Shule ya Turkish Maarif School Arusha ni tatizo

Shule ya Turkish Maarif School Arusha ni tatizo

Mh. Waziri,

Shule zimefunguliwa juzi, hii shule imekataa kupokea wanafunzi kwa madai hawajalipa ada. Wanafunzi waliotoka mikoani wanarudishiwa getini.

Nijuavyo mimi, wanafunzi hawajaingia mkataba na shule, bali tatizo ni mzazi na utawala wa shule. Nashauri kabla shule haijapatiwa kibali iwe inachunguzwa malengo yake. Hii shule ya Waturuki wana hujumu juhudi kubwa za serikali kukuza elimu.

Naomba Mh. Waziri fuatilia hii shule kwa karibu. Pia wananchi wanataka kujua waliwezaje kuchukua hili eneo na kilikuwa kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum. Eneo lilitolewa na serikali kwa minajili hiyo na sio biashara ya shule.
Bila ada walimu watalipwa nini, chakula chao umeme, na uendeshaji utafanyikaje. Tupunguze lawama
 
Mh. Waziri,

Shule zimefunguliwa juzi, hii shule imekataa kupokea wanafunzi kwa madai hawajalipa ada. Wanafunzi waliotoka mikoani wanarudishiwa getini.

Nijuavyo mimi, wanafunzi hawajaingia mkataba na shule, bali tatizo ni mzazi na utawala wa shule. Nashauri kabla shule haijapatiwa kibali iwe inachunguzwa malengo yake. Hii shule ya Waturuki wana hujumu juhudi kubwa za serikali kukuza elimu.

Naomba Mh. Waziri fuatilia hii shule kwa karibu. Pia wananchi wanataka kujua waliwezaje kuchukua hili eneo na kilikuwa kituo cha kulelea watoto wenye mahitaji maalum. Eneo lilitolewa na serikali kwa minajili hiyo na sio biashara ya shule.
tatizo lipo, kuna baadhi ya wazazi hawataki kulipa ada ya kipindi watoto walikuwa likizo ndefu, ati kwani walisoma? wamesahau kuwa hata kama ni likizo waalimu huwa wanalipwa mshahara kila mwezi. mihula yote 4 lazima ulipe ada as long as mtoto wako yupo shule fulani. binafsi sijataka ubishi kwenye hilo, nimelipia watoto wangu wote ada bila ubishi. swali ni je? hiyo Turkish school wanarudisha watoto wote hata wale waliolipa au ninyi wabishi tu? na ni lazima asome hapo, si umuhamishe peleka kwenye shule za kachumbari huko kama uwezo huna? unafikiri kwa akili yako kweli waziri atapoteza muda wako kuingilia biashara ya mtu ya shule? hiyo ni biashara sio huduma, huduma nenda shule za kayumba.
 
Mtu anakuambia ntatoa mwezi ujao kwani ni mkopo huo?
Walishasema muende na Ada
ati anasema atatoa mwezi ujao, atangulize hata nusu basi ndio aanze kulialia, waalimu watalipwaje sasa, wakigoma kufundisha si ndio mtoto wake hatafundishwa kabisa? mafuta ya magari kubeba wanafunzi n.k. peleka mtoto shule ambayo una uwezo nayo. sisemi hivi kwasababu mimi Mungu amenisaidia nimelipa, Mungu awasaidie, najua maumivu ya kukosa ada ya watoto na namna tunavyopenda kuwasomesha watoto wetu shule nzuri hata kama hatuna hela.
 
Wanawake ndio wanaowaingiza mkenge wanaume kuingiza Watoto shule za Kingereza bila kujari uwezo halisi wa familia.

Wanaume wengi wamegeuzwa mateka na wake zao mbele ya familia, mama anatafuta shule ghari Baba utowe pesa ya ada.

Kwakweli inatia huruma 80% ya wanaosomesha Watoto shule za Kingereza hawana uwezo huo, ni kujiumiza tu.
Na wao wanakubali kuburutwa kama mbuzi wa maziwa!!?????. Kwanini wasiwe na misimamo kulingana na uhalisia wa kipato walichonacho???????

Siishi kwa kumuiga fulani, kwake ni kwake na kwangu ni kwangu ,kwishaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shule zote nchini zimefunguliwa jana, hii shule iko Ngaramtoni Arusha, inamilikiwa na Waturuki.

Viongozi wa shule wanawarudisha watoto kisa ni ada. Kuna watoto wametoka Manyara wamerudishiwa getini.

Wizara ya Elimu angalieni hii shule. Angalieni dhima ya mnaowapa vibali vya kuendesha shughuli za elimu hapa Tanzania.

Baadhi ya wazazi wameshalipa zaidi ya nusu ya ada ya mwaka lakini watoto wanarudishiwa getini. Siamini kwamba huu ni utaratibu mzuri.

Mtoto ana kosa gani?

Utawala unatakiwa kuangalia utaratibu mzuri na wazazi na sio kuwatesa watoto.
Mkuu pole

Ila ni utaratibu wa shule zote binafsi. Hata mtoto angetokea Mwanza angerudishwa tu sembuse Manyara. Ustaarabu ni ungeongea na mkuu wa shule kabla hujampeleka mtoto bila risiti ya Ada.

Pole mkuu Mungu akujalie upate ada.
 
ati anasema atatoa mwezi ujao, atangulize hata nusu basi ndio aanze kulialia, waalimu watalipwaje sasa, wakigoma kufundisha si ndio mtoto wake hatafundishwa kabisa? mafuta ya magari kubeba wanafunzi n.k. peleka mtoto shule ambayo una uwezo nayo. sisemi hivi kwasababu mimi Mungu amenisaidia nimelipa, Mungu awasaidie, najua maumivu ya kukosa ada ya watoto na namna tunavyopenda kuwasomesha watoto wetu shule nzuri hata kama hatuna hela.
Nina vitoto viwili vya mwisho shule yao wametugea namba ya Airtel money kabisa siyo lazima uende bank, unapunguzapunguza na mhasibu yuko vizuri kutunza rekodi.

Kwahiyo ukijipanga hupati maumivu ya kutowa mihela Mingi Kwa pamoja.
 
Mkuu pole

Ila ni utaratibu wa shule zote binafsi. Hata mtoto angetokea Mwanza angerudishwa tu sembuse Manyara. Ustaarabu ni ungeongea na mkuu wa shule kabla hujampeleka mtoto bila risiti ya Ada.

Pole mkuu Mungu akujalie upate ada.
Na walivyo washenzi ukipeleka mtoto unaambiwa asubili nje ya geti, upeleke risiti Kwa mhasibu akupe risiti ya shule na gate pass ndio umpe mlinzi gate pass aruhusu mtoto wako kuingia ndani ya compound.
 
kama huna ada peleka mwanao shule ya kata hapo jirani na nyumbani.
 
kutokuwa na ada inauma sana, mpeni pole. ila huwa najaribu kufikiri mimi ningemiliki shule, hapo nina waalimu wanataka mshahara, nina madereva wanataka mshahara, nina magari ya kubeba hao wanafunzi yanataka mafuta, na nategemea faida kidogo juu niipate, halafu kuna mtu analeta mtoto wake na kusema hana ada nimsubiri...ungejisikiaje? hao wote wanaodai mishahara na gharama hizo wanakusubiri tu hawawezi kukuelewa ukisema wasubiri. ama la watakukimbia wote.
 
Shule zote nchini zimefunguliwa jana, hii shule iko Ngaramtoni Arusha, inamilikiwa na Waturuki.

Viongozi wa shule wanawarudisha watoto kisa ni ada. Kuna watoto wametoka Manyara wamerudishiwa getini.

Wizara ya Elimu angalieni hii shule. Angalieni dhima ya mnaowapa vibali vya kuendesha shughuli za elimu hapa Tanzania.

Baadhi ya wazazi wameshalipa zaidi ya nusu ya ada ya mwaka lakini watoto wanarudishiwa getini. Siamini kwamba huu ni utaratibu mzuri.

Mtoto ana kosa gani?

Utawala unatakiwa kuangalia utaratibu mzuri na wazazi na sio kuwatesa watoto.
Mtoto hana kosa ila anateseka kwa makosa anayofanya baba yake, LIPA ADA!!
 
Shule zote nchini zimefunguliwa jana, hii shule iko Ngaramtoni Arusha, inamilikiwa na Waturuki.

Viongozi wa shule wanawarudisha watoto kisa ni ada. Kuna watoto wametoka Manyara wamerudishiwa getini.

Wizara ya Elimu angalieni hii shule. Angalieni dhima ya mnaowapa vibali vya kuendesha shughuli za elimu hapa Tanzania.

Baadhi ya wazazi wameshalipa zaidi ya nusu ya ada ya mwaka lakini watoto wanarudishiwa getini. Siamini kwamba huu ni utaratibu mzuri.

Mtoto ana kosa gani?

Utawala unatakiwa kuangalia utaratibu mzuri na wazazi na sio kuwatesa watoto.
Gharama za Kufundishia hao wadau wanatoa wapi kama sio Karo ?

Mtoto hana kosa ila mzazi ndio ana Kosa..., Kwanini Mzazi umpeleke mtoto huko kama unaona ni gharama ?, Si umpeleke kwenye Shule Nyingine ?

Huwezi kujua huenda wenye shule wameweka rehani assets zao wana madeni mpaka kwenye kope na usiku hawalali kwa stress..., Its a contract kama ulikubali kulipa Karo na mda umefika Haulipi usilaumu sana sana kaa nao mezani uwaombe ki-ubinadamu wakufikirie
 
Wabongo wengi ni mabogas sana,ina maana mnaomponda mtoa hoja mnataka kusema hana logic???
 
Back
Top Bottom