Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,974
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 20:
Yule mtu aliondoka na kuniacha na mke wangu ambaye alionesha kushtushwa na hali yangu.
“Mume wangu vipi?” aliuliza huku akitokwa na machozi.
“Naumwa?” nilimjibu huku moyo wangu ukiniuma mpaka machozi yalinitoka kitu kilichomshtua mke wangu na kuzidisha kilio. “Maskini mume wangu, unaumwa nini baba Zawadi?”
“Malaria.”
Alinichukua hadi bafuni na kunivua nguo zote kisha alinimwagia maji, na kunisaidia kurudi ndani. Alinitengenezea uji haraka na kuninywesha, kila kitendo cha upendo alichonifanyia mke wangu kiliuumiza moyo wangu baada ya kuona ni unafiki.
Lakini mke wangu ugonjwa wangu ulimgusa sana, muda wote alikuwa karibu yangu mpaka nilipopitiwa na usingizi. Nilipoamka nilimkuta pembeni yangu mkono shavuni.
“Mume wangu,” aliniita kwa sauti ya upole.
“Naam.”
“Poleee.”
“Asante.”
“Unaendeleaje kwa sasa?”
“Sijambo kidogo.”
“Nikutayarishie chakula gani?”
“Sijisikii kula,” pamoja na huruma yake ya mamba sikuipenda zaidi ya kumuona mnafiki.
“Mume wangu, kumbuka umemeza dawa kali, unatakiwa kula ili dawa zifanye kazi.”
“Nitakula baadaye.”
“Hapana, kuna ndizi na nyama nimekuandalia, naomba ule kidogo.”
“Hapana sijisikii kula.”
“Mume wangu.”
“Naam.”
“Mimi nani yako?”
“Mke wangu.”
“Unataka nani akubembeleze ili umsikie?”
“Wewe.”
“Kwa nini hutaki kunisikia?”
“Si nimekueleza nitakula baadaye.”
“Ni wazi huna mapenzi na mimi hata kunisamehe kwako kulikuwa kwa uongo.”
“Jamani mi si naumwa?”
“Kuumwa gani, ni wazi najilazimisha kwako huna mapenzi nami.”
Nilishangaa mke wangu akizungumza kitu ambacho hakikuwepo zaidi ya mimi kutojisikia kula. Niliamini kama nitaendelea kukataa naweza kuzalisha mapya, nilikubali kula kitu kilichomfurahisha mke wangu.
Baada ya kula nilijitahidi kulala lakini usingizi uligoma kunichukua, kila nilipofumba macho niliyaona matukio yote yakijirudia toka la mwanangu kuchelewa kutembea na siku niliporudi ghafla na kumkuta mwanangu akiwa katika mazingira mabaya.
Pia nilipomshuhudia mke wangu akiteremka kwenye gari na pia siku aliyorudi siku ya pili na kunidanganya kuwa alikuwa kwenye sherehe ya harusi kumbe alikwenda kulala na mwanaume. Na la siku ile nililoshuhudia kwa macho yangu akiwa na mwanaume kama walivyozaliwa katika kitanda changu
Yule mtu aliondoka na kuniacha na mke wangu ambaye alionesha kushtushwa na hali yangu.
“Mume wangu vipi?” aliuliza huku akitokwa na machozi.
“Naumwa?” nilimjibu huku moyo wangu ukiniuma mpaka machozi yalinitoka kitu kilichomshtua mke wangu na kuzidisha kilio. “Maskini mume wangu, unaumwa nini baba Zawadi?”
“Malaria.”
Alinichukua hadi bafuni na kunivua nguo zote kisha alinimwagia maji, na kunisaidia kurudi ndani. Alinitengenezea uji haraka na kuninywesha, kila kitendo cha upendo alichonifanyia mke wangu kiliuumiza moyo wangu baada ya kuona ni unafiki.
Lakini mke wangu ugonjwa wangu ulimgusa sana, muda wote alikuwa karibu yangu mpaka nilipopitiwa na usingizi. Nilipoamka nilimkuta pembeni yangu mkono shavuni.
“Mume wangu,” aliniita kwa sauti ya upole.
“Naam.”
“Poleee.”
“Asante.”
“Unaendeleaje kwa sasa?”
“Sijambo kidogo.”
“Nikutayarishie chakula gani?”
“Sijisikii kula,” pamoja na huruma yake ya mamba sikuipenda zaidi ya kumuona mnafiki.
“Mume wangu, kumbuka umemeza dawa kali, unatakiwa kula ili dawa zifanye kazi.”
“Nitakula baadaye.”
“Hapana, kuna ndizi na nyama nimekuandalia, naomba ule kidogo.”
“Hapana sijisikii kula.”
“Mume wangu.”
“Naam.”
“Mimi nani yako?”
“Mke wangu.”
“Unataka nani akubembeleze ili umsikie?”
“Wewe.”
“Kwa nini hutaki kunisikia?”
“Si nimekueleza nitakula baadaye.”
“Ni wazi huna mapenzi na mimi hata kunisamehe kwako kulikuwa kwa uongo.”
“Jamani mi si naumwa?”
“Kuumwa gani, ni wazi najilazimisha kwako huna mapenzi nami.”
Nilishangaa mke wangu akizungumza kitu ambacho hakikuwepo zaidi ya mimi kutojisikia kula. Niliamini kama nitaendelea kukataa naweza kuzalisha mapya, nilikubali kula kitu kilichomfurahisha mke wangu.
Baada ya kula nilijitahidi kulala lakini usingizi uligoma kunichukua, kila nilipofumba macho niliyaona matukio yote yakijirudia toka la mwanangu kuchelewa kutembea na siku niliporudi ghafla na kumkuta mwanangu akiwa katika mazingira mabaya.
Pia nilipomshuhudia mke wangu akiteremka kwenye gari na pia siku aliyorudi siku ya pili na kunidanganya kuwa alikuwa kwenye sherehe ya harusi kumbe alikwenda kulala na mwanaume. Na la siku ile nililoshuhudia kwa macho yangu akiwa na mwanaume kama walivyozaliwa katika kitanda changu
