Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Hapa utaona kwamba kusema kweli viongozi wengine akili zao ni kama mchwa...Yaani ni ajabu sana kwa Mwinyi ambaye ni mchwa kuweza kuzungumzia ubovu ama uimara wa msonobari alokula ukaisha na kubakia ganda tupu.
.
Ni hawa hawa akina Mwinyi na viongozi wengine walioua mashirika ya Umma.. wao kama mchwa waliyafilisi mashirika kisha wakaamua kuyauza kama vile mapungufu yapo ktk mashirika..tatizo ni mchwa kwa nini wakayauza mashirika na sio kuthibiti hao mchwa? sii ndio yale yale ya kugawa vyandarua kuzuia malaria hali wakiacha mbu wakizaana!.

kwa akili zake za ajabu, Mwinyi anakiri kwamba kwamba haya mashirika yaligunguliwa na mchwa, ambao ndio wao...cha ajabu wameuza mashirika ambayo tayari yamekwisha liwa na mchwa, kisha Hilo Azimio la Zanzibar likawapa RUKSA hao mchwa walio yaharibu mashirka ya Umma wahamie miti mingine..

Mimi nadhani huyu Mwinyi anazeeka vibaya, anakosa hekima na busara zake za awali kwani hakuwa na sifa yoyote ya Uongozi zaidi ya hekima zake!

Sitaki kumtetea Mwinyi lakini naomba kuuliza hadi alipoingia Mwinyi madarakani hali ya uchumi wetu ilikuwa vipi tukifananinisha na hali ilivyokuwa wakati tunapata uhuru?
 
Companero thanks for this useful post, nadhani Mwinyi yuko sahihi kusema hakuliua. Hakuna sentensi inayo suggest hivyo, na sababu zake alizozitoa are still concrete

Mkuu ulitegemea aseme nimeliua Azimio la Arusha?? Ni mgeni na wanasiasa?

Ni wazi Azimio la Arusha linauliwa kwa vitendo, sera na misimamo mipya ya kiserikali zaidi kuliko hutba za kisiasa.
 
Companero,
Mkuu wangu ktk hotuba ile alisema hawakulifuta Azimio la Arusha ila wameliboresha kwa kufuta baadhi ya sheria ili kutuwezesha kitaifa kwenda na wakati! akilenga soko huria na Utandawazi.

Lakini kama kweli walitaka kulenga Soko Huria na Utandawazi, hapakuwepo na sababu ya kuuza mashirika ya Umma ikiwa makosa ni WATU walioharibu mashirika hayo. kifupi hawkuuza nyumba ama gofu ila waliuza viwanja..Sisi wananchi tunatazama thamani ya viwanja vile, wakati wao wanatupa hadithi za magofu...Ni hadithi hii hii wnaitumia kuuza pia nyumba za National housingi na Msajili.
Pili, hapakuwepo na sababu ya kuondoa miiko na maadili ya Uongozi ikiwa soko huria halihusianai na viongozi kufanya Biashara...kuepuka conflict of interest ni moja ya Maazimio makubwa ya Arusha.

Ndani ya roho zetu sisi sote tunajua fika kwamba - Siasa ya Ujama na Kujitegemea ilikufa na hakuna kitu wala mfano hata mmoja kiutawala unaolenga siasa ya Ujamaa na Kujitegemea hii leo, sasa nambie wewe mkuu wangu, ikiwa Ujamaa na Kujitegemea umekufa hilo Azimio la Arusha ni lipi analozingimzia Mwinyi?....


Unajua Mkandara unazungumzia theories wakati hali halisi inakusuta kwa hayo unayoyaeleza.au wakati anaingia mwinyi ulikuwa bado huujuwi dunia? Mashirika yalitowa ajira kwa watu jee wangelipwa nini wakati mashirika hayazalishi na wala serikali haina pesa za kuwagawia wafanyakazi kama ngawira?
Unapozungumzia kuondowa miiko ya uongozi unakusudia miiko hiyo ni ipi? Azimio la Arusha halikuwa na mipaka kati ya kiongozi na mwananchi wa kawaida kwani kwenye Azimio hilp unajua Kiongozi ni nani? Iwapo kila mfanyakazi anazuiliwa kupata kipato cha ziada nini maana yake? Wafanyakazi wafe njaa chini ya malipo dubi na yasiyokuwepo? Taifa la Watanzania hapo likisemwa kuwa la wafanyakazi na Wakulima sasa mihimili ya uchumi inaponyimwa mfanyakazi na mkulima yuko kijijini na Serikali haina Fedha za kuendesha biashara nchi itaenda vipi. Ndio maana Marmo amesema kuwa mambo mengi yanasababisha hali hii tunayojadiliana nayo.
 
