SEHEMU YA KUMI NA SITA
Mwanangu hebu amka, amka Samson nakwambia, ama kweli ng'ombe wa maskini hazai, amka chukua mbegu ya mahindi humo twende nazo shambani.
Yaani dada zako wanakuwa wa kwanza kuamka kuliko wewe mtoto wa kiume, hebu acha ujinga, wewe ni mkulima tu , na kilimo hikihiki ndiyo utakufa nacho. Maana toka uambiwe mpango wa kwenda mjini na huyo baba yako mkubwa basi hata kazi hutaki. aliongea Mama Mgaya katika harakati za kumwamsha mwanae.
Samson aliamka akiwa mnyonge sana akanawa uso na kuelekea shambani huku wazazi wake wakija nyuma wakipiga stori.
Ujue mke wangu naona una Imani sana na kaka yangu kuhusu yale aliyoyasema kuhusu Samson, labda nikwambie tu kuwa wewe humjui yule, Mimi yule ni ndugu yangu namjua kuanzia utosi hadi unyayo (akimaanisha anamjua vyema)
Mara oooh nitamsomesha huyu mtoto, Mara oooh nitawajengea nyumba nzuri, yaani Kila kitu anaongea yeye, na hakuna mtekelezaji pale, no kwamba Hawa kuku tunaomchinjia Kila siku anakula nyama basi anajiikuta anatoa ahadi za uongo, yule ni muongo sana, ni ndugu yangu lakini usimwamini haraka kauli zake,ohhooooh.
aliweka kituo mzee Mgaya.
Lakini baba Samson, kama kweli angekuwa muongo angekubali kupoteza nauli Hadi wilayani kuulizia matokeo? Yaani nauli ipotee kirahisi tu. alihoji mama Mgaya.
Mke wangu, wewe mtu mwenye sifa, mwenye kupenda kujikweza,mwenye kutaka kuonekana, humjui. anaweza kutumia gharama kubwa sana ili atimize lengo lake kutaka kukubalika.
Kwanza nishamchoka Bora aondoke tu, ananizurulisha tu, kazi zangu haziendi hata mke mwenzio huko kashaanza kunilaumu kuwa nafanya kazi upande mmoja lakini pia hata Mimi naona kabisa ninavyofeli hivyo lazima nikatae tu na safari hii siendi sehemu yoyote yule msumbufu tu.
alilaumu mzee Mgaya huku wakiwa wanakaribia kufika shambani kwao.
Mama Mgaya hakuwa na neno yeye alimshukuru MUNGU kwa Kila kinachoendelea akiamini huenda si riziki ya Samson.
Mwambie Samson, aendelee kuchimba mashimo, na dada zake watupie mbegu. aliamrisha Mzee Mgaya kwa ukali.
Halafu wewe Samson nakuona upo taratibu sana, hebu changamka usiniletee ujinga wako, hebu hakikisha mistari inanyooka sawa , wewe ndiye mwanangu pekee wa kiume halafu tena nikupeleke ukakae kwa watu. weeeee haiwezekani wewe ni mrithi wa haya Mashamba yangu , Hawa dada zako muda wowote wanaolewa.
Wewe ndiye mwenye kuendeleza jina langu. aliweka kituo mzee Mgaya.
Maneno yale yalimtisha na kumuhuzunisha Samson, alijikuta analia lakini hakuwa na namna mbaya zaidi hata baba yake mkubwa haoneshi Nia kama ilivyokuwa mwanzo.
Mama Mgaya alitambua muonekano na mawazo ya Samson, akajikuta anatoa kicheko cha kumuhurumia akiamini ndoto za mwanangu hazitimii.
***********************************HoHodi, hodi humu ndani, ilikuwa ni sauti ya James Mgaya, akibisha hodi kwenye nyumba ya mwl mkuu,
Nani, hebu nisubiri navaa, alijibu mwalimu yule huku akijifunga nguo ya kitenge , akatoka nje akashangaa kumuona yule mgeni ambaye alimuona Jana kwa mzee Mgaya.
