Ni kweli kila mmoja wetu atakufa na kwa mtu yeyote aliye makini ni lazima siku moja utajaribu kuimagine siku hiyo ya kifo chako itakuwaje na huku nyuma mambo yatabaki vipi? Lakini ni ukweli usiopingika kwamba marehemu huwa hana mamlaka na mwili wake bali wafiwa ndio wenye mamlaka, hivyo kuna mambo unaweza kuagiza lakini yasitekelezwe!
Mfano: Huwezizuia watu wasikulilie pindi utakapokufa, kilio huja kutokana na hisia za huzuni pale watu wanajaribu kukumbuka katika umuhimu na uwepo wako!
Pia huweziamrisha watu watawanyike masaa 7 tu baada ya kifo chako maana huwezijua utakufa lini na utafia wapi na wakati unakufa je wale ndugu muhimu kama Mama, Baba, kaka,dada, mke, watoto watakuwa karibu nawe? Hawa ndio wataamua uzikwe wapi na uzikwe lini!
Hiyo pesa uloanza kujiwekea nashauri usiiweke bali kama unaishi katika nyumba yako mwenyewe basi tenga chumba maalum, kanunulie sanduku unalotaka kuziwa nalo na vingine vyote uhifadhi humo ili siku ya kifo chako wavichukue na kuvitumia, lakini ukiacha pesa zitachukuliwa na hazitatumika bali michango ya watu ndo hutumika kufanikisha hilo suala, kwanza siku hiyo hata mkeo tu hawezi kabisa kuwa na nguvu hata ya kuinuka kwenda huko benk, chezea kufiwa na mtu wa tegemeo kwa familia kama baba wa familia huwa si mchezo!