Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

Sikia maajabu haya ya Mwalimu wa shule ya Kata

We can not speak as native speakers.Mi sioni ajabu huyo mwalimu cha msingi wanafunzi wameelewa na kama hawajaelewa msisitizo utawekwa kwa kiswahili.Mwalimu mwenyewe katoka kwenye mfumo huo huo wa kiswahili as a medium of instruction kwa miaka saba ulitegemea nini hapo.

Sawa kabisa. Si vema kumlaumu. Mimi sina elimu ya chuo kikuu, lakini kwa miaka niliyosoma, wapo wenye digrii wengi tu nawatoa KO kwa Kiingereza wakiwamo wanangu ambao nawasahihisha kila siku. Wamefika chuo kikuu. mimi na form six yangu nawaelekeza. Mfumo umebadilika sana. Kiswahili chenyewe ni shida, itakuwa Kiingereza?
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata. Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED? Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake? Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!

:israel:

Kwani alikuwa anafundisha Grammar? Sasa wewe mwenyewe mwenye elimu kubwa Jografia una "Jiographia" tukueleweje?
 
Umekosea sana kutaja UDSM, mada kama hizi kwenye jina la chuo unatakiwa ukitaje chuo fulani kipo Dodoma :lol:
 
Wachina na wajerumani wenye maendeleo makubwa wanajua Kiingereza ?, pili ushasema ni mwl. wa Geography si kosa lake

Tatu ww kwa siku Kiswahili lugha yako unachapia mara ngapi ?

Nne ; watoto wenu mlokuwa mnawepeleka Kusoma Uganda na Kenya miaka michache ilopita mbona hamuwapeleki baada ya kuona watoto wanaendelea kuwa vilaza Tano Rekebisha ulitaka Mwl. aseme vp.

Mkuu una point.. Na umeweza kuitetea point yako.
 
Mtoa mada sio lazima mwalimu aongee lungha ya kingereza kwa ufasaha ndo wanafunzi wamwelewe, sie tulifundishwa na waholanzi hawajui kingereza vizuri lakin tulikua tunaelewa vema
 
mkuu ulimkagua hadi cheti ukagundua katoka UDSM??
 
Acha hiyo, hivi majuzi Nilijisikia aibu pale UDBS, jamaa yule ni tutor pale, kaongea kingereza kibaya Heri ya huyo mwalimu wa kata. Tatizo hata kwa wakufunzi wao wa vyuoni ni shiida.
 
Kwa watumiaji wa English kama second language na third language makosa hayo ni madogo sana.Kina Maximo na kina Paulsen walikuwa wana Kiingereza kibovu zaidi ya huyo Mwalimu wa Kata(kama ulivyo mwita).Watanzania tuache majivuno na lugha za watu.Tujivunie lugha yetu ya Kiswahili,tuiongee vizuri.Kujisifia Mbongo kuongea kiingereza vizuri ni colonial legacy ambayo haitusaidii.cha muhimu tuwe mahiri kwenye fani zetu tuta ya shinda wanao amini kwenye language fluency badala ya competency
 
Leo nimetembelea shule moja ya Kata nikashuhudia kituko cha mwaka kutoka kwa mwalimu mmoja shuleni hapo.

Mwalimu huyo amehitimu Chuo Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) hivi karibuni na akaajiriwa moja kwa moja kufundisha katika shule hiyo ya Kata. Wakati akiendelea kufundisha nilimsikia akiwauliza wanafunzi swali hili: WHERE DOES IT LOCATED? Inaonekana ni mwalimu wa somo la Jiographia, hivyo alikuwa akiwauliza wanafunzi wake wamtajie location ya kitu fulani kwenye ramani.

Jamani, hapa ndipo shule za kata zilipotufikisha. Ikiwa mhitimu wa Chuo Kikuu anaongea kiingereza kibovu kama hiki, tena mbele ya wanafunzi,mnategemea wanafunzi anaowafundisha watapata maarifa gani kutoka kwake? Chukulia huyu ni mwalimu wa Kidato Cha Kwanza, wanafunzi wake wanaoambiwa kila siku "SPEAK ENGLISH" wataiga kiingereza gani kutoka kwake? Si ndio atawapoteza kabisa?

Ikiwa walimu hawajui kiingereza unategemea nini kutoka kwa wanafunzi wao? Haya ndio madhara ya serikali yetu kuchanganya elimu na siasa. Tumekwisha hasa!!

:israel:

twende polepole ndugu yangu msomi na mjuzi wa kimombo.... "Jiographia" ndio nini? ulimaanisha "Geography?" au "Jiografia?" au "Jografi?" nijib.
 
tpaul,kama sitakosea utakua mpya kwenye tasnia hii.'ORAL LANGUAGE'INAMAKOSA KULIKO WRITEN.WAENDELEZWE KIMASOMO WALIMU.

ni kweli kabisa mkuu. halafu tatizo lingine ni kwamba serikali haiko makini sana katika kuboresha elimu yetu. badala ya kuboresha, wao wamekazana kuibomoa huku wakiwapeleka watoto wao kusoma ulaya na marekani.
 
Sasa mbona kuanzia masomo ya awali mpaka chuo kikuu wanataka iwe kiswahili,kingereza ibaki kuwa lugha ya kigeni si ndo watoto watatoka kapa?
 
Sawa kabisa. Si vema kumlaumu. Mimi sina elimu ya chuo kikuu, lakini kwa miaka niliyosoma, wapo wenye digrii wengi tu nawatoa KO kwa Kiingereza wakiwamo wanangu ambao nawasahihisha kila siku. Wamefika chuo kikuu. mimi na form six yangu nawaelekeza. Mfumo umebadilika sana. Kiswahili chenyewe ni shida, itakuwa Kiingereza?

ni kweli kabisa mkuu. serikali ya CCM imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuharibu na kuizika elimu yetu katika kaburi lenye kina kirefu na bado inazidi kushindilia udongo kwa nguvu ili kuondoa uwezekano wa kufufuka kwa elimu yetu. wakati nasoma darasa la 7 kuna fundi ujenzi aliyeishia darasa la 5 la mkoloni alikuja kujenga darasa shuleni kwetu. basi huyo fundi alikuwa akiongea kimombo kikali na kizuri sana...mpaka tukatamani bora tungezaliwa enzi zake ili tupate elimu ya uhakika. halafu kuna jamaa yangu kamaliza std vii mwaka 1973, wanafunzi waliohitimu form 4 hawampati kwa kiingereza na weledi...huyu mtu anajua kimombo na ni mwerevu na mjuzi wa mambo mengi sana.
 
Kwani alikuwa anafundisha Grammar? Sasa wewe mwenyewe mwenye elimu kubwa Jografia una "Jiographia" tukueleweje?

Sio JOGRAFIA ni JIOGRAFIA. na usifananishe typing errors na grammar errors....ni vitu viwili tofauti kabisa.

CC:mwalimu FaizaFoxy
 
Last edited by a moderator:
Ili mradi ni shule ya kata basi hapo sioni tatizo zaidi ya kumpongeza mwalimu kwa kazi nzuri
 
Umekosea sana kutaja UDSM, mada kama hizi kwenye jina la chuo unatakiwa ukitaje chuo fulani kipo Dodoma :lol:

hahahaha! mkuu una utani mbaya sana. subiri wenye chuo chao waje wakukabe koo.
 
Labda kosa la mtoa mada ni kuita maajabu. Lakini jamani haliondoi ukweli wa kujitahidi na kujifunza lugha hii maana ni muhimu katika nyanda mbalimbali. Watanzania ni watu intelligent saana. Wakati mwingine tunakosa fursa kubwa zaidi za kikazi kwa sababu tu ya lugha. Mi nadhani endapo huko nyuma tulikosa fursa ya kujua kiingereza kwa ufasaha ni vema kutafuta fursa mbalimbali ili kujiendeleza. Nakumbuka wakati ilivyosemwa ajira zinafunguliwa kwa EAC countries tulianza kuhaha kuwa wanakuja chukua kazi zetu. Endapo tulikosea nyuma basi turekebishe ili elimu inayotolewa kuanzia shule za msingi iwe sahihi ili kuepuka bomu la hapo baadae na kuweza kupata fursa za kazi mbalimbali pia.

Asante sana ndugu.
 
twende polepole ndugu yangu msomi na mjuzi wa kimombo.... "Jiographia" ndio nini? ulimaanisha "Geography?" au "Jiografia?" au "Jografi?" nijib.

hili unalolisema halihusiani na mada iliyopo hewani. kuna tofauti kubwa kati ya typing error na grammar error. huyo mwalimu alisikika akiongea, sio KUANDIKA. umeelewa? mtu asiyeoga mwili lakini anafua nguo zake huwezi kumfananisha na mtu anayeoga lakini hafui nguo. hawa ni watu wawili tofauti. kwa hiyo, kuchapia spelling hakuwezi kuwa sawa na kuchapia grammar. umeona eeh? una hoja lakini bado hujaijenga vizuri.
 
hili unalolisema halihusiani na mada iliyopo hewani. kuna tofauti kubwa kati ya typing error na grammar error. huyo mwalimu alisikika akiongea, sio KUANDIKA. umeelewa? mtu asiyeoga mwili lakini anafua nguo zake huwezi kumfananisha na mtu anayeoga lakini hafui nguo. hawa ni watu wawili tofauti. kwa hiyo, kuchapia spelling hakuwezi kuwa sawa na kuchapia grammar. umeona eeh? una hoja lakini bado hujaijenga vizuri.

ni "grammatical error" sio grammar error.. (grammatical=kisarufi...grammar=sarufi)
issue yangu ya jana hukunipatia jibu ujanjaujanja umekuwa mwingi..unazogoa wenzako wakati wajua huu ni ugonjwa wa wengi.. JITETEE NA HILI MKUU
 
Back
Top Bottom