Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Waberora,

Azimio la Arusha liliweka miiko. Ila kwa vipi lilikataza kuiba, hicho kitu hakipo duniani.

Hata leo Tanzania ukiuwa unaweza kunyongwa kikatiba, ila hiyo sheria haizuii watu kuuwa. Sasa unaponiuliza hilo, sijui uma maana gani. Isije kuwa yale ya kuuliza pua iko wapi wakati mdomo unauona.

Sasa hivi hiyo miiko tu haipo. Sasa hata Yona na Mramba kuwashitaki na kushinda ili jamaa waende jela hicho kitu hakipo. Walau zamani mtu anaweza kushtakiwa na akafungwa au kufukuzwa kazi. Lowassa pamoja na kuvunja miiko, bado WALIMUOMBA aangalie kipi cha maana akifanye. Yes, aangalie na si ashtakiwe na kufukuzwa kazi na mwisho kufungwa. Hii ndiyo hali mbaya ya vacuum iliyotokea baada ya kuvunjwa kwa AD.

Kukaa chini na kuangalia tabia zenu hilo ni kupoteza muda. tabia zetu pote duniani ziko sawa kabisa. Ila wenzetu wanafuatilia sana sheria. Kama JKN angelifahamu hili na kujenga kitu kama FBI, CIA na Sherrif/POLISI basi ninaimani leo hii watu kama Rostam Azzi, Lowassa na akina Mramba wangelikuwa wafanyakazi bora wa Tanzania huku wakiiletea Tanzania faida kubwa. Siwezi kushangaa kuwa hawa watu walikuwa na moyo sana ila wakakatizwa tamaa na wale wengine wa zamani. Kama Kikwete aliona wanavyoiba wengine, leo hii kawa juu unafikiri yeye ataacha? Ila kuna chombo chochote kinafanya ULINZI na USALAMA wa rasilimali zetu?

Haijalishi AD au katiba au chochote kile wewe utakaa na kusema tukifanye. Tanzania inabidi tuwe na chombo cha kuwalinda viongozi. Wabunge tumeshaona haliwezekani. Kama tukiwa na FBI yetu na hawa jamaa hawafanyi mchezo (kumfunga paka kengele) basi mchezo utakuwa umeisha. Miiko iwepo na chombo maalumu kisimamie. Huu ndiyo mzizi wa fitina.

Kama kuna kiongozi hafai, basi sidhani kama atakwenda juu. Leo hii tunasikia Mrema wa TANROAD kaajiliwa kwa mlango wa nyuma. Boss mpya wa NHC kaajiriwa kwa mlango wa nyuma. Pesa kibao zimetumia kumchagua CEO na watu wanakuja kuajiri kivyao na hakuna kitu kinatokea kwa hawa Mawaziri. Sasa unategemea huyu boss wa NHC atakuwa kweli makini? Kwanza ataambiwa achote pesa aipe CCM na hatapinga kwani wamemuajiri kwa kutumia penseli. Wanamtisha kuwa ukileta ya kuleta, form one utafutwa.

Asante Sikonge naona sasa umekuja mahali pazuri kabisa, Ikiwa leo hii sikonge tuitaitisha Azzimio la Arusha na kulipa nguvu ya kisheria badala ya maneno, nitakuwa wa kwanza kuandamana toka kwetu kijijini mpaka Arusha! Ikiwa leo hii tunasema vongozi hawana hofu ya woga kwani hakuna chombo cha kuwamonitor basi jibu lake ni kuwa hatuna dira, hatuna viongozi, hatuna taifa, AD can be in effective only kama litakuwa na nguvu za kisheria na watu mahususi wa kulitekeleza, offcourse TAKUKURU ingekuwa hivyo , lakini wote walewale,

Yes, lianzishwe na wananchi, liwe na nguvu ya wananchi, lwe na nguvu ya kisheria, liweze kuamua na kutekeleza wanayoyaona wao sawa , kama vile kukamata mafisadi n.k Japo tatizo kubwa tena itakuwa katiba , kuwa madaraka ya rais inabidi yapunguzwe.

Please lisiwe maneno wala kulazimishana, wala kuhubiriana kma dini vile! tukifanya hivyo tunakosea!

Mkuu Waberoya, I wish I had the time lakini hata hivyo nitatafuta muda nitoe majibu kwa kiasi ninachoweza. Bahati mbaya najaribu kufanya shughuli nyingi kwa wakati moja ingawa napitia humu kila nikipata muda mfupi.

Hata hivyo kabla sijaanza naomba tuelewane kitu kimoja. Kwanza, pamoja na kuwa kijana wakati huo, sikuwahi kujiunga na TANU hata siku moja wala sikuwahi kukipigia kura TANU (au CCM) hata siku moja. Sababu kubwa ni kuwa toka nikiwa shuleni sikuamini katika demokrasia ya chama kimoja na hata shuleni nilishiriki sana katika mijadalo kama ilivyoitwa "debate" wakati huo. Pili, sikuwahi kufanya kazi serikalini kama civil servant, kwani toka nimalize shule nilifanya kazi nje ya nchi kwenye makampuni mbalimbali - kazi nilizozitafuta mwenyewe.

Lakini pamoja na yote niliheshimu msimamo ulioonyeshwa na uongozi wa wakati huo. Nchi iliheshimika kwa kuwa na vision ya kitaifa na kuwa na kiongozi aliyekuwa tayari kuitetea kwa nguvu za hoja. Nilichoweza kugundua mapema kabisa ni kuwa ingawa wananchi wa kawaida wengi walimpa support, wako ambao mchana walihubiri maji lakini usiku walikunywa mvinyo. Mkuu Waberoya, nikipata nafasi tena nitapitia hoja zako moja baada ya nyingine kama ulivyozitoa ila tu naomba uelewe ni katika misingi niliyoyaelezea hapo juu.


Mzee Mag3 nimekuelewa asante kwa kuwa na misimamo, na kujitoa kunielimisha,

Caliber ya JKN ya kujitoa na kupenda watu that is the character that I will always adore him for, lakini madhaifu mengine tutayasema bila woga! na bila kuonyesha dharau , ni kujadili kwa sababu tuko huru na tuendako safari ni ndefu, naweza kuwa rais kesho ebo! nataka kujifunza na kukosoa.

Nimefurahi Mag kusema haukupenda chama kimoja, wengi wapenzi wa Nyerere ni washabiki na wapenzi! wana jukumu kubwa la kuwa wawazi!

Mtu mmoja alisema, nihubirie madhaifu yako, nihubirie wapi ulikwama na ukafanyaje kujikwamua, niambie wapi umeshindwa na unafikiri kwa nini ili na mimi niwe mwangalifu, niambie wapi niwe makini! Nyerere alikuwa mzuri yet alikuwa mwanadamu, kujua udhaifu wake ni mwanzo wa sisi kujifunza pa kukanyaga, kama na kama tu tutakuwa watu wa kufanya na sio kusema tunafuata AD ili hali vitendo haviko hivyo! AD ni dini kwangu mimi, ni hamasa kama vile jeshini nothing else



Kama utajibu jaribu pia kuweka faida za Ujamaa
 
Jamaaa wanaweweseka....sasa wanahangaika kukwepa lawama wangejibu Mwalim akiwepo .....kweli kabsa nchi haina miiko ya uongozi haki wala usawa.....sera moja tu kujilimbikiziaa mali kwenda mbele....kama wanadai azimio halijafa...watuonyeshe misingi yake kama kweli bado inafanya kazi!!wasitutanie hapa
 
Makoko,
Nadhani Sikonge anazungumzia miiko ya uongozi. Hata Marekani wanayo miiko hiyo licha ya kwamba wanazingatia sana utawala wa kisheria. Akina Mkapa na Lowassa waliweza kuiba kwa sababu walijua hakuna atakayewatia hatiani baada ya Azimio la

Zanzibar kushika hatamu. That is a big difference to me.

Js,
Kinachompeleka mtu Mahakamani ni uvunjaji wa Sheria. Uvunjaji wa miiko utakuwa na hukumu nyingine na haitolewi Mahakamani. Tuwe na miiko au isiwepo, Sheria zipo na zimevunjwa nini kifuatie. tunde miiko au tutumie sheria tuliyonayo kuwasakama waliotukosea?
 
Makoko wa Uk , kama upo kwa malikia basi utaona hoja za mwalimu zilivyo fanikiwa , mfano ukitaka kupeleka maji kwa watu na ukapunguza gharama si utawashauri wakae sehemu moja ili uweze kuwapatia hiyo bidhaa iwe shule hospitali, maduka, barabara nk na hapo ulipo utaona watu wana kaa kwenye estate, na kuwezesha kujenga miji kutokana na kuwepo kwa watu.

Enzi za UDA basi usafiri mpaka mid night kutegemeana na sehemu, na la asubuhi linaanza mapema. neighbour hood watch ndio sawa sawa na hizo nyumba kumi kumi na kutambuana nani anafanya nini, tatizo kikifanyika kwetu sisi waswahili, unalalamika fulani mnoko kweli.

Sera za Mwalimu ilikuwa ni kuwaondoa Wathungu na ....... ili maduka tushikilie thithi ngozi nyeusi bali ilikuwa ni gradual process ya sisi kujitambua kwamba tunaweza, tuimarishe elimu yetu hata ingefika wakati wa soko huria nk tungekuwa tunajua kutetea kilicho chetu, sio sasa hivi aliye kuibia akikuletea kapelo unamfrahia na kumuongezea nguvu akuibie zaidi.

Yaani Mwl alitekeleza sera za Idi Amini kwa kutumia technique.

Ag,
Hoja za Mwl. zimefanikiwa huku kwa Malkia au Huko nyumbani? Hizi Estate Malkia huzijenga kwanza ndio akawapeleka Watu, tena kwa Hiyari yao!

Jingine ni kuwa ilikuwa mapema mno kuja na mfumo mpya ndani ya miaka sita ya Uhuru, Watendaji walikuwa hawajataarishwa na Pesa za Miradi Mwl. Hakuwanazo alitegemea Nguvu kazi ya wananchi na ushawishi wa kujitegemea na hayo pia yalihitaji Elimisho ambalo halikuwepo.

