Victoire
JF-Expert Member
- Jul 4, 2008
- 24,143
- 56,606
Silvio aliwahi kumiliki team ya AC Milan. Kwa kipindi chake AC Milan ilikuwa ya moto.
======
Aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Italia, Silvio Berlusconi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 86. Nguli huyo kwenye tasnia ya habari ameongoza Serikali tatu za Italia kutoka mwaka 1994 mpaka 2011 ambapo chama chake cha Forza kipo kwenye muungano unaoongoza nchi kwa sasa.
Berlusconi aliweza kurejesha jina lake kwenye siasa pamoja na kukumbwa na kashfa za ngono, rushwa pamoja na ukwepaji kodi.
Silvio amefariki katika hospitali ya Raffaele mjini Milan ambapo amekaa wiki sita akitibiwa maambukizi kwenye mapafu ambapo kabla hajapokelewa alikuwa pia na ugonjwa wa kansa ya damu.
Amezaliwa jijini Milan mwaka 1936 kwenye familia ya kipato cha kati na alijikita kwenye uwekezaji wa majengo wakati akianza biashara kabla ya kwenda kuanzisha kampuni ya Mediaset, chombo binafsi kikubwa zaidi cha habari nchini Italia, pia akamiliki timu ya AC Milan kuanzia mwaka 1986 mpaka 2017.
Chama cha Forza Italia kilianzishwa mwaka 1993 na mwaka mmoja baadae Berlusconi akawa waziri mkuu wa kwanza kupitia chama hicho bila kuwa na rekodi yoyote ya kuendesha ofisi ya Serikali. Silvio alilazimika kujiuzulu mwaka 2011 kutokana na mgogoro wa madeni
======
Aliyewahi kuwa waziri mkuu wa Italia, Silvio Berlusconi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 86. Nguli huyo kwenye tasnia ya habari ameongoza Serikali tatu za Italia kutoka mwaka 1994 mpaka 2011 ambapo chama chake cha Forza kipo kwenye muungano unaoongoza nchi kwa sasa.
Berlusconi aliweza kurejesha jina lake kwenye siasa pamoja na kukumbwa na kashfa za ngono, rushwa pamoja na ukwepaji kodi.
Silvio amefariki katika hospitali ya Raffaele mjini Milan ambapo amekaa wiki sita akitibiwa maambukizi kwenye mapafu ambapo kabla hajapokelewa alikuwa pia na ugonjwa wa kansa ya damu.
Amezaliwa jijini Milan mwaka 1936 kwenye familia ya kipato cha kati na alijikita kwenye uwekezaji wa majengo wakati akianza biashara kabla ya kwenda kuanzisha kampuni ya Mediaset, chombo binafsi kikubwa zaidi cha habari nchini Italia, pia akamiliki timu ya AC Milan kuanzia mwaka 1986 mpaka 2017.
Chama cha Forza Italia kilianzishwa mwaka 1993 na mwaka mmoja baadae Berlusconi akawa waziri mkuu wa kwanza kupitia chama hicho bila kuwa na rekodi yoyote ya kuendesha ofisi ya Serikali. Silvio alilazimika kujiuzulu mwaka 2011 kutokana na mgogoro wa madeni