Mkuu ulitegemea aseme nimeliua Azimio la Arusha?? Ni mgeni na wanasiasa?

Ni wazi Azimio la Arusha linauliwa kwa vitendo, sera na misimamo mipya ya kiserikali zaidi kuliko hutba za kisiasa.

Unachosema ni sahihi, kuwa hajasema directly kuwa ameua, at the same time tunataka kusema ameua! kwa sababu ya kuruhusu mambo mengi!

Hoja yangu ni kuwa AD lilikufa natural death, lilishakufa kabla ya kuanza kuw in effect, unless mtu aje na atoe mafanikio ya azimio wakati liko in effect

Huwezi kuchanganya UJAMAA NA KUJITEGEMEA wakati mmoja, hakuna kitu kama hicho! ukisema kujitegema na ujamaa lazima viende pamoja lazima uweke mipaka ya kujitegemea basi.

Lilikufa natural death si Mwinyi aliliua wala nani, after all nataka niwafahamu hao waanzilishi wa Azimio, kuwa walikuwaje waka 'kubaliana' na sera za Mwinyi kiasi hicho? what made them to abandon Azimio?
 
Serikali ya Mzee Mwinyi haiwezi kukwepa makosa ya kuyaua mashirika ya umma kwani hao mchwa walioyala yakaisha waliteuliwa na walikuwa wakilindwa na serikali hata pale wafanyakazi walipotaka kupambana nao.

Serikali kwa ujumla ndo ilikuwa mwangalizi wa mashirika hayo ikiteua menejimenti na bodi za kuyaendesha mashirika na kuzisimamia. Mashirika yalikufa huku serikali ikiangalia bila kuchukua hatua yoyote. Hata pale ilipochukua hatua hatua hizo mara nyingi ilikuwa kuwalinda mchwa walaji na waharibifu. Hali iko hivyo hadi leo hii. Mashirika ambayo serikali inatakiwa iyaendeshe kwa niaba ya wananchi yanabaki kama mali isiyo na mwenyewe yakiharibiwa na kufirisiwa na watendaji wachache ambao hulindwa na serikali ambayo huwaweka madarakani.

Ujamaa na ubepari zote ni sera makini. Tafsiri zinazotolewa kutokana na maneno ya mzee mwinyi ni kuwa Tanzania leo ni mabepari ndo maana kuna wizi na jinai zilizokithiri serikalini. Sikubaliani na maoni hayo kwani jinai na wizi unaoendelea si ubepari na si matokeo ya kuja kwe sera ya ubepari. Ni matoke ya kukosekana kwa uwajibikaji kunakosababishwa na wale waliopewa majukumu ya kuwawajibisha watu kushindwa kutekeleza wajibu wao.

Kushindwa kwa rais wa awamu ya pili kufanya kazi yake ndo kuliko sababisha mmomonyoko wa maadili na ufisadi uliokithiri kujikita serikalini hadi kufikia kuurasmisha kwa kutangaza Azimio la Zanzibar. Hili halikuwa azimio kikweli kweli ila ilikuwa ni uhuni tu wa kuondoa masharti ya viongozi kuzitumia ofisi zao kujinufaisha. HUU KAMWE SI UBEPARI. Nchi zote za kibepari (ubepari wa kisasa) zina sheria kali sana zinazozuia viongozi kutumia ofisi za umma kujitajirisha.

Viongozi sasa waliruhusiwa kutumia ofisi zao moja kwa moja kufanya shughuli binafsi bila kubughudhiwa na yeyote kwa sababu uongozi ulikuwa umekufa; ingawa mzee Mwinyi alikuwepo kama kiongozi, uongozi ilikuwa hakuna.
 
Sitaki kumtetea Mwinyi lakini naomba kuuliza hadi alipoingia Mwinyi madarakani hali ya uchumi wetu ilikuwa vipi tukifananinisha na hali ilivyokuwa wakati tunapata uhuru?


