Simu ya milioni 1+ ila unahangaika na bando, utafaidi kweli? Kwanini usinunue simu mid range ya kati halafu hela inayobaki uwekee kwenye bando?

R-K-O

JF-Expert Member
Jun 27, 2023
482
2,138
Walengwa hasa ni wale wanaopata pesa za ghafla (zawadi, kuhongwa, betting, michezo, kuotea, boom la chuoni, n.k) na wale wanaojidunduliza.

kununua simu ni hatua ya kwanza tu, bado kuna mambo yanafuata. ni sawa na gari inabidi ununue kwa kuzingatia ulaji wa mafuta, bei za spare, gharama za mafundi, n.k. ukiparamia na huna pesa ya uhakika utaumia

Hizi simu za kisasa kwa wenzetu huko zinakotengenezwa, mambo ya internet hayanaga kikomo waweza kutumia hata gb 20 kwa siku, ni wewe tu, Kimbembe kipo huku sasa, mpaka leo ni mwendo wa kupimiwa GB,
Yani ukitaka kuiga matumizi ya simu kama huko majuu inabidi uwe na bando lisilo na mawazo ndio utapata raha hata ya teknolojia mpya zilizomo, Vinginevyo utakuwa umevamia mtumbwi wa vibwengo,

Sasa unakuta mtu ananunua simu ya bei kali sana mfano milioni 1 wengine hadi 2

Kwenye matumizi sasa anachofanya ni heri angebaki na simu ya laki 1 hadi 2 maana hata bando tu ni la mawazo.

Kwa usahauri wangu kama unataka ku enjoy hizi simu na uchumi wako si wa kipedeshee, angalia gharama ya simu + bando viwieane.

mfano kama una bajeti ya milioni na unajua kabisa bando linaweza kukupiga chenga, nunua simu ya laki 4 unaweza kupata google pixel nzuri kabisa halafu hio laki 6 wekeza kwenye bando, nenda hata tigo wakupe huduma ya postpaid gb 60 kila mwezi kwa elf 50.

Kama una bajeti ya milioni 2, nunua simu hata ya laki 8 hivi, nenda vodacom wakupe internet isio na kikomo laki 1 kila mwezi, utaenjoy zaidi kuliko kuwa na simu ya milioni 2 alafu bando hata la elf 2 kwa siku linakupiga chenga.
 
Yanawakuta watu wa Dar,kukimbilia kununua ma-range rover halafu mafuta na service changamoto,wanaishia kuyapaki😁
 
Yanawakuta watu wa Dar,kukimbilia kununua ma-range rover halafu mafuta na service changamoto,wanaishia kuyapaki😁
Ni heri ununue hata Premio yako kama una uchumi wa kawaida, mafundi kibao hata wa elf 20 utamkuta, spare hata ya el 50 utaikuta mpaka vijijini,

Jichanganye kwenye hayo ma range sasa, mafundi ni wachache sana utapigwa gharama za ufundi hata milioni 2 na huna pengine pa kukimbilia, spare inaweza kuagizwa na ndege gharama milioni 3 ....lazima ukae,
 
Mtu anunue simu 2m ya pamoja halafu bando la afutatu limishinde? Inawezekana? Alipataje 2m?
Watu wengi sana mkuu, ni hawa wanaopata pesa za ghafla (zawadi, betting, michezo, kuotea, boom la chuoni, n.k) ama wengine wanaodunduliza
 
Ni heri ununue hata Premio yako kama una uchumi wa kawaida, mafundi kibao hata wa elf 20 utamkuta, spare hata ya el 50 utaikuta mpaka vijijini,

Jichanganye kwenye hayo ma range sasa, mafundi ni wachache sana utapigwa gharama za ufundi hata milioni 2 na huna pengine pa kukimbilia, spare inaweza kuagizwa na ndege gharama milioni 3 ....lazima ukae,
Kinachowasumbua ni kutojiamini....
 
Hii inatokea sana, niliwai pewa iPad pro la mwaka 2022 nafikiri, hilo dude halitumii laini, nilijaribu kulihotspot nipo google tu, naingia JF speed inasoma 1.5MBps nikahisi labda kuna update zinafanyika lakini skukuta, nka amini tunda ni za Matajiri.
 
Hii inatokea sana, niliwai pewa iPad pro la mwaka 2022 nafikiri, hilo dude halitumii laini, nilijaribu kulihotspot nipo google tu, naingia JF speed inasoma 1.5MBps nikahisi labda kuna update zinafanyika lakini skukuta, nka amini tunda ni za Matajiri.
Eka opera mini?

Sidhani kama kifaa kikiwa ghali ni lazima kile bando.

Kifaa kikiwa ghali kinakuwa na processor, gpu, ram, storage nzuri kwa ajili ya kufanyia kazi nzito, kama unakesha ku edit video unaweza tumia bando kidogo kuliko mtu mwenye low end anayekesha insta na Youtube.
 
Eka opera mini?

Sidhani kama kifaa kikiwa ghali ni lazima kile bando.

Kifaa kikiwa ghali kinakuwa na processor, gpu, ram, storage nzuri kwa ajili ya kufanyia kazi nzito, kama unakesha ku edit video unaweza tumia bando kidogo kuliko mtu mwenye low end anayekesha insta na Youtube.
Shukran sana mkuu, make lilibaki la kusomea vitabu tu.
 
Back
Top Bottom