bali aliinuka na kutoka nje ya ofisi na kuona ni bora aende kuandika kule kule kwenye mashine ambako kuna watu wengi wakitenda kazi, kwahiyo alielekea kule kule kwenye mashine.
 
SEHEMU YA 393

Mchana wa siku hii Angel alienda kukaa bustanini ambapo Erica na Sarah walimfata na kuanza kuongea nae mambo mbalimbali, ambapo Sarah alimuuliza Angel,
“Eti dada, nini maana ya mapenzi?”
“Mmmh na nyie mna mambo sana, mnataka kujua maana ya mapenzi! Na wewe Erica unataka kujua?”
“Mmmh ndio, ningependa nijue”
“Mapenzi ni kumpenda anayekupenda”
Erica akauliza kitu,
“Je mapenzi ni kuangalia video za watu wanaofanya mapenzi?”
Angel alishtuka na kumuangalia vizuri Erica, kisha akamuuliza,
“Ni video gani mnazizungumzia?”
“Ni video za wakubwa, zipo kwenye simu ya Sarah”
“Kheee Sarah ndio huwa unaangalia hizo video?”
Erica akajibu tena,
“Tena, aliangalia na Elly hadi wakapeana mimba”
Angel alishangaa sana na kuwaangalia kwa makini, kisha akasema,
“Mnajua nyie bado wadogo sana? Mimi tu wala sithubutu kuangalia hizo video, eeeh Sarah ulijisikiaje ulivyo nanii na huyo Elly?”
Sarah akapumua kidogo na kumuangalia Angel kwa aibu kidogo huku akiogopa kusema na kumfanya Angel amuulize tena,
“Niambie Sarah ulijisikiaje?”
“Kwani wewe dada hujawahi kujaribu?”
“Mmmh naogopa, nasikia kuna maumivu”
“Mmmh hamna, ni kidogo tu ndio maumivu”
“Halafu inaendeleaje?”
“Sijui ila nitakuonyesha video”
Erica akadakia na kusema,
“Mimi hizo video sitaki kuonyeshwa”
“Sawa hakuna tatizo, leo Sarah njoo ulale chumbani kwangu”
“Sawa dada, kwakweli nitafurahi sana kupata mtu wa kukubaliana nami kwa hizi video maana zingine ni nzuri”
“Mmmh!”
Erica aliguna na kuinuka zake kwani aliona zile mada kumuendea kushoto kabisa kwa wakati ule, basi moja kwa moja Erica alienda kufanya kazi zake zingine.

Usiku wa leo wakati Erica anataka kulala tu, muda sio mrefu chumbani kwake aliingia Erick na kumfanya Erica ashtuke kidogo na kumkaribisha,
“Karibu Erick”
“Oooh umenikaribisha leo, hadi nimejihisi furaha”
Basi Erick alienda kukaa kitandani kwa Erica na kuanza kumwambia,
“Erica, ndugu yangu, pacha wangu, mpendwa wangu naweza kukuita pia mpenzi wangu. Kuna jambo nahitaji kuongea na wewe, maana uliniambia niwe huru kuongea nawe”
“Niambie tu hakuna tatizo Erick”
“Ni hivi, kule kwenye kazi za yule mwarabu ambako huwa naenda, huwa nakutana na mdada mmoja anaitwa Zaby, kwakweli yule mdada huwa ananiweka kwenye majaribu sana, na leo ndio kaniongezea majaribu”
“Kivipi?”
“Yani, kunai le wiki nilikuwa naenda kwenye duka la yule mwarabu basi huyo mdada alikuwa akinifata sana, mara aanze kunipapasa kwakweli ananipa majaribu na kunikosesha amani, nikimkemea hata hanisikii kabisa. Sasa leo ofisini kaja kuvua nguo mbele yangu, nimejihisi vinaya sana na kutoka mule ofisini”
Erica alipumua na kumpa pole Erick,
“Pole sana kaka yangu”
“Asante, sijui nawezaje kuendelea kuishi na yule kiumbe kwenye ile ofisi”
“Dah!! Pole sana hata sijui nikusaidiaje”
“Cha kunisaidia kipo”
“Kipi hiko?”
“Inatakiwa mimi na wewe tulale pamoja tukiwa watupu kabisa”
“Mmmh isiwe nyumbani basi maana itakuwa balaa, hawatafikiria kama hatuna lengo baya au unasemaje?”
“Ni sawa isiwe nyumbani, kwahiyo tuombe ruhusa siku twende hotelini au unasemaje? Tuwaambie kuwa tunaenda kutembea, mimi na wewe tu kama siku ile tulivyoenda ufukweni”
“Aaaah hapo sawa, ila tutafanya nini humo?”
“Itajulikana tu humo humo tukiwa pamoja”
“Sawa, nenda kalale basi”
Erick alimuangalia Erica, kisha alimsogelea na kumbusu kwenye paji la uso kisha alimuaga na kuondoka, ila Erica alibaki tu ameduwaa kwa muda kidogo yani siku hiyo pia alilala huku akijifikiria vile hadi alijiuliza,
“Kwani ni mara ya kwanza Erick kunibusu? Hapana, kwanini leo imekuwa tofauti na siku zote?”
Alikosa jibu kabisa ila aliamua tu kulala kwa muda huo.

Baba Angel akiwa ofisini kwake, alipigiwa simu na mwarabu kisha alimuelekeza ofisi yake ilipo ambapo yule mwarabu alienda ofisini kwa baba Angel na kumkuta pale, alianza kuongea nae,
“Hongera sana, sikuwahi kufika kwenye ofisi yako, ila una ofisi nzuri sana, na ipo kwenye mpangilio mzuri, nimependa watu uliowaweka mapokezi ila mbona ni wamama watu wazima sana?”
“Aaaah ni mke wangu huyo ndio aliamua vile, alisema ofisi zinazoweka vijana ni kwaajili ya kuvutia wateja, ila hapa hatupo kwenye mvuto ni tupo kwenye kazi tu, wateja wetu ni wa kwenye mitandao, kwahiyo naona hakuna tatizo kuwa na watu wazima hapa”
“Ila mkeo ana akili, kaona mabinti wasijekukuungiza majaribuni mume wake, maana mabinti wengine nao kama wametumwa vile. Kuna kamoja nimekafukuza kazi pale kwenye ofisi zangu, kalikuwa kana mambo ya ajabu sana, huwa nawaambia watu waje kwa maadili kazini, ila yeye kila siku anavaa vimini tena vimini haswaa halafu akifika ofisini kwangu ni lazima ainame hata kama hana sababu ya kufanya hivyo, juzi nikamwambia mjinga wewe na kazi huna kuanzia leo, kila siku kuniweka kwenye majaribu tu”
Baba Angel alicheka sana, na kuendelea kuongea,
“Yani hapa ukikuta wanawake basi ni wamama wa makamo, ila ninachowapendea wapo vizuri sana kwenye kazi. Hata kipindi naumwa walijitahidi kumpa mwanangu ushirikiano mzuri sana, kwakweli mke wangu anataka mtu akiomba kazi hapa basi usahili amfanyie yeye, mke wangu nimemzoea mwenyewe, kule kiwandani tumeajiri wanaume tu, anasema kama kuna mwanamke anahitaji basi lazima amuone yeye kwanza”
“Aaaah mke wako atakuwa na wivu sana”
Mwarabu alicheka kiasi, muda kidogo alikuja yule bibi wa matunda na kuwaletea matunda pale, ila alipokuwa akiwasalimia yule mwarabu alimwambia,
“Hivi wewe si ushawahi kufanya kazi nyumbani kwangu ukiwa na mtoto mdogo kipindi kile?”
“Ni kweli ni mimi, sikujua kama ungenikumbuka”
“Sura yako haibadiliki, yani sura ipo vile vile”
Walisalimiana pale na kuongea mawili matatu kisha yule bibi alitoka, na mwarabu aliongea tena na baba Angel,
“Kweli umeajiri watu wazima hapa, hadi huyu mwanamke! Ni siku nyingi sana aliwahi kufanya kazi kwangu”
“Aaaah huyu sijamwajiri, ni mama ambaye huwa anatusambazia matunda”
Ila baba Angel leo alishangaa pia maana hata hakumwambia huyu bibi alete matunda ila huyu bibi alileta matunda kwa baba Angel, kisha mwarabu alianza kueleza azma yake ya kufika siku hiyo,
“Nahitaji kujua ukweli kuhusu yule mtoto wa jana”
“kivipi?”
“Erick sikia, nina uhakika asilimia mia moja kuwa yule ni mjukuu wangu, yani haiwezekani kupinga hiyo, naomba uniambie ukweli tu”
“Sawa, je ni mjukuu wako kwa mtoto wako yupi?”
“Mimi sijui ila nahisi ni mjukuu wangu tu”
“Basi, nenda kamuulize vizuri mwanao Rahim, muulize kuwa imekuwaje na yeye atakujibu kuwa imekuwaje ukiniuliza mimi hakutakuwa na jibu zuri”
“Ila ungeniambia wewe ingekuwa vizuri zaidi”
“Najua ila itapendeza zaidi akikwambia Rahim”
“Kesho nitajitahidi nikutane na kijana wangu nimuulize hayo maswala”
Sababu muda nao ulikuwa umeenda ikabidi yule mwarabu amuage baba Angel, naye baba Angel muda kidogo tu alitoka ili kuondoka ila moja kwa moja alienda kwa yule bibi muuza matunda na kumuuliza,
“Mbona sijakuagiza matunda leo ila ukaniletea?”
“Nilitaka yule mwarabu anione”
Baba Angel alicheka sana na kuondoka zake.

Usiku wa siku hiyo, baba Angel alimweleza mkewe jinsi mwarabu alivyofika kuongea nae ofisini kwake,
“Nimemwambia akamuulize mwanae”
“Yani angekuja kuniuliza mimi mwenyewe hata asingejisumbua kumuuliza huyo mwanae”
“Ila mwanae ndio atampa jibu zuri”
“Kesho nimepanga kwenda kumtembelea Junior na Vaileth ili kuona maendeleo ya ndoa yao maana Junior haaminiki ujue, yani Junior huwa namuamini robo robo”
“Ni kweli Junior haaminiki na utakuwa umefanya jambo jema sana kwenda kuwaangalia ni jinsi gani wanavyoishi na kuendelea na maisha yao ya ndoa.”
Walipanga mambo mengi na kuamua tu kulala kwa muda huo, ila simu ya mama Angel ilianza kuita kabla hata ya kulala vizuri ikabidi mama Angel aipokee na kuanz akuongea nayo,
“Unaongea na Manka hapa”
“Kheee Manka!!”
“Nakuuliza, mwanangu Sarah yupo kwako?”
“Kama ungetaka kujua yupo kwangu au hayupo kwangu ungekuja nyumbani kwangu na sio kuniuliza kwenye simu”
“Erica, mimi na wewe hatuna ugomvi na wala hatujawahi kugombana, ninavyomuulizia Sarah nina maana yangu kubwa sana, Sarah ni mwanangu na Sarah ndio maisha yangu na kwa kifupi siwezi kuishi pali na Sarah nimevumilia lakini nimeshindwa”
“Ni usiku huu Manka, ukimtaka mwanao njoo nyumbani sio tuongee kwenye simu”
“Haya nitakuja kesho kutwa maana nipo mbali”
Halafu Manka alikata ile simu na kumfanya mama Nagel amuangalia mumewe kwa makini na kusema,
“Jamani, unajua huyu mwanamke kaanza kuwa chizi, hivi mtoto utamuuliziaje usiku huu? Siku zote hizi alikuwa wapi kuja kumuulizia Sarah hapa? Kwanza sina amani kwa Sarah kurudi kwenye himaya yake maana huyu mwanamke kwenye kulea ni ziro kabisa”
“Ila utamkataliaje mtoto wake?”
“Aaaah sijui, ila hajui kulea mtoto kabisa. Mimi natamani Sarah nimlee mwenyewe maana naona hapa kwangu kabadilika vitu vingi sana”
Muda huo waliamua kulala tu kwani muda nao ulikuwa umeenda sana.
Kulipokucha kama kawaida baba Angel alitoka zake, mama Angel nae alijiandaa na muda huo huo kutoka zake kuelekea nyumbani kwa Junior na Vaileth.

Angel alimuomba Sarah simu yake na kumpigia Samir ili aende kumchukua aweze kwenda nae kwa bibi yake kuchukua simu yake ambayo bado ilikuwa kwa bibi yake.
Basi baada ya muda kidogo tu, Samir alifika kwahiyo Angel aliondoka na Samir na pale nyumbani kuwaacha wadogo zake tu.
Samir na Angel walikuwa wakiongea mambo mengi sana walipokuwa njiani,
“Hivi uliwaza kweli kama kuna siku itatokea kama hivi mimi na wewe kuongozana wote njiani?”
“Mmmh ni ngumu kwakweli, ila nilikuwa naamini maana ni kweli nakupenda sana Angel”
“Je kwa bibi tutaingia wote?”
“Uwiiii kwa yule bibi yako alivyokuwa na mdomo, akituona wote itakuwa balaa. Kwahiyo mimi nitakusubiri mahali ili ukitoka tu tuwe pamoja”
“Niambie ni wapi utakapo nisubiria maana yule bibi huwa anajishauwa utasikia anataka kunisindikiza”
“Mbona dawa yake ndogo, mwambie bibi nakuonea huruma na utu uzima huo, najua tu miguu itakuuma kwenda nami mpaka barabarani. Ngoja niite bodaboda”
“Mmmh kwa yule bibi alivyo, utasikia na mimi nataka kufanya zoezi, nitembee tembee hadi stendi”
“Basi mwambie kuwa umechoka kutembea na utakodi bodaboda, halafu mimi na wewe tutakutana pamoja”
“Halafu tutaenda kuongea wapi?”
“Kuna kitu nikuombe leo Angel”
“Niambie tu”
“Naomba leo tukaongee hotelini, yani ukitoka tu kwa bibi yako tutakodi bajaji na moja kwa moja tutaenda nayo hotelini kule kidogo nje ya mji halafu hatutaongea sehemu ya wazi bali tutakodi chumba na kuongea humo”
“Mmmmh hiko chumba utakodi wewe!!”
“Ndio, kwnai tatizo liko wapi Angel hata usiwe na wasiwasi”
Na kweli waliongozana hadi kwa bibi wa Angel ambapo Angel alienda moja kwa moja kwa bibi yake ambaye alifurahi kumuona na kumsifia kuwa amekuwa,
“Kwakweli mjukuu wangu umekuwa mkubwa sasa, yani mwanadada mkubwa kabisa, najiona kuzeeka zaidi”
“Bibi bhana, kumbuka Junior ana mtoto”
“Kwani Junior tupu, umesahau watoto wa mamako mkubwa Mage, yani mimi nishazeeka jamani. Haya karibu”
“Bibi, nimemaliza shule nahitaji ile simu”
“Umekubaliana na mama yako hivyo au?”
Angel alijaribu kumwambia maneno bibi yake ya kumbembeleza ili ampatie ile simu, kwahiyo bibi yake ilibidi tu akaitoe ile simu na kumkabidhi Angel ambaye alifurahi sana, na muda kidogo akamuaga bibi yake,
“Khaaa mbona mapema hivi, hutaki hata kusubiri chakula?”
“Bibi, nimetoka nyumbani nimeshiba sana halafu nimemwambia mama kuwa sitachelewa kurudi”
Yani Angel alitumia maneno yote ya kumshawishi bibi yake na mwisho wa siku bibi yake mwenyewe alikubali na kumpa ruhusa Angel ya kuondoka, ambapo Angel aligoma kabisa kusindikizwa na bibi yake kisha akatoka na moja kwa moja alienda kukutana na Samir na kuondoka zao kuelekea kwenye hoteli waliyopanga kuwa wataenda kwa siku hiyo.
 
SEHEMU YA 394

Leo, Elly alienda nyumbani kwa mama Angel yani yeye hakutaka tu kuonana na wengine pale, kwahiyo siku hiyo wakati Erica na Sarah wamemwambia kuwa wamebaki wenyewe aliamua kwenda pale na kuongea nao mambo mbalimbali, ambapo kama kawada Elly alianza kulalamika kuhusu wazazi, aliamua kuwaeleza Erica na Sarah ukweli,
“Hivi unajua kuwa mimi yule ninayeishi naye sio mama yangu mzazi!”
Erica na Sarah walishtuka na kumuuliza vizuri,
“Kivipi?”
“Siku zote nilikuwa nikiishi na mama na nilijua ni mama yangu mzazi, ila swala la mimi kugundua baba yangu ni nani ndilo ambalo lilianza utata, na hapo nikaja kutajiwa mama yangu kuwa mwanamke mwingine kabisa ambaye sifikirii kuwa anaweza kuwa mama yangu”
“Kwahiyo umeambiwa mama yako ni nani?”
“Eti mama yako Sarah ndio mama yangu”
Hapo Sarah alishtuka sana kwani hakuelewa ukizingatia anachojua ni kuwa kwa mama yake yeye ni mtoto wa pekee ilibidi amuulize vizuri Elly kuhusu tarehe, mwezi na mwaka wa kuzaliwa, alipotajiwa ndio alichoka zaidi kwani ndio tarehe ile ile, ila Erica alisema,
“Mbona hata mimi na Erick tumezaliwa tarehe hiyo hiyo!”
“Sasa inamaanisha mimi na Elly ni mapacha?”
Erica alijibu,
“Inawezekana”
Sarah aliinama chini na Elly nae aliinama chini, ndipo Erica aliposema,
“Uwiii halafu mkapeana mimba, toka lini mapacha wakapeana mimba? Mtakuwa na laana nyie”
Elly na Sarah wote walikuwa kimya kwa muda, ila Erica akasema tena,
“Inawezekanaje lakini? Imekuwaje mlelewe sehemu tofauti tofauti? Mnajua hairuhusiwi kwa ndugu kuwa na mahusiano? Yani nyie ni laana”
Sarah akapumua kidogo na kupiga magoti kwa Elly huku akimwambia,
“Naomba unisamehe Elly, sio kwamba nakubali kama sisi ni mapacha hapana, ila hata kama sio mapacha bado sisi tuna undugu halafu ni mimi ndio nilikuingiza kwenye dhambi hii naomba unisamehe Elly”
Kwa muda huo Sarah na Elly wote walijikuta wakianza kulia na kujutia kile ambacho kimefanywa kati yao.

Mama Angel alipofika nyumbani kwakina Junior, alifurahi jambo moja kumkuta dada yake yupo kule kwa wale watoto na kuanza kuongea nae,
“Dada nimefurahi sana kukukuta, ni leo ndio umefika?”
“Hapana, nipo hapa toka juzi, tabia za mtoto wangu nazijua lazima niwe nae karibu, nimemuomba hadi mume wangu ruhusa, nitakaa huku kwa wiki nzima”
“Oooh vizuri sana dada, ila ulikutaje?”
“Unajua Junior alianza habari zake za kutoka na kurudi usiku wa manane ila nipo hapa nimemdhibiti, nataka afanye mambo ya maana sio afikirie ujinga ujinga wa kwenda kuzunguka huko na wanawake”
“Umefanya jambo la maana sana, sababu hata mimi nilikuwa nafikiria jambo hili”
Waliongea vitu vingi sana, ila mama Angel hakutaka kukaa sana mahali pale na kuamua kumuaga dada yake tu pamoja na Vaileth na Junior.
Wakati mama Angel anarudi, njiani alikuta na Rahim ambaye alifurahi sana kukutana na mama Angel kisha akamwambia,
“Ingawa baba yangu kaniambia kuwa leo ana maongezi na mimi, ila nimefurahi sana kukuona wewe, nina mengi ya kuzungumza na wewe. Naomba usikatae maana haya ninayotaka kuzungumza na wewe ni ya muhimu sana, naomba tutafute mahali tuweze kuzungumza haya”
Mama Angel alifikiria kidogo, akaona pengine Rahim ana jambo la muhimu sana la kuweza kuzungumza nae kwahiyo aliona ni vyema kufanya mazungumzo nae, maana hakutaka kufikiria katazo la mume wake kwa muda huo.
Basi waliondoka na kwenda mahali na kukaa hapo kisha kuanza mazungumzo,
“Niambie cha maana Rahim, usinianzie mambo yasiyoeleweka”
“Sina mambo yasiyoeleweka, hapa nataka tuongee kuhusu mapacha wako yani Erick na Erica”
“Mmmh wamefanyaje tena watoto wangu?”
“Kuna tatizo kubwa sana kati ya wale watoto”
“Lipi hilo?”
Rahim alikaa vizuri na kutaka kuanza kumuelezea mama Angel, ila kabla hajaanza kumuelezea alishtuka sana kiasi hata mama Angel alishtuka pia na kugeuka sehemu ambayo Rahim alikuwa akiangalia, hapo alimuona Angel akiwa ameongozana na Samir huku wameshikana mikono.

Rahim alikaa vizuri na kutaka kuanza kumuelezea mama Angel, ila kabla hajaanza kumuelezea alishtuka sana kiasi hata mama Angel alishtuka pia na kugeuka sehemu ambayo Rahim alikuwa akiangalia, hapo alimuona Angel akiwa ameongozana na Samir huku wameshikana mikono.
Mama Angel alishtuka sana, na kufanya ainuke ambapo nae Rahim aliinuka na kutaka kuwafata wale watoto wao, ila gafla kuna upepo unapita kati yao kwa muda na kufanya wajifikiche macho, kitendo kile kilifanya Angel na Samir kupotea mbele ya macho yao na kufanya Rahim na mama Angel waangaliane kwa mshangao, huku Rahim akisema,
“Unaona haya mambo Erica? Wote wale ni watoto wangu! Hasira zako za kutokutaka mtoto aufahamu ukweli ndio umeniletea mambo kama haya, wameenda wapi wale watoto?”
“Mimi sijui, unanilaumu bure Rahim, mimi sijui kitu”
“Hujui kitu wapi? Unajua kila kitu wewe”
“Rahim, utanilaumu bure tu, ni kweli huyo Samir kaanza kumfatilia Angel kwa muda mrefu sana ila siku zote nimekuwa nikipinga mahusiano kati yao hadi kumpeleka mwanangu kwenye shule ile ya mbali ila bado nikaja kwenye mahafali na kuwakuta”
“Ulishindwa nini kuniambia mapema?”
“Sikujua mimi kama Samir ni mwanao pia”
“Mara ngapi nimekwambia kuwa Angel awajue ndugu zake? Mara ngapi Erica nimekuomba juu ya jambo hili? Nitaweka wapi sura yangu mimi? Nataka kurekebisha nyumba ya mwenzangu wakati na ya kwangu inateketea! Hebu niambie cha kufanya kwasasa?”
“Sijui mimi nahisi kuchanganyikiwa hapa”
Rahim alichukua simu yake na kumpigia Samir simu ila simu iliita hadi kukatika yani haikupokelewa kabisa, basi alimuuliza mama Angel,
“Naomba namba ya Angel nimpigie”
“Angel hana simu”
“Aaaargggh nilikuwa nakusifia siku zote ila sikuwahi kufikiria kuwa wewe ni mwanamke mshamba kiasi hiki, mtoto mkubwa kama Angel asiwe na simu kweli!! Aaaarrgh, nitafutie wanangu Erica na ole wako chochote kibaya kitokee kwao”
“Usinitishe baba, tena usinitishe kabisa, ungejua kama ni wanao wanatakiwa kuwa karibu basi toka zamani ungejiheshimu na kuheshimu wengine. Ulinifanyia visanga vyako wakati mtoto mdogo hadi nikambadilisha jina sababu ya ujinga wako. Haya, Erick akakupa ruhusa ili mtoto akuzoee ukataka kunibaka, ulitaka tukubebe mgongoni au ndio ujue namna ya kulea mtoto? Mara ngapi umenitukana na kumtukana huyo Erick bila kujali kitu, wala hukujali kuwa mimi ni mwanamke ambaye uliniacha kwa aibu nikalea mtoto mwenyewe, ila usivyokuwa na haya ukanitukana na kuniita malaya, nakumbuka vizuri usidhani sikumbuki, mtoto kafanana kila kitu na wewe hata mtu baki akimuona hapingi kuwa ni mwanao ila wewe ukathubutu kusema huenda hata mtoto sio wako, eti nimempata kwenye umalaya, hivi unafikiri hiyo kauli inanitoka kichwani kwangu? Nakumbuka vizuri, yani Rahim uliniona mimi kama takataka ya kutupwa, leo unanikoromea na kunipa vitisho eti nitafutie wanangu, baba niache tena uniache kabisa, kama kulia nishalia sana, kama kumkanya huyo mtoto nishamkanya sana, usinichefue mie”
“Yani unavyoongea utadhani hakuna kitu kibaya kilichotokea hapa, hebu tutafute watoto hayo mambo yaliyopita tuyaache”
“Hiyo kazi ya kutafuta watoto nakuachia wewe, kwaheri”
Mama Angel aliondoka zake kwa muda huo hata hakutaka kuangalia nyuma wala nini na kumuacha pale Rahim akijiuliza maswali mengi sana.
Rahim alikaa chini kwanza huku akijiuliza kuwa wale watoto ataanza kuwakuta wapi, alijisemea,
“Yani wanawake ni watu wa ajabu sana, yeye ndio mwenye makosa halafu yeye ndio wa kwanza kulalamika hapa, hata kama mimi nina makosa ila yeye hakupaswa kumficha mtoto kuhusu ukweli halisi wa mimi baba yake, hata sijui naanzia wapi kuwatafuta, ila huyu Samir huyu nadhani hanijui vizuri”
Ila akaona ni vyema arudi nyumbani kwake ili aongee na mke wake waweze kumtafuta Samir kwanza.

Mama Angel alifika nyumbani kwake akiwa amejichokea kwa kiasi Fulani siku hiyo kutokana na aliyoyaona, basi moja kwa moja alimuita Sarah na Erica na kuwauliza kuhusu Angel kuwa ameenda wapi, ndipo Sarah aliposema,
“Aliniomba simu yangu kuwasiliana na yule mchumba wake, halafu alisema kuwa anenda sijui kwa bibi”
“Aaaah jamani!!”
Mama Angel alienda chumbani kwake na moja kwa moja kumpigia mama yake simu ambaye alisema kweli Angel alienda na alichukua simu yake akisema kuwa kaagiziwa na yeye, yani mama Angel alisikitika sana ila hakumwambia ukweli mama yake na kuagana nae tu, alijiuliza mno kuwa atampata wapi huyo Angel! Aliwaza sana na kukosa jibu, ila alijipa imani kuwa Angel atarejea tu nyumbani.
Mpaka baba Angel anarudi nyumbani, bado Angel hakuwasili na kumfanya mama Angel aongee na mumewe juu ya swala hilo,
“Kheee kwahiyo ulimuona Angel na huyo Samir kabisa?”
“Ndio, yani ni upepo tu ndio umetupoteza. Kwahiyo Angel hadi muda huu yupo na yule kijana, kuan usalama kweli hapo?”
“Asilimia kubwa hakuna usalama ila tunatakiwa kuwa wapole kwasasa ili tuweze kumpata Angel”
“Tatizo tunampataje? Yani hadi nimechanganyikiwa”
“Nipatie namba ya simu ya huyo Samir!”
Mama Angel alimpatia namba aliyoitoa kwa Sarah ambapo hata kwake iliita tu bila ya kupokelewa, basi baba Angel nae aliipiga kwa muda kidogo ila haikupokelewa, na kufanya watazamane wasijue cha kufanya kwa muda huo,
“Sasa tutafanyaje mume wangu, kwanini Angel kaamua kunidhalilisha hivi?”
“Ni ujana tu unamsumbua mke wangu, halafu wamejua wazi kuwa mmewaona ndiomana hawapokei simu. Angel anajua jinsi ulivyomkali, yani hapo anajua kipigo atakachokipata toka kwako, mbona atamsahau huyo Samir muda huo huo. Nakuona mke wangu jinsi ulivyofura kwa hasira ila inatakiwa tuwe wapole kwanza ili kuweka mambo sawa”
“Hii ni aibu mume wangu, tena aibu kubwa sana. Tunafanyaje sasa?”
“Ngoja niwatumie ujumbe, inatakiwa tuwe wapole tu kwasasa mke wangu ili huyu mtoto arudi nyumbani”
Basi baba Angel akaandika ujumbe na kuutuma kwenye namba ya Samir,
“Samir, najua upo na mwanangu kipenzi Angel, mimi baba yake nampenda sana na ninatambua ni jinsi gani wewe na yeye mnapendana. Ila inatakiwa kuwepo na utaratibu wa nyie kutambulika vizuri kwetu ili muwe huru kabisa, mimi sina kipingamizi chochote juu ya mapenzi yenu. Naomba mpatie simu mwanangu Angel niongee nae japo kidogo tu, nimemkumbuka sana na ninaumia sana juu yake, natamani kusikia sauti yake ili roho yangu itulie kuwa mwanangu yupo salama”
Kisha baada ya nusu saa, baba Angel alipiga ile simu ambayo iliita kama mara mbili na kupokelewa, kisha baba Angel alianza kuongea nayo,
“Unaendeleaje mwanangu Angel?”
“Naomba unisamehe baba”
“Sina tatizo mimi, ila nahitaji kujua hali yako”
“Nipo salama baba, sijapenda kufanya hivi ila naogopa kurudi nyumbani”
“Naelewa mwanangu, ila mimi baba yako ninakuhakikishia kuwa kuna usalama kabisa nyumbani, hakuna mtu yoyote wa kukubugudhi wala nini, mimi kama mzazi nahitaji kupata heshima, sio jambo zuri kwa mtoto wa kike kama wewe kulala nje ya himaya ya wazazi wake. Nakuhitaji nyumbani mwanangu. Niambie ulipo nije kukufata”
“Mmmmh baba, naogopa mama atanipiga”
“Hapana, wala mama yako hawezi kukupiga. Niambie ulipo Angel mwanangu kipenzi, mimi nitakuja kukufata. Nimekwambia nilipo mimi hakuna yoyote wa kukudhuru, sina nia mbaya kwako wala kwa huyo Samir, tena nitakuwa namkaribisha vizuri sana nyumbani kwangu”
“Basi baba nitakutumia ujumbe wa mahali nilipo”
“Sawa, nitumie sasa hivi mwanangu maana nishajiandaa hapa, nakuja kukufata malkia wangu”
Kisha simu ilikatwa, halafu mama Angel alimuangalia mume wake na kumwambia,
“Yani mtoto kafanya ushetani kiasi hiko halafu unakazana kumbembeleza!! Akirudi hapa, kwakweli leo lazima nimfundishe adabu”
“Nani kakwambia kuwa ni fimbo pekee ndio zinafundisha mtoto adabu? Muulize mamangu mkubwa yule aliyenilea, muulize alinipiga mara ngapi ila niliweza kuelewa? Alikuwa hadi akilia yule ninapofukuzwa shule, fimbo hazifundishi mtoto mke wangu, mimi nitaenda kumfata, tafadhari usimpige Angel niachie hiyo kazi mwenyewe kama huwezi kumfundisha kwa mdomo nitamfundisha mwenyewe”
Muda kidogo ujumbe uliingia kisha baba Angel alitoka muda ule ule kwenda kumfata Angel.
Kwakweli mama Angel alitulia kwa muda na kutafakari sana huku akijisemea,
“Yani sijui damu ya Erick na Angel zimeendaje, yani hawa watu wanapatana sana. Nakumbuka Angel wakati mdogo analilia simu anaongee na Erick, hajui kuongea ila nikimuwekea simu anatulia tuli, sijui Erick alikuwa akimwambia nini mtoto, ndio anambembeleza hivi hata akiwa na makosa!! Kwakweli Angel ana haki ya kumpenda huyu, baba zetu sisi, leo angepigwa hadi meno ya mbele yangemtoka.”
Mama Angel akapumua kidogo na kuamua kutulia ili kusikilizia kuwa mwanae amefika.

