Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Siku ya saba (Sabato) ni Jumamosi

Miafrika akili zetu zilijazwa kamasi sana. Kutwa kucha kubishania mambo ya dini ambazo hata hazina chimbuko la Uafrika. Acheni ujinga na Utumwa wa Kubishania mara Ukristo na Uislamu hizo ni imani tu tuheshimiane bila kukwazana maaana mwishoe huwa tunamwaga damu. Huuu nao nia aina fulani ya Ujinga na Ukichaaa. Marx alisema RELIGION IS THE OPIUM OF THE PEOPLE. Ama kweli....
Mbona haueleweki na wewe unachosimamia wewe akili yako iliyosawa mbona hujamnukuu babu yako au muafrika mwenzako ukamkimbilia Marx?

Huoni na wewe bado ni mtumwa au unamuamini sana Marx? wewe unaishi kijamaa kama role model wako Marx?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Kwani kuna mtu kakuzuia kuwa myahudi, usitulazimishe wote tuwe wayahudi. Sabato ni siku ya saba inategemea umemua kuhesabu kuanzia wapi
Siungani na mleta mada lakini hili la kusema unaweza kuhesabu wiki kuanzia popote umelitunga wewe!
 
KWANZA SIKU INAANZA JIONI
.... Ikawa jioni ikawa asubuhi siku moja... Mwanzo 1:5..Ikawa jioni ikawa asubuhi... Mwanzo 1: 8, 13, 19, 23, 31.

SIKU YA SABA MUNGU HAKUFANYA KAZI

.. Mungu akaibariki siku ya saba akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya Mwanzo 2:3

SIKU YA SABA NI LINI?

-Yesu alikufa saa tisa siku ya maandalio ya Sabato.... Marko 15:33 & 42 na alifufuka siku ya KWANZA ya juma baada ya Sabato... Marko 16: 1-6

-Siku ya maandalio ya Sabato ni ijumaa
USHAHIDI: Katoliki na waprotestanti wote wanaadhimisha "IJUMAA KUU" kwa dhana ya kwamba Yesu aliuwawa IJUMAA


-Sabato ni Jumamosi
USHAHIDI: Wayahudi hawajawahi kuacha kutunza Sabato "SIKU YAO YA SABATO NI JUMAMOSI"


Mungu hajawahi kusimama kufanya kazi. Yesu ambaye alihusika katika uumbaji anasema Baba yake hajawahi kuacha kufanya Kazi. Kwa hiyo,kama unasema alisitisha kazi,ni kazi zipi? Ni lazima ufahamu kwamba Kitabu cha Mwanzo hakiwasilishi matukio halisi kwa mfuatano(progressive events) Bali kinatumia lugha ya picha katika kueleza kwamba Mungu alitumia muda Fulani katika kufanya uumbaji na baadaye viumbe wake wakakengeuka. Conception ya muda tulionayo wanadamu sio aliyo nayo Mungu.

Tunavyohesabu sisi muda sio ambavyo Mungu anahesabu pia. Ile kauli kwamba siku moja ni sawa na miaka 1000 kwa Mungu haimaanishi kweli kwamba ni miaka 1000 Bali muda mrefu.

Kwa hiyo,naona mnahangaishwa sana la conception ya 6days literal creation. Biblia inaposema ikawa jioni ikawa asubuhi haimaanishi Jumapili,Jumatatu...na ulimwengu haukuumbwa kwa siku sita.
 
Mungu hajawahi kusimama kufanya kazi. Yesu ambaye alihusika katika uumbaji anasema Baba yake hajawahi kuacha kufanya Kazi. Kwa hiyo,kama unasema alisitisha kazi,ni kazi zipi? Ni lazima ufahamu kwamba Kitabu cha Mwanzo hakiwasilishi matukio halisi kwa mfuatano(progressive events) Bali kinatumia lugha ya picha katika kueleza kwamba Mungu alitumia muda Fulani katika kufanya uumbaji na baadaye viumbe wake wakakengeuka. Conception ya muda tulionayo wanadamu sio aliyo nayo Mungu.

Tunavyohesabu sisi muda sio ambavyo Mungu anahesabu pia. Ile kauli kwamba siku moja ni sawa na miaka 1000 kwa Mungu haimaanishi kweli kwamba ni miaka 1000 Bali muda mrefu.

Kwa hiyo,naona mnahangaishwa sana la conception ya 6days literal creation. Biblia inaposema ikawa jioni ikawa asubuhi haimaanishi Jumapili,Jumatatu...na ulimwengu haukuumbwa kwa siku sita.
Unaonaje kama ukisema huwa reference yako ni kitabu gani? Maana nionavyo ni kama unaiponda biblia..

Je nyie wakatoliki mwasemaje.. jumapili siyo siku ya kwanza ya juma?..
 
Kwamba utaenda mbinguni kwa kusali jumamosi? wasabato hamnaga akili aisee, EGW kaziteka zote!!

Ukiona watu walikuwa wanasoma Biblia na kuelezwa kwamba Yesu alishafunga suala la lini atarejea kwa kuweka wazi kwamba suala hilo hata yeye halijui lakini akaja mtu kuwaaminisha watu kwamba yeye anaifahamu tarehe ya kurudi kwa YESU na kweli wakatokea watu Wa kuamini hivyo, basi ujue watu hao wana matatizo katika kufikiri.
 
Ukiona watu walikuwa wanasoma Biblia na kuelezwa kwamba Yesu alishafunga suala la lini atarejea kwa kuweka wazi kwamba suala hilo hata yeye halijui lakini akaja mtu kuwaaminisha watu kwamba yeye anaifahamu tarehe ya kurudi kwa YESU na kweli wakatokea watu Wa kuamini hivyo, basi ujue watu hao wana matatizo katika kufikiri.
Biblia au katekisimu au mithale ya waumini? Sema unasoma kitabu gani
 
Unaonaje kama ukisema huwa reference yako ni kitabu gani? Maana nionavyo ni kama unaiponda biblia..

Je nyie wakatoliki mwasemaje.. jumapili siyo siku ya kwanza ya juma?..

Kila kitu unataka reference ya Biblia tu? Unaposoma Kitabu cha mwanzo lazima ufahamu kiliandikwa na nani na katika lugha gani. Kitabu cha Mwanzo kiliandikwa kwa Kiebrania na katika kiebrania kila namba ina maana yake na wala siyo hiyo inayoisoma na wala usiitafsiri kadri ya mazingira yako ya namba.
 
Biblia au katekisimu au mithale ya waumini? Sema unasoma kitabu gani

Kwa hiyo, hauifahamu historia ya Kanisa lako kwamba mumekuwa mkijaribu Mara kadhaa katika historia ya dunia kuwaaminisha watu kwamba mnaijua tarehe ya kurudi kwake Yesu? Kwa nini unaifahamu sana Jumamosi kuliko jinsi ambavyo mumewahi kupotosha watu?
 
Mkuu hilo ni neno la kiarabu na waarabu walipotosha makusudi ila ukweli ni kwamba jumamosi ndiyo siku ya 7
kwahiyo waarabu walianza kutumia neno mosi ili kupotosha siku ya sabato?
ina maana majina ya siku yote yamepotoshwa na waarabu ili kuficha siku ya kweli ya sabato?
Kati ya neno mosi na huu usabato kipi kimetangulia?
 
kwahiyo waarabu walianza kutumia neno mosi ili kupotosha siku ya sabato?
ina maana majina ya siku yote yamepotoshwa na waarabu ili kuficha siku ya kweli ya sabato?
Kati ya neno mosi na huu usabato kipi kimetangulia?
Mkuu hata Qur an imetaja sabato ni jumamosi mkuu na ikaongeza kuwa wanaovunja watageuzwa kuwa manyani
 
Mkuu hata Qur an imetaja sabato ni jumamosi mkuu na ikaongeza kuwa wanaovunja watageuzwa kuwa manyani

Kwa hiyo, wewe unaiamini Quran kwa sababu tu humo ndani kumetajwa sabato? Kwa hiyo Quran ni document genuine na kama ndivyo unaimini inaposema YESU sio Mungu,sio mwana Wa Mungu na hakufa msalabani?
 
kwahiyo waarabu walianza kutumia neno mosi ili kupotosha siku ya sabato?
ina maana majina ya siku yote yamepotoshwa na waarabu ili kuficha siku ya kweli ya sabato?
Kati ya neno mosi na huu usabato kipi kimetangulia?

Kama ndivyo kumbe wakatoliki wanaohusishwa na kuharibiwa kwa sabato basi hawahusiki.
 
Wiki au Juma ina siku saba. Siku ya kwanza ni
Jumamosi(siku ya kwanza ktk Juma)
Jumapili(siku ya pili ktk Juma)
Jumatatu( siku ya tatu ktk Juma)
Jumanne(siku ya nne ktk Juma)
Jumatano(siku ya tano ktk Juma)
Alhamisi(siku ya sita ktk Juma)
Ijumaa( siku ya saba ktk Juma/ manake Juma limetimia watu waenda kuswali Shekheee.)
 
Back
Top Bottom