Karibu, una shida gani baba. aliuliza
Ni kweli Nina shida ila ni vyema tungekaa maana ni maelezo marefu.
alijibu mzee Mgaya mkubwa huku akikaribishwa ndani.
Wakati huo mwl mkuu yule bado alikuwa hajiamini, maana huwa si rahisi kutembelewa na ugeni hasa nyumbani kwake mbaya zaidi hamfahamu.
Samahani baba, Leo ni Mara ya tatu nakuona, mlikuja na baba yake Samson kuulizia matokeo na Jana nilikuona pale pale vipi Kuna shida gani. aliuliza yule mwalimu kwa shauku ya kutaka kujua.
Naitwa James Mgaya ni ndugu wa damu kabisa na baba yake Samson. alijitambulisha.
Ooooohooo sawa ni kweli mnafanana baadhi ya vitu hata masikio yenu mnafanana, vipi wewe ni mdogo wake eeeeh. aliuliza mwalimu.
Hapana yule ni mdogo wangu Tena nimemzidi miaka kumi nzima na hapa Kati tuna dada yetu ambaye nimemzidi miaka sita nzima. alifafanua
Haaaa dah basi ulivyo unaonekana kijana kabisa, maana siamini kama umemzidi umri Baba yake sam.labda ni kazi ngumu zinamzeesha
Ehhee na unaishi wapi maana inaonesha hauishi hapa kijijini kwetu. aliuliza mwalimu.
Naishi jijini Dar es salaam, tangu miaka kama thelathini iliyopita, akaanza kujitambulisha vitu vingi sana James Mgaya kiasi Cha mwalimu kugundua kuwa kumbe anaongea na mtu mwenye uzito wake.
Safari hii mwalimu hakuwa na wasiwasi kwani, alishamtambua mgeni kwa kiasi fulani, ambaye ni mtulivu kwenye kuongea lakini pia ana mvuto........
Licha ya dharau za mwalimu yule kwa wanaume wengi lakini huyu alipenda hata akae tu.
We mzee unasema umepigana hadi vita vya Uganda? taratibu usije umbuka Mimi mume wangu ni mtoto wa marehemu (jina kapuni) huyo marehemu alipigana vita hivyo akiwa mmoja wa wanajeshi wanaoheshimika kwenye nchi hii, huyo ndiye kamuinspire mume wangu kuingia jeshini. Je, huyo mkwe wangu unamfahamu? aliuliza mwalimu yule.
Nimeshakwambia nimepigana vita hivyo, Ina maana huniamini mwalimu?
Huyo marehemu mkweo alikuwa mwanajeshi wa kawaida sana, ila alionesha ubunifu mkubwa akiwa jeshini, ikiwemo ushapu, uharaka wa kutengeneza vitu, kama mahema, lakini pia kuwa na uwezo wa kutambua aina za silaha, alikuwa anajua hiyo ni silaha gani hata ambazo jeshi letu halikuwa nazo.
Lakini pia alikuwa fundi, licha ya Idd Amin kubomoa daraja mzee yule alikuwa mwepesi wa kubuni na kufanikisha kujenga temporary bridge hali iliyofanya aaminike jeshini na baada ya kuisha vita ni mmoja wa wanajeshi waliopata vyeo vya juu.
alifafanua mzee Mgaya.
Hapo sawa nimeamini ni kweli,Sasa karibu maana tumeongea porojo nyingi bila kuuliza shida iliyokuleta, aliongea mwalimu yule ambaye alivaa kinyumbani nyumbani.
Unasema mumeo ni mwanajeshi, yupo wapi kwa Sasa maana watu tunaogopa fumanizi ndugu yangu. alijihami mzee Mgaya.
(Huku akicheka)hapana bwana Mr hayupo yupo nje ya nchi kusoma hivyo usiwe na hofu. wakati hayo yakiendelea kililetwa Chakula na Fulani kama chai ya asubuhi wakajikuta wote wanajumuika kula huku wakipiga stori.
