Aliyeachiwa kwa msamaha wa Rais ahukumiwa miaka 30 jela

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,304
JOHN Chibuga (31), mkazi wa Kijiji cha Bugolola wilayani Ukerewe, mkoani Mwanza, ambaye Desemba 9, mwaka jana aliachiliwa kwa msamaha wa Rais, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kukutwa na kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Aidan Nziku, alidai kuwa Chibuga alimvamia Mdala Mangu (34), mkazi wa Ukerewe akiwa nyumbani kwake na kumkata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kuiba simu ya mkononi na kukimbia.

Hukumu hiyo ilitolewa Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe, Lucas Nyahega, aliyesema kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani huko haukutia shaka, mshtakiwa alitenda kosa hilo kwa kukusudia na hivyo mahakama inamhukumu kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30.

Awali Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nziku akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 15, 2023 katika Kijiji cha Kakerege, wilayani Ukerewe.

Alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa la namna hiyo kwa mara ya pili ambapo awali alihukumiwa kwa kosa la kuvunja duka usiku na kuiba, hivyo kutiwa hatiani na Mahakama ya Mwanzo Nansio kisha kuachiliwa huru Desemba 9, 2023 kwa msamaha wa Rais.

Alidai kosa hilo la unyang'anyi wa kutumia silaha ni kinyume cha kifungu namba 287(A) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 (2022), hivyo kuiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi yake ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Mshtakiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kutokana na kosa linalomkabili, aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hakuwa na fedha ya kujikimu baada ya kutoka gerezani, ndiyo sababu ya kupora.

Source - Nipashe
 
Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Aidan Nziku, alidai kuwa Chibuga alimvamia Mdala Mangu (34), mkazi wa Ukerewe akiwa nyumbani kwake na kumkata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kuiba simu ya mkononi na kukimbia.

Mahakama zingekuwa zinatoa adhabu sawasawa na mtuhumiwa alivyotenda...

Kama huyu wa kukata wenzake na mapanga, ilibidi ahukumiwe kucharangwa mapanga + kifungo...
 
Alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa la namna hiyo kwa mara ya pili ambapo awali alihukumiwa kwa kosa la kuvunja duka usiku na kuiba, hivyo kutiwa hatiani na Mahakama ya Mwanzo Nansio kisha kuachiliwa huru Desemba 9, 2023 kwa msamaha wa Rais.
Kwanza ilikuwajw huyu akaachiwa huru kwa kosa hilo na akiwa bado kijana?

Au kijana wa Kada?
 
Mahakama zingekuwa zinatoa adhabu sawasawa na mtuhumiwa alivyotenda...

Kama huyu wa kukata wenzake na mapanga, ilibidi ahukumiwe kucharangwa mapanga + kifungo...
ndio utaona umuhimu wa Sharia hapo.
Sharia ndio suluhisho la matatizo ya binadamu,kisiasa,kiuchumi,kijamii n.k
 
Wafungwa ni watu na wanamahitaji ya kiutu hivyo ni lazima waandaliwe namna ya kuishi uraiani, Kenye wanawafundisha ufundi na kuwapa vifaa vya kuanzia maisha kama vile cherehani na vitambaa, useremala, fundi bomba na fundi magari, yote hayo hufanyika wakiwa jela hivyo akitoka anao uhakika wa kuendelea na maisha yake.
 
Wafungwa ni watu na wanamahitaji ya kiutu hivyo ni lazima waandaliwe namna ya kuishi uraiani, Kenye wanawafundisha ufundi na kuwapa vifaa vya kuanzia maisha kama vile cherehani na vitambaa, useremala, fundi bomba na fundi magari, yote hayo hufanyika wakiwa jela hivyo akitoka anao uhakika wa kuendelea na maisha yake.
Hakuna justification ya wizi,wizi ni tabia ya mtu,unaweza kukuta mtu ana milioni moja mfukoni ila akaiba buku ya mwenzake ndani ya Dala Dala,

Mbona mtaani wengi tu hawakuandaliwa wala hawana huo ujuzi ila wanatafuta maisha kwa njia ya halali tu,halafu sio kila mwenye ujuzi ana kazi ya kufanya,wau wanahangaika kutafuta ajira kila siku hata humu JF.
 
JOHN Chibuga (31), mkazi wa Kijiji cha Bugolola wilayani Ukerewe, mkoani Mwanza, ambaye Desemba 9, mwaka jana aliachiliwa kwa msamaha wa Rais, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kukutwa na kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Aidan Nziku, alidai kuwa Chibuga alimvamia Mdala Mangu (34), mkazi wa Ukerewe akiwa nyumbani kwake na kumkata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kuiba simu ya mkononi na kukimbia.

