Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Mbona mnatuchanganya akili sasa kama Ijumaa,Jumamosi na Jumapili sio sabato tushike lipi?maana tukisema jumamosi mnasema ooh jumapili ndio sabato,haya tukikubali kama sabato ni jumapili mnasema tena ooh sabato ni ijumaa haya tukisema tena ni ijumaa mnasema cjui al khamees kwa kiarabu maana yake ni siku ya sita....Msiwe mnaleta maswali ambayo majibu yake hamna...acheni watu na imani zao....
 
Hata Kiswahili kinakushinda masikini,unajua neno MOSI lina maana gani? Tafakari kisha chukua hatua mapema maana unaishi kwenye upotofu!!
Hzo siku za juma zilingizwa na makabila yanayokaa pwani mwa tanzania ndyo mana hata misanogogi waliita misikiti.ILA siku za Mungu zpo palepale hazijabadilika
 
Fundisho hilo la "tarehe ya kurudi Yesu" halipo kabisa katika "imani za msingi 28" za waadventista Wasabato.... (acha uongo... usimshuhudie jirani yako uongo... Kutoka 20). Kama una ushahidi weka hapa. Na usilete habari za "Miller".. maana wakati wa" great disappointment" hapakuwa na "waadventista Wasabato" wala Miller hakuwa msabato

1. Kwa hiyo umeamua kumkana William Miller mchana kweupe?

2. Je,unamkubali Hiram Edson( baba Wa Sabato) "aliyevuliwa" na William Miller pamoja wengineo kama Ellen White, James White, Joseph Bates?

3. Usabato ulisajiliwa rasmi Mwaka 1863 huko Marekani na sio kwamba ndio ulianzishwa. Imani ya kurudi kwa Yesu Mara ya pili mwaka 1843/1844 iliasisi na Miller mwaka 1818 na ndio ilikuja kuzaa Usabato.

4. Kama unakataa kwamba ramli ya kurudi kwa Yesu Mwaka 1844 haiwezi kuhusishwa na wasabato kwa sababu walikuwa hawajasajiliwa muda huo, je,unafahamu kwamba hata Ellen White (usabato ukiwa umeshasajiliwa) alitoa ramli nyingine ya kurudi kwa Yesu Mwaka 1885?

4./
 
Kimtazamo wangu siku ya saba ni ijumaa,Jumamosi ya kwanza,Jumapili ya pili na kuendelea...
 
Wiki au Juma ina siku saba. Siku ya kwanza ni
Jumamosi(siku ya kwanza ktk Juma)
Jumapili(siku ya pili ktk Juma)
Jumatatu( siku ya tatu ktk Juma)
Jumanne(siku ya nne ktk Juma)
Jumatano(siku ya tano ktk Juma)
Alhamisi(siku ya sita ktk Juma)
Ijumaa( siku ya saba ktk Juma/ manake Juma limetimia watu waenda kuswali Shekheee.)
Hii ni KALENDA uliyotunga wewe? au ya sayari ipi? Unaishije bila hata kujua kusoma KALENDA? Soma hii hapa chini
Screenshot_2018-11-09-07-41-53.jpeg
 
Kwa wengine ni ijumaa then Jumamosi ni siku ya kwanza na Jumapili ni siku ya pili................... Inategemea unaitazama kwa muktadha upi
Mimi nimeandika kwa muktadha wa biblia wala siyo vinginevyo.
 
Kwahiyo tufanye nini kama sabato ni siku ya jumamosi?
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
Enheee...mimi sijabisha.Kwa hiyo....?
 
1. Kwa hiyo umeamua kumkana William Miller mchana kweupe?

2. Je,unamkubali Hiram Edson( baba Wa Sabato) "aliyevuliwa" na William Miller pamoja wengineo kama Ellen White, James White, Joseph Bates?

3. Usabato ulisajiliwa rasmi Mwaka 1863 huko Marekani na sio kwamba ndio ulianzishwa. Imani ya kurudi kwa Yesu Mara ya pili mwaka 1843/1844 iliasisi na Miller mwaka 1818 na ndio ilikuja kuzaa Usabato.

4. Kama unakataa kwamba ramli ya kurudi kwa Yesu Mwaka 1844 haiwezi kuhusishwa na wasabato kwa sababu walikuwa hawajasajiliwa muda huo, je,unafahamu kwamba hata Ellen White (usabato ukiwa umeshasajiliwa) alitoa ramli nyingine ya kurudi kwa Yesu Mwaka 1885?

4./
Hapa msingi ni "fundisho la tarehe ya kurudi Yesu" unalodai Wasabato wanalo.. Nimekuomba utoe ushahidi... Badala yake unaleta hadhi... toa ushahidi hapa... "Sema kitabu au kijizuu ambacho kina mafundisho hayo"

Nimefurahi kwamba unajua kuwa kanisa la waadventista Wasabato lilisajiliwa miaka zaidi ya 30 baada ya mafundisho ya unabii wa Daniel yaliyofanywa na Miller. Kwa hiyo Miller hakuwa msabato kipindi hicho.
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
Mwisho wa siku matendo yako mema pamoja na kupokea wokovu kwa kumkiri Kristo ndio vitakupeleka mbinguni na si sabato itakayokupeleka
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
ACHA KUKOMAA NA DINI ZA WAKOLONI MKUU!

.. Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.
SIKU INA MASAA MANGAPI??? JE, SIKU HIZI ZA LEO, MFANO IJUMAA, JUMAMOSI, JUMAPILI ZILIKUWAPO TOKA ZAMA ZILE?? KALENDA ZILIKUWEPO???
MAANA BIBLIA INATAJA SIKU KWA NAMBA NA SIO KWA MAJINA KAMA NYIE WASABATO. ILIKUWAJE NYIE MKAIPA JUMAMOSI NAMBA YA SIKU YA MWISHO (7)??? JUMAPILI SIKU YA KWANZA YA JUMA NK??
HAKUNA MSTARI WA BIBLIA UNATAJA SIKU KWA MAJINA ZAIDI NI NAMBA TU ILA NYIE MMEAMUA KUZIPA MAJINA AMBAYO NI YA KILEO, POSSIBLY MNAJIPA NAFUU.
 
Miafrika akili zetu zilijazwa kamasi sana. Kutwa kucha kubishania mambo ya dini ambazo hata hazina chimbuko la Uafrika. Acheni ujinga na Utumwa wa Kubishania mara Ukristo na Uislamu hizo ni imani tu tuheshimiane bila kukwazana maaana mwishoe huwa tunamwaga damu. Huuu nao nia aina fulani ya Ujinga na Ukichaaa. Marx alisema RELIGION IS THE OPIUM OF THE PEOPLE. Ama kweli....

kwani hapo mtoa mada kakosea wapi? kama hauna jambo la kuongezea bora ukaa kimya tu jombaa, utapungukiwa nn?
mada yenyewe mbn inajieleza yenyewe,
jamaa katoa hoja, hoja inapingwa kwa hoja, toa hoja zako tukuelewe kuliko kuanza kutoa povuu!!!
 
Kwahiyo tufanye nini kama sabato ni siku ya jumamosi?

Biblia haikuandikwa na Mungu ila na wanadamu kwa kuongozwa naye. Kwa hiyo, kwa kuwa ni Kazi ya Mungu pamoja na wanadamu lazima ufahamu kwamba imetumika lugha ya wanadamu,mazingira ya wanadamu,tamaduni mbalimbali za wanadamu. Katika Biblia kilicho cha Mungu pekee ni maudhui au ujumbe tu. Namba, Maneno,staili ya uandishi na au wahusika hivyo sio vyake.
 
Mambo ya kipuuzi kama haya nilishaacha kuyapatia nafasi!
Upuuzi mtupu.
penye ukweli tukubali ukweli, ukikimbia ukweli ipo siku huo ukweli utakufanya huonekane si mkweli
 
Hata Kiswahili kinakushinda masikini,unajua neno MOSI lina maana gani? Tafakari kisha chukua hatua mapema maana unaishi kwenye upotofu!!
unapomwita mwenzako kipofu hebu jitazame kwanza labda inawezekana we ndo ukawa kipofu zaidi yake
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"
Sio kweli, jumamosi sio siku ya saba hivyo haiwezi kuwa sabato ya Bwana Mungu wako.
Jumamosi ni siku ya saba kwa kalenda ya Gregorian ambayo ni ya kipagani. Hivyo kwa kalenda hiyo umepata sabato ya bandia.
Sabato ya kweli utaipata kwa kutumia kalenda ya kiyahudi ambayo imepigwa marufuku kuwa official calendar.
Hivyo kwa kutumia kalenda ya bandia unapata sabato ua bandia.
Ukitumia kalenda aliyoitoa Mungu baada ya uumbaji unapata true sabbath.

Swali: wapi kwenye biblia wamesema jumamosi ni siku ya saba, ukiondoa kutumia biblia ya kisasa.

Note: evidence ya siku kuu ya Easther au pasaka haitoshi kuproove usahihi wa sabato maana hata pasaka wanayoiadhimisha protestants ni ya bandia.
Pasaka ya kweli huadhimishwa tarehe 14 ya mwezi wa abibu (mwezi wa abibu ni mwezi wa kwanza wa kiyahudi) kila mwaka ambayo huwa ni siku ya sita ya juma.
Pasaka ya waprotestant haina tarehe maalumu ila hufanyika kwa kuifananisha na ya wayahudi kuwa siku fake ya sita au ijumaa ya Gregorian kalenda.

Tafuta maarifa mwenyewe ukiwategemea wa SDA wakulishe wanakupoteza.
 
Tofauti na kiswahili nikuhakikishie tu kuwa shule yangu ni kubwa sana.

Hata hivyo rejea kwenye KALENDA angalia siku ya kwanza ni ipi na siku ya saba ni ipi.
kalenda nyingi siku hizi zimeanza kuchakachuliwa
chukua sm yako unayotumia angalia kalenda utapata majibu sahihi
hata wachina wenyewe wanalitambua hilo japokuwa wanaamini miungu mingne kama budha n.k
ukweli utabakia kuwa ukweli milele
 
Biblia haikuandikwa na Mungu ila na wanadamu kwa kuongozwa naye. Kwa hiyo, kwa kuwa ni Kazi ya Mungu pamoja na wanadamu lazima ufahamu kwamba imetumika lugha ya wanadamu,mazingira ya wanadamu,tamaduni mbalimbali za wanadamu. Katika Biblia kilicho cha Mungu pekee ni maudhui au ujumbe tu. Namba, Maneno,staili ya uandishi na au wahusika hivyo sio vyake.
Kwa mtazamo huo, hata UWEPO WA MUNGU kwako ni "fiction". Kwa hiyo mimi nawewe ni kama maji na mafuta. Mimi biblia ndiyo kitabu ninachokiamini 100% na ushahidi wa mambo yote natumia biblia, hata Yesu alitumia ushahidi wa biblia....
 
Hapa msingi ni "fundisho la tarehe ya kurudi Yesu" unalodai Wasabato wanalo.. Nimekuomba utoe ushahidi... Badala yake unaleta hadhi... toa ushahidi hapa... "Sema kitabu au kijizuu ambacho kina mafundisho hayo"

Nimefurahi kwamba unajua kuwa kanisa la waadventista Wasabato lilisajiliwa miaka zaidi ya 30 baada ya mafundisho ya unabii wa Daniel yaliyofanywa na Miller. Kwa hiyo Miller hakuwa msabato kipindi hicho.


Unataka nikupe ushahidi Wa andiko kwamba Ellen White aliwahi kupiga ramli ya kurudi kwa Yesu mwaka 1885? Au unataka nionyeshe ni fundisho gani kati ya 28 munayoiamini? Swali hili linaonyesha kwamba huijui historia yako na huelewi maana ya historia. Kwa hiyo, kama kuna mambo ya hovyo waanzilishi wenu waliwahi kuyafanya na baadaye mumeamua kuachana nayo hilo nalo unataka uthibitisho kama jambo hilo ni miongoni mwa mambo 28 munayoyaamini? Mambo mfanye nyie na kisha muyakimbie halafu unataka mimi nikupatie ushahidi. Kwani Ellen White alikuwa anafanyia usabato kisiwani ambako hakukuwa na watu wakiona au kusikia akilaghai watu kwamba YESU angalirudi Mwaka 1885?
 
Back
Top Bottom