James Mgaya, ujue jina lako si geni kwangu, nimejikuta nazidi kukumbuka zaidi, ni kwamba Mara ya mwisho mwezi uliopita nilichukua barua Za sanduku letu, nikamtumwa mwalimu wangu aipeleke kwa ndugu yako si hilo tu, pia Kuna telegram ya hela ilitumwa mwaka Jana ikiwa inaenda kwa ndugu yako huyo huyo Hadi nilijiuliza nani katuma hela nyingi hivi , ilikuwa takribani lakini moja na nusu, si kawaida ujue. alitamia yule mwalimu mkuu wote wakacheka.
Hata shida iliyompeleka pale James Mgaya alisahau, hata mwalimu alijikuta amesahau kuuliza Nini kimemleta pale yule jamaa badala yake walijikuta wanatamaniana wazi wazi, James ni mmoja wa wanaume wakware tangia zamani huwa hapendi kupitwa na mwanamke mzuri,Licha ya umri kusogea lakini bado alikuwa yumo.
Mwalimu Agness, au Anyes kama walivyomuita wanakijiji wa pale alijikuta anababaika na mwanaume mmoja mzee wa mjini, anayejua kuchana nywele zake vizuri, anayejua kuvaa, suti ya bluu iliyonyooka kwa pasi ya mkaa yenye kijogoo inayopatikana kwa akina Samson, ilitosha kuonesha na kudhihirisha umaridadi wa James Mgaya. lakini kubwa lilimvutia mwalimu mkuu ni perfume ya kiume toka uarabuni ambayo mzee Mgaya alinunua kwa wapemba huko Zanzibar.
Ilifanya Kila muda mwalimu amwangalie mzee James Mgaya, na Kila walipogongana macho mwalimu aliangalia pembeni huku akionesha hajiwezi.
James Mgaya mkongwe, mwanasaikolojia aligundua ile hali akaamua kupiga ndege wawili kwa jiwe moja, yeah alijua fika huyu ndiye aliyeuza jina la Samson kwa watu wengine hivyo atambembeleza Hadi atajua ukweli na atasaidia kurahisisha matokeo ya kijana wao kupatikana, la mwisho kabisa angefaidi uzuri na utamu, wa penzi la mwanamama yule.
Mwalimu alimuaga mzee James akiingia chumbani huku, akiwa tayari mwili wake upo kwenye hali isiyoridhidha, ni mwanamke, ni mwanadamu, anakula ana afya njema, kubwa zaidi hajakutana na mwanaume kwa muda mrefu, lakini hatimaye alimpata mtu ambaye huenda akakidhi haja zake.
Akajikuta anaapa kwamba lazima aoneshe mitego yake Kisha akatoka akaja sebuleni.
Samahani mgeni tumeshindwa hata kukupokea briefcase yako, aliongea yule mwalimu kwa madaha.
Mzee James akajikuta ananyang'anywa mkoba wake Kisha ukawekwa kando, alielewa somo huku akijitahidi kuwa mwepesi na kumrahisishia somo mwalimu yule, alipanga kuwa lecture wa muda kwa yule mwalimu.
***********************************
Mke wangu mpaka saizi saa nane watu tumeenda shamba tumerudi lakini ndugu yangu hata hajarudi, huyu kaja kuzurura mke wangu yaani hata haeleweki kaja kufanya nini
Sasa wewe kwenda kwa mwalimu mkuu kuomba matokeo, hadi saizi, Mimi mke wangu nibishie tu lakini ukweli utaujua tu kaka yangu kabahatika tu kuwa na hela lakini Kuna mambo huwa yanamshinda sana alilaumu sana mzee Mgaya.
Milango ya mafanikio itafunguka kwa Samson? au ataishia kuwa mkulima wa jembe la mkono kama anavyosema baba yake?
Itaendelea..........