Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

". . . The Arusha Declaration and the actions relating to public ownership which we took last week were all concerned with ensuring that we can build Socialism in our country. The nationalization and the taking of a controlling interest in many firms were a necessary part of our determination to organize our society in such a way that our efforts benefit all our people and that there is no exploitation of one man by another.'

a) Sikubaliani na serikali kumiliki njia kuu za uchumi kwani zinamuacha mwananchi asiweze kutumia uwezo wake katika kuweza kuzimiliki njia hizo kuu za uchumi. Matokeo yake serikali ilianzisha National Poultry Co. Ltd na nyinginezo ili ifuge kuku na badala ya kuwaachia wananchi wafanye biashara hiyo kwa ushindani zaidi.

b) Ningehakikisha kuwa serikali inajitoa katika kufanya biashara moja kwa moja na kuwaacha shughuli hizo zifanywe na wananchi ili wao ndiyo wawe ni mhimili wa kweli wa uchumi wa nchi hii. Ninatambua kuwa kujituma kw mtu mmoja mmoja ndiyo ndiyo njia nzuri ya kuifanya jamii izalishe na kutumia resources zake kwa mgawanyo unaotokana juhudi za uzalishaji.

Ningehakikisha kuwa mashirika yote ambayo ni mzigo kwa walipa kodi na hayachangiii katikapato la taifa ninayauza mara moja. Na yale mashirika mengine ambayo yanajimudu basi ningehakikisha yanabinafsishwa na wananchi wenye kupenda wananunua hisa humo. Ningehakikisha yale mashirika ambayo ni nyeti kama Reli, Bandari, Posta, Ndege na mengine machache kama hayo yanabinafsishwa na serikali inabakiza hisa chache kwa ajili ya interest ya watanzania wote.
Pundamilia07,

Hata Wamarekani walishindwa kubinafsisha reli na posta.
 
Pundamilia)07
Hata Wamarekani walishindwa kubinafsisha reli na posta.

Hata wakubwa pia wanaweza kujifunza kutoka kwa wadogo. Kutokubinafsisha mashirika hayo si sababu ya kutoandaa mpango wa kuyabinafsisha hapa kwetu. Hata hivyo kama mashirika hayo huko marekani yanaachwa kwa sababu maalum na wanaweza kuyaruzuku bila ya kushindwa kuendesha shughuli za serikali basi ni sawasawa kabisa.
 
Hata wakubwa pia wanaweza kujifunza kutoka kwa wadogo. Kutokubinafsisha mashirika hayo si sababu ya kutoandaa mpango wa kuyabinafsisha hapa kwetu. Hata hivyo kama mashirika hayo huko marekani yanaachwa kwa sababu maalum na wanaweza kuyaruzuku bila ya kushindwa kuendesha shughuli za serikali basi ni sawasawa kabisa.
Kwa sasa posta inajiendesha yenyewe, ingawa nimesikia malalamiko kuwa watumaji barua wamepungua. Reli bado inapata ruzuku ya bunge. Waliwahi kuibinafsisha lakini wakati wa vita vikuu vya pili duniani wakaona umuhimu wa reli kubaki mikononi mwa serikali.Kwa bandari wanatoa tenda kwa kampuni binafsi kuziendesha (kama utakumbuka mgogoro wa hivi karibuni pale kampuni ya Ghuba iliposhinda tenda ikabidi waifute tenda hiyo baada ya malalamiko.)
 
Hata wakubwa pia wanaweza kujifunza kutoka kwa wadogo. Kutokubinafsisha mashirika hayo si sababu ya kutoandaa mpango wa kuyabinafsisha hapa kwetu. Hata hivyo kama mashirika hayo huko marekani yanaachwa kwa sababu maalum na wanaweza kuyaruzuku bila ya kushindwa kuendesha shughuli za serikali basi ni sawasawa kabisa.
Nafikiri Zebra una miss onus ya kufanya hivyo au hujapitia post zote jambo ambalo linaeleweka.

Kwa sisi watanzania hakuna aliye kuwa na uwezo wa kumiliki viwanda, au supermarket nk, Mwl akaona ilikumkomboa huyu mtanzania na uchumi wa kumuachia Mtu mweupe aliye kuwa na mtaji aendele kukutumikisha wewe aliona tujipe maarifa, mwamko na mtaji thithi wenyewe kwa serikali kutoa huo mtaji na kukupa wewe exposure ya kuweza kummanage hizo shughuli, na pia faida zingine zinazo kwenda na sisi kumiliki nguzo kuu za uchumi, tuliona Ma-flat ya Bora, RTC, Hosco , BOT nk yote hiyo katika jitihada za kupiga hatua kwa kasi zaidi , kwa sababu kuna msemo united we stand.....

Sasa ukielewa hiyo concept utaelewa kwanini ilifanyika hivyo.

Sasa swali tulifanikiwa au hatufanikiwa huo ni mjadala mwingine, lakini aangalizo Mwl alipotoka alisema kuna mahali tumekosea nk nk, lakini kikuu kilicho takiwa kufanyika kwa walio mfuatia ni kurekebisha hizo kasoro, na kuacha vitu vya msingi, nalo ni sii kwa asilimia kubwa kumiliki nguzo kuu za kiuchumi.
 
August,

Unaonesha wewe ni academician zaidi ya hali halisi.

Wakati Mwinyi anakabidhiwa nchi kulikuwa na mashirika ya umma nadhani kama sikosei karibia 400. (naweza kurekebishwa). na mengi ya mashirika hayo yalikuwa yanategemea ruzuku ya serikali au kuchotewa toka benki za serikali kwa ajili ya kujiendesha. Wakati huo huo serikali inahitaji fedha za kuendesha shughuli zake kwa maana ya kuwatumikia wananchi, ambapo sehemu ya pesa hizo tumekuwa tukipatiwa na wafadhili kabla hata ya Mwinyi kuingia madarakani. Je, unadhani kulikuwa na muda kuyafanya hayo unayoyasema wakati huohuo wale ambao wanakupa msaada wanakuelekeza kuacha kumwaga pesa kwenye mashirika ambayo hayana tija badala yake hizo pesa zichangie katika bajeti yako?

Kumbuka masharti ya IMF na WB yalilenga katika kuboresha uchumi na kuifanya serikali ijitoe katika uendeshaji biashara na kuwaachia watu binafsi ili wajitegemee na kuwa mhimili wa kujenga uchumi. Mawazo yako ni mazuri lakini wazo la serikali kuendelea kufanya biashara hilo ninalikataa kabisa. Ninaunga mkono urejeshwaji wa shughuli za biashara kutoka serikalini na kwenda kwa watu binafsi.
Naona kumbe umejaribu kupitia post nyingi iwezekanavyo, sasa tukija kwenye practical side maana umesema nipo more in academic than in the practical point.

Wewe ukipewa ushauri na mtu au masharti si utaomba muda wa kuyatafakari na kuona faida na hasara zake.

Na zaidi ya hapo wewe ukiwa ulikuwa na dira yako ambayo sasa mtu mwingine anataka ubadilishe mwelekeo utakuwa na shaka zaidi, hivyo kama Kiongozi utawauliza wenzako na baadae wataalamu iwe Ma-lecturer UD, na wafanyakazi wengine wa serikali, na utaangalia hiyo experience na nchi zingine ikiwezekana.

Kwa mfano tuliambia NBC ni kubwa saana ivunjwe vipande vipande, lakini utaona Barclays ina matawi karibu nusu ya dunia, sasa sijui ipi ni kubwa saana inayo hitaji kuvunjwa vunjwa.

Kwenye techinical aspect ya re-organisation ya nbc wakati ule labda wangeanza kuuza nyumba za wafanyakazi ili kuongeza mtaji wao na kuongeza financial discipline , kuweleza kwenye IT na kuondoa matatizo ya control hasa madeni yasiolipika, rushwa, kupoteza kwa documents nk, mashirika mengine hata wange kodisha management kutoka nje ingekuwa afadhali kuliko walivyo fanya, hata sasa hivi wewe mwenyewe na wanataaluma wengi wakiulizwa nini njia ya kufuata utasema ni ya mtanzania kumiliki nguvu za kiuchumi, jinsi gani, sasa hapo ndipo mimi na wewe tunatakiwa tutafakari.

