SIMULIZI: Mkufu wa Malkia wa Goshen

*MKUFU WA MALKIA II 68*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

"Ha - hapana!" Mama akanena akikunja uso wake kwa hofu kuu. Mara akasikia ubaridi wa upanga begani mwake alafu akaulizwa:

"Bali?"

ENDELEA

Akabanwa na kigugumizi. Hakujua cha kujibu. Alihisi mdomo umekuwa mzito na mwili umeishiwa nguvu. Akageuka na kumtazana mlinzi aliyekuwa amemshikia upanga, akasema kwa huruma, "Nisamehe!"

Yule mlinzi akavuta hewa kwa mshangao. Alah!! Akaanza omba msamaha maana yule aliyemsumbua ni mkwe wake na mfalme.

"Nisamehe!" Akapiga magoti akikutanisha viganja. "Niwie radhi, sitarudia tena!"

Mama akabaki anaduwaa. Bado hakujua ni nini mlinzi huyo alikuwa anafanya.

"Tafadhali, usimwambie mfalme tafadhali. Ataninyonga kwa mkono wake wa kushoto!"

Hapo mama sasa akaelewa. Akamtaka mlinzi huyo anyanyuke upesi kwani hatomfanya lolote. Aliponyanyuka, mama akajikaza. Akaona anaweza kutumia fursa hiyo kujikomboa na kutimiza haja yake.

Akamuuliza yule mlinzi, "Njia hii huwa mnailinda masaa yote?"

Mlinzi yule akatikisa kichwa. Kisha akamwambia mama Tattiana kuwa wana ratiba ya kulinda eneo lao kwa mujibu wa nyakati. Akamweleza nyakati hizo. Basi mama Tattiana akafurahishwa. Akaendelea kuongozana na mlinzi huyo mpaka pale alipopata haja ya moyo wake.

Kisha kuua ushahidi wa hilo zoezi, akamwambia yule mlinzi kwamba mfalme amemtuma akatekeleze zoezi hilo. Yule mlinzi akaamini.

Mama akaenda zake na kwenda kukutana na mwanae akamweleza yaliyotokea.

"Umefanya kazi kubwa," Tattiana akampongeza. "Sasa tunaweza kutoroka!"

Ila mama akasita. Akamwambia mwanaye kuwa bado hawapo tayari. Kuna vitu baadhi anatakiwa kuvifanya kabla hawajaamua kudumbukiza miguu yao yote dimbwini.

"Tumetambua kuhusu hilo la nje, ila hapa ndani bado ni shida. Naomba nilifanyie kazi kwa muda huu."

Basi Tattiana akaridhia mama akatende kazi yake.

**

"Oragon!" Ottoman aliita akimtikisa kaka yake usingizini. "Amka! Muda umeenda sasa!"

Oragon akaamka na kujinyoosha mwili. Akatazama dirishani, mwanga ulikuwa unapiga. Akapiga mihayo na kujibandua toka kitandani.

Akauliza, "Kwani nini?"

Ottoman akamuuliza, "kwani hujui? ... amka twende sasa! Muda haungoji!"

Oragon akafikicha macho yake yaliyolewa usingizi. Akamtazama vema Ottoman, alikuwa amebebelea kifurushi mgongoni.

Akauliza, "Cha kwangu kipo wapi?"

Ottoman akastaajabu, "mimi nitajuaje ulipokiweka?"

Usingizi ukamkata Oragon. Akatazama huku na huko. Alikuwa amesahau alipoweka kifurushi chake. Na alihofia kwa namna wanavyokaa mule ndani na wadokozi na wezi, pengine hakitakuwapo.

Akasaka chumba kizima, hakuona! Jasho likamtiririka. Baadaye ndipo akagundua alikuwa amekiweka uvunguni mwa kitanda. Haraka akatazama. Napo hakikuwepo! Kilikuwa kimebebwa.

Akaketi akishika kichwa. Roho ilimuuma sana kukipoteza kifurushi chake. Alilalama na akitaka kwenda kuwatafuta wale majamaa wawili wanaoishi nao, ila Ottoman akamsihi asifanye hivyo. Watapoteza muda ilhali wana safari.

Kishingo upande, Oragon akaridhia. Sasa walikuwa na kifurushi kimoja tu cha thamani. Wakaanza safari yao kwa tahadhari.

Njia nzima wakawa wanaangaza usalama wao. Kama wangelikamatwa na askari basi ungekuwa mwisho wao papo hapo. Wakafanikiwa kutembea kwa muda nusu saa. Wakafika mahali ambapo askari walikuwa wamejikusanya kwa uwingi wakiwa wanateta. Wakabadili njia.

Wakatembea tena kwa mwendo wa dakika arobaini na tano, mbele yao wakawaona askari wanne wakiwa juu ya farasi. Walikuwa wameshikilia mikuki na migongoni wakiwa wamebebelea pinde za mishale.

Wakajibanza nyuma ya migongo ya watu, wakafanikiwa kupita salama. Sasa wakawa wamebakiza kama hatua kama mia mbili kuukuta mpaka wa falme ya Goshen. Huko nyumbani walipoamua kurudi baada ya kushindwa maisha himaya zingine.

Ila wakiridhia na kutenda hilo baada tu ya kudhani kuwa Goshen mambo yatakuwa yamebadilika maana walishaona ishara kadhaa. Moja, matunda ya Cedar yamekuwa yakiuzwa falmw zingine tofauti na awali. Pili, walisikia utawala wa Goshen umebadilika japo hawakujua umebadilikaje.