Nimeuliza swali hilo hakuna aliyejibu , mtu aje na tangible proof kuwa jamani ehe! wakati wa AD mafaniko yalikuwa haya, na wakati wa Mwinyi tulidorora kiasi hiki!

AD was talks, na Mwinyi amejibu hizo talks na kusema hakuliua! we are living in the world of no talks! action ambazo zinaendana na hali halisi ya natural behaviour ya binadamu!

Ujamaa na kujitegemea (if it make sense) ili uwe effect basi lazima kiongozi awe dictator, kama Nyerere hakuwa na dictator basi maana yake alianzisha siasa ambayo asingeweza kuitekeleza bila kuwa dictator! which is again is another failure!

Somethings just happens, kutafutana uchawi wakati hatuwezi kupima mafanikio ya Azimio hili ni kudanganyana! Laws and order are far superior than AD au whatever!
 
Huyu Mzee ni heri angekaa kimya bila kusema kitu kuhusu Azimio la Arusha!

Analia eti viongozi walihujumu mashirika, je yeye na Nyerere walifanya nini kudhibiti uzembe na utovu wa nidhamu wa viongozi hao ili tabia chafu na mbaya zisiendelee?

Pili ni chini ya uongozi wake, ndio msukumo wa kujenga Taifa linalojitegemea kwa kupitia uzishaji wa ndani ulifutwa na kipaumbele kikatengwa kuleta wawekezaji!

Nahisi kana kwamba viongozi wengi ama hawakutumia muda wa kutosha kulisoma Azimio la Arusha na kulielewa au kwa kuwa hawakukubaliana nalo na hasa kuhusu miiko ya uongozi ambayo ni sehemu ndogo sana wakaamua kuliua kwa nguvu zote!

Je tumuulize Mzee Mwinyi, ile azma ya kujenga Taifa linalojitegemea ilikwenda wapi? Kwa nini basi badala ya kurekebisha kasoro za udhifu wa uongozi na uendeshaji wa mashirika na mfumo mzima wa uchuni, yeye na wenzake walikimbilia kujenga mfumo wa uchumi tegemezi kupitia wawekezaji na hata kuwapa ruhusa ya kutuchuna mpaka ngozi kwa misamaha ya kodi na ushuru na Sheria mbovu ambzo ndio zinaifanya kampuni kama Barrick inenepe na kuneemeka kupita kiasi?
 
Serikali ya Mzee Mwinyi haiwezi kukwepa makosa ya kuyaua mashirika ya umma kwani hao mchwa walioyala yakaisha waliteuliwa na walikuwa wakilindwa na serikali hata pale wafanyakazi walipotaka kupambana nao.

Serikali kwa ujumla ndo ilikuwa mwangalizi wa mashirika hayo ikiteua menejimenti na bodi za kuyaendesha mashirika na kuzisimamia. .

Mashirika ya umma yamekufa kipindi Nyerere yupo na yeye alikuwa anawahamisha watu kutoka shirika moja kwenda lingine, Mashirika ya umma yamekufa kipindi cha Mwinyi, mashirika ya umma yamekufa kipindi cha Mkapa, leo hii mwaka juzi au jana general tyre imekufa vizuri tu!

Lazima tuangalie msingi wa kufa haya mashirika, then we can jump into conclusion, lazima tujue matatizo yetu kama watanzania pasipo kusukumia watu mizigo fulani. We will always be living in the world of excuse and passing blames to others

Mrema mpaka anahizmiza watu kuwahi kazini miaka ile na kuchora mistari myekundu! leo hii uozo ulioko serikalini wa kucheza karata asubuhi au computer games si za Mwinyi kubeba!

I can simply suggest ujamaa wa Saint Nyerere ndio ulioleta uvivu!, ujamaa wa Nyerere ungekuwa kama wa wachina (yaani awe dictator) tusingekuwa wavivu!
 
Hakuna kitu kibaya kama kinachocost watu maisha... zile roho zao husuta watu waliochangia mateso yao hadi mwisho!!! tunachokiona kwa mze ruksa, juzi hapa alileta sumaye (na ya EPA) na che-nkapa (RADA na kuzomewa) na wengineo!!!