Na pia kushindwa kwa mashirika yetu kuna sababu nyingi, moja ilikuwa kujaribu ku-subsidies vita vya ukombozi, ku-create nafasi za kazi, na siasa nayo ilichochea jambo hili ambapo watu waliojaria kwa vi-note walikuwa wengi, na utaalamu mdogo, na mikopo kutolewa bila kufuata vigezo, hivyo tatizo letu kubwa lilikuwa management, financial discipline , na siasda hivyo basi tungeaanza na hayo marekebisho, halafu tukajipima tunaenda sawa au ndio tumfuate IMF, au world bank.

Kuongezea tu unaona Sasa hivi Mkapa anajuta kuwafuata WB/IMF bila kupimia uzuri na ubaya wa hayo mambo, na hao hao waliotekeleza sera za IMF/WB bila kupimia leo hii wanona waliuzwa au walichuuzwa.

Maana leo hii kumtoa ABSA nbc ni shughuli, pili makampuni yao yote yanaweka fedha kwenye Bank zao, sasa hapo mshindi ni nani.

tatizo letu sisi ni viongozi kufanya vitu vyote kama vile wao ndio wanajua kila kitu, na matatizo ya mikataba mingi inaonekana toka siku "A" lakini watu hufumba macho, baada ya siku "c" hao hao walio amua wanaanza onja machungu ya uamuzi wao.
 
Nafikiri Zebra una miss onus ya kufanya hivyo au hujapitia post zote jambo ambalo linaeleweka.

Kwa sisi watanzania hakuna aliye kuwa na uwezo wa kumiliki viwanda, au supermarket nk, Mwl akaona ilikumkomboa huyu mtanzania na uchumi wa kumuachia Mtu mweupe aliye kuwa na mtaji aendele kukutumikisha wewe aliona tujipe maarifa, mwamko na mtaji thithi wenyewe kwa serikali kutoa huo mtaji na kukupa wewe exposure ya kuweza kummanage hizo shughuli, na pia faida zingine zinazo kwenda na sisi kumiliki nguzo kuu za uchumi, tuliona Ma-flat ya Bora, RTC, Hosco , BOT nk yote hiyo katika jitihada za kupiga hatua kwa kasi zaidi , kwa sababu kuna msemo united we stand.....

Sasa ukielewa hiyo concept utaelewa kwanini ilifanyika hivyo.

Sasa swali tulifanikiwa au hatufanikiwa huo ni mjadala mwingine, lakini aangalizo Mwl alipotoka alisema kuna mahali tumekosea nk nk, lakini kikuu kilicho takiwa kufanyika kwa walio mfuatia ni kurekebisha hizo kasoro, na kuacha vitu vya msingi, nalo ni sii kwa asilimia kubwa kumiliki nguzo kuu za kiuchumi.

Mimi sikubaliani na hiyo concept kwani ilikuwa ni mbaya sana, haikuwa endelevu hata kidogo. Kilichotakiwa kwa serikali ni kuwacha kumiliki njia kuu za uchumi na kuchukua sera ambazo zitaimarisha uwezo wa wananchi waweze kujiletea maendeleo ikiwamo kukuza uchumi kwa njia halisia na wala si za kufikirika.

Laiti kama serikali ingechukua njia sahihi za kuwapa na kuweka mazingira ya watanzania kujitegemea kwa kufanya biashara leo tungekuwa mbali sana. lakini kama utakumbuka maneno haya nadhani utanielewa vizuri sana nina maananisha nini.

Maneno kama KABAILA, MNYONYAJI, BEPARI yalitosha kuwaondoa watanzania katika kufikiri jinsi ya kujenga uchumi wao. Kuwa na utajiri au kuutafuta ilikuwa ni kama kutenda dhambi. Kuna baadhi ya watu (viongozi) ambao walitofautiana na Mwl na leo hii wamesimama vizuri sana. Na kuna wengine walimzunguka wakajilimbikizia utajiri ndani ya imani ya Azimio la Arusha.

Kana kwamba haitoshi leo hii waastafu wengi wa wakati wa mwalimu na hata wa siku za karibuni wakishastaafu na maisha yao huishia hapo. Sikushangaa majuzi-juzi niliposikia kuna Profesa mmja maarufu alitaka kuendelea kuajiriwa / kuwa tegemezi kwa serikali kwa vile hana mwamko wa kujituma mwenyewe kuzalisha.
 
Ngekewa tuko pamoja
Licha ya mashirika kuwa mengi na karibuni yote kundeshwa kwa kodi za wananchi na uchapishwaji wa noti mpya kila kukicha (refer Nyirabu-Nyerere relationship), serikali ilikuwa inafanya kazi ambayo haiihusu kabisa. Hebu angalia utitiri wa kazi au biashara ambazo serikali ilikuwa inahodhi:
Kampuni ya Kuku
Kampuni ya Maziwa
Kampuni ya Ng'ombe
Kampuni ya Usagishaji
Kampuni ya Usafirishaji ( UDA, KAMATA, KAU...RU, MA, etc.)
Kampuni ya Uvuvi
Kampumi ya Kilimo na Chakula
Kampuni ya Viatu
Kampuni ya Chai
Kampuni ya Chumvi
Kampuni ya Sukari (SUDECO)
Kampuni ya Magari
Na mengine mengi (orodha ni ndefu) ambayo serikali haikuwa na ulazima wa kuyaanzisha kuyahodhi huku yote yakiendeshwa kwa urasimu wa serikali. Watendaji wake wakuu wakilipwa mishahara na marupurupu yasiyolingana kamwe na uzalishaji wake. Namba ya ajira katika makampuni yote hayo haikujali uwezo halisi wa mahitaji ya biashara.
Tungeendelea kuchekesha na tusingekuwepo hapa tulipo kamamaamuzi sahihi ya kurekebisha uchumi yasingechukuliwa.
Azimio la Arusha halikuwa ni msahafu au biblia kana kwamba haliwezi kurekebishwa.
Azimio la Arusha msingi wake pia uliegemea katika mawazo ya mtu mmoja au kikundi kidogo cha watu.
Azimio la Arusha ndiyo lililoweka misingi mibovu ya uchumi wa nchi yetu kwa kuwanyang'anya uwezo wa kufikiri watanzania wazawa katika kuchemsha bongo zao na kuibuka kuwa wafanyibiashara wakubwa, badala yake walitakiwa wafanye kazi zaidi kwenye serikali au mashirika yake kwa ajili ya kujenga uchumi wa nchi yetu changa na huku ikwaachia uwanja mpana usiokuwa na upinzani watanzania wenye asili ya kiasia wakitawala fursa ya kufanya biashara kwani wao Azimio la Ausha halikuwagusa kabisa. Walipewa haki zote za kufanya biashara bila ya kuulizwa kama wana maduka mawili au zaidi, biashara zaidi ya moja, nk.

Turudi nyuma katika ukweli, kipndi ambacho Mwiny yuko madarakani ilikuwa ni kipindi ambacho mabadiliko mengi na makubwa ya kiuchumi na kisiasa yalikuwa yana fanyika duniani. Kwa mfano, mabadiliko ya mfumo wa siasa ya vyama vingi, kuanguka kwa Soviet, urekebishaji wa uchumi kwa nchi masikini nk. Wote tunakumbuka jinsi IMF na WB walivyokuwa wanatuasa tubadilishe sera zetu ili kuvutia mabadiliko ya kiuchumi. Ili kuyakubali yote hayo kama kiongozi wa nchi kunahitaji ujasiri na busara tele la sivyo ukigoopa kugeuka jiwe basi itabidi ung'atuke tu.
Hata hivyo ni lazima tuangalie ni kwani nini tunakuwa na Kiongozi wa nchi anayechaguliwa na wananchi kila baada ya muda fulani na kumwekea ukomo?
Hii ni wazi kuwa tunahitaji mawazo mbadala ndiyo maana kwa kila nchi yenye busara imeweza kuona mbali na kuhakikisha kuwa kuna kuwa na uongozi mpya kabisa kila baada ya miaka fulani. Kwa mantiki hiyo basi ni vema kila kiongozi aingiaye madarakani afanye jambo ambalo litaweza kusahihisha ukomo wa kufikiri wa kiongozi aliyepita. Kwa mfano kabla ya uongozi wa Mwinyi, kiongozi aliyekuwepo
aliamini kuwa wananchi kupiga mswaki wa mti na mkaa ilikuwa ni 'sawa tu', kuogea sabuni ya kufulia iliyo katika kiwango cha chini kabisa ni 'sawa tu',
kupangia wananchi kiwango cha manunuzi ya bidhaa muhimu kwa wiki au mwezi kama vile sukari nusu kilo kwa mwezi mzima kwa familia ni 'sawa tu'
kuogea sabuni ya Lux na kutumia Colgate ni kuhujumu uchumi.
kutopatia nafasi watoto wanaomaliza darasa la saba nafasi ya kuendelea na elimu ni 'sawa tu'
Sasa unapofikia mahali unapewa nchi ipo katika hali kama hiyo wewe kama kiongozi mpya wa nchi utaendelea kutumikia mawazo ya kiongozi aliyepita? ni wazi kuna limitations, ni vema kiongozi akaja na mikakati ya kubadilisha hali hiyo na hasa anapoona kuwa 'si sawa'.
Pamoja na mambo mengi, siasa zote za nchi yeyote zisifike mahali masuala muhimu ya ustawi wa wananchi yakataifishwa kwa kisingizio cha kulinda madili ya viongozi, ni vema wakati hao viongozi walipoweka namna ya kudhibitiana basi hayakupaswa kutuathiri sisi wananchi wa kawaida ambao si sehemu yao.

