Hali ya uchumi alipoingia Alhaj ilikuwa mbaya kweli, lakini unapotaka kufanya chochote kuna vitu vya msingi , na vingine ni vile vinavyo imarisha vitu vya msingi, na niliwahi kuongea na mtu moja ambaye ni swahiba/rafiki/ndugu wa alhaj ambaye ni mtu wa system mpaka leo, yeye alilalamika rukhsa ya mwinyi ambayo haikuwa na taratibu, yaani mambo yanajiendea holela holela.
Sasa nikirudi kwenye suala la uchumi wakati Alhaji anaingia ndio ulikuwa na mapungufu yake na hata mwalimu alisema yeye hakuwa malaika au hakukosea, sasa nini kilicho takiwa kufanywa na Alhaji, ni kujaribu kuondoa au kupunguza mapungu yalio tokea huko nyuma, nayo ni ya management za haya mashirika ambayo yalikula taji na mapungufu mengine. madhali yalionekana na mimi na wewe ni wazi na yeye na viongozi wake waliyaona. sasa ni ilitakiwa kifanyike, moja ilitakiwa kufanyika semina elekezi kwa viongozi wa hayo mashirika na makatibu wakuu na mawaziri kuwaelezea nini kinachotarajiwa toka kwao na faida ya kusimamia vizuri mashirika yalio chini ya wizara zao, kubadili mfumo wa uteuzi wa Bodi members, na kuachana na kuweka rafiki/shemeji nk wa kwenda kukuleta pororo.
Kupunguza mzigo wa kiuongozi kwa serikali/raisi angeongeza nguvu kwa bunge kuwa-grill viongozi wa haya mashirika kuhusu matokeo ya biashara zao, na pale walipo hiyaji kuuza iwe nyumba nk wange fanya tathimi ya njia bora ya kutekeleza hiyo sera. na kwa kuwa tulikuwa tunaelekea kwenye soko huria iwe soko la mitaji nk , basi wange ya tayarisha vizuri haya mashirika kufika huko na hata kutuwekea watanzania wote mazingira mazuri ya kununua hizo shares panapo majaliwa, iwe ni kiongozi au mtanzania wa kawaida.
Lakini kilicho fanyika kipindi cha mzee ruksa ni mipango ya siku hadi siku, badala ya kuwa na mikakati ya muda mrefu.
Na kwa kuwa wewe naelewa unajua Management basi ni vizuri sisi sote tukajikita katika ile pyramid ya Management na aina ya mikakati ya kila moja.
Top Management 5 to 10 to 20 years
Middle management 1 year to 5 years
Operational level ni daily.
Lakini kilicho fanyika na Top management Yetu ( Baraza la Mawaziri ) ni kufanya Operational level decision, kwamba unauza shirika bila kujua baada ya hapo nini kitatokea, yaani hawakufanya Socio-economic impact assesment na ku-control hizo after effects za matokeo ya maamuzi yao, in short waliangalia maslahi binafsi zaidi kuliko ya nchi.
Hivyo ndio kosa la Mzee ruksa lilipo na litaendelea kutula mpaka atakapo tokea Dikteta moja akarekebisha hali.