Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Sikulifuta Azimio la Arusha - Mwinyi

Facts zinabaki kuwa facts tu, Japo nchi kama Marekani na za Ulaya zinajiita ni za Kibepari lakini Serikali zao zinaact socialism ya nguvu kuliko hata hii waliyokuwa wanaipinga ya Mwalimu, ni ukweli ulio wazi Nchi ikiwa ya kibepari moja kwa moja Haitaweza kutawalika hata kidogo na ili kuwapumbaza watu (Walio wengi) ili Ubepari usimame, basi Serikali pamoja na hao Mabepari wanakuwa na jinsi ya kuwasidia kwa njia moja ama nyingine
 
Makofi!!!

JKN was simply genius, he was unique na hakuna aliyeweza kumfikia si kwa raia wala kwa viongozi! alifikiri, kutenda na kusimamia.

I said na ninafurahi umekuja hapo hapo kuwa failure ya JKN ni kwa sababu alikuwa saint! hakuwa dictator enough wa kuweza kusimamia ujamaa! JKN aliamini kila mmoja anawaza na ana moyo kama wake! kwangu mimi ni failure hiyo! aidha tumuhukumu kwa kutuamini raia wake tuamini kama yeye, au tumuhukumu kwa sababu alitupenda mno, au tumuhukumu kwa kuleta systema ambayo asingeweza kusimamia? I bet is difficult

Kisaikolojia watu kama JKN huwa wanaumizwa sana, because they trust people too much, hakujua nchi anaiweka rehani kwa kuwapa akina Mwinyi, Mkapa na sijui kama anaweza kuamini mgawa kadi wa TANU Kikwete anajiona kazaliwa mwaka 2000! hajui lolote kuhusu Nyerere!

Kwa hiyo leo hii, kama atatokea kiongozi atakayesema anataka ujamaa basi awe tayari kuwa dikteta! ujamaa unakuwa praticed naturally kama wote mko sawa kiuchumi na kiutamaduni, aidha wote tuwe maskini tu adopt ujamaa, au wote tuwe matajiri then tu-adopt ujamaa!

Ndiyo maana inakuja concept ya kuwa we need kuwashawishi watu na sio vinginevyo!

Fo God sake kwa nini huyu mzee hakuwa dictator? he could have think little like Idi amin who said!


In any country there must be people who have to die. They are the sacrifices any nation has to make to achieve law and order.”--Idi Amin Dada

Ni ukweli usiopingika ujinga wa serikali na viongozi unaoendela leo ni kwa sababu hakuna kizazi kilichoteseka kuijenga nchi hii, na nchi iendelee lazima hao watu wawepo,, leo watu hwana uchungu na taifa kwa sababu tuko 'eden' hakuna wenye uchungu na nchi kwa sababu hatujateseka!

Na tusitegemee muujiza kama tusipopita hii hatua, na hata JKN aliposema lazima uwe kichaa kuhubiri na kulitekeleza AD alisema

so JKN alishashindwa kabla hata hajaanza kuadopt ujamaa! ila angeweza tu kama angeamua kila kitu kiende kimabavu na sio kikatoliki!

Sorry nisichuliwe harsh, hata leo hii kuna mamia wanaosema tunahitaji rais dikteta!!

Waberoya,

Hii mada kama sikosei ilikuwa inazungumzia kauli ya Mzee Mwinyi kuwa hakuliua azimio la Arusha bali lilijiua lenyewe au lilikuwa limeshakufa before. Wengi mkakubaliana. Wengine tunakataa na tunaona hiyo kama ni ujanja ujanja wa kuhamisha hoja na kukwepa kuwajibika kwa makosa waliyo yatenda. Naona umeshaingia kwenye pipa hilo sasa unahamishia hukumu kwa Nyerere ambayo nafikiri inaakisi tofauti yako ya kibinafsi na Mwalimu.

Ikiwa hoja ni kuuawa kwa azimio la Arusha na the aftermath, ni nani hasa alihusi? Basi nadhani hayo niliyochukua hapo juu yako nje. Azimio lilikuwepo na wengi hapa wameshasema lilikuwa roadmap. Mlio upande wa mzee mwinyi kujiondoa kuliua azimio la Arusha mnasema after all azimio lilikuwa failure kwa hivyo alichofanya mzee mwinyi ni kuliachia lijifie lenyewe. Wengine tunasema siyo hivyo kamwe. Azimio lilikuwepo na lilikuwa bado linatishia kuwang'ata ndo maana waka-formalize mambo kupitia azimio la Zanzibar. Wengine mnasema AA haikuwa sheria kwa hiyo haikuwa binding na hiyo ndo failure yake.

Sasa nijaribu kujibu baadhi ya hizo hoja. Kusema kuwa azimio tayari lilikuwa ni failure ni kutoelewa AA has ilikuwa ni nini. Waliotusaidia wameshasema hilo halikuwa sheria lilikuwa ni vision, ni mahali tunapotaka kwenda. Kuna sheria nyingi zilitungwa na jitihada nyingi zilifanyika. Mfano ni kuanzishwa mlolongo wa mashirika ya umma; Yameshatajwa hapa. Zilianzishwa tume za bei, Mali zilitaifishwa, Siasa ni kilimo, Universal Primary Education (UPE) - Tanzania iliapata kiwango cha juu cha literacy kipindi hicho, n.k. Hizi zote hazikuja kwa bahati mbaya, ilikuwa ni juhudi zilizokuwa na lengo moja la ku-achieve kile kilichokuwemo kwenye Azimio la Arusha (AA).

Mashirika yote yaliyoanzishwa, yalikuwa na business models ambazo zilikuwa sound na zina-atract funding. Na kusema ukweli mitaji iliyoanzisha mashirika na makampuni hayo ya umma ilikuwa inakopwa kutoka nje kwa sababu the business models was compelling. Tatizo ni failure ya management, ambayo mi nasema wazi wazi Mwalimu hawezi kukwepa lawama ya management lapses zilizotokea kwenye hayo mashirika ya umma. Mashirika kuendeshwa kisiasa zaidi halikuwa kosa la visheni ya kuwa na mashirika; tatizo lilikuwa ni too much human approach ya mwalimu. Na mwalimu alikubali kubeba lawama kwa failures kama hizo.

Tatizo baada ya Mwalimu kuondoka wengi tuliamini kuwa management lapses zilizofanyika wakati ule zingefanyiwa fixing. Kilichotokea ni kuwa si tu kwamba Management ziliendelea kuwa za kisiasa zaidi bali sasa na wizi ulianza kuwa sehemu muhimu ya management inayokubaliwa. Kisingizio? Tunaondoka kwenye ujamaa.

Tunachomlaumu mzee Mwinyi ni kujaribu kujiondoa kwenye lawama kuwa si yeye aliyeondoa Azimio la Arusha. Kimsingi mzee Mwinyi kakiri kuwa hilo bado anaamini bado ni Mwongozo bora. Ila Mzee Mwinyi hajui kuwa viongozi walikuwa wanawajibika kuweka mikakati halisi na inayotekelezeka ya kuhakikisha tunapata kile kilichomo kwenye AA. Hakuna anayeamini hapa kuwa Mzee Mwinyi pekeee angefanya maajabu ya kurudisha AA, lakini tunachosema ni kuwa hata kilichobakia, ambacho ilikuwa ni maadili ya uongozi (kwa upande wa Chama) yaliondolewa kimsingi. Hayakuwa sheria, lakini yalikuwa binding kwa maana kuwa wanachama wa chama kinachotawala wangeweza kuyatumia yale kuwawajibisha viongozi, siku ikifika.

Ikiwa Mzee Mwinyi bado anaamini kuwa AA lilikuwa na bado ni kitu bora, Je Ruksa ndo ilikuwa sera yake ya kuhakikisha taifa hili linapata kile kilichomo ndani ya AA? Kwa nini leo asiseme kuwa ruksa ilizaa viongozi Mamluki na wala rushwa waliotopea ambao sasa hawakuwa na uwezo wa kuwajibishwa na hata Chama chenyewe? Mzee mwinyi kwa nini asikubali tu kuwa ikiwa juhudi zetu za kuelekea kwenye AA zilikuwa hazijazaa matunda, basi yeye aliamua kufutilia mbali hizo juhudi bila kuweka kingine chochote kama mbadala?

OK ilishaonekana AA ni Dreamland. Haikuwa achievable. Sawa then what? Sijajibiwa kuwa ikiwa yale maadili ya uongozi hayakuwa na maana yoyote kwa nini kikakaa kikao kikubwa tu kuyafuta na bila kuweka kingine mahali pake?
 
Ngekewa, Pundamilia, Makoko, August n.k

Nadhani tatizo linalotokea hapa na ambalo inabidi tulikwepe au tusema wazi ni kuwa;

1. Nyerere anayo aliyofanikiwa na anayo aliyofeli
2. Mwinyi anayo aliyofanikiwa na anayo aliyofeli

Never mention Mkapa na Kikwete.

Kosa ni pale kumlaumu mwinyi pasi kusema ukweli na aliyofanikisha, na kosa pia kumlaumu Nyerere pasi kusema uzuri wake.

Sehemu walizofeli hawa wakuu hatusemi wao , tunasema tulishindwa hapa, hiyo inakuwa lugha ya kifamilia zaidi kama taifa ni moja.