Ninadiriki kusema kuwa Azimio la Arusha ndiyo chanzo cha kuona wanazuoni wetu wazuri tu wanaacha kazi zao nzuri na kukimbilia siasa kwani tayari walishajengwa mawazoni mwao kuwa kwenye siasa ndiyo kila kitu. Kila mtu anafikiria ubunge na si kufanya biashara kwani kila mtendaji mkuu katika mashirika ya serikali alipewa nyumba bure, usafiri wa kumwaga yeye na mkewe na watoto na mjomba na shangazi. Hakukuwa na ufuatiliji wa mtendaji huyo, sana sana akiharibu basi atahamishwa kwenda kuharibu pengine


Ngekewa, Pundamilia, Makoko, August n.k

Nadhani tatizo linalotokea hapa na ambalo inabidi tulikwepe au tusema wazi ni kuwa;

1. Nyerere anayo aliyofanikiwa na anayo aliyofeli
2. Mwinyi anayo aliyofanikiwa na anayo aliyofeli

Never mention Mkapa na Kikwete.

Kosa ni pale kumlaumu mwinyi pasi kusema ukweli na aliyofanikisha, na kosa pia kumlaumu Nyerere pasi kusema uzuri wake.

Sehemu walizofeli hawa wakuu hatusemi wao , tunasema tulishindwa hapa, hiyo inakuwa lugha ya kifamilia zaidi kama taifa ni moja.

Tumethibitishiwa na kuhakikishiwa mara nyingi kuwa AD lilikuwa ni wazo, wazo lile lilikuwa zuri, ulikuwa mwongozo, chombo cha kuleta ari, umoja na hamasa!

Tamko lile au wazo lile hata kama lilishindwa halimfanyi ,mtoa wazo kuwa mshindwa, wala halimlazimishi mpokea wazo kulazimishwa kulikubali wazo.

Ila wazo hili kama tunaona linapositive ideas why bother? kwa nini tusiseme Ok, it was good Idea let amend and move on with it!

Tukiendela na mchezo wa kumsema Mwinyi vibaya na Nyerere vibaya hatutakaa tujue , tuna matatizo gani, tulianguka wapi, na tuamke vipi!

Ukikosea ukasema mazuri ya Mwinyi basi unaweza ukashangaa watanzania asilimia 90 wanasema afadhali mwinyi kuliko Nyerere aliyefanya tusugue meno kwa mkaa! But even Nyerere that was a process, tena naweza kusema tungekaa zaidi pale tujifunze zaidi shida zilivyo, pengine viongozi leo wangekuwa na utu! we can never by any means kumlaumu mto wazo na mwenye nia nzuri na taifa! kushindwa ni alama tosha ya kutokuwa na watu wa kusaidia,

Mbio za kijiti hizi ,ni teamwork, kulaumiwa Mwinyi wakati JKN alikuwa yupo pembeni ni sawa na kusema JKN alitusaliti baadae! mbaya zaidi watu walilipiga chini waliokuwa wanafunzi wa JKN, Mkapa leo hatuwezi tukampachika jina ulikuwa mbaya kwa kukataa Azimio wakati kafundishwa kabisa na JKN! what went wrong? tukasema pia tusikosee na kufana azimio kama dini!

AD ni wazo, haukuwa mfumo, tatizo ni kuwa ngau JKN tulijua anaamini nini, akina marais wengine wote hawana wanachoamini, kama ni dini basi siasa ya nchi ytu ni ya kipagani.

However, still we can move on, kama Sheria na Katiba zitafuatwa vyema, still tumeona Katiba na sheria vinahitaji mabadiliko mengi tu.

AD kama anatokea leo mtu analifufua basi lipate nguvu ya kisheria, bila hivyo tutakuwa tunacheza

Enyi wana wa nchi hii, stop pointing fingers to JKN and Mwinyi, simameni kwa miguu yenu na kuamka leo!
 
Naona kumbe umejaribu kupitia post nyingi iwezekanavyo, sasa tukija kwenye practical side maana umesema nipo more in academic than in the practical point.

Wewe ukipewa ushauri na mtu au masharti si utaomba muda wa kuyatafakari na kuona faida na hasara zake.

Na zaidi ya hapo wewe ukiwa ulikuwa na dira yako ambayo sasa mtu mwingine anataka ubadilishe mwelekeo utakuwa na shaka zaidi, hivyo kama Kiongozi utawauliza wenzako na baadae wataalamu iwe Ma-lecturer UD, na wafanyakazi wengine wa serikali, na utaangalia hiyo experience na nchi zingine ikiwezekana.

Kwa mfano tuliambia NBC ni kubwa saana ivunjwe vipande vipande, lakini utaona Barclays ina matawi karibu nusu ya dunia, sasa sijui ipi ni kubwa saana inayo hitaji kuvunjwa vunjwa.

Kwenye techinical aspect ya re-organisation ya nbc wakati ule labda wangeanza kuuza nyumba za wafanyakazi ili kuongeza mtaji wao na kuongeza financial discipline , kuweleza kwenye IT na kuondoa matatizo ya control hasa madeni yasiolipika, rushwa, kupoteza kwa documents nk, mashirika mengine hata wange kodisha management kutoka nje ingekuwa afadhali kuliko walivyo fanya, hata sasa hivi wewe mwenyewe na wanataaluma wengi wakiulizwa nini njia ya kufuata utasema ni ya mtanzania kumiliki nguvu za kiuchumi, jinsi gani, sasa hapo ndipo mimi na wewe tunatakiwa tutafakari.

Na pia kushindwa kwa mashirika yetu kuna sababu nyingi, moja ilikuwa kujaribu ku-subsidies vita vya ukombozi, ku-create nafasi za kazi, na siasa nayo ilichochea jambo hili ambapo watu waliojaria kwa vi-note walikuwa wengi, na utaalamu mdogo, na mikopo kutolewa bila kufuata vigezo, hivyo tatizo letu kubwa lilikuwa management, financial discipline , na siasda hivyo basi tungeaanza na hayo marekebisho, halafu tukajipima tunaenda sawa au ndio tumfuate IMF, au world bank.

Kuongezea tu unaona Sasa hivi Mkapa anajuta kuwafuata WB/IMF bila kupimia uzuri na ubaya wa hayo mambo, na hao hao waliotekeleza sera za IMF/WB bila kupimia leo hii wanona waliuzwa au walichuuzwa.

Maana leo hii kumtoa ABSA nbc ni shughuli, pili makampuni yao yote yanaweka fedha kwenye Bank zao, sasa hapo mshindi ni nani.

tatizo letu sisi ni viongozi kufanya vitu vyote kama vile wao ndio wanajua kila kitu, na matatizo ya mikataba mingi inaonekana toka siku "A" lakini watu hufumba macho, baada ya siku "c" hao hao walio amua wanaanza onja machungu ya uamuzi wao.

August,

Sisemi kwa mba what you are saying si sawasawa bali situation unayokuwa nayo huchangia pia katika maamuzi ya nini kifanyike. Mawazo yako unaweza kuyatekeleza endapo haya mawili yafutayo yapo ndani ya uwezo wako

1. Kama unafedha ya kuendesha bajeti ya serikali yako
2. Una muda wa kusubiri na kufanya hayo yote bila ya kuathiri majukumu ya kila siku ya serikali.

