the ultimatum
JF-Expert Member
- Dec 16, 2012
- 408
- 118
Tusivuruge chama kwa kumfukuza Zitto, yaliyotokea ni masuala ya kuzungumzika kwny meza moja.
Ndiyo wakuu! Heshima kwenu! Natambua uwepo wenu hapa JF. Ninaomba kukishauri chama changu cha CDM kumtimua Zitto haraka. Sababu zifuatazo:-
rais.
kukivuruga chama. Naomba zitto atimuliwa.
kila kitu zitto, ebu muacheni apumzike jamani, hili jambo tayali lipo katika ngazi ya chama kwa utatuzi wa mgogoro uliojitokeza.
Ni pia ni mchawi mkubwa hata panya anaweza kuwaua kimazingara.zitto ni popular humu na mtaani ,haipiti siku hajatajwa
mnataka wabaki kina mangi tu?????acheni hizo bana!Zitto ni jembe ambalo mpaka kesho CDM inalitegemea!!
Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
Ni pia ni mchawi mkubwa hata panya anaweza kuwaua kimazingara.
Hiyo ndiyo kazi ya Zitto na bado mtakimbia mwakani.Zitto kabwe hagombee ubunge tena anautaka urais ila namuomba atuambie ninani anataka aongoze jimbo maana hawa ADC hapa kigoma ni hatariiiiiiiiiii wameshabeba vijiji takribani vyoteeee zitto imarisha chama jimboni kwako achana na hao wapiga kelele
Hata sisi wanaCCM tunathamini mchango wa Zitto ndani ya CHADEMA.Mshauri baba yako amtimue mama yako. Kwetu wanachadema Zitto tunahitaji mchango wake
Kivipi?Watu wa aina hiyo lazima wawepo kwenye chama.pamoja na matatizo yao lakini wanafaida pia kwenye chama.
zitto yupo akilini mwao kila muda
Zitto hajawahi kuwa mwanaCCM hata siku moja, siku zote amekuwa mwanaCHADEMA.Kazi uliyoifanya umemaliza na haujafanikiwa rudi kwa magamba wenzio kawaeleze ZZK ni moja kati ya nguzo za CDM hatakaa aondoke kwa ushawishi maandazi wala kufukuzika. Wape taarifa na kina Kalafurira CHAUMA ilitaka kutokea mgongo wa CDM wamekwaa kisiki
Meza moja ipi? Chadema? Masalia? Uchawi?Tusivuruge chama kwa kumfukuza Zitto, yaliyotokea ni masuala ya kuzungumzika kwny meza moja.
Ndiyo wakuu! Heshima kwenu! Natambua uwepo wenu hapa JF. Ninaomba kukishauri chama changu cha CDM kumtimua Zitto haraka. Sababu zifuatazo:-
Mosi siku zote amekuwa mtu wa kuanzisha chokochoko na asiyeeleweka. Katika nafasi yake aliyonayo katika chama alipaswa awe mtu wa kukijenga chama siyo kubomoa. Kwa MFANO:- Wakati chama kinapambana ili kulinyakua jimbo la Arumeru mashariki kwa Joshua Nasari Zitto akaona ili kukivuruga chama aufanye huo ni muda wa kukivuruga chama kwa kutangaza kugombea Urais.
Pili huwa hashiriki katika kazi za chama kikamilifu. Siku zote amekuwa akionyesha kushiriki shughuli za chama kwa manati.
Tatu, amekuwa akipingana na maamuzi ya chama Tena waziwazi. Akiwa kama kiongozi alipaswa awe mstari wa mbele kupigania na kuyatetea maamuzi ya pamoja ya chama. Kwa mfano siku ile bungeni wezake wanatoka kwa kuonyesha kutorizika na matokeo yaliyompa ushindi kiwete yeye hakufika kabisa bungeni kuonyesha kutokubaliana ma maamuzi ya chama.
Nne, ana makundi ya sirisiri ndani ya chama yanayolenga kuwabomoa wapinzani wake kitu amabacho kinaweza kuvuruga chama pia
Tano, Mshirikina. Siku zote uchawi ndiyo limekuwa tumaini lake. Si mara ya kwanza kwa huyu ndugu kusema ameaga kwao................ Hizo zote ni tambo za kishirikina. Katika karne hii hayo mambo ya kishirikina yamepitwa na wakati.
NB:- Wamekuja wakina Pro. Safari ndani ya muda mfupi wamekisaidia sana chama lakini zitto ana lengo la kukivuruga chama. Naomba zitto atimuliwa.
Zitto hajawahi kuwa mwanaCCM hata siku moja, siku zote amekuwa mwanaCHADEMA.
Huku CCM hatutaki washirikina kabisa, ufisadi mwenyewe bado unatusumbua sana.
Aendelee na CHADEMA yake huko huko alipojifunzia Ushirikina ama mkimzingua aende kule kwa Kafulila yaani CHAUMA.