Sijawahi kuona kitu kama hiki

Sijawahi kuona kitu kama hiki

Tofauti ya kipato kati ya walicho nacho na wasicho kimetanuka sana. Hii ikitokea inawafanya watu wengine kukosa utu na kudai kusujudiwa na wale wengine kuudharau utu wao na kujinyenyekesha! Hapa wanataka huruma ya Mama, wanataka awape kitu kidogo na wanaamini anacho.

Mambo yamegeuka sana. Enzi za Ujamaa na Kujitgemea hata asiye nacho alikuwa na sauti. Mwenyekiti wa Nyumba 10 alikuwa na uwezo wa kumshikiza adabu mtu yeyote bila kujali kipata na hadhi yake ndani ya jamii halikadhalika watu wengine. Hapakuwepo na kuonewa kwa kivile, labda uitwe msaliti maana hapo duh kulikuwepo na mamlaka maalum (presidential detention orders).

Hebu fikiria ni baba yako anampigia goti girl ambaye anaweza akawa rika lako!
 
Waliopiga na Waliopigiwa Magoti wote ni Wapumbavu...

Huwezi kumpigia Magoti Binadamu mwenzako kama una akili timamu na si mtumwa..

Huwezi kukubali binadamu mwenzako akupigie magoti kama una akili timamu na si mwehu..
 
Siyo tanzania ya kina mzee Nyari, , urassa, Nkya, shoo, massawe, duh munisi na mushi patachimbika Nk hawa ndio wanaochelewesha maendeleyo
 
Dina hata wimbo style ya kupiga magoti itakuwa ni wimbo wa kuomba msaada au kuomba fadhila na kote huko ni kujidhalilisha haswa huyo babu hapo mbele

Hasa kweli jamani mtu mzima akajitoe ufahamu kufanya hayo....nashukuru ni baba wa mwingine labda mwenye nae ataongea naye...Ila kama yuko kwenye mstari wa nyuma hapo..basi tena!
 
wale wa lumumba mbona siwaoni pande hizi .?????????????
 
Subiri uchaguzi mkuu 2015 utaona sana. Jifanye mwana ccm alafu kuwa mpambe wa mgombea, utaombwa Tsh.mia moja kila kijiji.
 
Wimbo watu huchagua style za kucheza zile za kudhalilisha huwezi kuzifanya.
 
Ni kama anasema eeh mama unitazame mimi na hawa wenzangu katika ufalme wako!
 
Huyo mama ni "Makamu wa Rais"....

Bado Ridhiwani kupigiwa magoti!~
 
Tutarudishwa utumwani bila pingu wala kengele
 
You must be half minded or something wrong with your upstairs. If you know whom you are and value yourself as human being cant do this especially to the politicians,
 
Siyo tanzania ya kina mzee Nyari, , urassa, Nkya, shoo, massawe, duh munisi na mushi patachimbika Nk.
hawa ndio wanaochelewesha maendeleyo
 
Siamini kama hili kweli limetokea katika nchi iliyoonja machungu yote ya 'ujamaa' na 'ubepari (uchwara)'. Ninafikiri ni photoshopping tu.
 
hapana sitaki kuamini kuwa walikuwa wananyenyekea,,,, awalikuwa wanimba wimbo wa kumkaribisha maza! si unaona wote wamenyoosha mikono wakiashiria kuna kitendo kulikuwa kinafanyika zaidi ya kupida magoti!

Ngoja niamini hivyo maana Tz ni zaidi na niijuavyo kwa kweli!
 
Back
Top Bottom