Endapo kama unaweza kuwa na hayo mawili maana yake sehemu ya mishahara ya mwezi huo unaosubiria hautategemea wafadhili. Na vilevile unawezo mkubwa wa kuendelea kumwaga pesa za walipa kodi biala ya tatizo.

Juu ya ukubwa wa NBC nadhani ukweli wa jambo hili haujaongelewa kwa kina zaidi ya mapokeo ya kisiasa hasa ukizingatia kauli ya kufanisha NBC na mabenki kama Barclays ilitolewa na respected man. Hata hivyo hebu tuiangalie NBC na Barclays, Barclays ina matawi mangapi hapa Tanzania? Je, NBC ilikuwa na matawi mangapi Duniani kote?

Tafakari!!!!!!!!!
 
". . . The Arusha Declaration and the actions relating to public ownership which we took last week were all concerned with ensuring that we can build Socialism in our country. The nationalization and the taking of a controlling interest in many firms were a necessary part of our determination to organize our society in such a way that our efforts benefit all our people and that there is no exploitation of one man by another.'

a) Sikubaliani na serikali kumiliki njia kuu za uchumi kwani zinamuacha mwananchi asiweze kutumia uwezo wake katika kuweza kuzimiliki njia hizo kuu za uchumi. Matokeo yake serikali ilianzisha National Poultry Co. Ltd na nyinginezo ili ifuge kuku na badala ya kuwaachia wananchi wafanye biashara hiyo kwa ushindani zaidi.

b) Ningehakikisha kuwa serikali inajitoa katika kufanya biashara moja kwa moja na kuwaacha shughuli hizo zifanywe na wananchi ili wao ndiyo wawe ni mhimili wa kweli wa uchumi wa nchi hii. Ninatambua kuwa kujituma kw mtu mmoja mmoja ndiyo ndiyo njia nzuri ya kuifanya jamii izalishe na kutumia resources zake kwa mgawanyo unaotokana juhudi za uzalishaji.

Ningehakikisha kuwa mashirika yote ambayo ni mzigo kwa walipa kodi na hayachangiii katikapato la taifa ninayauza mara moja. Na yale mashirika mengine ambayo yanajimudu basi ningehakikisha yanabinafsishwa na wananchi wenye kupenda wananunua hisa humo. Ningehakikisha yale mashirika ambayo ni nyeti kama Reli, Bandari, Posta, Ndege na mengine machache kama hayo yanabinafsishwa na serikali inabakiza hisa chache kwa ajili ya interest ya watanzania wote.

- Sawa sawa tupo wote hapo.


FMEs!
 
Sasa Wareboya na Pundamilia ( Mnyama Mpole, mtaratibu hope mwenye Busara pia).

Kuna Pepsi walikuwa wafanya biashara na hakuna share holding ya serikali, na ushindani ulikuwa kama hakuna, kuna Coca Cola, kuna Toyota Tanzania LTD, KJ motors, JV Group of Companies, Somaia Group, na mengineyo mengi tu, je kwanini hawapo mpaka leo au katika ili nguvu waliokuwa nayo mwanzo, na licha ya kupewa exmption za kila aina na wizi juu?

Tukaona new kids on the block kama marehemu Gulamali, Dewji Kassim na nduguze yule wa Pan African na yule wa Simba SC sio huyu Mo' Dewji mbunge wa Singida, Afro Cooling System imeishia wapi, haya makampuni ya kutengeneza mafuta ya kula ndio hayo tena, yanaenda kinyume nyume badala ya quality na prduction kuongezeka, kulikuwa na VOIL, na yale mafuta ya pamba wapo wapi nk nk.

Maana kipindi kile cha IMF/WB tulitekeleza kila kitu walicho kitaka je mafanikio yapoje? Mimi nilitegemea shs yetu sasa ingekuwa atleast 1 to centi hamsini za kenya lakini utaona ndio tumezidi kuchwa mbali, wakati Kenya ardhi iliyo na rutuba ni 1/3 sisi ni 3/4, mahindi S'wanga na kwingine yanalimwa na watu binafsi, Shinyanga mchele kibao, lakini leo hii sehemu maskini ni hizo mbili au yenye miundo mbini mibovu, uje Singida na alizetti yao, hivyo hivyo, tabora na tumbaku yao mambo ni hayo hayo.
 
a) Sikubaliani na serikali kumiliki njia kuu za uchumi kwani zinamuacha mwananchi asiweze kutumia uwezo wake katika kuweza kuzimiliki njia hizo kuu za uchumi.
Hapa tutazungumzia magnitude ya kufanya hivyo; leo hii nchi za Kibepari zinaingilia kati umiliki wa uchumi na zimekuwa zikifanya hivyo kwa muda mrefu. Tusingeweza kuacha njia za uchumi zote ziwe mikononi mwa kikundi cha watu watu wachache. Tusingeweza kusubiri kama kina Obama miaka 40 baadaye kuona kuwa wananchi ni lazima wawe na interest katika kuendesha uchumi wao.

Matokeo yake serikali ilianzisha National Poultry Co. Ltd na nyinginezo ili ifuge kuku na badala ya kuwaachia wananchi wafanye biashara hiyo kwa ushindani zaidi.
Kwenye hili la kuku inaonekana hujui lengo la shirika hilo lilikuwa ni nini. Sisi tulikuwa wafugani wa kuku wa mayai na wa nyama. Shirika la Kuku lilikuwa linafanya urahisi wa sisi wengine kwenda kununua vifaranga kutka katika matawi yake mbalimbali. Ulikuwa unaweka oda halafu unaenda kuchukua au wanakutumia maboxi yenye matobo matobo ya vifaranga. Ilikuwa inahakikisha chakula cha kuku kipo na chenye mchango wa lishe inayotakiwa.

Sisi wananchi tuliokuwa tunafanya shughuli hiyo hatukulazimika kwenda Zambia kutafuta vifaranga.

b) Ningehakikisha kuwa serikali inajitoa katika kufanya biashara moja kwa moja na kuwaacha shughuli hizo zifanywe na wananchi ili wao ndiyo wawe ni mhimili wa kweli wa uchumi wa nchi hii.
Serikali karibu zote duniani zinafanya aina fulani ya biashara. La maana ni kuchagua ni biashara gani na kwa kiasi gani. Fannie Mae na Fred Mac ni makampuni ya biashara ya serikali, leo hii GM na Chrysler ni makampuni binafsi lakini serikali ya Marekani ina hisa? why is that? Kwa sababu kuna mambo fulani kwenye uchumi uwezi kuachia tamaa za watu za fedha kuyafanya, matokeo yake ndiyo haya tunayoyaona.

Amtrak ni shirika la reli la nchi ya kibepari zaidi; angalia hata matreni ya DC na NY


Ninatambua kuwa kujituma kw mtu mmoja mmoja ndiyo ndiyo njia nzuri ya kuifanya jamii izalishe na kutumia resources zake kwa mgawanyo unaotokana juhudi za uzalishaji.
Nipe mfano wa nchi yoyote duniani yenye mfumo ambao hauusishi serikali kwa namna fulani hata kwa umiliki?

Ningehakikisha kuwa mashirika yote ambayo ni mzigo kwa walipa kodi na hayachangiii katikapato la taifa ninayauza mara moja.
Hilo ni suluhisho potofu, suluhisho bora ni kuangalia jinsi gani unaweza kuyasaidia kuyafanya ya faida. Kuyauza tu hakutayafanya kuwa na faida. Kuuza mashirika hakutasababisha yawe na faida. Mtu mwenye hekima na utaalamu ni yule anayejiuliza jinsi ya kuyafanya mashirika hayo yawe bora na yenye faida.

Na yale mashirika mengine ambayo yanajimudu basi ningehakikisha yanabinafsishwa na wananchi wenye kupenda wananunua hisa humo. Ningehakikisha yale mashirika ambayo ni nyeti kama Reli, Bandari, Posta, Ndege na mengine machache kama hayo yanabinafsishwa na serikali inabakiza hisa chache kwa ajili ya interest ya watanzania wote.
Hoja yako ya mwisho ina negate kabisa hoja nyingine. Kama serikali haifai kufanya biashara kwanini tena iwe na hisa badala ya kuacha sekta binafsi ifanye mambo yote? Unless unaamini upande mwingine kuwa serikali inaweza kushiriki katika biashara ya aina fulani.
 