Ni fukuto la ajabu ndani ya nafsi hasa unapokutana na mrundikano wa roho hai zenye nia njema, its the power of love and God inayowapeleka watu kukiri au kukosea kwenye kukanusha makosa
 
Hivi kwanini tunapoteza nguvu nyingi katika ya kuililia Azimio la Arusha badala ya katiba ya nchi ambayo ndio mwongozo kwa kila mwananchi na viongozi pia.

kwanza Azimio la Arusha halina nguvu kikatiba kama sikosei,pia
linawahusu CCM na ndio maana limefutwa kirahisi.

Hivi chadema wakichukua inchi Azimio la Arusha nafasi yake itakuwa wapi?

Hivi unafikiri katiba ya nchi ingekuwa inakizi bora tungeyahitaji haya maazimio ya chama furani ndio urekebishe viongozi.
 
Unachosema ni sahihi, kuwa hajasema directly kuwa ameua, at the same time tunataka kusema ameua! kwa sababu ya kuruhusu mambo mengi!

Hoja yangu ni kuwa AD lilikufa natural death, lilishakufa kabla ya kuanza kuw in effect, unless mtu aje na atoe mafanikio ya azimio wakati liko in effect

Huwezi kuchanganya UJAMAA NA KUJITEGEMEA wakati mmoja, hakuna kitu kama hicho! ukisema kujitegema na ujamaa lazima viende pamoja lazima uweke mipaka ya kujitegemea basi.

Lilikufa natural death si Mwinyi aliliua wala nani, after all nataka niwafahamu hao waanzilishi wa Azimio, kuwa walikuwaje waka 'kubaliana' na sera za Mwinyi kiasi hicho? what made them to abandon Azimio?

Sidhani kaa ni kweli kwamba kuwa na Ujamaa na Kujitegemea kwa pamoja ilikuwa ni kuji-cotradict. Kujitegemea kunakoongelewa ni kama taifa kuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yake na kuagiza kutoka nje ya nchi yetu tu vile vinavyotushinda kuwa navyo kutokana kuwa nyuma kitecknoljia au kihali yeyote ile.

Ujamaa ni kwamba state have a total control of major means of economy, kama mashirika ya kutoa huduma a.k.a mashirika ya umma, n.k. Ndo maana kwamba kulikuwa na kuanzishwa viwanda ambavyo mchwa walikuja kuviua, kuimarisha kilimo, kujenga miundombinu kaa Tazara etc etc..

I' m still a big fan of this ideas. Yet I know things never turned-out, lakini kulikuwa na prospect ya kuwa na nchi imara ktk muda wa miongo miwili mitatu. Pia ni shurti izingatiwe maadui wa siasa hii walikuwa wengi na very strong polarization hasa kutoka kwa mabwanyenye waliokuwa wamejikita huko Kenya na wakoloni waliokuwa Norh & South Rhodesia na maadui wote wa vita ya ukombozi kusini mwa Africa.
 
...........wangeacha hata ile miiko ya uongozi....duh hivi ile tume ya maadili ya viongozi pale Ohio next to Holland house inafanya kazi bado?....

Ipo
Ila Mzee Kitudu alikufa nayo, hawa wa sasa hivi wanachukua mshahara tuu
 
Waberoya,

Hao mabepari wenyewe wamekwama. USA walipewa uhuru wa watu/mashirika binafsi kujifanyia kila kitu wanavyotaka wenyewe. Nini kimetokea?

Msiandike kwa kutumia mfano mmoja. Angalieni mbele na nyuma na ndipo mje na hizo zenu za kutetea kufa kwa Azimio la Arusha. Mwinyi na Mkapa walitakiwa kurekebisha yale tu ambayo kwao wanaona yanafanya uchimi ukwame. Pia unaporekebisha si kuwa ubadili kila kitu. Unafanya kwanza majaribio na kidogokidogo unaangalia umetoka wapi na umefikia wapi. Wachina wanafanya hivyo hadi leo kwa mafanikio makubwa. Wangelitangaza kuwa wako HURU kama sisi tulivyofanya, nafikiri leo wangelikuwa na vita na machafuko ya kila aina.

