Simiyu: Ahukumiwa kuchapwa viboko 8 kwa kosa la ubakaji

Mahakama ya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu imemhukumu Boniphace Abel (18) mkazi wa Nyashimba Magu Mkoani Mwanza adhabu ya kuchapwa viboko nane (8) kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 17 na kumsababishia majeraha.

Mbali na adhabu hiyo, Mshtakiwa ametakiwa na Mahakama hiyo kumlipa Mwathirika kiasi cha Sh. 300,000 (Laki tatu) kama fidia kutokana na kitendo alichomfanyia.

Hakimu wa Mahakama hiyo Robert Kaanwa, wakati akitoa hukumu hiyo ameamuru Mshitakiwa kupimwa kwanza Afya yake na Daktari kama anaweza kuhimili adhabu hiyo ya viboko.

Awali, kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Wilaya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Jaston Mhule alielezea Mahakama kuwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(2) vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyo fanyiwa marejeo Mwaka 2022.

Mhule ameeleza kuwa Mshtakiwa akiwa katika msiba wa Babu yake mnamo tarehe 10/07/2023 huko Kijiji cha Mahembe ndani ya Wilaya Itilima alimbaka mhanga mwenye umri wa Miaka 17 na kumsababishia maumivu.

Mhule amesema Sheria inaweza isizungume moja kwa moja muathirika kupewa fidia lakini Mahakama inaweza kuamua hivyo kutokana na kusikiliza pande, ndipo inaweza kuamua fidia au la.

Kifungu cha 131 Kifungu Kidogo cha Pili cha Sheria Kanuni ya Adhabu inaeleza kama mshtakiwa wa kesi ya ubakaji akiwa na umri wa miaka 18 kushuka chini adhabu yake ni viboko tu, idadi ya itategemea na afya ya mhusika.

Mshtakiwa kabla ya kuchapwa viboko inatakiwa afanyiwe vipimo vya afya na Daktari atoe cheti cha kuonesha kuwa kwa idadi vya viboko ambayo amehukumiwa na Mahakama inaweza kumfaa au inatakiwa kupunguziwa adhabu.

Sheria inaeleza mshtakiwa wa ubakaji akiwa na umri wa miaka 19 kuendelea akikutw ana hatia kifungo cha chini ni miaka 30 na inaweza kwenda mbele zaidi ya hapo hadi kuwa kifungo cha maisha.
Mtoto amebakwa mahakama inasema hajabakwa ila amlipe ujira wa uchangudoa! Haikubaliki kitendo cha mahakama kumfundisha mtoto kuwa mwanaume akikuingilia basi ni lazima akulipe pesa ya huduma.
 
nipe elimu,ukweli sijuagi adhabu ya viboko inayoongelewa hutolewaje.

Nielimishe.
Inatolewa Magereza na kuna watu special wamesomea kazi hiyo(inaitwa corporal punishment).

Unanyukwa uchi kwa kuwekewa kitambaa maalumu ili kiboko kisipite na ngozi ya tako huku mikono imefungwa ili usijipapase kupoza maumivu ya mboko!

Kuna fimbo maalumu imetengenezwa kwa ngozi nzito, ukiiona ni nyeusi.

Urefu wake ni kama ft3.5, kwa juu karibu na mshikio ni nene, kadri inavyokwenda nchani unene hupungua na kuwa nyembamba mwishoni, hata apigeje haikatiki, inanesa na kurudia hali yake.

Ukilambwa mboko mbili zinatosha kukumbuka maisha yako yote.

Ndiyo maana wafungwa lazima wachekiwe afya zao kabla ya kutekelezwa kwa adhabu hiyo.

Zinavyopenya kwa maumivu, mtu mzima anaweza kujinyea, kujikojolea ama kutoka roho mazima.
 
Mahakama ya Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu imemhukumu Boniphace Abel (18) mkazi wa Nyashimba Magu Mkoani Mwanza adhabu ya kuchapwa viboko nane (8) kwa kosa la kumbaka mtoto mwenye umri wa miaka 17 na kumsababishia majeraha.

Mbali na adhabu hiyo, Mshtakiwa ametakiwa na Mahakama hiyo kumlipa Mwathirika kiasi cha Sh. 300,000 (Laki tatu) kama fidia kutokana na kitendo alichomfanyia.

Hakimu wa Mahakama hiyo Robert Kaanwa, wakati akitoa hukumu hiyo ameamuru Mshitakiwa kupimwa kwanza Afya yake na Daktari kama anaweza kuhimili adhabu hiyo ya viboko.

Awali, kabla ya hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Wilaya Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Jaston Mhule alielezea Mahakama kuwa Mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na kifungu cha 130(1)(2)e na 131(2) vya Sheria ya Kanuni ya Adhabu Sura ya 16 kama ilivyo fanyiwa marejeo Mwaka 2022.