Kuna Pepsi walikuwa wafanya biashara na hakuna share holding ya serikali, na ushindani ulikuwa kama hakuna, kuna Coca Cola, kuna Toyota Tanzania LTD, KJ motors, JV Group of Companies, Somaia Group, na mengineyo mengi tu, je kwanini hawapo mpaka leo au katika ili nguvu waliokuwa nayo mwanzo, na licha ya kupewa exmption za kila aina na wizi juu?

Tukaona new kids on the block kama marehemu Gulamali, Dewji Kassim na nduguze yule wa Pan African na yule wa Simba SC sio huyu Mo' Dewji mbunge wa Singida, Afro Cooling System imeishia wapi, haya makampuni ya kutengeneza mafuta ya kula ndio hayo tena, yanaenda kinyume nyume badala ya quality na prduction kuongezeka, kulikuwa na VOIL, na yale mafuta ya pamba wapo wapi nk nk.

Maana kipindi kile cha IMF/WB tulitekeleza kila kitu walicho kitaka je mafanikio yapoje? Mimi nilitegemea shs yetu sasa ingekuwa atleast 1 to centi hamsini za kenya lakini utaona ndio tumezidi kuchwa mbali, wakati Kenya ardhi iliyo na rutuba ni 1/3 sisi ni 3/4, mahindi S'wanga na kwingine yanalimwa na watu binafsi, Shinyanga mchele kibao, lakini leo hii sehemu maskini ni hizo mbili au yenye miundo mbini mibovu, uje Singida na alizetti yao, hivyo hivyo, tabora na tumbaku yao mambo ni hayo hayo.

August umejibu swali moja zuri. Wapo watu wanaotaka tuamini kabisa kuwa wakati wa Mwalimu (waakati wa Azimio la Arusha) hakukuwa na makampuni binafsi yaliyokuwa yakipata faida.
 
Sasa Wareboya na Pundamilia ( Mnyama Mpole, mtaratibu hope mwenye Busara pia).

Kuna Pepsi walikuwa wafanya biashara na hakuna share holding ya serikali, na ushindani ulikuwa kama hakuna, kuna Coca Cola, kuna Toyota Tanzania LTD, KJ motors, JV Group of Companies, Somaia Group, na mengineyo mengi tu, je kwanini hawapo mpaka leo au katika ili nguvu waliokuwa nayo mwanzo, na licha ya kupewa exmption za kila aina na wizi juu?

Tukaona new kids on the block kama marehemu Gulamali, Dewji Kassim na nduguze yule wa Pan African na yule wa Simba SC sio huyu Mo' Dewji mbunge wa Singida, Afro Cooling System imeishia wapi, haya makampuni ya kutengeneza mafuta ya kula ndio hayo tena, yanaenda kinyume nyume badala ya quality na prduction kuongezeka, kulikuwa na VOIL, na yale mafuta ya pamba wapo wapi nk nk.

Maana kipindi kile cha IMF/WB tulitekeleza kila kitu walicho kitaka je mafanikio yapoje? Mimi nilitegemea shs yetu sasa ingekuwa atleast 1 to centi hamsini za kenya lakini utaona ndio tumezidi kuchwa mbali, wakati Kenya ardhi iliyo na rutuba ni 1/3 sisi ni 3/4, mahindi S'wanga na kwingine yanalimwa na watu binafsi, Shinyanga mchele kibao, lakini leo hii sehemu maskini ni hizo mbili au yenye miundo mbini mibovu, uje Singida na alizetti yao, hivyo hivyo, tabora na tumbaku yao mambo ni hayo hayo.
Post hii sijaielewa mkuu, unasema nini kuhusu hayo makampuni. Na unahusianisha na nini? Na AD, Mwinyi n.k sijakupata kabisa, hayo makampuni ni ya miaka gani? Baada ya Mwinyi au kabla? Na kwa nini ni makapuni ya watu binafsi? Yaani umeniacha lengo la post yako sijalielewa samahani kwa usumbufu
 
Hapa tutazungumzia magnitude ya kufanya hivyo; leo hii nchi za Kibepari zinaingilia kati umiliki wa uchumi na zimekuwa zikifanya hivyo kwa muda mrefu. Tusingeweza kuacha njia za uchumi zote ziwe mikononi mwa kikundi cha watu watu wachache. Tusingeweza kusubiri kama kina Obama miaka 40 baadaye kuona kuwa wananchi ni lazima wawe na interest katika kuendesha uchumi wao.


Kwenye hili la kuku inaonekana hujui lengo la shirika hilo lilikuwa ni nini. Sisi tulikuwa wafugani wa kuku wa mayai na wa nyama. Shirika la Kuku lilikuwa linafanya urahisi wa sisi wengine kwenda kununua vifaranga kutka katika matawi yake mbalimbali. Ulikuwa unaweka oda halafu unaenda kuchukua au wanakutumia maboxi yenye matobo matobo ya vifaranga. Ilikuwa inahakikisha chakula cha kuku kipo na chenye mchango wa lishe inayotakiwa.

Sisi wananchi tuliokuwa tunafanya shughuli hiyo hatukulazimika kwenda Zambia kutafuta vifaranga.

Serikali karibu zote duniani zinafanya aina fulani ya biashara. La maana ni kuchagua ni biashara gani na kwa kiasi gani. Fannie Mae na Fred Mac ni makampuni ya biashara ya serikali, leo hii GM na Chrysler ni makampuni binafsi lakini serikali ya Marekani ina hisa? why is that? Kwa sababu kuna mambo fulani kwenye uchumi uwezi kuachia tamaa za watu za fedha kuyafanya, matokeo yake ndiyo haya tunayoyaona.

Amtrak ni shirika la reli la nchi ya kibepari zaidi; angalia hata matreni ya DC na NY


Nipe mfano wa nchi yoyote duniani yenye mfumo ambao hauusishi serikali kwa namna fulani hata kwa umiliki?


Hilo ni suluhisho potofu, suluhisho bora ni kuangalia jinsi gani unaweza kuyasaidia kuyafanya ya faida. Kuyauza tu hakutayafanya kuwa na faida. Kuuza mashirika hakutasababisha yawe na faida. Mtu mwenye hekima na utaalamu ni yule anayejiuliza jinsi ya kuyafanya mashirika hayo yawe bora na yenye faida.

Hoja yako ya mwisho ina negate kabisa hoja nyingine. Kama serikali haifai kufanya biashara kwanini tena iwe na hisa badala ya kuacha sekta binafsi ifanye mambo yote? Unless unaamini upande mwingine kuwa serikali inaweza kushiriki katika biashara ya aina fulani.

Mkuu sijakupata, lengo la post yako unataka serikali imiliki makampuni tena? au kuwa ubinafsishwaji ulikosewa? au ubinafsishaji usingefanyika kabisa?
 
Watanzania mara nyingine sijui tukoje, tuko tuko tuu, ndio mana siku hizi najitamkia Tanzania Jamhuri ya vyura.

Kuna watu leo wanaodai hawaoni mafanikio yeyote ya Azimio la Arusha.

Je Utaifa wako unaojivunia, ulishamiri na kuneemeka wapi? Siku tulipopata Uhuru au siku tulipong'amua kwa sisi kama watu huru tuna uwezo wa kujitawala na kujizalishia bila kumtegemea mtu?

Kwa Azimio liligusia Uchumi tuu? Je utu wetu, Utaifa wetu, uzalendo na hata Imani ya kuishi Kijama na hasa Ujamaa wa kiafrika tulivitoa wapi?

Hata watu wanapolalamika kuhusu watu kuliwa na Simba wakati wa Sera ya vijiji vya Ujamaa mwaka 1976, je kuna hata mmoja ambaye amediriki kujiuliza Tanzania tulipata wapi fedha za kuweza kujenga makao ya wilaya 120 katika Miaka 25 ya kwanza ya Uhuru? Makao haya ambayo yana Hospitali, Polisi, Benki (NBC enzi zile) vyama vya Ushirika, Ofisi za Serikali na Idara zote anzia Kazi, Kilimo, Ufugaji, Maji, Misitu, Maliasili, Biashara na kadhalia? Je Makao makuu ya Mikoa ambako nako kuna ofisi na vitengo vya kiutawala kama nilivyovitaja hapo vya wilaya?