Tumethibitishiwa na kuhakikishiwa mara nyingi kuwa AD lilikuwa ni wazo, wazo lile lilikuwa zuri, ulikuwa mwongozo, chombo cha kuleta ari, umoja na hamasa!

Tamko lile au wazo lile hata kama lilishindwa halimfanyi ,mtoa wazo kuwa mshindwa, wala halimlazimishi mpokea wazo kulazimishwa kulikubali wazo.

Ila wazo hili kama tunaona linapositive ideas why bother? kwa nini tusiseme Ok, it was good Idea let amend and move on with it!

Tukiendela na mchezo wa kumsema Mwinyi vibaya na Nyerere vibaya hatutakaa tujue , tuna matatizo gani, tulianguka wapi, na tuamke vipi!

Ukikosea ukasema mazuri ya Mwinyi basi unaweza ukashangaa watanzania asilimia 90 wanasema afadhali mwinyi kuliko Nyerere aliyefanya tusugue meno kwa mkaa! But even Nyerere that was a process, tena naweza kusema tungekaa zaidi pale tujifunze zaidi shida zilivyo, pengine viongozi leo wangekuwa na utu! we can never by any means kumlaumu mto wazo na mwenye nia nzuri na taifa! kushindwa ni alama tosha ya kutokuwa na watu wa kusaidia,

Mbio za kijiti hizi ,ni teamwork, kulaumiwa Mwinyi wakati JKN alikuwa yupo pembeni ni sawa na kusema JKN alitusaliti baadae! mbaya zaidi watu walilipiga chini waliokuwa wanafunzi wa JKN, Mkapa leo hatuwezi tukampachika jina ulikuwa mbaya kwa kukataa Azimio wakati kafundishwa kabisa na JKN! what went wrong? tukasema pia tusikosee na kufana azimio kama dini!

AD ni wazo, haukuwa mfumo, tatizo ni kuwa ngau JKN tulijua anaamini nini, akina marais wengine wote hawana wanachoamini, kama ni dini basi siasa ya nchi ytu ni ya kipagani.

However, still we can move on, kama Sheria na Katiba zitafuatwa vyema, still tumeona Katiba na sheria vinahitaji mabadiliko mengi tu.

AD kama anatokea leo mtu analifufua basi lipate nguvu ya kisheria, bila hivyo tutakuwa tunacheza

Enyi wana wa nchi hii, stop pointing fingers to JKN and Mwinyi, simameni kwa miguu yenu na kuamka leo!


Tunakubali kuwa wahusika wote ni binaadamu na ndio maana tunawatetea wahusika kwa yale wanayolaumiwa bila sababu za msingi. Ama kwahili tunalozungumza sasahivi nafikiri tuna haki kumtetea Mwinyi dhidi ya shutuma. Laiti ingekuwa thread inaelekea katika kujadili na kuangalia mifumo miwili hii basi tungekuwa tayari kuzungumzia mapungufu na faida za mifumo hii, lakini kulaumu kimoja na huku hakuna uhalali wala ushahidi wa kuonyesha ubora wa hicho kinachopambwa kunapelekea haki yetu ya kumtetea Mwinyi.

Mwinyi na Nyerere wana mafanikio na makosa yao kama binaadamu na tutakuwa tayari kumlaumu na kumpongeza yeyote kwa aliyoyatenda. Bahati mbaya ni kuwa mbali na ubinaadamu makosa ya viongozi yanawagusa wengi hivyo kulaumiwa isionekane kuwa nia jambo la ajabu lakini tuwe tukiwatendea haki.
 
Lakini ni kwa nini inapokuwa tunapojadili failures za Mwinyi wengine tunakuwa quick kusema kuwa OK failure za Mwinyi zilianzia kwa Mwalimu, does it mean kuwa Mwinyi kama kiongozi hawezi kusimama peke yake na kuwahukumiwa kwa aliyoyafanya au kutoyafanya? Siku zote apologists wa Mwinyi kwa nini wanakimbilia kwenye kichaka cha sera za Mwalimu?

Miaka kumi in Power Mwinyi couldn't salvage anything? Sasa na yeye anakimbilia kurusha Madongo kwa waliomtangulia na mfumo alioukuta!! KAMA KIONGOZI, UONGOZI WAKE KWENYE HILO ILIKUWA NINI?

Was Mwinyi so insignificant to matter? Because debaite about Mwinyi is easily sinking into his predecessor!!
 
Nyerere aliongoza nchi hii hadi Mwaka 1985, Lakini mpaka leo, alot of problems are still blamed on Nyerere policies, 25 years later with a third president!

Ni lazima tujenge utamaduni wa viongozi kukubali Makosa yao ili historia iwahukumu kwa waliyoyatenda na waliyoshindwa kutenda wao Kama viongozi. Rais wa Tanzania ana full constitutional powers za kufanya mambo mengi mno. Haiwezekani filures za Kila rais ziwe zinasababishwa tu na waliomtangulia.

This is a shame!
 
mtazamo wangu tu,

huyu mzee JKN alikuwa na mawazo ambayo wengi wetu mpaka leo tunashindwa kumwelewa alikuwa na theory ambazo ni misingi hasa ya utu, nadhani kama Nyerere angekuwa dictator basi hii nchi kwa sasa ingekuwa mbali sana kimaendeleo kutokana na filosofia zake,

Wakina Mwinyi walilianzisha hilo Azimio lao bila kuwa na upeo na tafakuli za maana, sasa wamefikia point kwa kuanza kutafunwa na Dhambi ileile ya kulikataa Azimio La Arusha na Nchi pamoja na Chama kimeshawashinda na kila mmoja anataka kunawa mikono kwamba yeye sio aliyetuleta hapa tulipo

hebu tujaribu kuangalia baadhi ya filosofia za Mwalimu

1. 'WATU WOTE NI SAWA'
"...Kama hukubali hilo, yaani kama unadhani watu wengine ni miungu wengine, malaika, wengine nusu-nyani, basi hukubali ujamaa. Ujamaa kwako hauna maana, kwa sababu ujamaa unahusu usawa wa watu: hapo ndipo unapoanza...Sisemi usawa wa urefu wala ufupi; kwa urefu namzidi Kawawa, sana tena. Sisemi maguvu, hata; nasema utu, watu, na ubinadamu wao. Kuna binadamu zaidi ya mwenziwe? Kama huliamini hilo, utakuwa mjamaa? Hilo la kwanza... mkaliulize-ulize, mlielewe maana yake. Na mtu anayepinga ujamaa naye ajiulize kama anapinga hilo nalo. Mtu mpingaji ujamaa aseme, 'Hilo nalo, usawa wa watu, napinga; kwamba binadamu wote hivi si sawa'" - Mwalimu Julius K. Nyerere

2. 'LAZIMA MTU AFANYE KAZI'
"...Binadamu hao unaotuona hapa, na hao waliosambaa dunia nzima wanaishi kwa kazi. Hawana namna nyingine ya kuishi. Wakiacha kufanya kazi watakufa; hawana namna nyingine; kuishi kwao, na kuendelea kuishi, lazima wafanye kazi...Lakini binadamu haishi kama farasi. Binadamu haridhiki kuishi kama farasi au punda; binadamu ana kitu anakiita maendeleo; lazima aendelee...Wakati mwingine ili kusudi maendeleo haya yaje wana shughuli za kupigana misasa akili, wanapanuana mawazo tu, nayo ni kazi...nendeni mkaulizane...kama kazi si kitu cha lazima, kama binadamu anaweza kujikalia tu hafanyi kazi, akaishi, na maendeleo yakaja bila kazi. Na huyo anayepinga ujamaa naye ajiulize kama hilo analipinga? Na hilo la kufanya kazi analipinga au kuna jingine analopinga?" - Julius K. Nyerere

3. 'HAKUNA MTU KUMNYONYA MTU'
"...Kama binadamu ni sawa, tunalikubali hilo...Pili tunasema kitu kazi ni jambo la lazima kwa kila mtu, hakuna aliyesamehewa kazi. Basi siwezi kukufanyia kazi. Kukufanyia kazi maana yake ni kwamba wewe unasamehewa kazi! Siwezi kukufanyia kazi. Wewe utafanya kazi, na mimi nitafanya. Sio mimi nifanye, wewe hufanyi; lazima ufanye kazi. Kwa hiyo wewe utafanya kazi, na mimi nitafanya kazi; kila mtu atafanya kazi. Yaani namna ya kulitamka hilo ni kwamba kunyonyana hakuna. Hakuna mtu kumnyonya mtu; sasa tena msingi wa kumnyonya unatoka wapi? Tumesema watu sawa; na mtu ili aishi hana budi afanye kazi, na kazi ndio msingi wa maendeleo. Sasa mwanachama... ajiulize kama anaweza kuwa mjamaa na huku ananyonya! Unamnyonya mkeo; mkeo anakwenda kufanya kazi wewe unakwenda kupiga chibuku; hivi kweli mjamaa wewe? Tunasema kazi jambo la lazima, lakini wewe hufanyi kazi, unamnyonya mkeo. Wewe mjamaa? Nasema na hilo mjiulize...Unaweza kuwa mjamaa na huku unanyonya? Na anayepinga ujamaa ajiulize hilo nalo analipinga, kwamba yeye anaona kunyonya ni sawa tu! Sawa yeye kunyonya mwingine au wengine kumnyonya yeye, huyu anayesema kunyonya ni sawa. Kama kunyonya ni sawa baba, sasa tuanze kunyonya, au mkuki kwa nguruwe?" - Julius K. Nyerere