USA kimegoma na mwisho serikali imerudi na kusema itakuwa inaweka mkono wake kila sehemu ili walau wafahamu nini kinaendelea kwenye mashirika. Ilishindikana nini kuwapa Watanzania hata kama kwa Mkopo mashirika yote na serikali ibaki kuwa mwangalizi tu na kuchukua kodi. Leo hii haya mashirika yangelikuwa yanaongozwa/kumilikiwa na wazawa na sidhani kama yangelikuwa yamekufa.

Siyo siri kuwa wapinzani wa NYERERE walifanya makusudi kuyauwa mashirika ili tu kuonyesha Azimio la Arusha ni la ovyo. Walipokipata wanachokitaka, wakaliingilia Azimio la Arusha na kuliuwa kwa ndani na kuacha mwili wake nje (jina) ili mtu akisema, wawe wadai kuwa ahhh, AD bado ipo hai kabisa na inaendelea vizuri sana. Too sad.

Ndiyo maana Nyerere anasema "wenye akili tukajua AD imekufa". Yaani hata Miiko ya viongozi? Nakubaliana na member mmoja hapo juu kuwa AD iingizwe kwenye Katiba ya nchi hasa kile kipengele cha Miiko ya viongozi. Haya ya juzi kumsikiliza Mkono na Genge lake wakitetea kuwa CCM inatakiwa iwe na mafiga matatu yaani Wakulima, wafanyakazi na Wafanya biashara, kwa kweli ni kichekesho. Wafanyabiashara wenyewe ni CCM ambao hata unashindwa lini wameanza kuwa wafanyabishara zaidi ya kuwa na pesa za ufisadi.

UJAMAA na Kujitegemea: Wayahudi waliweza sana kuanza na hii system. Imewasaidia sana sana. Sisi tumekwama sijui ni Miafrika ndivyo tulivyo au viongozi wetu?
 
Mzee Mwinyi afadhali amesema maana kizazi hiki walikuwa hawajui kuwa ni mtu asiekuwa makini kabisa kwenye kauli zake.
Aseme wazi tu kuwa kama kuna mtu si mcha Mungu na alishirika kuliua Azimio ni yeye then atubu, tutamuelewa...
Mzee mnafiki sana huyu!
 
Sidhani kaa ni kweli kwamba kuwa na Ujamaa na Kujitegemea kwa pamoja ilikuwa ni kuji-cotradict. Kujitegemea kunakoongelewa ni kama taifa kuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji yake na kuagiza kutoka nje ya nchi yetu tu vile vinavyotushinda kuwa navyo kutokana kuwa nyuma kitecknoljia au kihali yeyote ile.

Ujamaa ni kwamba state have a total control of major means of economy, kama mashirika ya kutoa huduma a.k.a mashirika ya umma, n.k. Ndo maana kwamba kulikuwa na kuanzishwa viwanda ambavyo mchwa walikuja kuviua, kuimarisha kilimo, kujenga miundombinu kaa Tazara etc etc..

I' m still a big fan of this ideas. Yet I know things never turned-out, lakini kulikuwa na prospect ya kuwa na nchi imara ktk muda wa miongo miwili mitatu. Pia ni shurti izingatiwe maadui wa siasa hii walikuwa wengi na very strong polarization hasa kutoka kwa mabwanyenye waliokuwa wamejikita huko Kenya na wakoloni waliokuwa Norh & South Rhodesia na maadui wote wa vita ya ukombozi kusini mwa Africa.

Haiwezekani ukaongelea kujitegema kama taifa bila individual kuwa na input, watu wanaojenga taifa ni watu ni raia ni mmoja mmoja, sielewi unavyotaka kutenganisha kujitegema kwa taifa na mtu mmoja mmoja

Lingine ni kuwa hivi tusingetangaza AD basi tungekuwa ombaomba na kutegemea nchi za watu? Je leo hii JK anyooomba omba anafanya hivyo kwa sababu azimio la arusha lilikufa? . Kujitegemea is not human responsibility anymore katika planet hii, unataka kusema waasisi wa kujitegemea walifanya hivyo kwa sababu hatukuwa na mind ya kujitegemea muda huo? Misada mingapi tulipokea kipindi tunaishi katika azimio la Arusha? kuna fedha tulizikataa kwa sababu tunajitegemea?

