Sijamuelewa CAG, kwamba anataka wastaafu wachangie bima ya afya? Hizi ni akili za wapi? Tukatae Kwa Sauti

Dr Matola PhD

JF-Expert Member
Oct 18, 2010
56,569
93,236
Nimemsikiliza CAG Ikulu Dodoma wakati wa kuwasilisha report yake Kwa Rais nimeshtuka sana.

Moja ya sababu alizozitaja za NHIF kupata hasara ni wastaafu kutibiwa bila kuchangia.

Sasa swali langu Kwa CAG anaelewa kweli maana ya mstaafu? Hii nchi yetu ina laana gani? Ni Kwa nini watu wakiwa kwenye maofisi hawafikirii maisha ya wastaafu?

Tanzania kamwe Mungu hawezi kuibariki kama itaendelea kutowathamini wazee.

Hawa watu ni wa kukemewa vikali, madhara ya kuwakalia kimya watakuja na Sera ya wazee kuchangia matibabu Kwa kisingizio wanaitia hasara NHIF wakati ujana wao wote wametumika serikalini na sasa wamejichokea nyumbani CAG anataka wanyang'anywe hata haki ya matibabu, hii ni roho mbaya na ubinafsi uliopitiliza.

Tuseme Kwa Sauti Kwa hili hapana mnatafuta laana.

Wajifunze nchi za ulaya na Marekani serikali zao zinatowa ajira kabisa Kwa watu wa kulea wazee Sisi Tanzania tunataka kuwauwa kabla ya siku zako, tulikatae wazo ovu la CAG.
 
Hao wazee kwanza Ni wachache Sana na hawaugui wote kwa mkupuo wapamoja...

Wazee wastaafu kwa rasilimali zote tulizo nazo kweli?? Ni sahihi kwa serikali yetu kulalama na makelele ??!!?!!

NB:
Mfano kwanini serikali ya Tanzania ikizielekeza kampuni kubwa let say 50 companies kupitia
CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITY (CSR)
Mbona ingepata pesa ya ku TOP UP Kama kukitokea deficit

Serikali inabidi wawe wabunifu kalagha bao!!!
 
Nimemsikiliza CAG Ikulu Dodoma wakati wa kuwasilisha report yake Kwa Rais nimeshtuka sana.

Moja ya sababu alizozitaja za NHIF kupata hasara ni wastaafu kutibiwa bila kuchangia.

Sasa swali langu Kwa CAG anaelewa kweli maana ya mstaafu? Hii nchi yetu ina laana gani? Ni Kwa nini watu wakiwa kwenye maofisi hawafikirii maisha ya wastaafu?

Tanzania kamwe Mungu hawezi kuibariki kama itaendelea kutowathamini wazee.

Hawa watu ni wa kukemewa vikali, madhara ya kuwakalia kimya watakuja na Sera ya wazee kuchangia matibabu Kwa kisingizio wanaitia hasara NHIF wakati ujana wao wote wametumika serikalini na sasa wamejichokea nyumbani CAG anataka wanyang'anywe hata haki ya matibabu, hii ni roho mbaya na ubinafsi uliopitiliza.

Tuseme Kwa Sauti Kwa hili hapana mnatafuta laana.

Wajifunze nchi za ulaya na Marekani serikali zao zinatowa ajira kabisa Kwa watu wa kulea wazee Sisi Tanzania tunataka kuwauwa kabla ya siku zako, tulikatae wazo ovu la CAG.
Bima ya afya na Medicare pia unachangia kabla ya kustaafu.

Sometimes inaitwa social security & medicare. Yote unakatwa ukiwa unafanya kazi na bima ya Afya ni lazima ununue private au Obamacare ya serikali, ila kama huna kipato na una watoto unapewa medicare (free).

Tanzania sasa hivi unaweza kupata quality healthcare kama una hela, ila wengi hawana hela na serikali haiwezi kuwalipia.

Mtu anataka upasuaji wa moyo akiwa miaka 60, zamani hiyo ni service wanayopata mawaziri tena nje ya nchi.

Siku hizi watu wa kawaida wanapata huduma hizo wakiwa wamestaafu, lakini hawajawahi kuchangia walipokuwa wanafanya kazi. Hii inazalisha deficit kwenye mfuko wa bima.

Itachukua miaka karibu 20 kabla ya deficit hiyo kuondoka kwa sababu kizazi cha NHIF ya lazima, bado hakijastaafu ndiyo kwanza kinakunywa bia na kula nyama choma. Wakizeeka na kuwa bed ridden, angalau watakuta mfuko wa NHIF umetengemaa, iwapo tu hakutakuwa na ubadhirifu.

So, he stated facts.
 
Back
Top Bottom