4. 'VYOMBO MUHIMU VIMILIKIWE PAMOJA'
"...Kama watu ni sawa; binadamu wote ni sawa; kazi ni jambo la lazima kabisa; kunyonya ni haramu; la nne linafuata: Vyombo vyote vya lazima, vinavyohitajika kwa maisha ya binadamu kwa kufanyia kazi lazima vimilikiwe kwa jumla. Ardhi lazima imilikiwe kwa jumla maana tusipoimiliki ardhi kwa jumla tutamwachia Rashidi Kawawa na Sheikh Karume wao wawe ndio wenye ardhi, na ardhi ni kitu cha lazima kwa maisha, hebu tuone kwanza usawa utakuwaje. Itakuwa lazima twende kwa Rashidi na kwa Karume, 'tafadhali bwana nataka ardhi'. Umekwishamwita 'Bwana' huyu; usawa umekwisha. Lakini vilevile kama Sheikh Kawawa ana ardhi, na Sheikh Karume ana ardhi, hawa hawalazimiki kufanya kazi. Kwa nini wafanye kazi? Hawawezi kufanya kazi. Tumesema kazi ni kitu cha lazima kwa kila mtu, lakini hawa hawawezi kufanya kazi, watakaa tu wanatutoza kodi kwa ardhi yao. Ndiyo wanatunyonya hivyo tena. Mimi nafanya kazi; mimi nalima. Halafu Rashidi anasema, 'Ukishalima mahindi ukapata magunia matano, moja langu'. Ndio ananyonya hivyo. Anavunja kanuni ya usawa; anavunja kanuni ya kazi; anavunja kanuni ya kutonyonya. Kwa nini? Kwa sababu tumemruhusu amiliki yeye vitu ambavyo vinastahili viwe vya wote. Mtu ambaye yeye ana ardhi; umemkabidhi viwanda, ukishakuwa umemkabidhi majambo mengine haya, umemwongezea nguvu zake, yeye utu wake umeongezeka-ongezeka na wangu mimi umeupunguza-punguza. Kwa hiyo vitu vilivyo vya lazima kwa kila mtu, kama ardhi ambayo ni ya lazima kwa kila mtu, lazima vimilikiwe na wote. Sasa...mjiulize kama unaweza kuwa mjamaa kweli huku unajidai ardhi yangu? Na wanaopinga wanatakaje? Hao wanaosema ujamaa mbaya. 'Eti vitu vyote viwe vya ujumla'; wengine waongo, 'Eti wanasema hata wakina mama wawe wa jumla'. Tunasema ardhi, hatusemi kina mama, tunasema ardhi viwanda, madini: kwa nini mtu mmoja anakwenda kuvinyakua vikawa vyake hivi!" - Julius K. Nyerere

5. 'KUUNDA NCHI BILA MATABAKA'
"..Kama tunakubali kuwa watu wote ni sawa; na watu wote ni lazima wafanye kazi, mtu asimnyonye mtu; na mali, mali kubwa, sikusema shati langu liwe la Rashidi: misingi ya uchumi kama mabasi yale yanapita iwe kwamba tunasema mabasi yetu, asiweko mheshimiwa mmoja pale anasema 'Basi langu lile!' Basi lako! Yupo dereva mle anaendesha, anasema dereva wake! 'Dereva wangu' - dereva wako, wewe unaweza kuwa na dereva? Dereva anaweza kuwa dereva wa umma, sio dereva wako. Dereva ni sawa sawa na mwalimu; mwalimu wa umma, daktari wa umma, dereva wa umma. Huyu anakuwaje 'wako'? Hata askari siku moja utasema wako. Kama tunakubali watu wote ni sawa; watu wote lazima wafanye kazi, hakuna kunyonyana; mali,vitu vyote vile vya jumla lazima viwe vya umma; maana yake ndio kusema tunataka kuunda nchi ambayo haina tabaka: hakuna mabwana na watwana." - Julius K. Nyerere


asilimia kubwa ya aliyoyasema sasa tunayashuhudia mbele ya macho yetu na ndio maana watu walioliua Azimio wanatapatapa kujitoa kwenye lawama kuwa hawakuhusika na uvunjaji wa hilo Azimio la aArusha


Ubora wa kitu chochote unapatikana katika mafanikio ya kitu hicho, AD lilikuwa ni tangazo si application ya yanayozungumzwa ndani ya Tangazo hilo. Pengine Nyerere alihitajika kuwa filosofa tu sio filosofa na kiongozi wa kutekeleza filosofa yake. Baada ya kukaana nae na filosofa yake va AD kwa miaka karibu ishirini alishindwa kuitekeleza na kutowa faida iliyostahiki. Kama hakukuwa na haki sawa ya kugawana mapato, kulikuwa na matabaka ya walionacho na wasio nacho, kulikuwa na uchumi mbaya nchini tofauti na tulipopata uhuru, viongozi hawakuwa na maadili ( vitu vya msingi vinavyozungumziwa na AD) kuna kosa gani kuondowa mfumo huo na kujaribu mwengine? (kiasi gani umefanikiwa huo wa Mwinyi, tunayo haki ya kujadili)
Kwanini Tumlaumu Mwinyi binafsi kwa kuondowa mfumo ambao ulifeli? Hivyo katika akili zetu tunakubali kuwa Nyerere mwenyewe hana mkono kwa hili? Nyerere tunaemjuwa akae kimya kwa jambo asilolipenda? Mbona tuna mifano mingi aliingilia kati maamuzi wakati wa huyo Mwinyi? Hapana! AD liliondoshwa kwa vile kulihitajika kufanyika hayo,
Kama mambo yaliyokuwa ndani ya AD yanaweza kutusaidia kujinasua na hali tulionayo sasa basi na tuunde sera nyengine yenye uboresho na sio kulirejesha AD.
 
Was Mwinyi so insignificant to matter? Because debaite about Mwinyi is easily sinking into his predecessor!!

Pengine ime-hit the point hapo! Unafikiri Mwinyi aliingia madarakani akiwa na nguvu za kisiasa kuliko Nyerere? Kuwa mkweli na nafsi yako na ujiulize Rais gani allishawahi kutukanwa hadaharani na kaufyata? Umesahau kitendo alichotaka kufanya only kuzuiliwa na taasisi fulani nchini?

Tungemfanyia haki Mwinyi kwa kutombebesha msalaba wakati tukijuwa kuwa alichokifanya hakikuwa kitendo chake binafsi.
 
Kama mambo yaliyokuwa ndani ya AD yanaweza kutusaidia kujinasua na hali tulionayo sasa basi na tuunde sera nyengine yenye uboresho na sio kulirejesha AD.
Kitu kikubwa kilichoshindikana by that time ni NYERERE kutokuwa dictator kwa kiasi kile, yaani Nyerere angekuwa kama Hitler au Mussolin Tanzania ya leo Nadhani tungekuwa tunashindana na nchi za ulaya, maana katika hizo theory zake ilikuwa inatakiwa force, mathalani ile force iliyotumika kuanzisha vijiji vya ujamaa, japo watu walikufa na wengine kulalalmika lakini manufaa yake na malengo yake kwa asilimia kubwa yalifikiwa
 
kitu kikubwa kilichoshindikana by that time ni NYERERE kutokuwa dictator kwa kiasi kile, yaani Nyerere angekuwa kama Hitler au Mussolin Tanzania ya leo Nadhani tungekuwa tunashindana na nchi za ulaya, maana katika hizo theory zake ilikuwa inatakiwa force, mathalani ile force iliyotumika kuanzisha vijiji vya ujamaa, japo watu walikufa na wengine kulalalmika lakini manufaa yake na malengo yake kwa asilimia kubwa yalifikiwa
Hivi ni nani katufundisha lazima ya kuwa watu wafe ndio kuwe na maendeleo? are you guys thinking about development au revolution?

hamna maendeleo kwa namna ya udikteta maendeleo hutokana na changamoto za vichwa vingi, misingi imara ya kutoka serikalini kuleta maendeleo, na sera zenye kuhimasisha wananchi kujifunza kujitegemea. Sasa haya mambo yenu ya majembe sijui udikteta kwa kweli ni old school thinking.
 
kitu kikubwa kilichoshindikana by that time ni NYERERE kutokuwa dictator kwa kiasi kile, yaani Nyerere angekuwa kama Hitler au Mussolin Tanzania ya leo Nadhani tungekuwa tunashindana na nchi za ulaya, maana katika hizo theory zake ilikuwa inatakiwa force, mathalani ile force iliyotumika kuanzisha vijiji vya ujamaa, japo watu walikufa na wengine kulalalmika lakini manufaa yake na malengo yake kwa asilimia kubwa yalifikiwa


Uko sahihi kusema kuwa hakuwa dictator wa kiasi kile lakini kwa kiasi fulani alikuwa dictator kiasi cha kulazimisha vijiji vya Ujamaa. Hata hivyo hao madikteta alikokopia hizo sera walishindwa mbeleni hivyo pengine hiko kinachohubiriwa kina destiny ya kufeli baadae.
 
Waberoya,

Hii mada kama sikosei ilikuwa inazungumzia kauli ya Mzee Mwinyi kuwa hakuliua azimio la Arusha bali lilijiua lenyewe au lilikuwa limeshakufa before. Wengi mkakubaliana. Wengine tunakataa na tunaona hiyo kama ni ujanja ujanja wa kuhamisha hoja na kukwepa kuwajibika kwa makosa waliyo yatenda. Naona umeshaingia kwenye pipa hilo sasa unahamishia hukumu kwa Nyerere ambayo nafikiri inaakisi tofauti yako ya kibinafsi na Mwalimu.

Ikiwa hoja ni kuuawa kwa azimio la Arusha na the aftermath, ni nani hasa alihusi? Basi nadhani hayo niliyochukua hapo juu yako nje. Azimio lilikuwepo na wengi hapa wameshasema lilikuwa roadmap. Mlio upande wa mzee mwinyi kujiondoa kuliua azimio la Arusha mnasema after all azimio lilikuwa failure kwa hivyo alichofanya mzee mwinyi ni kuliachia lijifie lenyewe. Wengine tunasema siyo hivyo kamwe. Azimio lilikuwepo na lilikuwa bado linatishia kuwang'ata ndo maana waka-formalize mambo kupitia azimio la Zanzibar. Wengine mnasema AA haikuwa sheria kwa hiyo haikuwa binding na hiyo ndo failure yake.

Sasa nijaribu kujibu baadhi ya hizo hoja. Kusema kuwa azimio tayari lilikuwa ni failure ni kutoelewa AA has ilikuwa ni nini. Waliotusaidia wameshasema hilo halikuwa sheria lilikuwa ni vision, ni mahali tunapotaka kwenda. Kuna sheria nyingi zilitungwa na jitihada nyingi zilifanyika. Mfano ni kuanzishwa mlolongo wa mashirika ya umma; Yameshatajwa hapa. Zilianzishwa tume za bei, Mali zilitaifishwa, Siasa ni kilimo, Universal Primary Education (UPE) - Tanzania iliapata kiwango cha juu cha literacy kipindi hicho, n.k. Hizi zote hazikuja kwa bahati mbaya, ilikuwa ni juhudi zilizokuwa na lengo moja la ku-achieve kile kilichokuwemo kwenye Azimio la Arusha (AA).

Mashirika yote yaliyoanzishwa, yalikuwa na business models ambazo zilikuwa sound na zina-atract funding. Na kusema ukweli mitaji iliyoanzisha mashirika na makampuni hayo ya umma ilikuwa inakopwa kutoka nje kwa sababu the business models was compelling. Tatizo ni failure ya management, ambayo mi nasema wazi wazi Mwalimu hawezi kukwepa lawama ya management lapses zilizotokea kwenye hayo mashirika ya umma. Mashirika kuendeshwa kisiasa zaidi halikuwa kosa la visheni ya kuwa na mashirika; tatizo lilikuwa ni too much human approach ya mwalimu. Na mwalimu alikubali kubeba lawama kwa failures kama hizo.

Tatizo baada ya Mwalimu kuondoka wengi tuliamini kuwa management lapses zilizofanyika wakati ule zingefanyiwa fixing. Kilichotokea ni kuwa si tu kwamba Management ziliendelea kuwa za kisiasa zaidi bali sasa na wizi ulianza kuwa sehemu muhimu ya management inayokubaliwa. Kisingizio? Tunaondoka kwenye ujamaa.

Tunachomlaumu mzee Mwinyi ni kujaribu kujiondoa kwenye lawama kuwa si yeye aliyeondoa Azimio la Arusha. Kimsingi mzee Mwinyi kakiri kuwa hilo bado anaamini bado ni Mwongozo bora. Ila Mzee Mwinyi hajui kuwa viongozi walikuwa wanawajibika kuweka mikakati halisi na inayotekelezeka ya kuhakikisha tunapata kile kilichomo kwenye AA. Hakuna anayeamini hapa kuwa Mzee Mwinyi pekeee angefanya maajabu ya kurudisha AA, lakini tunachosema ni kuwa hata kilichobakia, ambacho ilikuwa ni maadili ya uongozi (kwa upande wa Chama) yaliondolewa kimsingi. Hayakuwa sheria, lakini yalikuwa binding kwa maana kuwa wanachama wa chama kinachotawala wangeweza kuyatumia yale kuwawajibisha viongozi, siku ikifika.

Ikiwa Mzee Mwinyi bado anaamini kuwa AA lilikuwa na bado ni kitu bora, Je Ruksa ndo ilikuwa sera yake ya kuhakikisha taifa hili linapata kile kilichomo ndani ya AA? Kwa nini leo asiseme kuwa ruksa ilizaa viongozi Mamluki na wala rushwa waliotopea ambao sasa hawakuwa na uwezo wa kuwajibishwa na hata Chama chenyewe? Mzee mwinyi kwa nini asikubali tu kuwa ikiwa juhudi zetu za kuelekea kwenye AA zilikuwa hazijazaa matunda, basi yeye aliamua kufutilia mbali hizo juhudi bila kuweka kingine chochote kama mbadala?

OK ilishaonekana AA ni Dreamland. Haikuwa achievable. Sawa then what? Sijajibiwa kuwa ikiwa yale maadili ya uongozi hayakuwa na maana yoyote kwa nini kikakaa kikao kikubwa tu kuyafuta na bila kuweka kingine mahali pake?


Asante umesema kuwa umesoma post za nyuma, nikukumbushe kuwa AD lilikuwa ni wazo na lilitakiwa ushawishi na leo hii bado linahitajika ushawishi sana tu. Kitu kikubwa ni kuwa hakuna sehemu Mwinyi aliyokiri kuwa alishawishika kuwa AD is the only best na kuwa aliliamini, kusifia kitu siyo kuabudu kitu.

JE leo kuna mtu anayeweza ku-proof/hakikisha kuwa Mwinyi kabla ya kuwa rais na wakati anakuwa rais , alishawishika kwa asilimia ngapi kuwa mfuasi wa AD ?

Kuna mkataba au kipimo chochote kilichoonyesha kuwa Mwinyi alikuwa muumini wa AD tangu awali?

Wakati Mwinyi anaapa kututumikia aliapa kulilinda Azimio? au Katiba?

Sasa ikiwa pengine mtu tangua anaichukua nchi haamini wala hakushawishika na AD why today we poor Tanzanians tumuhukumu kuwa aliliua??

Previous posts nimesema, leo hii tukisema tulianzishe, tulimodify, tulitafutie nguvu ya kisheria na kikatiba! kitu hicho hakikufanyika!
 
Lakini ni kwa nini inapokuwa tunapojadili failures za Mwinyi wengine tunakuwa quick kusema kuwa OK failure za Mwinyi zilianzia kwa Mwalimu, does it mean kuwa Mwinyi kama kiongozi hawezi kusimama peke yake na kuwahukumiwa kwa aliyoyafanya au kutoyafanya? Siku zote apologists wa Mwinyi kwa nini wanakimbilia kwenye kichaka cha sera za Mwalimu? Miaka kumi in Power Mwinyi couldn't salvage anything? Sasa na yeye anakimbilia kurusha Madongo kwa waliomtangulia na mfumo alioukuta!! KAMA KIONGOZI, UONGOZI WAKE KWENYE HILO ILIKUWA NINI?

Was Mwinyi so insignificant to matter? Because debaite about Mwinyi is easily sinking into his predecessor!!

Nyerere aliongoza nchi hii hadi Mwaka 1985, Lakini mpaka leo, alot of problems are still blamed on Nyerere policies, 25 years later with a third president! Ni lazima tujenge utamaduni wa viongozi kukubali Makosa yao ili historia iwahukumu kwa waliyoyatenda na waliyoshindwa kutenda wao Kama viongozi. Rais wa Tanzania ana full constitutional powers za kufanya mambo mengi mno. Haiwezekani filures za Kila rais ziwe zinasababishwa tu na waliomtangulia. This is a shame!

You are very right Kipima Pembe;

Kuna issue ambazo inabidi kuwa waangalifu are we fault finders or are we rectifiers

Pia kuna mitizamo ya generation na nyaakti.

Ndiyo maana nashauri unaposema mabaya ya Mwinyi, weka mazuri yake pia
Unaposema mabaya ya Nyerere weka na mazuri yake pia

Failure to do that will always creates groups, maana hawa watu sio mambuzi, kila mtu ana uhuru wa kufikiri na kuamua.

Wapenzi wengi wa JKN wamekuwa wakumrudikia shutuma Mwinyi kana kwama hakuna jema alilofanya lolote lile, hapo ndio tatizo linapoanzia!

Tofauti ya hawa wawili ni kuwa mmoja anaonekana mdogo sana kwa mwenzake, surely, ukija kwenye dhana na uwezo wa JKN katika ushawishi, vision na misimamo, Mwinyi kaachwa mbali, na kwa hili inasababisha wapenzi wa JKN kumrushia makombora , lakini naona story haijaishia hapo wengine wote waliofuatia hakuna aliyeweza kuvaa na kutoka na theores zake ni JKN tu.

Ndiyo maana unaona kama vile JKN anaishi hata leo hii!

However, trukisema tufanye performance ya nani kafanya nini kilichoonekana na kukubaliwa na watu wengi, hasa baada ya zama zile za shida, basi watu watam-rank Miwnyi kwa juu sana.

Ndiyo maana nasema hwa viongozi tuwasome na kujua madhaifu na nguvu zao.

we still have lots to learn from Mwinyi , though I am not his fan!
 
- Kuzungumzia kifo cha Azimio bila kutaja faida zake kwa hili taifa ni kufukuza upepo, so far zimetajwa hasara nyingi za Azimio kuliko faida, maana yake ni moja kwamba Azimio halikuwa effective at all, sasa alaumiwe nani aliyelileta Mwalimu, au aliyeliua Mwinyi?

- Kwangu it does not matter, cha muhimu ni reconciliation na tusonge mbele, Azimio halitakuja kurudi tena hiyo ni fact, kulumbana kuhusu aliyelileta au aliyeliua ni waste of time, ni muhimu kujadili effective zake kwa taifa lakini in the process ya ku-move forward sio kutafutana uchawi.

- Bado ninasisistiza kwamba taifa linatakiwa kuongozwa na sheria, sio maa-Azimo flani hivi, haya maazimio ndiyo yamechangia sana kuturudisha nyuma katika utawala wa kuheshimu sheria, tujali sheria kwanza ndio tutasonga mbele.

Respect.


FMEs!
 
Mjadala ni mzuri
Hata hivyo nina maswali kadhaa kama ilivyo ada yetu hapa JF kwenye mijadala mototo....However,i don't know about many of us,mimi huwa nina tabia ya kuupitia mjadala wote kabla sijaposti ama kutoa maoni/mchango wangu kwenye mada husika....Na kila nilipokuwa nikipitia page after page,maswali ambayo ambayo yalikuwa yakiibuka kichwani mwangu na ambayo nilitaka kuwauliza baadhi ya members yamekuwa yakijibiwa,ila kuna ambayo bado...


Ndugu Waberoya;

Umetoa msisitizo kuwa AD liingizwe kwenye sheria na wengi wanaonekana kukubaliana na wewe.Hata hivyo naomba kusahihishwa,"AD haikuwa mojawapo ya sources za sheria za nchi?" Nasema hivyo kwasababu najiuliza kama kweli AD lilikuwa haliwabani viongozi mafisadi then AZ lilikuwa la nini? Je AZ halikuwa foundation ya kubadili baadhi ya sheria zilizowabana viongozi kujilimbikizai mali?ie sheria ya maadili ya uongozi? Ninashangazwa sana pale unaposema kuwa warithi wa mwalimu ie Mwinyi na genge lake hawakuwa wasanii,either walifanya kwa makusudi ama bahati mbaya,wao tofauti na mwalimu ni usanii,na utapeli dhidi ya wananchi period!


Ukisoma kwa makini hotuba ya Rais mstaafu Mh Alhaji Ali Hassan Mwinyi kwa wazee wa Dar na Taifa kwa ujumla(wazee wa ccm) ilikuwa ni hotuba ya kisanii na ya kinafiki! Ya madai kwamba ili twende na wakati basi viongozi ni Rhuksa kujilimbikia mali,huku akitumia mabadiliko ya vitu kama kima cha chini cha mishahara,ambapo kulikuwa na takwimu zilizowekwa kuhusiana na kujilimbikizia mali kinyume na kazi unayofanya,wao walichofanya ni kuiondoa hiyo cap moja kwa moja na wala si kui analyze na kuona kama ni shifting ifike wapi,yani ni kiasi gani kina constitute kujilimbikizia mali,hakuna mipaka ya tafsiri ya "Kujilimbikizia mali" na pia hakuna tofauti kati ya mali anayoipata kiongozi na mali anayoipata mwananchi wa kawaida,binafsi naamini kama unataka mali basi usijishughulishe na uongozi wakati wa kutafuta mali hiyo kwasababu ni lazima utumie ofisi ya umma kufanya hivyo na migongano ya kimaslahi inakuwepo!Hata hivyo ukitaka kujua ni usanii,kwenye hotuba yake hiyo alisema ni situation mbili tu zitakazowaruhusu viongozi wawe na nyumba za kupangishia;moja ni kama wamehamishwa kikazi kwenda mkoa mwingine ama kama kuna ulazima wa kupangisha baadhi ya vyumba ili kuwafanikisha kwenye ulipaji wa deni kama ulichukua mkopo,lakini kiukweli si ni mtoto wake amerithi nyumba za kupanga?mtoto wake naye si kiongozi?na kama Jasusi anavyosema kuwa alirithi kutoka kwa baba yake?je yeye mwenyewe kama si unafiki mbona alifanya tofauti na mwalimu?Ukipata mali ukiwa kiongozi ni lazima usema umepata vipi!

Je mwalimu alishindwa kuwa na apartments za kupangishia watu na mali lukuki?Kiukweli viongozi hawana haja ya kujilimbikiza mali kutokana na nature ya kazi zao,na kama wakifanya hivyo na tiafa likapata maendeleo,bado wataenziwa na hawatakuwa na shida,shida inaletwa na ubinfasi na kutokujali kwa viongozi mafisadi kwasababu system nzima ikiwa corrupt basi hakuna heshima kwenye uongozi kama usipojilimbikizia mali.


Kwa kifupi naamini AD lilikuwa kikwazo kwa mafisadi na ndio maana wakalikalia kikao huko Zanzibar....Hivyo Myinyi anapoibuka sasa na kusema kuwa hakuliuwa AD,nina amini kuwa anazeeka vibaya,kwasababu nashangazwa kwanini unafiki wake haumuumbui!Kama amesahau kwasababu ya uzee,then na wasaidizi wake nao wanamsaidia kusahau,huku na wao wakisahau kuwa Tanzania ya sasa ni ya tofauti kwa kiasi kikubwa.

Tulipokwama:

Tulipokwama sisi ni kutolenga kwenye solution...Na hivyo labda swali langu la pili linalokwenda kwa Mag3 litakuwa mojawapo ya changamoto ya ku analyse wapi na kwanini tumekwama....


Ndugu Mag3; Kama ilivyo kwa Ndg Jasusi,ulikuwepo Mnazi Mmoja mnamo mwaka 1967,kwanza awali ya yote "shikamoo Mzee" Lol! Ukweli heshma ya JF iko juu! Na mara nyingi nimekuwa nikiona JF kama licha ya ukweli kwamba ni kioo cha jamii yetu,pia ni kisima cha hazina ya fikra za kimapinduzi,pengine hata hadhi ya kama Nationa Archives....Mkuu pamoja na wengineo kama Rev Kishoka,MKJJ,Abdulhalim,Sikonge,Jasusi nk,maoni yako ni mazito,specifically kwenu waumini wa AD kama nilivyo mimi.....Tofauti yetu however ni kwamba wakati AD likitolewa mwaka 1967, kulikuwa na mwamko wa kisiasa kwa vijana wakati huo,hata hivyo kama sijakosea pia umeimply kuwa you was some sort of a rebel coz hukutaka kushiriki,i believe you had a cause....Ulichofanya kwa wakati huo,yani kwenda nje ya nchi na kutafuta maisha ndicho wanachofanya vijana wengi hata sasa,yani kuanzia huo mwaka 1967 hadi sasa,vijana wengi wanafanya yale yale,kukimbia nchi kusaka life,je ni zipi hasa sababu zilizokufanya ukazira?


Tunajuwa kuwa AD lilianzishwa mara baada ya viongozi kuanza kujilimbikizia mali na wananchi kuanza kugawanyika kimatabaka nk,na Mag3 inavyyonekana ulifurahishwa na idea nzima ya AD,je ni kwanini hukutaka kushiriki?Ni kipi kilikukatisha tamaa?Certainly wananchi wa sasa ama kizazi chetu,binafsi bado nawalaumu viongozi wetu kwasababu wanachofanya ni kinyume cha mapenzi ya wananchi...Tofauti na wakati wenu ambapo inaonekana wananchi walikubaliana na AD moja kwa moja,ila still kuna vijana kama nyie mliokuwa rebels licha ya kuona kuwa idea inafaa,Je ni kwasababu umuhimu wa AD haukuonekana kwa wakati ule kama ilivyo sasa?


Nilikuwa bwana mdogo kipindi cha mwinyi especially miaka ya tisini baada ya AZ na kwa ukweli licha uelewa wangu ndogo bado niliona usanii wa wazi wa viongozi wetu,na nilikuwa nikishangazwa licha ya kuwa bwana mdogo kuwa ni kwanini viongozi hao bado wanachaguliwa,kipindi hicho pia mwamko ulikuwepo na Mrema ndipo alipokuja....Ni ukweli hata mwalimu mwenyewe aliuona usanii na ikampelekea kuandika kitabu hususan Uongozi wetu na hatma ya Tanzania.


Hivyo wazee wetu Jasusi na Mag3 ambao mlikuwepo mwaka 1967,na mnaonekana kukubaliana na AD,lakini pia mkionekana kuwa mlikatishhwa tamaa na mambo flani flani na pengine kuwa sababu ya kutokushiriki moja kwa moja kwenye utekelezaji wa azimio ambalo lilionekana kama mkombozi wa watanzania dhidi ya unyonyaji na ufisadi...Nina amini pia sababu zenu zinaweza kuwa tofauti na zetu sisi vijana wa kizazi hiki kwasabau AD lilianzishwa mara baada ya viongozi kuanza kujilimbikia mali na hivyo matabaka kuanza na chuki miongoni mwa wananchi,ni wazi basi AD lilikuwa kipenzi cha wananchi na hatua ya kutia moyo na hivyo mapenzi dhidi ya viongozi wetu yakazidi na mwamko wa kisiasa ukawepo,tofauti na sasa ambapo hata viongozi hawajali kabisa,na ambapo ni wazi kuwa vita ni kati ya maslahi ya watawala dhidi ya maslahi ya wananchi ambayo ana constitute maslahi ya Taifa.


Wazee wetu; Pia kama mnayozumgumza yanatoka moyoni,basi sifa moja kubwa mliyonayo ni kutokuwa wanafiki,kwasababu licha ya wengi kutoshiriki kwenye utekelezaji wa AD,bado walioshiriki ndio waloliuwa,hence unafiki kwasababu bado wanadhani sisi "Hamnazo' Nitakalomlaumu mwalimu ni kama kweli hakutaka ushauri,lakini kama wanayoyafanya viongozi hawa na wengineo waliokuwa washauri na wanafunzi ndiyo haya,bado najiuliza ni ushauri gani huo walimpa mwalimu,na certainly kama haya wanayoyafanya ndiyo walimshauri mwalimu,then hata kama ingekuwa mimi ningeitwa "haambiliki!" Honestly,kwa mtaji huu utasikiliza ushauri huu si ufisadi?ninaamini kabisa tabaka la viongozi waliomrithi mwalimu ndilo lilitulet down watanzania...Na hapo ndipo nakuja kwenye pointi ya tatu....

Reverand Kishoka:

Hapo ndipo pointi bado inaendelea kuhusiana na wapi tumekwama,tumekuwa tukitofautiana wengi wetu humu ndani,wengine wakisema kwa sababu miafrika ndivyo ilivyo basi vongozi hawana haja ya kulaumiwa,mkuu Rev. Mimi msimamo wangu bado uko pale pale,na ninaona kuwa tunakubaliana kwa kiasi kikubwa kwasababu wengi wetu sasa wana conclude kuwa tatizo ni uongozi,licha ya kwamba bado kuna wanaosema na wananchi pia.


Tukiangalia kwa makini,mafanikio ya AD ndio exactly what its letting the declaration itself down,yani umoja na udugu uliojikita kwenye misigi ya "Amani" matunda hayo ni ya AD,na matunda hayo ndiyo yametunyima uthubutu wa kujaribu mabadilko kwa hofu ya kukosekana kwa amani inayoletwa na umoja na udugu huo....Ukiangalia kiundani,mafanikio ndio weaknesses,viongozi wanajuwa kuwa mafaniio hayo ndiyo weakness na wakati sisi tunajuwa ndio mafanikio period,kwa hivyo kama mwenye kuona mafanikio hayo ndio weakness na akaamuma kutumia weaknesses hizo ambazo machoni mwa wananchi zinaonekana kama mafanikio,ndio hapo mkorogo wa kisanii unapoanza.


Ni lazima tukae chini tutafakari kweli tuona ni wapi tumekwama,na tukiangalia kwa makini tutaona ni kwenye uongozi,tutizame nini haswa maana ya umoja na udugu kwenye maslahi ya Taifa,wananchi tuliassume kuwa usawa uko hata kwenye nia,yani wote tuna nia sawa,na bado tunaamini kuwa nia yetu ni sawa na nia za viongozi,hilo ukweli ni kwamba lilifutwa na azimio la Zanzibar,sasa hivi wananchi na hadi waelewe kuwa ni maslahi yao vs ya viongozi.

Mzee Mwinyi alisema kuwa ni muhimu kwenda na wakati,kwamba tusije tuka "pelea" mara baada ya "kupwa kwa bahari" Hata hivyo ukweli ni kwamba wananchi ndio samaki walioachwa wakapelea maana azimio la Zanzibar linahusu maslahi ya viongozi,na hivyo hapo vita ndipo ilianza rasmi,ila wananchi kwa kutapeliwa hawakujua kuwa huo ndio mwanzo wa ule umoja unaoletwa na haki na usawa kupotea,kifikra wananchi bado wako huko,vitendo tofauti vinaanza kuwaonyesha mambo ya tofauti,hakuna tena cha Taifa,ni "mimi mimi mimi!" "Me myself and i" hakuna aliyeko kwenye ofisi ya umma kwa maslahi ya umma,sasa ukitizama kwa undani solution pekee inaweza kuwa mapinduzi,kama inavyoonekana pia kuwa baadhi yetu tunaanza kukubaliana na hilo,hivyo binafsi siwalaumu wananchi kwa kiasi kikubwa na pia siamini kuwa miafrika ndivyo ilivyo!Naamini kuwa viongozi wetu wanautumia udhaifu wa kisiasa,kiuchumi na hata kijamii,dhaifu ambazo causations zake zinaenda all the way back to maybe slavery....


Hitimisho langu kwasasa;

Wakati nikisubiri majibu kutoka kwa members niliowauliza maswali,bado siamini kama wanavyosema members wengine sijui mazuri ya mwinyi whatsoever....Najiuliza ni yapi hayo?maana once youre wrong from the beggining with the basics,basi always you're all the way wrong.


Mara zote usanii na utapeli huwa na dalili za mazuri,unaweza kudhani ama kuona kuwa everthing is right na still ukawa absolutely wrong!Kuchukua a wrong way haina maana hakuna dalili kwamba uko right,ama kwamba hautafika karibu na destination,tatizo utakalogundua however,ni kuona wazi kuwa uko in a wrong destination,yanayoonekana kwamba ni mazuri yataonekana njiani,lakini mkishafikaka ndio mtajuwa kuwa mazuri hayo yaliwalenga wale waliokuwa wakitaka kwa makusudi tufike kwene wrong destionation,huku wakitudanganya kuwa we're still in a right way,na tukiangalia around tunaona kama vile tuko in a right way ama kwamba mwenye kutu mislead alikuwa na nia nzuri,(ie Mwinyi)hata hivyo nia nzuri kwa wananchi haiwezi kuwa na matokeo tofauti na maslahi ya wananchi wenyewe na bado ikawa nia nzuri kwa wananchi,na kwahiyo udugu,amani na umoja vinatulazimisha tuamini kuwa nia ya viongozi hao ni nzuri na wenye kusema tofauti hawataki umoja wetu,ni lazima tujiulize huo umoja tunaouzungumzia ni wa aina gani?

Mbona wamarekani wana umoja lakini hawana huo udugu lakini bado wana maendeleo?Tukishaondoa ule udugu wa kuoneana haya mbele za sheria za nchi,hatutafika,umoja wetu ni lazima ujikite zaidi kwenye malengo ya kitaifa na si individual basis,ni heri nijenge mazingira bora ya kizazi kijacho kuliko kuwa na umoja na fisadi!


Tabaka tulilokuwa tukilipiga vita kabla hata ya uhuru ndilo tabaka ambalo ndugu zetu kabisa wameamua kulichukua against us,hili linapelekea vita sasa kuwa ya tofauti,ni kama vita ya terrorisma,ambapo wamo miongoni mwetu,tofauti iliyoko sasa ni kwamba wanajilinda kwa kutumia system na dola the same way tabaka la kikoloni lilivyofanya.


Tujiulize mwaswali ya msingi as this mjadala goes on......What is it gonna take kumwondoa mkoloni mweusi?How do we fight this war?Je kwanini wale wanaoonekana kuwa ndiyo walikuwa na nia nzuri na taifa kama kina Mag3 na Jasusi hawakupata nafasi ya kushiriki kwenye ujenzi wa taifa,je nini haswa kiliwakwamisha...?


Wote tunakubali pia kuwa miiko ya viongozi ni muhimu iwepo,tatizo ambalondilo lililopelekea yaliyotokea mwaka 1967,swali ni kwamba sasa ni kipi tutakachofanya cha tofauti kama tukiirudisha miiko hiyo?


Binafsi i believe tunahitaji uongozi mpya kabisa ili kuweza just kuanza kufikiri wapi pa kuanzia....Waberoya yeye anasema kuwa AD liingizwe kwenye sheria za nchi,jambo ambalo nimejaribu kulitolea ufafanuzi based on ma knowledge on it,naweza kuwa wrong na hivyo ninasubiri maoni ya members wengine,hata hivyo kama sikosei kuna pahala Sikonge alisema kuwa sheria ya kunyonga haizuui watu kuuwa!

Hilo halina maana kuwa tusiweke sheria kali dihidi ya mafisadi,ila ni kwamba hata sheria zilizopo zinatafutiwa namna ya kubadilishwa,kusema tusiwalaumu viongozi ni unafiki uliopindukia!

Kupunguza mazingira yanayochangia mauwaji ni bora kama vile sheria hizo dhdi ya wauwaji,kama alivyosema mzee Mkandara,kwamba badala ya kujenga mazingira ya kumaliza uzalianaji wa mbu,sisi tunajikita kwenye uzalishaji wa neti, biashara zaidi ya utu?hayo ndiyo manufaa ya kujikita kwenye ubepari bila tafiti kwasababu viongozi wetu wako hapo kwa maslahi binafsi,sasa hao wenye kutengeneza pesa kutokana na biashara ya uzalishaji neti watataka mbu ziishe kweli?Kama ni kiongozi mwenye kiwanda hicho atataka mazingira yasafishwe na kuboreshwa kwa manufaa ya nani?ubepari si ndio huo wa kutengeneza magonjwa ili mtengeneza na dawa za kuutibu simply kwasababu ya "Uzalishaji"?


