"Leo nimesoma mtandaoni, Dar es salaam kuna watu wanajaribu kupima kina cha maji, viujambazi ujambazi na uporaji vimeanza kuja juu,naomba nitoe meseji wasijaribu kina cha maji, IGP upo hapa, mitandaoni wanamtaja Afande mmoja alikomesha ujambazi, wanasema 'Mama turudishie',IGP kaliangalie hilo vizuri" -- Rais Samia Suluhu wakati akizungumza na wazee Dar es salaam.
Swali; Tangu aliyekuwa Rais wa JMT John Magufuli kufariki mbona haya matukio yanarudi kwa kasi?
Mbona madawa ya kulevya mitaani yanarudi kwa kasi sana na siku za karibuni kuna mzigo mkubwa ulikuwa unaingizwa nchini?
Maoni ya wadau

Sio IGP bali aliyekuwa nyuma ya IGP alikuwa ni Moto usiosogeleka! Tunashukuru kuwa mmeanza kuona tofauti ndani ya kipindi hiki kifupi.Jiwe was real hard mpaka majambazi walipiga saluti.

Haki nobody like JPM. Alikuwa one man show.Nguvu kubwa isiyoonekana nyuma yake ilinyamazisha kelele na fujo za kila mtu na kila kitu.Alitamka na kila mwenye akili timamu alimwelewa waovu walitulia,Hadi mapepo ya Corona na ujambazi yalitii.Sasa vyote vinarudi kwa kasi ya 5G.Mungu baba ahsante kwa maisha ya Magufuli kabla yake tulikuomba kwa pamoja utupe rais wa aina yake ukatupa,ukatuonjesha tu atufungue macho na tuone tofauti ya uongozi na uongozi.Umemhitaji ukamchukua.Wewe ni Mungu.Ushukuriwe milele.
Je,Unadhani kwanini imekuwa mapema mno utofauti wa juhudi za hayati JPM na uongozi uliopo kuonekana miongoni mwa watanzania?