Namalizia kuwa Mwl. alikuwa na nia njea sana (kama mmoja wetu alivyosema ni vita ilitangazwa) Lakini kwa masikitiko makubwa Mwl. hakuwa ameaanda jeshi kwa vita hiyo, matokeo ndio haya Vita ameshindwa lakini yaelekea mapambano yungalimo na ndio maana leo tunlijadili AD.
 
Dear Makoko;

Nyerere

Nyerere was and he will still be a great leader to our nation, no matter what

Great leader/ famous people/ great people wengi ni wale wenye uwezo wa kuwaza na kutekeleza mawazo na imani zao. Nyerere aliwaza na kufanya kadiri alivyoona ni sawa kwake hata hiyo ya kuwa ''Mzee haambili'' ni tabia za watu wengi wenye misimamo na wnayoyaamini, na wale wasioamini wengine, japo hii inafaa sana kwa scholars wengine na sio kwa kiongozi!

Leo hii tangu ametoka madarakani, hana rais aliyeweza kusimamia na kuwziweka aideology zake wazi akakumbukwa vizazi vijavyo, hii inamweka Nyerere kuonekana bado anatawala hata hii leo! kama leo hii hatujaweza kuwa na ideology, systema na style nyingine za kutupeleka tunakoona kuzuri, then we have done nothing and JKN is credited and he is top by that very reason

Ujamaa wa Nyerere

Nyerere alikuwa msomi, mwenye exposure na aliyejua kuwa Ujamaa nchi zingine ulifanikiwa tu kwa style ya udikteta, So aidha awe dikteta ili ujamaa uoendelee mbele au asiwe dikteta. Ninaposema udikteta ni kuwa ujamaa ama kwa hakika ni level ya juu ya upendo, uzalendo, umoja, mshikamano, sio system ya ubinafsi, choyo, kutokujali wengine n.k. Hizi tabia nilizosema ziko within hatakama mtu atakuchekea na kukubeba kama mchoyo ni mchoyo tu! ni system ambazo inabisi unyoshe watu kwa lazima!

Nyerere ujamaa wake alihybrid, na kuleta upendo wake na kujitoa kama tunavyomfahamu leo, KUJITOA huku na UPENDO aliokuwa nao kwa raia wengine ndiko kulikomfanya aamini kama wengine wana tabia kama yake! akatuwekea Mkapa...

JKN hakuwa dikteta, na ujamaa ulifeli kwa sababu hiyo....... so kwa usomi wake alitakiwa yeye aidha aamue moja, kuwa typical dikteta au kuacha ujamaa!

naona ujamaa hapa umeshafeli kabla haujaingia kazini


Nyerere kama Kiongozi

Achilia mbali upendo aliokuwa nao kwa taifa lake, lakini alijawa na ubishi unaousema (kasoro hii) ambayo ikapelekea kutukuzwa, na kusema fikra zake ni sahihi. concept ya zidumu fikra sahihi na ujamaa ndio- I am assuming imetuleta hapa;

1. Leo hii viongozi hawasikilizi cha mtu, kwani ukishakuwa kiongozi ni bora na unajua kila kitu
2. Udumavu wa kufikiri na watu kuona kila kitu kinatakiwa kifanywe na kufikiriwa na viongozi
3. Kwa sababu hizo hapo juu, leo watu hawawezi kuuliza maswali karibu kila kona, hawawezi kuchagua viongozi wazuri

Kama hizo sio failure za huu msemo basi ndiyo tulivyo thena again AD is not solution!

Nyerere kama Mentor

Hakuweza na hajaweza kutoa kiongozi kama yeye au wa aina yake! sifa ya kiongozi yeyote lazima uwe influential na kutengeneza watu kama wewe, waliobaki ni waumini wa Nyerere, wapenzi wa Nyerere, CCM aliyoiacha tangu anaondoka hakuna aliyemkumbuka Nyerere, achila mbali Kikwete aliyeingia CCM ikiwa TANU, in leadership this is a failure na kujua ni kwa nini lazima tuangalie mambo mengine! moja ya sababu ni kuwa ideology ya kuwa 'najua kila kitu' ikawapoteza viongozi wengine wazuri maana watu walikuwa anamwogopa

Back to AD

If we real believe in democracy; AD then haikupata support ya wananchi!

Here is two sided of this AD!

''Ujamaa villages are intended to be socialist organizations created by the people, and governed by those who live and work in them. They cannot be created from outside, nor governed from outside. No one can be forced into an Ujamaa village, and no official - at any level - can go and tell the members of an Ujamaa village what they should do together, and what they should continue to do as individual farmers''

''Politically and socially the declaration was hugely unpopular. In 1974 Operation Dodoma forced collectivization of farming with the use of the military. Following the murder of Kleruu, a regional commission who sezied all of a Mr's Mwanwindi's land in 1975 and the public attention to the trial the collectivism of the Arusho Declaration finally ended. It was a complete failure and only plunged Tanzania into further debt, a crisis in its balance of payments deficits and worsened relations with international donors''

If it was free will kuanzisha vijiji vya ujamaa kwa nini jeshi waliingilia kati? leo hii tunataka tuanzishe vijiji wapi? maana kikubwa kinchokumbukwa ni kuwancishwa kwa vijiji vya ujamaa, is this was the only solution ya kuleta maendeleo?


My take

There is nothing wrong in putting your ideology, theories etc. hakuna tatizo kabisa kama ile AD ilikuwa sauti ya wanamapinduzi na kauli mbiu ya watu kuwa wazalendo! There is nothing wrong leo hii akatokea mtu ambaye ataayesema tuanzishe convincing debate tuwabadilishe mind ya watu na waweze kuwa raia bora!

There is nothing wrong kumpenda na kumuheshimu Nyerere , bila matusi n.k

Tatizo ni pale tunapotaka kuamini it was the only solution ya kutatua matatizo yetu, tatizo na kutokubali kulikuwa na makosa na AD inataka kuwa dini na siyo reality, tatizo ni kutokuwa na watu shupavu wa kulisimamia kwa vitendo.,Kuhubiri na kushawishi watu, AD ni ushawishi zaidi,

How to go about

Kwa sababu ilikuwa ni beliefs then watu employ techniques za marketing kuwashawishi watu-kivyao vyao na sio kulazimishana!!! sijaona sensible au necessityya kuwa lazima liwepo kama tuna sheria na katiba

Mkodini Komba na bendi yake apite kila mkoa akiwashawishi watu walihubiri azimio la Arusha, ili watu wafanye kazi na kujitegemea!!

Ila wale wanaotaka liwepo, litangazeni, lichambueni lilete ushawishi kwa watu, maana halina ulzaima wala sio excuse ya matatizo yetu, TUNA MATATIZO MENGINE MENGI TU! kama mtu unasema huwezi ukajitegema mpaka Nyerere atangaze AD si ndiyo matatizo hayo!

Kama watanzania walilikataa kipindi cha Nyerere leo hii kazi ipo.

wala asiseme mtu kuwa mbona lilipokolewa nchelea kusema imani za woga na kufuata mkumbo zimetuonyesha vitu vingi huwa vinadhaniwa sivyo


Hata mkisema ije AD au sijui nini, tabia ya Nyerere ya kupenda watu na kujitoa kwa watu wake ilikuwa exceptional, na hii tabia wengine wana changanya wanafikiri ilitokana na ideology zake---, leo hii hata kama kila raia atasema kutoka moyoni kuwa KARIBU AZIMIO la arusha kuwa sawa na Nyerere haiwekani ng'o ni ndoto, naam kwa tabia yake personal we have watu kama yeye hata kwa mifumo isiyo na AD ! KAMA WEWE BINAFSI una tabia za unyama na zisizo na utu , kuwa sawa na Nyerere ahaiwekani

Binadamu wanawekwa sawa tu na 'sheria na katiba' that is the only thing makes us equal!!!

Dear Waberoya ;

Kwa waraka huo naona tumeelewana kiasi kikubwa, nadhani kuna umuhimu wa kukubaliana na wezetu tuchukue yale mazuri toka AD ambayo bado yangeweza kutumika katika siasa zetu za leo na kuziboresha.

Sijui kama ulibahatika wakati AD limeshika kasi kulikuwa na vijembe vya Propaganda kila baada ya Taarifa ya Habari na Mada ya siku huja katika mazungumzo baada ya habari saa 2 15 kila siku usiku.

Kijembe kimoja kilikuwa kinasema: Mwenzetu huyu anaumwa, tena anaumwa sana........................Unyonyaji ni Haramu!

Ikiwa AD limefutwa na miiko yake pamoja, SHERIA za nchi bado zipo nazo zinasema: WIZI ni HARAMU!
 
Js,
Kinachompeleka mtu Mahakamani ni uvunjaji wa Sheria. Uvunjaji wa miiko utakuwa na hukumu nyingine na haitolewi Mahakamani. Tuwe na miiko au isiwepo, Sheria zipo na zimevunjwa nini kifuatie. tunde miiko au tutumie sheria tuliyonayo kuwasakama waliotukosea?

Makoko in UK,

Ntakujibu kwa ujumla makala zako zote hapo juu/nyuma.

Si kweli kuwa UK wanajenga na ndipo wanapeleka watu kwa hiari. Huko kuna kitu kinaitwa Urban planing. Mji unawekwa kwenye makaratasi na baada ya kila kitu kupangwa, ndipo watu wanaruhusiwa kwenda kujenga/kuishi.
Nina jamaa yangu yupo UK alikuwa akilalamika alipokuja likizo kuwa nyumba aliyonunua, kuna chumba zamani ilikuwa garage ya kuhifadhia gari. Wenye nyumba akaibadilisha na kuwa ............. na sasa yeye akataka kubadilisha na kuwa sehemu ya watoto kuchezea. Wakamwambia gharama za kubadilisha kuanzia vibali, ujenzi na takataka nyingine, zitamtoka Paund 10,000. Yes, paund elfu kumi. Sasa wee hebu nenda UK ujijengee sehemu unapotaka ndipo utakiona. Wao wanasheria zao na miiko yao na hiyo inafuatwa sana. Ukivunja miiko ya chama, wanakufukuza. Ukivunja miiko ya ujenzi wanakuambia ulipe faini na gharama za kurudishia kwenye hali ya zamani. Kama umeshajenga, unaambia ubomowe/ulipie gharama za ubomoaji na faini juu kwa kuvunja miiko. Usipofanya hivyo watabomoa na kukuletea bill yake. Usipolipa basi mahakamani na mwisho jela.

