Siku ya Kifo Changu

Siku ya Kifo Changu

Nasoma lkn sielewi,mtu anakuwa na courage ya kusema sitaki mwili wangu as if ni kitu cha maana sana,ninachoamini mimi ni kuwa there is life after death,hii miili tunayoita ya kwetu na kuipangia masharti itabaki hapa duniani na itaoza,roho zetu ndio zitabaki hai,hii ni either peponi au motoni...

How did you come to that conclusion of Motoni or Peponi?
 
Mimi nikifa sitaki mambo mengi nichomwe moto tu, ila Kama haiwezekani Basi nifukiwe tu futi sita bila mambao Wala manguo... Raw and unsugarcoated!

Kama ulikuwa hujui mtu akifa funza na minyoo wanaingia ndani ya mwili(Mzoga) na kuchukua nutrients zote na kuzirudisha Tena ardhini ambapo udongo unautumia tena Kama rutuba... Ni proper system ya recycle ndio sababu nikiona mtu anajengewe na masimenti nachukizwa saana sababu naona Kama watu wanajaribu kuidhibiti nature isifanye kazi yake.

Death is inevitable!
Boss , kuna ujumbe wangu DM kwako kiongozi
 
Sawa mkuu nimekueleza hayo sababu nakumbuka hata mzee wangu aliagiza akifa akazikwe kijijini alikozikwa mama yake mzazi, lakini baada ya kifo chake kamati ya mazishi iliamua tofauti na akazikwa palepale mkoa alipofiwa na hayo yalikuwa maombi ya mkewe kuwa awe jirani na kaburi la mumewe.
Pia mzee aliacha wosia na mgawanyo wa mali, lakini suala la mirathi lilipofikishwa mahakamani, mahakama iliukataa wosia wake na kuagiza kitu tofauti na maagizo yake japo mahakama yenyewe inakiri kuwa wosia wa marehemu unawakilisha kauli yake halisi!
Mimi binafsi ningependa nikifa nizikwe tu kwa taratibu za kawaida kama walivyozikwa marehemu wengine walionitangulia, Lakini zaidi ningependa kila anayenifahamu popote alipo akinikumbuka aseme neno lolote kuniombea pumziko la amani huko nitakakokuwa sababu mimi pia nina utamaduni wa kuwaombea marehemu wote popote kila ninapohudhuria misiba au ibada makanisani!

Ha ha ; Sawa Bwana, atleast wewe umekikubali kifo. By the way mirathi yangu ipo kisheria na sio kimaandiko tu. Sasa hiyo mahakama itakayopinga mirathi yangu itabidi hakimu muhusika aje kunifufua.

Mirathi nyingi za KITZ ni matamko na paper based ambayo haya nguvu mahakamani.

Nimeshasema mali zangu zote ni mke wangu na watoto wangu. Na hili lipo kisheria zaidi kuliko kimaandishi . Ndugu zangu watapata chao wakati nipo hai kama kuna umuhimu.

Halafu haya mambo ya waafrika kutolea macho mali za ndugu yanatoka wapi? Halafu walivo mental illness, wanasahau watoto. Mimi hili swala nimeliweka bayana kabjsa na hakuna ndugu niliyemuweka karibu na mali yangu except my wife and my kids. Same to my wife, she has done the same.

Hii mambo baba yao au mama yao walikuwa na hela but now watoto hata Shule hakuna wa kuwalipia Ada Sitaki kusikia
 
Nikifa sitaki Kuzikwa kwenye makaburi ya Jumla nataka wanizikie nyumbani kwangu.
Sure. Hata mimi mambo ya kubaba na kunukiana sitapenda kabisa. Nizikwe Kijijini kwetu kwenye shamba langu.
 
Wanichome moto nianze kupata experience mapema ya jehanamu kama tuaminishwavo na watawala wa kidini.
 
Wanichome kama Wahindi nione siku ya mwisho nitaludije
Mkuu, jiulize kabla wazazi wako ambao ndio waliokuleta hapa duniani hawajazaliwa, ulikuwa wapi..?!

Jibu ni: Haukuwepo! Na wala haukuwa ni mwenye kutajwa kabisa!

Kwahiyo usipate tabu, Yeye Aliyekuanzisha mara ya kwanza hashindwi kukurejesha mara ya pili!
 
Ndugu zangu wote na marafiki zangu wote wanajua kuwa siku yakufa kwangu nizikwe kwa kutumia kitanda ninacho lalia na mke wangu. Fedha yajeneza mnunulieni kitanda kipya na godoro. Wekeni pilo ya pili kando yangu ili akifa mfungue kaburi mmlaze tu hapo kando mrudishie mfuniko.

Kaburi natarajia kulichimba na kulijengea mwenyewe tiyari kwa maziko yangu
Sasa ukifa halafu shemeji akaolewa na mwanaume mwingine, na mauti yakamkuta huko... Unadhani mumewe atakubali mkewe azikwe kwenye 'kitanda' chako..?!
 
Kwenye mali za baba yao? Hawakuambulia hata soks hata kijiko. Yuko mtoto wa nje ya ndoa ndo alijimilikisha vyote.

Hawa watoto wa nje ya ndoa ni hatari.

Nazidi kumngojea Mungu aje aamue mwenyewe.
Looh, pole sana!
 
Yani mtu afate maagizo ya marehemu?ukifa huna lako na huwezi kupangia watu kitu cha kufanya

Mimi ndio nimeagiza. Na Mimi ndio nitakuwa nimekufa. Mimi familia yangu marhemu wote wanasikilizwa kwa yale yote yanayotekelezeka. Kwanza Mimi ndio nimekufa why mnipangie nyie namna ya kunizika
 
Mimi kifo najua kipo na kitakuja tu...hakina siku saa.
Hivyo Basi...najiandaa na maisha baada ya kifo ambayo naamini yapo.

Nachoomba nife Hali ya kuwa Mola want yu radhi nami.

Kuzikwa nizikwe kwa taratibu za Dini yangu..ya uisilamu.

Hivyo yaani

Sawa ila hakuna anaekufa hajaridhiwa Na Mola. Hayo maneno mengine ni Faraja ya insecurities Tu
 
Hili jambo watu wengi hawalitilii maanani, unakuta familia nzima wanasafiri kwenye chombo kimoja cha usafiri, ikitokea bahati mbaya mnaondoka wote kwa pamoja

Na huyo kwenye DP ndio wewe ?
 
Sijui hawa watu wanaofanya kazi mochwari huwa wanalalaje!
Siku mzee wangu alipofariki. Wakati wa kwenda kuchukua mwili niliingia monchwari kwenda kusaini. Pembeni kulikua na meza mbili juu wamelazwa maiti nadhan walikua wanataka kuwasafisha. Niliwaangalia kwa kweri nilinyong'onyea sana. Kifo kinatisha hata kukiongelea
 
Back
Top Bottom