Je barabara za kuunganisha mikoa yote iwe za vumbi, kokoto au lami ni zote alitujengea Mkoloni? Je Mashule katika kata ,wilaya na mikoa?

Je ajira zilizotolewa katika wilaya, mikoa na Taifa na hata zile nyingine ambazo si serikali tuu bali mashirika?

Je lile tabaka la kati lililoshamiri Tanzania kutokana na kuwepo kwa Corporate Welfare hatuoni kuwa tulifanya kafara ya mambo fulani na kusaidia mengine? hivi wale wote walioajiriwa kwenye mashirikwa wakalipiwa gharama za afya bila wao kulipia hata senti, wakalipiwa usafiri, wengine wakapewa na nyumba na huduma nyingine zote za muhimu, Polisi na Jeshi kupewa upendeleo maalumu na bei robo ya anazo nunua mtu wa Kawaida, ili kutoa unafuu kutokana na mishahara na kipato chetu kuwa kidogo, bado mtu anadiriki kusema Azimio halikusaidia chochote?

Leo hii tulipokaa na kuishi kama jamii moja bila hata kubainikuwa tuna matabaka ya walionazo na wasionazo, je umoja huo, ambao leo hii tunaudhulumu haki yake na wengine kunufaika kuimba Amani ,Utulivu na Mshikamano ulitokana na nini?

Ntaomba asemaye Azimio halikuwa si chochite, aende Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Zambia, Malawi , Congo-Zaire na Msumbiji ongezea na Komoro aangalie kwa upembuzi yakinifu maisha ya wenzetu na kuyalinganisha na sisi.

Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Msumbiji, Comoro na Congo-Zaire hawaishi kutiana ngeu za mfarakano wa Kikabila!

Hata hiyo Kenya tunayojivunia kuwa eti ina uchumi mzuri, jiulizeni uchumi kaushika nani na wanufaika ni wangapi?

Kama nilivyosema awali, Azimio la Arusha kilicholeta upungufu si Tamko, bali ni utekelezaji mbovu uliotokana na uongozi mbovu.

Na ndio maana hata leo hii na mfumo wa soko huria bado utekelezaji wake ni mbovu kutokana na uongozi mbovu.

Hivyo tatizo si Azimio, Wazo au Kauli, tatizo la Tanzania ni mfumo mbovu wa utendaji unaoongozwa na kusimamiwa na uongozi mbovu na dhaifu ambao hauna mwamko na nguvu za kutumia mamlaka na sheria kumnufaisha na kumletea neema Mtanzania.

Mkandara hujisemeaga WATU na Mazingira na wengi wenu humuona kama kichaa, basi niongezeni nami katika kundi la vichaa na nitawaambia tatizo ni Watu, Mazingira na Uongozi mbovu na si Sera!
 
". . . The Arusha Declaration and the actions relating to public ownership which we took last week were all concerned with ensuring that we can build Socialism in our country. The nationalization and the taking of a controlling interest in many firms were a necessary part of our determination to organize our society in such a way that our efforts benefit all our people and that there is no exploitation of one man by another.'

a) Sikubaliani na serikali kumiliki njia kuu za uchumi kwani zinamuacha mwananchi asiweze kutumia uwezo wake katika kuweza kuzimiliki njia hizo kuu za uchumi. Matokeo yake serikali ilianzisha National Poultry Co. Ltd na nyinginezo ili ifuge kuku na badala ya kuwaachia wananchi wafanye biashara hiyo kwa ushindani zaidi.

b) Ningehakikisha kuwa serikali inajitoa katika kufanya biashara moja kwa moja na kuwaacha shughuli hizo zifanywe na wananchi ili wao ndiyo wawe ni mhimili wa kweli wa uchumi wa nchi hii. Ninatambua kuwa kujituma kw mtu mmoja mmoja ndiyo ndiyo njia nzuri ya kuifanya jamii izalishe na kutumia resources zake kwa mgawanyo unaotokana juhudi za uzalishaji.

Ningehakikisha kuwa mashirika yote ambayo ni mzigo kwa walipa kodi na hayachangiii katikapato la taifa ninayauza mara moja. Na yale mashirika mengine ambayo yanajimudu basi ningehakikisha yanabinafsishwa na wananchi wenye kupenda wananunua hisa humo. Ningehakikisha yale mashirika ambayo ni nyeti kama Reli, Bandari, Posta, Ndege na mengine machache kama hayo yanabinafsishwa na serikali inabakiza hisa chache kwa ajili ya interest ya watanzania wote.

This is where you are wrong.

Serikali bado inamiliki njia kuu za uchumi isipokuwa kwa sasa mfumo umebadilishwa kidogo ili kuruhusu ubinafsi ushamiri kama unavyotaka, na matokeo yake tunayaona. Serikali bado inamiliki majengo, inakusanya kodi, vitendea kazi, wafanyakazi, hizi zote ni njia za kiuchumi. Ilichofanya sasa kujiondoelea wajibu wake wa kugavi huduma mbalimbali na kumuacha the common mwananchi apambane moja kwa moja na ruthless capitalist system.

Mambo kama ya mfumuko wa bei na kutengenezwa kwa social strata yanajitokeza. Na mambo mengine lukuki kama kuvuniika kwa uzalendo, uhalifu na ufisadi kwa sababu pesa imetangulia utu, kuvurugika kwa social pillars kutokana na wengi kuachwa wakina na vipato duni.

Umiliki au udhibiti wa njia kuu za uchumi wa enzi zile, ilikuwa na lengo la kuifaidisha jamii nzima badala ya mtu mmojammoja ambapo ni source ya matatizo mengi sana, ambayo ni shurti yatokee kutokana na ku-adopt mfumo wa kibepari..ambao in actual sense is self-defeating.
 
Mkuu sijakupata, lengo la post yako unataka serikali imiliki makampuni tena?

Ndiyo, kuna mambo ambayo katika Tanzania yetu yangeendelea kuwa mikononi mwa wananchi (siyo serikali per se). Kosa mojawapo la Azimio la Arusha ni kuweka makampuni mikononi mwa serikali moja kwa moja (100 percent) badala ya kutafuta mfumo wa jinsi gani Watanzania wangeweza kumiliki makampuni hayo. Hii ndiyo modeli yangu mpya ya uendeshaji wa TRL.

au kuwa ubinafsishwaji ulikosewa?

Ndiyo ulikosewa sana; huwezi kubinafsisha tu ilimradi umelitoa shirika mikononi mwa umiliki wa umma. Ubinafsishaji ulifanyika kwa minajili ya kuua mashirika yetu ya umma ili mashirika ya binafsi yafanikiwe; hawakutumia akili wala kusudi la kutaka kuyaendesha kwa faida. Ulifanywa kwa misingi ya kuwa "tumeshindwa" labda wageni "wataweza".

au ubinafsishaji usingefanyika kabisa?

Ungesoma msingi wa ubinafsishaji ulikuwa ni nini; sera ya CCM wakati ule ilisemwa wazi kuwa ni kubinafsisha "mashirika yenye hasara".. siyo kubinafsisha mashirika ya umma yenye faida. Badala kukaa chini na kutumia ubongo na kuona ni jinsi gani tunaweza kuboresha mashirika hayo mengine tukaamua kuyaachia tu!

Hivi unafikiri ni kwanini Serikali ya Obama imeweka hisa kwenye Chrysler, GM na kusaidia makampuni kadhaa ya kifedha kupitia TARP wakati makampuni hayo yalikuwa ni ya binafsi? Kwanini kwa mfano hata pamoja na kufanya hasara Marekani haijauza Posta yake, haijauza Amtrak, haijauza Freddie Mac na inayo hata OPIC? Unajua kwanini serikali inaendesha PBS, Export Import Bank of the United States, North Dakota Mill and Elevator? Nchi hii ndiyo ya kibepari yenyewe!! Hadi kampuni ya Bima ya FDIC ni ya serikali.. why why why? Wakifanya Wamarekani tunaelewa lakini Nyerere kutaka kuanzisha kampuni ya Taifa ya Bima tumeona kosa!

pointi yangu ni kuwa karibu nchi zote duniani (sijapata nchi ambayo haifanyi hivyo) serikali inaendesha makampuni mbalimbali kwa kanuni za biashara za kibinafsi. Yaani, makampuni ya serikali yanaendeshwa na kushindanishwa na makampuni mengine na yale yanayopata ruzuku (kama Amtrak) yanasimamiwa kwa namna ambayo inaongeza ubora na kuhakikisha kuna japo faida ya aina fulani na yanapewa uhuru mkubwa wa kujiendesha kibiashara.

Kuna ubaya gani wa kufanya makampuni yanayomilikiwa na serikali yetu kuendeshwa kibiashara siyo kama charities?
 
mtazamo wangu tu,

huyu mzee JKN alikuwa na mawazo ambayo wengi wetu mpaka leo tunashindwa kumwelewa alikuwa na theory ambazo ni misingi hasa ya utu, nadhani kama Nyerere angekuwa dictator basi hii nchi kwa sasa ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na filosofia zake,

Wakina Mwinyi walilianzisha hilo Azimio lao bila kuwa na upeo na tafakuli za maana, sasa wamefikia point kwa kuanza kutafunwa na Dhambi ileile ya kulikataa Azimio La Arusha na Nchi pamoja na Chama kimeshawashinda na kila mmoja anataka kunawa mikono kwamba yeye sio aliyetuleta hapa tulipo

hebu tujaribu kuangalia baadhi ya filosofia za Mwalimu

1. 'WATU WOTE NI SAWA'
"...Kama hukubali hilo, yaani kama unadhani watu wengine ni miungu wengine, malaika, wengine nusu-nyani, basi hukubali ujamaa. Ujamaa kwako hauna maana, kwa sababu ujamaa unahusu usawa wa watu: hapo ndipo unapoanza...Sisemi usawa wa urefu wala ufupi; kwa urefu namzidi Kawawa, sana tena. Sisemi maguvu, hata; nasema utu, watu, na ubinadamu wao. Kuna binadamu zaidi ya mwenziwe? Kama huliamini hilo, utakuwa mjamaa? Hilo la kwanza... mkaliulize-ulize, mlielewe maana yake. Na mtu anayepinga ujamaa naye ajiulize kama anapinga hilo nalo. Mtu mpingaji ujamaa aseme, 'Hilo nalo, usawa wa watu, napinga; kwamba binadamu wote hivi si sawa'" - Mwalimu Julius K. Nyerere

2. 'LAZIMA MTU AFANYE KAZI'
"...Binadamu hao unaotuona hapa, na hao waliosambaa dunia nzima wanaishi kwa kazi. Hawana namna nyingine ya kuishi. Wakiacha kufanya kazi watakufa; hawana namna nyingine; kuishi kwao, na kuendelea kuishi, lazima wafanye kazi...Lakini binadamu haishi kama farasi. Binadamu haridhiki kuishi kama farasi au punda; binadamu ana kitu anakiita maendeleo; lazima aendelee...Wakati mwingine ili kusudi maendeleo haya yaje wana shughuli za kupigana misasa akili, wanapanuana mawazo tu, nayo ni kazi...nendeni mkaulizane...kama kazi si kitu cha lazima, kama binadamu anaweza kujikalia tu hafanyi kazi, akaishi, na maendeleo yakaja bila kazi. Na huyo anayepinga ujamaa naye ajiulize kama hilo analipinga? Na hilo la kufanya kazi analipinga au kuna jingine analopinga?" - Julius K. Nyerere

3. 'HAKUNA MTU KUMNYONYA MTU'
"...Kama binadamu ni sawa, tunalikubali hilo...Pili tunasema kitu kazi ni jambo la lazima kwa kila mtu, hakuna aliyesamehewa kazi. Basi siwezi kukufanyia kazi. Kukufanyia kazi maana yake ni kwamba wewe unasamehewa kazi! Siwezi kukufanyia kazi. Wewe utafanya kazi, na mimi nitafanya. Sio mimi nifanye, wewe hufanyi; lazima ufanye kazi. Kwa hiyo wewe utafanya kazi, na mimi nitafanya kazi; kila mtu atafanya kazi. Yaani namna ya kulitamka hilo ni kwamba kunyonyana hakuna. Hakuna mtu kumnyonya mtu; sasa tena msingi wa kumnyonya unatoka wapi? Tumesema watu sawa; na mtu ili aishi hana budi afanye kazi, na kazi ndio msingi wa maendeleo. Sasa mwanachama... ajiulize kama anaweza kuwa mjamaa na huku ananyonya! Unamnyonya mkeo; mkeo anakwenda kufanya kazi wewe unakwenda kupiga chibuku; hivi kweli mjamaa wewe? Tunasema kazi jambo la lazima, lakini wewe hufanyi kazi, unamnyonya mkeo. Wewe mjamaa? Nasema na hilo mjiulize...Unaweza kuwa mjamaa na huku unanyonya? Na anayepinga ujamaa ajiulize hilo nalo analipinga, kwamba yeye anaona kunyonya ni sawa tu! Sawa yeye kunyonya mwingine au wengine kumnyonya yeye, huyu anayesema kunyonya ni sawa. Kama kunyonya ni sawa baba, sasa tuanze kunyonya, au mkuki kwa nguruwe?" - Julius K. Nyerere

4. 'VYOMBO MUHIMU VIMILIKIWE PAMOJA'
"...Kama watu ni sawa; binadamu wote ni sawa; kazi ni jambo la lazima kabisa; kunyonya ni haramu; la nne linafuata: Vyombo vyote vya lazima, vinavyohitajika kwa maisha ya binadamu kwa kufanyia kazi lazima vimilikiwe kwa jumla. Ardhi lazima imilikiwe kwa jumla maana tusipoimiliki ardhi kwa jumla tutamwachia Rashidi Kawawa na Sheikh Karume wao wawe ndio wenye ardhi, na ardhi ni kitu cha lazima kwa maisha, hebu tuone kwanza usawa utakuwaje. Itakuwa lazima twende kwa Rashidi na kwa Karume, 'tafadhali bwana nataka ardhi'. Umekwishamwita 'Bwana' huyu; usawa umekwisha. Lakini vilevile kama Sheikh Kawawa ana ardhi, na Sheikh Karume ana ardhi, hawa hawalazimiki kufanya kazi. Kwa nini wafanye kazi? Hawawezi kufanya kazi. Tumesema kazi ni kitu cha lazima kwa kila mtu, lakini hawa hawawezi kufanya kazi, watakaa tu wanatutoza kodi kwa ardhi yao. Ndiyo wanatunyonya hivyo tena. Mimi nafanya kazi; mimi nalima. Halafu Rashidi anasema, 'Ukishalima mahindi ukapata magunia matano, moja langu'. Ndio ananyonya hivyo. Anavunja kanuni ya usawa; anavunja kanuni ya kazi; anavunja kanuni ya kutonyonya. Kwa nini? Kwa sababu tumemruhusu amiliki yeye vitu ambavyo vinastahili viwe vya wote. Mtu ambaye yeye ana ardhi; umemkabidhi viwanda, ukishakuwa umemkabidhi majambo mengine haya, umemwongezea nguvu zake, yeye utu wake umeongezeka-ongezeka na wangu mimi umeupunguza-punguza. Kwa hiyo vitu vilivyo vya lazima kwa kila mtu, kama ardhi ambayo ni ya lazima kwa kila mtu, lazima vimilikiwe na wote. Sasa...mjiulize kama unaweza kuwa mjamaa kweli huku unajidai ardhi yangu? Na wanaopinga wanatakaje? Hao wanaosema ujamaa mbaya. 'Eti vitu vyote viwe vya ujumla'; wengine waongo, 'Eti wanasema hata wakina mama wawe wa jumla'. Tunasema ardhi, hatusemi kina mama, tunasema ardhi viwanda, madini: kwa nini mtu mmoja anakwenda kuvinyakua vikawa vyake hivi!" - Julius K. Nyerere