Kwa Tanzania, zamani tulikuwa na chama kimoja. Hivyo hiyo miiko ilikuwa ukiivunja, unafukuzwa kwenye chama na ndipo unakuwa mwisho wako. Tuseme kama una duka la vyakula, na wewe ni waziri wa elimu na unaagiza wizara yako inunue chakula kwenye duka lako kwa ajili ya mashule ya sekondari kwa bei utakayopanga wewe, huo siyo wizi, hasa kama utaweka bei ambayo ni ya ukweli. Ila utakuwa umevunja tu miiko ya uongozi ambapo unaweza usiende mahakamani ila kwa uongozi unatakiwa uondolewe. Utaondolewa kwa sababu hukutangaza zabuni kama sheria inavyotaka ila ukajifanyia mambo unavyotaka mwenyewe.

Mengine naandika chini kumjibu Waberoya.
 
Waberoya,

Kusema leo turudi kwenye AD ni kupoteza muda. AD ilikuwa kwa ajili ya chama kimoja. Haya mambo mazuri ya AD yanatakiwa yaingizwe kwenye katiba na hiyo AD waiache ijifie. Kubadilisha mambo leo hii ni kupoteza muda mwingine kwani katika kipindi hiki, kuna mazuri mengine mengi tu yametokea. Itakuwa ni kichekesho kujifanya hatuyaoni.

Serikali inabidi iwasaidie wananchi kuwekeza. Iwape shule wafanya biashara ikiwezekana ili waweze kutoa ushindani kwenye soko la dunia hii. Kuwe na mikutano ili wafanya biashara waweze kukaa na kubadilisha mawazo. Wahindi na Wayahudi mnafikiri huwa wanakaa kwenye Mahekalu/sinagogi yao kusali tu? Huko zinafanywa deal zote safi san chafu. Huko kunapangwa nani asaidie na nani asaidie na kila kitu kiko chini ya Rabin. Serikali ibaki na ubiya mchache kwenye mashirika yote yanayoingiza faida na kuyaacha mikononi mwa Wazawa wakiyaendesha. Wao wabaki walinzi tu. Serikali ibaki kwenye mashirika yote ambayo ndiyo mhimili wa uchumi na usalama wa Taifa. Vitu kama DAWASCO lazima viwe chini ya nchi kiusalama. POLISI, Magereza, JWTZ nk. Pia kwangu mie vyombo vyote vya kuzalisha energy kama Mafuta na umeme hivyo pia inabidi viwe chini ya serikali pamoja na barabara. Haya mengine acha watu wajifanyie na wao (serikali) wabaki wakitoa msaada tu pale unapohitajika na kukusanya kodi.

Miiko ya viongozi ibadilishwe na ziwe sheria. Kwenye AD kuna mambo mazuri tu ambayo kwa nchi kama Tanzania kwa sasa, itakuwa kazi sana kuyafanya kwani AD iko chini ya chama. Lakini kama tutayafanya yawe chini ya katiba na kiwepo chombo cha kulinda katiba, nafikiri itakuwa swafi sana. Leo hii Waziri anaenda kuweka sahihi mkataba huko UK, hafanywi kitu na sheria bado hajavunja. Ingelikuwa imewekwa wazi kwenye sheria, basi Mtikila angelimburuza mahakamani waziri huyo kwa kuvunja katiba na angelishtakiwa na hata kufungwa kwa kuvunja katiba.

MWISHO: Niko na wewe katika hili la Madaraka ya RAIS lazima yapunguzwe.
 
Kinachoendelea Tanzania sasa si Ubepari si ujamaa na kujitegemea. Kinachoendelea ndani ya mifumo ya utawala ni ukosefu wa uongozi. Sera ya ujamaa na Azimio lake la Arusha havikuleta tija kwa sababu uongozi ulilegalega na sheria zikabaki kwenye makaratasi tu.

Azimio la Arusha lilikuwa na miiko ya uongozi na hasa msingi wa miiko hiyo ilikuwa kuzuia viongozi wa umma kutumia vyeo vyao kujinufaisha. Au kuzitumia ofisi zao kama za binafsi. Ikiwa masharti haya hayakuwa na maana kama Waberoya anavyosema mara kwa mara kwa nini walilazimika kukaa Zanzibar na kutangaza Azimio la Zanzibar? Ni kweli kutokana na udhaifu kwenye uongozi sheria zile au masharti yale yalikuwa hayafuatwi. Lakini ikiwa hayakuwa na maana kwa nini walitangaza kuyaondoa? Lazima kulikuwa na sababu.

Masharti yale ya uongozi ndo legacy pekeee ya Azimio la Arusha iliyokuwa imebaki. Kimsingi mambo ya umilikaji wa njia kuu za uchumi kuwa kazi ya state ilishaonekana kushindwa. Na sera zilishabadilishwa. Lakini mwiba uliokuwa umesalia ni masharti ya uongozi ambayo kimsingi Mwinyi aliyaondoa kupitia hilo la Zanzibar. Je baada ya kutangaza kuwa viongozi wa umma wanaruhusiwa kufanya biashara ni sheria gani nyingine iliwekwa mahali pake?? Hakuna!! Sheria ni maandishi. Utekelezwaji wake hutegemea zaidi mifumo iliyopo na uongozi wake. Lakini huwezi kusema kuwa, mbadala wa kushindwa kwa uongozi kusimamia sheria au masharti ni kufuta sheria au masharti hayo.

Kwa kutangaza Azimio la Zanzibar, Mzee Mwinyi na serikali yake waliondoa masharti ambayo hadi hapo ni kweli yalikuwa hayatekelezwi kikweli kabisa. Lakini angalau yalikuwepo! Ni nini athari za kuwaruhusu viongozi wa umma kufanya biashara bila kuwepo na masharti ya aina yoyote? Kwa nini viongozi wa wakati huo waliona ni lazima masharti hayo yaondolewe? ...... Kulikuwa na hatari kuwa pamoja na kuwa wanavunja hayo masharti, iko siku watahukumiwa nayo. Ndo maana wakatangaza kuyafuta ili kurasmisha kitu walichokuwa wakifanya.
 
Unajua Mkandara unazungumzia theories wakati hali halisi inakusuta kwa hayo unayoyaeleza.au wakati anaingia mwinyi ulikuwa bado huujuwi dunia? Mashirika yalitowa ajira kwa watu jee wangelipwa nini wakati mashirika hayazalishi na wala serikali haina pesa za kuwagawia wafanyakazi kama ngawira?
Unapozungumzia kuondowa miiko ya uongozi unakusudia miiko hiyo ni ipi? Azimio la Arusha halikuwa na mipaka kati ya kiongozi na mwananchi wa kawaida kwani kwenye Azimio hilp unajua Kiongozi ni nani? Iwapo kila mfanyakazi anazuiliwa kupata kipato cha ziada nini maana yake? Wafanyakazi wafe njaa chini ya malipo dubi na yasiyokuwepo? Taifa la Watanzania hapo likisemwa kuwa la wafanyakazi na Wakulima sasa mihimili ya uchumi inaponyimwa mfanyakazi na mkulima yuko kijijini na Serikali haina Fedha za kuendesha biashara nchi itaenda vipi. Ndio maana Marmo amesema kuwa mambo mengi yanasababisha hali hii tunayojadiliana nayo.

Sikonge,
Mkuu sina maana ya kutukana ila kuzungumzia Ukweli.. Wakati Mwinyi anaingia madarakani nina hakika tena sii kidogo kwamba naijuia Tanzania ile kuliko wewe!...Naijua kwa sababu nilikuwa katikati ya mgawanyiko wa pande zote za kisiasa nikiwa nimewahi kufanya kazi serikalini, mashirika na hata kuishi na kutembelea Ulaya nchio za kibepari kabla kabisa hatujauvaa Ubepari tukipigwa msasa wa Ujamaa. hivyo mimi niliufahamu Ubepari na Ujamaa kinyume nyume na yawezekana wewe ukikuwa bado ukisoma shule...

Na ninakuhakikisha kwamba mashirika yote ya Umma yalikuwepo na yakifanya kazi vizuri sana isipokuwa tatizo kubwa lilikuwa urasimu, wizi na ufisadi ulofanyika makusudi ktk kipindi cha kwanza cha mwinyi kuyaua hayo mashirika kama vile Mramba alivyoliua shirika la ATC makusudi.

Viongozi wote wa mashirika haya walitajirika kipindi cha Mwinyi kama tunnavyoona leo viongozi wa serikali na taasisi zake wakijitajirisha chini ya Utawala wa Kikwete. Sasa itaka[po fika mashirka hata binafsi kufa tutakuja sema Ubepari hauna faida?..hali tatizo sii uwekezaji chini ya mfumo wa Kibepari bali ni sisi WATU wenyewe..
Leo hii huwezi kupata huduma safi pasipo kutoa kitu, hakuna biashara ama kiwanda hata kimoja kisicho ibiwa.. wizi imekuwa part ya matumizi ktk mahesabu.

Hadi Mwinyi anaingia madarakani, hayo mashirika ya Umma yalikuwa hayazalishi kwa kiwango chake..hili lilikuwa tatizo la kiutendaji na sii la viwanda ama mashirika ni sawa na tatizo la Umeme leo hii wakati Mitambo yetu inauweza wa kuzalisha MW 3000 ila ni asilimia 15 tu ya umeme huo unazalishwa! tatizo la maji nalo ukiangalia linachangiwa na utekelezaji na sii kutokuwepo kwa maji ama mitambo..

Sasa itakuwa ujinga mkubwa ukinambia jibu sahihi hapa ni kuuza mitambo yote ya Umeme kwa sababu ni magofui hali sisi wenyewe ndio tumeshindwa kuikarabati na tatizo sii fedha wala uwezo wa wataalam wetu..
Kifupi, Tatizo la Umeme na maji nchini ni tatizo linalosababishwa na WATU kama vile ajari inaposomwa kwamba sababu imetokana na Human error!
na kikubwa hapa mkuu wangu hatubishani ili mradi bali kuitafakari hotuba ya Mwinyi na kuapata jibu..