Baaada ya kuelimika nykatai hizi still watu wanaenda kuombaomba, no innovations, no research, no what, simply kwa sababu hakuna AD anymore?

Unataka ku-blame wengine kwa failure zetu, maana naona ushaanza kutaja watu wa nje! Africa nzima tulikuwa na maadui?? na hao wakorea tulikokuwa nao sawa kiuchumi mwaka 1961 walitumia siasa gani kuwafikisha walipo leo?

Ukiingiza siasa za mataifa ya nje kuwa walichangia kwa sisi kutoendelea ndipo unapomsafisha Mwinyi!

ATC is dying today simply because AD is not there! TUTAFUTE MATATIZO MENGINE TULIYONAYO si kwa sababu hatuna AD!
 
Waberoya,

Hao mabepari wenyewe wamekwama. USA walipewa uhuru wa watu/mashirika binafsi kujifanyia kila kitu wanavyotaka wenyewe. Nini kimetokea?

Msiandike kwa kutumia mfano mmoja. Angalieni mbele na nyuma na ndipo mje na hizo zenu za kutetea kufa kwa Azimio la Arusha. Mwinyi na Mkapa walitakiwa kurekebisha yale tu ambayo kwao wanaona yanafanya uchimi ukwame. Pia unaporekebisha si kuwa ubadili kila kitu. Unafanya kwanza majaribio na kidogokidogo unaangalia umetoka wapi na umefikia wapi. Wachina wanafanya hivyo hadi leo kwa mafanikio makubwa. Wangelitangaza kuwa wako HURU kama sisi tulivyofanya, nafikiri leo wangelikuwa na vita na machafuko ya kila aina.

USA kimegoma na mwisho serikali imerudi na kusema itakuwa inaweka mkono wake kila sehemu ili walau wafahamu nini kinaendelea kwenye mashirika. Ilishindikana nini kuwapa Watanzania hata kama kwa Mkopo mashirika yote na serikali ibaki kuwa mwangalizi tu na kuchukua kodi. Leo hii haya mashirika yangelikuwa yanaongozwa/kumilikiwa na wazawa na sidhani kama yangelikuwa yamekufa.

Siyo siri kuwa wapinzani wa NYERERE walifanya makusudi kuyauwa mashirika ili tu kuonyesha Azimio la Arusha ni la ovyo. Walipokipata wanachokitaka, wakaliingilia Azimio la Arusha na kuliuwa kwa ndani na kuacha mwili wake nje (jina) ili mtu akisema, wawe wadai kuwa ahhh, AD bado ipo hai kabisa na inaendelea vizuri sana. Too sad.

Ndiyo maana Nyerere anasema "wenye akili tukajua AD imekufa". Yaani hata Miiko ya viongozi? Nakubaliana na member mmoja hapo juu kuwa AD iingizwe kwenye Katiba ya nchi hasa kile kipengele cha Miiko ya viongozi. Haya ya juzi kumsikiliza Mkono na Genge lake wakitetea kuwa CCM inatakiwa iwe na mafiga matatu yaani Wakulima, wafanyakazi na Wafanya biashara, kwa kweli ni kichekesho. Wafanyabiashara wenyewe ni CCM ambao hata unashindwa lini wameanza kuwa wafanyabishara zaidi ya kuwa na pesa za ufisadi.

UJAMAA na Kujitegemea: Wayahudi waliweza sana kuanza na hii system. Imewasaidia sana sana. Sisi tumekwama sijui ni Miafrika ndivyo tulivyo au viongozi wetu?

Huwezi ukafananisha ujamaa wa Nyerere na hao wachina, warussia n.k ,. Ujamaa wa Nyerere ulikuwa ni hybrid ya hizo siasa na influence ya watu wengi

Hakuna sehemu pia ninayosuggest kuwa Ubepari ni bora, mind yangu haijawekwa kwenye kapu kuwa kama si ujamaa basi ni ubepari!

Nyerere na waasisi wengine wa siasa ya ujamaa ya Tanzania, still they have credit to gain, wanastahili sifa na heshima zao na hasa kuwa na siasa ya ujamaa na kujitegemea ya kwetu sisi! Nyerere angeiga wachina angekuwa dictator!

My argument katika dunia ya leo, na kizazi cha leo, cha watu millioni 45 we have to sit down na kuona AD ilikuwa na uzuri upi, na kasoro ipi! lazima tujue pia nature na tabia zetu watanzania wa leo, lazima tuangalie influence ya globalisation, climate change, terrorist, ambayo hatuwezi kujitoa kwayo, lazima tuangalie je Kujitegemea kunakosemwa kulikuwa na vision ipi, malengo yapi?

Hakuna siasa 100% perfect kama JKN aliweza kutoka na siasa yake, we dont have people ambao wakasimama na kusema lets take Nyerere's idea na kujumlisha na idea zingine na tufuate hivi kwa leo hii.JKN idea will never be our compass.

Kurudi nyuma na kulilia AD ni sawa na kurudi tulipofeli, AD is katiba? ni biblia au Quran? watu leo hii wameiba hawapelekwi jela wala kurudisha mali zetu ni kwa sababu ya AD haipo?? i dont get it!

Hata leo hii JKN angekuwa hai , na tukampa nchi tena, his mind today lazima ni tofauti na nyakati hizo. We need to start now and make our future! siamini kabisa kuwa system za dunia hii ni ubepari na ujamaa tu. Tumefikia hapo, tumekwama hapo na kuamini ubepari mzuri kwa sababu hatujafanya assignment zetu vizuri.

Kulilia AD ni kupoteza muda, kama hakuna anayeweza kupima mafanikio ya siasa hii na imebaki fiction, then ndiyo kufeli kwenyewe huko, hatuihitaji story nyingi wala sababu, ambazo tunazo kila siku na hazikosekani!

Kama leo hii mtu bado anaona pamoja na hii kitu kufail still anaona ni bora zaidi, basi tuna matatizo mengi na makubwa ambayo lazima tuyatatue hayo ili kufikia ujamaa na kujitegema, kwa namna nyingine JKN alitoa idea ambayo pengine it will work next century! we have big big problems na matabia yetu haya ili kuishi kwenye hilo azimio!

However, I am still thinking whether kama matatizo ya leo ni kutokana na sera ya ujamaa!

If this is our mind, lets Kikwete and his partner plunder our wealthy because AD IS DEAD na yeye siye aliyeliua!

I believe in Law, order and JUSTICE.

I believe every human shall work and improve our society and the universe siyo kwa sababu mtu fulani kasema ni kwa sababu tumezaliwa tukijua hilo!

Ninachokataa ni kuwa kuna watu hawataki kungalia failure ya hizi siasa, hatutaki kukaa chini na kusema JKN and so and so walikosea hapa na walipatia hapa., na sisi leo tuchuke idea znuri za JKN na kuacha makapi na kuungansiha na hali yetu ya sasa na kusonga mbele!
 
Huwezi ukafananisha ujamaa wa Nyerere na hao wachina, warussia n.k ,. Ujamaa wa Nyerere ulikuwa ni hybrid ya hizo siasa na influence ya watu wengi

Hakuna sehemu pia ninayosuggest kuwa Ubepari ni bora, mind yangu haijawekwa kwenye kapu kuwa kama si ujamaa basi ni ubepari!

Nyerere na waasisi wengine wa siasa ya ujamaa ya Tanzania, still they have credit to gain, wanastahili sifa na heshima zao na hasa kuwa na siasa ya ujamaa na kujitegemea ya kwetu sisi! Nyerere angeiga wachina angekuwa dictator!

My argument katika dunia ya leo, na kizazi cha leo, cha watu millioni 45 we have to sit down na kuona AD ilikuwa na uzuri upi, na kasoro ipi! lazima tujue pia nature na tabia zetu watanzania wa leo, lazima tuangalie influence ya globalisation, climate change, terrorist, ambayo hatuwezi kujitoa kwayo, lazima tuangalie je Kujitegemea kunakosemwa kulikuwa na vision ipi, malengo yapi?

Hakuna siasa 100% perfect kama JKN aliweza kutoka na siasa yake, we dont have people ambao wakasimama na kusema lets take Nyerere's idea na kujumlisha na idea zingine na tufuate hivi kwa leo hii.JKN idea will never be our compass.

Kurudi nyuma na kulilia AD ni sawa na kurudi tulipofeli, AD is katiba? ni biblia au Quran? watu leo hii wameiba hawapelekwi jela wala kurudisha mali zetu ni kwa sababu ya AD haipo?? i dont get it!

