Habari zenu wanajamii forum
Katika harakati za kutafuta binti anayeendana na sifa zangu nazotaka, eeh bwana macho yangu yakatua kwa binti mmoja wa kinyaturu ambaye nimekutana anaye hapa Moshi, Kilimanjaro. Yaani kwa kumwangalia ni mpole hana mambo mengi na kizuri nilichokipenda alikuwa muda wote anashinda kanisani, tena moja ya kanisa la kilokole na muda wote anaimba mambo ya Mungu.
Basi nikaanza harakati za kumfatilia maana kwa mimi ninaona kabisa ni aina ya mke nayemhitaji, basi bwana kama tabia ya wanawake ilivyo alinisumbua sana mpaka kumpata sasa mwaka jana mwisho nikafanikiwa kumiliki lakini sasa nimeanza kuona tabia zake sio kabisa.Kwanza ana kiburi kisicho na mfano na kitu cha pili nimegundua ana connection ya wanaume wengi sana japo ni msiri sana.
Kitu kingine nimegundua anapenda maisha ya juu sana kuanzia nimeanza kuwa naye, Pamoja na hilo mavazi anayovaa anapenda yale yanayo take attention kwenye jamii,yaani anavaa vimini huku mtaani ya nguo za kubana makalio mpaka najiuliza huyu sijui anasali nini yeye anadai yeye ni kijana wa kisasa na amenionya nisimfatilie maana nitaumia sana ana mambo mengi
Jamani nimeamini wanawake wapole wana siri nzito sana.Naombeni ushauri wadau niendelee naye au nifanyeje???[/QUOTE Mkuu ulikuwa unaangalia cover la nje la kitabu kabla ya kukisoma kujua yaliyomo,but nadhani umejifunza kitu