Haya, ukimsoma Waberoya utashindwa hata kuelewa anacholenga kwani ni huyu huyu anayesema Azimio la Arusha halikuwa na maana lakini akiunga mkono maneno ya Mwinyi kwamba halijafa!..I mean anajipinga mwenyewe kwa kusifia kifo cha Azimio hilo wakati huo huo akikubaliana na Mwinyi kwamba Azimio la Arusha limeboreshwa..
Mkuu nisome vizuri maeklezo yangu yote yanazunguka ktk kupinga kauli ya Mwinyi.. Ubora ama Ubovu wa Azimio la Arusha haikuwa Issue kabisa ktk maelezo yangu lakini maadam unataka tuzungumzie mazuri ya Ujamaa naweza kabisa kutafuta muda tukadali ingawa swala hili tumekwisha lizungumzia sana huko nyuma..Kisha basi haiwezi kukusaidia chochote kwani maadam umeisha ondoka ktk Ukristu (Ujamaa) ukasilimu na kuwa Muislaam Bepari) itakuwa kazi kubwa kwangu ama Padre kukurudisha ktk Ukristu -Usishtuke, natoa ni mfano tu mkuu!
 
We are wasting our time kwenye hili Azimio,kila kukicha Maazimio tu..Hivi hatuwezi kwenda mpaka maazimio?
 
Nadhani wengi tunakumbuka pale Mwalimu alipolalamika kuwa ni kweli walikuwa na makosa. Lakini badala ya kurekebisha makosa tuliamua kubeba makosa na kuondoa yale yaliyokuwa mazuri. Hili lilielekezwa kwa mzee Mwinyi moja kwa moja na serikali yake. Kuwa badala ya kurekebisha masharti na kuweka yale ambayo tulidhani yanafaa, tukaamua kufuta masharti bila kuweka kitu mahala pake. Huu ulikuwa upungufu mkubwa na uongozi ndo wa kubeba lawama.

Mashirika ya umma, sera ilikuwa kuuza yale yaliyokuwa kwenye hali mbaya, kuyarekebisha yale yaliyokuwa hayafanyi vizuri lakini yalikuwa hayaleti faita na tija kama ilivyotarajiwa. Lakini tafsiri ya uongozi wa Mzee mwinyi na waliofuata baadaye ilikuwa ni kuuza yoote. Hata yale yaliyotakiwa kuingia ubia, utekelezwaji wake imekuwa ni balaa na uongozi wa serikali umeonekana kuwa haupo kabisa.

Nakumbuka wakati NBC inavunjwa na kuuzwa, ni kweli benki ilikuwa na matatizo. Lakini mengi yalikuwa ni matatizo ambayo yangetatuliwa. Washauri wa world bank walikuwa wakisema the Bank was too big. Ndo maana ikalazimika kuvunjwa. Lakini historia imetufundisha kuwa mambo yote hayo yalifanyika ili kuwanufaisha wanunuzi na NBC haikuwa kwenye status ya kuitwa too big bank!!

Kifupi ni kuwa Nyerere hakuwa malaika, alikuwa kiongozi wa kawaida, Lakini wakati wa Nyerere uongozi ulionekana; kwa mazuri na hata mabaya pia. Sasa hivi kimsingi uongozi hauonekani na inaonekana nchi inaenda tu kama vile maji yanapomwagwa mlimani. Hushuka bondeni kwa kufuata mtelemko ulio mkali zaidi.

Tumeshindwa kusema tunafuata mfumo gani, bali tumetunza maandishi ambayo hatuyaamini. Waulize CCM, hivi ujamaa na kujitegemea ni nini hasa katika mazingira ya leo? Ujamaa na kujitegemea bado unatajwa katika katiba ya nchi na ni CCM wenye uwezo wa kuirekebisha. Hivi ni kweli kuwa viongozi waliopo sasa hivi hawana vichwa wala fikra za kurekebisha hayo maandishi? Au wameona kuwa kwa kuwa maandishi hayafuatwi hivyo hakuna maana ya kuendelea kuwepo? Au yoyote yatakayokuwepo, we fanya yale yanayokuzukia kichwani kila siku?

Haishangazi basi kuwa rushwa na ufisadi ndo mfumo wetu. Sababu ni kuwa hakuna mfumo wowote tunaoufikiria wala kuuamini. Tunaendeshwa na common interrest ambayo ni kufanya kazi serikalini na kupata mishahara, posho na marupu rupu mengine. Kujikusanyia mtaji na kuanzisha biashara nyingi hapa na pale zitakazotuhakikishia mapato pale tutakapotoka madarakani. Hatuna dira, hatuna mwelekeo. Na kusema kweli mzee Mwinyi ndo mwanzilishi wa hii ya nchi kuwepo bila mfumo wala mwelekeo unaoeleweka na cha kushangaza zaidi CCM zote zilizofuatia zimeamua kufuata mfumo huo. Huo ni mfumo usiomwajibisha kiongozi kwa lolote na hivyo ni rahisi tu kwa kiongozi yeyote kusema "mimi sikuhusika". Ikiwa mwinyi hakuhusika na kuangamia kwa mashirika ya umma na kuingia kwa rushwa na iliyokithiri serikalini ni nani basi alihusika? Rais anawajibika kwa makosa ya serikali yake, na mzee mwinyi hana budi kukubali kuwa alikosea ili wengine warekebishe alipokosea.
 
Kinachoendelea Tanzania sasa si Ubepari si ujamaa na kujitegemea. Kinachoendelea ndani ya mifumo ya utawala ni ukosefu wa uongozi. Sera ya ujamaa na Azimio lake la Arusha havikuleta tija kwa sababu uongozi ulilegalega na sheria zikabaki kwenye makaratasi tu.

Azimio la Arusha lilikuwa na miiko ya uongozi na hasa msingi wa miiko hiyo ilikuwa kuzuia viongozi wa umma kutumia vyeo vyao kujinufaisha. Au kuzitumia ofisi zao kama za binafsi. Ikiwa masharti haya hayakuwa na maana kama Waberoya anavyosema mara kwa mara kwa nini walilazimika kukaa Zanzibar na kutangaza Azimio la Zanzibar? Ni kweli kutokana na udhaifu kwenye uongozi sheria zile au masharti yale yalikuwa hayafuatwi. Lakini ikiwa hayakuwa na maana kwa nini walitangaza kuyaondoa? Lazima kulikuwa na sababu.

Masharti yale ya uongozi ndo legacy pekeee ya Azimio la Arusha iliyokuwa imebaki. Kimsingi mambo ya umilikaji wa njia kuu za uchumi kuwa kazi ya state ilishaonekana kushindwa. Na sera zilishabadilishwa. Lakini mwiba uliokuwa umesalia ni masharti ya uongozi ambayo kimsingi Mwinyi aliyaondoa kupitia hilo la Zanzibar. Je baada ya kutangaza kuwa viongozi wa umma wanaruhusiwa kufanya biashara ni sheria gani nyingine iliwekwa mahali pake?? Hakuna!! Sheria ni maandishi. Utekelezwaji wake hutegemea zaidi mifumo iliyopo na uongozi wake. Lakini huwezi kusema kuwa, mbadala wa kushindwa kwa uongozi kusimamia sheria au masharti ni kufuta sheria au masharti hayo.

Kwa kutangaza Azimio la Zanzibar, Mzee Mwinyi na serikali yake waliondoa masharti ambayo hadi hapo ni kweli yalikuwa hayatekelezwi kikweli kabisa. Lakini angalau yalikuwepo! Ni nini athari za kuwaruhusu viongozi wa umma kufanya biashara bila kuwepo na masharti ya aina yoyote? Kwa nini viongozi wa wakati huo waliona ni lazima masharti hayo yaondolewe? ...... Kulikuwa na hatari kuwa pamoja na kuwa wanavunja hayo masharti, iko siku watahukumiwa nayo. Ndo maana wakatangaza kuyafuta ili kurasmisha kitu walichokuwa wakifanya.

Kipimapembe,

Umetaja Masharti na Seria hivyo ni vitu viwili Vyenye nguvu tofauti. kimoja ni dhaifu (masharti) kingine kina Nguvu (Sheriea) Ina waundaji, wasimamizi, walinzi na Watekelezaji.

Halafu kuna Biashara na Wizi Kimoja ni Sawa kwa mujibu wa sheria (Biashara) na kingine si sawa Wizi. Sasa hata kama hao vingozi wameruhusiwa kufanya biashara baada AZ, haikuwa na maana wawe Wezi na au Wakiiba ndio basi hatuna cha kuafanya eti AD Limefutwa na miiko yake imekwenda.

Sheria za nchi ziko wapi na Wananchi tuko wapi?
 
Alibaba,

Huwezi kujua tofauti ya wizi na usio wizi kama hakuna masharti au sheria zinazoweka tofauti hizo. Sheria na masharti ni vitu tofauti. Miiko ya uongozi ndugu yangu haikuwa sheria, kwa nini waliiondoa?? Kwa nini hawakuiacha kama walivyoacha ujamaa na kujitegemea kwenye katiba??
 
Dear Waberoya;

Kwa waraka huo naona tumeelewana kiasi kikubwa, nadhani kuna umuhimu wa kukubaliana na wezetu tuchukue yale mazuri toka AD ambayo bado yangeweza kutumika katika siasa zetu za leo na kuziboresha.

Sijui kama ulibahatika wakati AD limeshika kasi kulikuwa na vijembe vya Propaganda kila baada ya Taarifa ya Habari na Mada ya siku huja katika mazungumzo baada ya habari saa 2 15 kila siku usiku.

Kijembe kimoja kilikuwa kinasema: Mwenzetu huyu anaumwa, tena anaumwa sana........................Unyonyaji ni Haramu!

Ikiwa AD limefutwa na miiko yake pamoja, SHERIA za nchi bado zipo nazo zinasema: WIZI ni HARAMU!

Asante, afadhali mpo mliokuwepo kipindi hicho, maana yake inaonyesha humu kuwa kuna watu wa zama hizo, bado wanaona kuna walakini!

Waberoya,

Kusema leo turudi kwenye AD ni kupoteza muda. AD ilikuwa kwa ajili ya chama kimoja. Haya mambo mazuri ya AD yanatakiwa yaingizwe kwenye katiba na hiyo AD waiache ijifie. Kubadilisha mambo leo hii ni kupoteza muda mwingine kwani katika kipindi hiki, kuna mazuri mengine mengi tu yametokea. Itakuwa ni kichekesho kujifanya hatuyaoni.

.

MWISHO: Niko na wewe katika hili la Madaraka ya RAIS lazima yapunguzwe.

Asante Sikonge, asante tena kwa kuonyesha kulizungumzia hili wakati tuna vyama vingi tunapoteza muda pia, ILA kuna challenge nimesema kwenye post zilizopita. IKIWA leo tunataka AD, basi tukubaliane wananchi, tuanzishe wananchi, lipate nguvu ya serikali, na liwe na watu maalumu wa kulitekeleza. Ili iwe hivyo maana yake lazima Katiba ibadilishwe na iruhusu ushiriki (baraza la kusimamia AD) katika maamuzi ya serikaLI. MY ARGUMENT LIES ON THE FACT THAT usitegemee CCM leo na JK wakasema turudi kwenye azimio, mbaya zaidi AD halina nguvu za kisheria NDIYO concept yangu ya DINI ikaingia.

Hakuna jinsi ya kusema tu kwa maneno AD halafu watu waseme ndiyo, watu hawamogopi Yesu wala Mtume MAW ndiyo ije AD!

Wanaolitaka wanasema tu, how we will implement hawasemi.....ugonjwa na upofu wa kupenda kitu bila kuangalia implementation. Ukitaka ku-implement AD then hauna tofauti kabisa na chama cha siasa leo hii chenye sera za AD!Lakini sio kutegema Kikwete eti aanzishe hayo mavuguvugu

Sikonge,
Viongozi wote wa mashirika haya walitajirika kipindi cha Mwinyi kama tunnavyoona leo viongozi wa serikali na taasisi zake wakijitajirisha chini ya Utawala wa Kikwete. Sasa itaka[po fika mashirka hata binafsi kufa tutakuja sema Ubepari hauna faida?..hali tatizo sii uwekezaji chini ya mfumo wa Kibepari bali ni sisi WATU wenyewe..
Leo hii huwezi kupata huduma safi pasipo kutoa kitu, hakuna biashara ama kiwanda hata kimoja kisicho ibiwa.. wizi imekuwa part ya matumizi ktk mahesabu.

Hadi Mwinyi anaingia madarakani, hayo mashirika ya Umma yalikuwa hayazalishi kwa kiwango chake..hili lilikuwa tatizo la kiutendaji na sii la viwanda ama mashirika ni sawa na tatizo la Umeme leo hii wakati Mitambo yetu inauweza wa kuzalisha MW 3000 ila ni asilimia 15 tu ya umeme huo unazalishwa! tatizo la maji nalo ukiangalia linachangiwa na utekelezaji na sii kutokuwepo kwa maji ama mitambo..


Haya, ukimsoma Waberoya utashindwa hata kuelewa anacholenga kwani ni huyu huyu anayesema Azimio la Arusha halikuwa na maana lakini akiunga mkono maneno ya Mwinyi kwamba halijafa!..I mean anajipinga mwenyewe kwa kusifia kifo cha Azimio hilo wakati huo huo akikubaliana na Mwinyi kwamba Azimio la Arusha limeboreshwa..
!

Mkuu nadhani kwa upeo wetu wa kipindi hiki lazima tufanye analysis na kupata ukweli kuwa AD lilikufa kipindi cha Mwinyi kwa hiyo aliliua Mwinyi!

Sidhani kama kitu kikimfia mtu mikononi basi rais wa wakati huo ndiyo kaliua, sijapata convincing reasons inayo suggest hivyo.

Ninachoona ni kuwa AD ilikufa natural death, ina maana hata JKN mwenyewe angekuwepo lingekufa, AD halikupokelewa na kila mtu jamani, acheni kutaka kusema mind za watanzania zote zilikuwa sawa! hapa ni uongo!

Nimesema AD was a call for unity, moral, au hamasa, it was like Jeshini mnapopigana na kupiga mayowe ya kuwaongezea mukali wa kupigana, it was as a beliefs na miongozo yake ya uongozi IMEJAA --COMMON ETHICS AND COMMON SENSE, COMMON HUMAN RESPONSIBILITIES--ambayo kwa yeyote mwenye akili hata leo hii lazima afuate!

Azimio linasema swala la kutokutafuta misaada nye ya nchi, sidhani kama leo hii JK anaenda kutafuta fedha kwa sababu hakuna Azimio. Ni kutokuwa na akili tu ya kuwa ukiwa ombaomba hutakuwa na uwezo wa kufikiri kuzalisha! hata wanaotoa misaada wanafanya hivyo purposely

Issue siyo waberoya hapa mkuu, issue ni hoja, weka hoja na sio kutaja waberoya, nenda kwenye post yangu yoyote jibu word to word kama anavyofanya Sikonge na Mag3 Mjadala unanoga ikiwa hivyo, wahubiri wa AD wamekimbia humu, wameshindwa kusema kuwa AD ilikuwa dini, ilikuwa hiyari, ilikuwa ukubaliane na JKN anasema nini, lakini kama haikutoka moyoni ..kilichoendelea ni unafiki! na ndiyo maana JKN alivyotoka madarakani tu watu wakawa huru!

Mchana wanashinda kwenye hotuba na hamasa za JKN usiku wanafanya tofauti, this happened hata Nyerere akiwa bado yu hai , bado yu madarakani, nadhani Sokoine unakumbuka kazi yake kubwa ya kuweka usawa, Mwinyi anasema mabepari walikuwepo hata nyakati hizo jamani! kabla ya Azimio walikuwepo, hawa watu hawawezi kubadilika kwa maneno tu!

Mwinyi anaingia madarakani, japo pia unasema viwanda vilikuwa havizalishi sana, sijajua kwa nini, naweza kusema tulikuwa na wataalamu wachache sana, leo hii mashirika ya ATC, TRL, General tyre yanakufa si kwa sababu ya azimio jamani, tuna UGONJWA MWINGINE WA TOFAUTI

Tumeona na hakuna aliyepinga kuwa sheria na katiba are far superior than AD, kuwaweka watu sawa, AD ilikuwa ni wito, halikuwa na nguvu ya kisheria na ndiyo maana limezimia kama sio kufa. Sheria zitamlazimisha mtu ku-obey

Let me ask u; hivi leo ikatungwa sheria hatutaki kiongozi kufanya biashara serikalini, hii sheria inahitaji AD???????

Katika maisha ya kila siku mtanzania aliyelelewa kwenye AD anaishi vipi?, ufanye kazi halafu ugawane mapato na wenzako(directly au indirectly)? jamani ujamaa kama ujamaa unaenda kinyume na tabia za kibinadamu, choyo, ubinafsi, na ndiyo ujamaa kwengine duniani viongozi walikuwa ma-dikteta, JKN WET hakuwa dikteta! unaona kabisa failure ya AD hata kabla haijaanza!!!!!

Kama unataka kupiga shule ya ujamaa karibu, ila sema uzuri wake na ubaya wake!

I dont support ujamaa neither that Ubaperi, we need to have our own system that benefits us, kubaki kusema ujamaa na ubepari ni matusi ya ukoloni pia na walioendelea. I ADORE JKN kwa sababu ujamaa wake ulikuwa wa tofauti, ulikuwa hybrid hautaupata popote , ile ilikuwa yake yeye! hata kama ulifeli alionyesha njia na kuweka mlango kuwa sisi WEUSI wengine, we too we can think of our systems systems that can accomodate economic crisis, innovations, climate change, technocracy, researches,terrorist, globalisation, CULTURE etc, systems hizi sio ujamaa wala ubepari ! I thought wanafunzi wa JKN mgejaribu ngau kufanya kama yeye, haiwezekani karne ya 21 mtu ukasema ujamaa au ubepari, lazima kuna tatizo sehemu! ndiyo maana kuna watu wanamwona JKN kama saint he was free thinke and a man of action! we can be like him, take his idead, chukua mzuri acha mabaya, tusonge mbele SIYO AD , AD, AD.. common!

I insist AD ilikufa Natural death! tabia zetu hazifai kuishi kwenye AD, na ukitaka ziishi humo, basi liwe na nguvu ya kisheria, siyo mahubiri kama ya kanisani, nikatoa joke sehemu ni kasema kama mnadhani AD is the only solution, basi tunahitaji azimio lingine tena, ambalo ni kubadilisha tabia za watu kwanza kabla ya AD!

I repeat haiwezekani uwezo wetu wa kufikiri uishie kwenye ujamaa au ubepari!

Jibu hoja mkuu, copy my particular post jibu na sio kuongelea mbali na kutajana majina!

This is what I am thinking! by the way, Mwinyi lolote atakalosema halimaanishi lipate baraka zako au zangu bado anaweza kukosolewa kwa lolote lile! hasa kama anataka kudanyanya ulimwengu kwa namna yoyote ile

wewe unamwona mwongo kwa sababu unaona aliliua

mimi ninamwona mwingo kwa sababu AD halipo, halikuwepo! na hakuna namna ambayo lingeweza kusustain kwa tabia za watanzania hwa ninaowaona leo! AD ilikuwa dini, ethics zile ni common sense tu ambazo hazikuhitaji kutukanw uwa nyie wavivu kafanyeni kazi! naama kama Nyerere aliona kuna tatizo na tabia za watanzania, basi bado hatujapata ufumbuzi wa kukabiliana na matabia yetu mabaya ya uchoyo, unafiki, majungu, uvivu, ubinafsi au umimi n.k,

I think unanipa kibarua cha kufikiri kama mwalimu na kutoka na system yangu, ila sio kuwa obsessed au kuwa possed na mwalimu! nikiona mtu ana insist hivyo narudi nyuma na kuona negative impact za Mwalimu zinafanya kazi hata leo! that we can not think differently, wafuasi wa JKN hapa mnajidhalilisha, mmeumbwa kuleta change, JKN alifanya yake, chukueni yake mazuri , modify songeni mbele acheni kujidhalilisha kimawazo namna hii!
 
Alibaba,

Huwezi kujua tofauti ya wizi na usio wizi kama hakuna masharti au sheria zinazoweka tofauti hizo. Sheria na masharti ni vitu tofauti. Miiko ya uongozi ndugu yangu haikuwa sheria, kwa nini waliiondoa?? Kwa nini hawakuiacha kama walivyoacha ujamaa na kujitegemea kwenye katiba??

Hapa ndio mnapokosea sana, sijui tuwaeleze vipi, haya mimi ni mwizi, nimeamua kuiba kwa hiyari yangu, sijali cha raia wala nani? utanizuia kutokuwa mwizi kwa sababu ya miiko?? Ikiwekwa na kuandikwa ukutani basi nitaacha?

Nani siyejua kuwa ili baya na ili zuri? yaani tabia ya asili ya mwanadamu inaweza kuzuiwa na miiko?? na siyo sheria?? you must be kidding!
 
Mkandara, nafikiri ulitaka kumjibu Ngekewa.

Nafikiri wote tunakubaliana sasa kuwa kwenye UONGOZI wa nchi ya Tanzania, hakuna sheria inayowabana viongozi katika maamuzi yao ya utawala. Hata kama sheria zipo hazifuatwi. Na kibaya zaidi, hakuna chombo sawa na mahakama ya viongozi ambayo itahakikisha viongozi wetu wanashughulikiwa mara pale wanapovunja sheria.

Hii ilitakiwa iwe kazi ya bunge ila bunge letu la leo, wabunge wengi wa CCM ni au wa kuchaguliwa na au wameingia kwa pesa za EPA/Rostam Azziz (soma sahihi yangu). Sasa hata mbunge fulani akisema kitu na hasa hawa wa CCM, basi wanamtishia kwa kumuonyesha mkanda siku akipokea milioni 5 za RA na jamaa analowana.

Labda kama wabunge wengi wakiingia kwa kutokutumia rushwa, mambo yanaweza kubadilika. Ila kwa hali inavyoonekana sasa, mwaka huu wengi wataingia kwa kutumia nguvu ya pesa. TAKURURU wataweka data ili kumrudi mtu yeyote atakayejifanya much know. Hii itaendelea hadi nguvu kutoka nje ije iondoe hii hali.
 
Kwanza kabisa pamoja na kuwa mimi ni Muumini mkubwa wa Azimio la Arusha, nakubali kuna mambo yaliyofanyika na kupokelewa visivyo.

Azimio kama Biblia au Quran ni maandiko ambayo yanaelezea azma ya jamii ifanye jambo fulani. Ni wale wanaopokea mafundisho na maandiko ambao wana wajibu wa kufanyia kazi kilichoandikwa.

Hata kama tukidai kuwa Azimio zilikuwa ni ndoto au kufikia kudai kuhalalisha wanachosema wengine kuhusu Ujamaa na kudai kuwa ni Utopia, je iweje leo hii Wazungu, Wahindi, Waarabu na hata Wachina waweze kujenga nchi zao na kuendeleza maendeleo kutokana na ndoto na njozi za waasisi wa Mataifa yao?

Leo hii huishi kusikia Watanzania wakisifia American Dream ambayo ndiyo imekufikisha hapo. Lakini si ilianza kama njozi ya kujenga Taifa litakalo kuwa mahiri, huru na linalojitegemea na kutoa haki kwa watu wake? Infact Ukilisoma Azimio la Arusha with open mind, you will find out it was a Blue print that outlined several things that could help and shape us as Taifa to become self sufficient.

Ni watu, anzia Nyerere mwenyewe, Kawawa, Sokoine, Kambona, Malecela, Msuya, Mwinyo, Mkapa na hata leo hii Kikwete na timu yake ambao ndio walioharibu utimilifu wa ndoto hiyo.

Kila mmoja wa niliwataja hapo juu na wafuasi wao, kwa namna moja au nyingine walihusika kuharibu na kudhoofisha azma na ndoto hiyo.

Ikiwa Keneddy alipoona Warusi wanaruka nje ya anga akasema "Nasi tutafika Mwezini", iweje Wananchi wake walilipokea tamko hilo kama changamoto na miakak karibu baada ya Yuri Gagarin kuzunguka dunia, Amstrong na wenzake wakakanyaga Mwezini, sisi tukae mguu pande na kuinua mikono juu na kudai kuwa Azimio limeshindwa au lilikuwa ni baya na kukubali kunyong'onyea? Kwa nini nasi tusiwe kama watuwa Dubai ambao waliazimia katia maandiko na ndoto kuwa Dubai utakuwa mjii mkuu wa kibiashara Duniani na leo hii tunaona kwa kasi ya juu kukaribia kwa utimilifu wa ndoto hiyo?

Ukisoma Azimio, hakuna sehemu hata moja iliyosema Watu wanyanganywe nyumba, watu wanyanganywe viwanda au mambo yoyote yaliyotokea baada ya kutangazwa Azimio ambayo tunadai kuwa ni chimbuko la Tanzania kuwa masikini na kukosa maendeleo.

Azimio lilitamka, ;
(h)Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda
sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia
muhimu za kuukuza uchumi; na
(i) Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe,
kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili
kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya
mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine
na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani​
na siasa ya watu wote kuwa sawa.

Lakini kwangu mimi tamko hili nimelipokea tofauti na nitalieleea tofauti kinyume na kilichotokea. Mapokeo yangu ya kuwa Serikali ni lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia muhimu za kukuza uchumi ina manaa uwepo wa udhibiti, sheria na kanuni ambazo zitahakikisha kuwa kila kitu kinafanyika ipaswavyo. Hata kama ilivyotokea kuwa mashirika binafsi ya "Wazungu na Wawekezaji wa nje ya nchi" yalibinafsishwa haina maana kuwepo kwa GAPEX, NBC au Lake soap kulitupa mwanya wa kushindwa kuwa makini na kudhibiti uendeshaji wa mashirika na viwanda hivyo.

Hata kipengele (i) kinavyoendelea kusema ni Wajibu wa Serikali kuingilia kati kwa vitendo vya maisha ya uchumi, it all falls on regulation, monitoring and even revenue collection and ensure transparency, openness and correct measurements when things go awry.

Kilichotokea Marekani in the last 3 years mpaka merikebu imegota mchangani ni kujivua kwa Serikali ya Marekani hivyo vipengele viwili hapo juu ambavyo vipo kwenye Azimio, na matokeo yake ni udhaifu wa Watu na uongozi ambao ulikaribia kulifilisi Taifa Tajiri kama Marekani!

Kwetu Tanzania, tulichofanya ni kukiuka kipengele hiki cha Azimio;
Kuona kwamba Serikali inaondoa kila namna ya dhuluma,​
vitisho, ubaguzi, rushwa na upotofu;
kitu ambacho kilifanywa na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Chama na Serikali na Uongozi wa Juu wa nchi ukiongozwa na Mwasisi wa Taifa, kwa udhaifu ulifumbia macho makosa ya kiutendaji na ndio maana uwiano ukakosekana, usimamizi ukapotea, kila mtu akajifanyia analotaka na kadri mambo yalivyoendelea kudoda, tukaanza kutafuta mchawi wa kubebesha lawama huku tukisahau kuwa ni sisi wenyewe kama Wananchi na Viongozi wetu tulioruhusu kuzorota kwa kila kitu na wala si maandiko ya Azimio.

Kama jinsi vile kina Karl Peter na wenzake walivyotumia Biblia kutunyanyasa, kutunyonya na kututawala kwa kutufanya tuamini kuwa sisi ni watu duni na wa hali ya chini (inferior), ndivyo watendaji wa TANU na Serikali yake walivyoanza kuwaburuza Wananchi na kuachia kila kitu kifanyike kiholela na mpaka mchwa wakatafuna kila kitu.

Kama kungekuwa na umahiri wa kuwa thabiti na kakamavu katika safu ya Viongozi wetu na hata Wananchi, tusingefika hapa tulipo.

Azimil lilitamka wazi nia yetu ya kuachana na Unyonge, kuondoa Ujinga Umasikini na Maradhi na kutumia Juhudi na Maarifa na mfumo wa Kijamaa kufanikisha azma hiyo. Lakini udhaifu wa kibinadamu ndio uliofanya Wanasiasa waendelee kuwa ni wanyanyasaji, wasio wasikivu (Nyerere na U-Haambiliki wake pamoja na kuwa I will never cease to love the guy) na kwa udhaifu wa Wananchi, wakawa wafuasi walioa waoga na rahisi kurubuniwa.

Waliokuwa wa kima cha chini, wakaendelea kuwa kima cha chini zaidi na wale waliokuwa kima cha juu wakaendelea kuneemeka na wa kima cha kati badala ya kunona na kupanuka wakashuka daraja na kuelekea kuwa kima cha chini.

Aidha mgongano wa kifikra ndani ya TANU na uongozi wake ambao ulikuwa ni wa kudhibiti mawazo na maoni lakini ukishindwa kudhibiti vitndo vichafu, ndio uliotufikisha hapa tulipo. Kama wangewekeza nguvu kudhibiti vitendo vichafu na kurudi kwenye Juhudi na Maarifa na kumulika mianya ya kulinyonya Taifa kulikofanywa na Viongozi na Watendaji, tungepiga hatua kubwa sana.

Sasa ninapohoji kauli ya Mwinyi ni kutokana na ukweli kuwa yeye alikuwa na nafasi ya kurekebisha kasoro za kiutendaji na kitabia na si kusema kwa kuwa Nyakyoma kaliangusha GAPEX, basi tunauza shirika kwa Botha aliendeshe na sisi tushangilie anachofanya Botha!

Cha kujiuliza iweje Botha aje atumie nyenzo hizi hizo ambazo Nyakyoma alikuwa nazo lakini Botha anapata mafanikio makubwa? Jibu lake ni Uongozi mahiri na fanisi.

Ndio maana leo kuna watu wanaoshangaa ninapoelekeza vidole vya kuwalaumu Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwa kuendeleza udhaifu ule ule wa Nyerere katika uwajibikaji na kuwa na uongozi imara. Wao Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamepewa nafasi ya kurekebisha kasoro za kiutendaji, lakini badala ya wao kuwka mguu chini na kisimika nguvu za kulizalisha Taifa upya lenye watuwaadilifu, wachapa kazi , wawajibikaji wenye juhudi na maarifa katika kusukuma gurudumu la maendeleo na hivyo kuhakikisha kuwa tunakuwa Wazalishaji, Wamilikaji na Wanufaika wa Maliasili yetu kwa kujiendesha wenyewe, wao wamekimbilia kukabidhi dhamana hiyo kwa kina Sinclair, IPTL, na hata leo tunaenda Uturuki na kwingineko tukiwaomba waje kutuonyesha jinsi ya kulima na kufanya kazi!

U wapi mwako ndani ya safu ya Uongozi wa kuwasisimua Watanzania warudi kwenye misingi ya awali iliyoafanya wakaandamana kwa nguvu kupigania Uhuru, kupiga vita unyonyaji na hata kulishabikia Azimio? Je ni wajibu wa kina Barrick na Shoperite? kwa nini tusimfuate Bakhresa na kumuuzia yeye NMC au kumpa wajibu wa kuwa NMC yetu kwa kuwa yeye ni Mzawa na anatamkwa kwenye Azimio kuwa apewe kipaumbele
(f)Kwamba kila mtu anayo haki ya kupata malipo ya haki
kutokana na kazi yake
(g) Kwamba raia wote kwa pamoja wanamiliki utajiri wa asili
wanamiliki utajiri wa asili wa nchi hii ukiwa kama dhamana​
kwa vizazi vyao;
ili kuhakikisha ni sisi tunaokuwa Wanufaika wa mali asili yetu?

Watu wakae chini na kukubali kuwa hawajakaa chini na kutafakari ni vipi Azimio lilikuwa na maana gani na ni jinsi gani wao katika nafasi zao wanaweza kulifanikisha Azimio litimilike na hivyo Tanzania iweze kufurahia matunda ya Tanzanian Dream.

Leo hii miaka karibu 20 tangu tulipokumbatia mfumo mpya wa kiuchumi, bado tunashindwa kujingoza na kuleta maendeleo. Umasikini bado uko pale pale na lile tabaka la kati ndio linafutika!

Nimesema mapokeo na utekelezaji wa Azimio ulifanyika kwa namna tofauti na leo hii akipewa mtu mwenye upeo mzuri atalitumia Azimio hilo hilo na kuleta maendeleo. Mfano, tulipoamua kutaifisha umiliki wa uzalishaji mali, hata kama ni kosa la kiutendaji na si Azimio lilivyotaka, tuliposema wamiliki wa Uchumi wawe ni Watanzania, je tulijielewa tulikuwa na maana gani au tulishindwa nini kuhakikisha kuwa Serikali iendelee kukusanya kodi na kusimaia kanuni na sheria na mashirika, viwanda, taasisi na mfumo mzima wa kiuchumi unakuwa mikononi mwa Wananchi wakiwa true shareholders na si kila kitu kumilikiwa na Serikali as an entity of political team?

Leo hii tuna nafasi nzuri sana ya kumilikisha Tanesco, TRL, ATC, NUwa, Dawaco na hata Bodi za Mazao kwa Serikali kuuza hisa zake kwa Wananchi na kujivua uendeshaji na kuwaachia Wananchi waendeshe mashirika haya.

Ikiwa Bakhresa, Mengi, Manji, Kimaro wa Precision na Wazawa wengine wana uwezo wa kuwa wazalishaji wenye umahiri na kuwa na mafanikio, kwa nini tukimbilie kutafuta Mchina, Mthailand, Mjerumani au Mkuwait waje kuendesha makampuni na uchumi wetu?

Au nao kina Bakhresa na Kimaro hatuwaamini kama vile tusivyotaka kuwaamini Wakikuyu, Watutsi na Waankole wanapotuomba ardhi kuja kulima tunawakatalia lakini tunakwenda China na Sweden na kuwaambia njooni ardhi tunayo bwelele?

Ukiangalia sana with open mind, it was not Azimio which failed us, bwana, but UONGOZI kitu ambacho kimeendelea hadi leo hii kuwa ndio udhaifu wetu!
 
Je Azimio la Uhuru la Marekani lilifanikiwa? Je lilipotangazwa Marekani ilikuwa na kila kitu kilichokuwepo au kilichohitajika kukamiliza njozi yake? Liliposema kuwa "we hold these truths to be self evident" ina maana watu wote walikwua sawa wakati ule? Je watu weusi wa Marekani walikane Azimio lao kwa sababu wakati linatolewa wao bado walikuwa ni watumwa?

Azimio la Arusha huwezi kulielewa isipokuwa kwa kuliangalia kama a declaration of certain Principles ambazo zinamfanya Mtanzania kuwa ni Mtanzania. Haijalishi kaanm mimi sikuwa na shamba au nilikuwa tofauti au wakati linatolewa sikuwa hai.
 
Kwanza kabisa pamoja na kuwa mimi ni Muumini mkubwa wa Azimio la Arusha, nakubali kuna mambo yaliyofanyika na kupokelewa visivyo.

Azimio kama Biblia au Quran ni maandiko ambayo yanaelezea azma ya jamii ifanye jambo fulani. Ni wale wanaopokea mafundisho na maandiko ambao wana wajibu wa kufanyia kazi kilichoandikwa.

Hata kama tukidai kuwa Azimio zilikuwa ni ndoto au kufikia kudai kuhalalisha wanachosema wengine kuhusu Ujamaa na kudai kuwa ni Utopia, je iweje leo hii Wazungu, Wahindi, Waarabu na hata Wachina waweze kujenga nchi zao na kuendeleza maendeleo kutokana na ndoto na njozi za waasisi wa Mataifa yao?

Leo hii huishi kusikia Watanzania wakisifia American Dream ambayo ndiyo imekufikisha hapo. Lakini si ilianza kama njozi ya kujenga Taifa litakalo kuwa mahiri, huru na linalojitegemea na kutoa haki kwa watu wake? Infact Ukilisoma Azimio la Arusha with open mind, you will find out it was a Blue print that outlined several things that could help and shape us as Taifa to become self sufficient.

Ni watu, anzia Nyerere mwenyewe, Kawawa, Sokoine, Kambona, Malecela, Msuya, Mwinyo, Mkapa na hata leo hii Kikwete na timu yake ambao ndio walioharibu utimilifu wa ndoto hiyo.

Kila mmoja wa niliwataja hapo juu na wafuasi wao, kwa namna moja au nyingine walihusika kuharibu na kudhoofisha azma na ndoto hiyo.


Ukisoma Azimio, hakuna sehemu hata moja iliyosema Watu wanyanganywe nyumba, watu wanyanganywe viwanda au mambo yoyote yaliyotokea baada ya kutangazwa Azimio ambayo tunadai kuwa ni chimbuko la Tanzania kuwa masikini na kukosa maendeleo.

Azimio lilitamka, ;
(h)Kwamba ili kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi unakwenda
sawa Serikali lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia
muhimu za kuukuza uchumi; na
(i) Kwamba ni wajibu wa Serikali, ambayo ni watu wenyewe,
kuingilia kati kwa vitendo maisha ya uchumi ya Taifa ili
kuhakikisha usitawi wa raia wote na kuzuia mtu kumnyonya
mtu mwingine au kikundi kimoja kunyonya kikundi kingine
na kuzuia limbikizo la utajiri kufikia kiasi ambacho hakipatani

na siasa ya watu wote kuwa sawa.

Lakini kwangu mimi tamko hili nimelipokea tofauti na nitalieleea tofauti kinyume na kilichotokea. Mapokeo yangu ya kuwa Serikali ni lazima iwe na mamlaka kamili juu ya njia muhimu za kukuza uchumi ina manaa uwepo wa udhibiti, sheria na kanuni ambazo zitahakikisha kuwa kila kitu kinafanyika ipaswavyo. Hata kama ilivyotokea kuwa mashirika binafsi ya "Wazungu na Wawekezaji wa nje ya nchi" yalibinafsishwa haina maana kuwepo kwa GAPEX, NBC au Lake soap kulitupa mwanya wa kushindwa kuwa makini na kudhibiti uendeshaji wa mashirika na viwanda hivyo.

Hata kipengele (i) kinavyoendelea kusema ni Wajibu wa Serikali kuingilia kati kwa vitendo vya maisha ya uchumi, it all falls on regulation, monitoring and even revenue collection and ensure transparency, openness and correct measurements when things go awry.

Kilichotokea Marekani in the last 3 years mpaka merikebu imegota mchangani ni kujivua kwa Serikali ya Marekani hivyo vipengele viwili hapo juu ambavyo vipo kwenye Azimio, na matokeo yake ni udhaifu wa Watu na uongozi ambao ulikaribia kulifilisi Taifa Tajiri kama Marekani!

Kwetu Tanzania, tulichofanya ni kukiuka kipengele hiki cha Azimio;
Kuona kwamba Serikali inaondoa kila namna ya dhuluma,

vitisho, ubaguzi, rushwa na upotofu;
kitu ambacho kilifanywa na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Chama na Serikali na Uongozi wa Juu wa nchi ukiongozwa na Mwasisi wa Taifa, kwa udhaifu ulifumbia macho makosa ya kiutendaji na ndio maana uwiano ukakosekana, usimamizi ukapotea, kila mtu akajifanyia analotaka na kadri mambo yalivyoendelea kudoda, tukaanza kutafuta mchawi wa kubebesha lawama huku tukisahau kuwa ni sisi wenyewe kama Wananchi na Viongozi wetu tulioruhusu kuzorota kwa kila kitu na wala si maandiko ya Azimio.

Kama jinsi vile kina Karl Peter na wenzake walivyotumia Biblia kutunyanyasa, kutunyonya na kututawala kwa kutufanya tuamini kuwa sisi ni watu duni na wa hali ya chini (inferior), ndivyo watendaji wa TANU na Serikali yake walivyoanza kuwaburuza Wananchi na kuachia kila kitu kifanyike kiholela na mpaka mchwa wakatafuna kila kitu.

Kama kungekuwa na umahiri wa kuwa thabiti na kakamavu katika safu ya Viongozi wetu na hata Wananchi, tusingefika hapa tulipo.

Azimil lilitamka wazi nia yetu ya kuachana na Unyonge, kuondoa Ujinga Umasikini na Maradhi na kutumia Juhudi na Maarifa na mfumo wa Kijamaa kufanikisha azma hiyo. Lakini udhaifu wa kibinadamu ndio uliofanya Wanasiasa waendelee kuwa ni wanyanyasaji, wasio wasikivu (Nyerere na U-Haambiliki wake pamoja na kuwa I will never cease to love the guy) na kwa udhaifu wa Wananchi, wakawa wafuasi walioa waoga na rahisi kurubuniwa.



Ndio maana leo kuna watu wanaoshangaa ninapoelekeza vidole vya kuwalaumu Mwinyi, Mkapa na Kikwete kwa kuendeleza udhaifu ule ule wa Nyerere katika uwajibikaji na kuwa na uongozi imara. Wao Mwinyi, Mkapa na Kikwete wamepewa nafasi ya kurekebisha kasoro za kiutendaji, lakini badala ya wao kuwka mguu chini na kisimika nguvu za kulizalisha Taifa upya lenye watuwaadilifu, wachapa kazi , wawajibikaji wenye juhudi na maarifa katika kusukuma gurudumu la maendeleo na hivyo kuhakikisha kuwa tunakuwa Wazalishaji, Wamilikaji na Wanufaika wa Maliasili yetu kwa kujiendesha wenyewe, wao wamekimbilia kukabidhi dhamana hiyo kwa kina Sinclair, IPTL, na hata leo tunaenda Uturuki na kwingineko tukiwaomba waje kutuonyesha jinsi ya kulima na kufanya kazi!

U wapi mwako ndani ya safu ya Uongozi wa kuwasisimua Watanzania warudi kwenye misingi ya awali iliyoafanya wakaandamana kwa nguvu kupigania Uhuru, kupiga vita unyonyaji na hata kulishabikia Azimio? Je ni wajibu wa kina Barrick na Shoperite? kwa nini tusimfuate Bakhresa na kumuuzia yeye NMC au kumpa wajibu wa kuwa NMC yetu kwa kuwa yeye ni Mzawa na anatamkwa kwenye Azimio kuwa apewe kipaumbele
Leo hii tuna nafasi nzuri sana ya kumilikisha Tanesco, TRL, ATC, NUwa, Dawaco na hata Bodi za Mazao kwa Serikali kuuza hisa zake kwa Wananchi na kujivua uendeshaji na kuwaachia Wananchi waendeshe mashirika haya.

Ikiwa Bakhresa, Mengi, Manji, Kimaro wa Precision na Wazawa wengine wana uwezo wa kuwa wazalishaji wenye umahiri na kuwa na mafanikio, kwa nini tukimbilie kutafuta Mchina, Mthailand, Mjerumani au Mkuwait waje kuendesha makampuni na uchumi wetu?

Au nao kina Bakhresa na Kimaro hatuwaamini kama vile tusivyotaka kuwaamini Wakikuyu, Watutsi na Waankole wanapotuomba ardhi kuja kulima tunawakatalia lakini tunakwenda China na Sweden na kuwaambia njooni ardhi tunayo bwelele?

Ukiangalia sana with open mind, it was not Azimio which failed us, bwana, but UONGOZI kitu ambacho kimeendelea hadi leo hii kuwa ndio udhaifu wetu!

Asante Rev, your post is not only inspiring but also convincing

Nimesoma na kunyonya issue kadha hapo juu na nina-zi highlight

1. Kuwa tuna matatizo ya uongozi, so Azimio liwepo au lisiwepo kama hakuna watu suitable wa kusema tufuate muongozo huu we will be playing

2. Asante umeleza kwa namna ya tofauti athari za ubinafsishaji, concept ya ubinafsishaji kwa ujumla ni nzuri tena sana, ila tu serikali lazima iwe na nguvu zake pale, mbaya zaidi unapo binafsisha mashirika kwa wazungu ni matusi mengine ya wazi kuwa watanzania hatuwezi kufanya wala kufikiri, na ni msimamo huu nina ukataa kuwa kuna mambo ndani ya AD yalionyesha kama vile tuna kilema fulani same concepts za kuudharau utu wetu ndizo zikatumika kuwafanya akina Mwinyi, Mkapa , JK n.k kuuza mashirika hata yale yenye faida

3. Nimeoona pia ni kama unasema ni matatizo yetu pia kuwa huko nyuma tulishindwa au kufail na kila mmoja anahusika katika kugawana hii blame; japo waasisi wa ubinafsishaji wanaona kama ndiyo ilikuwa jadi yetu kuua mashirika ,bado kama VIONGOZI wa nchi walipaswa kupigana kushindana na hali hii au matatizo yetu kama yalikuwepo

4. Pamoja na kuwa AD tunalichukulia kama mwongozo (kwa maelezo yako) lakini kumbe mwongozo huu unaweza ukafa hata leo hii endapo atapatikana kiongozi anaye SISIMUA kama unavyosema, nimeona maelezo kadhaa ya wazee wetu kwa nini wanalipenda au kulikumbuka azimio, lilikuwa kama kitu cha kuongeza ari, umoja, upendo, utu n.k na misisimuko ile ya JKN ndiyo ikawamaliza kabisa watu.

Leo hii kumbe akitokea kiongozi mwenye ushawishi ngau kama wa Nyerere au zaidi, basi tunaweza tukajenga azimio imara zaidi linaloendana na wakati huu na hali tuliyonayo! na halitakuwa tena AD!!! we can modify it; kwa sababu hatuna kiongozi wa aina hiyo na watu wamechoka na hali hii watu wanaona Azimio is the solution, LAKINI tukumbuke kuwa kama hakuna watu hao wenye ushawishi na kusisimua tusiliwazie! Here I concluded realier that laws are superior and can bulldoze watu wa tabia zote!



Rev. umekuwa muumini wa AD nina maswali ya unisaidie;

1. Angalia hali ya kisiasa, challenge zinazotuface local and globaly , je unafikiri how we can implement Azimio na kila mmoja akalifuata? kumbuka hili la zamani linaonekana lilikuwa ni hiyari, na nguvu za ushawishi na misisimuko ya hotuba za Nyerere uliweza hata ukadumu, msisimko huu ulipoondoka AD likafa, so lazima kuna mapungufu ni yapi hayo ?

2. Is it possible by anyway we can hybrid , Ujamaa, ubepari na AD au systems zingine? I mean is Ujamaa na ubepari the only systems za kutuweka duniani?

3. What is our problem?, najua ulishawahi kugusia hili ktk thread zilizopita, because I do believe AD kama ni ushawishi tu halitaenda popote pale, unless lipate nguvu ya kisheria ambalo litaendana na mabadiliko ya katiba, na implementers wa hii AD wawe wananchi na si serikali, they cann't hung themselves!

4. Piga picha ya Tz leo hii na maendeleo tuliyofikia na damage iliyofanyika ya kuwapa wageni mashirika, je HOW CAN WE REMEDY THE PROBLEM?



I need step by step method ya kuturudisha kwenye azimio au system njyingine unayoona inafaa, let say

-leo ipitishwe sheria serikali lazima iwe na share say 40% kila kampuni ya kigeni au mtu binafsi
-
-.......

My aim is to see practically how today we can go back to AD (assumptions are allowed)
 
Je Azimio la Uhuru la Marekani lilifanikiwa? Je lilipotangazwa Marekani ilikuwa na kila kitu kilichokuwepo au kilichohitajika kukamiliza njozi yake? Liliposema kuwa "we hold these truths to be self evident" ina maana watu wote walikwua sawa wakati ule? Je watu weusi wa Marekani walikane Azimio lao kwa sababu wakati linatolewa wao bado walikuwa ni watumwa?

Azimio la Arusha huwezi kulielewa isipokuwa kwa kuliangalia kama a declaration of certain Principles ambazo zinamfanya Mtanzania kuwa ni Mtanzania. Haijalishi kaanm mimi sikuwa na shamba au nilikuwa tofauti au wakati linatolewa sikuwa hai.

Kaka point uliyoitoa ni kubwa na muhimu sana, ila ina matatizo mengi sana

Umsema ni declaration of certain prinples, just declaration? nothing else? AD kama lingekuwa na nguvu ya kisheria au liko 'katibani' that is good to me,

Delaration za kutufanya waislamu na wakristo tunazisema kila siku na hatuzifuati! naweza nika declare kuwa mtanzania hili hali si mtanzania

Huwei kusem Chenge, Karamagi, RA, EL, na mafisadi wengine wengi ni watanzania wameisaliti nchi hii, na wengi watatokea , siamini kabisa kuwabana mafisadi tunaanza na declaration.

MKJJ najua unajua kuan watu leo hii wanatamani wangezaliwa ulaya, kuna watu wanatamani wassitwe watanzania , infact ndani ya Tz kuna watu hawajioni kama watanzania, declaration of these princples ni nzuri tena sana, ila,kama hakuna system ya kuwabana watu waishi sawa na walivyo declare ndiyo failure yenyewe! tuikosee na kulifanya AD lazima likubalike na wote, kuna watu ni madudu ni msonster hayana hata chembe ya huruma! hawa watu sheria tu ndiozo za kuwabana sio kwa declaration!

Kibaya zaidi hatutegemei wasio watanzania watusemee hizi declaration, CCM is failure waliyoyafanya nchii hii they dont qualify to be called Tanzanian! hivyo basi kila anayetaka AD we should find the other way not through CCM!!

Kuwa na uzalendo inatokea automatic, to love the land where I was born, siyo swala la kushawishiwa na mtu, kuwa nipende wazazi wangu waliponizaa, ni nitunze sehemu watakayoishi wajukuu zangu! nilinde mali asili ya vizazi vijavyo haihitaji AD!! if we are not able to live with these common senses mpaka AD liseme then bado hajuaanza kuishi basi, Kutochagua kiongozi mzuri ni ishara ya utokuwa wazalendo na hii ni watanzania asilimia 98% hatuko serious kuchagua viongozi! tuna matatizo jamani!

ndiyo maana nasema tuna matatizo mengi basi ya kuyatatua kabla ya kuingia kwenye Azimio! it seems AD was supposed to be declared when all Tanzanian are equal in their senses!

Hivi Chenge si alikuwepo kipindi cha hayo azimio, ina maana Mwinyi alikuwa na uwezo wa kuwavua mpaka utanzania!!!!
 
Back
Top Bottom