Baada ya masaa kadhaa, baba Angel aliwasili nyumbani na binti yake ambapo moja kwa moja Angel alienda chumbani kwake kulala kisha baba Angel alirudi chumbani na kumsihi mke wake kuwa walale tu kwa muda huoyani hakutaka mkewe aende kumsema Angel kwa muda huo wala nini.
Kulipoucha asubuhi, baba Angel leo hakwenda popote, alitulia nyumbani na familia yake huku akiwataka watoto wake wampikie chakula ambacho anakipenda yeye ili aweze kula na kufurahi, kwahiyo walikazana kupika, muda huu wa asubuhi Erica alikuwa akipika chapati huku Angel alikuwa akitengeneza supu kwaajili ya baba yao, halafu Sarah alikuwa akichemsha maziwa basi walikuwa wakiongea mambo mengi jikoni, basi Angel akamuuliza Sarah,
“Kwahiyo Sarah ulikuwa hujui kupika?”
“Ndio, nilikuwa sijui kabisa, yani hizi ni juhudi za Erica, yeye kanifundisha mambo mengi na sasa nimejikuta naweza kupika baadhi ya vitu”
Erica akachekesha pale,
“Eti alikuwa hawezi kukaanga hata mayai”
Angel alimcheka sana Sarah na baada ya hapo waliandaa kile chakula, ila siku hiyo ile asubuhi asubuhi alifika mgeni nyumbani kwao ambaye alikuwa ni Elly kwahiyo walijumuika nae mezani katika kula kile chakula cha asubuhi.
Kwakweli, mama Angel bado alikuwa na kinyongo na binti yake kiasi kwamba hata hakuweza kwenda kukaa nao mezani na kunywa nao chai, moja kwa moja alitoka nje ya nyumba na kujifanya akifanya usafi nje ya nyumba yao, mara kidogo alifika mgeni na mgeni huyo alikuwa ni Manka, mama Angel alimkaribisha pale na kuanza kuongea nae,
“Karibu Manka”
“Sijaja kukaa sana, nimekuja kumuulizia mwanangu Sarah”
“Tena uzuri wapo wote, yani Sarah na Elly”
“Hivi na wewe unaamini kuwa Elly ni mwanangu?”
“Kama Sarah na Elly wamezaliwa siku moja, hospitali moja, halafu wewe ndio uliyeweza kumchangia damu Elly, kwanini nisiamini kuwa Sarah na Elly ni watoto wako?”
“Inamaana mzee Jimmy alimchukua mtoto wangu mmoja na kumgawa?”
“Tatizo ulikuwa karibu na mzee Jimmy ila ambacho hukujua ni kile ambacho mzee Jimmy anaweza kutenda kwa watati wowote ule, yule mzee ni mafia kama ulikuwa hujui naomba nikujuze, kwahiyo hiko kitu anaweza kabisa kukitenda tena kwa upana zaidi”
“Ila sidhani kama nilijifungua mapacha mimi?”
“Utafahamu vipi na walikupiga nusu kaputi, usikatae ndugu yangu. Haya tuseme basi ulijifungua mmoja, ila Elly ndio mwanao na yule uliyemlea miaka nenda, miaka rudi sio mwanao”
Hapo Manka alinyamaza kidogo, na kumuangalia vizuri mama Angel kisha akamwambia,
“Unamaanisha Sarah!”
“Ndio, Elly ni mwanao ila Sarah sio mwanao”
“Haiwezekani, nasema haiwezekani kabisa”
“Basi, kubali kuwa ulijifungua mapacha”
Manka alikaa chini kwanza akiwa kama mtu anayetafakari jambo, kisha aliinuka na kuondoka bila hata kumuaga mama Angel yani alijihisi kuchanganyikiwa kabisa.
 
SEHEMU YA 395

Leo, moja kwa moja Sia aliamua kwenda kwa madam Oliva sababu alifikiria mambo mengi sana kuhusu yule mtoto wa madam Oliva yani Paul.
Alivyofika pale siku ya leo, alimkuta Paul yupo mwenyewe ndani ya nyumba yani leo madam Oliva alitokana pia Steve alitoka basi alianza kuongea na Paul.
“Unajua wewe umefanana sana na mwanangu aliyepotea miaka mingi iliyopita”
“Mmmh kwahiyo una mtoto ambaye alipotea?”
“Ndio, akiwa na miezi mitatu kasoro, niliumia sana kupotea kwa mwanangu. Nakumbuka kuna alama nilimuweka”
“Hiyo alama ulimuweka klabla ya kupotea? Ulijua kama atapotea?”
“Hapana, ila nilimuweka alama tu akiwa mdogo kabisa, alipopotea niliumia sana. Nilimuweka alama pembeni ya paja la mguu wa kushoto”
Paul alimuangalia na kumuuliza,
“Alama gani?”
“Nilimuweka alama ya herufi S, nadhani kwasasa itakuwa ni ndogo sana katika mwili wake maana nilimuweka ilea lama akiwa mdogo”
“Mmmh ulimuweka na kitu gani?”
Hapo Sia alinyamaza kimya kwa muda na kuendelea kusisitiza kuwa aliweka hiyo alama,
“Lengo langu ilikuwa ni kupata kumtambua kwa haraka pindi akipotea”
“Ulikuwa unajua kama atapotea?”
“Hapana, ila kuna kipindi watoto walikuwa wakipotea sana ndiomana nikafanya vile”
“Ila unajua hata mimi nina alama hapo unaposema, tena alama yenyewe huwa nikiiangalia sana naona kama herufi S”
Hapo Sia akapumua kidogo kwani akazidi kupata uhakika kuwa yule ndio mtoto wake kabisa, basi alimwambia
“Unajua inawezekana kuwa wewe ndio mwanangu?”
“Ukimaanisha kuwa mama aliniiba?”
“Hapana, sina maana hiyo kabisa, ila huwezi jua wala walimbadilishia mtoto hospitali”
“Unataka kusema kuwa wewe ni mama yangu?”
“Sikulazimishi kuamini hilo, ila mimi niliona vyema nije kukwambia hili maana naona kuwa unafanana na mwanangu aliyepotea miaka ya nyuma iliyopita”
Paul alikaa kimya kwa muda, na kufanya hata Sia kumuaga na kuondoka zake kwahiyo alimuacha ajifikirie mwenyewe tu bila ya yeye kusema chochote kile.

Jioni hii mama Angel baada ya kuongea kwa muda na mumewe, aliamua kumfata mwanae chumbani na kuongea nae,
“Unajua kwanini leo sijaweza kula siku nzima mwanangu?”
“Hapana sijui mama”
“Sababu ya matendo yako, kwakweli Angel umeniumiza sana. Kama mama nimeumia sana”
“Nisamehe sana mama, naomba unisamehe”
“Usione nimekaa kimya ukafikiri napenda hiki ulichokifanya. Haya naomba tuongee kirafiki, ni nini kimetokea kati yako jana na Samir?”
“Nisamehe mama”
“Sio nisamehe, nimeomba uniambie kilichotokea, mimi ni rafiki yako kwasasa”
“Hakuna kilichotokea mama”
“Una uhakika?”
“Ndio, nina uhakika mama hakuna kilichotokea kati yetu”
“Kuwa makini sana Angel. Mimi ni mama yako na unaniaibisha sana, unanikosesha raha, amani na furaha, unanifanya niwe na hudhuni sana. Naomba hiki kitu kisijirudie tena, ila napenda ujue kuwa Samir ni ndugu yako”
“Aaaah sawa mama nimekuelewa”
Mama Angel alifurahi kwa mwanae kumuitikia haraka vile ila hakujua ni kwanini mwanae kamuitikia haraka kiasi kile, basi aliongea nae kidogo tu na kuondoka zake, ila Angel alijisemea,
“Yani hawa jamani, mtu mmoja unaambiwa kila mtu ni ndugu yako, yani naona dalili ya kupata ndugu dunia nzima, ila nitawafurahisha”
Kisha akaendelea na mambo yake mengine.

Usiku wa leo, wakati Erick akitaka kulala alipigiwa simu na Zaby, basi alipokea simu ile na kuanza kuongea nayo,
“Erick upo wapi muda huu?”
“Ndio nataka kulala”
“Umevaa nini hapo?”
“Kivipi?”
“Kheee wewe Erick vipi lakini, una matatizo gani yani unajibu kama vile sio mwanaume. Hivi yote ambayo huwa nafanya kwako hunielewi au kiburi”
“Kukuelewa nini?”
“Mimi nakupenda sana Erick, nahitaji uwe mpenzi wangu”
Erick alikaa kimya kisha Zaby akamwambia tena,
“Naomba kwa usiku wa leo tufanye ngono kwa njia ya simu”
Erick alikata ile simu, kisha Zaby aliendelea kumpigia kwa muda kidogo, Erick aliacha simu chumbani kwake na moja kwa moja kwenda chumbani kwa Erica ambaye alikuwa akijiandaa kulala pia, kisha Erick akamwambia,
“Naomba kwa usiku wa leo nilale pembeni yako Erica”
“Kheee kivipi? Si tulishakubaliana?”
“Ndio, ila kuna kitu sitaki kulala mwenyewe chumbani kwangu”
Muda huo huo alifika na Sarah, alisikia Erick akisema anaomba kulala humo na kusema,
“Kama Erick unakataliwa na Erica kulala humu chumbani kwake basi twende ukalale chumbani kwangu”
Erica alimuangalia Sarah na kumwambia,
“Yani wewe Sarah, laana za Elly hujazimaliza halafu unataka tena laana za Erick, una nini lakini wewe? Hujui kama Erick ni ndugu yako!”
“Najua, kwani kuna ubaya gani ninaotaka kuutenda? Si Erick kasema leo anashindwa kulala mwenyewe ndiomana mimi nimemwambia tukalale wote, kwani tatizo ni nini? Basi wote watatu tulale humu humu”
Walikubaliana, kisha wote watatu wakalala kitandani kwa Erica.

Kulipokucha, wote watatu walichelewa sana leo kuamka, kiasi kwamba mama Angel alienda moja kwa moja chumbani kwa Erick ila hakumkuta na kwenda chumbani kwa Erica na kukuta Erica, Erick na Samir wote wamelala pamoja tena wakiwa hawana habari kabisa, kwakweli mama Angel alitikisa kichwa chake na kushangaa sana, kisha aliwaamsha,
“Hivi na wewe Erick, kuja kulala na wasichana ndio nini mwanangu jamani? Hebu amka hapo, uende chumbani kwako”
Erick aliinuka na kuona hata aibu, moja kwa moja alielekea chumbani kwake, mama Angel aliwakaripia Erica na Sarah kisha kutoka zake na kwenda kumfata mumewe kumueleza,
“Nimekuta wote watatu wamelala pamoja, Erica, Erick na Sarah”
“Kwahiyo ule ugonjwa aliokuwa akiusema Sia kuwa Erica na Erick wanapendana sana ndio umehamia kwa Sarah pia!”
“Alisema ugonjwa gani?”
“Eti alisema watoto wetu wanapendana sana, upendo usio wa kawaida kabisa, nikamwambia wale ni ndugu tena ni haki yao kupendana. Akadai kuwa tuwachunguze, sasa tuwachunguze kitu gani!”
“Yule Sia nae huwa haponi kichaa chake kile, nadhani bado akili yake haifanyi kazi vizuri, ila hawa watoto leo wamenishangaza sana, kulala wote watatu halafu wamepitiliza hata muda wa kuamka. Au kwavile leo Erick haendi popote pale?”
“Itakuwa ni sababu pia, ila leo pia nitakuwepo hapa nyumbani”
Basi mama Angel na baba Angel waliendelea na mambo yake mengine.

Leo ni siku ambayo mwarabu alipata muda wa kuweza kuongea na mwanae Rahim, maana alimuita na kuanza kuongea nae kuhusu Angel,
“Rahim, niambie ukweli kuhusu Angel”
“Oooh baba kumbe umemjua Angel! Ni mtoto wangu yule, ni mtoto wangu kabisa”
“Ni kwanini hafahamiki kwenye ukoo?”
“Kwakweli baba, nakiri wazi kuwa nimefanya jambo ambalo sio sawa kabisa, nilikuwa na yule mwanamke na kumfanyia mambo mengi ya ajabu sababu ya ujana ulionisumbua. Kwa kipindi kile, mimi nilikuwa napendwa sana na wanawake, na walikuwa wakinipa pesa, nilikuwa nikipewa pesa na wanawake nami ndio nampa Erica yani mamake Angel, ila badae kuna mmoja aliiteka kabisa akili yangu basi nilijikuta kutokumpenda tena Erica, na vile ulivyonitafutia mchumba ndio kabisa sikumtaka tena”
“Ila mwanangu hilo sio tatizo, ila tatizo ni kuwa kwanini hukumuweka wazi mtoto kwa siku zote hizi?”
“Walinificha, yani Erick na Erica walikuwa wakimficha yule mtoto kwangu”
“Ungeomba usaidizi hata kwa sisi watu wazima tungekusaidia, yani ulichofanya sio sawa kabisa mwanangu”
Basi Rahim alimueleza baba yake na lile tukio la kumkuta Angel na Samir na kumfanya baba yake ashangae zaidi,
“Hiyo ni laana ujue, inawezekana vipi kaka na dada kufanya hivyo?”
“Sielewi mpaka muda huu baba, yani lile toto nimetamani hata kulitupa ila limetetewa na mama yake. Toto jinga lile kama mama yake”
“Hata wewe ni mjinga, kukataa mtoto uliyezaa mwenyewe nao ni ujingahuo, kwahiyo usimseme tu huyo wakati hata wewe ni mjinga tena mjinga namba moja kabisa. Hapa cha muhimu ni kujua cha kufanya na watoto hawa”
“tutafanyaje sasa baba?”
“Kesho, twende tukamfate huyo Angel, na aambiwe mbele ya mama yake kuwa sisi ni ukoo wake natumaini ataelewa kisha tumchukue akafahamu ndugu zake wote”
Wakaelewana kufanya hivyo kisha kila mmoja kuondoka zake.

Jioni ya siku hii, Sia alikutana na Manka na kuanza kuzungumza nae kuhusu watoto wao, ambapo Sia alimwambia Manka,
“Ngoja nikwambie kitu, yule mwanamke wa kuitwa Oliva, na yeye alijifungulia hospitali ile ile ya majanga, na hivi nikwambiavyo ni kuwa yule mtoto aliyenaye ndio mwanangu”
“Kheee na mwanae yeye yuko wapi?”
“Inawezekana mwanae akawa Sarah”
“Hebu nenda huko, haya mambo yanawezekanaje? Mbona haieleweki?”
“Inaeleweka vizuri kabisa, labda kama hutaki kuelewa kitu cha namna hii ila inaeleweka vizuri kabisa, mzee Jimmy alifanya jambo kubwa sana kwa watoto wetu. Mimi nilipewa Elly kumlea ambaye ni mwanao, Oliva alikuwa akimlea Paul ambaye ni mwanangu halafu wewe umemlea Sarah ambaye ni mtoto wa Oliva”
“Haiwezekani hiyo kitu, unajua kwanini?”
“Kwanini?”
“Ngoja nikwambie kitu leo, ili uweze kujua kuwa hiyo kitu haiwezekani”
“Haya niambie”
“Ni hivi, mimi nilikuwa na mahusiano na mzee Jimmy, wakati huo nina mahusiano na Derrick. Mzee Jimmy alinihitaji mimi nilale na Erick ili niweze kuzaa na Erick, sijui alikuwa na lengo gani juu ya hilo, basi tulimnyeshwa pombe sana Erick na mimi nikaenda kulala nae”
Hapo Sia alishtuka kidogo na kumuuliza vizuri Manka,
“Ni kweli ulilala na Erick?”
“Aaaah hiyo ni siri yangu, ila nilipotoka hapo nilienda kulala na mzee Jimmy ila kipindi hiko nilikuwa tayari nina mimba na nilikubali kufanya vile ili kumsingizia mzee Jimmy mtoto sababu ana mali aweze kumtunza mtoto wangu. Nilipomwambia nina mimba, hakusema hata kidogo kuwa ni mimba ya Erick ila alisema kuwa ni mimba yake na alifurahi sana juu ya hilo. Yani hadi najifungua, mzee Jimmy alikuwa akiamini kuwa Sarah ni mtloto wake, tena alimpa jina la mamake mzazi, alimuita Sarah basi ndio jina hilo amekuwa nalo hadi sasa, kwahiyo mzee Jimmy aliamini kuwa Sarah ni mtoto wake, iweje ambadilishe?”
“Sasa jiulize, iweje Elly awe mtoto wako? Cha kukusaidia tu nenda kapime damu na Elly, ila hakuna haja ya kupima mbona inaonyesha wazi kuwa Elly ni mwanao? Unakataa vipi Manka? Kubali au kata, mzee Jimmy kakufanyia mchezo labda sio mimi ninayekwambia haya, nenda kamshikilie huyo dokta Jimmy vizuri akwambie ukweli nimemaliza”
Sia aliondoka zake, na muda huo Manka nae aliondoka zake huku akiwa na mawazo sana na moja kwa moja aliona ni vyema amfate dokta Jimmy.

Usiku wa leo, wakati baba Angel akijiandaa kwaajili ya kulala alipigiwa simu na mama yake na kuamua kupokea simu ile,
“Pole mwanangu kwa mimi kupiga usiku huu ila nakuomba kesho asubuhi twende pamoja hadi kwenye kaburi la mzee Jimmy”
“Kuna nini mama?”
“Kuna jambo la muhimu sana, kuna mtu kaniambia, inapaswa twende ili tuonane na huyo mtu”
“Ni nani huyo?”
“Ni mlinzi wa pale, kuna jambo huwa linaendelea kwenye kaburi la baba yako yule. Nahitaji twende kwani kuna mambo mengi yamuhusuyo mzee Jimmy nimeyatambua”
“Sawa mama”
Basi ile simu ilikatika kisha mama Angel alimuuliza mumewe ambaye alimjibu kitu ambacho kilikuwa kinazungumzwa mahali hapo, basi mama Angel akamwambia,
“Mmmh jamani mimi huko kaburini kwa huyo mzee huwa napata hofu sana katika moyo wangu, yani nakosa raha na amani kabisa”
“Usijali mke wangu, nitakuwa salama kabisa”
“Haya, tufanye yetu basi maana nishaanza kuigopa siku ya kesho”
Baba Angel alitabasamu ila upande mwingine aliipenda ile kauli ya mke wake.

Asubuhi na mapema, baba Angel alitoka na kukutana na mama yake kisha safari yao ilikuwa moja kwa moja kwenye kwenye kaburi la mzee Jimmy huku wakiongea mambo mengi sana njiani.
Walipofika pale, walisogea hadi kwenye kaburi ila walishangaa sana kumuona mwanamke akigalagala juu ya lile kaburi huku akilia sana.........

Walipofika pale, walisogea hadi kwenye kaburi ila walishangaa sana kumuona mwanamke akigalagala juu ya lile kaburi huku akilia sana.
Mama mzazi wa Erick, alisogea pale karibu na kaburi na kumuangalia kwa makini yule mwanamke, ndipo Erick alipogundua kuwa yule mwanamke alikuwa ni Manka, basi wakamkalisha na wao walikaa pale pale juu ya kaburi la mzee Jimmy na kumuuliza vizuri huyu mama,
“Tatizo ni nini Manka?”
“Sikujua kama mzee Jimmy ni mtu mbaya kiasi hiki”
“Kivipi?”
“Yani, wakunibadilishia mtoto mimi kweli?”
Baba Angel na mama yake walitazamana kwa muda, ambapo baba Angel alimpa maelezo mafupi mama yake kuhusu mtoto aliyenaye Manka, kisha alimuuliza,
“Inamaana Sarah sio mwanao?”
Manka alilia sana na kusema,
“Sarah sio mwanangu jamani, mwanangu ni Elly mimi, sitaki kukubali hiki kitu”
Baba Angel alishangaa kwakweli na kumuuliza,
“Kwahiyo wazazi wa Sarah wako wapi?”
“Ooooh niacheni jamani mimi, Sarah binti yangu kipenzi, kwanini mzee Jimmy kanitenda hivi mimi, nimemkosea kitu gani? Kwanini anifanyie hivi jamani?”
“Dah!! Pole sana”
“Kwakweli, huu mzee ipo siku mimi nitamfukua na kumzika tena sio kwa jambo hili alilonifanyia mimi”
Kisha Manka akainuka na kuondoka zake, na kufanya baba Angel na mama yake kuangaliana kwa muda kisha mamake baba Angel akasema,
“Yani huyu Jimmy akili zake sijui zikoje, mambo yake ya kujaribu vitu ndio yalifanya nimkimbie, hata nisiweze kuishi nae, Mungu anawapa pesa na vichaa wanatusumbua tu duniani kama huyu mzee, hela ilimchanganya sana huyu. Sasa kumbadilishia mwenzie mtoto ndio nini?”
“Mama, sio huyo tu yani baba kabadilishia wengi sana watoto hata sijui alikuwa na maana gani au alikuwa akitaka kitu gani toka kwenye hilo jaribio lake”
“Duh!! Hiyo hatari sana, haya twende kwa yule mlizni tuongee nae”
Basi moja kwa moja walienda kwa mlinzi wa eneo hilo ambaye aliwaona fika wakiongea na Manka pale ila alikuwa akiwaangalia tu, kwahiyo walivyomfata na kusalimiana nae, baba Angel alianza kumuuliza,
“Yule mwanamke aliyekuja unamfahamu vizuri lakini?”
“Ndio namfahamu, hata leo namshangaa kuja kulia na kugalagala pale kwenye kaburi labda kamkumbuka sana mzee”
“Alikuwa akija mara kwa mara?”
“Ndio, alikuwa anakuja na binti yake mmoja hivi, utakuta wanaleta maua na mishumaa kuzunguka kaburi la mzee ila leo nimeshangaa kwa kitendo chake kuja kulia, tena mwanzoni alikuwa akilia kwa nguvu kama mtu aliyefiwa”
Basi mamake baba Angel alianza kuongea na yule mlinzi sasa,
“Eeeeh ile simu uliyonikurupua nayo jana, na kusema kuwa nije huku ulikuwa unamaana gani?”
“Unajua watu ambao huwa wanakuja huku kwenye kaburi la mzee mara nyingi ni watu walewale yani hata sura zao nimezizoea, ila jana kuna mtu amekuja wa tofauti sana, alikuwa amevaa miwani”
“Hukumuuliza?”
“Nilimfata, nikamuuliza kuwa yeye ni nani?”
“Akasema kuwa yeye ni rafiki mkubwa sana wa mtoto wa mzee Jimmy, ambaye ktoto huyo anaitwa Erick”
Baba Angel akamuangalia kwa makini na kumuuliza,
“Nani huyo?”
“Sijui, hakunitajia jina lake ila alisema kuwa yeye ni rafiki yako mkubwa sana, pia alisema kuwa kuna siri kubwa sana ipo kwenye familia yako”
Baba Angel akashtuka hapa na kuamuangalia kwa makini huyu mlinzi kisha akamuuliza,
“Siri gani hiyo?”
“Alisema kuwa nikwambie umtafute dokta Jimmy, umwambie kuwa umeujua ukweli, ni bora yeye akueleze ilivyokuwa maana ukweli umeujua. Kasema dokta Jimmy atakuelezea ilivyo halafu yeye atakuja kumalizia”
“Mmmh sielewi”
Mamake akaingilia kati na kusema,
“Hapo inatakiwa tu uelewe mwanangu, hakuna ya sielewi ukaeleweka wala nini, yani unatakiwa uelewe tu mwanangu”
“Kwahiyo tufanyaje mama”
“Ni kumtafuta huyo dokta Jimmy, hakuna namna ni kumtafuta tu”
“Sawa, itabidi nifanye hivyo”
Waliongea na yule kisha waliamua kumuaga ambapo baba Angel aliamua kumpeleka kwanza mama yake sehemu aliyofikia kisha yeye ndio kufanya safari ya kurudi nyumbani kwake.

Mama Junior akiwa nyumbani kwa Junior huku amembeba mjukuu wake, alisikia simu yake ikiita ila alipoletewa ilikuwa tayari imeshakatika na kumuomba Junior ampatie simu yake ili aweze kupiga,
“Ni baba yako ndio alikuwa akipiga, naomba tu simu yako nimpigie”
Basi Junior alimuachia mama yake pale simu halafu yeye alienda zake dukani kwa muda huo, mama Junior alipiga kwa mumewe ila mumewe alimwambia,
“Nipe kama nusu saa mama Junior, nitakupigia mwenyewe”
Simu ilikatika, muda ule ule kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya Junior, mamake aliposoma mtumaji aliona jina Daima, na kushangaa sana kuwa mwanae bado anaendeleza mawasiliano na Daima, basi akafungua ule ujumbe na kuusoma,
“Safari hii Junior, uje na kinga. Maswala ya kupata mimba tena halafu nionekane malaya sitaki”
Kisha ukaingia ujumbe mwingine toka kwa huyo huyo Daima,
“Mbona hilo nalijua wazi kabisa kuwa huyo mtu mzima humpendi wamekulazimisha tu kumuoa, yani mara nyingine wazazi wana mambo ya ajabu sana, unaweza hata kuwawekea sumu na kuwamaliza kabisa”
Mama Junior alisikitika sana, kuna ujumbe mwingine ukaingia kutoka kwa huyo huyo Daima,
“Nakupenda pia Junior, wewe ndio mwanaume wa maisha yangu”
Yani mama Junior aliumia sana moyo wake, hakutaka fanya kitu kwanza zaidi ya kufuta zile jumbe zote, kisha akamuita Vaileth na kuanza kuzungumza nae,
“Eti Vai mwanangu, ni jinsi gani unampenda Junior?”
“Nampenda sana, yani nampenda sana”
“Kwa asilimia ngapi unampenda?”
“Sijui ila kwa asilimia zote nampenda Junior, kiasi kwamba sitaki kumkosa katika maisha yangu”
“Kwasasa mnashirikiana nae vizuri tu kama mke na mume?”
Hapo kidogo Vaileth aliona aibu ila alijibu,
“Ndio”
Basi mama Junior alimkabidhi Vaileth mtoto kisha aliinuka na kumsubiria mwanae arudi, yani alimsubiria nje ya nyumba kabisa. Aliporudi tu, mama Junior alimzaba kofi na kumuuliza,
“Vaileth unampenda au humpendi?”
“Mbona nampenda mama?”
Huku Junior akiugulia lile kofi alilozibuliwa na mama yake,
“Unampenda na Daima je?”
Junior akajiuma uma, kisha mama yake akamwambia,
“Junior ukiniletea ujinga wako wewe mtoto, utafanya nikupige wakati una familia tayari, naomba ujinga uache Junior, nimemaliza”
Kisha Junior alichukua simu yake na kurudi nayo ndani tu moja kwa moja.

Kama ambavyo mwarabu na Rahim walipanga, basi siku hii moja kwa moja walienda nyumbani kwa mama Angel ili kuweza kuongea vizuri na Angel na kama ikiwezekana wamchukue Angel aweze kutambulikana na ndugu zake wengine.
Mama Angel alipowaona tu alitoka nje kwenda kuzungumza nao,
“Eeeeh niwasaidie nini?”
Mwarabu alimuangalia mama Angel na kumwambia,
“Kheee mwanamke mkavu wewe loh!! Yani umekuja hapa kabisa, niwasaidie nini kwani hujui shida yetu? Shida iliyotulea hapa ni mtoto, namuhitaji Angel akawatambue ndugu zake, mimi ndio babu yake nimesema”
“Aaaah sawa”
Mama Angel hakuwakatalia kwani muda huo huo alienda ndani na kumuita Angel ambaye alitoka nje na kuwakuta wale watu na kuwasalimia, kisha mama Angel akawaambia,
“Angel mwenyewe huyo hapo”
“Mtambulishe sasa mtoto sio kusema kuwa Angel mwenyewe huyo hapo, kwani wanawake kwanini mnakuwa na visirani kiasi hiko!! Ukimtambulisha utapungukiwa na nini?”
Mama Angel alimuangalia mwanae na kumwambia,
“Angel, huyu ndio baba yako mzazi anaitwa Rahim na huyu ndio babu yako yani baba yake na huyu Rahim”
“Mama, sikuelewi”
“Hunbielewi nini sasa na wakati nilikwambia kila kitu”
“Ndio uliniambia ila mama sikuelewi kwakweli, mimi nishasema sina mababa wawili. Baba yangu ni mmoja tu na yeye anaitwa Erick, haya mengine sitaki kuyajua”
Kisha Angel alikimbilia ndani, mwarabu alimuangalia mama Angel na kumwambia,
“Umemfundisha vitu gani mtoto? Lazima umemfundisha mambo yasiyokuwa mazuri, nyie wanawake mna nini lakini, Mungu anawaona kwa haya mnayoyafanya kwa watoto”
“Hata mwanaume unapomkana mtoto kumbuka kuwa Mungu anaona maana si vizuri kukana damu yako”
“Haya, hayo yameisha, mtoto umemwambia nini hadi atutaki kabisa?”
“Sina jibu”
Mwarabu hakuwa na sababu ya kuendelea kuwa hapo na kumtaka kijana wake tu waondoke kwa wakati huo.

Baba Angel akiwa amechoka kutokana na kwenda kutembelea kaburi la mzee Jimmy, na vile jinsi walivyomkuta Manka akiomboleza kwenye kaburi, alitaka moja kwa moja alale ila Mama Angel alimua kumueleza kuhusu ujio wa mwarabu na Rahim na jinsi Angel alivyofanya kiasi cha wakina Rahim kuhisi kuwa amemfundisha vibaya mtoto wake,
“Yani huyu Angel ni balaa ujue, ndio kaondoka kabisa, mtoto ana dharau huyu sijapata kuona”
“Kwahiyo tufanyeje mke wangu?”
“Sielewi kwakweli, ila huyu mtoto ni mtihani halafu wakina Rahim wanataka kumtambulisha kwa ndugu zake. Hili ni tatizo kwakweli maana mtoto haujui ukweli toka siku nyingi, hili ni tatizo kwakweli”
“Basi kosa ni lako kwa kumficha mtoto, mama Angel kwakweli kichwa changu kina mambo mengi sana kwasasa, yani sijui kama nitaweza kuendelea kufikiria hayo ya wakina Rahim kwakweli. Nadhani nifanye yangu kwanza halafu ndio nifikirie hayo ya wakina Rahim”
Kwa muda huo baba Angel aliamua tu kulala.
Kulipokucha tu, Angel ndio alikuwa wa kwanza kugonga mlango wa wazazi wake, kisha alimuomba baba yake aweze kuzungumza nae, basi baba yake alitoka na moja kwa moja kwenda nae kwenye sebule yao nyingine ili kuzungumza nae,
“Niambie Angel”
“Bado kuna utata kuhusu maisha yangu, mimi ni mwanao au sio mwanao”
“Kwani ni kitu gani unataka kufahamu Angel?”
“Nataka kufahamu ukweli”
“Upo tayari kwaajili ya kuubeba ukweli?”
“Ndio baba”
“Ipo hivi, mimi nilikupenda sana, na nilimpenda mama yako, niliamua kumuoa ili wewe ubaki kuwa mtoto wangu milele”
“Kwahiyo mimi sio mtoto wako baba?”
“Hapana, sijasema hivyo”
Yani baba Angel alikuwa akiona hili swali ni gumu sana ingawa kwa wakati huo alielewa wazi kuwa yeye ndio anayetakiwa kutoa ukweli kwa Angel dhidi ya baba yake ila kila anapojaribu kumwambia, aliona ulimi wake kuwa mzito sana, alijiona wazi akishindwa kuzungumza kuhusu swala hilo kabisa, yani alikosa amani katika moyo wake.
Basi alimpooza tu pale Angel na kumuhakikishia kuwa yeye ndiye baba yake mzazi kisha akarudi chumbani kwake na kuongea na mke wake,
“Roho inanisuta sana kung’amg’ania uongo kuwa ukweli kwa Angel ila nawezaje kumweleza Angel ukweli ikiwa hautaki huo ukweli?”
“Hapo ni pagumu ila kwa nilichomweleza ni wazi Angel amefahamu ukweli halisi ila hataki tu kukubaliana na ukweli. Acha muda utasema na atakubaliana tu na ukweli halisi, na hivi Rahim ana watoto kama mchanga, nahisi Angel atachukia sana kuwafahamu hao ndugu zake”
“Dah!! Ngoja niondoke, leo nitaenda ofisini ila kesho nitaenda kumfata huyo dokta Jimmy ili niweze kuongea nae vizuri”
Baba Angel alijiandaa na kuondoka zake kwenda kazini.
Muda mfupi tu, mama Angel alipigiwa simu na Manka na kuanza kuongea nae, yani Manka alikuwa akiongea huku akilia,
“Tatizo nini Manka?”
“Unajua mzee Jimmy ni mzee mpuuzi katika wote chini ya jua”
“Kivipi?”
“Unajua kama Sarah sio mtoto wangu halafu Elly ndio mtoto wangu”
“Kheee nani kakwambia? Na Sarah ni mtoto wa nani?”
“Wakina Erick hawajakueleza au? Nimejikuta jana nikiomboleza juu ya kaburi la mzee Jimmy, yani sina raha hata kidogo, hivi mimi nafanyeje? Nishamzoea Sarah mimi”
“Kwahiyo Sarah ni mtoto wa nani?”
“Sijui, yani sijui ni mtoto wa nani naomba hilo fatilieni wenyewe maana huyo mtoto kafanana na ukoo wenu, kwakweli mzee Jimmy alaaniwe huko huko kaburini alipo”
Kisha Manka alikata ile simu na kumuacha mama Angel akiwa na swali moja tu kichwani kuwa Sarah ni mtoto wa nani.
 