Mhule ameeleza kuwa Mshtakiwa akiwa katika msiba wa Babu yake mnamo tarehe 10/07/2023 huko Kijiji cha Mahembe ndani ya Wilaya Itilima alimbaka mhanga mwenye umri wa Miaka 17 na kumsababishia maumivu.

Mhule amesema Sheria inaweza isizungume moja kwa moja muathirika kupewa fidia lakini Mahakama inaweza kuamua hivyo kutokana na kusikiliza pande, ndipo inaweza kuamua fidia au la.

Kifungu cha 131 Kifungu Kidogo cha Pili cha Sheria Kanuni ya Adhabu inaeleza kama mshtakiwa wa kesi ya ubakaji akiwa na umri wa miaka 18 kushuka chini adhabu yake ni viboko tu, idadi ya itategemea na afya ya mhusika.

Mshtakiwa kabla ya kuchapwa viboko inatakiwa afanyiwe vipimo vya afya na Daktari atoe cheti cha kuonesha kuwa kwa idadi vya viboko ambayo amehukumiwa na Mahakama inaweza kumfaa au inatakiwa kupunguziwa adhabu.

Sheria inaeleza mshtakiwa wa ubakaji akiwa na umri wa miaka 19 kuendelea akikutw ana hatia kifungo cha chini ni miaka 30 na inaweza kwenda mbele zaidi ya hapo hadi kuwa kifungo cha maisha.
Viboko vya Polisi nasikia ukichapwa viwili ndio wanahesabu kimoja...
 
Utakuta kasshinikizwa, au ni wazazi au walezi au jamii.

Wangapi wadogo kuliko huyo wanalambwa mimba kiulaini na mambo yanaishia kwenye mabaraza ya kifamilia au kijuujuu tu.

Kuna mila Tanzania hii mtoto wa kike alivunja uongo tu kama hajashulikiwa anasakamwa kwao.

Hali kashalika kama mvulana hajaanza kuonesha urijali wake mapema.

Tanzania kesi kama hizo inatakiwa hakimu atumie hekima sana, kuna sheria za dola, kuna sheria za dini na kuna sheria za kimila na zote zinatumika kwa namna moja au nyengine.
Daah, FaizaFoxy tangu nimeanza kukufuatilia humu jamii forum ni leo pekee umeandika jambo la kweli. Hongera sana
 
Hakubaka huyo, wote wanalingana rika, hiyo ni "ashki majnun".

Kiislam hapo litakiwa walambwe viboko wote wawili halafu waowane.

Hao vijana ni afadhali kuliko wale wanaofanya ushoga na kusagana.


Kila siku nazidi kuthibitisha wewe sio mzima.




Kulingana rika ndio ruksa ya kumuingilia mwingine kimwili bila ridhaa yake?


Uislamu unalazimisha mwanamke kuolewa na mbakaji wake Kisa wanalingana umri?


Mahakama za Juvenile kazi yake nini? Magereza ya Juvenile yametengwa kwa ajili ya nani?

Ubakaji ni kosa la jinai, ni kitendo kinachodhuru mwili na afya ya akili. Kubakwa sio starehe ni udhalilishaji.
 
Mtoto amebakwa mahakama inasema hajabakwa ila amlipe ujira wa uchangudoa! Haikubaliki kitendo cha mahakama kumfundisha mtoto kuwa mwanaume akikuingilia basi ni lazima akulipe pesa ya huduma.


Nimeshangaa.

Na hakimu anavimba kabisa eti Mahakama inaweza kuamua alipwe faini na imeamua alipwe shilingi laki 3!

Mtuhumiwa aliebaka na kujeruhi mwili na saikolojia ya binti anachapwa fimbo 8!?

Ange rule tu kwamba Mahakama imeamua kusamehe na sio hii ya panya kung’ata na kupuliza.





Dkt Gwajima D
 
Kila siku nazidi kuthibitisha wewe sio mzima.




Kulingana rika ndio ruksa ya kumuingilia mwingine kimwili bila ridhaa yake?


Uislamu unalazimisha mwanamke kuolewa na mbakaji wake Kisa wanalingana umri?


Mahakama za Juvenile kazi yake nini? Magereza ya Juvenile yametengwa kwa ajili ya nani?

Ubakaji ni kosa la jinai, ni kitendo kinachodhuru mwili na afya ya akili. Kubakwa sio starehe ni udhalilishaji.
Hawajabakana hao, hata hakimu kaliona hilo. Usifikiri hakimu aliyeamuwa achapwe viboko ni mjinga.
 
Utakuta tofauti ni miezi michache tu ya kuzaliwa.


Haijalishi hata wangepishana masaa tu!