5. 'KUUNDA NCHI BILA MATABAKA'
"..Kama tunakubali kuwa watu wote ni sawa; na watu wote ni lazima wafanye kazi, mtu asimnyonye mtu; na mali, mali kubwa, sikusema shati langu liwe la Rashidi: misingi ya uchumi kama mabasi yale yanapita iwe kwamba tunasema mabasi yetu, asiweko mheshimiwa mmoja pale anasema 'Basi langu lile!' Basi lako! Yupo dereva mle anaendesha, anasema dereva wake! 'Dereva wangu' - dereva wako, wewe unaweza kuwa na dereva? Dereva anaweza kuwa dereva wa umma, sio dereva wako. Dereva ni sawa sawa na mwalimu; mwalimu wa umma, daktari wa umma, dereva wa umma. Huyu anakuwaje 'wako'? Hata askari siku moja utasema wako. Kama tunakubali watu wote ni sawa; watu wote lazima wafanye kazi, hakuna kunyonyana; mali,vitu vyote vile vya jumla lazima viwe vya umma; maana yake ndio kusema tunataka kuunda nchi ambayo haina tabaka: hakuna mabwana na watwana." - Julius K. Nyerere


asilimia kubwa ya aliyoyasema sasa tunayashuhudia mbele ya macho yetu na ndio maana watu walioliua Azimio wanatapatapa kujitoa kwenye lawama kuwa hawakuhusika na uvunjaji wa hilo Azimio la aArusha
 
Ndiyo, kuna mambo ambayo katika Tanzania yetu yangeendelea kuwa mikononi mwa wananchi (siyo serikali per se). Kosa mojawapo la Azimio la Arusha ni kuweka makampuni mikononi mwa serikali moja kwa moja (100 percent) badala ya kutafuta mfumo wa jinsi gani Watanzania wangeweza kumiliki makampuni hayo. Hii ndiyo modeli yangu mpya ya uendeshaji wa TRL.



Ndiyo ulikosewa sana; huwezi kubinafsisha tu ilimradi umelitoa shirika mikononi mwa umiliki wa umma. Ubinafsishaji ulifanyika kwa minajili ya kuua mashirika yetu ya umma ili mashirika ya binafsi yafanikiwe; hawakutumia akili wala kusudi la kutaka kuyaendesha kwa faida. Ulifanywa kwa misingi ya kuwa "tumeshindwa" labda wageni "wataweza".



Ungesoma msingi wa ubinafsishaji ulikuwa ni nini; sera ya CCM wakati ule ilisemwa wazi kuwa ni kubinafsisha "mashirika yenye hasara".. siyo kubinafsisha mashirika ya umma yenye faida. Badala kukaa chini na kutumia ubongo na kuona ni jinsi gani tunaweza kuboresha mashirika hayo mengine tukaamua kuyaachia tu!

Hivi unafikiri ni kwanini Serikali ya Obama imeweka hisa kwenye Chrysler, GM na kusaidia makampuni kadhaa ya kifedha kupitia TARP wakati makampuni hayo yalikuwa ni ya binafsi? Kwanini kwa mfano hata pamoja na kufanya hasara Marekani haijauza Posta yake, haijauza Amtrak, haijauza Freddie Mac na inayo hata OPIC? Unajua kwanini serikali inaendesha PBS, Export Import Bank of the United States, North Dakota Mill and Elevator? Nchi hii ndiyo ya kibepari yenyewe!! Hadi kampuni ya Bima ya FDIC ni ya serikali.. why why why? Wakifanya Wamarekani tunaelewa lakini Nyerere kutaka kuanzisha kampuni ya Taifa ya Bima tumeona kosa!

pointi yangu ni kuwa karibu nchi zote duniani (sijapata nchi ambayo haifanyi hivyo) serikali inaendesha makampuni mbalimbali kwa kanuni za biashara za kibinafsi. Yaani, makampuni ya serikali yanaendeshwa na kushindanishwa na makampuni mengine na yale yanayopata ruzuku (kama Amtrak) yanasimamiwa kwa namna ambayo inaongeza ubora na kuhakikisha kuna japo faida ya aina fulani na yanapewa uhuru mkubwa wa kujiendesha kibiashara.

Kuna ubaya gani wa kufanya makampuni yanayomilikiwa na serikali yetu kuendeshwa kibiashara siyo kama charities?

Mkuu swali langu lililenga kutaka kujua msimamo wako, ni vizuri kujua mtu unayejadiliana naye anasimamia wapi na kuamini nini.Sijalenga kubisha au vinginenvyo nimejenga kuukuza mjadala na ulenge kuleta shule kwa wengine na mimi; Kwa hiyo tatizo si ubinafsishaji , ila ni kuwa ulikosewa, na hili nalo ni muhimu kuangaliwa maana kuna watu wana sema 'ubinafsishaji ni m'baya' bila kutoa sababu .

Kama niliyosema huko nyuma kwenye thread hii, mawazo yangu ya ubinafsishaji wa kuwapa wageni ulilenga kutudhalilisha na kufuta utu wetu, hatukufikia kiwango cha kusema 'wameshindikanika'

As I speak, majuzi wakati Barrick wanauza share, nilimtafuta mtu na kumuuliza serikali ina percent ngapi ya umiliki wa migodi, haina kitu! Nchi ya Mali serikali inashare ya asilimia 30 kwenye kila mgodi!!!

Here comes another question, je watanzania walikuwa na uwezo wa kuyanunua na kuyaendesha makampuni?, na je tungeweza kwenda kwa kasi ile ile ya globalisation?----

Hii failure ya viongozi katika hili hautokani na kutokuwa na Azimio kama wengine wanavyosema, kama sera tu watu wanashindwa kutekeleza , je azimio ambalo ni wazo litawezekanika?

I believe we have big problems in our brains tukijaribu kutafuta matatizo haya nadhani tutapona. Hainiingii akilini kwa viongozi kutokuwaza kuwa na asilimia fulani kwenye makampuni!
 
mtazamo wangu tu,

huyu mzee JKN alikuwa na mawazo ambayo wengi wetu mpaka leo tunashindwa kumwelewa alikuwa na theory ambazo ni misingi hasa ya utu, nadhani kama Nyerere angekuwa dictator basi hii nchi kwa sasa ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na filosofia zake,

Makofi!!!

JKN was simply genius, he was unique na hakuna aliyeweza kumfikia si kwa raia wala kwa viongozi! alifikiri, kutenda na kusimamia.

I said na ninafurahi umekuja hapo hapo kuwa failure ya JKN ni kwa sababu alikuwa saint! hakuwa dictator enough wa kuweza kusimamia ujamaa! JKN aliamini kila mmoja anawaza na ana moyo kama wake! kwangu mimi ni failure hiyo! aidha tumuhukumu kwa kutuamini raia wake tuamini kama yeye, au tumuhukumu kwa sababu alitupenda mno, au tumuhukumu kwa kuleta systema ambayo asingeweza kusimamia? I bet is difficult

Kisaikolojia watu kama JKN huwa wanaumizwa sana, because they trust people too much, hakujua nchi anaiweka rehani kwa kuwapa akina Mwinyi, Mkapa na sijui kama anaweza kuamini mgawa kadi wa TANU Kikwete anajiona kazaliwa mwaka 2000! hajui lolote kuhusu Nyerere!

Kwa hiyo leo hii, kama atatokea kiongozi atakayesema anataka ujamaa basi awe tayari kuwa dikteta! ujamaa unakuwa praticed naturally kama wote mko sawa kiuchumi na kiutamaduni, aidha wote tuwe maskini tu adopt ujamaa, au wote tuwe matajiri then tu-adopt ujamaa!

Ndiyo maana inakuja concept ya kuwa we need kuwashawishi watu na sio vinginevyo!

Fo God sake kwa nini huyu mzee hakuwa dictator? he could have think little like Idi amin who said!


In any country there must be people who have to die. They are the sacrifices any nation has to make to achieve law and order."--Idi Amin Dada

Ni ukweli usiopingika ujinga wa serikali na viongozi unaoendela leo ni kwa sababu hakuna kizazi kilichoteseka kuijenga nchi hii, na nchi iendelee lazima hao watu wawepo,, leo watu hwana uchungu na taifa kwa sababu tuko 'eden' hakuna wenye uchungu na nchi kwa sababu hatujateseka!

Na tusitegemee muujiza kama tusipopita hii hatua, na hata JKN aliposema lazima uwe kichaa kuhubiri na kulitekeleza AD alisema

so JKN alishashindwa kabla hata hajaanza kuadopt ujamaa! ila angeweza tu kama angeamua kila kitu kiende kimabavu na sio kikatoliki!

Sorry nisichuliwe harsh, hata leo hii kuna mamia wanaosema tunahitaji rais dikteta!!
 
Back
Top Bottom