SEHEMU YA 397

Asubuhi na mapema, walishtuliwa na mlio wa simu ya baba Angel ambapo aliichukua na kupokea ila aliyepiga alikuwa ni Manka na alikuwa akilia sana huku akisema,
“Dada yangu Linah amekufa”
Baba Angel alishtuka sana na kushangaa.
Mama Angel alimuangalia kwa makini na kumuuliza,
“Kwani kuna nini?”
“Nasikia Linah amekufa”
“Kheeee mbona makubwa haya, imekuwaje tena?”
“Ukitaka kujua imekuwaje jiandae hapo twdende huko msibani ili tujue kilichotokea maana hata mimi hii habari imenishtua”
“Mmmmh!”
Mama Angel alijiandaa, kisha baba Angel akajiandaa pia, kwahiyo walipokuwa wakitoka waliwaambia wakina Erick wasiende popote tena kwani wao wanatoka, kisha wakaondoka zao.
Nyumbani walibaki wakina Erick tu wakijiuliza kuwa kuna kitu gani,
“Kwani nini kimetokea?”
“Mmmh hata sijui”
Muda kidogo, alifika pale mama Sarah na kumuita mwanae ambaye alitoka ndani na kumkuta mama yake akiwa amejaa machozi, kisha mama Sarah alisogea na kumkumbatia Sarah huku akimwambia,
“Mwanangu, mamako mkubwa amekufa”
“Nani mama, yupi? Mamkubwa Linah?”
“Ndio mwanangu, mamako mkubwa Linah amekufa”
Sarah alihisi kama kuchomwa na kitu katika moyo wake kwani ilikuwa ni habari ya gafla sana kwake, alilia sana na hapo kuamua kuondoka na mama yake ili kuelekea msibani na kujua kitu kitakachoendelea.

Nyumbani alibaki Angel na wadogo zake, ambapo bibi yao alipiga simu na moja kwa moja alipokea Angel ile simu,
“Mama yenu yupo?”
“Hamna, ametoka bibi”
“Katoka na mtoto?”
“Hapana, Ester yupo”
“Basi nikuombe kitu”
“Niambie bibi ni kitu gani?”
“Naomba uje na Ester, mlete Ester nyumbani kwangu hapa. Jitahidi ufanye hivyo Angel”
“Sawa bibi”
Kisha Angel aliandaa chai na kunywa, halafu kumlisha vizuri Ester na kumuomba dereva wao ili awapeleke yeye na Ester kwa bibi yao.
Basi Erica akauliza,
“Kwahiyo ndio unaniacha mwenyewe!!”
“Mwenyewe kivipi? Si upo na Erick tatizo liko wapi?”
“Basi tuondoke wote, mimi, wewe, Ester na Erick”
“Halafu hapa nyumbani abaki nani? Kumbuka mama hajui kitu, halafu yeye na baba wameondoka tu, jitahidi hapa nyumbani ubaki na Erick, usiende popote Erica, angalieni hata sinema jamani”
Kisha Angel alimchukua Ester na kuondoka nae, kwahiyo pale nyumbani walimuacha Erick na Erica tu.

Baba Angel na mama Angel, wakiwa kule nyumbani kwa Linah, ndio wakapata taarifa vizuri sasa kutoka kwa mdada wa kazi wa Linah,
“Kwani ilikuwaje?”
“Mama, aliniambia nimweleze mtu mmoja tu”
“Mtu gani huyo?”
“Alisema anaitwa Erick”
Basi mama Angel na baba Angel waliangaliana kwa muda kisha mama Angel alisogea pembeni halafu baba Angel alimwambia yule mdada wa kazi,
“Mimi ndio Erick”
“Mama alikuwa akiumwa sana kwa siku nzima ya jana, hali yake ilikuwa mbaya, aliamua kupiga simu kwa mtu aliyeitwa Erick alisema kuwa mtu huyo akifika anaweza kuokoa maisha yake. Alikataa wote kumpeleka hospitali hadi huyo Erick afike, na hakutaka tumueleze mtu yoyote hadi afike Erick. Tulikaa kama lisaa bila huyo Erick kufika, mama akaomba karatasi na peni aliandika ujumbe na kunipatia mimi, kisha alisema huo ujumbe usisomwe na mtu yoyote yule zaidi ya Erick, nilipoenda kuhifadhi ule ujumbe chumbani kwangu, niliporudi nikamkuta tayari mama ameshaaga dunia”
Yule mdada wa kazi alianza kulia, ikabidi baba Angel amnyamazishe, huku akimuomba ampatie ule ujumbe, basi yule dada alienda kutafuta ule ujumbe, ila muda kidogo pale alifika mama Sarah akiwa ameongozana na Sarah sasa sababu ndiye mtu aliyeona ataweza kumfariji kwa wakati huo wa kuondokewa na dada yake mpendwa.
Ila mama Sarah alimsogelea Erick na kuanza kumpiga kama vibao huku akilalamika na kulia,
“Utatumaliza ukoo wote mjinga wewe”
“Kwani nimefanyaje Manka jamani!”
“Mjinga wewe, dada yangu nasikia alikuwa akihitaji sana msaada wako, ila ulivyo na roho mbaya umeshindwa hata kuja kumsaidia kweli! Mbaya sana wewe”
Hapo mama Angel alisogea maana hakuelewa ile hali ila mumewe alisogea nae pembeni na kumueleza kwa kifupi, na kufanya mama Angel ashtuke,
“Mmmh kwahiyo hizi lawama za kifo cha Linah sasa zinataka kunihangukia mimi? Wazima wa akili kweli hawa? Mimi ndio nilimwambia atembee na mwane, mimi ndio nilimshauri kutoa mimba? Nilichofanya ni kumzuia mume wangu kwaajili ya ndoa yetu, nina upendo na mume wangu, kwani Linah ana ndugu wangapi kwanini asiwapigie wote hao simu aje kumpigia mume wangu? Jamani, sitaki hizi lawama kabisa, nahisi kuchanganyikiwa, ngoja niende kwa mama yangu”
Mama Angel hakutaka hata kusikia kitu kwa muda huo kwani alipanda kwenye gari na moja kwa moja alifanya safari ya kwenda kwa mama yake.

Erick na Erica walikuwa wenyewe ndani kwao, walipokunywa chai tu waliambizana waende sebule nyingine ya nyumba yao,
“Twende kule Erica tukaangalie muvi”
“Zile alizokuwa akileta Samia?”
“Ndio, tukiangalia hapa haipendezi, tufanye kama kipindi kile kwa kuangalia kwa kificho, kipindi kile wakati tunaangalia na Junior”
“Sawa twende tu”
Kisha waliinuka na kwenda kwenye sebule nyingine ya nyumba yao na kuanza kuongea ambapo Erick alimuuliza Erica,
“Hivi imekuwaje? Jana mimi na wewe tulipanga kwenda sehemu ya mbali ambapo sehemu hiyo tungekuwa wawili tu ila leo eti tumeachwa wawili tu humu ndani, hii umeielewa kweli Erica?”
“Kwakweli nimeshindwa kuelewa kabisa, ni kwanini tumeachwa wawili tu”
“Mmmh au wanataka tujaribu”
“Tujaribu nini sasa?”
“Ile tuliyopanga siku ile ya wote wawili kubaki watupu kabisa”
“Mmmmh!!”
Erica alijihisi moyo kwenda mbio sana kisha Erick akamwambia,
“Ngoja nikafunge mlango wa chini”
Yani Erica alikuwa akihema sana kwa muda kidogo, kisha Erick alirudi toka kwenye kufunga mlango na kumwambia Erica sasa,
“Kuna kitu tufanye kwanza”
“Kitu gani?”
“Twende kuoga pamoja”
“Yani mimi na wewe?”
“Ndio, kwani tatizo nini? Mbona zamani tulikuwa tukifanya hivi? Ni mara ngapi tumeoga wote, ni mara ngapi tumelala wote?”
“Ila kweli, kwani kuna nini kitatokea?”
“Sijui, ila kikitokea chochote itakuwa ni siri yetu maana humu ndani tupo wawili tu”
Wakaongozana muda huu, hadi chumbani kwa Erick kisha kila mmoja alitoa nguo na kwenda kuoga pamoja, ila walipotoka kuoga kila mmoja alijikuta akishikwa na matamanio zaidi kwa kumtazama mwenzie kiasi kwamba hadi wote wawili walipatwa na aibu kubwa sana, Erica alijiziba uso kwa aibu, Erick alimsogelea na kumkumbatia na kufanya Erica aongee kwa sauti ya kutetemeka,
“Unataka kufanya nini Erick?”
“Sijui”
Walijikuta kwa pamoja wakikumbatiana kwa nguvu sana.

Angel akiwa na mdogo wake, walifika moja kwa moja kwa bibi yao na kumkuta bibi yao akiwa na mgeni mwingine pale, basi bibi yao alifurahi sana na kuwakaribisha, huku akianza kuwatambulisha kwa yule mgeni,
“Huyu ni bibi yenu pia, anaitwa Ester, nimekuita na mtoto ili aweze kumuona wajina wake”
“Aaaah sawa”
Basi alimasalimia pale na kuanza kuongea mambo mbalimbali ya kuhusu shule na kila kitu ambacho kilikuwa kikiendelea, basi Angel alimuacha pale Ester kwa bibi yake na yule mgeni halafu yeye aliaga kuwa anaenda dukani, bibi yake alimkubalia tu.
Angel alitoka nje na kwenda kukutana na Samir ambaye alikuwa ameshampigia simu toka anatoka kwao, kwahiyo Samir moja kwa moja alienda pale kwa bibi yake Angel. Walisimama nje na kuanza kuongea,
“Yani nilipopata nafasi tu ya kutoka nyumbani nikaona cha kwanza kabisa nikutafute wewe Samir, kwakweli nimekumiss sana”
“Mimi zaidi Angel, huwa muda wote nakuwaza”
“Eeeeh kwanza ikawaje siku ile, maana hata hatukuongea vizuri, kwenu ilikuwaje?”
“Sio ilikuwaje tu ila kwetu ni balaa, baba yangu hataki kusikia kabisa habari za mimi kuwa na wewe, nasikia alirudi nyumbani na kufoka sana. Mama alinipigia simu akasema nisirudi kabisa nyumbani, basi toka siku ile nakaa kwa mjomba, yani nyumbani kwetu ni balaa, hapakaliki, nasikia baba kamwambia mama kuwa hataki kuniona.”
“Ila baba yako nae loh!! Anataka nini kwani?”
“Sijui mwenyewe, sijui anafikiria nini. Kanisema sana, eti anahofia wewe utapata mimba yangu, halafu cha kushangaza eti baba yangu ameanza kusema wewe ni mwanae eti, mimi na wewe ni ndugu”
“Khaaaa!! Baba yako anaitwa nani kwani?”
“Anaitwa Rahim”
“Khaaa mimi sio mwanae kabisa, asiniletee balaa. Sikia Samir, siku hizi pale nyumbani kwetu huwa wanatoka toka sana, kiasi kwamba nahisi nitabaki peke yangu pale nyumbani”
“Naomba siku ya kubaki mwenyewe uniite”
“Mbona umewahi! Ndio nilikuwa nataka kukwambia hivyo hivyo”
Kuna gari waliiona kwa mbali inakuja, Samir alishtuka na kumwambia Angel,
“Sio gari ya mama yako ile?”
Angel alipoangalia aliona kuwa ndio yenyewe, basi Samir muda huo huo akazunguka kidogo na kuondoka, halafu Angel akaingia ndani na kutoa vyombo vichafu nje na kuanza kuviosha.
Muda kidogo tu mama yake aliingia ndani na kumuuliza bila hata salamu,
“Angel, umekuja kufanya nini huku? Na mbona niliona mtu kama wewe umesimama na mwanaume nje?”
“Aaaah ni bibi kaniita nimlete Ester mdogo, halafu sijaenda nje mama. Nilenda dukani tu, na sasa nimeona nimsaidie bibi kuosha vyombo maana bibi hana msichana wa kazi kwasasa”
“Mmmmh ila wewe mtoto!!”
Kisha mama Angel aliingia ndani na kufurahi sana kumuona yule mama wa kuitwa Ester, basi aliwasalimia pale na kuanza kuongea nao, ambapo bibi Angel alianza kwa kuomba msamaha kwanza,
“Kwanza mwanangu nisamehe kwa kumwambia Angel aje bila ruhusa yako, hii ni kutokana na kupiga simu yako bila ya kupokelewa, basi nikaona ni vyema nimwambie Angel aje maana ni mkubwa sasa”
“Ni kweli, amekuwa mkubwa kwasasa”
“Ila mtoto Ester jamani, ni mpole hadi raha, yani mtoto sio mlizi kabisa”
“Ni kweli mama, huyu sio mlizi, ukimuona analia ujue njaa, halafu usimuone kimya huwa ana mtindo wa kusoma mazingira. Kama unamkumbuka vizuri Angel alipokuwa mdogo basi ndio kama huyu Ester, yani yeye anasoma mazingira halafu anaweza kuja kukuumbua badae. Kuna siku nilimficha kitu baba yao, nilitaka kumuonyesha kwa kumshtukiza tu, kheee kumbe Ester kaniona nilipoficha, yani baba yao aliporudi tu akawa wa kwanza kumtolea na kumpatia”
Wote wakacheka kisha bibi Angel alisema,
“Kaanza mapema umbea wa Erica jamani. Sijamuulizia mjukuu wangu bingwa wa kupika anaendeleaje?”
“Hajambo, naona nyumbani atakuwa kabaki na kaka yake tu”
Yule Ester mkubwa akasema,
“Halafu hao watoto hamjawahi kuwaleta kwangu jamani, muwalete siku moja wajukuu zangu”
“Usijali mama tutawaleta, nilikuwa nangoja wamalize shule ndio nianze kuzunguka nao”
Waliongea mengi sana pale, kisha yule mama ambaye aliitwa Ester pia aliondoka kwa muda huo, ni Angel ndio aling’ang’ania kumsindikiza yule mama, kwahiyo mama yake na bibi yake waliishia njiani, kisha Angel ndio alimsindikiza hadi kituoni huku wakiongea mambo mbalimbali.
“Umeokoka Angel!”
“Mmmh nimeokoka lakini kidogo”
“Kwanini?”
“Wokovu mgumu, masharti yake magumu”
“Nani kakwambia hivyo Angel? Siku njoo nyumbani kwangu tuongee vizuri, mwambie mama akuelekeze”
“Sawa hakuna tatizo”
Yule mama alipanda basi na kuondoka kisha Angel alimpigia tena simu Samir ambaye hakuwa mbali, halafu alianza kuongozana nae kurudi kwa bibi yake,
“Kwani mama yako kaja kufata nini?”
“Najua basi!! Sijui kitu gani kimemleta huyu, mama ana machale balaa”
“Na huyu mgeni ndio alikuwa ndani kwenu?”
“Ndio, ananiambia niokoke”
Samir alicheka sana na kusema,
“Ili nikukose, wanaokokaga waliozeeka kama yeye”
Wote wakacheka sana na kufurahi kwa muda huo, kisha Samir alimsindikiza Angel hadi kwa bibi yake huku wakipanga kuwasiliana vizuri kwa siku zijazo kwani Angel alisikia sikia kuhusu safari ya Erick na Erica kwahiyo akawa na uhakika siku wakiondoka hao basi hapo kwao kutakuwa hakuna mtu mwingine zaidi yake.
 
SEHEMU YA 398

Mama Angel alimueleza mama yake kuhusu tukio la Linah na jinsi walivyopata ujumbe kuhusu kifo cha Linah,
“kwahiyo ndio wanalaumu hapo mama, sasa kosa langu ni nini hapo?”
“kwani nani kasema kuwa ni kosa lako?”
“Baba Angel huyo, anadai kuwa nisingemkataza basi huyo Linah angepona, nawezaje kumkubali mume wangu aende kumsaidia usiku mwanamke aliyewahi kuwa na mahusiano nae jamani!”
“Huo ujinga hata mimi niliukataa hata kipindi nipo na baba yenu, naita ni ujinga huo tena ni ujinga kabisa, ni mume wangu halafu akatoe msaada kwa mtu usiku ambaye aliwahi kuwa na mahusiano nae, tena huyo mtu ana ndugu zake. Kuna uhakika gani? Akienda kule na kukumbushiana je na ruhusa umetoa wewe mwenyewe!”
“Aaaah ila mama nimefikiria kitu”
“Kitu gani?”
“Kwanini ile usiku nisingemwambia mume wangu twende wote!”
“Kweli ni jambo jema hilo ulilofikiri, ila mwanangu naomba usijihukumu kwa hilo. Kitu kimeshatokea, huwezi jua ni kwanini imekuwa hivi, kila kitu katika maisha kina sababu zake”
Bibi Angel na mama Angel waliendelea kupeana moyo pale, na kisha Angel aliporudi ilibidi wajiandae kwaajili ya kurudi nyumbani maana na muda nao ulikuwa umeenda.
Walipokuwa kwenye gari na Angel wakati wa kurudi, njiani alimuoa rafiki yake Johari ndipo alikumbuka pia ujumbe ambao aliwahi kupewa na mumewe ila hakuufanyia kazi kwa kumtafuta Johari wala nini, ilibidi asimamishe gari na kushuka kisha alianza kuongea na Johari kidogo,
“Wapi unaenda muda huu Johari?”
“Narudi nyumbani kwangu yani kwa mume wangu, nimetoka huko kwetu”
“Salama lakini?”
“Salama wapi ndugu yangu! Si unakumbuka mtoto wa kwanza mimi nilizaa na yule mwalimu wa nidhamu, unakumbuka lakini?”
“Nakumbuka ndio”
“Unajua kwanini hakunioa?”
“Kwanini?”
“Mwalimu mjinga yule, alinidanganya mimi kumbe alikuwa na mke wake, kipindi yupo na mimi yule mkewe alikuwa safarini tena alikuwa kwenye likizo ya uzazi huko kwao halafu ndio akanidanganya mimi na kuzaa na mimi jamani. Yani watu wengine hadi kichefuchefu. Haya sasa unajua kilichotokea?”
“Nini kimetokea?”
“Yule mwalimu alidai mtoto wake alee mwenyewe, basi sikugoma ikabidi tumruhusu tu amlee, na kweli kamlea sasa kidato cha pili toto likapata mimba, mweeeh yule mwanaume kamtimua mtoto nyumbani kwake, basi akaja kwangu analia, kama kawaida wamama ndio tunabeba madhaifu yote, nakwambia nikaongea na mume wangu na yeye hakuwa na hiyana, tumelea mtoto kwa kipindi chote hiki wala hakuna nini wala nini. Sasa kuna siku mume wangu kamuuliza baba wa yule mtoto ni nani maana mtoto ameshakuwa mkubwa, kheee jamani kumbe akaanza kumktukana mume wangu, nasikia alimtukana sana, ila nilikuwa mbali kwenye biashara zangu sikujua hilo na wala mume wangu hakuniambia. Sasa juzi ndio kuna mtu kaniambia kuwa alimuona mwanangu njiani na kijana, basi niliporudi nilimwambia mume wangu kuwa tumuulize, ndipo mume wangu alipokataa na kunieleza hayo yaliyopita, ila sikuamini kabisa. Jana nilimlazimisha tena mume wangu amuulize, loh alianza kumporomoshea matusi mume wangu hatari, sijawahi kumpiga yule mtoto ila jana nilimpiga sana na leo nimemleta kwa bibi yake yeye na mwanae, hata mimi nimemchoka”
“Duh!! Sasa bibi yake atamuweza? Na kwanini sisi wazazi tukishindwa huwa watoto tunawatupia kwa mabibi kama wenyewe ndio wenye makosa?”
“Ndugu yangu, sina cha kufanya sasa, unadhani mwanangu ataishi na nani ikiwa anamuudhi mtu anayutuhudumia ndani ya nyumba? Babake hamtaki tena sababu ya ujinga wake, je ni nani atakayemuweza? Nadhani ujinga huu kaupata kwa baba yake”
“Pole sana ndugu yangu, nadhani tutaongea vizuri kesho maana nitakuja nyumbani kwako”
“Sawa sawa hakuna tatizo, karibu sana”
Kisha mama Angel aliagana na rafiki yake halafu yeye alirudi kwenye gari na kuendelea na safari yao ya kurudi nyumbani kwao.

Baba Angel akiwa kule msibani, aliendelea kumfatilia yule mdada wa kazi ili ampatie ule ujumbe ambao alipewa na marehemu, ila huyu binti kidogo alikuwa akihangaika kwahiyo hakutoa lile karatasi kwa muda muafaka.
Baba Angel aliendelea kusubiria, muda huu aliitwa tena na Manka na kisha Manka akampatia simu na kumwambia aongee nayo,
“Dokta Jimmy anaongea hapa, mbona hatujakutana leo?”
“Aaaah sababu ulisema kwanza watoto waende kule”
“Ndio, watoto waende kule halafu mimi na wewe tukutane”
“Tulipata taarifa ya msiba kwahiyo ikawa ngumu kwa mimi kukutafuta hata watoto niliwazuia”
“Aliyekufa ni nani yako?”
“Ni rafiki yangu”
“Yani rafiki tu ndio anakufanya uache kufatilia mambo ya msingi? Hujui umuhimu wa mimi na wewe kukutana? Kama hujui ni kwanini ulinitafuta? Si usingenitafuta”
“Naomba unisamehe sana ndugu yangu, yani sikujua kama haya yatatokea, sikujua kabisa”
“Unafiwa na rafiki unashindwa kufika kwenye mambo ya muhimu, kwani usingeenda huko msibani leo ungepungukiwa na nini? Haya, mmeshazika”
“Hapana bado”
“Kesho nitafute, ila kabla ya kunitafuta hakikisha wale watoto wameenda kule kwa babu yao”
“Sawa, hakuna tatizo”
Ile simu ilikatika, baba Angel alijiuliza, inamaana dokta Jimmy hafahamu kwamba aliyekufa ni ndugu yake Manka mpaka kuuliza vile? Baba Angel alishangaa sana ila hakutaka kuanza kufatilia ile karatasi maana huyu msichana wa kazi nae alionekana kumzungusha tu mpakagiza liliingia akiwa pale, basi moja kwa moja aliamuaga mama Sarah pamoja na Sarah na kuondoka zake kuelekea nyumbani kwake.

Mama Angel akiwa na Angel na Ester ambaye alikuwa amelala kwa muda huo waliwasili nyumbani kwao.
Moja kwa moja waliingia ndani na kumkuta Erica akiandaa chakula mezani huku akisaidiana na Erick, basi mama yao alifurahi huku akisema,
“Leo mmeachwa watoto wa kazi, nilijua tu kila kitu nitakikuta sawa”
Angel akasema,
“Mmmmh jamani mama, kwani mimi sio mtoto wa kazi?”
“Aaaah sijasema kwa ubaya ila nimewasifia tu wadogo zako, huwa najua akiwepo Erica nyumbani na Erick huwa akiharibiki kitu. Vipi baba yenu amesharudi?”
“Bado mama hajarudi”
Mama Angel alichukia sana kusikia kuwa bado mumewe hajarudi, aliamua kumpigia simu ambapo mumewe alidai kuwa yupo njiani kurudi nyumbani, na kweli baada ya muda mfupi tu baba Angel aliwasili nyumbani, na hivyobasi wote walikaa mezani na kuanza kula huku kama kawaida wakisifia chakula kilichopikwa na Erica,
“Lakini leo mama tumepika wote wawili, yani mimi na Erick”
“Kheee Erick nae kapika nini?”
“Kapika mama”
Erick nae akasema kuwa amepika pia basi mama yao aliwasifia wote wawili, kisha walipomaliza kula ndipo baba yao alipowaita na kuongea nao kuhusu kwenda kwa babu yao,
“Sasa mjiandae kesho ndio mtaenda kwa babu yenu, si mnajua kulivyo mali? Kwahiyo mjiandae mapema halafu dereva atawapeleka”
“Sawa baba”
“Mkifika, mimi nitawaambia kitu cha kwanza cha kufanya pale kwa babu yenu”
“Hakuna tatizo baba”
Kisha baba Angel aliwatakia wanae usiku mwema halafu yeye alienda moja kwa moja chumbani kwake.

Wakiwa chumbani baba Angel alimwambia mke wake kuhusu alichoongea na dokta Jimmy na alichoenda kuwaambia watoto kuwa kesho wajiandae,
“Ila huyu dokta Jimmy ana nini na watoto wangu lakini? Kwanini anataka waende huko kwa babu yao?”
“Mimi na wewe hatujui kuna nini ila tunahitaji kuufahamu ukweli ndiomana nimekubali tu kuwa waende na mimi nitaenda kuzungumza nae ili tujue kisa na mkasa”
“Mmmmh yani najikuta kutokumuamini amini huyo dokta jamani, hebu angalia hiyo simu unayosema umeongea nae akilalamika kwanini umeenda kwenye msiba bila kukutana nae, inamaana hajui kama dada wa Manka amekufa?”
“Mke wangu, nimejiuliza swali kama hilo pia. Labda sababu yeye ni daktari, kazoea kuona maiti mara kwa mara kwahiyo kwake kifo ni kitu cha kawaida”
“Hata kama, tunawaona madaktari wangapi ikitokea msiba wa karibu na wao wanashtuka? Yani huyo amenishangaza kwakweli, ila sitaki tena kuwa kikwazo kwa hili, nenda kakutane nae tu ingawa mimi simuamini”
“Usijali kitu mke wangu, kila kitu kitaenda sawa, hakuna kitakacho haribika”
“Sawa, mimi nakubaliana tu na wewe mume wangu ila kesho nitatoka, nitaenda kwa rafiki yangu Johari kuongea nae”
“Aaaah kuhusu maswala ya mtoto wake eeeh!!”
“Ndio, nitaenda kuongea nae kuhusu hilo”
“Sawa, hapa nyumbani atabaki Angel peke yake?”
“Aaaah kwani Angel anaogopa nini hapa? Hata hivyo, Ester yupo kwahiyo sioni kama ni tatizo”
“Basi sawa, nimekuelewa”
Kisha kwa muda huo waliamua tu kulala kwaajili ya kujiandaa kwa mambo ya kesho.

Erica akiwa anajiandaa kulala, chumbani kwake aliingia Erick na kuanza kuongea na Erica ambapo Erica alikaa na kumsikiliza,
“Naomba unisamehe kwa mchana wa leo”
“Ila hakuna kibaya kilichotokea kati yetu”
“Hakuna ndio ila dah sijui nisemeje”
“Usijali wala nini”
Kisha Erick aliinuka na kwenda chumbani kwake, basi Erica alianza kufikiria kuhusu kilichotokea mchana,
“Mmmmh ni nini kilitaka kutokea kile? Mimi na Erick tulikumbatiana tukiwa watupu kabisa, nashukuru Mungu niliweza kumtoa Erick mwilini mwangu na kukimbia, ila kama ningebaki ni kitu gani kingetokea kwani? Mbona mwili wangu nilihisi ukipokea mabadiliko ya hali ya juu?”
Alikuwa akijiuliza sana bila ya jibu, kitu hicho kilimfanya muda wote akumbuke jinsi alivyokumbatiana na Erick chumbani huku wakiwa watupu kabisa.
Kulipokucha tu, Erica alijiandaa na baada ya hapo alitoka nje na kumkuta Erick nae kajiandaa kisha wakaenda kwenye gari ambapo dereva nae alikuwa tayari na kuanza safari ya kwenda huko kwa babu yao.

Baba Angel nae alijiandaa na kumpigia simu dokta Jimmy ambaye alimjulisha mahali pa kukutana ambako hapakuwa mbali sana na kule walipoenda watoto wake, basi moja kwa moja baba Angel alienda kukutana na dokta Jimmy ambapo alimpata na kusalimiana nae kisha kuongea mawili matatu halafu dokta jimmy akamwambia,
“Washaenda watoto?”
“Ndio, nadhani watakuwa wanakaribia kufika maana hapa sio mbali na kule halafu wenyewe waliondoka mapema zaidi”
“Aaaah sasa wapigie simu halafu nipe niongee nao”
Baba Angel alipiga simu kwa Erick ambapo muda ule ule Erick alipokea ile simu,
“Mmeshafika?”
“Ndio tumefika muda sio mrefu baba”
“Basi, msikilizeni huyu awape maelekezo cha kufanya:”
Basi baba Angel alimkabidhi simu dokta Jimmy ambapo alianza kuongea nayo,
“Sikia, nenda moja kwa moja kwa mlinzi hapo mwambia akupe funguo, halafu mkiingia ndani kuna funguo kwenye kabati ya hapo sebleni ichukueni hiyo funguo mwende nayo hadi chumba cha mwisho hiko ndio kilikuwa chumba cha babu yenu. Kisha mkiingia humo ndani, mtakuta kuna CD imewekwa juu ya deki, chukueni CD hiyo muiweke kwenye deki halafu muwashe hiyo Tv. Angalieni kama nusu saa halafu ndio mtapiga simu”
“Sawa tumekuelewa”
Kisha walikata simu halafu dokta Jimmy alikaa na baba Angel sasa akiongea nae mambo mengine huku akimwambia wasubiri hiyo nusu saa ipite.

Erick na Erica walifanya kama ambavyo walielekezwa, na walipoingia ndani waliona jinsi nyumba ile ilivyosafi kwamaana kuwa huwa inafanyiwa usafi mara kwa mara ingawa mwenye nyumba amekufa.
Walienda moja kwa moja hadi chumbani na kufanya kamavile walivyoelekezwa, basi ile video ilianza kuonyesha ambapo walimuona mdada na mkaka ambao walikuwa ni vijana yani rika kama lao, halafu mule kwenye video ilisikika sauti ya mtu kama akiwaelekeza cha kufanya, waliona yule mkaka na mdada wakianza kushikana shikana na mwishowe wakavua nguo zote.


Walienda moja kwa moja hadi chumbani na kufanya kamavile walivyoelekezwa, basi ile video ilianza kuonyesha ambapo walimuona mdada na mkaka ambao walikuwa ni vijana yani rika kama lao, halafu mule kwenye video ilisikika sauti ya mtu kama akiwaelekeza cha kufanya, waliona yule mkaka na mdada wakianza kushikana shikana na mwishowe wakavua nguo zote.
Kisha Erick akamwambia Erica kuwa wafanye kamavile ambavyo wanafanya kwenye ile video, basi Erica akamwambia Erick,
“Unaona kuwa ni sawa kwa sisi kufanya vile Erick?”
“Sijui, labda tujaribu mbona kama wanafurahia wale! Hebu na mimi jaribu kunifanyia kama yule dada anavyomfanyia yule kaka!”
“Mmmmh Erick jamani!”
“Jaribu Erica, mbona naona itakuwa ni raha sana”
Erica akainama na kuanza kufanya kamavile wanavyoangalia kitendo ambacho kilimchanganya sana Erick na kumfanya apige kelele huku akisema,
“Mungu wangu Erica, sijawahi kuona kitu cha namna hii”
Kitu kile kilifanya Erick atoe ute ute na kumfanya Erica aruke pembeni na kusema,
“Ndio nini sasa Erick?”
Erick alikaa kimya kwa muda huku akijitathimini na baada ya muda akasema,
“Nahisi raha sana Erica, natamani hii raha uipate na wewe pia”
“Aaaah ila mimi naogopa”
“Unaogopa nini? Naomba basi nikufanyie kama huyo mkaka anavyomfanyia huyo mdada”
“Hapana Erick”
Basi waliwaangalia tena wale wa kwenye video na kuona kwa muda huu staili yao imebadilika huku wakionekana kufurahia sana kufanya vile wanavyofanya, Erick alimuangalia Erica na kumwambia,
“Sasa bado kufanya kama vile”
Kisha Erick alimkumbatia Erica na kumuangusha kitandani ila kabla Erick hajafanya chochote, Erica alimwambia Erick,
“Huu ni mtego Erick”
“Mtego kivipi? Tufanye Erica jamani!”
“Huu ni mtego, tumechunguliana inatosha”
“Hapana, haitoshi erica naomba jamani nashindwa kuvumilia kikweli naumia sana hapa, nahisi hadi misuli inaniuma”
“Kwahiyo tufanye nini ili hiyo misuli iache kuuma?”
“Basi naomba nifanyie kama mwanzo”
Erica hakubisha na alifanya vile, kisha alipoona tena ute aliinuka na kuzima ile video kisha alikimbilia bafuni na nguo zake.
Alijifungia mule bafuni na kumwambia Erick,
“Naomba uvae nguo zako Erick, nitakwambia kwanini ukishamaliza kuvaa”
Basi Erick akaona bora aende kwenye bafu lingine na kujisafisha ili na yeye avae nguo vizuri.
 
