Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 97,149
- 137,116
Hivi kama una uhakika binti yako hajabakwa lakini anamsingizia kijana fulani kwa kuwa tu hawaelewani kazini, na kumbuka huyo kijana ni mtuhumiwa tu, utaacha kumtetea huyo kijana kama wewe ni wakili? Au kama una uhakika mkeo ni mwingi na una uhakika yeye ndiye kasababisha kubakwa bado utamtetea? Suala la uwakili na utetezi nadhani linahitaji uelewa mpana kabla Marando hajatuhumiwa na kuonekana mnafiki. :cheer2:
Kwani anapowachana hao watuhumiwa wa ufisadi huwa anawachana kwa misingi gani? Kwa ushahidi gani?
Huyo Marando wenu aache kujifanya ni mwanaharakati mpinga ufisadi halafu mahakamani awatetee hao hao watuhumiwa wa ufisadi.
Machoni mwangu huyo ni mnafiki tu. Sasa unafiki haukatazwi. Ni halali yake kuwa mnafiki na ni haki yangu kumuona yeye ni mnafiki na kutokumpa kura yangu endapo akija kugombea nafasi ya kiuongozi.