Nusu ada mwezi wa tisa? Kwani umelazimishwa? Mtoe mtoto wako mpeleke kwenye bureShule zote nchini zimefunguliwa jana, hii shule iko Ngaramtoni Arusha, inamilikiwa na Waturuki.
Viongozi wa shule wanawarudisha watoto kisa ni ada. Kuna watoto wametoka Manyara wamerudishiwa getini.
Wizara ya Elimu angalieni hii shule. Angalieni dhima ya mnaowapa vibali vya kuendesha shughuli za elimu hapa Tanzania.
Baadhi ya wazazi wameshalipa zaidi ya nusu ya ada ya mwaka lakini watoto wanarudishiwa getini. Siamini kwamba huu ni utaratibu mzuri.
Mtoto ana kosa gani?
Utawala unatakiwa kuangalia utaratibu mzuri na wazazi na sio kuwatesa watoto.