Mkuu watu huwa hawaogopi kifo bali huwa wanaogopa huko waendako watajibu kitu gani mbele ya Mungu ukizingatia kwamba wengi wetu tunaishi maisha ya anasa na kusahau wajibu wetu mbele ya Mungu, hofu hasa ipo hapo.
Ndiyo mkuu, hebu tuambie ni kwa jinsi gani utajua kuwa siku zako za kifo zimekaribia???--- angalia, hiyo inamaanisha kwamba hata namna na aina ya kifo chako unakijua!!
Kaburi lako lisijengewe au hata kuandikwa jina kwani wewe ni muhalifu??, hata wahalifu makaburi yao hupambwa na ndugu na jamaa zao wanaotambua mchango mzuri waliowafanyia katika uhai wao. Vipi watoto na wajukuu zako wakitaka kuona kaburi lako itakuaje??!!, kwani kaburi lisilojengewa ni kaburi lililopotea.
Kwanini unataka tupu zako tu zifunikwe na sio mwili wote??-- mkuu,ukiamua kula nguruwe kula aliyenona, bora wakuache wazi kabisa.
Nadhani katika masharti yote juu ya mazishi yako hilo litakuwa ni sharti gumu, ili uzikwe katika hali hiyo unayoitaka labda uajiri watu binafsi kwa kazi ya mazishi y ako.
Sio akili za kuambiwa ni kwa habari za kuambiwa tumia akili yako. Wewe kwa umri ulionao umepata wapi kusikia kuna kitu kinaitwa AKILI ZA KUAMBIWA??
Kwenye mazishi ya mwili wako nitahudhuria