SEHEMU YA 399

Baba Angel akiwa anaangalia saa yake, aliona kama muda umeenda sana, basi akamwambia dokta Jimmy,
“Kwasasa ni karibia lisaa linapita”
Dokta Jimmy alicheka sana na kumuangalia baba Angel kisha akamwambia,
“Unajua ni kwanini hawajapiga?”
“Eeeeh kwanini?”
“Muda huu watoto wako wapo kuzini, itakuwa wapo kukumbatiana kwa shughuli nzito waliyopeana”
“Kivipi? Sikuelewi”
“Hebu nisikilize kwa makini sana nikueleweshe Erick”
“Nieleweshe tu nakusikiliza”
“Ni hivi, baba yako yani mzee Jimmy alikuwa akimpenda sana mke wako uliyemuoa yani Erica, alikuwa akimpenda sana tena sana na alikuwa tayari kufanya chochote juu yake huyo mwanamke. Kuna siku huyo mkeo akiwa mjamzito wa hao mapacha wako, alimjibu vibaya sana baba yako, unaweza kumuuliza na atakwambia kama anakumbuka. Kitu hiko kilimkera sana mzee Jimmy, alikuja na kunilalamikia, akasema kuwa lazima mkeo amkomeshe, alisema kuwa lazima mkeo amlee mtoto ambaye sio wake, na mpango wa baba yako ulikuwa ni kubadilisha watoto, tulitaka kumbadilisha mtoto wa mkeo na mtoto wa Sia, na ndio mpango ulivyokuwa ila badae wakati mimba ya mkeo imefikia ukingoni ndio wazo likabadilika kwani kuna mtaalamu mmoja hivi alisema kuwa anadawa ambayo akiwawekea watu wakati wadogo basi watu hao wataanza kuingiwa na hisia za kimapenzi wakiwa wakubwa, ndipo baba yako aliposema kuwa dawa zile tujaribu kwa watoto wako na sio kuwabadilisha tena. Mkeo alijifungua, kuna kitu kilitokea kabla hata ya kuwachoma sindano, alikuja mama mzazi wa mke wako na kusema kuwa aonyeshwe watoto ambao mwanae alijifungua, basi ilibidi akaonyeshwe na wazo la kuwabadilisha likafa muda ule ule, tukaendelea na wazo la sindano tu. Basi baada ya muda tuliwachoma zile sindano ambazo ni wazi zinaanza kufanya kazi vizuri baada ya watoto kufikia umri wa balehe. Nilichofanya leo ni kujaribu kuhusu zile dawa kuwa zimefanya kazi au la maana watoto wako wale mapacha wapo kutamaniana kimapenzi kwa muda mrefu sana, kwahiyo ule mkanda niliowaambia waweke ni mkanda wa ngono wa kuweza kuwahamasisha na wao kufanya ngono na mpaka muda huu wameshafanya ndiomana unaona simu haijapigwa halafu…..”
Baba Angel aliinuka kwa hasira na kusema,
“Stooop, nakwambia nyamaza dokta Jimmy, ni ujinga gani huu kunitendea kwa watoto wangu, watoto ambao mke wangu kabeba mimba kwa shida na kuwazaa kwa uchungu halafu nyie mmenda kunifanyia ufedhuli huu kweli! Wanangu wakishafanya mapenzi nyie mnapata raha gani? Wanangu wakipeana mimba kwenu ni furaha gani?”
Kwa mara ya kwanza baba Angel alijikuta akiongea huku akibubujikwa na machozi ya nguvu, alikuwa akilia kwa hasira sana, alijiona kama kabeba kitu katika moyo wake, alijikuta akiwa na hasira kiasi kwamba alitamani hata amchukue dokta Jimmy na kumponda ponda, basi akaanza kuondoka na dokta Jimmy akamuuliza,
“Unaenda wapi sasa?”
“Nawafata wanangu”
“Unajisumbua, kama bikra washavunjana hao. Njoo tujadili cha kufanya”
“Mjinga wewe achana na mimi”
“Unajifanya una hasira sana na mwanao, na huyo Erica mdogo akipata hiyo mimba mlee, sijui mtoto wake atawaitaje, masikini jamani mnatia huruma”
Dokta Jimmy alikuwa akiongea huku akicheka na kutikisa kichwa, kwakweli baba Angel alizidi kupandwa na hasira kwani kwa muda huo mawazo yake yote ilikuwa ni juu ya wanae, alikuwa akitembea huku machozi yakimtoka na kuingia kwenye gari yake ila dokta Jimmy aliingia pia na kumwambia,
“Erick, naomba niruhusu nikuendeshe tu twende eneo la tukio, bado nakuhurumia. Najua uchungu ulionao ila kosa sio langu ni kosa la baba yako”
Baba Angel hakujibu kitu, kwahiyo dokta Jimmy alianza kuendesha na kuelekea nyumbani kwa mzee Jimmy.

Dokta Jimmy na baba Angel walipofika pale hata hawakuuliza kwa walinzi kuwa imekuwaje moja kwa moja waliingia hadi chumbani kwa mzee Jimmy ila Erick na Erica hawakuwepo na kumfanya baba Angel azidi kupatwa na mawazo alijaribu kuwaita lakini hawakuitika, basi dokta Jimmy aliwasha ile CD maana bado ilikuwa kwenye deki, na ilianza kuonyesha, huku dokta Jimmy akicheka alimwambia baba Angel,
“Angalia hata kitanda, kilikuwa kimetandikwa hiki ujue, halafu sikiliza harufu ya hiki chumbakwa mbali utasikia kama harufu ya shahawa”
Kile kitu kilizidi kumchanganya baba Angel, kisha dokta Jimmy alimwambia tena baba Angel,
“Naona bado huamini, twende ukaone”
Kisha baba Angel akiwa anatikisa kichwa na machozi ya hasira yakimtoka alifatana na dokta Jimmy hadi kwenye chumba kingine ambacho kulikuwa na Tv kisha dokta Jimmy akawasha na kusema,
“Kuna CCTV camera tumefunga kwenye chumba cha mzee wako, nataka ujionee mwenyewe”
Baba Angel akaona pale Erick na Erica wakivua nguo, kisha akamuona Erica akiinama kwenye maungo ya Erick, kwakweli baba Angel alishikwa na hasira ya gafla na kuvunja ile Tv, kisha alimgeukia dokta Jimmy na kuanza kumkaba hadi dokta Jimmy alianguka chini na kupoteza fahamu halafu baba Angel akatoka mule akiwa na hasira zaidi hata mlinzi alipomuuliza,
“Mzee kuna nini kwani?”
Alimpiga ngumi moja ya sura kiasi kwamba yule mlinzi alianguka chini na damu kuanza kumtoka puani, mlinzi wa pili alitaka kukimbia ila baba Angel akamuuliza,
“Wewe mjinga, watoto wangu waku wapi?”
“Sijui mzee ila walitoka gafla na kuondoka”
Baba Angel alianza kumsogelea yule mlinzi ila yule mlizni alikimbia haraka haraka na kutoka nje kwani alimuogopa baba Angel ambaye alionekana kubadilika sura kabisa. Baba Angel alirudi kwenye gari lake na kuondoka nalo, alivyofika njiani alilisimamisha pembeni na kujikuta akilia sana, yanbi alilia kama mtu aliyefiwa vile, kwanza hakuelewa watoto wake watakuwa wapi baada ya kitendo kama kile, hakuelewa ni kwanini baba yake kaamua kumuumiza kiasi kile, hakuelewa ataweka sura yake wapi baada ya Erica kuonekana kuwa ana mimba ya Erick, yani alijikuta anawaza hata vitu visivyokuwepo, hata aliwaza huenda watoto wake wamejidhuru baada ya yale, yani alilia sana na kukosa raha kabisa.

Siku ya leo ilikuwa ni nzuri sana kwa upande wa Angel kwani ni siku ambayo alibaki mwenyewe tu na Ester, hivyobasi aliamua kumpigia simu Samir ambaye hakuchukua muda mrefu na kufika pale kwakina Angel, halafu alianza kuongea nae,
“Naona hii ndio siku ile uliyoniambia Angel”
“Ndio, ni hii”
“Sikia nikwambie kitu Angel”
“Kitu gani”
“Wanakazana kusema kuwa mimi na wewe ni ndugu ila hili mimi nimelipinga au mwenzangu umelikubali?”
“Hata mimi nimelipinga”
“Sasa inabidi tufanye kitu kudumisha mapenzi yetu na ili kuonyesha kuwa tunapingana na mawazo yao”
“Kitu gani Samir?”
“Inatakiwa tufanye mapenzi Angel, kwanini kila siku tunaahirisha? Kumbuka ulisema siku kama hii ndio itakuwa nzuri kwa mimi na wewe kuwa pamoja”
“Sawa, hakuna tatizo. Ngoja mtoto alale basi”
Muda huu Angel alimbembeleza mdogo wao ambaye hakuchukua muda mrefu sana akapitiwa na usingizi na kulala, basi Angel akamlaza kwenye kochi halafu yeye na Samir moja kwa moja walienda chumbani.
Kama walivyopanga, walienda kutimiza adhma yao tu waliyokuwa wakiitaka kwa siku zote, kitendo kile kilimfurahisha sana Samir na kumshukuru sana Angel,
“Nafurahi sana mimi kuwa mwanaume wa kwanza kwako”
“Mmmmh!! Mimi naona aibu”
“Aibu ya nini Angel wakati mimi ndio mumeo”
Hapo Angel alifurahi na wote wawili kuanza kucheza cheza mule chumbani kisha wote wawili walilala pamoja mule mule chumbani kwa Angel.

Mama Angel kama ambavyo alipanga kwa siku hii, moja kwa moja alienda kwa rafiki yake Johari maana alishapanga kwenda kuzungumza nae, basi alimkuta pale na kuanza kuongea nae kuhusu mambo yaliyopo baina yake na mtoto wake,
“Johari kuwa makini sana, mtoto atafanya ugombane na mumeo huyu”
“Ndiomana nimemrudisha kwetu maana alikuwa akitaka kuniletea balaa”
Muda huu alifika Juma yani mume wa Johari na kuanza kumsalimia mama Angel, na kama kawaida ya Juma alianza kumuulizia Erick kwanza kama kawaida yake,
“Vipi Erick hajambo? Anaendeleaje na pacha wake?”
Mama Angel alihisi moyo wake ukifanya paaa, na kuema,
“Jamani, mbona moyo umeniuma gafla”
Johari alimuangalia na kumuuliza,
“Kivipi? Kwani kuna tatizo?”
“Hapana, kila kitu nimeacha kikiwa salama kabisa ila najiona gafla sina raha tena, nahisi kama sijui moyo wangu umefanyeje”
“Oooh pole sana ndugu yangu”
Basi Johari akaenda kumletea maji ambapo mama Angel alikunywa kidogo tu ila bado hakujisikia vizuri maana bado moyo wake ulikuwa ukimuuma sana na muda huo kuamua kumpigia simu mume wake ambapo simu ya mume wake iliita tu bila ya kupokelewa, basi walianza kuongea nae taratibu na kumpooza kuwa hakuna baya lililotokea,
“Unajua kuna kipindi moyo huwa unashtuka tu, kwahiyo usijali mama Angel, hakuna baya kati yako”
“Ila najihisi kupumzika, yani nimejikuta tu gafla nikiwa sina raha tena, hapa nilipo nahisi kama kichwa changu kimeingiliwa na kitu”
“Pole sana”
Johari aliona ni vyema kama rafiki yake akipumzika basi alimtafutia chumba cha wageni pale kwake ili aweze kupumzika ila napo bado alikuwa anajihisi vibaya na kuamua kuaga kabisa ili aende kwake, basi Juma alijitolea kumpeka hadi nyumbani kwake.

Mama Angel alipofika nyumbani kwake, Juma alimuaga halafu moja kwa moja yeye aliingia ndani na kuona pako kimya sana, akajua Angel na mtoto lazima watakuwa wamelala chumbani kwa Angel, kwahiyo moja kwa moja mama Angel alienda chumbani kwa Angel, alipofungua mlango tu alitamani hata kupiga yowe,
“Angel!! Angel!! Angel!! Nakuita mara tatu mwanangu, ndio uchafu gani huu umekuja kunifanyia Angel jamani, kwanini Angel?”
Samir na Angel waliinuka huku Samir akivaa haraka haraka na kutaka kuondoka, ila kabla ya kutoka mama Angel alimshika mkono Samir na kumwambia,
“Wewe mjinga, baba yako hajakueleza kuwa Angel ni nani yao au kiburi?”
Samir alikaa kimya tu, kisha mama Angel alimzaba vibao mfululizo Samir na kufanya Angel asogee karibu ila mama yake aache kumpiga Angel, kitendo hiko kilimkera sana mama Angel na muda huo alimuacha Samir na kuanza kumpiga Angel ambapo Samir alikimbia, kwahiyo mama Angel alibaki akimpiga Angel kwa hasira,
“Mjinga wewe, nimekulea kwa shida, nikakupeleka hadi shule za masister ili uwe na maadili halafu bila aibu unaenda kuleta mwanaume kulala nae nyumbani kwangu! Halafu mwanaume mwenyewe ni kaka yako, mjinga sana wewe”
Mama Angel aliendelea kumpiga Angel kwa hasira huku akihisi kama kitu kikimkaa kwenye moyo wake maana alikuwa na hasira sana tena hasira zilizopitiliza.
Ila gafla walisikia sauti ya Samir ikisema,
“Moto, moto huku jamani moto”
Hapo mama Angel alimuacha Angel na kushuka chini huku wakimkuta Samir kamkumbatia mtoto Ester halafu mlinzi wao akijaribu kuuzima ule moto ambao ulitapakaa jikoni yani ilikuwa ni kitu cha ajabu sana, ikabidi Angel amchukue mdogo wake halafu Samir alianza kusaidiana na yule mlinzi katika kuuzima ule moto sababu nyumba yao ilikuwa na vifaa maalumu vya kuzumia moto, na Samir aliweza kuvitumia kwahiyo ikasaidia swala lile la kuzima moto.
Mama Angel alijikuta akiishiwa na nguvu, alikaa chini tu huku machozi yakimtoka kwa mfululizo yani hakuamini kile kilichotokea.
Angel alimuuliza Samir,
“Kwani imekuwaje?”
“Wakati nakimbia, nilipofika sebleni nilikumbuka kuwa mtoto ulimlaza kwenye kochi ila sikumuona na kuona moshi ukitokea maeneo yale, basi niliamua kwenda yani Mungu tu amesaidia, nilimuona mtoto huyu akiwa katikati ya moto halafu kashika kiberiti”
Mama Angel alisisimka sana, alijihisi kukosa amani katika moyo wake na kujikuta akiangua kilio cha nguvu maana kwa siku hii ndio angekuwa kampoteza mtoto wake Ester kwasababu ya hasira alizokuwa nazo, basi mama Angel aliinuka na kwenda chumbani kwake ambapo alilia sana, kisha Angel na Samir pamoja na yule mlinzi walisaidiana kuweka baadhi ya vitu sawa huku Angel kambeba mdogo wake mgongoni.

Mama Angel alitoka chumbani kwake wakati giza limeshaingia tayari, alifika sebleni moja kwa moja na kumkuta Angel amejiinamia tu kisha akamuuliza,
“Baba amerudi?”
“Bado hajarudi”
“Erick na Erica?”
“Bado hawajarudi”
“Ooooh Mungu wangu, ni nini hiki jamani? Siwezi mimi, naomba Mungu nirudishie familia yangu, siwezi mimi”
Alijikuta akitoa tena machozi, kitu kilichokuwa kikimchanganya ni ile hali ya kuwapigia simu na kutokupokea, yani alihisi kuchanganyikiwa kabisa.
Walikaa kwa muda pale sebleni na Angel ila bado ndugu zao hawakurejea, kwenye mida ya saa tatu usiku ndipo Erick na Erica waliporudi na kufanya mama yao afurahi kwani alikuwa na uhakika na mumewe sasa kuwa atarudi, ila baada ya salamu ilibidi Erick na Erica kila mmoja kwenda chumbani kwake kuoga.
Basi mama Angel aliendelea kusubiri pale, hata Angel alipoinuka na kwenda kulala bado yeye aliendelea kusubiri, kwenye mida ya saa sita kasoro usiku ndipo baba Angel aliporudi nyumbani kwake, kwakweli mama Angel alifurahi sana ambapo moja kwa moja walienda chumbani na baba Angel cha kwanza kabisa aliuliza,
“Erick na Erica wapo ndani?”
“Ndio, wapo ndani mume wangu”
“Oooh asante Mungu”
Kisha baba Angel alienda kuoga kwanza na mkewe alimuuliza kuwa akamuandalie chakula gani maana hata hamu ya kupika toka litokee seke seke la moto haikuwepo mule ndani,
“Nikuendalie chakula gani mume wangu?”
“Sina hata hamu ya kula”
“Kwani tatizo ni nini mume wangu”
“Sijui kama nikikuelezea utaweza kuvumilia”
“Nieleze tu hakuna tatizo”
“Ooooh hapana niache nilale kwanza”
Baba Angel hata hakutaka kuongea na moja kwa moja alilala kwanza.

Usiku huu Erick alienda chumbani kwa Erica na kuanza kuongea nae kwa yale yaliyotokea baina yao siku hiyo, alianza kwa kumuomba msamaha,
“Naomba unisamehe sana Erica, nisamehe sana hata sijui ni kitu gani huwa kinaingia katika akili yangu. Naomba unisamehe sana”
“Usijali Erick, mimi bado najiuliza kuna nini kati yetu?”
“Sijui, ila nakushukuru sana Erica maana siku zote umekuwa mstari wa mbele kutuepusha katika kutenda haya ingawa leo ilibaki kidogo tu tuangukie kwenye hayo mambo”
“Ila Erick umeona? Umegundua kitu?”
“Kitu gani?”
“Kumbuka muda ambao mimi na wewe tulipokuwa kule wakati tunataka kufanya yale mambo, unakumbuka lakini?”
“Nakumbuka ndio, ila ulininanii vizuri Erica, nilijihisi kama napaa vile”
“Acha maneno yako Erick, sikia kwanza umeona hapa nyumbani imetokea ajali ya moto? Nasikia bado kidogo Ester angeungua, tungemkosa mdogo wetu kwa ujinga wetu”
“Dah!! Kwani ilikuwaje?”
“Wewe ukishatenda dhambi huwa hata hutaki kusikiliza yaliyotokea, nasikia leo jikoni kumewaka moto, bado kidogo tu Ester angeungua, ameokolewa tu. Yani kulikuwa na balaa”
“Kheee kwahiyo hilo balaa ndio tumesababisha sisi?”
“Sijui, nahisi ni hivyo kuwa ni sisi ndio tumesababisha. Ila kama kule tulikuwa tumewekewa mtego itakuwaje?”
“Haitakuwa kitu, kwani tumefanya kitu gani kibaya?”
“Kile nilichokufanyia ni kizuri? Erick tumekosea sana maana sisi ni ndugu ujue, sisi ni mapacha”
“Naelewa hilo Erica, ila sio kosa langu na pia sio kosa lako kwani nahisi hata wewe unahamu kubwa ya kuwa na mimi kimapenzi”
“Mmmh ishia hapo, usiku mwema na urudi chumbani kwako”
Erick aliondoka na kwenda chumbani kwake, basi Erica alikaa kwanza kitandani na kuanza kufikiria yale matukio yaliyotokea baina yake na Erick.
Akakumbuka muda alipoingia bafuni na kumuomba Erick avae nguo, ambapo alipotoka alimuomba Erick waondoke waende ufukweni kupunguza mawazo, akakumbuka jinsi Erick alivyolalamika kuwa anahisi kuwa na hali mbaya basi akakumbuka alivyotumia muda mrefu kuweza kumbadilisha Erick mawazo, basi akajisemea,
“Kwanini lakini? Kwanini inakuwa hivi? Kama mimi na Erick ni mapacha, sasa kwanini tunatamaniana? Na kwanini iwe hivi kati yangu na Erick”
Aliwaza Erica kwa muda mrefu sana bila ya jibu la aina yoyote ile na kuamua tu kulala kwa muda huo.

Asubuhi na mapema, Erica alienda chumbani kwa Erick na kumuamsha kisha akaanza kumueleza kila kitu kilichotokea hapo kwao hadi mama yake alivyowafumania Angel na Samir, Erick alimuangalia dada yake na kumuuliza,
“Yote hayo umeyaona ndotoni?”
“Ndio, na hadi moto ulivyoanza. Ni kuwa, Ester alikuwa amelala sebleni kwenye kochi, alipoamka akainuka na moja kwa moja alienda jikoni na kuanza kuchezea vitu vilivyokuwepo jikoni. Kama unakumbuka kuna chupa ya mafuta ya taa ililetwa ndani na baba, sasa ile chupa ilikuwa jikoni, basi Ester aliichezea na kuifungua ile chupa basi mafuta yalimwagika pale, kisha akaanza kuchezea kiberiti na mwisho wa siku wa siku akafanikiwa kuwasha, yani moto umewaka halafu Ester wala hakushtuka. Bila yule Samir ingekuwa balaa kwa siku ya jana. Kwahiyo chanzo cha moto ni Angel na Samir”
“Aaaah ila wewe Erica ni noma kwenye maswala ya ndoto, kila kitu unaota. Hivi huwa unafanyeje hadi unaota?”
“Hata sijui ila huwa najikuta tu nikiota”
“Je hujawahi kuota kuhusu mimi na wewe? Hujawahi kuota kuhusu safari ya jana? Hujawahi kuota kinachoendelea kati yangu na yako?”
“Mmmmh Erick hata mimi mwenyewe sielewi ni kwanini sijawahi kuota baina yangu na yako, nilichowahi kuota nikikwambia hata wewe kitakuacha mdomo wazi”
“Kitu gani hiko?”
Muda huu baba Angel aliingia humu chumbani kwa Erick bila hata ya hodi na kumkuta Erick na Erica wamekaa kitandani wakiwa hawana hata habari yani wakiongea tu mambo yao, kiukweli baba Angel alijihisi vibaya sana kuwaona pamoja, upande mwingine alitamani kuwafokea ila upande mwingine aliona kuwa wale watoto hawakuwa na makosa, basi aliwaangalia tu ambao nao walishtuka na kumsalimia kwa pamoja, kisha kabla ya kuwaitikia salamu aliwauliza,
“Mnafanya nini pamoja?”
“Hamna kitu baba, ni Erica alikuwa akinisimulia ndoto aliyoota jana”
“Ndoto gani?”
Erica ilibidi aanze kumsimulia baba yake kutokana na jinsi alivyoota, ndio pale hata baba Angel alipogundua kuwa mkewe alitaka kumueleza kuhusu jambo hilo pia ila yeye alifanya haraka kwenda kumuona Erick kwanza, basi alimuuliza Erica,
“Kwani jana wakati panaungua ulikuwepo?”
“Hapana, tuliporudi tu tukakuta hivyo ila usiku ndio nikaota”
Baba Angel alitamani pia kuwauliza kuhusu kilichotokea kati yao kwa siku ya jana ila alijikuta akishindwa kuwauliza yani alibaki kuwaangalia tu halafu akamuomba Erica atoke ili aongee na Erick.
Basi baba Angel alipobaki na Erick alianza kumuuliza,
“Mwanangu umewahi kulala na mwanamke?”
Erick alishtuka sana hili swali kutoka kwa baba yake na kujibu,
“Hapana baba”
“Umewahi kufanya mapenzi?”
Erick alishangaa tena na kujibu hapana, kisha baba Angel alimuuliza tena,
“Je jana ulifanya mapenzi?”
Hapa Erick alishtuka zaidi na kumuuliza baba yake,
“Kwanini unaniuliza hivyo baba?”
“Aaaah basi tu”
Kisha baba Angel akatoka mule chumbani kwa Erick, kiukweli baba Angel alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa kabisa yani hakujielewa hata kitu gani anaongelea kabisa.

Usiku wa leo, baba Angel aliamua tu kumueleza ukweli mke wake maana aliona kuendelea kuumia kwa swala hilo ni hatari katika maisha yake, yani wala hata hakujali jinsi mkewe aivyomsimulia kuhusu Angel na Samir,
“Jamani mume wangu unaonekana hata hujali, unajua Angel na Samir ni mtu na dada yake? Wote ni watoto wa Rahim”
“Hebu tulia mama Angel, ukisikia ya kwetu huku nahisi utatamani ardhi ipasuke uingie”
“Ya kwetu ipi hiyo?”
“Ushawahi kusikia watoto wa baba mmoja na mama mmoja wamepeana mimba?”
“Mmmmh, hebu niambie vizuri baba Angel”
“Ni hivi Erick na Erica sio watoto tena”
“Kivipi?”
Baba Angel alimsimulia tu mama Angel kwa kifupi na kuhusu video waliyoikuta ya Erick na Erica, mama Angel alijikuta akipiga yowe na kutaka kuinuka kwenda kuwauliza vizuri watoto wake ila baba Angel alimzuia kwanza na kumwambia,
“Mke wangu swala hili hata sio la kwenda nalo kichwa kichwa, tutakosa yote”
“Kivipi?”
Mama Angel aliinama chini kwani alikuwa haelewi kitu kwa muda huo, hata hakujua cha kufanya, alichukua simu yake hata hakuelewa anataka kumpigia nani ila muda huo huo kuna ujumbe ukaingia kwenye simu yake, aliufungua na kuusoma,
“Mumeo ameua.

Mama Angel aliinama chini kwani alikuwa haelewi kitu kwa muda huo, hata hakujua cha kufanya, alichukua simu yake hata hakuelewa anataka kumpigia nani ila muda huo huo kuna ujumbe ukaingia kwenye simu yake, aliufungua na kuusoma,
“Mumeo ameua”
Mama Angel alimuangalia mumewe kwa uoga, kiasi kwamba hata baba Angel alihisi kuwa kuna kitu sio sawa na kuchukua ile simu kwa mkewe kisha alisoma huo ujumbe, na baada ya hapo mama Angel alimuuliza,
“Eeeeh mume wangu umemuua nani?”
“Mimi sijui maana sijui kama niliowashughulikia walikufa”
“Ulishughulikia wakina nani?”
Baba Angel alimuuleza mkewe kwa kifupi jinsi alivyomkaba dokta Jimmy, na jinsi alivyompiga ngumu mlinzi kisha akasema,
“Kwakwekli Mungu anisamehe tu ila nilikuwa na bhasira sana, huo ujumbe sio nani kautuma. Natumaini yule mlinzi hakufa maana sio kosa lake, na kama amekufa basi nitajilaumu sana mimi sababu yeye nimempiga kwa hasira ila huo ujumbe napenda uwe wa kumuhusu dojkta Jimmy yani waseme ndio amekufa. Siku ya mazishi naenda pale na panga langu yani maiti yake naikata na kichwa kabisa”
Mama Angel alimuangalia kwa makini mumewe ila kwa lile lililokuwepo alielewa ni kwanini mumewe anaongea kwa hasira kiasi kile, ndio na yeye sasa alianza kuingiwa na akili sawa kwani alishtuka kitu na kujisemea,
“Inamaana kweli mwanangu Erick na Erica wamefanya mapenzi!!”
“Sasa unafikiri mimi ningejianzia tu kuchukia? Mama Angel mimi nina hasira sana, naongea lakini sina raha kumbuka jinsi tulivyojitahidi kulea watoto wetu, katika maadili na njia za kumpendeza Mungu ila ni nini hiki? Eti kuna mjinga mmoja alikuwa akifanya majaribio kwa watoto wetu? Alikuwa akinikomesha mimi kwa damu yangu? Kwakweli nina hasira sana”
Muda huo baba Angel alioneka hata kusahau kama kitendo kile kimefanywa na baba yake mzazi, kwajinsi alivyokuwa akiongea na kumuita mjinga mmoja.
Basi baba Angel alichukua simu na kumpigia mama yake mzazi, ila muda ule mama Angel nae aliinuka kumbe alienda chumbani kwa Erica kwani huwa anajua kama mwanae huyu huwa anapenda kusema ukweli ingawa hakuwa na uhakika kama hilo angelisema ukweli pia.
Baba Angel moja kwa moja alimpigia simu mama yake na kuanza kuongea nae kwani kwa muda huo alishikwa tena na hasira kwa ule ujumbe kuwa amemuua mtu,
“Mama, nakuomba mama yangu jitahidi uwezavyo tuonane maana mtoto wako nipo kwenye hali mbaya sana. Nahisi utanikosa”
“Tatizo ni nini Erick?”
“Mama, sina wa kumweleza hii aibu iliyonifika. Naomba mama yangu uje, nabaki kutangatanga na moyo tu”
“Naona kweli haupo sawa, mimi sipo mbali sana ila nimefikia hotelini. Kama utaweza mwanangu kuja hotelini kwa muda huu ni sawa hakuna tatizo, njoo tuonane ili tuweze kuongea”
“Sawa mama hakuna tatizo, nakuja huko sasa hivi”
Kisha baba Angel alianza kujiandaa bila kujali kuwa ule ni usiku, kwavile anaijua hoteli ambayo mama yake anapenda kufikia kwahiyo alifanya tu upesi upesi ili aondoke na kuelekea huko kwa mama yake.
 
SEHEMU YA 400

Mama Angel alienda moja kwa moja chumbani kwa Erica na kumkuta Erica kajiinamia tu, kwanza moyo wake ulifanya paaa, ila alimsogelea binti yake na kukaa nae karibu,
“Unajua ni saa tano usiku hii Erica, mbona hujalala mwanangu?”
“Sina usingizi tu mama”
“Pole sana mwanangu, tatizo ni nini hadi umekosa usingizi?”
“Sijui mama”
“Nisikilize Erica, mambo mengi sana huwa unapenda kuniambia na mengine huniambia hata kabla hayajatokea, na mengine hata yakitokea basi huniambie. Najua kuna kipindi nilikuwa nakusema sana kuhusu wewe kuniambia ukweli na kukasababisha ukaacha kuniambia mambo ya muhimu kiasi kwamba ukawa mkubwa bila ya kuniambia ila mwanangu nilikuomba msamaha na ukaanza kuniambia tena. Mbona hili hujaniambia?”
“Lipi hilo mama?”
“Wewe na kaka yako mlifanya nini kwenye nyumba ya babu yako?”
Mama Angel aliuliza hilo swali kwa binti yake huku midomo yake ikimtetemeka, na Erica alishtuka na kuanza kumjibu mama yake kwa uoga,
“Nisamehe mama”
“Msamaha wangu ni pale wewe utakapoamua kunieleza ukweli, mimi ni mama yako na usinifiche chochote niambie ukweli halisi”
“Ni aibu mama”
“Kitu gani hiko cha aibu Erica eeeh!! Mwanangu wewe ni binti shupavu na mimi naelewa hilo kuwa wewe ni binti shupavu na huwa unasema dhahiri kuwa huogopi chochote, na siku zote hupenda kueleza ukweli. Niambie ukweli mwanangu”
“Mmmh mama, naomba unisamehe”
“Sawa, ila unajua kuwa ukweli humuweka mtu huru? Niambie ukweli mama, nakuomba mwanangu”
“Niahidi kuwa hutonipiga!”
Mama Angel akapumua kidogo na kumuahidi mwanae kuwa hatompiga, basi Erica alianza kumuelezea,
“Mama samahani, hata sikujua kama itakuwa hivi. Tunaona aibu mbele yenu na mbele ya macho ya baba, hata kuongea nae tunajikaa tu ila tunaona aibu hata sijui imekuwaje na sijui nianzie wapi kuelezea”
“Anzia popote unapoona panafaa kuanzia, hata ukianzia hapo kwa babu yenu ni sawa”
“Tulifika kwa baba mama, tukapewa maelekezo kuwa tuingie kwenye chumba cha babu na tuweke CD iliyopo kwenye video, kisha tukaanza kuangalia. Kiukweli ile video haikuwa nzuri mama, na haikuwa nzuri kwa umri wetu ila tuliangalia siwezi kukana hilo mama. Kwenye ile video walikuwa wakitenda matendo ya ngono ambayo huwa unatukataza hata video za kawaida tukiangalia ndani ikionekana mwanamke na mwanaume kitandani huwa mama unapeleka mbele sehemu hiyo ila kwenye ile video walikuwa watupu kabisa, na sisi tulivua nguo pia”
Mama Angel akapumua na kuendelea kusikiliza yani alihisi akitetemeka hadi masikio kwa muda huo,
“Eeeeh ikawaje?”
“Kile kitu cha mbele ya Erick kiliinuka juu na kuonyesha kama mishipa imesimama, niliogopa kiasi ila kwenye video kuna kitu kilionekana kwanza ndio Erick aliponiambia mimi nimfanyie kamavile kwenye video, ndipo nilipoinama na kunanii nanii yake”
Mama Angel alishtuka kwanza na kumuuliza erica,
“Erica mwanangu hebu nyoosha maelezo yako hapo, kunanii nanii yake ndio nini?”
“Nilianza kumnyonya mama halafu…..!”
Mama Angel alijikuta akiinuka na kumwambia Erica,
“Nyamaza mwanangu”
Akatoka na kurudi chumbani kwake, aliinama na kulia sana, yani alilia sana akajua pale ni kitu gani kilitokea baina ya watoto wake, alimuita baba Angel pale ila hakumuona basi alilia sana tena sana yani alijikuta akikosa raha ya maisha kabisa, alilia kwa muda mrefu sana kwani alielewa baada ya ile kitu lazima Erick na Erica waliharibiana tu.

Baba Angel alifika hotelini alipofikia mama yake na moja kwa moja alienda kwenye chumba ambacho mama yake anapenda kufikia, aligonga ila aliyefungua hiko chumba hakuwa mama yake kama ambavyo alizoea bali alikuwa ni mwanamke ambapo baba Angel alimshangaa kwa muda ila yule mwanamke alitabasamu na kumuangalia na kusema,
“Erick jamani!! Umenikumbuka lakini? Siamini kama nimekuona tena leo”
Mara mlango mwingine ulifunguliwa ndipo mama yake alipotoka na kumfata baba Angel kisha akamvuta na kumwambia,
“Wewe imefika chumba hiki leo”
Alimvuta hadi kwenye chumba alichofikia yani baba Angel bado alikuwa ameduwaa kama mtu aliyepigwa na ganzi vile.
Kisha baba Angel alipelekwa kwenye chumba ambacho mama yake alikuwa amefikia humo, basi alimkalisha kwenye kiti na kuanza kuongea nae,
“Wewe Erick una matatizo gani wewe? Yani hata kuuliza nimefikia chumba gani hakuna unfanya kukariri tu, haya niambie uzima upo lakini!”
“Upo mama ila nina matatizo”
“Kweli una matatizo maana kama umepigwa na shoti ya umeme vile, hata hueleweki, hebu nieleze kinachokusibu mwanangu”
Baba Angel hakusubiri muda kupita kwani alianza kumueleza mama yake kila kitu kuanzia alipoanza kumtafuta dokta Jimmy hadi alipopanga nae kuhusu watoto wake mpaka dokta Jimmy alivyomsimulia na kile alichokikuta kwa watoto wake, yani baba Angel alimaliza kusimulia huku machozi yakimtoka hadi mama yake aliamua kuanza kumbembeleza,
“Kwakweli mwanangu umeumia, hadi kukuona ukilia hivyo!! Kwa hakika umeumia, ila ni kweli hii kitu inaumiza, hivi huyu mzee Jimmy ni kwanini alikuwa na akili mbovu kiasi hiki jamani! Hapa ndio naanza kuwaelewa wale wa kusema kuwa tuwapime akili watu kabla ya kuzaa nao, jamani huyu mzee Jimmy kumbe alikuwa na akili mbovu kiasi hiki!! Nisamehe mwanangu kwa kitendo changu cha kuzaa na mtu mwenye akili mbovu kama mzee Jimmy”
Kisha huyu bibi alipumua kidogo na kuendelea kuongea,
“Unajua nini mwanangu?”
“Niambie mama”
“Kwa jinsi hali ilivyo, kwanza kabisa tuepuke aibu namba moja, twende tukampime Erica mimba ili tujue cha kufanya maana hii ndio itakuwa aibu kubwa kwetu”
“Kwahiyo tukikuta ana mimba twende tukamtoe mama?”
“Ndio, unadhani aibu hii tutaiepukaje?”
“Mama, tatizo haliepukwi kwa kuongeza tatizo. Mama nadhani kuna mambo ambayo kijana wako niliyatenda mwanzo ila ulikuwa huyajui, mama nishafanya dhambi hizo za kupeleka wadada kwenda kutoa mimba na mara zote Mungu aliacha salama kwani nilirudi nao salama ila kitendo cha kumtoa mimba binti yangu inaweza kuwa ni adhabu kwangu huwezi jua maana binti yangu anaweza kupoteza damu nyingi sana na kupoteza maisha”
“Kheee mwanangu, tunampeleka hospitali anatolewa kitaalamu”
“Mama, kutoa mimba haina fomula. Unaweza shangaa mtu katolewa hospitali na kupoteza uhai vile vile ndiomana hiki ni kitendo hatarishi. Kuna mwenzetu amekufa sababu ya kutoa mimba, siwezi kukubali binti yangu atoe mimba”
“Ila upo tayari kupambana na hiyo aibu ya mimba ya Erica?”
Baba Angel aliinama kwanza maana hakuwa na jibu, kisha mama yake akasema tena,
“Halafu mwanangu hilo swala la dokta Jimmy kwasasa niachie, naona huyo dokta hajielewi kama baba yako”
Ndipo baba Angel alikumbuka na ule ujumbe ambao mkewe alitumiwa kwenye simu, basi aliamua kumueleza mama yake kuhusu kile alichosoma na jinsi alivyofanya kwa dokta Jimmy na mlinzi, hapo mama yake alipumua kidogo na kusema,
“Erick, naomba nikuombe kitu mwanangu”
“Kitu gani mama?”
“Kwa leo, naomba ulale hapa mwanangu halafu kesho tutafikiria cha kufanya”
Mama yake aliamua kumlazimisha kufanya vile, kwahiyo aliamua kukubaliana na mama yake na kulala hapo kwani kile chumba alichochukuwa mama yake kilikuwa ni kikubwa, na mama yake alikataa kuchukua chumba kingine kwahiyo alimlazimisha baba Angel alale kwenye kochi pale sebleni halafu yeye alienda kulala chumbani maana kilikuwa ni chumba kikubwa chenye sehemu mbili yani chumba na sebule.

Mama Angel alilia pale na kulala pale pale alipokuwa, yani ni Ester tu ndio aliyemshtua na kulikuwa kumekucha tayari maana ilikuwa ni saa kumi na mbili alfajiri, basi aliamka, akamuona Ester kashika karatasi yenye maneno, basi mama Angel akaichukua na kuisoma akagundua ni ujumbe uliachwa na mume wake akimueleza kuwa ameenda hotelini kuonana na mama yake, basi hapo mama Angel ndio akaelewa ni kwanini hakumuona mume wake.
Muda kidogo mlango wa mama Angel uligongwa na aliyeingia alikuwa ni Erica ambaye alimsalimia mama yake na kumwambia,
“Mama, kuna wageni nje wanamuulizia baba”
Mama Angel akashtuka kidogo na kuamua kutoka ili kwenda kuongea nao.
Alifika hadi nje na kuwakuta pale, ambapo wale wageni walijitambulisha,
“Sisi ni maafisa usalama, tumekuja kumchukua ndugu Erick ili kwenda nae kituone kwaajili ya mahojiano”
Mama Angel akashtuka kwanza na kuwaambia kuwa mumewe hayupo, ila wale maafisa usalama hawakuamini ile kauli ya mama Angel basi wakamwambia,
“Naomba uturuhusu tuingie ndani na kukagua nyumba yako”
“Mmmmh hebu subiri kwanza”
Mama Angel akamuomba Erica akamletee simu yake ambapo alipofika nayo tu aliwaambia wale maofisa,
“Jamani kabla sijawaruhusu kufanya hivyo, kuna mtu naomba nimpigie kwanza simu”
“Ujue unatuchelewesha mama, kama mumeo yupo mwambie aje hapa tuondoke nae au tuachie tukakague ili tujihakikishie kama kweli hayupo”
“Nawaomba dakika tano tu niwasiliane na huyu mtu”
Kisha mama Angel alipiga simu moja kwa moja kwa shemeji yake na kumueleza kama watu wa usalama wamefika pale wanamtafuta mumewe ambaye hayupo ila wanataka kukagua nyumba ili kujihakikishia kuwa hayupo kweli, basi shemeji yake alimwambia vitu vinavyotakiwa kabla ya nyumba kukaguliwa kisha mama Angel alivyokata simu aliwaambia wale maofisa wamuonyeshe hivyo vitu alivyoambiwa,
“Hivi mama unautambuzi vizuri au hutambui?”
“Natambua vizuri ndiomana kabla ya kukubali niliamua kumpigia mwanasheria simu ili nijue cha kufanya, maana mimi sheria siijui vizuri”
“Unawezaje kuwakatalia polisi kukagua nyumba yako?”
“Sijakataa ila naomba kuonyeshwa barua inayoruhusu nyie kukagua nyumba yangu”
“Hivi hujui kama kuna vitu huwa ni vya dharula kama jambo hili? Tunahitaji kukagua nyumba ili kujiridhisha”
“Nitaruhusu endapo na mimi nikijiridhisha kuhusu nyinyi”
“Unawajua polisi vizuri wewe?”
Mama Angel alikaa kimya, kisha wakasema tena,
“Inaonyesha una kiburi sana wewe mwanamke, unawezaje kuwakatalia polisi kufanya kazi yao?”
“Sijakataa ila nahitaji kibali ili niweze kujiridhisha, nimeambiwa mnionyeshe vitambulisho vyenu kwanza mmegoma kunionyesha, barua ya kuwaruhusu nyie kukagua nyumba yangu napo mmegoma, je mwenye matatizo hapo ni mimi au ni nyie?”
“Aaaah sasa na wewe kesi yako inakuja”
Yule mmoja akamuitwa mwenzie aliyekuwepo kwenye gari,
“Afande Petro hebu lete pingu tumfunge huyu mama tumchukue kwa niaba ya mumewe”
Muda huo huo mama Angel aliingia ndani na kumtaka mlinzi afunge geti halafu yeye alikimbilia ndani kwake na kumpigia tena simu shemeji yake,
“Shemeji eti walitaka kunikamata mimi”
“Wakukamate kwa kosa lipi?”
“Sijui, nimewaambia wanionyeshe vitambulisho vyao wamegoma”
“Mmmmh shemeji sio mapolisi hao, mnatakiwa kuwa makini sana. Watu wakija kwako na kujitambulisha kuwa ni watu wa usalama, wakupe vitambulisho vyao kwanza uvisome ili ujihakikishie kuwa ni wenyewe, vinginevyo hao sio itakuwa ni matapeli wa mjini tu”
Mama Angel alihisi moyo kwenda mbio yani hadi kuanza kufatiliwa na matapeli wa mjini tena alihisi baridi kwenye mwili wake.

Leo Junior alitaka kwenda kwenye msiba wa Linah ila mama yake sababu kamzuia kutoka ikawa ni ngumu sana kwake ingawa alitumiwa jumbe nyingi sana za kifo cha Linah,
“Ila mama si vizuri kutokwenda kwenye msiba wake”
“Mjinga wewe, bora useme unaenda sehemu nyingine ila sio kwenye msiba wa huyo mtu”
Junior aliamua kujigelesha pale na kudai kutokwenda tena, ila kuna muda aliwaaga kuwa anaenda dukani kisha aliongoza moja kwa moja hadi nyumbani kwa Linah ambapo alikuta watu wamejaa kwenye ule msiba, basi alisogea karibu na mwanamama mmoja alimsogelea Junior na kumkumbatia huku akilia kwa kutaja shemeji shemeji na kufanya waliokuwepo pale kushangaa tu, kisha alipomaliza alianza kumueleza kwa kifupi,
“Kwani imekuwaje?”
“Sijui hata imekuwaje? Linaha hakuniambia ukweli mimi, mwisho wa siku nimekuja kupata taarifa tu kuwa amekufa, ila ngoja nikuibie siri maana hii tunajua wachache sana, inasemekana Linah alikuwa akitoa mimba”
Junior alishtuka na kusema,
“Inamaana alikuwa na mimba kweli?”
“Ndio, ulidhani hawezi kushika mimba au? Ulipomuona ni mtu mzima ukahisi hawezi kuzaa tena! Linah alikupenda kweli na alitaka mfike mbali ndiomana aliamua kuzaa na wewe, sijui nini kimempata hadi kutoa mimba hiyo, au ile kasumba ya kusema umeoa Junior! Hivi umeoa kweli au?”
Kuna mtu alisogea karibu yao na kumuuliza Junior,
“Hivi wewe sio mtoto wa marehemu James kweli?”
“Ndio ni mimi, naitwa Junior”
“Kheee Junior kumbe ndio umekuwa mkubwa hivi jamani!!”
Yule mtu alimkumbatia Junior na kumwambia,
“Mimi ni babako mdogo, yani kumbe Linah alikuwa akikufahamu halafu wala hakutuambia”
Ndipo yule rafiki wa Linah na Junior wakashtuka kisha rafiki wa Linah akauliza,
“Kwani huyu ni nani yenu?”
“Huyu ni mtoto wa kaka yangu James, yule marehemu yani ukimuangalia kwa mbali kama James vile, cheki alivyofanana nae jamani!”
“Kwani Linah na huyo James ni nani na nani?”
“Linah ni mtoto wa shangazi yetu, halafu Linah alipatana sana na James naona ndio sababu ya yeye kuwa karibu na mtoto wa James kuliko sisi ambao tulimuona huyu mtoto akiwa mdogo kabisa. Jamani Junior umekuwa sana, mama yako yuko wapi? Anajua kama kuna msiba wa wifi yake huku au hajui?”
Junior alibaki kimya akijiuma uma tu maana hata yeye alikuwa anashangaa tu kusikia kuwa Linah alikuwa ni ndugu yake, kwahiyo alikuwa na mahusiano na shangazi yake, hapo hata yule rafiki wa Linah aliweza kuelewa ni kwanini Linah alichanganyikiwa hadi kufikia hatua ya kutoa ile mimba ambayo imechukua uhai wake”
Junior alibaki kushangaa tu ila hakuwa na namna zaidi ya kuulizia ratiba ya mazishi maana msiba huu aliusikia muda hata akajua pengine wameshazika ila hadi siku hiyo wala hawakuwa wamezika, akamuuliza yule rafiki wa Linah kuwa mazishi ni lini,
“Wanasema kuwa mazishi ni kesho, ndio tupo kusubiria hapa ili ratiba kamili ipatikane”
“Aaaah sawa”
Kisha yule baba alimshika mkono Junior ili kwenda kumtambulisha kwa ndugu wengine, kwakweli yule rafiki wa Linah alibaki kustaajabu tu,
“Huyu hakuwa akimfahamu Junior ila nahisi alifahamu tu kuwa kaka yake alikuwa na mtoto wa kuitwa Junior, na alipomuona tu kamtambua kuwa kafanana na ndugu yake, iweje Linah alishindwa kutambua hili? Kwanini lakini? Uwiiii, rafiki yangu jamani”
Alifikiria na kukosa jibu kisha akaamua kuendelea na mambo mengine tu.
 
SEHEMU YA 401

Baba Angel kule hotelini, alitaka kuondoka mapema sana ila mama yake alimzuia hadi wapate kifungua kinywa kwahiyo walishuka chini na kuagiza kifungua kinywa huku wakila na kuongea mambo mbalimbali, ila alifika yule mwanamke ambaye usiku wake baba Angel alikosea mlango, basi yule mwanamke alifika na kuwasalimia kisha aliomba kuongea kidogo na baba Angel ambapo mama yake aliwapisha na kukaa meza ya pili,
“Inamaana Erick hujanitambua hata kidogo? Halafu mbona upo hivyo kama mtu aliyechanganyikiwa na maisha?”
“Acha tu”
“Tatizo ni nini?”
“Hakuna tatizo”
“Haya niambie hujanikumbuka tu!”
“Kweli kabisa sikukumbuki”
“Kuna kipindi ulikuwa Afrika Kusini, na ulikutana na mimi kwenye kasino, hapo tukazioeana na kupendana, tulianza mawasiliano na kuwa karibu. Tulipiga picha mbalimbali pamoja na uliahidi kunioa”
Kisha yule mwanamke alitoa baadhi ya picha alizokuwa nazo kwenye mkoba, zilikuwa kama picha tatu na kumpa baba Angel ambapo alipoziangalia tu alielewa na kusema,
“Khaaa kumbe Jack!”
“Ndio ni mimi, hata nimeshangaa kunisahau Erick jamani utadhani tuligombana!”
“Mbona umebadilika? Umenenepa sana kwasasa”
“Ukubwa huu Erick, saivi nimekuwa mmama ila bado huwa nakukumbuka sana. Niliporudi hapa nchini kitu cha kwanza nilikumbuka kuweka hizi picha katika mkoba wangu maana huwa nakukumbuka sana nikiziangalia, Erick bado nakupenda sana”
Baba Angel alitabasamu tu na kusema,
“Aaaah acha hizo Jack, kila mtu ana familia yake kwasasa. Nina mke na watoto wa kutosha tu”
“Ila unajua kama mimi na wewe tuna mtoto pia?”
“Mmmmmh Jack!”
“Ndio, kipindi kile ulipoondoka uliniacha na ujauzito Erick, sikutaka kukwambia tu kwani nilielewa kile kisirani chako cha kuwatoa wanawake mimba. Niliitunza ile mimba na sasa nina mtoto mkubwa kabisa ambaye ni mtoto wa mimi na wewe”
“Mmmmh!!”
“Usigune ila kubali tu siku umuone mtoto wako, nilikupenda kwa dhati. Niliitunza mimba na nikamtunza mtoto ingawa haukuwa pamoja nami, ila imani yangu ni kuwa dunia ni duara, nilijua ipo siku tu mimi na wewe tutakutana ndiomana sijaweza muzitupa hata hizi picha. Erick, mimi na wewe tuna mtoto mkubwa tu wa kiume”
Baba Angel alizidi kustaajabu yani alikuwa haelewi kitu kwa muda huo, hapo kengele ya hatari ikalia kichwani mwake kuwa kilichotokea kwa Rahim na watoto wake basi kinaweza kutokea na kwake pia, ni kweli alifanya makosa ila ilikuwa kipindi cha ujana, basi alimuangalia huyu Jack na kumwambia,
“Nimekuelewa, ila itakuwa vyema kama ukija kunitambulisha mwanangu ili nimtambulishe kwa ndugu zake aweze kufahamiana nao. Halafu naomba nitakulipa gharama zako, najua siwezi kukulipa kwa kiasi kikubwa ulichokifanya kwa mwanangu ila nitakupa hata hela ya kufutia machozi, naomba unitambulishe kwa huyo mwanangu tu.”
“Sawa, hakuna tatizo nitakutambulisha ila ningependa kujua anuani ya unapoishi, namba yako ya simu ili tuendelee mawasiliano baina yetu”
Baba Angel aliamua kumpa kadi yake ya mawasiliano, kwakweli muda huu baba Angel alikuwa haelewi kitu chochote aliona kama kuzidi kuchanganywa tu maana hata hakujua ni jinsi ataweza kumueleza mkewe kuhusu huyo mtoto ambaye hawakujua kama yupo, ila kama Jack alielewa vile na kumuuliza baba Angel,
“Inaonyesha unamuogopa mke wako eeeh!!”
“Aaaah hapana”
“Erick utakuwa mwanaume gani wewe wa kumuogopa mkeo? Yani ushindwe kumtambulisha mwanao kwa uhuru sababu ya mkeo? Tena hata usimwambie ila hiyo siku iwe ni mshtukizo tu kwake”
“Mmmmh nampenda sana mke wangu”
“Huo ndio ujinga wa baadhi ya wanaume, muda wote kukazana nampenda sana mke wangu, mwishowe maji yanakufika shingoni unashindwa cha kufanya. Wanaume kama wewe ndio wale ambao mnasikiliza kila kitu toka kwa wake zenu, yani mkeo akikukataza kufanya kitu basi hufanyi, unakuwa sio mwanaume kwakweli, unatakiwa kusimama kiume kwenye kila eneo. Mkeo yupo chini yako, sio swala la kumsikiliza mwanamke muda wote”
Baba Angel hakutaka kuendelea kuongea na huyu mwanamke maana huwa hapendi mtu akitoa tafsiri mbaya juu ya mke wake, kwahiyo aliamua kumuaga na moja kwa moja alimfata mama yake na kumuaga kisha aliondoka zake kuelekea nyumbani kwake.

Baba Angel alirudi nyumbani kwake na kumkuta mkewe kajifungia tu chumbani, basi alimgongea na kufunguliwa kisha alipoingia alimuelezea jinsi mama yake alivyomueleza kuhusu watoto wao, kisha mkewe nae alimwambia kuhusu polisi feki waliofika hapo nyumbani kwao, kisha akamuuliza,
“Hujapata taarifa yoyote kwani mume wangu?”
“Hakuna taarifa yoyote niliyoipata zaidi ya kutumiwa ujumbe kuwa kesho ni mazishi ya Linah”
“Kheee walikuwa hawajazika tu hadi leo?”
“Ndio na wamesema kuwa nisikose”
“Huu ndio ujinga nisioupenda, usikose kwani wewe ndio Mchungaji wa kuongoza sala kwenye huo msiba au kitu gani? Baba Angel, hakuna kwenda popote”
“Mmmh na wewe mama Angel, unajua kuna vitu unakataza bila hata kufikiria. Ule ni msiba lazima tushiriki, huo ndio ujamii”
“Hivi mambo yaliyokupata, unatakiwa kukaa chini na kutafakari sio kuanza kuhangaika baba Angel, naomba unisikilize kwa hili. Kama pole utaenda kuwapa, hapo ulipo hata hujui ni nani aliyekupa shutuma za kuua na hata hujui ni nani aliyekufa”
“Ninachojua ni kuwa hakuna niliyemuua, na kama dokta Jimmy amekufa basi natamani niende kwenye msiba wake nikamkate kichwa. Kiukweli mama Angel sipo sawa mimi, acha tu nikashiriki mambo mengine ya kijamii ili niweze kuwaza vitu vipya”
Mama Angel alishindwa hata namna ya kuendelea kumshawishi mumewe kuwa asiende huko kwenye mazishi ya Linah.

Usiku wa leo, Junior alimueleza ukweli mama yake kuwa alienda kwenye msiba wa Linah na kumueleza kitu alichoenda kukutana nacho huko, mama Junior alishangaa sana kwani hakutegemea na ndugu yake mama Angel hakumueleza ukweli kuhusu undugu wa Linah na Junio basi alishangaa pale,
“Ndio hivyo mama, yule bamdogo alienda kunufahamisha kwa ndugu wengine pale”
“Duh!! Jamani, mbona sijui mambo haya”
“Ndio hivyo mama”
Ila ambacho Junior hakumwambia mama yake ni ile hali ya kusema kuwa Linah alikuwa akitoa mimba, maana aliona ni swala la aibu.
Usiku huu mama Junior alijikuta akifikiria tu kuhusu swala hili, kulipokucha alijiandaa mapema kabisa na moja kwa moja kwenda nyumbani kwa mama Angel ambapo alipishana na baba Angel ndio alikuwa akitoka kwa muda huo, basi aliasalimiana nae na yeye kuingia ndani.

Baba Angel alifika msibani na kukuta watu pale kama kawaida na wengine walikuwa wakiongezeka kwaajili ya mazishi ya Linah.
Basi baba Angel aliitwa na Manka ambaye alimuuliza,
“Mbona umekuja peke yako? Mke wako yuko wapi? Tuseme hakumfahamu Linah?”
“Aaaah mimi nipo kumuwakilisha hata yeye pia”
“Erick,angalia nyuma yako”
Baba Angel aligeuka na kukutana uso kwa uso na watu wawili waliovalia sare za polisi, wakiwa wameshika pingu na kumsogelea kisha walimfunga zile pingu na kumwambia kuwa yupo chini ya ulinzi.

Baba Angel aligeuka na kukutana uso kwa uso na watu wawili waliovalia sare za polisi, wakiwa wameshika pingu na kumsogelea kisha walimfunga zile pingu na kumwambia kuwa yupo chini ya ulinzi.
Baba Angel alishangaa sana, ila Manka alimuangalia na kuanza kucheka kisha alimuuliza kwa kejeli,
“Kwani umefanya nini Erick?”
“Hata mimi sijui”
Basi baba Angel aliwauliza wale maaskari,
“Kwani nimefanya nini?”
“Inamaana hujui kama umeua?”
“Nimemuua nani sasa?”
“Utajua huko huko mbele ya safari”
Basi Manka alicheka tena na kumuuliza baba Angel,
“Na utanashati wako huo kumbe muuwaji eeeh! Hebu niambie uliuaje Erick”
Kwakweli baba Angel alikuwa akishangaa tu, jinsi alivyokamwatwa na jinsi wale maaskari walivyoacha apewe maneno na Manka, ambapo Manka aliendelea kuongea,
“Erick, sikia nikwambie. Unaijua kesi ya mauwaji vizuri? Yani ukiwa na kesi ya mauwaji basi ujue, kifungo chake ni maisha yako yote. Sasa kaa huko gerezani halafu uone huyo mwanamke unayejifanya unampenda sana kama hatoolewa na mwanaume mwingine”
Manka alicheka tena na kusema,
“Yani nakwambia utakuwa na maumivu sijui aina ngapi katika maisha yako, mapacha wako wamepeana mimba, kumbuka ni damu yako ile eeeh!! Mkeo alikuwa akimcheka Sarah wangu na kuniona sijui kulea, haya kiko wapi sasa kwa yeye anayejua kulea? Mbona watoto aliowaaa mwenyewe wameweza kupeana mimba? Tena watoto mapacha, ni aibu kubwa sana sijui suira zenu mtaziweka wapi kwenye jamii, lakini hakuna shida maana sura yako utaiweka gerezani. Haya maumivu ya kusalitiwa na baba yako mzazi, maumivu ya kufanya hasira na kuua, maumivu ya mkeo kuolewa na mwanaume mwingine. Halafu unajua mkeo ataolewa na nani? Hahaha ataolewa na dokta Jimmy”
Hapo baba Angel alishikwa na hasira zaidi na kutamani kumpiga Manka ingawa kafungwa pingu kwani alijikuta akimkata mtama na kumfanya Manka aanguke chini, basi wale maaskari wakamshikilia vilivyo baba Angel, halafu Manka akamwambi,
“Umechukia eeeh!! Ulihisi umemuua dokta Jimmy, kwa taarifa yako umemuua yule mlinzi wenu asiyekuwa na hatia, na subiria kifungo chako cha maisha halafu mkeo ataolewa na dokta Jimmy, nitakuletea picha za harusi yao huko huko gerezani utakapokuwa. Mjinga wewe, upo chini ya sheria halafu unanipiga, acha niongee yote ya moyoni. Naomba nikwambie kwamba, sikupendi Erick na sijawahi kukupenda mjinga wewe, muda wote kujifanya unampenda sana Erica, tuone kama ataenda na wewe gerezani”
Halafu Manka alimsogelea tena baba Angel pale alipokuwa ameshikiliwa na wale maaskari halafu akamnasa baba Angel vibao kadhaa na kusema,
“Vingine nitakuja kukumalizia unapopelekwa rumande, mjinga wewe. Hebu mtoeni hapa asijekuharibu mambo ya msiba bure. Nina machungu ila kukamatwa kwako, kwangu ni furaha sana. Mpelekeni huko mjinga huyu, nilikuwa nakuhimiza kuja ili ukamatwe na tumefanikisha hili oooh asante Mungu”
Wale maaskari walimshika baba Angel na kumburuza hadi kwenye gari ambalo walienda nalo pale na kumpakia kisha kuondoka nae katika eneo lile.

Mama Junior alikaa na mdogo wake huku wakizungumza mambo mbalimbali ambapo mama Angel alimueleza vile ambavyo aliambiwa na Dora kuhusu undugu wa Linah na James, na hapo alimuuliza dada yake juu ya swali ambalo Dora alimuuliza,
“Eeeeh dada ni kwanini mlikuwa hamuwatembelei ndugu zake James na wala ndugu zake kuja pale kwako kwanini?”
“Mmmmh mdogo wangu sijui nikwambiaje”
“Niambie tu dada”
“Ni hivi, kiukweli mimi zamani sijui nilikuwaje, nilikuwa na kinyaa sana kiasi kwamba ndugu wa James wengi walikuwa hawanipendi, halafu mume wangu alifanya mimi nijione ni bora kuliko mwanamke yoyote duniani, wanawake wengi wanaolewa wakiwa hawana bikra ila mimi nilikuwa mwanamke bikra na tena sikuwa na mahusiano na mwanaume yoyote kabla ya James. Mume wangu alikuwa akinipenda sana, nikisema hiki sitaki basi alikitoa kwangu. Mimi si kwamba nilikuwa sipendi wageni ila walikuwa wakiniona mimi wanadhani najivuna sana, ila ni sababu ya malezi tu ambayo nililelewa, nakumbuka kuna kipindi kulikuwa na msiba kwakina James, tulienda msibani ila huwezi amini pale kwakina James sikunywa hata maji yani sijui nilikuwa naonaje, nikiwa na njaa namwambia James twende hotelini tukale, alinitambua nilivyo kwahiyo alikuwa hakatai, kuanzia asubuhi hadi usiku tunakula cha hotelini kwahiyo kwenye msiba nilikuwepo tu, halafu kitu kingine mimi nilikuwa mvivu sana kiasi kwamba pale msibani hakuna kazi niliyokuwa naifanya na hata kulala ilibidi mimi na watoto wengine wa ndugu zao tukalale chumbani, sikuweza kulala kwenye majumuiko. Kumbe kile kitu kiliwakera sana ndugu wa James, na hapo walimwambia James mimi ni marufuku kukanyaga kwao na wala wao hawatakuja kukanyaga kwa James. Haikuwa tatizo sana kwangu kwani sikufikiria kama kwao nitaenda tena, na kweli sijaenda hadi tulivyoachana na James. Ila kitendo cha mimi kukaa nyumbani kimenifanya niwe nibadilike, nianze kuishi vyema na jamii inayonizunguka, niache kinyaa na majivuno, kwasasa uliza wifi yangu yoyote kwa Deo kama kuna mmoja atakwambia kuwa mimi najivuna! Na wote huwa wanakuja kwangu na mimi naenda kwao, kwakweli nilichokuwa nafanya ni kibaya sana”
“Ndiomana kwasasa ukaweza kuzoa watoto wote wa mumeo na kulea mwenyewe!”
“Ndio, ninawalea sitaki tena kuwa kama vile nilivyokuwa. Sio tabia njema kabisa, mama alikuwa mkali ila sijui kwanini mimi nilikuwa mvivu jamani loh!”
Basi mama Angel akamshauri dada yake kuwa wapange siku waende kwenye familia ya James ukizingatia familia hii dada yake hajaonana nayo toka kipindi hiko cha nyuma. Ni wachache sana waliomuona Junior wakati mdogo ndiomana wengi hawakumjua kama ni mtoto wa James.
Muda kidogo mama Junior alipigiwa simu kuwa aende mahali, basi akaongea na mdogo wake pale,
“Erick si anipeleke na gari tu huko ninapoenda?”
Ikabidi mama Angel amuite Erick ila hapo ndio akagundua kuwa Erick hakuwepo na ilisemeka na kuwa alitoka mapema kabisa kabla hata baba yake hajatoka,
“Kheee kaenda wapi? Mbona hajaniaga?”
“Hakuna aliyemuaga huku ndani mama, ila wote tumeshangaa tu hayupo”
“Khaaaa jamani, mambo gani haya sasa?”
Mama Angel hakuelewa, kwahiyo kwa muda huo alijikuta akianza kufikiria kuwa mwanae yuko wapi, ikabidi tu mama Junior aondoke mwenyewe maana aliona tayari mdogo wake kashaanza mambo mengine ya kumtafuta Erick.
Yani mama Angel kwa muda huo alijaribu hata kuwapigia simu watu wa karibu na Erick ili ajue kama wapo pamoja nae ila wote hawakujua Erick alipo.
 
SEHEMU YA 402

Erick siku hii aliondoka kwao mapema sana, kumbe alikuwa akisubiri baba yake atoke na alianza kumfatilia, na alifika nae hadi kule kwenye msiba kisha baba yake alivyochukuliwa na wale maaskari naye Erick alikuwa nyuma yao akiwafatilia ila yeye alikuwa na pikipiki maana ndio aliyotoka nayo nyumbani kwao.
Alimfatilia baba yake ila alichoshangaa Erick ni kuwa baba yake hakupelekwa kwenye kituo cha polisi ila moja kwa moja baba yake alipelekwa kwenye ile nyumba ya babu yake. Ndipo hapo akili ya haraka ikamcheza Erick na kumfanya kuweka pikipiki pembeni kisha kuanza kusogea pale karibu na kwa babu yake.
Alipofika pale, alichungulia na kumkuta dokta Jimmy kasimama pembeni halafu kuna mtu amelazwa chini huku baba Angel akiamriwa amkabe yule mtu aliyelazwa chini, baba Angel aliambiwa,
“Unachotakiwa kufanya kwasasa ni kumkaba huyo mtu kama ulivyonikaba mimi”
“Mbona siwaelewi!”
“Usiwe mbishi”
Baba Angel alishtukia akipewa ngumi ya mgongo na kupiga magoti mbele ya yule mtu, kisha yule aliyevalia nguo za kiaskari mmoja wapo alimfungua baba Angel zile pingu ili aweze kumkaba yule mtu.
Erick hakuelewa ni kwanini wanafanya vile ila muda ule ule Erick alisogea kati yao na kufyatua risasi juu na kusema,
“Wote mikono juu”
Kilikuwa ni kitendo cha haraka na hakuna alieyekitarajia kwa muda ule, waliacha kila kitu na kupandisha mikono juu, hakuna aliyeweza kuelewa kwa haraka kuwa Erick ametoa wapi ile risasi, kisha Erick alimuamuru baba yake atoke nje ya pale, ila mtu mmoja pale aliamua kujitoa muhanga na kumshika baba Angel, yani yule mtu alishtukia akipigwa teke la maana sana na Erick hadi aliangukia pembeni kisha Erick alimfata nyuma baba yake hadi kwenye bodaboda yake na kupanda naye kisha kuondoka kwenye eneo lile.
Kwakweli ilikuwa ni jambo la haraka sana kiasi kwamba hakuna hata mmoja aliyeelewa kuwa kuna kitu kama kile kinaweza kutendeka pale, ukizingatia baba Angel sio mtu wa mapigano wala sio mtu wa kutunza silaha ndani ya nyumba yake.
Kila mmoja alishangaa kuwa ile risasi yule Erick mdogo kaitoa wapi, na lile teke alilompiga nalo yule mtu kajifunzia wapi? Kila mmoja pale alibaki kustaajabu kwa kile kilichofanywa na Erick mahali pale.

Baba Angel alimuomba Erick wapiti kwenye hoteli ya karibu kwanza kwani alitaka kupiga simu nyumbani kwake kwanza kwa usalama wa familia yake, kwahiyo walifanya hivyo na kukodi chumba pale, kitu cha kwanza baba Angel alimpigia mke wake kuwa asiwe na wasiwasi naye wala Erick halafu alimpigia simu mlinzi wao ili asimkaribishe yoyote hapo nyumbani kwake. Kingine aliona vyema amtafute shemeji yake na kumwambia kwa kifupi tu ili shemeji yake ajue jinsi gani ataisaidia familia yake sababu mambo mengi ya sheria anayafahamu.
Baba Angel alitulia kwa muda kimya huku akitafakari, aliinua kichwa na kumuangalia Erick ambaye bado inaonyesha akiwa na hasira hadi mishipa ya fahamu ikiwa imemsimama, kisha baba Angel alimwambia mwanae,
“Asante kwa kuniokoa mwanangu, asante sana sijui hata wale watu walitaka nini na ili iwe ini sielewi mpaka muda huu nahisi tu kutetemeka mwili mzima”
“Pole sana baba”
“Ila ulijuaje mwanangu kuwa kuna matatizo hadi ukaja kunisaidia?”
“Mimi sikujua kitu, ila kuna muda jana usiku alikuja Erica chumbani kwangu akasema alikuwa akipita karibu na chumba chenu akakusikia wewe na mama mkiongea kuhusu kwenda mahali ambapo mama alikuwa akikukataza kwenda ila wewe ulikuwa ukikazana kuwa utaenda tu, ila badae Erica aliniambia anapata hisia mbaya sana juu ya sehemu unayotaka kwenda, anaona wazi si salama. Mara nyingi huwa napenda kuyaamini mawazo ya Erica ila nilijipanga bila yeye kujua, nilitaka kujua ni kitu gani kitaendelea kwako. Huwezi amini, mimi nimetoka asubuhi kabla hujatoka wewe, nilienda kufata ile pikipiki gereji ila nilikuta bado haijatengemaa vizuri basi nikakodi nyingine, nilikukuja karibu na nyumbani nikikuvizia utoke nianze kukufatilia, nilijua nikikwambia twende pamoja ungekataa”
Baba Angel alipumua kidogo na kumuuliza,
“Na hiyo bastola umeitoa wapi?”
“Kwanza, hii bastola sikujua hata kama ina risasi. Siku tumeenda kwa babu, kuna chumba mimi nilienda kuvaa nguo na ndipo nilipoiona hii bastola nikaificha hata Erica sikumwambia, na nilimwambia Erica twende ufukweni ili nikapunguze mawazo ila tulivyofika kule, kuna muda Erica alienda kujisaidia basi kuna mahali nilichimba na kuificha kule kule, sema kule watu huwa hawaendi mara kwa mara. Leo nilivyochukua ile pikipiki, kitu cha kwanza ni kwenda hadi ufukweni kufata bastola na kurudi kukuvizia wewe”
“Sasa bastola ulichukua ya nini?”
“Sijui ila nilikuwa nasema endapo kukitokea dharula”
“Duh!! Unajua umeniokoa mwanangu, ila mengi nimeshangaa ujasiri huo na nguvu hizo umezitoa wapi?”
“Sijui, labda sababu napenda sana kuangalia muvi za kivita”
Baba Angel alimuangalia mwanae bila hata ya kummaliza maana ni mambo mengi sana alijikuta akijiuliza juu ya mwanae, kiukweli alimchanganya sana yani kuna vitu alikuwa havielewi kabisa ingawa ile kuokolewa na mwanae ilikuwa ni njema.

Mama Junior akiwa njiani kuelekea nyumbani kwake maana alishatoka kule alikokuwa akienda, akakutana na mama Daima na kusalimiana nae pale, basi alimuaga na kutaka kuondoka ila mama Daima alimshika mkono na kumwambia,
“Ila unajua wewe ni mwanamke mwenzangu hata kama huna mtoto wa kike ila ulitakiwa kuwa na huruma kwa mtoto wa mwanamke mwenzio”
“Kwani nimefanyeje?”
“Kumbe nia yenu ilikuwa ni kumfanya Junior amuoe yule msichana wa kazi wa ndugu yako, uliona Junior akimuoa Daima basi Daima atafaidi sana au kitu gani?”
“Jamani, yametokea wapi hayo?”
“Nakuuliza mama mwenzangu, yani mmemlazimisha Junior aoe ili kunikomesha mimi au kumkomesha huyo Daima? Kumbuka ulichofanya kwa mwanangu kitafatilia hata wajukuu zako.”
“kheeee usione nimenyamaza ukadhani napenda, kwani una matatizo gani wewe! Huyo Daima hajakwambia ukweli kuwa alimsingizia shemeji yangu anataka kumbaka hadi aksababisha watu wengi kujaa na kutaka kumpiga shemeji! Hajakwambia huyo Daima wako?”
“haya tuachane na hayo, hivi unajua kuwa Daima ni mjamzito tena?”
“Mmmh!!”
“Guna tu ila Daima ana mimba nyingine ya Junior”
Mama Junior alisikitika kwanza ka kusema,
“Hivi watoto wa kike ni nani aliyewaroga jamani hata awahurumie kidogo, huyo Daima hajui kama Junior ni mume wa mtu kwasasa? Mbona kujitafutia tu matatizo jamani, mambo mengine yanasononesha na kusikitisha. Hiyo habari umeichukuliaje mama yake?”
“Aaaarggh!!”
Mama Daima hata hakuongea zaidi kwani muda huo huo aliondoka zake na mama Junior kwenda nyumbani kwake kwanza.

Baba Angel na mwanae Erick walifika nyumbani kwao wakati tayari usiku umeshaingia, basi waliingia ndani na kusalimia wale waliopo nyumbani kwao. Muda huo huo simu ya baba Angel ilianza kuita maana alikuwa nayo mfukoni tu, basi akaichukua na kupokea na kukuta mpigaji ni Sia, basi alianza kuongea nae,
“Kuna muda Fulani nilifika nyumbani kwako, nikaona kuna vijana kama watatu halafu kila mmoja alikuwa na pikipiki na walikaa nje ya nyumba yako kamavile kuna kitu walikuwa wanavizia”
“Mmmh!!”
“Sikuondoka hadi walipoondoka, walikaa pale nje kama masaa mawili hivi sijui ni kitu gani walikuwa wakivizia hapo nyumbani kwako”
“Sijui, hivi hujaenda kwenye msiba wa Linah yule ndugu wa Manka?”
“Aaaaah ule msiba nilienda mara moja tu, nilipoona haueleweki sikwenda tena kwenye ule msiba, yani pale katika msiba kuna watu wana mipango isiyoeleweka mwanzo wala mwisho. Nasikia jana wamezika”
“Kakwambia Manka?”
“Ndio, tena kanipigia simu huku akicheka kuwa wameshazika hata sikumuelewa mtu umefiwa halafu unacheka. Ule msiba sijauelewa kabisa, ila Erick kuna kitu nataka nikwambie”
“Kitu gani?”
“Kuwa makini sana na yule mwanamke, sio mtu mzuri kwako. Kuna siku nilimkuta na mtu huyo, yani mipango waliyokuwa wakipanga nikikwambia unaweza kupatwa na kichaa, nitakutafuta ili tuongee vizuri zaidi”
Kisha Sia alikata simu halafu baba Angel aliinuka moja kwa moja na kwenda chumbani kwake.

Baba Angel alimsimulia mke wake kuanzia mwanzo wa tukio hadi mwisho, na kumfanya mama Angel ashangae sana na kuogopa,
“Lakini nilikukataza mume wangu?”
“Nakumbuka, majuto ni mjukuu. Sijui ingekuwaje kwasasa na sijui walitaka nini”
“Nadhani walitaka kupata ushahidi ili uhukumiwe na mahakama moja kwa moja, hawakutaka kukuhukumu wao ila walitaka uhukumiwe na mahakama”
“Simpendi yule dokta Jimmy simpendi kabisa, ila simpendi zaidi Manka, ni mwanamke mbaya sana. Kanifanyia kitu kibaya ambacho sikukitegemea”
“Pole mume wangu, huwa tunamsema Erica kwa umbea kumbe kuna mahali umbea wake utatusaidia”
“Ila mke wangu swala la watoto wetu kuwa pamoja kimapenzi umefikia nalo wapi?”
“Baba Angel naomba hayo maswala tusizungumze kabisa maana nahisi kupatwa na uchizi jamani, nawapenda sana watoto wangu ila kila nikifikiria hayo nahisi kuchanganyikiwa. Ila mume wangu, tufanye swala moja unajua wakija kutukamata na bastola humu ndani itakuwa balaa sana!!”
“Naelewa, ila Erick sio mjinga kiasi cha kukaa na bastola humu ndani”
“Sasa ataiweka wapi? Yani hiyo ni kesi nyingine, hatuna kibali cha kumiliki hiyo kitu, ila duh Erick kajifunzia wapi hayo? Hadi naogopa yani nahisi kusisimka mwili mzima”
Waliongea siku hii yani waliongea sana, walijikuta wakiongea hadi panakucha maana ilikuwa ni siku ya ajabu sana kwao.

Sia, leo aliamua kwenda tena kwa mama yake Steve maana siku ile yule mama alipishana na Sia kwahiyo alitoka muda ule ule ambao Sia aliingia.
Leo alimkuta na kuanza kuongea nae,
“Kwanza mama naomba mnisamehe sana, kipindi cha nyuma nilikuwa kama nimepumbazwa”
“Eeeeh kilichokuleta?”
“Ni hivi mama, ni kweli mtoto yule niliyekuwa namlea hakuwa mtoto wa Steve”
“Nilijua tu, ulizaa na mwanaume mwingine halafu kuja kumdanganya mwanangu”
“Sio hivyo mama, ni kwamba yule mtoto hakuwa wa Steve wala hakuwa mtoto wangu ila yule wa mwanzo uchangani niliyempa jina Steve ndio alikuwa mtoto wetu kweli”
“Sikuelewi”
“Ni hivi mama, yani mimi nilimlea mtoto vizuri kabisa, ila siku nampeleka kliniki wakaniambia kuwa mtoto amepotea, basi nilipewa mtoto mwingine nimlee, sikutaka kurudi bila mtoto ndio nikamkubali yule na kuanza kumlea”
“Hivi unadhani hayo maelezo yako kuna mtu yanaweza kumuingia katika akili yake? Haya ikawaje sasa?”
“Mtoto wangu nimejua alipo kwasasa”
“Yuko wapi?”
“Mtoto wangu ni yule Paulo anayeishi na Steve na yule mke wake”
“Hivi una akili timamu wewe? Yule ni mtoto ambaye Steve alizaa na yule mwanamke ila alituficha tu”
“Mama, naomba nisiongee sana. Ila siku muulize yule Oliva ukweli kuhusu yule mtoto halafu atakujibu na ndio hapo utagundua kuwa yule ni mtoto niliyezaa na Steve, si unamuona anavyofanana na Steve?”
“Yani nilifikiri umepona kichaa kumbe kila kukicha ndio kinazaliwa upya, pole sana. Umeanza hadi kudai watoto wa wenzio, bila shaka utaanza kudai na wazazi wa wenzio maana unapoelekea sio penyewe. Pole sana binbti, wewe sio wa kufokewa ni wa kuonewa huruma tu”
“Sitaongea sana ila nitaongea kwa vitendo nanyi mtanielewa, maana yule ni mtoto wangu kabisa”
Sia aliona huyu mama hamsikilizi kabisa kwahiyo aliamua tu kuondoka kwa muda ule, alikuwa akitembea huku akiwaza cha kufanya.
Aliwaza vitu vingi sana, alitamani cha kwanza kabisa ampate mtoto wa madam Oliva kwani alihisi kuwa akimpata mtoto wa madam Oliva itakuwa rahisi kwa yeye kuaminika na maneno yake, akajiuliza,
“Je mtoto wa madam Oliva ni Sarah? Mmmmh nahisi Sarah ni mtoto wa madam Oliva, ila yule Sarah si anasoma shule anayofundisha madam Oliva, inamaana yule madam hajamgundua kuwa yule ni mtoto wake? Mmmh”
Alivyokuwa akitembea kuelekea stendi, akakutana na Manka akiwa kaongozana na Sarah ilibidi asalimiane nao ambapo Manka alimchukua pembeni Sia na kuanza kuongea nae,
“Mtoto ananisumbua huyu balaa, yani anachong’ang’ania yeye ni kwenda kuishi nyumbani kwa Erick na Erica, sijui nifanyeje na huyu mtoto unajua nashindwa kukubali ukweli kuwa huyu mtoto sio wangu!!”
“Ndio sio wako huyo, huyo ni mtoto wa Oliva”
“Haiwezekani, Oliva ni adui yangu, sidhani kama ningelea mtoto wake. Unajua nashindwa kukubali kabisa, kwanza sifikirii swala kuwa mzee Jimmy aliweza kunibadilishia mimi mtoto”
“Ila dokta Jimmy si amekuthibitishia hilo? Hata nashangaa unazidi kujitia uchizi, mimi ni chizi ndio ila mwenzangu uchizi wako umezidi. Huyo unayeona rafiki yako wa damu kakuthibitishia kabisa kuwa mtoto umebadilishiwa”
“Una uhakika gani?”
“Kilichokupeleka kwenye kaburi la mzee Jimmy na kukufanya ulie kwa uchungu ni kitu gani? Si baada ya kugundua kuwa ni kweli umebadilishiwa mtoto? Ila kwasasa unajifanya hukubali wala kuamini ukweli, ipo siku huyo mzee Jimmy atatamka pale pale kaburini kuwa alikubadilishia mtoto ndio akili itakukaa sawa”
Manka alikaa kimya kwa muda kidogo na kumtazama Sia, kisha alimwambia,
“Unajua kilichotokea jana?”
“Kipi hiko?”
“Kwasasa, Erick yupo rumande maana anatuhumiwa kumuua mlinzi wa nyumba ya baba yake”
“Kakamatwa lini?”
“Jana”
“Pole sana, nimeongea usiku na Erick ni mzima wa afya njema. Aliyekwambia Erick amekamatwa nani? Na hiyo ndio habari ya kukufurahisha?”
Manka alijaribu kumuelezea kwa ufupi Sia kuhusu kilichotokea siku ya jana, na jinsi alivyoongea na dokta Jimmy ambaye alimuhakikishia kuwa baba Angel yupo rumande, basi Sia alimuangalia Manka na kumwambia,
“Pole sana, hao ndio unaamini wanakupenda na kusaidiana nao. Hata una msiba wa dada yako ila unacheka kwaajili ya Erick, hao wamekudanganya, waambie wakwambie ukweli, ningekuwa ni wewe ningeachana na mambo ya dokta Jimmy na ningeenda kumueleza kila kitu Erick kuhusu mipango ya dokta Jimmy, pengine tukakomboka wote. Yani wewe huyo mtu kakufanyia ufedhuli ila bado unashirikiana nae, aaaah bora Mungu akunyime mali lakini sio akili”
“Kheee leo hii wewe umekuwa na akili kunizidi mimi wakati kila mtu anakuona ni chizi namba moja”
“Mimi chizi ndio, nimemuona mwanao anaondoka na wala sijakwambia”
Manka akaangalia sehemu aliyomuacha Sarah ni kweli hakumuona Sarah kwenye eneo hilo, katika vitu ambavyo vilijua kumchanganya Manka vizuri ni kitendo cha mtoto wake Sarah kupotea, basi hapo alihisi hata akili yake kumruka kabisa na muda huo huo kuondoka hapo na kuanza kumuangalia Sarah ili aone mahali ambapo Sarah ameelekea.
Sia aliondoka ila hata yeye alishangaa jinsi alivyojiamini siku hii na jinsi alivyoweza kumjibu Manka ambaye siku zote alikuwa akimuogopa sana, ila leo aliona kajitoa ufahamu kabisa maana alimjibu bila kujali lolote.
Moja kwa moja, Sia alirudi nyumbani kwake ila alipokuwa akikaribia nyumbani kwake alimuona madam Oliva akiwa kwenye gari yake, alipoangalia vizuri aliona madam Oliva kama amepanda na Sarah kwenye lile gari, Sia akapumua kidogo na kusema,
“Inamaana Oliva kampata mwanae sasa! Sijui ni mwanae kweli au la mmmh!!”
Aliangalia gari la madam Oliva hadi lilipoishia kisha yeye akaenda kuingia nyumbani kwake na kuanza shughuli zake huku akifikiria kama ni kweli madam Oliva ni mama mzazi wa Sarah.

Usiku wa siku hii, baba Angel na mama Angel walikuwa wakipanga mambo mbalimbali chumbani kwao maana kwa siku hii hakuna mtu ambaye alitoka nje ya nyumba yao ukizingatia kwa yale ambayo yalikwisha kutokea kwao, kwahiyo waliamua kuwa makini sana.
“Kwahiyo mke wangu tutakaa nyumbani hadi lini?”
“Hapana, ila tulikuwa tukiangalia upepo, sema kingine ni kutoa taarifa polisi ili iwe rahisi kwetu”
“Kweli kabisa, kesho nitaenda basi ofisini kwa shemeji yangu najua hata siku ile kuna kitu alifanya ila yule inabidi awe anakumbushwa kwa mambo mengi”
“Sawa, ila cha kwanza ni kutoa taarifa polisi ili iwe rahisi”
Walipanga mipango mingi sana kwa siku hii pia.
Kwa hizi siku baba Angel hakutaka kujishughulisha na mambo mengine na kulikuwa na ulinzi mkali nyumbani kwake kwani tayari alishatoa taarifa kuhusu watu wanaomfatilia, na aliweza kugundua ukweli kuwa hajafanya kosa lolote la kuua ila wale watu walihitaji kumtafutia ushahidi, hakuna aliposema kuwa Erick ndio amemuokoa zaidi ya kumwambia mke wake tu maana alijua lazima itaanza kupelelezwa kuwa Erick alitoa wapi ile silaha aliyokuwa nayo.

Angel alilalamika kuwa anaumwa sana na hata hakuwa na hali nzuri kabisa, ikabidi mama Angel amchukue na kwenda nae hospitali.
Walipofika, moja kwa moja alichukuliwa vipimo ila majibu yale yalimfanya mama Angel ahisi hata kuzimia maana aliambiwa kuwa Angel ni mjamzito.
 
SEHEMU YA 403

Walipofika, moja kwa moja alichukuliwa vipimo ila majibu yale yalimfanya mama Angel ahisi hata kuzimia maana aliambiwa kuwa Angel ni mjamzito.
Mama Angel alimuuliza daktari kwa hamaki,
“Una uhakika kuwa mwanangu ni mjamzito?”
“Ndio, mtoto ni mjamzito huyu”
Mama Angel alimuangalia Angel na kumuuliza,
“Unajijua kama wewe ni mjamzito?”
Angel alikaa kimya tu kiasi cha kumfanya mama yake achukie zaidi ila daktari pale alijaribu kumpa ushauri kidogo, sema mama Angel hakuelewa kitu kwakweli na alikuwa hakubaliani na ile hali iliyotokea.
Basi akainuka na Angel kuelekea nae nyumbani huku akiwa kimya tu, moja kwa moja alimshika Angel mkono hadi chumbani kwake kisha akamkalisha na kuanza kuongea nae,
“Kwahiyo Angel, hiyo mimba ni ya nani? Ya Samir?”
Angel aliitikia kwa kichwa tu na kumfanya mama yake azidi kupatwa na hasira, akainuka na kumzabua kofi kisha akamwambia,
“Mtoto mjinga sana wewe, nimekutambulisha baba yako, nimekwambia wazi kuwa huyo Samir ni ndugu yako ila ukaja kunidhalilisha kwa kulala na huyo Samir kwenye nyumba yangu halafu umepewa na mimba na huyo Samir ambaye ni kaka yako. Mbona Angel umekuwa mjinga kiasi hiko wewe!!”
Angel alikuwa kimya tu huku ameinama, mama Angel akaendelea kuongea kwa hasira,
“Jamani sijawahi kuwa na akili mbovu kama za kwako, kupata mwanaume na kumleta nyumbani kwetu tena chumbani kwangu halafu kulala nae humo!! Sijawahi kufanya huo ujinga, umetoa wapi hiyo akili wewe?”
Mama Angel alichukua simu na kumpigia mume wake,
“Baba Angel, asubuhi si niliondoka kumpeleka Angel hospitali sababu ya kujihisi vibaya, sasa majibu ni kuwa ana mimba”
“Ana mimba!!”
“Ndio, tena mimba ya huyo huyo mwendawazimu mwenzie Samir. Ongea na Rahim maana mimi hata sijui cha kufanya muda huu”
Mama Angel alikata simu na kumuangalia tena binti yake kisha alikaa na kuongea nae kwanza,
“Nadhani umefanya mambo sababu hujui historia halisi ya mama yako, hujui ni kwanini mimi nimekuwa na hasira sana ya wewe kukimbilia mapenzi. Binti yangu Angel wewe ni mzuri sana tena sana ila uzuri wako huo utaenda kuharibiwa na hiyo mimba uliyoibeba, baada ya hapo utasikia kwenye mabomba kuhusu swala la kuolewa maana hata huyo Samir hatoweza kukuoa. Licha ya kuwa ni ndugu yako ila ni hulka ya wanaume kuwapa wanawake mimba na kukimbia majukumu. Utalia na hiyo mimba, utakumbuka maneno yangu siku zote ya kukukanya wewe. Usifikirie Junior alipanga kumuoa Vaileth ila ni mimi ndio nilishikilia bango ili Junior amuoe Vaileth, nilimuhurumia sana maana soko lake la ndoa ndio lilizidi kushuka zaidi, sasa wewe mwanangu utafanyaje? Mbona umeenda kujitafutia mkosi na laana tu mwanangu jamani!”
“Nisamehe mama”
“Saizi ndio unakumbuka neno nisamehe ila najua hiyo nisamehe utaiomba maradufu zaidi ya hapa, ngoja nikwambie kwa kifupi tu. Baba yako mzazi huyo Rahim alijifanya kunipenda sana, hakuna mwanamke kama mimi duniani, alifanya nijione wa pekee alinipa chochote nitakacho, nikajitoa kwake kwa kila hali, nikapata mimba yake, ila bado hakuacha kunihudumia ila hakutaka kunitambulisha kwao wala hakutaka kuniona tena, hadi nimejifungua bado hakutaka kuniona, hapo ndio alianza kunifanyia kejeli na karaha akiwa huko huko mbali, yani hataki kuniona na bado ananipa maneno ya kashfa, nilinihisi vibaya, aligoma kuja kujionyesha kwetu na kufikia hatua ya mimi kutukanwa kuwa simjui baba wa mtoto. Nilihudhunika sana, sikuwa na raha nilikuwa nalia kila siku. Alisitisha huduma, kuwa na mimba hutoona tabu sana, balaa huanza zaidi ukijifungua ingawa wengine balaa huanza toka wakiwa na mimba. Sasa malezi ya mtoto mwenyewe utaona nanga inapaa, maisha yetu sisi yalikuwa ya kawaida tu, vingi tulikuwa tukimtegemea mama yetu, yani mamako mkubwa mama Junior ndio alikuwa akinipa msaada sana na mumewe maana kipindi hiko walikuwa na pesa ila kiukweli kwa upande wangu maisha yalikuwa magumu sana. Kipindi kibaya ni pale dada zangu waliponishauri niombe hela ya mtaji nami nikamuomba kweli Rahim, alinipa jibu hilo ambalo liliumiza sana moyo wangu, ni bora angesema sina hiyo pesa kuliko jibu alilonipa. Mwanangu, mapenzi ni matamu sana mkiwa mnaruka ruka hivyo ila ukianza kulea mtoto ndipo utakapoona uchungu wa mapenzi. Tena usiombe ukimbiwe ukiwa na mimba hivyo, na swala la wewe kukimbiwa lipo wazi ukizingatia Samir ni ndugu yako, nakuhurumia sana mwanangu. Ulidhani unatukomesha ila umejikomesha mwenyewe, maana ni wewe ndio utapigwa na maisha na utapambana mwenyewe na maisha yako, utajijua mwenyewe cha kumueleza mtoto wako kuwa baba yako wewe ni kaka yangu nilikuwa nawakomesha wazazi. Yani kila kitu ni juu yako, hujanikomesha mimi wala baba yako maana siku zote kakulea kwa upendo kama mwanae kabisa na hakuna siku uliyoona tofauti ila ulivyomjinga ukaamua kutukomesha, ungesubiri ndoa basi ndio ufanye huo ujinga wako ila kwasasa utajutia nakwambia. Nitaongea tena badae”
Mama Angel aliinuka na kwenda chumbani kwake maana alikuwa akijihisi hasira sana kwa muda huo.

Baba Angel baada ya ile simu ya mke wake, aliamua kumpigia simu Rahim na kuomba kukutana nae kwa siku hiyo ili aweze kuzungumza nae kuhusu swala hilo na wajue cha kufanya.
Walifika walipoahidiana na kukaa hapo kuanza kuzungumza, ambapo baba Angel alimwambia Rahim kuhusu simu aliyopokea kutoka kwa mkewe kuwa Angel ana mimba ya Samir, kwakweli Rahim alichukia sana na kusema,
“Nilijua tu haya mambo ndiomana nikawahi mapema kuwa mniruhusu nitamtambulishe mwanangu kwa ndugu zake, ona sasa ni kitu gani hiki?”
“Rahim, usitoe lawama zisizokuwa na msingi wala nini kwa wakati huu, unajua toka mwanzo ilikuwaje. Usimlaumu yoyote, tuongee tu hapa tujue cha kufanya”
“Sababu umegundua watoto wako wale mapacha wana mahusiano basi unataka na watoto wangu wawe hivyo, kwanini lakini Erick?”
“Nimekwambia usinipe lawama Rahim, tujadiliane kitu cha kufanya hapa. Mimi sina kosa maana mtoto tumemlea vizuri katika mstari ulionyooka”
“Ndio kulea mtoto vizuri huko? Mlijifanya watu wa dini kiko wapi sasa? Mtoto kapata mimba kabla hata ya ndoa, hivi unajua kulea vizuri wewe? Mtoto wa kike anatakiwa kujiheshimu mpaka ndoa, au ndio anajiachia kama mama yake? Ndio shida ya kuzaa na wanawake matahira”
“Rahim, usitake tugombane muda huu. Kama huna cha kujadiliana na mimi kuhusu mtoto ni sawa ila sio kuanza maneno yako ya kashfa kwa mke wangu”
“Hapa sijui kama kuna cha kujadiliana kwakweli, nahisi kuchanganyikiwa tu hapa, kwanza naanza na huyu Samir atanieleza vizuri ujinga wake huo halafu ndio nitajua cha kufanya. Kesho nitakuja huko nyumbani kwako”
“Haya mambo ni makubwa sio ya kuchukulia juu juu kiasi hiko”
“Sitaki hata kukusikiliza Erick, kwaheri”
Rahim aliinuka na kuondoka zake, basi baba Angel hakuwa na namna zaidi ya kuondoka zake tu, ila siku hii aliamua kwanza kwenda kwenye duka lake.
Basi alifika pale na kumkuta Rama kama kawaida, ila leo Rama alianza kuongea nae kwani ni muda mrefu sana baba Angel hakwenda huku dukani,
“Bosi, kuna baba mmoja aliwahi kuja hapa dukani”
“Alikuwa anasemaje? Ni baba gani huyo?”
“Mimi namuamini sana Mwenyezi Mungu, pia naamini kuwa mtoa riziki ni Mwenyezi Mungu, kwakweli sikuweza kukufanyia hii hujuma ingawa waliniahidi faida kubwa sana”
“Hujuma gani tena?”
“Waliniambia kuwa tufanye mpango wa kufilisi hili duka, niondoe hawa walinzi uliowaweka halafu watume watu kama majambazi waje kuvamia siku ambayo utashusha mzigo mpya ili tuweke hasara kwako na wakaniahidi kunipa mimi pesa mara mbili ya mtaji wa hili duka. Nadhani ni watu ambao wanakufahamu vizuri sana kwani wanajua kuwa mimi naelewa siku ya kufika mzigo mpya, walitaka niwaambie ila nikawaambia sijui kitu. Kwakweli mzigo ule ulishuka hapa mwezi uliopita, niliogopa sana kwani nilihisi wanaweza hata kunivamia kweli, ndiomana nimeamua kuongeza ulinzi, naomba msamaha sababu sikukutaarifu mapema”
“Aaaaah Rama, hakuna sababu ya kuniomba msamaha, nakushukuru sana Rama. Nakushukuru sana, nshukuru una hofu ya Mungu, nashukuru sana. Asante Rama”
“Usijali bosi wangu, mimi naridhika na hiki ninachopata, najua kama Mungu atapenda niwe sehemu nyingine basi ataniweka ila sio kwa kutoa hujuma kwa mtu mwingine”
“Yani Rama sijui nikwambie nini nashukuru sana, huhyo baba alikuwaje?”
Rama alianza kumueleza pale na moja kwa moja baba Angel alielewa kuwa yule mtu alikuwa ni ni Moses, yani hata alishindwa kumuelewa huyu mtu kwakweli kiasi cha kumfatilia yeye kama hivyo wakati aliishi nae vizuri kabisa kama ndugu yake.
Aliongea na Rama pale, kisha kuagana nae na kurudi nyumbani kwake.

Usiku wa leo, Angel anaamua kumpigia simu Samir ili kuongea nae kuhusu ile mimba aliyokuwa nayo, ila simu inaita sana bila ya kupokelewa hadi Angel anashangaa kuwa ni kitu gani kimetokea kwa Samir, basi alimpigia kwa mara tatu hizi ndipo Samir alipokea ile simu ya Angel na kuanza kuongea nae,
“Mbona ulikuwa hupokei simu yangu Samir?”
“Aaaah kuna tatizo Angel ndiomana ikawa hivi”
“Tatizo gani?”
“Aaaah acha tu, niambie sasa”
“Samir, mimi nina mimba”
“Duh!! Angel itakuwaje sasa?”
“Itakuwaje kivipi wakati nimekwambia nina mimba”
“Sikia Angel, unakumbuka siku ile tuliyolala pamoja?”
“Nakumbuka ndio”
“Je tuliongelea swala la mimba?”
“Hapana”
“Ndiomana nashangaa na kukuuliza inakuwaje maana mimi na wewe hatujapanga chochote kuhusu mimba”
“Ila si ulisema utanioa Samir?”
“Hivi umeuona moto uliowaka Angel? Baba yangu amekuwa mbogo, yani ninavyokwambia muda huu nimejifungia chumbani kwa mjomba, hali ni mbaya, baba anataka hata kuniua. Nakuomba Angel, usiseme kuwa hiyo mimba ni yangu”
“Kheee una wazimu wewe au? Nisiseme mimba ni yako? Kwahiyo nimejipa mwenyewe hii mimba au kitu gani? Sikuelewi ujue”
“Naelewa jinsi unavyosikia Angel, nakuomba sana hali si shwari kwasasa. Usiseme kuwa mimba ni yangu, yani mimi sielewi hapa, sielewi kabisa. Angel naomba unisamehe sana kwa hili ila mimi nitakukana kwakweli”
Halafu Samir alikata ile simu na kumfanya Angel kutokuelewa kitu chochote, hapo ndio alianza kujiwa na maneno ya mama yake kuwa mtu anaweza kukuachia ujauzito na badae kukukana kuwa ile mimba sio yake, alijihisi vibaya na kuanza kulia, alilia sana na mwishowe alijikuta akilala chini ya sakafu huku akilia, hapo aliona kila alichoambiwa na mama yake kikianza kuonekana mapema kabisa.