Hata leo hii JKN angekuwa hai , na tukampa nchi tena, his mind today lazima ni tofauti na nyakati hizo. We need to start now and make our future! siamini kabisa kuwa system za dunia hii ni ubepari na ujamaa tu. Tumefikia hapo, tumekwama hapo na kuamini ubepari mzuri kwa sababu hatujafanya assignment zetu vizuri.

Kulilia AD ni kupoteza muda, kama hakuna anayeweza kupima mafanikio ya siasa hii na imebaki fiction, then ndiyo kufeli kwenyewe huko, hatuihitaji story nyingi wala sababu, ambazo tunazo kila siku na hazikosekani!

Kama leo hii mtu bado anaona pamoja na hii kitu kufail still anaona ni bora zaidi, basi tuna matatizo mengi na makubwa ambayo lazima tuyatatue hayo ili kufikia ujamaa na kujitegema, kwa namna nyingine JKN alitoa idea ambayo pengine it will work next century! we have big big problems na matabia yetu haya ili kuishi kwenye hilo azimio!

However, I am still thinking whether kama matatizo ya leo ni kutokana na sera ya ujamaa!

If this is our mind, lets Kikwete and his partner plunder our wealthy because AD IS DEAD na yeye siye aliyeliua!

I believe in Law, order and JUSTICE.

I believe every human shall work and improve our society and the universe siyo kwa sababu mtu fulani kasema ni kwa sababu tumezaliwa tukijua hilo!

Ninachokataa ni kuwa kuna watu hawataki kungalia failure ya hizi siasa, hatutaki kukaa chini na kusema JKN and so and so walikosea hapa na walipatia hapa., na sisi leo tuchuke idea znuri za JKN na kuacha makapi na kuungansiha na hali yetu ya sasa na kusonga mbele!

Mzee mtazamo wako mie nimeuunga mkono kwa kiasi kikubwa mno... na inafurahisha kuona kuwa kumbe kuna watanzania wanafikiri vizuri tuu..
Sasa msiwe mnaishia humu tu jamani, jitanueni hata kwenye Ubunge n.k
Amini usiamini nchi yetu inataka watu wenye uwezo wa kufikiri na kutoa uamuzi.
 
NINAMUHESHIMU MZEE MWINYI ZAIDI YA MAELEZO ! UJAMAA(azimio la arusha) LINABAKI KUWA PEKEE MPAKA SASA LENYE NIA YA KWELI NA YA DHATI KUMSAIDIA MTANZANIA....! HUENDA BABA YETU MWINYI AMEGUNDUA HILO NDO HATA SASA AMEKUJA NA HOJA HII....MZEE HAJAKOSEA INABIDI TUMPONGEZE KWA KUNG'AMUA HILO.......AMELETA UBEPARI LAKINI AMEONA YOTE SI MAJIBU KWA MTANZANIA BALI UJAMAA....(azimio la arusha)HONGERA NA PONGEZI MZEE WETU KWA KUJIREKEBISHA....WENGINE NAO WAUNGE MSTARIIIIII....!

Kinyume cha ' thanks' ni nini ? JF Adminisstrator should provide something to denounce some comments. Mimi naona niseme kuwa wewe na mzee Mwinyi wote mmezeeka vibaya,
Mzee Mwinyi ndiye Baba wa ufisadi nchini. Period
 
Inaoenekana kuna watu wanabisha sana humu japo hawajasoma Azimio la Arusha. Ndio maana limechapishwa upya ili mlisome. Azimio linalenga kujitegemea kuanzia ngazi ya mtu binafsi, familia, mtaa/kijiji, wilaya, mkoa hadi Taifa. Ni mwongozo thabiti wa nchi yetu.
 
"Kujitegemea kwa mtu mmoja ni kujitegemea kwa nyumba kumi. Kujitegemea kwa nyumba zote kumi za balozi ni kujitegemea kwa tawi zima. Kujitegemea kwa matawi ni kujitegemea kwa Wilaya ambayo ni kujitegemea kwa Mkoa. Kujitegemea kwa Mikoa yote ni kujitegemea kwa Taifa lote ambalo ndilo lengo letu." - Azimio la Arusha
 
Back
Top Bottom