Rather "utekelezaji" wa sheria ndio muhimu,kama viongozi wako busy kutengeneza sheria zinazohalalisha ufisadi,then hatutaona mabadiliko,unless tuwapate viongozi wapya wenye nia ya kweli na utawala wa kisheria unaozingatia miiko ya uongozi,na kuwa na sheria ambazo ziko juu na si wengine kuwa juu ya sheria hizo,haijalishi sheria zinasema nini kama viongozi ama watu flani flani wako juu ya sheria hizo!


Kwa kumalizia ndugu waberoya,kama nilivyosema hapo nyuma,sheria zina sources zake,nikupe mfano wa Taifa la marekani ambazo primary sources zake ni katiba yenyewe ya marekani,federal satatutes and treaties,federal administrative law,federal case law,state constitution,state statutes,local ordinances,state case law nk.


Kimsingi sheria za maadili ya viongozi ndizo haswa zilitokea kwenye miiko ya uongozi,kimsingi sheria hizo za kupingana na maadili ya uongozi,ziliingizwa na mafuriko ya utandawazi kwa kupitia usanii wa azimio la Zanzibar.


Kama viongozi wetu walifanya usanii huu kwa makudi basi Mungu lazima atawapatiliza.Time will tell!Kama wasipojirudi na kushirikiana na wazalendo wa kweli mwisho wao unaweza usiwe mzuri maana theres no way forwrd before fixing di shyt first and foremost,we're stuck,ni heri kama tungekuwa tuko in a right direction,basi tungeweza kuignore and deal with it in a different situation,tatizo we're stuck kwasababu we're absolutely in a wrong way...Usanii certainly una kikomo na wakati ndo huu.....Theres no way forward without a change of direction.,or atleast go back to basics and build upon it!AD lirudi lfanyiwe marekebisho and "F" AZ !
 
Post hii sijaielewa mkuu, unasema nini? kuhusu hayo makampuni? na unahusianisha na nini? na AD,Mwinyi n.k sijakupata kabisa, hayo makampuni ni ya miaka gani? baada ya Mwinyi au kabla? na kwa nini ni makapuni ya watu binafsi?, yaani umeniacha lengo la post yako sijalielewa samahani kwa usumbufu
Samahani Wareboya, nilichotaka kusema kama kichocheo cha maendeleo ni kwa mtu Binafsi kushughulika na Biashara mbona biashara za hawa jamaa zile feli au haziendelei kwa spidi ambayo tungetajiria na kuongeza tija.
yaani KJ motors, JV group , Somaia Group nk nk wengine walikuwa na mashamba ya Mkonge kilosa, Mkumbara nk nk.
 
Mtanisamehe naomba nionge kitu binafsi kwanza kwa tabasamu na furaha kubwa kabla ya kujibu hoja hii ya kauli ya Mwinyi.

The evolution and progression of one JMushi is excellent. Mwanangu nakumbuka miaka miwili iliyopita nilikuwa nakupiga makonzi, ukapiga hatua nikakuambia tutakupa kyamba na mke, sasa nasema tukupe Uwaziri Mkuu! Bravo JMushi, I wish watu wangene wangekuwa objective kama wewe na kukua hasa Waandishi wa habari wa Tanzania ambao bado ni mambo mbofumbofu!

Nikirudi kwenye hoja naomba niegemee kwenye kitu nilichokitamka awali ambacho ni uongozi.

Hapa nitakuwa namjibu Ngekewa na watetezi wa Mwinyi.

Mzee Mwinyi alipoingia madarakani, nchi ilikuwa katika hali mbaya ya kiuchumi. Moja ya sababu za Mweinyi kupewa nafasi ya kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni kile kilichotokea Zanzibar kiuchumi baada ya yeye kumrithi Jumbe.

Ngekewa umetamka kwa maneno machache mfarakano uliokuwapo kati ya Mwinyi na Nyerere ambao ulileta mvutano wa nani kashika dola na nguvu za chama.

Alichotakiwa kukifanya Mwinyi na hata Mkapa alipokuja na sasa Kikwete si kubadilisha sera ambazo ni za chama kile kile, bali ni kuimarisha sera kwa kuongeza ufanisi na kuongeza uwajibikaji.

Laiti Mwinyi angekuja na kwa kuanza kupangua safu ya uongozi ya watu waliokuwa wakionekana wazi wamedoda, iwe ni uwaziri, ukatibu mkuu, wakurugenzi na mameneja wakuu na akaanza kuwa mfuatiliaji wa karibu wa uchapa kazi kama alivyokuwa Sokoine, basi hata hii sera ya kurekebisha Uchumi chini ya Mwinyi ingefanikiwa.

Kama tatizo lilikuwa ni mishahara midogo, kwa nini hakubadilisha mfumo wa mishahara na kutoa mishahara mipya na yenye uwezo wa kukimu kmaisha ya watu kwa kila mtu?

Hivyo kitendo cha yeye kama Mwenyekiti wa Chama kupitisha Azimio la Zanzibar ambalo lilivua uwajibikaji na miiko ya maadili kwa viongozi kwa kisingizio Viongozi wanahitaji vipato vinavyostahili ni jambo la kijinga na kinafiki. Matokeo ya Azimio hilo yametuonyesha kuwa Halmashauri ya CCM na Uongozi wa CCM ukiwa chini ya Mwinyi, ulikuwa ni safu ya Viongozi wenye tamaa ya ubepari na ndumilakuwili wenye kutaka yote.

Kwa nini hawakuwa tayari kuachana na siasa au madaraka wakawa Wafanyabiashara tujue moja? Kwa nini walitaka wawe Wafanyabiashara, wakihodhi mali na hapo hapo wawe viongozi wa Kisiasa na kutumia Ushawishi na Nguvu za Kidola za madaraka yao kuendelea kuneemeka?

Leo Kapuya ni Waziri wa Ulinzi, kisha Kazi, kisha Biashara na ana Migodi. siku akipelekwa kuwa Waziri wa Madini itkuwaje?

Leo Karamagi ni Waziri wa Biashara, Waziri wa Madini, kampuni kubwa ya uchukuzi Tanzania ni mali yake, je anawezaje kufanya kazi za kulitumikia Taofa kwa haki na uadilifu huku anamiliki hisa kubwa za kampuni si kubwa bali pekee ya uchukuzi na ukaguzi wa mizigo Bandarini?

Leo Daniel Yona waziri wa Uchumi na kisha Waziri wa Madini akishirikiana na Mkapa Rais wa nchi, wanajiuzia mgodi wa makaa ya mawe kwa bei ya chini kabisa na ya kutupa. Hakuna anayehoji kwanza wametoa wapi pesa za kununulia mgodi na pili kama wao ndio walikuwa wakipitia zabuni ya uuzaji au wao ndio waliotoa ajira kwa waendesha zabuni, hawaoni kuwa kilichofanyika ni upendeleo na kukiukwa kwa kanuni?

Je leo hii Mama Mkapa alipokwenda kukopa mkopo wa dola laki tano, je ni nani alitoa udhamini kuwa Mkapa na mkewe wana mali na fedha za thamani hiyo ya mkopo kuwea kuzikopa? Je walipoulipa mkopo huu katika miaka miwili au chini ya muda wa miezi 24 kuna aliyehoji waliwezaje kuulipa huo mkopo haraka namna hiyo? je hizi irregularities zote na abnormality za wao kukopa na kurudisha mkopo hazistahili kuchunguzwa na kufanyiwa kazi ili tuweze kuelewa ni vipi na ni nini kilichotokea? Kama mtu atadai ah, si waliliuza jengo kwa dola Milioni moja, swali jipya linakuja, je nyumba hii ilipanda thamani yake marudufu katika mwaka mmoja? je Serikali iliyouza nyumba hiyo haikuona mbeleni kutokana na mfumuko wa bei za nyumba kuwa wangeendelea kuishikilia nyumba hii kwa miezi 12 tu, thamani yake ingekuwa marudufu?

Sasa ukirudi kwenye hoja ya kuwa Viongozi walikuwa hawana mapato, je Mishahara hii mpiya au mapato haya mapya yalipangwa yawe na mipaka au kupitia muongozo gani? Je mishahara iliongezwa au viongozi walibakia na mishahara ile ile, ili kuzimisha kelele za Wananchi kama wangepewa wao mishahara mikubwa na Wananchi wakaachwa solemba na mishahara ya mwaka 1985?

Kama si Uhujumu na Udanganyifu, je Azimio la Zanzibar ni nini?

Nilirudi kwenye wajibu wa kiuongozi, narudia tena kusema Mzee Mwinyi, Mkapa na sasa Kikwete walikuwa na nafasi kubwa sana ya kurekebisha kasoro za kilichotokea nyuma.

Mfano leo hii, hata kama baada ya Kiwira na kikwete hataki kumfunga Mkapa, kwa nini mianya ile ile aliyotumia Mkapa haijazibwa na kuundwa nakuweka Sheria kali kudhibiti udhaifu uliotokea?

Au kwa nini kama sheria za uwekezaji na hasa mambo kama nishati na madini, ni wazi zinaliumiza Taifa na kulinyima mapato, kwa nini Kikwete anapata kigugumizi kubadilisha sheria na kurekebisha bila woga kasoro zilizofanywa na Mwinyi na hasa Mkapa kwenye sheria ya Madini na Uwekezaji ya mwaka 1998?

Si lazima kutunga sheri ampya, bali ni kufanyia marekebisho (ammendments) na kutoa tamko jipya la kusitisha kuingia mikataba mipya katika uwekezaji ambayo inainyima Taifa letu pato linalostahilli.

Leo hii Kikwete akitunga sheria kali na kurekebisha sheria mbovu na kuanza kudai uwajibikaji na kufukuza wale walio goigoi au wahujumu, basi si kuwa kampiku Mkapa, bali ni wazi anafanya kazi yake.

Sasa Mwinyi alikuwa na nafasi kubwa ya kusahihisha makosa ya Mwalimu kwa kufanya kazi kwa bidii na kuleta maendeleo kwa kupitia uzalishaji mali ambao kwanza alichopaswa kufanya ni kubadilisha mishahara na kufukuza kazi Watendaji wote ambao waliyatia mashirika na serikali hasara.

Kinyume chake, alilelea watu wale wale na mfumo uleule na yeye akadhani kujaza maduka na bidhaa za kuagiza kutoka nje ndiko kutaleta ushindani na ufanisi!

Labda kuhitimisha kwa sasa nimtupie Mzee Mwinyi swali, kama aliona mchwa wako na yeye ni yule Mzee Dudu Magic, alifanya nini kuua na kuwateketeza mchwa?

Maana yaelekea hakufanya lolote zaidi ya kuachia mchwa wamjaze mimba malkia wa mchwa na kuongeza uzao wa mchwa hawa ambao nao wakaanza kusambaa na kutafuta koloni jipya la kula na genge hili la mchwa likasambaa kuushambulia Utawala wa Mkapa na sasa limeshamiri katika utawala wa Kikwete!
 
...


Ndugu Waberoya;

Umetoa msisitizo kuwa AD liingizwe kwenye sheria na wengi wanaonekana kukubaliana na wewe.Hata hivyo naomba kusahihishwa,"AD haikuwa mojawapo ya sources za sheria za nchi?" Nasema hivyo kwasababu najiuliza kama kweli AD lilikuwa haliwabani viongozi mafisadi then AZ lilikuwa la nini? Je AZ halikuwa foundation ya kubadili baadhi ya sheria zilizowabana viongozi kujilimbikizai mali?ie sheria ya maadili ya uongozi? Ninashangazwa sana pale unaposema kuwa warithi wa mwalimu ie Mwinyi na genge lake hawakuwa wasanii,either walifanya kwa makusudi ama bahati mbaya,wao tofauti na mwalimu ni usanii,na utapeli dhidi ya wananchi period!



Mkuu Jmushi, we can debate over and over in this matter, kumbuka siko against na AD, May be to put in short! Naomba kusema Mwinyi hakuwa mtu sahihi wa kuliendeleza Azimio kama mnavyolazimisha nyie??!! Kama hakuwa mtu sahihi lawama mnazompa leo mnapiga upepo, hakulijua, hakuliamini, hakulitekeleza! alileta lake AZ kwanini mnalazimisha angefuata AD wakati hakuliamini??? mbona watu mnakuwa madikteta kiasi hicho??

AD-Nyerere, AZ -Mwinyi, tatizo liko wapi? kulikuwa na kitu gani cha kumlazimisha alifuate AD?? Kama hakukuwa na ulazima huo tatizo liko wapi? tunatoa hewani tu??

Kwa nini watu mnaona mawazo ya JKN yalikuwa ndiyo sahihi kabisa? Mwinyi kuonyesha hana mpango wala hamsujudii JKN akaweka mfumo wake , kwa sababu alikuwa rais! LEO ANAWAPIGA JIVEMBE WAUMINI WA AD!, kuwa hakuliua! bado mnalaumu wakati alileta AZ, akamaliza vipindi vyake na akaondoka, KAMA tunam-evaluate basi tumuhukumu kwa sera zake , lakini si kwa sababu eti hakulifuata Azimio!!!, Na kwa hilo Mwinyi anastahili SIFA, HESHIMA kama mwanadamu huru aliyefuata mawazo yake kuongoza Tanzania ambayo sisi tulimpa uongozi! hongera mwinyi!

So aidha alifanya kwa makusudi, au kutokujua au kwa intention yoyote ile, bado anabaki kuwa HAKUWA Mtu sahihi-kwa waamini wa AD, ! ILA alikuwa mtu sahihi kwa waamini wa AZ! simple and clear, tukitaka leo AD tuanzishe tuingie mitaani...!!

Kama hakuwa mtu sahihi, tunaweza tukawa tunafanya makosa kumlaumu (kama alifanya kwa makusudi akijua) au tujilaumu sisi kwa kumpa kura za 'NDIYO'

Kama FMES anavyosema lets move on;

Mchango wangu uliopita nimesema we can start kuleta vuguvugu la azimio hata pasi kuwa serikalini, maana ni ushawishi na tukiweza kushawishi umma kutaleta hamasa na ari ya kupigana na maadui wote ambayo imepotea

Kwa maana nyingine ili mjadala wetu uwe productive, wakati tunalaumu, tuseme solution tufanye nini leo, ndiyo unaona mijadala ya kutafuta wapi tulikosea, tu wapi na tukilitaka leo tufanye nini, nimeshaeleza huko nyuma, ili kukuthibitishia sina tatizo na AD-nimeweka njia jinsi gani we can start today!, hatuna la kumfanya Mwinyi! kusema Mungu atamuhukumu kama wanavyosema wengine ni ishara ya udhaifu

My argument will always be positive and unbiased! I believe in fairness, and free mind!

Naona umechanganya na issue za kisheria, ukija huko unaona tatizo sio mwinyi basi wengine wote waliofuata ni yaleyale, sheria zipo na hazifuatwi! this is another big problem

Huwezi ukampa mtoto wa miaka mwaka mmoja glass ya gharama na unaamini hatalivunja! akivunja kosa si lake. Tulitakiwa kuwa na X-ray maalumu ya kujua nani atalifuata AD na nani hatalifuata!!

Hiyo AZ inawezekana kwake yeye ni safi kabisa, tukisema alikosae wakati tulimpa kura ya NDIYO tena na tena, tunajianika zaidi kuwa ndivyi tulivyo! YES mwaka huu JK atapata kura aslimia 90 akiondoka tutaanza kumlaumu

If is that so then we need something special ambalo AD, halitaweza kutusaidia ka matabia yetu haya. Mwinyi alikuwa na uwezo wa kusema analiabudu AD na yet asitekeleze!!!!!!! ingekuwaje??,mbona tunakataa uwazi wa Mwinyi kiasi hiki? AD ni matendo halina nguvu ya x-ray ya kumchoma mtu, kuwa ukisema tu unaamini AD basi kila kitu shwari!

Tukianza kuchambua AZ ndiyo tunasema hafai, likuwa bomu, lilizaa wizi na wezi, n.k na kwa kusema hivi then tunapata conclusion kuwa Mwinyi alifanya makosa haya na alipatia mahali hapa!

Siyo Mwinyi alikosea mahali hapa kwa sababu hakulifuata AD! that is dead wrong! alikuwa mtu na utashi wake, akili zake na mipango yake!, na kama alikuwa shetani basi tulichemka, kama alikuwa malaika basi tulimpata

Kwa maana nyingine Mwinyi anatupa somo kuwa we can start our own systems na kusonga mbele japo lake likuwa bomu!! though still yako yaliyokuwa mazuri!

By the way, kuna mtu anaweza kuweka analysis jinsi WB na IMF walivyoathiri nchi zetu, na je AD lingekuwa in effect lingeathiriwa na WB au lisingeathiriwa??-msaada jamani

Kuna mtu ana Azimio la Zanzibar? aliweke hapa jamani?
 
Waberoya,
The problem I have with Mwinyi is that he has not even been able to come out and defend AZ.
At least angetuambia sababu zake za kuleta AZ ningemkubali. Sasa hivi anatupa lawama kwa wengine tu yeye anapeta. To me that is not leadership. Ni ubabaishaji.
 
- Kuzungumzia kifo cha Azimio bila kutaja faida zake kwa hili taifa ni kufukuza upepo, so far zimetajwa hasara nyingi za Azimio kuliko faida, maana yake ni moja kwamba Azimio halikuwa effective at all, sasa alaumiwe nani aliyelileta Mwalimu, au aliyeliua Mwinyi?

- Kwangu it does not matter, cha muhimu ni reconciliation na tusonge mbele, Azimio halitakuja kurudi tena hiyo ni fact, kulumbana kuhusu aliyelileta au aliyeliua ni waste of time, ni muhimu kujadili effective zake kwa taifa lakini in the process ya ku-move forward sio kutafutana uchawi.

- Bado ninasisistiza kwamba taifa linatakiwa kuongozwa na sheria, sio maa-Azimo flani hivi, haya maazimio ndiyo yamechangia sana kuturudisha nyuma katika utawala wa kuheshimu sheria, tujali sheria kwanza ndio tutasonga mbele.

Respect.

FMEs!

Mkuu kusonga mbele ni muhimu sana lakini hatuwezi kusonga mbele bila kuangalia kule tulikotoka na kuyatafakari mazuri na mabaya yote tuliyoyafanya hadi kufikia hapa tulipo leo. Hili litatuwezesha kuamua ni mazuri yepi ambayo yanafaa kuendelea nayo katika safari yetu na mabaya yapi tuliyoyafanya ili tuyaepuke kabisa katika kuweza kufanikisha safari yetu, vinginevyo tutajikuta tunayarudia makosa yale yale miaka nenda miaka rudi.
 
Back
Top Bottom