Simiyu: Marufuku kula Msibani, mnadani, mahindi ya barabarani

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,462
Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umepiga marufuku isiyokuwa na muda ya watu kula katika misiba, mnadani, magulio pamoja na wanafunzi kuuziwa vyakula mashuleni kutokana na ongezeko la watu waliobainika kupata magonjwa ya mlipuko ya kuharisha, tumbo na kutapika.

Zuio hilo limewekwa jana na Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Yahya Nawanda, ambapo ameeleza kuwa mpaka sasa wagonjwa waliobanika kupatwa na magonjwa hayo wamefika 60 hadi 100.

Kutokana na hali hiyo na ili kuweza kudhibiti ongezeko la wagonjwa, Dkt. Nawanda ameeleza kuwa wameamua kupiga marufuku uuzaji wa vyakula katika magulio, minada mkoa mzima, pamoja na ulaji wa vyakula kwenye misiba.

“ Kuanzia sasa hakuna kupika chakula kwenye minada, magulio, lakini pia ulaji wa chakula kwenye misiba nayo kuanzia sasa tunazuia, tukimaliza kuzika kila mmoja atawanyike, hakuna kula,” amesema Dkt. Nawanda.

Amesema kuwa magonjwa hayo yamebainika kusababishwa na watu kutokuwa na vyoo bora, lakini pia utumiaji wa maji yasiyokuwa safi na salama, ambapo amebainisha wameanzisha oparesheni ya kuwakamata watu wote wasiyokuwa na vyoo.

Pia soma:
- Madai ya Mlipuko wa Kipindupindu Simiyu, RC asema ‘Ni Ugonjwa wa Matumbo, tumewapiga faini Wananchi wasio na vyoo’

- Bariadi yakumbwa na mlipuko wa kipindupindu
 
Simiyu ni mkoa wa Binadamu wa Ajabu Sana,
Wale watu ni wachafu, hawatumii vyoo,
Mtoto asubuhi anazunguka tuu uani anakata gogo...

Hii niliona Bariadi Mjini, sasa najiuliza huko kijijini jee?

Wameendekeza Uchawi, roho mbaya, wizi na ukabila.....
Ni moja ya mikoa unaenda ukitoka hutotamani kukanyaga tena.

Wale watu kule Bado wapo zama za kale.
 
Homa ya matumbo ?! Wana maana ni typhoid au? Sasa mbona wagonjwa wao wanatibiwa kwa kufuata miongozo ya kutibu kipindupimdu??😄😄 Hii ndio Tz.
 
Back
Top Bottom