Sikieni hoja za wazanzibar

Sikieni hoja za wazanzibar

Mambo kama haya hata sipendi kuonesha maono yangu juu ya haya.
 
ndio maana nawashangaa wale wabunge wanaopinga kuwa zanzibar haikushirikishwa mchakato wa muungano kwani wazanzibar hawapokwa ajili ya muungano ndiomaana wanafanya kila njia tanzania ichafuke haiwezekani wapeperushe bendera ya tanzania kwani wao wana bendera yao kwanini wachukue bendera ya tanzania walitumia iran kukwepa vikwazo vyao kama umoja wa mataifa ungechukua hatua ya kuchukua vikwazo ambao wangeathirika ni watanganyika kwa kiasi kikubwa wangeathirika wao wazanzibar wangekimbilia Oman hakuna haja ya kuwashirikisha
 
acha upumbavu hivi pale mnapoipeleka jmt yako katika vita unafikiri wazanzibari tunakubalianb na hayo take the consequencies
Hoja ipo wapi? Consequences za kuuza Bangi?
Mbona hamkatai ulinzi na usalama usiwe wa muungano?
 
weweupo na akili lakini?kwani jmt ninini.. ni umoja wa kwetu sote ------- wa mawazo wewe.. eti tuliwaachia... chombo hicho unachojifany akukikaliani cha kwetu pamoja akili ndogo wewe.. anzisha nyikayako kwanza

Wewe unataka nini hela ni ya waznz na wataendelea kutumia jina la tz mpaka mtakapo waachia nchi yao munaogopa mendeleo ya znz kwanini na tanganyika yenu wezi watupu
 
weweupo na akili lakini?kwani jmt ninini.. ni umoja wa kwetu sote ------- wa mawazo wewe.. eti tuliwaachia... chombo hicho unachojifany akukikaliani cha kwetu pamoja akili ndogo wewe.. anzisha nyikayako kwanza
Kama ni umoja wetu sote bendera ya znz waliyokuwa wanadai ni ya nini? Kwanini walijiondoa JMT kuhusu usafiri wa majini mwaka 2003 na kuanzisha ZMA mwaka 2006?
Je, mamlaka kamili ni kuwa na chombo huru kama ZMA kinachotumia bendera zake na kulipa ada zake au ni kuuza bangi kwa jina JMT.
 
Kwa haya yote na sisi Watanganyika tuna sehemu ya lawama, nayo ni moja tu.......Tumewalea sana.
Na kawaida mtu ukimlea sana anabweteka, na ndiyo haya yanayochagiza 'Muungano wa Mkataba'.

Maadam tulikosa fursa ya kupiga kura ya maoni juu ya kuwepo ama kutokuwepo Muungano, nafikiri sasa tuanze
kufikiria tuwe na transition period tunapoelekea kwenye Serikali tatu.

1. Mawaziri na viongozi wanaoshughulika na mambo yasiyokuwemo kwenye Muungano waache kushiriki ama kutoa fedha
kuisaidia ama ku-support masuala yasiyokuwa ya Muungano (la usajili wa Meli mojawapo).

2. Nafasi za kazi zisizokuwa za Muungano na ambazo zimeshikwa na Wazanzibar ziondolewe ama kupewa Watanganyika.

3. Tuanze kufikiria Wazanzibar wanaoishi Tanganyika wapewe vitambulisho maalum (angalau vinavyofanana na working
permit kwa raia wa kigeni).

4. Vyama vya kisiasa vianze kufikiria miundo yao ya uongozi kulingana na mfumo mpya wa Serikali tatu.
Budget support kwa Serikali ya Zanzibar lazima ipitishwe na Bunge na iwe soft loan na sio sadaka.

Kwa sasa ni hayo.
Umesahau kuhusu nafasi za upendeleo elimu ya juu. Sasa ziwe katika ushindani na si kumyima Mtanganyika nafasi ili ichukuliwa na mznz kwasababu ya uzanazibar na siyo academic merits

Elimu ya juu kusiwepo na mikopo. Mwaka jana wzn 1000 walidhaminiwa na maelfu ya Watoto wa kianganyika kuhangaika na ada zao.

Nadhani sasa pesa za meli zibaki na kuhudumia jamii ya wznz.