Baba Angel na mama Angel walianza kuongea kuhusu cha kufanya na binti yao, kisha baba Angel akamwambia mkewe,
“Ila mimi naona kama tumeharakisha sana kumwambia Rahim?”
“Hapana, anatakiwa ajue, ni vyema ingekuwa ni mimba ya mtu mwingine ila sio mimba ya kijana wake”
Muda huo huo kuna ujumbe uliingia kwenye simu ya mama Angel, alipoangalia aliona ni namba ya Rahim, basi akafungua ule ujumbe na kuusoma,
“Mkishamaliza ya mwanangu, mwende mkampime na huyo Erica wenu mimba pia. Kesho nakuja kumchukua mwanangu”
Mama Angel alitazamana na mumewe na kumwambia kuhusu ule ujumbe, kisha mumewe akasema,
“Nilikwambia mke wangu kuwa tumeharakisha kuhusu hili jambo. Akili za Rahim nadhani unazijua vizuri sana zilivyo, huyu mtoto ni kweli kafanya makosa ila haitakiwi kumburuza kwa kiasi hiki maana hata sisi wazazi tuna makosa pia”
“Sasa tutafanyaje?”
“Kesho asubuhi nitaondoka na Angel, nitampeleka kwa mama yangu kule ila sitamwambia ukweli kuwa Angel ni mjamzito na hata Angel nitamwambia afiche hilo huku sisi tukijipanga cha kufanya”
“Halafu wewe ndio umefuga ubovu kwa huyu mtoto, umefanya Angel afanye ujinga kwa kujiamini sana kwani muda wote anaamini kuwa baba yake upo na utamtetea”
“Nilisema toka mwanzo, nitampenda Angel, nitamlinda na kumthamini, nitakuwa nae bega kwa bega, nitakuwa kama baba yake. Nimemlea mwenyewe na kaharibika kwenye mikono yangu mwenyewe, natakiwa nijue cha kufanya, sitoamuacha Angel aende kuadhibiwa na mtu asiyejua uchungu wa Angel, mimi mlezi ndio naujua uchungu wa Angel, najua ni wapi nimepita nae hadi kumfikisha alipo. Mama Angel niache tu nifanye nitakavyo, kama Angel kaharibika kwenye mikono yangu basi niache nifanye kile ninachoona sahihi kwasasa, haiwezekani Rahim aje kumchukua mtoto kwa wakati huu, tutaongea kwanza tujue jinsi ya kusuluhisha haya ndio atakuwa na nafasi ya kuzungumza na mtoto”
Mama Angel hakutaka kumbishia sana mume wake, ila alichopanga kwa muda huo ni kuwa pakikucha aende na Erica hospitali kwaajili ya kumpima ujauzito.

Kulivyokucha, mama Angel alimchukua Erica na kwenda nae hospitali kama alivyopanga kwenda nae, ila walipima na kukuta Erica hana mimba, basi mama Angel aliridhika na kurudi nyumbani ambapo muda huu Angel na baba yake waliondoka pamoja na Erick, kwahiyo ambavyo hakuwakuta nyumbani alijua ni lazima tu wameondoka na mtoto mdogo Ester.
Basi Erica aliamua kumuuliza mama yake,
“Ila mama, kwanini uliamua kwenda kunipima mimba?”
“Mmmmh Erica naomba unisikilize mwanangu, kitu ambacho mlifanya wewe na kaka yako sio kitu kizuri kabisa, na msirudie tena maana mtatutia aibu wazazi wenu”
“Ila mama sijafanya kitu na Erick”
“Hebu kwenda huko, watu mmechunguliana na kuachana watupu kabisa halafu unasema hamjafanya kitu? Mimi usinione naongea hapa, naongea huku nina maumivu sana najikaza tu. Kwanza najiuliza maswali mengi tu bila ya majibu, aliyekufundisha kufanya kile ulichomfanyia kaka yako ni nani?”
“Ni kwenye video mama, halafu….”
“Weeee hebu nyamaza huko, hivi unaona ni kitendo kizuri hiko hata kuweza kunielezea kwa uhuru kabisa? Hawa wanawapaga dawa na machizi, wameniharibia kabisa watoto mweeeh!!”
Mama Angel alimtaka Erica kwenda kuandaa chakula tu, kisha yeye alienda zake ndani kwake.

Baba Angel wakati anaondoka na Angel, walienda na kumuacha Erick kiwandani kisha baba Angel alifanya safari ya kwenda na Angel kwa bibi yake huku Angel akiwa amempakata mdogo wake Ester kwa muda huo,
“Sasa baba wakati wa kurudi huyu Ester atashikwa na nani?”
“Aaaah huyu nitamfunga kwenye kiti chake, hakuna tatizo”
“Halafu baba, huko nitaenda kuishi kwa muda gani?”
“Mpaka pale tatizo litakapoisha”
“Baba, kwanini unanipenda sana? Mama hanipendi, ananionyesha baba mwingine ila wewe baba hujawahi kunionyesha mama mwingine, unanipenda sana baba yangu.”
“Usijali, ila usimwambie bibi ukweli kuhusu swala lako la kuwa na mimba”
Walifika hadi kwa bibi Angel ambapo baba Angel alimuacha Angel mahali hapo na kuondoka na Ester, kwahiyo alimpigia tu mama yake simu ili kumpa taarifa kuwa kamuacha Angel pale nyumbani kwake.
Basi baba Angel alikuwa akirudi na Ester, ila alipomuangalia huyu mtoto aligundua kuwa muda huu atakuwa na njaa na ukizingatia kule kwa bibi yake ni safari ndefu, aliamua kupitia kwenye hoteli moja na kusimama pale kwaajili aweze kumuagizia Ester hata mtori ampe halafu ndio aendelee na safari ya kurudi nae, na yeye aweze kula chochote kile kitakachopatikana.
Akiwa pale hotelini na mtoto wake, ndipo alipomuona tena Jack ambaye alienda na kumsalimia,
“Kheee Erick, unalea mwenyewe!! Mkeo yuko wapi?”
“Aaaah kuna mahali nilienda na mtoto, ndiomana muda huu nimeamua nipite nae hapa niweze kumlisha”
“Tena vizuri nimekuona tena, huwezi amini napiga simu zako sizipati hewani, swala lililokuwepo hapa ni wewe kumuona mwanao”
Yule Jack aliinuka, na pale mtori ulifika na baba Angel alianza kumlisha mtoto wake.
Baada ya muda, Jack alirudi akiwa ameongozana na kijana mkubwa kabisa na kumwambia baba Angel,
“Huyu hapa kijana wako”
Baba Angel alishtuka kwanza na kumwambia Jack,
“Khaaa mbona mtoto kafanana na Rahim?”
Hapo hata Jack alishtuka pia,
“Rahim? Ndio nani?”
“Kuna rafiki yangu mmoja anaitwa Rahim, inamaana Jack humfahamu huyo Rahim? Yani huyu mtoto ni Rahim mtupu, nikikuletea hapa huwezi kubisha hata kidogo, huyu ni mtoto wake”
“Wewe Erick una wazimu au ni kitu gani? Huyo Rahim simfahamu mimi, huyu ni mtoto nimezaa na wewe”
“Kwani mimi nimekataa? Ila naomba siku nikukutanishe na huyo Rahim halafu wewe mwenyewe utasema ukweli kuhusu baba wa mtoto”
Hata kijana yule alichukia kwani aliinuka na kuondoka zake, basi Jack alimsonya baba Angel na kumfata mtoto wake na kumfanya baba Angel aongee mwenyewe,
“Yani ndio huyu mwanamke alitaka kunigombanisha na mke wangu, azae na Rahim huko halafu aniletee mtoto mimi. Anajifanya Rahim hamfahamu loh!! Aende zake huko, akinitafuta nitampeleka kwa Rahim, kajiongezea mtoto mwingine wa kiume. Huyu Rahim loh!! Hapana kwakweli”
Baba Angel aliendelea kumlisha mwane, alipomaliza, Jack alimfata tena na kumpa baba Angel namba zake za simu kisha akamwambia,
“Namba zangu hizo, ukipenda nitafute usipopenda potezea”
Halafu Jack akaondoka zake, zile namba baba Angel akaziweka vizuri na kuondoka zake moja kwa moja alielekea kwenye gari lake na kwenda nyumbani kwake.

Kwakweli mama Junior hili swala la Junior na Daima lilikuwa likimuumiza sana kichwa, kwahiyo jioni ya leo aliamua kumuita mwanae Junior na kuongea nae kuhusu Daima ukizingatia ukweli ni kuwa aliona ujumbe wa Daima kwenye simu ya junior,
“Hivi wewe Junior mwanangu unataka nini lakini? Yote yanayotokea hayakufunzi akili? Huyu mwanamke anakupenda ila wewe masikio na macho juu juu kwenda kuwatafuta tena wakina Daima, una nini lakini?”
“Hamna kitu mama”
“Haya, kwanini unaenda kukutana tena na Daima hadi umempa tena mimba?”
Junior alimshangaa mama yake na kusema,
“Mama, sijakutana na Daima tangu nimeoa”
“Mjinga wewe, na mimba aliyobeba ya nani?”
“Kwani Daima ana mimba? Mimi sijui kama Daima ana mimba”
“Unanifanya mimi mtoto eeeh!! Hebu mpigie hapo Daima nisikie, na uweke sauti kubwa na uongee nae maongezi ya kawaida ili nijue kama kweli hamjaonana toka ufunge ndoa”
Junior alipiga simu na kuweka sauti kubwa ili mama yake apate kusikia,
“Daima, niambie Daima”
“Nimekumiss tu Junior”
“Hivi hatujaonana siku nyingi eeeh!!”
“Ndio, halafu tuliongea vizuri siku ile nikakutumia ujumbe ila hukujibu”
“Ujumbe gani?”
“Mjinga wewe, sijui mke wako anakukataza kuongea na simu loh!! Mjinga sana wewe”
“Usijali, tutaonana tu. Ila kuna mtu kaniambia kuwa una mimba”
“Mimba? Nani ana mimba? Hiyo mimba nibebe ya nani? Mimi nangoja wewe ndio unipe mimba nyingine”
Basi Junior alikata ile simu na kumuangalia mama yake ila mama yake akamwambia,
“Niondolee upuuzi wako mimi, unaongea ujinga hata hufikirii kama ni mbele ya mama yako”
“Ila mama, kosa langu hapo ni nini?”
“Hebu nenda weee, usinichanganye mie”
Junior aliachana na mama yake tu na kwenda kufanya mambo mengine.

Kwa zile siku chache tu ambazo Sarah ameishi na madam Oliva, aliweza kuzoeana vizuri sana na Paul, na aliweza kugundua kuwa Paul anampenda ila yeye alikuwa akijigelesha juu ya Paul yani hakutaka kuonyesha kuwa na yeye kavutiwa nae.
Kwa upande mwingine aliona kuendelea kuishi hapo kwa madam Oliva kunaweza kupelekea yeye akaangukia kwenye mapenzi na Paul na hakutaka jambo hilo litokee, hakutaka kufanya kosa tena alilofanya na Elly.
Basi ule usiku aliamua kuongea na madam Oliva kuhusu yeye kurudi kwa mama Angel,
“Samahani madam, mimi kabla ya mama yangu kunichukua nilikuwa nikiishi kwa mama Erick, nitafurahi nikienda kuishi tena huko”
“Unampenda sana mama Erick eeeh!!”
“Ndio nampenda sana”
“Halafu umefanana nae balaa, kamavile wewe ni mwanae”
“Watu wengi wakiniona huwa wananifananisha nae, ila yeye mama Erick husema mimi ni mtoto wa ndugu yake Derrick”
Hapo madam Oliva alishangaa kidogo, kitu ambacho huyu madam alikuwa hajui ni kuwa Manka ndio mama wa Sarah, alikuwa hajui kuwa Manka ndio anahusika pia na ile shule anayofundisha yeye, alichokuwa akijua ni kuwa baba mzazi wa Sarah alishakufa na alikuwa ni tajiri sana, basi alimuangalia vizuri Sarah na kumuuliza,
“Kwani wewe, mama yako ni nani?”
“Mama yangu anaitwa Manka”
Hapa madam Oliva alishtuka pia, alimuangalia Sarah vizuri na kusema,
“Mbona hufanani nae, unaonekana kuwa mtoto mpole, mcheshi na msikivu, huyo Manka hufanani nae hata kidogo. Kwahiyo kuhusu ile shule na mama yako nae anasimamia?”
“Ndio, mama anasimamia pia ile shule ila tu huwa anaenda pale mara chache chache sana, nadhani wengi hawamfahamu kama anahusika pale. Mama aliacha nifahamike mimi sababu mimi ndio mmiliki wa ile shule”
“Mmmmh!!”
Madam Oliva alipumua kwanza na kumuuliza tena Sarah,
“Unataka kwenda lini huko kwa mama Erick?”
“Hata kesho”
“Basi kesho nitakupeleka hakuna tatizo”
Sarah alikubaliana na madam Oliva kuwa kesho yake atampeleka kwa mama Angel.

Usiku huu ndipo mama Angel anaamua kumwambia mumewe kuhusu kitu ambacho Rahim amefika kusema akiwa pale kwao,
“Yani Rahim kaja hapa na amefoka hatari, kasema anatupa siku mbili tu na Angel awe hapa au tumpeleke kule kwake”
“Khaaa ana wazimu huyo Rahim au kitu gani? Kwanza yeye ni baba mzazi tu ila hajui malezi yoyote aliyoyapata Angel, aache nipambane mwenyewe na Angel wangu. Kama aibu hata mimi nimepata aibu vilevile ila najaribu kuangalia swala hili tunalichukuliaje na sio swala la kuanza kuropoka tu bila kufikiria. Asinitishie hata kidogo”
“Yani alivyokuja amechukia, kwa hakika mume wangu usingeweza hata kumjibu yani alikuwa na hasira hatari”
“Pole sana, huyo Rahim nitashughulika nae mwenyewe. Halafu kitu kingine mke wangu tujue kuwa tuna mtoto bondia maana toka siku ile namvulia kofia Erick, kwahiyo hakuna wa kuja kubabaisha hii familia”
Mama Angel akaguna tu, basi ujumbe uliingia kwenye simu ya mama Angel, alipoangalia aliona ni namba ya Sia basi akafungua na kuusoma,
“Kesho nitakuja, kuna jambo nataka kuwaambia. Mwambie mumeo asiondoke, maana nahitaji niwakute wote”
Mama Angel alipomaliza kuusoma akamwambia mumewe,
“Ujumbe wako huu!”
“Aaaah huyu nae, mimi kesho kuna sehemu ya muhimu sana natakiwa kuwepo. Nitamngoja hadi saa mbili, nispomuona naondoka zangu, huo ujumbe nitaukuta kwako”
Kwa muda huo waliamua tu kulala.

Leo madam Oliva alijiandaa pamoja na Sarah na Paul maana alitaka kujua ni wapi ambapo Sarah anapelekwa, basi waliondoka kwa pamoja na kuanza kuelekea kwa mama Angel.
Walifika, muda huu mama Angel alikuwepo kwenye kibaraza cha nyumba yao amekaa tu, kwahiyo alivyowaona aliwakaribisha pale ila hata yeye alishangaa kidogo kwani hakujua kama Sarah angekuwa kwa madam Oliva.
Muda kidogo aliingia Sia, ambaye alisogea karibu yao, aliwaangalia kwa muda bila salamu na kusema,
“Bora Oliva umejiongeza kwa kuniletea mwanangu Paul halafu wewe ubaki na mwanao Sarah”
Madam Oliva alimuangalia akimshangaa kwakweli.
 
SEHEMU YA 406



Baba Angel alimuita Samir na kwenda nae kwenye bustani na kuzungumza nae kuhusu Angel na kuhusu kile kinachoendelea,
“Kwani wewe Samir umemtumia ujumbe gani baba yako?”
“Nilimtumia kuwa nahitaji kumuoa Angel”
“Kwanini sasa umemtumia ujumbe huo?”
“Sababu Angel analalamika kila muda kuwa mimi nilikuwa kumdanganya ila mimi sikuwa nikimdanganya Angel maana ninampenda kweli”
“Je, hujaambiwa na baba yako kuwa Angel ni ndugu yako?”
“Yani baba yangu kila leo anatutambulisha mtoto mpya nadhani hadi sasa haijuilikani idadi kamili ya watoto wake, halafu ndio aseme mimi dada yangu Angel? Hilo nimekataa”
“Sikia Samir nikwambie kitu, Angel ni dada yako yani hili lipo wazi kabisa kuwa Angel ni dada yako na ulitakiwa kuwa makina nae vizuri sana”
“Nilikuwa tayari nishampenda na yeye alikuwa tayari ananipenda, yani sijui kama naweza kuvumilia kwa kumuangalia Angel akiwa na mwanaume mwingine”
Baba Angel alisikitika na kumuuliza tena,
“Unahisi kwanini mimi nimekusaidia?”
“Ni sababu ya moyo wa huruma uliokuwa nao, hata Angel aliuwahi kuniambia hivi. Nakumbuka nilimwambia kuwa natamani ungekuwa ni baba yangu mzazi, kwanza una moyo wa huruma na pili ni mwerewa”
“Basi naomba nikuombe kitu”
“Niambie tu”
“Naomba kwasasa muone Angel kama dada yako, muone kamavile umezaliwa nae tumbo moja yani baba na mama mmoja. Wakati mimi najaribu kuweka mambo sawa, tulia nirekebishe kwanza halafu nijue hatma yako na hatma ya mwanangu Angel”
Samir hakumbishia kabisa baba Angel kwani huyu baba Alionekana kuwa na roho ya tofauti sana.

Usiku huu mama Angel hakuridhika na kuanza kumlalamikia mume wake kuhusu kumruhusu Samir kuishi hapo kwao,
“Kwakweli baba Angel nashindwa kukuelewa jamani, umewezaje kufanya kitu cha namna hii?”
“Kwani tatizo ni nini mke wangu?”
“Kwahiyo huoni tatizo kabisa hapa, yani mtu kampa binti yetu mimba halafu unamchukua huyo mtu na kumkaribisha ndani kwetu jamani!!”
“Hivi mama Nagel nilikuuliza asubuhi, kwani huyu Samir alimbaka Angel? Ni wapi ulipowakuta pamoja? Si uliwakuta wamelala wote! Ingekuwa nyumba yetu ya hovyohovyo basi tungesema Samir alikuja na kumshawishi Angel, ila ni wazi kuwa Angel alimuita Samir kwa matakwa yake mwenyewe. Kwanini utake kumuhukumu huyu kijana?”
“Najua huna uchungu, sababu Angel sio mtoto wako”
“Mama Angel, usitake tugombane sababu ya ujinga. Lini nimesema vibaya juu ya Angel? Nilimpenda na bado ninampenda kama mzazi wake, pia najaribu kuokoa hili jahazi, haya hayo mambo ya kusema nafanya hivi sababu Angel sio mtoto wangu yanatoka wapi? Uliona wapi mwanaume ambaye anaishi na mtoto sio wake na anajua ila akampenda kama ambavyo mimi nampenda Angel? Nimemuandikisha mali zangu Angel ila nikijua wazi kuwa sio damu yangu, unawezaje kusema kuwa nafanya hivi sababu Angel sio mwanangu? Mimi najaribu kuangalia hali halisi ilivyo na jinsi ya kufanya ili tuweze kutatua hili”
“Kwahiyo kulitatua ni kumchukua muhalifu na kumkalisha ndani ya nyumba?”
Mara simu ya baba Angel ilianza kuita, ambapo baba Angel aliichukua na kuanza kuongea nayo, moja kwa moja alijua wazi anayeongea na Rahim sababu alianza kwa kumtusi tena alimtusi sana huku akimsema vibaya,
“Unajua Rahim, hebu kuwa na heshima basi”
“Heshima unaijua wewe? Kilichokufanya kumchukua huyo Samir ni kitu gani?”
“Nisingeweza kuvumilia wewe umpige Samir au umuue mbele yangu, kwa kosa gani alilolifanya?”
“Kwahiyo huoni kama kosa la kumpa mimba Angel ni kosa kubwa sana?”
“Yani wewe huyu Samir ni mwanao au sio mwanao?”
“Toto linamaudhi sana hilo hujui tu, mimi nalifundisha halafu linaniambia intake au nisitake lazima yeye amuoe Angel”
“Sasa sio swala la kuchukia hivyo, ni kweli Samir kampa mimba Angel ila wote wawili wana makosa hapa.Na pia sisi wazazi tuna makosa pia maana watoto hawakujua ukweli mapema”
“Weee makosa unayo mwenyewe, toto hilo kabla halijaharibu mambo nimeliambia kuwa Angel ni dada yake, halafu limeenda kufanya ujinga. Limenitia aibu sana, sasa huyo mtoto wao ataniita mimi nani?”
“Atakuita babu, hebu acha maneno mengi sana Rahim, nisikilize kwanza, acha kuropoka utafikiri una matatizo ya kinywa. Angel ni mtoto wetu na Samir ni mtoto wetu, tunatakiwa kukaa chini na kuyazungumza haya na sio kufanya hasira tu”
“Huna uchungu na Angel wewe, ndiomana ulikuwa unamtaka”
“Khaaa yani mimi nilikuwa namtaka Angel!! Ndio shukrani yako hii kwangu?”
“Shukrani gani nikupe mjinga kama wewe usiyejua kulea, mapenzi gani ya baba na mtoto hayo unayompa Angel kiasi hata baba yake mzazi hamtaki? Na usikute hiyo mimba wewe na Samir mmeshirikiana ndiomana unamtetea”
Baba Angel alichukia sana na kuamua kukata simu na kuizima kabisa, kwa muda huu hakutaka hata kuzungumza na mke wake kwani aliamua tu kulala basi kwani na muda ulishaenda.

Asubuhi na mapema, baba Angel anaondoka nyumbani kwake na kuelekea ofisini kama kawaida, alipanga kwenda kumuona Angel ila alijikuta akiahirisha tu ile safari kwa siku hiyo.
Mama Angel alitoka ndani muda huu na kukuta mezani wapo watu watatu wakinywa chai, Erica, Sarah na Samir yani Erick alikuwa ameondoka.
Basi mama Angel aliwafata karibu na kusema,
“Aliyewaambia make karibu na huyu ni nani?”
Erica alijibu na kusema,
“Hamna mtu mama ila baba katutambulisha kuwa huyu tumtambue kama kaka yetu”
“Kaka yenu wa wapi huyo ni mbakaji, halafu wewe Samir usiniletee ujinga kwneye nyumba yangu kabisa, kaa mbali na watoto wangu usije ukawabaka bure”
Samir alinyong’onyea sana na kutaka kuinuka ila Erica alimshika mkono kuwa akae, basi mama yao aliondoka na Erica akamwambia Samir,
“Usichukie, sijui ni kitu gani kimemkumba mama, huwa hayupo hivi. Ukimzoea utampenda, hana roho mbaya kiasi hiki mama yetu”
Sarah nae akaongezea,
“Ni kweli hana roho mbaya, ukimzoea utampenda tu, itakuwa kuna upepo mchafu umempitia. Jisikie huru”
Basi jambo lile lilimfanya Samir sasa akae vizuri bila kujali kuwa ni maneno gani mama Angel ametoka kuyasema muda mfupi uliopita, alikunywa chai na wakina Erica pale na walipomaliza walikaa nae na kuanza kuzungumza nae, hadi Samir alijikuta akifurahia maana aliwaona hawa wawili kuwa ni wacheshi sana, ukizingatia Sarah alipenda sana kuongea ndio kitu kilichomfanya Samir afurahi zaidi halafu Erica nae alikuwa ni mtu wa kumzoea mtu mwingine haraka zaidi.

Baba Angel akiwa ofisini kwake akiendelea na mambo yake, ndipo kwa muda huu alipofika madam Oliva mule ofisini kwa baba Angel na kuanza kuongea nae kuhusu aliyoyapata kwa dokta Jimmy.
Alikaa na kumuelezea kila kitu ambacho kimetokea,
“Kheee kwahiyo dokta Jimmy ana mtoto wako?”
“Ndio, mjinga yule kampa mwanangu mjina wake jamani, nimechukia sana”
“Pole sana, kwahiyo anasemaje huyo dokta feki”
“Anasema kuwa yupo tayari kumueleza kila mtu kila kitu kilichotokea.”
“Vipi kuhusu wazazi wa Sarah?”
“Hajaniweka wazi ila nina uhakika asilimia mia moja kuwa Sarah sio mtoto wa Manka, lazima kuna namna ilifanyika na dokta Jimmy anajua kila kitu sema alichofanya ni kumdanganya”
“Dokta Jimmy alinipigia simu kuwa anataka kuniambia ukweli kuhusu watoto wangu”
“Ungekutana nae kumsikiliza, lazima lipo la maana analotaka kuongea na wewe maana kwa jinsi nilivyomsema lazima anataka kukwambia ukweli tu”
“Basi huo ukweli napenda uwepo na wewe ndio auseme maana siwezi kuusikiliza peke yangu, haaminiki yule dokta”
“Pole sana, basi tutaenda wote. Muulize ni wapi anahitaji kuonana na wewe ili aseme ukweli halafu tutaenda wote”
“Sawa ngoja nimpigie muda huu nimuulize alipo”
Baba Angel alichukua simu na kumpigia dokta Jimmy ambapo baada ya muda kidogo tu dokta Jimmy alipokea simu ile na kuanza kuongea nae,
“Erick, upo tayari kuongea na mimi?”
“Ndio nipo tayari”
“Chagua sehemu ambayo tutaweza kuzungumza”
“Sijui, hata nyumbani kwangu”
“Hapana, ni vizuri ikiwa kwenye kaburi la mzee Jimmy maana haya mambo ni yeye ndio aliyoyafanya”
“Duh!! Kwahiyo lini tutazungumza hayo?”
“Nipe wiki moja, ni vizuri ukija wewe na mke wako maana nina mengi ya kuongea nanyi wawili”
“Sawa, nimekubali”
Ile simu ilikatika, kisha baba Angel aliongea na madam Oliva,
“Natumaini umesikia, kwahiyo tutaenda wote eeeh!”
“Ndio, usijali, tutaenda wote, najua ni wapi pa kumkomeshea dokta Jimmy hadi atasema ukweli”
Basi madam Oliva aliagana na baba Angel pale halafu akaondoka zake kwa muda huo.

Erick alipotoka kiwandani, moja kwa moja aliamua kupitia kwenye duka la baba yake, na alipofika alimuona mtu pale dukani akizungumza na Rama, alipata hisia mbaya kuhusu yule mtu. Ila hakutaka kujitokeza kati yao, badala yake yule mtu alivyoondoka ndipo Erick alipoamua kumfatilia na aliweza kumfatilia hadi nyumbani kwake huyo mtu, kisha alimfata wakati akitaka kuingia ndani, yule mtu alishangaa sana kumuona yule kijana, halafu Erick alimsogelea huyu baba na kumkaba kisha akamuuliza,
“Ulienda kufanya nini pale dukani?”
“Wapi tena jamani wapi?”
“Mjinga wewe hujui ulipotoka au? Kwanza unaitwa nani?”
“Naitwa Moses”
“Haya, pale dukani ulienda kufanya nini?”
Moses alimuangalia huyu Erick ambaye ni kijana mdogo ila muda ule alionekana kujawa na misuli katika mwili wake, alionekana kuwa na nguvu sana tena ngu za ajabu mno.
Basi kwa wasiwasi Moses alijikuta akijielezea,
“Aaaah mimi nilienda kununua bidhaa pale”
Erick alimshushia ngumi moja ya shavu kiasi cha kumfanya Moses damu zianze kumtoka mdomoni, na hapo Moses alianza kumuogopa zaidi huyu Erick, basi akamwambia kwa woga,
“Naomba unisamehe sana”
Erick alimpiga mtama Moses na kumuangusha chini, basi Moses alianza kusema,
“Mimi ni sawa na umri kama baba yako”
“Unamjua baba yangu wewe?”
“Aaaah hapana lakini wewe ni kama kijana wangu”
“Sasa sikia nikwambie kitu, leo iwe mwisho na mwanzo wa wewe kwenda dukani kwangu tena, lile ni duka langu kama ulikuwa hujui. Nasema hivi, leo iwe mwanzo na mwisho, kama hujupendi jua nitakupa ukilema, mimi sitakuua bali nitakupa ukilema ili ukae ndani bila kutembea. Jina langu ni Erick, na mali zozote za mtu anayeitwa Erick uzione kama ukoma. Mjinga wewe umefanana na yule mjinga mwenzio”
Kisha Erick alimpiga teke Moses ambaye alijikuta akiangukia karibu na geti lake halafu Erick akaondoka zake kwa muda huo.
Kwakweli Moses hakuelewa kitu chochote, alihisi akili yake kutokupata nafuu kabisa.

Erick alipotoka hapo alipitia tena dukani ambapo Rama alikuwa tayari kashafunga kisha Erick alirudi nyumbani kwao ambapo alimkuta mama yake akiwa na mashaka maana Erick amechelewa sana kurudi kwa siku hii.
“Jamani mwanangu, mbona umechelewa hivi?”
“Nilipita dukani mama”
“Ulikuwa unasubiri wafunge duka au?”
“Ndio mama”
“Siku nyingine uwe unasema, yani hapa umenifanya roho iwe juu juu hatari”
Basi mama Angel alimuandalia mwanae chakula ambapo Erick alikula kidogo kile chakula ili kumridhisha mama yake na kisha kwenda chumbani kwake kupumzika maana bado alikuwa na hasira kiasi ila mama Angel hakuweza kwa haraka kumgundua mtoto wake kwani hajawahi kumuona vizuri akiwa amepandisha hasira.
Erick alipokuwa chumbani kwake tu, muda kidogo alienda Erica na kumwambia,
“Nimesikia kuwa umerudi, mbona leo umechelewa sana? Halafu unaonekana umefura kwa hasira, hivi umeweza kula kweli leo?”
“Nimekula ndio”
“Hapana Erick, mimi nakufahamu vizuri sana. Niambie tatizo ni nini pacha wangu?”
“Niite mpenzi wangu ndio nikwambie”
Erica alimpiga kibao kidogo mgongoni Erick ili asiendelee na utani ule, ila Erick alicheka tu kwa kile kibao kisha Erica alimwambia,
“Najua sasa ni kwanini umesema hivyo?”
“Kwanini?”
“Ushakorofisha huko, yani hapo akili ishakuruka”
“Hata nahisi kuwa sitaweza kulala peke yangu leo, tunaweza kulala wote Erica?”
“Kwa yale maswahibu yaliyotokea hadi mama ananishika na kwenda kunipima mimba halafu tulale wote!! Hapana Erick, jikaze ulale mwenyewe tu, au njoo chumbani tulale pamoja yani mimi, wewe na Sarah”
Erick alikubali hilo pia maana alijiona kuwa na hasira sana na hakuhisi kama angeweza kulala mwenyewe kwa hasira zile alizokuwa nazo.
 
SEHEMU YA 407


Kulipokucha kwa siku ya leo, baba Angel aliongea na mkewe kwa kifupi tu kuhusu alichoongea na madam Oliva maana usiku wake hakumwambia kitu kisha akamwambia kuwa kesho ataenda kumuona Angel.
“Kwahiyo tutaenda wote kwa huyo dokta Jimmy?”
“Ndio, inabidi twende wote, kwahiyo inabidi twende wote tukamsikilize”
“Sawa nimekuelewa, ngoja nikawaamshe wakina Erica waje kufanya usafi”
Baba Angel aliondoka zake, halafu mama Angel moja kwa moja alienda chumbani kwakina Erica na kukuta wamelala wote watatu, kwakweli alisikitika sana yani zile dawa ambazo mzee Jimmy aliwapa watoto hawa bado hakuzielewa, inamaana hapo asingekuwepo Sarah basi wangekuwa wamelala watu wawili tu ambao ni tatizo zaidi.
Basi mama Angel aliwaamsha pale ambapo moja kwa moja Erick aliinuka na kuelekea chumbani kwake huku mama yake akisikitika tu, halafu akawaambia wakina Erica wakafanye usafi.
Mama Angel alitoka nje ya nyumba na kumkuta Samir akipalilia maua ya pale nyumbani kwao, basi alimuangalia na kumsogelea ambapo Samir alimsalimia mama Angel, naye aliitikia kisha alianza kumuuliza Samir,
“Umemfahamu kipindi gani baba yako Rahim?”
“Nikiwa na miaka mitano, wakati huo mdogo wangu alikuwa na mwaka mmoja”
“Yani ilikuwaje? Mama yako alikuzaa kabla ya ndoa?”
“Ndio, mimi nilizaliwa nje ya ndoa hata mdogo wangu ni hivyo hivyo ila badae baba aliamua kumuoa mama, na hapo tukawa watoto wa familia moja”
“Mamako anampenda sana baba yako eeeh!!”
“Eeeeh anampenda ila mama huwa anasema baba alimtendea kitu kibaya sana, huwa hataki kukisema ila najua ni kitu kibaya sana. Sitaki kitokee kwenye familia yangu pia”
“Swala la wewe kuwa na Angel, mama yako analichukuliaje?”
“Tatizo mama yangu muda wote yupo kwenye kazi, ila mama yangu hajachukia kabisa mimi kuwa na Angel. Mwanzoni alichukia baada ya kujua kuwa Angel anaitwa Angel Erick, ila badae alivyogundua kuwa Angel ni mtoto wa baba alifurahi na yeye ndio aliniambia kuwa nikaishi kwa mjomba na kunipa baraka zote, kabla sijamtumia ujumbe baba kuwa nahitaji kumuoa Angel, ni mama aliniambia kuwa baba asinibabaishe natakiwa kusimamia msimamo wangu”
“Mmmmh!! Mama yao hajafikiria madhara ya wewe kufunga ndoa na dada yako?”
“Mama anasema sio mbaya, yani mama kabariki hili swala kwa baraka zote ni baba tu ndio ataki”
Hapo mama Angel akaelewa wazi lazima kuna tatizo kati ya Rahim na mke wake ndiomana mke wa Rahim anaona kawaida, labda anataka kumkomesha mumewe bila kujali athari watakazozipata watoto. Ila siku hii mama Angel hakuongea vibaya na Samir, hata Samir alimshangaa jinsi huyu mama alivyobadilika gafla vile.

Baba Angel akiwa ofisini kwake huku akiendelea na kazi zake, muda huu anapigiwa simu na namba ngeni na kuipokea,
“Ni Moses anaongea hapa”
“Unasemaje Moses”
“Kwakweli hapa ninavyoongea na wewe nipo kitandani, mbavu zote zinaniuma yani naumwa sana”
“Mmmmh!!”
Baba Angel aliguna tu sababu kwa kpindi hiko Moses alikuwa ni adui yake namba moja ukizingatia kwa mambo ambayo Moses ameyafanya na jinsi alivyoambiwa na Rama, basi Moses aliendelea kuongea,
“Kwakweli Erick sijui ulimtuma kijana wako anifatilie sijui ni kitu gani, ila kanifatilia jana halafu kanipiga sana. Hivi yule mtoto ni mtu au ni mzimu?”
“Unamuongelea nani?”
“Namuongelea Erick, yani nimepigwa mimi jana na kijana wako hatari. Kanipiga sana, hapa taya linauma, na mgongo unauma, mbavu zote zinaniuma, nilitaka nikupigia simu siku ya jana ila sikuweza maana nilikuwa na hali mbaya sana”
“Mmmmh mwanangu ndio kafanya hivyo!!”
“Ndio, yani kanipiga sana. Inamaana hujui kitu? Erick, kwani mwanao umeenda kumfundisha kareti au kitu gani? Umemfundisha mtoto wako ubondia? Mbona amekuwa hivi? Dah kanipiga sana”
Baba Angel hakusema kitu maana hata kutoa pole alishindwa ukizingatia akikumbuka jinsi Moses alivyompiga risasi zile zilizomfanya asifanye chochote kwa mwaka mzima, basi alimsikiliza tu mpaka Moses alipokata simu.
Kisha baba Angel alijiuliza juu ya mtoto wake Erick,
“Katoa wapi hizo nguvu Erick? Hata kile kitendo chake cha kuniokoa mimi kilinishangaza sana maana nilimuona mwanangu akiwa amebadilika na mwili wake wote ukijaa misuli kama mtu wa mazoezi mazito, katoa wapi hizo nguvu?”
Baba Angel akapanga kuwa akirudi nyumbani aende kumuuliza mwanae vizuri, ila muda huo akapigiwa simu na mama yake na kupokea ile simu,
“Erick, kwakweli Angel anaumwa, kajifungia ndani hataki kutoka nikimuita anasema anayemtaka ni baba yake tu. Kwahiyo anakutaka wewe”
“Kheee toka lini mama?”
“Toka juzi alivyoingia ndani basi hajatoka tena, jana kutwa nzima hajatoka. Leo pia, nimeshindwa kuvumilia ndiomana nimekupigia, hebu uje upesi”
Hapo baba Angel aliacha kila kitu, maana huwa akisikia Angel anaumwa anaona kama akili yake ikimruka, yeye alijikuta akiwa na uchungu zaidi na Angel kuliko mtu yoyote yule.
Aliacha kila kitu na muda huo huo alitoka na kupanda gari lake na kuelekea nyumbani kwao kwaajili ya mtoto wake Angel.

Baba Angel alipofika, alimkuta mama yake akiwa amekaa na kusema kuwa aende sasa akaongee na binti yake ili afungue mlango.
Baba Angel alisogea hadi chumba anacholala Angel na kumuita,
“Angel mwanangu, naomba ufungue mlango”
Angel alifungua ule mlango, baba Angel alipomtazama chini aliona kuna damu inamchirizika Angel miguuni.

Angel alifungua ule mlango, baba Angel alipomtazama chini aliona kuna damu inamchirizika Angel miguuni.
Baba Angel alimuwahi binti yake na kutoka nae nje ambapo alienda kumpakiza kwenye gari na kuondoka nae huku akimwambia mama yake kuwa atampigia simu, moja kwa moja baba Angel alimpeleka Angel hospitali ambapo aliwekwa kwenye matibabu halafu baba Angel alikuwa akimsubiria huku ajiuliza mambo mengi sana,
“Sijui ndio mimba imetoka au sijui ni kitu gani?”
Alikosa jibu kwakweli na kuendelea kusubiri, muda kidogo alipigiwa simu na mke wake ambaye alikuwa na maagizo kwake,
“Baba Angel unaporudi naomba upitie pale….!”
Baba Angel aliamua amkatishe maongezi kwanza kwa kumwambia kuwa sio kwamba atarudimuda huo,
“Mama Angel, sipo karibu nipo mbali kidogo kwahiyo nitachelewa kurudi”
“Uko wapi kwani?”
“Nikirudi nitakwambia mke wangu”
“Niambie bhana, tatizo nini kwani?”
“Ila usipaniki”
“Sawa, niambie tu”
“Nipo na Angel hospitali hajisikii vizuri kidogo”
“Tatizo nini tena?”
“Nkirudi naye nitakwambia”
Baba Angel alikata ile simu na kumfata daktari maana alikuwa ameitwa naye, basi alivyofika daktari akamwambia,
“Huyu binti alikuwa ni mjamzito, sasa mimba yake imetoka”
“Oooh asante Mungu”
“Kheee yani kitendo cha kutoka mimba unashukuru?”
“Dokta, kulikuwa na mgogoro kuhusu hiyo mimba balaa, huyo ni binti yangu ila nashukuru kama mimba imetoka maana tulikuwa na mawazo sana”
“Kivipi?”
“Mara nyingine kuna vitu vingine ni Mungu tu anaviiruhusu ili kuepuka baadhi ya migogoro, nashukuru kama mimba imetoka yenyewe kuliko binti yangu angepatwa na matatizo mengine”
“Mmmh!! Ila ngoja nikushauri kitu kuhusu hawa watoto wa kike”
Huyu dokta alimshauri pale baba Angel, kisha alimwandikia dawa za kutumia Angel na kumpa ruhusa kuwa anaweza kuondoka nae.
Kwakweli muda ulikuwa umeenda ila baba Angel muda ule ule aliondoka na mwanae kuelekea nyumbani kwake.

Angel alianza kuongea kwenye gari kwa uchungu akimwambia baba yake,
“Nisamehe baba, sijui kwanini inanitokea hivi mimi”
“Pole mwanangu”
“Hakuna kitu ambacho nimekosa kwenu kama wazazi wangu, mnanipa mapenzi ya kweli, hakuna shida ninayopata halafu nisisaidiwe, hakuna kitu ninachotaka ambacho hamkunipatia wazazi wangu hata nashangaa ni kwanini nimewatenda hivi. Nisamehe baba yangu, najua ni jinsi gani nimekudharaulisha”
“Usijali mwanangu, ngoja tufike nyumbani upumzike tu halafu tutaongea kwesho”
Bibi Angel nae alipiga simu ili kujua hali ya mjukuu wake maana aliona kimya kimezidi, basi baba Angel alimwambia kuwa mtoto anaendelea vizuri na wanaenda nyumbani ambapo bibi Angel aliahidi kwenda kumuona huko huko nyumbani kwao.
Baba Angel na Angel waliingia saa sita usiku pale nyumbani kwao, mama Angel alikuwepo maana toka aambiwe kuwa wapo hospitali alikuwa na mashaka sana na hali ya mtoto wake, ila walivyofika baada ya salamu, baba Angel alimuomba mama Angel kuwa Angel apumzike kwanza na kama kuongea nae basi aongee nae kesho yake, ni kweli mama Angel hakubidha na kumuacha binti yake aende kupumzika.
Ila walipokuwa ndani mama Angel aliamua kumuuliza mumewe ili amwambia kiundani zaidi ambapo alimweleza kuhusu kutoka kwa mimba ya Angel, yani mama Angel alifurahi sana na kumwambia mumewe,
“Yani nimefurahi sana kusikia hivyo, basi kesho naomba huyu kijana Samir arudi kwao maana hapa hapa tena atampa Angel mimba nyingine maana ni rahisi zaidi”
“Ila mke wangu kumbuka kuwa mtoto hachungwi, ni swala la kumfundisha mtoto tabia njema ili aweze kuishi vizuri. Hatuwezi kumchunga Angel, akiamua ataonana tu na huyo Samir hata asipokuwa hapa nyumbani. Wote wawili, Angel na Samir wanahitaji Elimu wale ili waweze kujichunga na kujitunza wenyewe wakati tukiendelea kufatilia swala la undugu wao”
“Ila mume wangu, kinga ni bora kuliko tiba, tuliwahi tatizo mapema kwa kumuondoa huyu Samir hapa nyumbani, tukichekelea tu jambo hili kwa hakika tutalia sana maana mambo yatakuwa magumu zaidi”
“Tutaongea kesho asubuhi mke wangu, kwasasa acha nipumzike”
Waliamua kulala kwa muda huo, na palipokucha tu, alijiandaa baba Angel na kwenda kumuita Samir ili kuweza kuongea nae maana aliona ni vyema kuongea nae kwanza.

Mama Angel nae ile mapema kabisa, alienda chumbani kwa Angel kuongea nae ambapo Angel alipiga magoti na kumuomba msamaha mama yake,
“Naomba unisamehe mama”
Mama Angel alimuinua na kumuuliza,
“Kwahiyo kwasasa hutorudia huo ujinga tena?”
“Sirudii mama, nimekoma na sirudii tena nakuahidi mama nitakuwa binti mzuri kwasasa”
“Ukimuona Samir utafanyaje? Bado una wazo la kuoana na Samir?”
Hapo Angel alikaa kimya kwa muda, ambapo mama Angel alimuuliza tena,
“Ukimuona Samir utafanyaje?”
“Hamna kitu mama”
“Hebu kaa chini nikwambie Angel”
Angel alikaa na kumsikiliza mama yake,
“Mimi nilipobeba mimba yako, nilikuwa najificha kwanza ili nisionekane kama nina mimba, nilimaliza chuo ila niliogopa kurudi nyumbani maana mama angenigundua na mimba ilikuwa ni kubwa tayari, niliongea na baba yako ambapo alinitumia pesa za kupanga chumba, nikawa naishi mwenywe. Asikudanganye mtu mwanangu, mimba ya kulea mwenyewe tena kisirisiri inaumiza sana moyo, nakumbuka muda mwingi nilikuwa najiinamia na kulia sana chumbani kiasi kwamba sikuwa nakula vizuri wala nini. Mama Akatonywa na rafiki yangu, kuja kuniona ndio nilikuwa na hali mbaya, nikawahishwa hospitali na kwenda kujifungua wewe, mama yangu akawa ndio kila kitu kwangu, yeye ndio alikuwa wa kunihurumia na kunisaidia, sikuona sura wala jicho la baba yako. Nilirudi nyumbani tukakuficha ndani maana kila mmoja anaogopa ile aibu tutakayoipata ya kusema mimi nimezaa, ikiwa nilihesabika kama mtoto mwema mtaani, mtoto niliyependa masomo na dini, aibu ile ilikuwa maradufu pale baba yako alipogoma kuja kujitambulisha kwetu, alipogoma kuja kukuona mtoto wake, nilikuwa naumia kila siku, nalia sana na kumuomba Mungu anisaidie, yani kuna mwanaume nilitaka kuolewa nae, sio kwamba nilimpenda hapana, ila alinipenda sana, ila kwavile alitaka kunioa nikawa tayari kwa hilo ili kuificha aibu yangu, nilijua nitajifunza kumpenda ndani ya ndoa ila ndugu zake nao walipogundua nina mtoto wa kiarabu waligoma nisiolewe nae, na walinipa maneno ya kashfa sana, unaweza kuelewa ni jinsi gani machozi yalikuwa ndio rafiki yangu kwa kipindi hiko. Ndipo alipotokea huyu baba yako, aliyenipenda kwa dhati na alikuwa tayari kwa chochote kile juu yangu japo tulipigwa vita ila alinioa na kunionyesha mapenzi ya dhati kwangu na kwa mwanangu hadi kesho bado anatupenda sana. Tukakulea katika maadili mema na kukuepusha ili usitende ubaya, ila Angel ukaenda kubeba mimba kabla ya ndoa na mbaya zaidi umeenda kuzaa na kijana niliyekukataza kuwa naye. Unaweza kuelewa ni jinsi gani umeweza kumfedheesha na kumsononesha baba yako, unaweza kuelewa jinsi gani huyu baba anayetupenda anasononeka baada ya sisi kumlipa kwa kumfanyia mabaya badala ya mema, sijui unanielewa mwanangu?”
Mama Angel alimuangalia Angel ambapo Angel alikuwa amejawa na machozi kwenye sura yake, yani Angel alikuwa akilia sana kiasi kwamba hakuweza kunyamaza kiurahisi, Angel alionekana kujutia vitu vingi sana, basi mama Angel ilibidi ambembeleze, kisha Angel alimuuliza mama yake,
“Mama kwanini hukuniambia haya mapema?”
“Sikutaka kukuchanganya mtoto wangu, sikutaka kukuchanganya na masomo yako, kwani siku zote unajua na kuamini kuwa huyu ni baba yako mzazi, nikajua wazi ikiwa nitakwambia kuwa kuwa mwingine ni lazima nitakuwa nimekuchanganya sana binti yangu”
“Mama, nahitaji kutubu zaidi kwa baba. Ananipenda sana, kwanini mimi nimefanya hivi? Baba mzazi hakunitaka ila huyu alinipenda na bado ananipenda, ananihurumia, ananiangalia, kwanini lakini huyu hakuwa baba yangu mzazi?”
“Hilo ni kosa langu mwanangu, hata mimi nilitamani sana kama huyu angekuwa ni baba yako mzazi yani ingekuwa ni nzuri sana, ila mwanangu hakuna kilichoharibika maana huyu anakupenda kwenye kiwango kile kile”
“Mama, namuomba baba ili niweze kumuomba msamaha tena, mama naomba niitie baba yangu”
Angel alikuwa akilia sana, na alionekana kukosa amani kabisa kwa muda huo, basi mama Angel aliinuka na kwenda kumuita baba Angel ambaye alikuwa bado akiongea na Samir, kisha alimwambia kuwa Angel anahitaji kuongea nae, ambapo baba Angel alimalizana na Samir pale na kwenda chumbani kwa Angel huku mama Angel akimfata kwa nyuma.
Baba Angel alipoingia pale, Angel alianguka kwenye miguu ya baba yake huku akilia sana na kuomba msamaha kwa kile kitendo alichokuwa amekifanya, ila baba Angel alimnyanyua na kumkumbatia ingawa Angel alikuwa akilia sana,
“Nyamaza mwanangu, mimi nilishakusamehe mbona toka siku ile”
“Najua baba, najua sababu unanipenda sana. Nisamehe baba yangu kwa kutokuthamini upendo wako kwangu, naomba unisamehe sana”
“Usijali, na Samir yupo hapa nyumbani kwani baba yake alitaka kumuua kwa kitendo hiko ila mwanangu nakuomba sana muone Samir kama kaka yako”
“Ila mimi simtambui yule baba”
“Sikia Angel, wewe ni mwanangu. Naomba Samir mchukulie kama mwanangu pia, mchukulie Samir kuwa mimi ni baba yake na umuheshimu kama kaka yako kutoka kwenye uzao wangu”
Angel alimuitikia baba yake, kisha baba Angel aliwaaga pale kwani kuna mahali alikuwa akienda kwa muda huo.
 
SEHEMU YA 408


Baba Angel akiwa ofisini kwake, alifikiwa na mgeni ambaye alikuwa ni Sia, alimkaribisha na kuanza kuongea nae,
“Kheee Erick hata kuniuliza kilichonileta nyumbani kwako siku ile?”
“Usinilaumu yani nina mambo mengi hatari, kichwa kimoja lakini kinabeba vitu vingi sana hadi nahisi kupagawa”
“Mmmmh pole sana, kwakweli nakupa pole. Unajua kuna vitu vingine vikiwa vinatokea katika maisha unajiuliza ni kwanini vimetokea ila badae unakuja kujua ni kwanini vile vitu vimetokea”
“Unamaanisha nini?”
Simu ya baba Angel ilianza kuita kwa muda huo na mpigaji ilikuwa ni ile namba ya Moses, basi baba Angel alipokea na kuongea nae,
“Hapa ninapoongea na wewe taya inaniuma na mbavu zote zinaniuma, kwani kijana wako ni mwalimu wa karate?”
“Khaaaa!! Ila Moses usiendelee kunishangaza, uliniambia kuwa umepigwa na Erick halafu nikashangaa pia, halafu muda huu unaniuliza kama mwanangu ni mwalimu wa karete, mimi na karete wapi na wapi?”
“Hapana yani unajua kanipiga sana, kijana mdogo kama yule wa kunipiga hivi!! Tena alikuwa akijitapa kuwa hakuna chochote anachoogopa na kusema kwamba nisimbabaishe”
“Mmmmh hayo mambo ni makubwa, ngoja nikupe pole labda utapona. Pole sana”
Kisha baba Angel alikata simu, ambapo Sia nae alimuuliza maana yale maongezi aliyasikia pia,
“Kapigwa na Erick huyo?”
“Ndio anasema kapigwa na Erick”
“Yule mtoto wako sio, yani yule mtoto wako sio kabisa, siku aliyonipiga mimi hadi nilihisi kuwa naenda kukata roho, jamani mwanao hafai. Yule mtoto namuogopa hadi leo, huwa siongei kitu mbele yake, yani mwanao Erica yupo vizuri ni mtu wa watu ila yule ni moto wa kuotea mbali”
“Unajua hata mimi nashangaa kwa habari hizi”
“Hebu mtafute dokta Jimmy muulize ni kitu gani alifanya kwa Erick”
Basi muda huo huo baba Angel alimpigia simu dokta Jimmy ambaye alipokea na kuanza kuongea nae,
“Hivi ni kitu gani kilifanyika kwa mwanangu Erick maana nasikia kawa bondia sana siku hizi?”
“Katoka kuniambia Moses kuhusu hiko kitu, anaumwa sana nasikia kapigwa na Erick, halafu yule ambaye alipigwa teke na Erick siku ile ni ameumwa wiki nzima. Nimejaribu kutafakari sana sijui ni sababu Erick alipewa dawa nyingi wakati mtoto!”
“Dawa nyingi!! Kivipi?”
“Si nilikwambia kuwa wale mapacha wako walichomwa sindano wakati wadogo! Yule wa kiume tulimpa dawa nyingi sana ili awe wa kwanza kumshawishi mwenzie sababu watoto wa kiume huwa wanawahi kupatwa na hamu”
“Mjinga wewe, kumbe ndio mlichokifanya!! Wajinga sana nyie”
“Sio kosa langu Erick, nisamehe sana”
“Toka hapa, mjinga wewe na ngoja awakomeshe wenyewe na ujinga wenu”
Baba Angel alikata ile simu ambapo Sia alikuwa makini kabisa akisikiliza na kusema,
“Itakuwa kweli, hawakuelewa mambo ya hizo dawa, ni lazima zimemuathiri Erick. Ndiomana yupo vile”
“Tuachane na hayo, niambie kilichokuleta”
Muda huu, baba Angel hata hakuwa na hamu ya mazungumzo wala nini kwahiyo alikuwa akiongea kwa kujilazimisha tu, basi Sia alianza kumwambia,
“Ni hivi, kuna kitu nimegundua kuhusu jambo Fulani”
“Ni kitu gani hiko?”
“Ni hivi, nilienda kule kwenye duka lenu na kumkuta Moses kule, moja kwa moja nilihisi kuwa Moses ana mpango usiokuwa wenyewe kuhusu lile duka lako. Nilijaribu kufatilia na nilionana na mke wa Moses na kusema kuwa yeye hataki kushiriki kwenye hiyo dhambi ambayo mumewe anataka kuitenda, nasikia siku ya jana ndio alipanga iwe siku ya kuvamia duka lako, ingawa Rama kakataa ila alitaka kutumia nguvu na ndiomana nilikuja siku ile ili nikupe huo ujumbe mapema kabisa”
“Asante sana kwa ujumbe, mambo yalikuwa mengi yakafanya nishindwe kufatilia ila huyo Moses kakomeshwa, kwa kipigo alichopata toka kwa Erick sidhani kama ataendelea na huo mpango tena maana sijasikia chochote, nikitoa kazini leo nitaenda kupita na dukani kwangu kuona kuna kitu gani kinaendelea kule”
“Aaaah sawa, halafu nisaidie jambo moja. Nisaidie niweze kuishi na mwanangu Paul hata kidogo”
“Sio rahisi hivyo, kumbuka mtoto hajakuzoea kabisa kwahiyo inatakiwa ufanye taratibu”
“Nifanye vipi ili anizoee?”
“Kwasasa jifunze kuwa karibu na madam Oliva ili uweze kuwa karibu na mtoto wako, na hapo anaweza kukubali kuja kuishi na wewe hata kidogo”
“Ila mbona Elly amekubali kirahisi kuwa karibu na baba yake Derrick, ila mama yake ndio hamtaki”
“Inategemea Elly na Derrick walikutana katika mazingira gani, ila kama nilivyokwambia kuwa unatakiw akuanza kuwa karibu na madam Oliva kwanza kabla ya yote ili ujenge ukaribu na mtoto. Yule madam ni mwelewa sana, ukiwa nae karibu utapenda zaidi”
Basi Sia aliamua kumuaga baba Angel na kuondoka zake.

Baba Angel muda huu alipotoka, moja kwa moja alipitia dukani kwake ili kuangalia maendeleo, alipakuta pako vizuri kabisa hapakuwa na tatizo lolote lile, na kumfanya afurahi sana ila alimuuliza kama hata jana hapakuwa na tatizo,
“Jana ilikuwaje lakini? Palikuwa shwari kabisa?”
“Ndio palikuwa shwari ila kuna muda alikuja yule kijana wako yani yule Erick, basi alikuwa kama anakagua kagua nje ya duka, akamuona kijana Fulani anachungulia, kwakweli alimrusha na teke hilo, yule kijana aliangukia kule barabarani, ilikuwa bado kidogo tu yule kijana agongwe na gari”
Baba Angel akapumua na kushangaa sana kwani kama alikuwa haelewi na kuuliza vizuri,
“Alikuwa akichungulia wapi?”
“Alikuwa akichungulia hapo mbele, yani kila aliyeona tukio lile alishangaa sana. Lilikuwa ni tukio la ajabu”
“Ila alipona huyo mtu?”
“Ndio, aliinuka na kuanza kukimbia hata kila mtu alimshangaa ila kijana wako ni kiboko”
Muda mfupi alifika Juma pale dukani na kuanza kuongea na baba Angel kuhusu Erick.

Usiku wa leo baba Angel aliamua kumueleza mke wake kuhusu Erick, vile alivyoambiwa kwenye simu na Moses na vile Sia alivyomwambia na jinsi alivyoambiwa na dokta Jimmy na mambo aliyoyakuta dukani, basi mama Angel akafurahi na kusema,
“Afadhali kuna bondia kwenye nyumba yangu”
“Kumbe umefurahia mke wangu!”
“Ndio, wangekuwa wametuibia wale wajinga, tena Erick awe anawapa kipigo cha hali ya juu. Natamani Erick akutane na huyo dokta Jimmy halafu ampe kipigo kilichoenda shule yani huyo dokta Jimmy atakuwa na heshima na adabu. Ila mume wangu haya mambo ya Erick na Erica tunayamalizaje? Maana kwasasa tumekazana na mambo ya Angel na Samir tu”
“Naelewa mke wangu kuhusu Erick na Erica, yani hadi kichwa kinachanganya nikiwafikiria hawa watoto na sijui jinsi ya kuwanusuru”
“Halafu nimegundua kitu”
“Kitu gani?”
“Inawezekana Erick akimaliza hayo mapambano yako huwa anajikuta akitamani sana kulala na Erica maana siku ile nilimkuta kalala chumbani kwakina Erica huku pembeni yake kuna Erica na Sarah”
“Duh!! Mke wangu, hii hatari ujeue, yani mtu unafikiria hadi akili inaacha kufanya kazi. Kwanza hatuna uhakika kama siku ile walitoka salama kweli maana vitendo vyote walishafanya aarrghh huwa sitaki hata kuwaza mambo hayo maana hasira huzidi kwenye akili yangu aaargh”
“Pole mume wangu, ila tunapofikiria maswala mengine basi tufikirie pia na hili la watoto wetu mapacha maana hatuna cha kufanya dhidi yao”
“Tuache hayo kwanza, tukienda kuongea na dokta Jimmy nina uhakika tutajua vitu vingi sana, yeye ndio atatuambia cha kufanya. Sema cha muhimu kwasasa ni kutokuwapa nafasi Erick na Erica wawe pamoja kwa moda mrefu”
Baba Angel aliamua kulala maana aliona kama akili yake ikigoma kuendelea kuwaza.

Leo baba Angel alitaka tu kukaa nyumbani kwake bila ya kwenda popote pale, ila akapigiwa simu na Jack ambaye alimuuliza baba Angel nyumbani kwake ili aweze kwenda,
“Hapana, usije kwangu niambie ulipo nije”
“Sawa, ila unachonifanyia Erick sio kizuri, Mungu anakuona kwakweli”
“Sikia Jack, niambie ulipo halafu nitakuja. Unanihisi vibaya, ila niambie ulipo”
“Sawa, njoo tuongee vizuri”
“Na mtoto upo naye?”
“Ndio nipo naye”
“Sawa nakuja”
Basi baba Angel alijiandaa na kumuaga mke wake kuwa anaenda kwenye kazi, kisha akaondoka pale nyumbani ila mke wake hata hakumuuliza sana.
Basi baba Angel njiani akampigia simu Rahim kuwa akutane nae ili aende mahali kuzungumza nae, na kweli Rahim hakuwa mbali sana na eneo alilokuwepo baba Angel kwahiyo alimwambia kuwa anaenda kuonana nae.
Baba Angel alifika pale alipo Jack na kuanza kuongea nae ambapo Jack alimlalamikia sana kwa kitendo chake cha kukataa mtoto,
“Unajua Erick unanisikitisha, unamkataa mtoto wetu kweli? Unajua shida niliyoipata kwa huyu mtoto hadi unafikia hatua ya kumkataa?”
“Naomba unisamehe kwanza, yuko wapi mtoto?”
Jack alimpigia simu na mwanae alifika pale na kumsalimia baba Angel, muda kidogo Rahim nae alifika eneo lile, ambapo baba Angel alimkaribisha pale ila Jack na Rahim hata hawakuwa watu wanaofahamiana kwani walisalimiana juu juu tu, ila Rahim alipomuona yule mtoto akasema,
“Jamani, hii kopi yangu imetokea wapi?”
Jack alikaa kimya akimuangalia Rahim na baba Angel na kumuuliza baba Angel,
“Ni ndugu yako huyo?”
“Hapana ni rafiki yangu, umeona jinsi alivyofanana na mwanao?”
Jack alimwambia mwanae aondoke tena eneo lile, ambapo mwanae aliondoka halafu Jack akamuuliza Rahim,
“Samahani kaka, eti mimi na wewe tunafahamiana?”
“Hapana, ndio kwanza nakuona leo”
“Ni hivi, yule mtoto ni mtoto wangu na nimezaa na huyu mtu hapa ila anasema mtoto kafanana na wewe, inakuwaje na mimi nimezaa na yeye? Kwakweli hakuna kitu ninachoelewa hapa, hebu jiulizeni zaidi ya urafiki mlionao nyie sio ndugu?”
Baba Angel na Rahim waliangaliana na kusema kwa pamoja,
“Kheee ndugu tena!!!”
Kisha Rahim akasema,
“Inawezekana hiyo ikawa kweli, maana huyu jamaa mke wake ana nyoto ya kutembea na watu wa ukoo wangu tu. Kwahiyo inawezekana mimi na yeye tukawa ndugu”
“Acha maneno yako Rahim”
“Aaaah hebu jiulize na wewe, simjui huyu mwanamke, sijawahi kumuona kabisa iweje mtoto wake afanane na mimi!! Na anadai kuwa mtoto ni wako, hata kama duniani ni wawili wawili ili ule mfanano umezidi jamani, yani hadi nilipomuona mtoto ni wazi kuwa nimejiona mimi mtupu. Erick, itakuwa mimi na wewe ni ndugu hebu tuchunguze hili, halafu mkeo ana nyoto kubwa sana ya kutembea na ukoo wangu”
Hakuna kitu ambacho baba Angel alikuwa hakipendi kama kitu cha kumsema vinaya mke wake, kiasi kwamba aliona yale mazungumzo magumu sana kwake. Basi aliamua kuyakatisha kwa kusema,
“Jack, naomba tumalize utata wa jambo hili, mimi nipo tayari kupima DNA na mtoto wako, kama ikikubali basi nitamkubali kuwa ni wangu hakuna tatizo juu ya hilo”
“Sawa, mimi nina uhakika kuwa ni mwanao. Na vipimo vitathibitisha hilo, umeniletea huyu mtu simjui kabisa, labda nimuite shemeji”
“Ila na wewe, siku zote hukuona kama mtoto hafanani na mimi?”
“Mimi sikujua, nilijua kwenye ukoo wenu ndio mpo vile. Nakumbuka kuna mwaka Fulani nilikuwa nikiingia facebook nakuona umejirusha wewe na mtoto wako mmoja wa kike ambaye sura yote kafanana na mwanangu”
Baba Angel alicheka kidogo na kutikisa kichwa, alihisi kamavile kuna mchezo anafanyiwa baina ya Rahim na Jack, waliongea kidogo tu halafu baba Angel aliaga na kuamua kuondoka zake.
Rahim hakuondoka kwa muda huo na alitaka kuongea zaidi na Jack ila Jack aliinuka na kumuaga pia,
“Mmmh hutaki tuongee kidogo”
“Tuongee kuhusu nini? Mimi sio muongeaji sana, Erick ananifahamu vizuri”
“Mbona unanyodo sana, umeolewa kweli wewe!!”
“Niolewe ili nigundue nini?”
“Mmmmh”
Rahim aliishia kuguna na kumuacha huyu Jack aendelee na mambo yake mengine.

Baba Angel alifika nyumbani kwake ila getini alikutana na mama yake ambaye nae alikuwa amefika kwaajili ya kumuona mjukuu wake, basi alisalimiana nae pale na kumkaribisha ndani.
Walipofika mlango wa kuingia ndani, Samir alikuwa kafungua mlango akitoka basi bibi Angel alishtuka sana kumuona Samir na kumuuliza baba Angel kwa mshangao,
“Ni nani huyu!?”
 

Similar Discussions

6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom