Ndiyo wakuu! Heshima kwenu! Natambua uwepo wenu hapa JF. Ninaomba kukishauri chama changu cha CDM kumtimua Zitto haraka. Sababu zifuatazo:-
Mosi siku zote amekuwa mtu wa kuanzisha chokochoko na asiyeeleweka. Katika nafasi yake aliyonayo katika chama alipaswa awe mtu wa kukijenga chama siyo kubomoa. Kwa MFANO:- Wakati chama kinapambana ili kulinyakua jimbo la Arumeru mashariki kwa Joshua Nasari Zitto akaona ili kukivuruga chama aufanye huo ni muda wa kukivuruga chama kwa kutangaza kugombea Urais.
Pili huwa hashiriki katika kazi za chama kikamilifu. Siku zote amekuwa akionyesha kushiriki shughuli za chama kwa manati.
Tatu, amekuwa akipingana na maamuzi ya chama Tena waziwazi. Akiwa kama kiongozi alipaswa awe mstari wa mbele kupigania na kuyatetea maamuzi ya pamoja ya chama. Kwa mfano siku ile bungeni wezake wanatoka kwa kuonyesha kutorizika na matokeo yaliyompa ushindi kiwete yeye hakufika kabisa bungeni kuonyesha kutokubaliana ma maamuzi ya chama.
Nne, ana makundi ya sirisiri ndani ya chama yanayolenga kuwabomoa wapinzani wake kitu amabacho kinaweza kuvuruga chama pia
Tano, Mshirikina. Siku zote uchawi ndiyo limekuwa tumaini lake. Si mara ya kwanza kwa huyu ndugu kusema ameaga kwao................ Hizo zote ni tambo za kishirikina. Katika karne hii hayo mambo ya kishirikina yamepitwa na wakati.
NB:- Wamekuja wakina Pro. Safari ndani ya muda mfupi wamekisaidia sana chama lakini zitto ana lengo la kukivuruga chama. Naomba zitto atimuliwa.