Tumechoka. Tumechoka
 
Wewe unataka nini hela ni ya waznz na wataendelea kutumia jina la tz mpaka mtakapo waachia nchi yao munaogopa mendeleo ya znz kwanini na tanganyika yenu wezi watupu
Mamlaka kamili vipi? Mkitumia neno Tanzania msahau mamlaka kamili.
 
ndio maana nawashangaa wale wabunge wanaopinga kuwa zanzibar haikushirikishwa mchakato wa muungano kwani wazanzibar hawapokwa ajili ya muungano ndiomaana wanafanya kila njia tanzania ichafuke haiwezekani wapeperushe bendera ya tanzania kwani wao wana bendera yao kwanini wachukue bendera ya tanzania walitumia iran kukwepa vikwazo vyao kama umoja wa mataifa ungechukua hatua ya kuchukua vikwazo ambao wangeathirika ni watanganyika kwa kiasi kikubwa wangeathirika wao wazanzibar wangekimbilia Oman hakuna haja ya kuwashirikisha
Tena wanapeperusha bndera juu ya tani 30 za bangi. Hakuna tusi zaidi ya hilo.

Akina Masogange wapo jela kwasbabu wana passport ya Tanzania. Wazanzibar wanakusanya pesa za bangi kwa jina lile lile alilotumia Masogange. Hapo kuna haki?

Akina masogange waachiwe huru kwasababu JMT yote inauza mihadarati kupitia meli za SMZ ingawa mshiko unabaki znz.

Ukilipa kodi IMO kudhamini ZMA umedhamini mzigo wa bangi na huna tofauti na Masogange.
Sote tumedhamini uuzaji wa mihadarati kwa kutumia ZMA
 
Hapo ndo unapokuja umhimu wa zanziba kushirikishwa katika huu mchakato wa katiba ilia baadae isije vikatokea visingizio vya kwamba sisi hatukushirikishwa maara sisi koloni la Tananyika kwa mfano zanzibari wana wizara zinazoshughulikia mambo ambayo siyo ya muungano Tanganyika ziko wapi hizo wizara?
Zanzibari kuna baraza la wawakilishi linalojadli mambo ya zanzibari ambayo siyo ya muungano liko wapi bunge la Tanganyika ale Dodoma tunapojadili mambo yasiyo ya muungano kwa nini wale wabunge wanaotokea Zanzibari huwa hawtoki nje? kwa nini washiriki mambo ya Tanganyika wakati sisi hatuna mwakilishi hata mmoja katika baraza la wawakilishi?
 
Waletaka nchi yao siku nyingi tu nyinyi bado mnaikumbatia sasa ndio mtatia akili wale hawana nguvu za kivita kama nyinyi sima watatumia akili ya hali ya juu mpaka mtawapa nchi yao na wale vibaraka wenu wale cufccm wanajua hilo
Mbona wanataka muungano wa mkataba? Kwanini wasiende zao!

Hivi hapa huoni unathibitisha kauli kuwa Zanzibar hainyonywi bali inaionyanya Tanganyika?
Fikiria kabla ya kuandika maana unaweza kutoa majibu tusiyohitaji.
 
Hapo ndo unapokuja umhimu wa zanziba kushirikishwa katika huu mchakato wa katiba ilia baadae isije vikatokea visingizio vya kwamba sisi hatukushirikishwa maara sisi koloni la Tananyika kwa mfano zanzibari wana wizara zinazoshughulikia mambo ambayo siyo ya muungano Tanganyika ziko wapi hizo wizara?
Zanzibari kuna baraza la wawakilishi linalojadli mambo ya zanzibari ambayo siyo ya muungano liko wapi bunge la Tanganyika ale Dodoma tunapojadili mambo yasiyo ya muungano kwa nini wale wabunge wanaotokea Zanzibari huwa hawtoki nje? kwa nini washiriki mambo ya Tanganyika wakati sisi hatuna mwakilishi hata mmoja katika baraza la wawakilishi?
Siyo kwamba hawajui utaratibu ni mazoea ya kutumia jina tu kujisetiri ambako sasa lazima kufike mwisho. Na mwisho wa hayo ni Tanganyika irejee

Kwasasahivi wanakazania sana ulinzi na usalama uwe wa JMT wakijua kuwa kama ilivyo kwa meli za bangi, hili nalo watajificha katika gharama.

Kila siku utasikia wakisema wanataka vyeo husikii hata siku moja mznz akiongelea gharama. Anajua linapokuja suala la gharama hana cha kuchangia na hilo ni zigo la Mtanganyika.

Sasa hivi wana mbinu mpya, wanataka passpor iandikwe Tanzania-Tnganyika na Tanzania-Zanzibar ili kujificha nyuma ya Tanzania na kutumia neno Tanzania wakati wa biashara kama hizi za bangi.

Watanganyika tunayaeleta haya muone wenyewe, msibabaishwe na kelele za wao kudai asilimia 21 ya ajira au kunyonywa, wao ndio wana mirija katika mfuko wako. Wana mirija kwa kodi ya baba na mama yako kule kijijini.
 