Hukumu hiyo ilitolewa Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe, Lucas Nyahega, aliyesema kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani huko haukutia shaka, mshtakiwa alitenda kosa hilo kwa kukusudia na hivyo mahakama inamhukumu kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30.

Awali Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nziku akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 15, 2023 katika Kijiji cha Kakerege, wilayani Ukerewe.

Alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa la namna hiyo kwa mara ya pili ambapo awali alihukumiwa kwa kosa la kuvunja duka usiku na kuiba, hivyo kutiwa hatiani na Mahakama ya Mwanzo Nansio kisha kuachiliwa huru Desemba 9, 2023 kwa msamaha wa Rais.

Alidai kosa hilo la unyang'anyi wa kutumia silaha ni kinyume cha kifungu namba 287(A) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 (2022), hivyo kuiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi yake ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Mshtakiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kutokana na kosa linalomkabili, aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hakuwa na fedha ya kujikimu baada ya kutoka gerezani, ndiyo sababu ya kupora.

Source - Nipashe
Mshtakiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kutokana na kosa linalomkabili, aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hakuwa na fedha ya kujikimu baada ya kutoka gerezani, ndiyo sababu ya kupora.
 
JOHN Chibuga (31), mkazi wa Kijiji cha Bugolola wilayani Ukerewe, mkoani Mwanza, ambaye Desemba 9, mwaka jana aliachiliwa kwa msamaha wa Rais, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kukutwa na kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Aidan Nziku, alidai kuwa Chibuga alimvamia Mdala Mangu (34), mkazi wa Ukerewe akiwa nyumbani kwake na kumkata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kuiba simu ya mkononi na kukimbia.

Hukumu hiyo ilitolewa Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe, Lucas Nyahega, aliyesema kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani huko haukutia shaka, mshtakiwa alitenda kosa hilo kwa kukusudia na hivyo mahakama inamhukumu kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30.

Awali Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nziku akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 15, 2023 katika Kijiji cha Kakerege, wilayani Ukerewe.

Alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa la namna hiyo kwa mara ya pili ambapo awali alihukumiwa kwa kosa la kuvunja duka usiku na kuiba, hivyo kutiwa hatiani na Mahakama ya Mwanzo Nansio kisha kuachiliwa huru Desemba 9, 2023 kwa msamaha wa Rais.

Alidai kosa hilo la unyang'anyi wa kutumia silaha ni kinyume cha kifungu namba 287(A) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 (2022), hivyo kuiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi yake ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Mshtakiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kutokana na kosa linalomkabili, aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hakuwa na fedha ya kujikimu baada ya kutoka gerezani, ndiyo sababu ya kupora.

Source - Nipashe
Jela ni eneo la wasio na fedha
 
JOHN Chibuga (31), mkazi wa Kijiji cha Bugolola wilayani Ukerewe, mkoani Mwanza, ambaye Desemba 9, mwaka jana aliachiliwa kwa msamaha wa Rais, amehukumiwa kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya kukutwa na kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha.

Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Aidan Nziku, alidai kuwa Chibuga alimvamia Mdala Mangu (34), mkazi wa Ukerewe akiwa nyumbani kwake na kumkata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili wake kisha kuiba simu ya mkononi na kukimbia.

Hukumu hiyo ilitolewa Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama ya Wilaya ya Ukerewe, Lucas Nyahega, aliyesema kuwa ushahidi uliotolewa mahakamani huko haukutia shaka, mshtakiwa alitenda kosa hilo kwa kukusudia na hivyo mahakama inamhukumu kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30.

Awali Mwendesha Mashtaka wa Serikali Nziku akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo, alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Desemba 15, 2023 katika Kijiji cha Kakerege, wilayani Ukerewe.

Alidai kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa la namna hiyo kwa mara ya pili ambapo awali alihukumiwa kwa kosa la kuvunja duka usiku na kuiba, hivyo kutiwa hatiani na Mahakama ya Mwanzo Nansio kisha kuachiliwa huru Desemba 9, 2023 kwa msamaha wa Rais.

Alidai kosa hilo la unyang'anyi wa kutumia silaha ni kinyume cha kifungu namba 287(A) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura 16 (2022), hivyo kuiomba mahakama hiyo kutoa adhabu kali dhidi yake ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Mshtakiwa huyo alipopewa nafasi ya kujitetea kutokana na kosa linalomkabili, aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa hakuwa na fedha ya kujikimu baada ya kutoka gerezani, ndiyo sababu ya kupora.

Source - Nipashe
80% ya wanao samehewa wanarudia uhalifu.
Gerezani wanajifunza mbinu za kushi nda kesi, mbinu za uhalifu na mbinu a mauaji.
 
Back
Top Bottom