Nikifa sitaki Kuzikwa kwenye makaburi ya Jumla nataka wanizikie nyumbani kwangu.
Ninyi mnatuamrisha mara tuwafanyie hivi mara tusiwafanyie vile wakati siku hiyo mtakuwa marehemu!??? Tulieni hivyohivyo, tutafanya yetu kadiri tutakavyoamua sie, OK!???
Bibi unapiga nota ?Sitaki niwekwe mortuary namwogopa Mshana Jr atanibaka.
Sitaki wakanizike alikozikwa Mr. kule wana roho mbaya maana hata mali zote za Mr. plus nyumba niliyojenga Naye wamenipora,
Wanizike na joho langu la uzee wa kanisa, Bible yangu na kinanda changu.
Siyo lazima wawasubiri ndugu zangu wafike ndo nizikwe acha wakifika wakute kaburi.
Mali nimeshawaambia, kila mtu anajua chake, mali zangu binafsi wafanye watakavyoamua.
Kifo kipo tukubali tu.
Kwenye mali za baba yao? Hawakuambulia hata soks hata kijiko. Yuko mtoto wa nje ya ndoa ndo alijimilikisha vyote.
Hawa watoto wa nje ya ndoa ni hatari.
Nazidi kumngojea Mungu aje aamue mwenyewe.
Naunga mkono hoja hapo post #43.
Jukumu lako wewe ni kufa tu mengine tuachie wanaobaki, kulia au kutolia, kupiga bia au kutopiga bia, kutawanyika ama kukaa hilo wataamua wao kulingana na mazingira ya wakati huo.
Umeandika meengi what if ukipotea kwenye ajali ya ndege kama ile ndege ya Malaysia ?
Nikirudi kwenye mada, kifo ni bayana.
Wengine sisi ni wachimbaji, tunaweza kufia kwenye makurukunta huko na ikawa mwisho wa show yetu
Ila ikitokea nikafia uraiani basi nizikwe kwa sheria zote za kiislam.
Mimi kifo najua kipo na kitakuja tu...hakina siku saa.
Hivyo Basi...najiandaa na maisha baada ya kifo ambayo naamini yapo.
Nachoomba nife Hali ya kuwa Mola want yu radhi nami.
Kuzikwa nizikwe kwa taratibu za Dini yangu..ya uisilamu.
Hivyo yaani
Na wewe kwanini unipangie mimi kunywa pombe nikija kukuzika?kwani utaninunulia wewe marehemu?si ninakunywa kwa hela zangu?au umesikia hizo bia tunalipa kwa rambi rambi?Mimi ndio nimeagiza. Na Mimi ndio nitakuwa nimekufa. Mimi familia yangu marhemu wote wanasikilizwa kwa yale yote yanayotekelezeka. Kwanza Mimi ndio nimekufa why mnipangie nyie namna ya kunizika
Read the Bible...How did you come to that conclusion of Motoni or Peponi?
ndo hivo sasaHuruhusiwi ku quote any verse from scriptures maana huu Sio Uzi wa kidini. No Bible nor Quran. Maana nyie watu soon mta deviate hii mada na kuanza mabishano yenu yasiyo na mwisho
Mungu ni Mungu tu🙌Wakuchome na majivu wakayatupe baharini ALIYEKUUMBA KUTOKA SPERM HADI KUWA WEWE FOR SURE ATAKURUDISHA.
Huwa nawaza ili swala mpaka nakosa majibuMkuu, jiulize kabla wazazi wako ambao ndio waliokuleta hapa duniani hawajazaliwa, ulikuwa wapi..?!
Jibu ni: Haukuwepo! Na wala haukuwa ni mwenye kutajwa kabisa!
Kwahiyo usipate tabu, Yeye Aliyekuanzisha mara ya kwanza hashindwi kukurejesha mara ya pili!
Na wewe kwanini unipangie mimi kunywa pombe nikija kukuzika?kwani utaninunulia wewe marehemu?si ninakunywa kwa hela zangu?au umesikia hizo bia tunalipa kwa rambi rambi?
Nitakachofanya kama maeehemu unanidai nitalipa kwanza deni, kisha naita kreti ya bia kukusindikiza kuzimu
Yaani unafanana na mue kwa kila kitu,mimi sitaki hata kuagwa,au eti kusomewa historiaBaada ya kuhudhuria mafunzo ya FBI na China-MSS, nilielewa kwamba binadamu yeyote mwenye AKILI kubwa ni lazima ailazimishe akili yake kukikubali KIFO.
-
Tukiwa na training team ya China MSS, swali la kwanza kuulizwa ni; " Do you fear death ? My honest answer, as we were taught never to lie, was Yes, I do.
-
Tulijibiwa kwamba How could that possibly be , you fear something you never had any experience before? is there any person in all our recorded history ever experienced The Go and Return to share the experience, they asked.
-
We said, We don't know!
-
Wakatuambia, ili mjifunze haya mliyojia and to serve the world as well as the state; you guys have to accept death as the matter of TRUTH. Pili, No one knows the TRUTH but we think we do. We are all living in myths and fantasies of the past just to secure our insecurities.
-
It is one of those days I came to realize that many people have been dying without living the life . Ni wachache sana wamefanikiwa kufunua BUSWATI na PAZIA ili kuona the glimpse of life. Kibaya zaidi haya mambo you can not be taught. Verily, you have to check it by yourself. Curiosity never killed the Cat. THINK!
-
Siku ya KIFO Changu
1. Sitotaka mwili wangu kusafirishwa kupelekwa Kilimanjaro Unless nimefia NAMIBIA, kitu ambacho siamini hivo, siku zangu zikikaribia, for sure I will know, nitarejea nyumbani. Nitapenda kuzeekea Dar es salaam, mji ambao ninaupenda sana.
2. Nimefungua death account kila mwezi naweka dola 100 kwa ajili ya kugharamia maziko yangu, I have documented that on my Diary. sitaki yeyote atoe senti yake kwa maziko yangu.
3. Sitohitaji watu wakae matanga, nikishafukiwa, kila mtu aondoke kwenda kufanya yanayomuhusu.
4. Masaa 7 Tangu kifo changu niwe nimeshazikwa, naamini nitakuwa sijaanza kutoa harufu ya kuliwa na bacteria.
5. Kaburi langu lisijengewe wala kuandikwa jina.
6. Nisivikwe nguo yoyote zaidi ya kitambaa kitakachohifadhi tupu zangu.
7. Sitoruhusu kwa mtu yeyote aliyelewa kuhudhuria maziko yangu na wala kwenye maziko yangu sitoruhusu pombe
8. Sitopenda nyimbo zozote zipigwe wala mtu yeyote kuimba. It is the moment of silence to honor my existence
9. Haitoruhusiwa Kulia. Kwanini ulie? Kwani hukuwahi kujua kwamba tumezaliwa ili tufe, jiandae kwa sababu for sure Utakufa.
10. Ndugu yoyote hausiki kwenye Mali zangu kwa namna yoyote ile , mali zangu ni za watoto wangu na mke wangu tu , I have documented that on my diary, Bank accounts and legal issues.
-
Je, siku ukifa, ungependa vitu gani usifanyiwe kwenye maziko yako? na je ungependa ni nani awe mrithi wa mali zako?
Thank you and Rest In Peace to all the humans who have stepped into the truth of death. To all the humans who Have died due to Covid-19, and for those who continue dying due to COVID -19.
Chukua Tahadhari. Akili za kuambiwa, Changanya na zako.