Jamani kwani si muaachie wazanzibari nchi yao na kisiwa chao. Mnachong'ang'ania muungano ni kitu gani?
 
ndio maana nawashangaa wale wabunge wanaopinga kuwa zanzibar haikushirikishwa mchakato wa muungano kwani wazanzibar hawapokwa ajili ya muungano ndiomaana wanafanya kila njia tanzania ichafuke haiwezekani wapeperushe bendera ya tanzania kwani wao wana bendera yao kwanini wachukue bendera ya tanzania walitumia iran kukwepa vikwazo vyao kama umoja wa mataifa ungechukua hatua ya kuchukua vikwazo ambao wangeathirika ni watanganyika kwa kiasi kikubwa wangeathirika wao wazanzibar wangekimbilia Oman hakuna haja ya kuwashirikisha
Hili la bangi EU tayari wameshaweka alama kwa Tanzania. Meli inayotoka Tanzania ina walakini, kama si mzigo wa mihadarati ni mbovu.

Sijui wawekezaji wakisikia hata meli zetu haziaminiki tutawavutia kwa lipi.

Hii ni aibu kwa taifa, kwamba JMT inafanya biashara ya mihadarati. Ni JMT kwasababu ndiyo inalipa ada kule IMO.
SMZ na ZMA zinakusanya mapato na faini, Tanganyika inahangaika na mabalaa kama hili la mihadarati
 
Ukweli ni kwamba zanzibar iko kimaslahi kwenye huu muungano. Na ukweli ni kwamba yale yanayoiumiza bara wao huwa hawayapi kipaumbele la wanaona sawa tu.

Waziri wao katuonyesha wazi kwamba hata uelewa juu mahusiano yetu ya majini hayajui na hivyo hajali kwake yeye liwalo na liwe.
Tatizo lake ni kwanini habariimeandikwa magazetini wala si zigo la bangi la tani 30 zilizokamatwa.
 
Jamani kwani si muaachie wazanzibari nchi yao na kisiwa chao. Mnachong'ang'ania muungano ni kitu gani?
Hapana ni wao wanao ng'ang'ania. Sisi tumewapa kila 'maujanja' wao wamekomaa na mamlaka kamili(siyo kujitoa) huku wakisema ulinzi na usalama ni juu ya Mtanganyika.

Leo BAKAZA limetoa maoni kuwa makao makuu ya JMT yahamishiwe Znz eti Tanganyika imekuwa makao makuu tangu mwaka 1964. Tena anayesema hivyo ni profesa Sheriff, hapo ndipo unatakiwa ujue kuna tatizo gani zaidi ya muungano.
 
Ndugu yangu Nguruvi, Zanzibar ni ya Wazanzibari na Tanzania ni ya Watanzania wote; Wazanzibari wanataka kuwa na mamlaka kamili kwa kadiri ya kwamba mamlaka hayo kamili yamejificha ndani ya Muungano. Jambo la kwanza ambalo Wazanzibari walitakiwa kufanya ni kujiunga na chombo cha vyombo vya majini cha kimataifa ili waweke bendera yao halafu waanze kurusha bendera yao.

Ndio maana wengine tulipata ahueni kidogo baada ya tukio la watu kumwagiwa Tindikali vyombo vyote vya kimataifa vilisema hilo limetokea "Zanzibar"! ...
MMM, wao tatizo si tindikali hasa maana wanajua mwisho wa siku jina la JMT ltajitokeza tu. Tatizo lao ni kujificha katika malipo.

Wameondoka na kuunda ZMA kwa mbwembwe sana na wanajua wanapaswa kulipa ada iwe kwa JMT au IMO.
Wameminya tu kwasababu hiyo ni haki ya Mtanganyika, haki yao ni huduma tu.

Utashangaa sasa hivi wanaongelea kugawana vyeo ndani ya JMT, hata siku moja hutasikia wakizungumzia uendeshaji na gharama, hilo ni zigo la Mtanganyika. Wao wanataka mgao 7% wanataka watoto wao wapate mikopo wasiorudisha na wakimaliza watengewe asilimia 21% huko nyumbani wakipanga mikakati wanatumia umeme wa bure n.k.

Halafu ni wazuri wa mdomo, wakikueleza wanavyonyonywa na znz ilivyokuwa nzuri wakati wa utumwa unaweza kutoa machozi. Yaani znz ilikuwa na neema sana ni huu muungano umeharibu kila kitu.

Sisi hatuna njia ila ujio wa Tanganyika ili kila mtu asimamie mambo yake. Sisi tutahangaika na wabeba passport na mihadarati wetu na wao wahangaikie meli zilizosheheni tani za bangi. Kila mtu ale kwa mkono wake habari ya kupakuliana sasa basi.

Tumechoka, watuache tupumue.
 
Muungano huu unafaa kufuata ile China-Hong Kong model.
 
Back
Top Bottom