Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Kwa heshima kubwa tunapenda kutoa shukrani zangu pekee kwa wana JF ambao kwa namna moja au nyingine walishiriki nasi katika kutufariji katika kipindi kigumu cha kuondokewa na mama wa mke wangu na mama mkwe wangu.
Marehemu mama mkwe alifariki Jumanne tarehe 30/4/2013 na kuzikwa Ijumaa tarehe 3/5/2013 mkoani Kilimanjaro. Mama Mkwe amefariki akiwa na umri wa miaka 79 na ameacha mume na watoto 9, watoto wa kiume watano na wa kike wanne, pamoja na wajukuu 16. Shukrani za pekee zimuendee Bwana Mwita Maranya kwa kutoa taarifa kwa wana JF kuhusu msiba tuliyoupata. Tangu kuwekwa kwa taarifa hiyo, hapa JF nilipokea simu nyingi sana na ujumbe wa simu ya mkononi kutoka kwa wadau mbalimbali wa JF wakitupa pole na kutufariji.
Shukrani zangu ziwaendee wana JF wote kwa umoja wao na ushirikiano. Nisingependa kutaja jina la kila mmoja ili kuonyesha shukrani zetu lakini naomba nitambue ushiriki wa hawa wafuatao ambao walishiriki nasi bega kwa bega katika msiba wa mama yetu mpendwa.
Tunapenda kutambua ushiriki wa Pasco, Mwita Maranya, Maxence Melo, Asnam, Kipipi, charminglady, Bujibuji, Kipaji Halisi, Mentor, Madame B, sweetlady, Paloma, FirstLady1, Mamndenyi, King'asti, Bishanga, AshaDii na KOKUTONA.
Pia tungependa kutambua ushiriki wa KakaKiiza, Babu DC Dark City, BAK, Ruttashobolwa, Zahra White Kaizer mdida ZeMarcopolo, Boflo, Kiranga, TIQO, sakapal, Neylu, Nivea, Chauro, Preta, LiverpoolFC, Arushaone, Mungi, Don Mangi, Erickb52, kitalolo, marejesho, Blaki Womani, platozoom, Jackbauer, nitonye, Samaritan, Dingswayo, kuberwa, Somoche, Tized, Toria, @RR, @FP, Borat69, Mtoto halali na hela, MankaM, UmkhontoweSizwe, Baba V, Chum Chang, Lady doctor, Mayasa, Mzee wa Rula, Katavi, bucho, Passion Lady, BADILI TABIA, Lyagwa, saragossa, Mwanaweja, mwaJ, Swts, neggirl, Chocs, Teamo, Angelicious, jeneneke, queeny, vanmedy, MMAHE, MY LOVE, Mrembo by Nature, PakaJimmy, Lokissa, Jiwe Linaloishi, ram, kabanga, Tetra, Ndoa, Munkari, MziziMkavu, Zion Daughter, raiza, Elizabeth Dominic, mimisa, Mr Rocky, ladyfurahia, snowhite, HorsePower, jouneGwalu, idawa, Thanda, Rich woman, ndetichia, moto2012 na wengineo ambao walishiriki nasi kwa njia moja ama nyingine.
Tunasema ahsanteni sana.