Hadithi za kutisha walizozisikia kuhusu Goshen hazikuwaingia akilini maana waliamini hakuna mtu yeyote aliyekuwa anaijua Goshen mbali na wao ambao ni wenyeji.

Basi wakiwa wanasonga, wamekaribia na mpaka, wakaanza kuona mwanga ukipungua. Anga lilianza kutwaliwa na wingu jeusi zito kana kwamba mvua yataka kushuka!

Wakadhani wafanye upesi kabla mvua hiyo haijawashukia. Wakakimbia na kuzama ndani ya himaya ya falme ya Goshen. Sasa wakajikuta wapo kizani.

Kiza lisilo na kikomo na hapo hawana hata tone la ginga la moto kuwapa mwanga.


**

"Mfalme! Mfalme!" Sauti ya kijakazi wa Jayit ilipaza. Alikuwa ana uso uliowehuka na macho yaliyobebelea hofu.

Kichwani alikuwa amefunikwa na ngao ya chuma. Mkononi amebebelea jambia refu lenye kutu. Mwili wake ulikuwa umemomonyoka akitembea kama mtu aumwaye mifupa.

Alisimama mlangoni mwa chumba alalacho mfalme, akiwa mhafifu wa subira. Alitamani hata apasue mlango na kuzama ndani.

Basi muda si mrefu mlango ukafunguliwa, Jayit akatoka. Alikuwa amevalia joho lake refu jeusi lililotengenezwa na ngozi za binadamu.Macho yake yanatisha na kuwaka mithili ya paka! Uso wake unaogofya. Na hata ananuka umauti!

Akamuuliza yule kijakazi kuna nini? Basi yule kijakazi akiwa anaogopa mno, akasema, "Ee mfalme, tumevamiwa!"

Jayit akatoa macho. Akatisha zaidi! Akamnyaka yule kijakazi wake na kumuuliza, "ni nani huyo anathubutu kumvamia Jayit?? Jabali la mwamba mgumu. Mfalme wa anga jeusi?"

Kijakazi yule akiwa anatetemeka, akasema, "sijui Ee mfalme. Ila naye si binadamu. Ni mlozi! Na amesema anataka kuonana nawe kule kondeni!"

Jayit akang'ata meno na kunguruma kama simba! Akafoka, "yu kwapi jemedari?" Kijakazi akamjibu yu tayari kondeni akiwa na askari. Basi Jayit akaagiza kijakazi huyo atoe taarifa ya kuvamiwa falme nzima. Wote wakutane huko kondeni!

Basi ndani ya muda mfupi, tarumbeta kubwa likalia likipulizwa juu kabisa ya jengo la kasri. Falme nzima ikapata kusikia! Na kujua kuwa ipo hatarini.

Wapo vitani.

**

"Wewe ni nani? Na unathubutuje kutia mguu kwenye makazi yangu?" Sauti nzito iliuliza ilhali mtu aulizaye akiwa haonekani.

Venis aliyekuwa amesimama mbele ya jeshi lake mamia ya maelfu, akakunja shingo kuangaza. Mbele yake, hatua hamsini, alikuwa amesimama Phares akiwa na askari wapatao mia tatu kwa idadi. Askari hao hawakuwa wanamtisha hata kidogo japo alipigwa na mshangao kukuta Goshen imekaliwa na walozi!

Hakuwa anajua mabadiliko hayo yamefanyika lini na nani akiyaongoza. Ila kama kuna kitu alikuwa anaamini, basi na kuitia Goshen mikononi mwake.

"Wewe ni nani?" Venis akapaza sauti. Kisha akakodoa macho yake, "Kama u kweli wajiamini, jitokeze na upambane kilingeni!"

Lakini kama kuna kitu hakukijua, ni kwamba aliyekuwa anaongea ni Jayit. Jabali la kilozi. Lakini pia Jayit hakuwa peke yake wakiwa hawaonekani. Walikuwa na kundi lake kubwa lingine la kijeshi mbali na lile lililokuwapo pale!

Na wakati huo Venis akiwa anatafuta nani anaongea na yupo pande gani, basi jeshi la Jayit lilikuwa tayari limeshamzunguka.

"Wataka kuniona, sio?" Akasikia swali. Kabla hajajibu, kugeuka kushoto akastaajabu kumwona Jayit amesimama akimtazama. Mikono yake ameitandaza kana kwamba anangoja kumbato.

"Umeniona sasa," mwanaume huyo akasema kwa kiburi cha majivuno. "Sasa unaweza ukaniambia unataka nini kwangu?"

Kabla Venis hajajibu, akastaajabu kuwaona askari wa Jayit wakiwa wamemzunguka. Kwa haraka walikuwa kama wanaume alfu tano! Hakuona wametokea wapi. Alijikuta tu tayari yu mtegoni.

Akajikaza na kusema akimtazama Jayit, "nimerudi nyumbani. Na kamwe hautanizuia kuichukua Goshen!"

Jayit akapaliwa na kicheko. Akacheka sana tena sana. Akiwa kichekoni, akapiga makofi mawili, na mara jeshi lake likavamia askari wa Venis.

Mapambano makubwa yakazuka! Ila askari wale wa Venis wangewezaje kupambana na watu wasioonekana?? Ndani ya nusu saa, wakajikuta wote wakiwa wameshauawa! Hakuna hata mmoja aliyebaki anahema.

Napo ndipo Jayit akakoma kucheka. Akakaza uso na kumsogelea Venis. Akamuuliza, "ulikuwa unasema??"


**
 
Duuu....jeshi la Venis sio binadamu na la Jayit sio binadamu. Sasa.mbona la Jayit lilikuwa halionekani? Ina maana hata kwenye giza pia kuna giza na mwanga?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom