Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Kwa wale ambao tulikuwepo Tz enzi hizo, mafisadi walikuwepo atra enzi za AD tatizo ni kuwa Tz ilikuwa na chama kimoja hivo Kina dr Slaa wasingekuwa na nafasi ya kuwaweka wazi mafisadi.

Na vilevile Tz magazeti yote yalikuwa yanamilikiwa na serikali au chama. Mtu yeyote ambae anasema kuwa it was better then than now, is kidding him/herself...Mwinyi alifanya la maana kuondoa AD neema taratibu ikaanza rudi TZ tukaacha kukimbiza magari ya ugawaji na unga wa Yanga. Tz ilikuwa na chuo kikuu Kimoja tu shule nyingi hazikuweza kupeleka watoto Sekondari sababu hazikuwepo wenye uwezo wakawapeleka Kenya au Uganda...sasa nchi gani hii ilikuwa Mwalimu alitufikisha pabaya economically na ki fikra vilevile...Wote wazee wenzangu tulikuwa tunaimbishwa shuleni ili tuendelee tunahitaji vitu vinne watu, ardhi siasa safi na uongozi bora. Obviously what was lacking ni Siasa safi na uongozi bora kuanzia kwake Mwalimu.

Ila kwa kuwa alikuwa mwelewa mwalimu alingatuka maana mambo yalikuwa hayawezekani hata IMF waligoma kutu-bail out he had no way out...

Ila big up katika kuyaweka makabila karibu na kuleta mshikamano TZ.

Buriani Ujamaa Buriani Azimio, watanzania hatutaki hayo tena ila ni historia yetu.

Nawakilisha
 
Inaoenekana kuna watu wanabisha sana humu japo hawajasoma Azimio la Arusha. Ndio maana limechapishwa upya ili mlisome. Azimio linalenga kujitegemea kuanzia ngazi ya mtu binafsi, familia, mtaa/kijiji, wilaya, mkoa hadi Taifa. Ni mwongozo thabiti wa nchi yetu.

Companero leo hii unajitegemea kwa sababu ya Azimio la Arusha? na kwa wale wasiofanya kazi tuwa-support kwa sababu AD limeuliwa na Mwinyi?

Yaani hatuwezi kujitegemea mpaka watu fulani wakae kikao waamue tujitegemee, hamuoni tatizo hapo!kuna tatizo la kutatua kabla ya kufika kwenye hiyo level ya kujitegemea, kama ni kubwa kiasi hicho!
 
Halafu kwa nini watu wengine wanaongea kana kwamba wao ndio wawakilishi wa Watanzania wote, kana kwamba wao ndio wanajua sisi wananchi tunataka nini? Hii mijadala ya Azimio ni ishara kuwa kuna Watanzania wengi tu tunataka lirejee. Ndio maana hawa kina Sumaye na Mwinyi wanaanza kulizungumzia pia - wamesoma ishara za nyakati. Na wananchi tumelichapisha na kulisoma upya ili tujue siri ya mwelekeo wa nchi hii. Huu ni mwamko wa aina yake. Watu tumegundua tumepotea njia. Sasa tumeamua kuyarejea mapito ya kale, tuangalie wapi tumeanguka, tunyanyuke, tujifute mavumbi na kuifuata njia iliyo sahihi na tuwe na mwelekeo thabiti wa kuelekea Egalite. Hivi wengine hamjalichoka tu Azimio la MKUKUTA?
 
Haiwezekani ukaongelea kujitegema kama taifa bila individual kuwa na input, watu wanaojenga taifa ni watu ni raia ni mmoja mmoja, sielewi unavyotaka kutenganisha kujitegema kwa taifa na mtu mmoja mmoja

Lingine ni kuwa hivi tusingetangaza AD basi tungekuwa ombaomba na kutegemea nchi za watu? Je leo hii JK anyooomba omba anafanya hivyo kwa sababu azimio la arusha lilikufa? . Kujitegemea is not human responsibility anymore katika planet hii, unataka kusema waasisi wa kujitegemea walifanya hivyo kwa sababu hatukuwa na mind ya kujitegemea muda huo? Misada mingapi tulipokea kipindi tunaishi katika azimio la Arusha? kuna fedha tulizikataa kwa sababu tunajitegemea?

Baaada ya kuelimika nykatai hizi still watu wanaenda kuombaomba, no innovations, no research, no what, simply kwa sababu hakuna AD anymore?

Unataka ku-blame wengine kwa failure zetu, maana naona ushaanza kutaja watu wa nje! Africa nzima tulikuwa na maadui?? na hao wakorea tulikokuwa nao sawa kiuchumi mwaka 1961 walitumia siasa gani kuwafikisha walipo leo?

Ukiingiza siasa za mataifa ya nje kuwa walichangia kwa sisi kutoendelea ndipo unapomsafisha Mwinyi!

ATC is dying today simply because AD is not there! TUTAFUTE MATATIZO MENGINE TULIYONAYO si kwa sababu hatuna AD!

Sijaelewa ni wapi nimeongelea mambo ya mtu mmojammmoja. Kuna tatizo hapa la kung'ang'aniza hoja hapa. Sijasema popote hapa kwamba siasa ya ujamaa na kujitegemea ilifaulu (rejea post yangu iliopita). Kuna mapungufu mengi yalijitokeza kutokana na sababu mbalimbali.

Ku-ignore influence ya mataifa ya nje kwa siasa za enzi zile ni sawa na ku-ignore existence of cold war. Sitaenda huko maana it is obvious, unless kaa mtu anataka kwa hiari yake mwenyewe kujisahaulisha au kukataa lkuuona ukweli. Kumbuka kuwa Tz ilikuwa ni nchi changa, na kufuata kwake siasa zile zinazokingana na mangaribi ilikuwa ni kujipalia makaa kichwani. Pia Tz ilijitwisha jukumu zito la ukombozi kusini mwa AFrika, ingawa tunaona leo hii hawa watu tuliowasaidia kwa damu ya wapiganaji wetu, hali, na mali (pamoja na umaskini wetu) wametutupa mkono na kusahau that we even exist.
 
Bw. Waberoya umeuliza mafanikio ya AD.

Kuu ktk hilo ni njia kuu za kiuchumi kumilikiwa na umma. Hakuna mambo ya nyang'au mmoja kwenda kwenda kusaini mikataba ya ki-Chifu Mangungo London halafu bungeni mnaambiwa si ruksa kuuona!. Pia uzalendo ulikuwa A++ kwa mtu. Morali ya kuipenda nchi ilikuepo. Pia kuondoa influence ya siasa kwenye utendaji wa kiserikali kwa kueliminate ujinga wa vyama vya siasa.

With time kaa mambo yangeenda vile inavotakikana, keki ya taifa ingegaiwa based on the needs na utaalam na sio lobbies za kisiasa na watu kujenga mabarabara na maji ya bomba hadi kijijini kwao, wakati mikoa mingine haijaunganishwa hata na barabara za vumbi achilia mbali wananchi wengine wanakunywa maji na mifugo yao ktk chanzo kimoja.
 
"Kujitegemea kwa mtu mmoja ni kujitegemea kwa nyumba kumi. Kujitegemea kwa nyumba zote kumi za balozi ni kujitegemea kwa tawi zima. Kujitegemea kwa matawi ni kujitegemea kwa Wilaya ambayo ni kujitegemea kwa Mkoa. Kujitegemea kwa Mikoa yote ni kujitegemea kwa Taifa lote ambalo ndilo lengo letu." - Azimio la Arusha

Comp, Azimio la Arusha Lilizinduliwa 1967 mpaka hapo inapodaiwa kuwa lilifutwa, ni hatua ipi ya kujitegemea liliwafikisha Watanzania, kati ya hizo ulizotaja?
 
Halafu kwa nini watu wengine wanaongea kana kwamba wao ndio wawakilishi wa Watanzania wote, kana kwamba wao ndio wanajua sisi wananchi tunataka nini? Hii mijadala ya Azimio ni ishara kuwa kuna Watanzania wengi tu tunataka lirejee. Ndio maana hawa kina Sumaye na Mwinyi wanaanza kulizungumzia pia - wamesoma ishara za nyakati. Na wananchi tumelichapisha na kulisoma upya ili tujue siri ya mwelekeo wa nchi hii. Huu ni mwamko wa aina yake. Watu tumegundua tumepotea njia. Sasa tumeamua kuyarejea mapito ya kale, tuangalie wapi tumeanguka, tunyanyuke, tujifute mavumbi na kuifuata njia iliyo sahihi na tuwe na mwelekeo thabiti wa kuelekea Egalite. Hivi wengine hamjalichoka tu Azimio la MKUKUTA?

Kaka nadhani uko kwenye position nzuri ya kuwaaminisha watu kuhusu Azimio,acha hizo politics zingine, kama leo unaona kuna member JF anasema kama anawawakilisha watanzania wote basi tumeshindwa hoja! sidhani kama tumefika kuwa eti Mwinyi, Sumaye, sijui nani wakisema turudi kwenye azimio la Arusha, watu 'watapanda' magari na kwenda Arusha,

is AD systems at work or talks at work?

Kujitegemea ni vitendo siyo mahubiri, ili watu wafanye kazi weka system za watu kufanya kazi siyo kutangaziana kuwa huu ni muda wa kujitegemea! what a shame!

JKN alianzisha hiyo ujamaa yake akiwa na masters tu na courage na uchungu wa wa taifa lake, leo hii tuna maprofesa wa kweli na wa uongo, still people are thinking of going back in 60s, jamani hamuoni kuna tatizo!

Tukikosea, AD itageuka dini nyingine na Nyerere atageuka nabii au mtume! kuwa watu fulani wako tayari kufuata chochote kile ambacho huwezi hata kuki-evaluate simply ka sababu Mwinyi anasema turudi huko

waamini wa AD wameshindwa ku-convince watu kuwa dunia ya leo tunaishi tofauti kivipi na KUJITEGEMEA? sheria zipo na watu wanajitegemea what else do we need? Kama AD it was an ideology lazima liwe accepted na watu wote, ni wote walilikubali Azimio au kwa sababu Nyerere alisema na ''wakasema zidumu fikra sahihi za Mwenyekiti'' wangapi ni waislamu na wakristo na still they dont follow their religions?

kwa nini watu mnataka kusema AD was powerful than laws na magereza? which is superior here, AD siyo wote watalitaka is theory, concepts, declaration, which there was no law to make it effective! SHERIA inaheshimiwa na kila mtu ukikosea tu jela, WHICH IS SUPERIOR BTN laws and AD. watu hata tunaowajua kabisa wenzi hawaendi mahakamini hivi leo hili hali tunasheria mtu bado anaamini tukilitangaza Azimio basi watu wote watakuwa walokole na masheikh safi swala tano!

Unless kuwa mtu aseme Nyerere aliona watanzania wote wavivu na ili kuwaamsha inabidi tuwatangazie hili azimio,

Nadhani mnakoenda mnataka tuseme AD lilikuwa tusi kwa watanzania, yaani babu zetu walikuwa hawalimi na kujitegema mpaka tutangaziwe?

I believe this is a right place to revisit this AD and see how actually it make sense

I insist watanzania tuna matatizo mengine ambayo inabidi kuyatatua kwa njia nyingine nyingi na sio kusema eti azimio la Arusha! tuaandamana nchi nzima na kusema karibu Azimio karibu mwana mpotevu! tutahubiri kila kona! kama ni maneno tu na sio systems than let me declare again, litakuwa limeshakufa tena!

Sijaelewa ni wapi nimeongelea mambo ya mtu mmojammmoja. Kuna tatizo hapa la kung'ang'aniza hoja hapa. Sijasema popote hapa kwamba siasa ya ujamaa na kujitegemea ilifaulu (rejea post yangu iliopita). Kuna mapungufu mengi yalijitokeza kutokana na sababu mbalimbali.

Ku-ignore influence ya mataifa ya nje kwa siasa za enzi zile ni sawa na ku-ignore existence of cold war. Sitaenda huko maana it is obvious, unless kaa mtu anataka kwa hiari yake mwenyewe kujisahaulisha au kukataa lkuuona ukweli. Kumbuka kuwa Tz ilikuwa ni nchi changa, na kufuata kwake siasa zile zinazokingana na mangaribi ilikuwa ni kujipalia makaa kichwani. Pia Tz ilijitwisha jukumu zito la ukombozi kusini mwa AFrika, ingawa tunaona leo hii hawa watu tuliowasaidia kwa damu ya wapiganaji wetu, hali, na mali (pamoja na umaskini wetu) wametutupa mkono na kusahau that we even exist.

Asante mkuu, nimekupata

Umenifurahisha kuwa tuna sababu nyingi mno za sisi kuwa hivi leo tulivyo na sio kutaka kumtwisha mzigo Mwinyi!

Asante
 
Asante mkuu, nimekupata

Umenifurahisha kuwa tuna sababu nyingi mno za sisi kuwa hivi leo tulivyo na sio kutaka kumtwisha mzigo Mwinyi!

Asante

Sijakuelewa!

Hiyo conclusion yako unaipata kutoka wapi kuwa Mwinyi hakuhusika?

Just curious.
 
Bw. Waberoya umeuliza mafanikio ya AD.

Kuu ktk hilo ni njia kuu za kiuchumi kumilikiwa na umma. Hakuna mambo ya nyang'au mmoja kwenda kwenda kusaini mikataba ya ki-Chifu Mangungo London halafu bungeni mnaambiwa si ruksa kuuona!. Pia uzalendo ulikuwa A++ kwa mtu. Morali ya kuipenda nchi ilikuepo. Pia kuondoa influence ya siasa kwenye utendaji wa kiserikali kwa kueliminate ujinga wa vyama vya siasa.

With time kaa mambo yangeenda vile inavotakikana, keki ya taifa ingegaiwa based on the needs na utaalam na sio lobbies za kisiasa na watu kujenga mabarabara na maji ya bomba hadi kijijini kwao, wakati mikoa mingine haijaunganishwa hata na barabara za vumbi achilia mbali wananchi wengine wanakunywa maji na mifugo yao ktk chanzo kimoja.

Siwezi kusema kila shirika lililokufa kipindi hicho! wala sitasema kuhusu General tyre, ATC, TRL na Kiwira leo hii, sitasema waliokuwa migodi ya serilikari, vifaa vikiharibika vinavyochukua hata mwaka kuwafikia walengwa ! sitasema hayo that will be long topic

Abdul, to sum up which is superior between Laws, Katiba, and AD?

Ukinipa jibu hapo nipe tofauti kati ya dini na AD! maana naona zote ni beliefs

Tatu oanisha AD na operation Sangara (OS) ya Chadema.

OS inasema CCM mafisadi na tuiondoe, AD declaration ni 'kama' inasema watanzania wavivu na wabinafsi tufanye kazi na kuwa wazalendo!

Haihitaji AD ili niwapende na kuwa na uzalendo na raia wangu, wala haihitaji AD ili niwe mchapa kazi!

Nimesema tena, kama sheria nakatiba haziwezi kufanya kazi basi AD wala tusiifikires ni mahubiri tu, unless mtu leo aseme sheria na katiba tulizo nazo zinaruhusu wizi wa mali za umma na uvivu!
AD has no power ya kumbadilisha mtu, afadhai uhubiri wokovu wa Bwana Yesu au dini safi ya Mtume na siyo AD!

Katiba na sheria ni superior 'utake usitake' ukikosea jela, thats why experince shows human must be ruled out by laws and laws alone.

Sorry to say, Abdu, siamini kuwa ili uwe mzalendo na nchi hii mpaka utangaziwe azimio, tunajitukana !

Sorry agaian to say, kuwa ubinafsi, uvivu, anasa., tamaa za haraka, maisha ya kujionyesha, njia za mkato, wizi, n.k ndio vimaetufanya tuwe hivi tulivyo hivi leo!
 
Kwa wale ambao tulikuwepo Tz enzi hizo, mafisadi walikuwepo atra enzi za AD tatizo ni kuwa Tz ilikuwa na chama kimoja hivo Kina dr Slaa wasingekuwa na nafasi ya kuwaweka wazi mafisadi. Na vilevile Tz magazeti yote yalikuwa yanamilikiwa na serikali au chama. Mtu yeyote ambae anasema kuwa it was better then than now, is kidding him/herself...Mwinyi alifanya la maana kuondoa AD neema taratibu ikaanza rudi TZ tukaacha kukimbiza magari ya ugawaji na unga wa Yanga. Tz ilikuwa na chuo kikuu Kimoja tu shule nyingi hazikuweza kupeleka watoto Sekondari sababu hazikuwepo wenye uwezo wakawapeleka Kenya au Uganda...sasa nchi gani hii ilikuwa Mwalimu alitufikisha pabaya economically na ki fikra vilevile...Wote wazee wenzangu tulikuwa tunaimbishwa shuleni ili tuendelee tunahitaji vitu vinne watu, ardhi siasa safi na uongozi bora. Obviously what was lacking ni Siasa safi na uongozi bora kuanzia kwake Mwalimu
Ila kwa kuwa alikuwa mwelewa mwalimu alingatuka maana mambo yalikuwa hayawezekani hata IMF waligoma kutubail out he had no way out...
Ila big up katika kuyaweka makabila karibu na kuleta mshikamano TZ
Buriani Ujamaa Buriani Azimio, watanzania hatutaki hayo tena ila ni historia yetu
Nawakilisha

Wamzz,
Kuna tatizo moja ambalo tunashindwa kulizingatia Azimio la Arusha ilikuwa ni Sera na Mawazo ya Mtu mmoja. Nae alitaka ahakikishe Linakubalika Hatakama alikubaliki, Linatekelezwa Hatakama Halitekelezeki. Mwl Aliamini na Ameondoka Duniani akiamini Hivyo kuwa Fikra zake ni sahihi siku zote hivyo hakuhitaji mchango/msaada wa Mawazo toka popote.

Wakati tunagutishwa "Zidumu Fikra sahihi za Mwenyekiti", Washauri wake wanadai kuwa "Mzee Haambiliki".Sidhani sera inayokwenda mrama isipokubali ushauri na kufanyiwa marekebisho ingeweza kufika au kumfikisha yeyote alipokusudia.
 
Sijakuelewa!

Hiyo conclusion yako unaipata kutoka wapi kuwa Mwinyi hakuhusika?

Just curious.

AD lilikufa natural death kutokana na sababu nilizosema hapo juu, huyu mwinyi sijui nani ,tunawaonea.

AD ni dini, ni imani ili kufuata lazima uiamini, na sio lazima, kitu pekee ambacho kitamlazimisha kila raia ku-obey rules na kuwa raia mwema ni sheria na si AD!

You know allthis while, niko radhi kukubali mafanikio na faida ya AD ambayo haiwezi kufikiwa na sheria na katiba! akitokea huyo mtu nitamuunga mkono, sasa hivi!
 
AD lilikufa natural death kutokana na sababu nilizosema hapo juu, huyu mwinyi sijui nani ,tunawaonea.

AD ni dini, ni imani ili kufuata lazima uiamini, na sio lazima, kitu pekee ambacho kitamlazimisha kila raia ku-obey rules na kuwa raia mwema ni sheria na si AD!

You know allthis while, niko radhi kukubali mafanikio na faida ya AD ambayo haiwezi kufikiwa na sheria na katiba! akitokea huyo mtu nitamuunga mkono, sasa hivi!
Azimio la Arusha halikufa natural death. Azimio la Arusha ni revolutionary declaration ya kichama ilikuwa na lengo la kushape sera za kiserikali. Sasa sitaenda kwenye legality kwamba kulikuwaje, wenye ufahamu zaidi wataeleza. ila nafahamu kuwa kuna some enforcements were done pale mambo fulanifulani yanapokiukwa. Sasa hii huezi kuita dini mzee.

Na-iterate mchango wa Mzee Mwinyi. Pamoja na mambo mengine, huyu mzee alisimamia kubadilishwa au kuvunjwa kwa misingi mingi ya AD through sera zake za chukua chako mapema. Nadhani post ya kwanza imegusia baadhi ya mambo. Kwamba biashara ilipewa kipaumbele na maelekezo ya kutokuwa na kipato zaidi ya kimoja yakapigwa chini. Pia zilianzishwa idea mpya za mabwana vita wa kimerikani (World Bank & IMF) kupunguza wafanyakazi kleta policy za ubinasishwaji na kupunguza wafanyakazi wa umma. Milango ya biashara kufunguliwa kulisababisha bidhaa za ndani kufishwa na matokeo yake viwanda vingi vilikufa kwa sababu moja au nyingine. Pia ktk kipindi hiki ndio mismanagement kubwa ya mali ya umma ilitokea, kwa watu kuiba fedha za umma kutokana na ukweli kwamba uzalendo huyu mzee aliuweka mfukoni. Taifa liligeuka kwa kiasi kikubwa kuwa taifa la wachuuzi ktk kipindi cha huyu mzee, and things has never recovered eversince.

Sasa inashangaza huoni mchango wa huyu mzee ktk kuigalagaza misingi ya AD. Inashangaza.
 
hata alete ushahidi wa namna gani lakini kwa mwenye akili za upembuzi hawezi kukubaliana na huyu mzee, anataka kuleta hadithi za kale hapa, kama hakulifuta liko wapi? na nini ushahidi wa lipo? tunataka vitendo na siyo uwepo wa kufikirika kweli watanzania tumekuwa mambumbumbu lakini si kwa kiasi hiki......Ole wao wasemao uongo mbele ya macho ya Mungu.
 
Abdulhahim,

Kuhusu post yako hapo juu #73...si kweli baadhi ya comments sababu kama unakumbuka nchi tayari ilikuwa kwenye hali mbaya na si kosa la mwinyi IMF/ World Bank hawakuja kwetu tuliwafuata baada ya sera za Nyerere kuboronga na huo ndio ukweli...IMF ni last resort hawa wanadeal na mataifa ambayo yameboronga kupindukia na wala sio the other way. Hapa kwetu tayari tulishaviua viwanda kama unakumbuka early 80's Tz viwanda vilishashindwa b4 Mwinyi took over...

Ninakumbuka Nyerere alisema haendi huko akienda atageuka jiwe akamuachia mwenzie nchi imechoka kulikuwa hakuna donors na wala mtu anayelipa kodi infact SU zetu zilikuwa hoi zinategemea ruzuku ya serikali sasa hapo sidhani kama Mwinyi had any choice zaidi ya kukubali whatever IMf walichomuambia na hiyo haikuanza hadi second term yake baada ya restructing iliyoanza late 80s.

Nami nakumbuka enzi zile mishahara ilikuwa inachelewa na serikali ilikuwa hoi, ukweli ni kuwa Nyerere alikataa ushauri mapema wa watu ambao wanajua uchumi kama kina Mtei ndio maana wakajitenga na huyu Mzee
 
Huyu Mzee ni heri angekaa kimya bila kusema kitu kuhusu Azimio la Arusha!

Analia eti viongozi walihujumu mashirika, je yeye na Nyerere walifanya nini kudhibiti uzembe na utovu wa nidhamu wa viongozi hao ili tabia chafu na mbaya zisiendelee?

- Mkuu Rev, this coming from you inatia moyo sana kwamba sasa pole pole tunaanza kukaribia ukweli, na tupo pamoja sana, ni kwamba hawa mafisadi walizaliwa siku nyingi sana, isipokuwa zamani walikuwa wanajificha ficha lakini siku hizi wamejitokeza wazi,

- Azimio lilikuwa ni sawa na Prohibition Act ya US, ambayo ilikuwa inazuia pombe kali, matokeo yake wajanja kama kina Kennedy wakaishia kuwa Millioneas kwa kuizunguka hiyo Act, exactly kilichofanyika kwetu wajanja wachache walitajirika sana under awamu ya kwanza kwa kutumia majina ya ndugu zao kuyaweka kwenye mali zao, sasa wengine wakawa wanajiuliza wapo vipi ndio maana ulipokuja mwanya na wao wakajitosa na sasa ni matajiri wa ajabu sana tena kwa kipindi kifupi sana na wote katika kutafuta cover ya utajiri wao mchafu wamejificha nyuma ya ubunge na CCM, wengine wakatimkia Upinzani lakini ni maagent wa CCM, matokeo yake tupo hapa tulipo, tumekwama sasa tunatafutana uchawi na kwa mara ya kwanza tuna uhuru wa kusema, kila mmoja anasema lake na yeye Mwinyi anaona bora aseme hata kama anachosema ni nonsense!

- Kwani kabla ya Azimio kuvunjwa Zanzibar, Tanzania tuna nini cha kuonyesha kama positive results za Azimio La aArusha? kuanzia maisha ya wananchi mpaka uongozi wa serikali nini cha kuonyesha kuwa ni matokeo mazuri ya policies za Azimio? Sasa tizama huyu Mwinyi anavyotucheka kwamba Azimio halikuvunjwa, hivi lisingevunjwa Kapuya angediriki kumiliki Mgodi na kutuambia bila kuogopa? Hawa kina Mkapa wangemiliki wazi wazi mabenki na Kiwira?

Tunasema hivi tunamuheshimu sana Mwalimu kwa sababu nyingi ikiwa ni pamoja na maisha yake siku zote ku-reflect maneno yake na in some cases matendo yake pia, lakini haya ya Maazimio nonsense ndiyo yametufikisha hapa tulipo! Mpaka siku tutakapoweza kutenganisha mapenzi yetu kwa Mwalimu na mapenzi yetu kwa taifa ndio tutasonga mbele, ukiona taifa kila siku linalilia ya zamani ujue hilo taifa halina cha kulilia mbele ya safari! and that is where we are as a nation.

- Azimio la Arusha lilivunjwa na Mwinyi na 2/3 ya viongozi wetu wa sasa walikuwepo kwenye ule mkutano, tatizo sio Azimio kuwepo au kutokuwepo, tatizo ni maviongozi mengi magoi goi tuliyonayo yasiyo na uwezo wa kuongoza, lakini ni matajiri, I mean the dataz ni kwamba kuna mbunge mmoja siku hizi huko bungeni ni tajiri kiasi kwamba amegeuka benki ya kuwakopesha wabunge wengine kuanzia Shillingi Millioni 10 mpaka 20, nasikia sasa hivi anawadai karibu nusu ya wabunge ambao hawana uwezo wa kumlipa that is how bad we are na uongozi wa sasa, I mean China si walikuwa kama sisi sasa wao mbona hawana leadership crisis kama sisi? Ni kwa sababu sisi tulikwua waongo, wababishaji na imitators yaani wasanii wa kutupwa, huwezi kupanda mahindi ukavuna mihogo sasa hivi hili taifa tunavuna tulichopanda tu na ni nothing else!

Mungu Aibariki Tanzania.

Respect.


FMEs!
 
Wamzz,
Kuna tatizo moja ambalo tunashindwa kulizingatia Azimio la Arusha ilikuwa ni Sera na Mawazo ya Mtu mmoja. Nae alitaka ahakikishe Linakubalika Hatakama alikubaliki, Linatekelezwa Hatakama Halitekelezeki. Mwl Aliamini na Ameondoka Duniani akiamini Hivyo kuwa Fikra zake ni sahihi siku zote hivyo hakuhitaji mchango/msaada wa Mawazo toka popote.

Wakati tunagutishwa
"Zidumu Fikra sahihi za Mwenyekiti", Washauri wake wanadai kuwa "Mzee Haambiliki".Sidhani sera inayokwenda mrama isipokubali ushauri na kufanyiwa marekebisho ingeweza kufika au kumfikisha yeyote alipokusudia.


Dear Makoko;

Nyerere

Nyerere was and he will still be a great leader to our nation, no matter what

Great leader/ famous people/ great people wengi ni wale wenye uwezo wa kuwaza na kutekeleza mawazo na imani zao. Nyerere aliwaza na kufanya kadiri alivyoona ni sawa kwake hata hiyo ya kuwa ''Mzee haambili'' ni tabia za watu wengi wenye misimamo na wnayoyaamini, na wale wasioamini wengine, japo hii inafaa sana kwa scholars wengine na sio kwa kiongozi!

Leo hii tangu ametoka madarakani, hana rais aliyeweza kusimamia na kuwziweka aideology zake wazi akakumbukwa vizazi vijavyo, hii inamweka Nyerere kuonekana bado anatawala hata hii leo! kama leo hii hatujaweza kuwa na ideology, systema na style nyingine za kutupeleka tunakoona kuzuri, then we have done nothing and JKN is credited and he is top by that very reason

Ujamaa wa Nyerere

Nyerere alikuwa msomi, mwenye exposure na aliyejua kuwa Ujamaa nchi zingine ulifanikiwa tu kwa style ya udikteta, So aidha awe dikteta ili ujamaa uoendelee mbele au asiwe dikteta. Ninaposema udikteta ni kuwa ujamaa ama kwa hakika ni level ya juu ya upendo, uzalendo, umoja, mshikamano, sio system ya ubinafsi, choyo, kutokujali wengine n.k. Hizi tabia nilizosema ziko within hatakama mtu atakuchekea na kukubeba kama mchoyo ni mchoyo tu! ni system ambazo inabisi unyoshe watu kwa lazima!

Nyerere ujamaa wake alihybrid, na kuleta upendo wake na kujitoa kama tunavyomfahamu leo, KUJITOA huku na UPENDO aliokuwa nao kwa raia wengine ndiko kulikomfanya aamini kama wengine wana tabia kama yake! akatuwekea Mkapa...

JKN hakuwa dikteta, na ujamaa ulifeli kwa sababu hiyo....... so kwa usomi wake alitakiwa yeye aidha aamue moja, kuwa typical dikteta au kuacha ujamaa!

naona ujamaa hapa umeshafeli kabla haujaingia kazini


Nyerere kama Kiongozi

Achilia mbali upendo aliokuwa nao kwa taifa lake, lakini alijawa na ubishi unaousema (kasoro hii) ambayo ikapelekea kutukuzwa, na kusema fikra zake ni sahihi. concept ya zidumu fikra sahihi na ujamaa ndio- I am assuming imetuleta hapa;

1. Leo hii viongozi hawasikilizi cha mtu, kwani ukishakuwa kiongozi ni bora na unajua kila kitu
2. Udumavu wa kufikiri na watu kuona kila kitu kinatakiwa kifanywe na kufikiriwa na viongozi
3. Kwa sababu hizo hapo juu, leo watu hawawezi kuuliza maswali karibu kila kona, hawawezi kuchagua viongozi wazuri

Kama hizo sio failure za huu msemo basi ndiyo tulivyo thena again AD is not solution!

Nyerere kama Mentor

Hakuweza na hajaweza kutoa kiongozi kama yeye au wa aina yake! sifa ya kiongozi yeyote lazima uwe influential na kutengeneza watu kama wewe, waliobaki ni waumini wa Nyerere, wapenzi wa Nyerere, CCM aliyoiacha tangu anaondoka hakuna aliyemkumbuka Nyerere, achila mbali Kikwete aliyeingia CCM ikiwa TANU, in leadership this is a failure na kujua ni kwa nini lazima tuangalie mambo mengine! moja ya sababu ni kuwa ideology ya kuwa 'najua kila kitu' ikawapoteza viongozi wengine wazuri maana watu walikuwa anamwogopa

Back to AD

If we real believe in democracy; AD then haikupata support ya wananchi!

Here is two sided of this AD!

''Ujamaa villages are intended to be socialist organizations created by the people, and governed by those who live and work in them. They cannot be created from outside, nor governed from outside. No one can be forced into an Ujamaa village, and no official - at any level - can go and tell the members of an Ujamaa village what they should do together, and what they should continue to do as individual farmers''

''Politically and socially the declaration was hugely unpopular. In 1974 Operation Dodoma forced collectivization of farming with the use of the military. Following the murder of Kleruu, a regional commission who sezied all of a Mr's Mwanwindi's land in 1975 and the public attention to the trial the collectivism of the Arusho Declaration finally ended. It was a complete failure and only plunged Tanzania into further debt, a crisis in its balance of payments deficits and worsened relations with international donors''

If it was free will kuanzisha vijiji vya ujamaa kwa nini jeshi waliingilia kati? leo hii tunataka tuanzishe vijiji wapi? maana kikubwa kinchokumbukwa ni kuwancishwa kwa vijiji vya ujamaa, is this was the only solution ya kuleta maendeleo?


My take

There is nothing wrong in putting your ideology, theories etc. hakuna tatizo kabisa kama ile AD ilikuwa sauti ya wanamapinduzi na kauli mbiu ya watu kuwa wazalendo! There is nothing wrong leo hii akatokea mtu ambaye ataayesema tuanzishe convincing debate tuwabadilishe mind ya watu na waweze kuwa raia bora!

There is nothing wrong kumpenda na kumuheshimu Nyerere , bila matusi n.k

Tatizo ni pale tunapotaka kuamini it was the only solution ya kutatua matatizo yetu, tatizo na kutokubali kulikuwa na makosa na AD inataka kuwa dini na siyo reality, tatizo ni kutokuwa na watu shupavu wa kulisimamia kwa vitendo.,Kuhubiri na kushawishi watu, AD ni ushawishi zaidi,

How to go about

Kwa sababu ilikuwa ni beliefs then watu employ techniques za marketing kuwashawishi watu-kivyao vyao na sio kulazimishana!!! sijaona sensible au necessityya kuwa lazima liwepo kama tuna sheria na katiba

Mkodini Komba na bendi yake apite kila mkoa akiwashawishi watu walihubiri azimio la Arusha, ili watu wafanye kazi na kujitegemea!!

Ila wale wanaotaka liwepo, litangazeni, lichambueni lilete ushawishi kwa watu, maana halina ulzaima wala sio excuse ya matatizo yetu, TUNA MATATIZO MENGINE MENGI TU! kama mtu unasema huwezi ukajitegema mpaka Nyerere atangaze AD si ndiyo matatizo hayo!

Kama watanzania walilikataa kipindi cha Nyerere leo hii kazi ipo.

wala asiseme mtu kuwa mbona lilipokolewa nchelea kusema imani za woga na kufuata mkumbo zimetuonyesha vitu vingi huwa vinadhaniwa sivyo


Hata mkisema ije AD au sijui nini, tabia ya Nyerere ya kupenda watu na kujitoa kwa watu wake ilikuwa exceptional, na hii tabia wengine wana changanya wanafikiri ilitokana na ideology zake---, leo hii hata kama kila raia atasema kutoka moyoni kuwa KARIBU AZIMIO la arusha kuwa sawa na Nyerere haiwekani ng'o ni ndoto, naam kwa tabia yake personal we have watu kama yeye hata kwa mifumo isiyo na AD ! KAMA WEWE BINAFSI una tabia za unyama na zisizo na utu , kuwa sawa na Nyerere ahaiwekani

Binadamu wanawekwa sawa tu na 'sheria na katiba' that is the only thing makes us equal!!!
 
Hadi BBC Wakubwa wanamhoji anajidai kutoa point, aliua elimu huyo mzee alafu!!
 
Mimi tofauti na maoni ya wengi nakuwa na wasi wasi na msimamo wa wachangiaji wengi hapa. Inaonekana wazi kabisa kuwa si wote wamelisoma na kulielewa Azimio la Arusha na hivyo kutojua kwa nini swala lake linaanza kuibuka hivi sasa. Wanachojaribu ni kulitafsiri na kulihukumu kwa kuangalia wanachodhani yangestahili kuitwa mafanikio yake. Matokeo yake wanashindwa kuelewa malengo na sababu za kupitishwa kwa Azimio la Zanzibar na athari za kitendo hicho kwa Azimio la Arusha na mustakabali wa taifa kwa jumla. Nashauri watu watafute muda walisome kwanza kabla ya kuchangia ili wakwepe kukurupuka kama anavyokurupuka Mwinyi hivi sasa - ni ushauri tu.

Tuliokuwapo viwanja vya Mnazi Moja mwaka 1967 tuliziona sura nyingi zilizojaa matumaini na pia sura chache zilizofadhaika na kujaa woga. Tulijua vita vimetangazwa - vita iliyowaweka wananchi wenye moyo wa kujenga taifa lao upande moja na wenye meno ya kuila taifa upande wa pili. Ninachoweza kusema ni kuwa ilikuwa vita ngumu hasa kwa upande moja kwani pamoja na kuwa wengi, hawakuwa na nyenzo kama wenzao waliotumia nguvu ya pesa. Hivyo mwaka 1991 ushindi ulipatikana kwa upande moja huko Zanzibar na jemadari aliyeongoza hivyo vita ni Al Haj Ali Hasan Mwinyi. Leo hii anatokea na kudai hakushinda, sasa waliotangaza ushindi ni akina nani ?
 
Kweli huyu Mzee sasa anataka kupanua midomo isivyotakiwa,au hii heshima anayopewa na watanzania anadhani anahistahili kuipata kama kweli tukiamua ukweli uchukue mkondo wake?

Au kuitwa mzee ruksa anadhani sifa? kweli huyu mzee ni bora akae kimya hana sababu ya kupanua midomo yake.Anyway remember ''Each generation must out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it or betray it by Frantz Fanon" sasa yeye alichagua kuwasaliti watanzania kwa kuua Azimio la Arusha, na hilo ndo anastahili kuomba msamaha na siyo vinginevyo.
 
Mimi tofauti na maoni ya wengi nakuwa na wasi wasi na msimamo wa wachangiaji wengi hapa. Inaonekana wazi kabisa kuwa si wote wamelisoma na kulielewa Azimio la Arusha na hivyo kutojua kwa nini swala lake linaanza kuibuka hivi sasa. Wanachojaribu ni kulitafsiri na kulihukumu kwa kuangalia wanachodhani yangestahili kuitwa mafanikio yake. Matokeo yake wanashindwa kuelewa malengo na sababu za kupitishwa kwa Azimio la Zanzibar na athari za kitendo hicho kwa Azimio la Arusha na mustakabali wa taifa kwa jumla. Nashauri watu watafute muda walisome kwanza kabla ya kuchangia ili wakwepe kukurupuka kama anavyokurupuka Mwinyi hivi sasa - ni ushauri tu.

Tuliokuwapo viwanja vya Mnazi Moja mwaka 1967 tuliziona sura nyingi zilizojaa matumaini na pia sura chache zilizofadhaika na kujaa woga. Tulijua vita vimetangazwa - vita iliyowaweka wananchi wenye moyo wa kujenga taifa lao upande moja na wenye meno ya kuila taifa upande wa pili. Ninachoweza kusema ni kuwa ilikuwa vita ngumu lakini mwaka 1991 ushindi ulipatikana kwa upande moja huko Zanzibar na jemadari aliyeongoza hivyo vita ni Al Haj Ali Hasan Mwinyi. Leo hii anatokea na kudai hakushinda, sasa waliotangaza ushindi ni akina nani ?
Leo Jemadari anayakana majeshi yake! Lo, makubwa haya. Mag3 kumbe ulikuwepo Mnazi Mmoja 1967, basi labda tulipigana vikumbo au tukionana tunaweza kukumbukana sura zetu.
 
Back
Top Bottom