Simu yako ya kwanza ilikuwa ipi?

Simu yako ya kwanza ilikuwa ipi?

Motorola yangu siioni. Wakati huo kampuni ya simu ilikuwa ni tritel baadaye ikaja mobitel
 
Nimeiona pale #7 alcatel, nilienda nayo kijijini nikafikiri imeharibika kumbe hakukuwa na mtandao
 
Mi hapo haipo,yenyewe ilikuwa inaitwa Philips Savy yaani vibration yake ilikuwa matata Sana,kama unachota maji kisimani ikaita unaweza tumbukia,nilikiwaga naipendea ilikuwaga haivungi network,nilipewaga na mama yangu wa kambo wakati naenda shule
 
Nokia flani hivi hazikuwa na laini halafu Nokia jeneza Kisha Siemens a31
 
1539746792595.png
 
Mimi nilianzia hiyo ya kwanza (NOKIA).

Dunia yaenda kasi kiteknolojia miaka kadhaa ijayo huenda zikawepo simu za audio tu yaani unaongea inatype yenyewe meseji(NI IDEA TU).
Wewe tuu ndio hujui kutumia simu mkuu, huko tumeshafika kitambo sana. Ukiwa kwenye eneo lolote unalotype bonyeza alama ya mic anza kuingea na kila kitu kitajoandika mkuu. Kiingereza kinahusika
 
Namba 1, nilipewa nyumbani baada ya kutakiwa kwenda kuripoti form five na sikuwa na mtu wa kunipeleka
 
Nokia 3310 aka jeneza hii niliinunua tzs 110,000 mwaka 2001 kwa duka la simu lililokuwa ndani ya mgahawa unaoitwa Food world ulikuwa pale azikiwe street opposite lps building. Yaani hiyo bei nilichukua ka mkopo ofsini. Haha laini ya simu nilinunua tzs 27,000. Wakati huo voucher was in usd. Hatari kabisa
 
Muhenga mm nilianza na siemens twanga pepeta enzi hizo watoto wajuzi sijui kama wanaijua
Done gumba!
Hiyo Siemens iliwahi nipatia mtoto mkaleeeee wa Kibasila! Daaah! Hatari Sana.
 
Ha ha haa,No 4, wife nilimnunulia No 6 alivyokuwa anaenda Kondoa Hs form 5. Ilikuwa inawashwa w/end hadi w/end! alikuwa bosi kila ikifika w/end anawapangisha foleni mashosti zake kupiga kwao na kwa vichenchede vyao. Misi thoz deiz.
 
Back
Top Bottom