Kumwingilia mwingine kimwili bila ridhaa yake ni ubakaji na ubakaji ni kosa la jinai.

Kamwingilia kimwili na kusababisha majeruhi ya mwili na afya ya akili.

Sio Sawa.
 
Inatolewa Magereza na kuna watu special wamesomea kazi hiyo(inaitwa corporal punishment).

Unanyukwa uchi kwa kuwekewa kitambaa maalumu ili kiboko kisipite na ngozi ya tako huku mikono imefungwa ili usijipapase kupoza maumivu ya mboko!

Kuna fimbo maalumu imetengenezwa kwa ngozi nzito, ukiiona ni nyeusi.

Urefu wake ni kama ft3.5, kwa juu karibu na mshikio ni nene kadri inavyokwenda nchani unene hupungua na kuwa nyembamba mwishoni, hata apigeje haikatiki, inanesa na kurudia hali yake.

Ukilambwa mboko mbili zinatosha kukumbuka maisha yako yote.

Ndiyo maana wafungwa lazima wachekiwe afya zao kabla ya kutekelezwa kwa adhabu hiyo.

Zinavyopenya kwa maumivu, mtu mzima anaweza kujinyea, kujikojolea ama kutoka roho mazima.
Du!mbona inatisha
 
Hawajabakana hao, hata hakimu kaliona hilo. Usifikiri hakimu aliyeamuwa achapwe viboko ni mjinga.


Ni mjinga wa makusudi kabisa.


Hakuna tendo la “kubakana” , ni kubaka na kubakwa.

Kubaka ni kosa la jinai. Kudhuru mwili ni kosa la jinai.


Nimekuuliza Uislamu unaagiza binti kuolewa na mbakaji wake?
 
Hakubaka huyo, wote wanalingana rika, hiyo ni "ashki majnun".

Kiislam hapo litakiwa walambwe viboko wote wawili halafu waowane.

Hao vijana ni afadhali kuliko wale wanaofanya ushoga na kusagana.
Mbona unaanza kuongea ujinga Sasa... so Bora mwanamke abakwe....acha kutuletea dini zako ambazo zinamchukulia mwanamke Kama ng'ombe
 
Inatolewa Magereza na kuna watu special wamesomea kazi hiyo(inaitwa corporal punishment).

Unanyukwa uchi kwa kuwekewa kitambaa maalumu ili kiboko kisipite na ngozi ya tako huku mikono imefungwa ili usijipapase kupoza maumivu ya mboko!

Kuna fimbo maalumu imetengenezwa kwa ngozi nzito, ukiiona ni nyeusi.

Urefu wake ni kama ft3.5, kwa juu karibu na mshikio ni nene kadri inavyokwenda nchani unene hupungua na kuwa nyembamba mwishoni, hata apigeje haikatiki, inanesa na kurudia hali yake.

Ukilambwa mboko mbili zinatosha kukumbuka maisha yako yote.

Ndiyo maana wafungwa lazima wachekiwe afya zao kabla ya kutekelezwa kwa adhabu hiyo.

Zinavyopenya kwa maumivu, mtu mzima anaweza kujinyea, kujikojolea ama kutoka roho mazima.
Wanafunzi wa siku hizi kitu kama viboko wanaweza kuona kama ni mwisho wa dunia. Tuliosoma siku za nyuma viboko ilikuwa na ndiyo maisha. Na unachapwa matakoni na fimbo kubwa. Mwalimu anatumia nguvu zote.
 
Nimeshangaa.

Na hakimu anavimba kabisa eti Mahakama inaweza kuamua alipwe faini na imeamua alipwe shilingi laki 3!

Mtuhumiwa aliebaka na kujeruhi mwili na saikolojia ya binti anachapwa fimbo 8!?

Ange rule tu kwamba Mahakama imeamua kusamehe na sio hii ya panya kung’ata na kupuliza.





Dkt Gwajima D
Mkuu hatujawasikiliza wahusika huyo kijana wa kiume na binti. Mi sidhani kama hakimu ni mpuuzi kutoa adhabu hiyo ambayo nadhani wewe unaona haifai kwa hilo kosa naamini kuna mazingira fulani hakimu aliyashtukia kwenye maelezo ya hao madogo.

Nakwambia hivi kwasababu mimi kwenye utoto wangu around miaka 16 kuna mama mmoja alinikuta kwake na binti yake nae umri huo huo alivyokuja kusema kwa wazazi wangu alimpanga mwanae aseme nilimlazimisha huku tulikubaliana ( halafu nilikuwa mrefu kabinti kadogo dogo unaweza kuamini yaani) sijui walimalizana vipi na wazazi wangu baadae ila nahisi alitaka kuomba hela.

Sent from my M10_Max using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom