Shoka la TRA latua CHADEMA

Shoka la TRA latua CHADEMA

Je ile bajeti ya vitafunwa pale Ikulu imeshalipiwa kodi?
 
Je ile bajeti ya vitafunwa pale Ikulu imeshalipiwa kodi? kwakua katika ilani yetu tulishasema tukiingia madarakani tu tunafuta hiyo bajeti kwakua inazidi hata mshahara wa JK na baraza lake.
 
Kwa chama cha siasa au mwanasiasa kutolipa kodi ni jambo la aibu sana!!...kuhusu hayo maswali mengine,mimi naona ni sawa na kumkatalia mtu mwingine asijikinge na jua kwa kutumia kivuli chako....it won't solve your problem!

Tatizo ukikomalia dr slaa anayoita posho. TRA wataulizwa wamekusanya shilingi ngapi kutoka wenye sitting allowance za wajumbe wa bodi, wabunge, mashiria ya umaa na hata over time wanazolipwa wafanyakazi wa serikali zinazozidi mishahaar yao hata mara mbili .


I can See kama chadema wanadiwa milioni 100 basi TRA watachota mapeza mengi utoka kwa hawa

  • bunge linaweza kudaiwa mapesa kibao.
  • Mashirika kama NSSF, PPF BOT, TANROADS
  • Wizara na idara za serikali kutoana na honoraium wanazowalipa wafanyakazi
Kama wako serious basi tuwatakie kazi njema ma mafanikio mema otheriwise TRA wameamua kuingia kwenye siasa.

kama wanatafuta jinsi ya kufidia deficit ya makusanyo yaliungua kutokana na mgao basi wanatakiwa kuwa ctreatve beyond kuchokonoa vyama vya siasa
 
Swali:Chadema walikuwa wanalipa kodi?.....Huu ni ufisadi wa hali ya juu,kuweni mfano bora jamani dah!!!

@Kobello, ni lini TRA waligundua kuwa CHADEMA hawalipi kodi? Why now? Wamefanya audit kwa vyama vingapi au tuamini kuwa vyama vyote vinalipa kodi except CHADEMA? Kwa uwezo wao huo wa kufuatilia mambo TRA wanaweza kutumbia ni nani mwingine hajalipa kodi?
 
Thats not the issue at all!!! you dont break the law just bcoz somebody did.
Kwani kuna statue of limitation kwenye tax issues?
Kuhusu hayo maswali mengine,I don't know.They are irrelevant though!
 
Hela ya uchaguzi IGUNGA inatafutwa kwa njia yoyote na moja wapo ni hii.
 
CHADEMA lazima kilipe kodi.Tunajua wapo watu,makampuni mbali mbali yanakwepa kulipa kodi lakini hiyo si sababu itakayozuia CHADEMA isilipe kodi.
 
Nyie watu mbona ni waajabu hivi. Kisa chadema wameambiwa walipe kodi imekuwa nongwa. ingeambiwa cuf, tlp au ccm ungeona jinsi TRA inavyosifiwa. lakini chadema no, ni kupinga kila kitu. Narudia kusema nyinyi ni watu wa ajabu sijapata kuona kwenye hii dunia.
chadema lipeni kodi. pia TRA nendeni kaangalieni maeneo mengine yanayosemwasemwa kuwa na loophole za ukwepaji wa kodi kama mlivyoziba hii ya chadema.
 
Thats not the issue at all!!! you dont break the law just bcoz somebody did.
Kwani kuna statue of limitation kwenye tax issues?
Kuhusu hayo maswali mengine,I don't know.They are irrelevant though!

Hahha Mwanzo mzuri tunategema tutasikia maagiz waliyopwa pewa CHADEMA wanapewa pia

  • TRA wenyewe, BOT, NSSF, PPF, TANROADS, BIMA ya AFYA hasa kwenye zile posho, bonus na vikao vya bodi wanavyolipana.
  • Posho za overtime za Wizara na Idara za serikali
  • Posho za wabunge na kamati za bunge
Kama si siasa basi tutarajie deficitt ya mgao wa umeme itafidiwa na vyanzo hivi........
 
Lazima tudhibiti wakwepa kodi ili kukuza uchumi wetu.

Kweli kabisa. Mjenga nchi ni mwananchi na vivyo hivyo mbomoa nchi. Wameanza na Chadema na wengine watafuata.
 
Hahha Mwanzo mzuri tunategema tutasikia maagiz waliyopwa pewa CHADEMA wanapewa pia

  • TRA wenyewe, BOT, NSSF, PPF, TANROADS, BIMA ya AFYA hasa kwenye zile posho, bonus na vikao vya bodi wanavyolipana.
  • Posho za overtime za Wizara na Idara za serikali
  • Posho za wabunge na kamati za bunge
Kama si siasa basi tutarajie deficitt ya mgao wa umeme itafidiwa na vyanzo hivi........

Kwa bahati mbaya huko ulikokusema kote wamekuwa wakitekeleza jukumu hilo toka siku nyingi sana.
 
wanaotakiwa kulipa kodi hii inayoongelewa (PAYEE) ni wafanyakazi wala si chama au taasisi! Hapo ndo tunapopotoshana....Anayelipa kodi ni mwajiliwa na si mwajili.Sasa mbona wanaituhumu chadema wakati wao(CHADEMA) ni waajili tu?

Wakuu,

Tuache politics hata kwenye mambo ya maana kwenye ustawi wa nchi yetu. Suala la kulipa kodi ni wajibu wa kila mtu na kila mwajiri kuhakikisha anafikisha kodi ya wafanyakazi wake TRA. Kitendo cha chama cha siasa chochote kile kutokulipa kodi ni cha kusikitisha sana.

Inapotokea kwamba hata watu wanaotaka kuwa viongozi wa nchi yetu hawalipi kodi kwa visingizio vyovyote vile ni jambo la kusikitisha mno. Mimi namwelewa Dr. Slaa na mapambano yake dhidi ya ufisadi. Hata siku moja nisingetegemea Dr. Slaa apokee mshahara wake bila kulipa kodi. Ningetegemea awe na mjanja vyakutosha na kusema hapana, hapa kuna tatizo.

Kwa sheria zet za kodi wenye kosa hapa ni CHADEMA maana kama mwajiri lazima uhakikishe kila mfanyakazi analipa kodi. Lakini pia mwajiriwa una hata moral responsibility ya kuzijulisha mamlaka husika pale unapoona jambo fulani haliko sawa.

Arguments nyingi tunazotoa hapa ni shallow mno kwa maana ya kwamba kujifanya hujui sheria si utetezi kwenye mambo ya sheria. Ninaamini CHADEMA, CCM na vyama vingine vina watu wenye elimu zao na ambao wanajua kwamba ni wajibu kwa kila raia mwenye kipato kulipa kodi.

TRA imeshindwa kazi na is not fit for purpose. Inakuwaje kwa miaka yote hii wameshindwa kujua kwamba vyama vya siasa vina mapato ya kutosha kwa wafanyakazi wao kulipa kodi? Inakuwaje miaka yote hii wameshindwa kukusanya hata senti tano kutoka CHADEMA?

Je kuna vyama vingapi vingine ambavyo havilipi kodi? Kuna watu wangapi wengine ambao hawalipi kodi? Haya mambo yanafanyika wakati Machinga na wauza vitumbua mitaani wanalipishwa kodi kupitia leseni. Iweje hawa watu ambao wana mapato kidogo sana wanalipa kodi wakati wenye mamilioni hawalipi kitu? Huyo CEO wa TRA anaendelea kupewa muda wa kuongoza shirika kwa mafanikio gani wakati Watanzania wengi tu wenye mapato hawalipi kodi?

TRA ni failure na kuna haja ya kuifanyia mabadiliko makubwa ili kodi ikusanywe hasa kutoka kwa matajiri mbalimbali ambo wanakwepa kulipa kodi.

Kule kwetu Kyela sisi tulipoanza biashara, moja ya majukumu niliyowapa vijana ilikuwa ni kuonana na TRA na kujadiliana nao juu ya nini tunatakiwa kufanya kwenye suala la kodi. Sisi tuna majengo pale tunakodisha vyumba vya biashara, mikataba yote tunaipeleka sisi wenyewe kwa hiari yetu TRA na kuhakikisha 10% withholding tax ya pango inapelekwa.

Hata tulipoanza biashara zingine tumeenda kuwaona na wametupa ushauri mzuri tu na kutushukuru kwa kutambua umuhimu wa kulipa kodi. Kwa nilivyowaona mimi tungeweza kuendesha biashara zetu bila kulipa kodi kama tungelitaka. Lakini kama ni mfanybiashara ni muhimu kuwa na uhusiano mzuri na mamlaka ya kodi.

Hata ukiwa na matatizo ni kuwaambia ili waone kama wanaweza kukusaidia. Kama umejenga uaminifu kwao nina uhakika hata kama una shida kuna nafasi kubwa ya kukuelewa na kukuruhusu kuchelewa kupeleka kodi au kulipa taratibu.

Ningependa kuona vyama vya siasa vyote vinatoka clean kwenye hili. Wahakikishe wafanyakazi wao wote pamoja na vifaa vyote vinavyonunuliwa kwamba vinalipiwa kodi. Vinginevyo wananchi tusahau kupata nafuu yoyote kutoka kwa hawa viongozi wetu. Binafsi ningependa TRA iunde tume ambayo ipite kwenye kila chama na kuhakisha wanakagua mahesabu yao yote na kuangalia wapi wanakwepa kodi.

Adhabu ya 100m kwa kushindwa kulipa kodi kwa miaka 11 ni ndogo sana. Kuna haja ya kuwafilisi na kuwapeleka jela wale wanaoshindwa kulipa kodi kama wanavyofanya Wajerumani na hii ndio itafanya watu wawe waoga.
 
wanaotakiwa kulipa kodi hii inayoongelewa (PAYEE) ni wafanyakazi wala si chama au taasisi! Hapo ndo tunapopotoshana....Anayelipa kodi ni mwajiliwa na si mwajili.Sasa mbona wanaituhumu chadema wakati wao(CHADEMA) ni waajili tu?
Lakini mwajiri ndiyo mwaenye jukumu hili ingawa inakatwa kwenye msharaha wa mfanyakaz mfano mimi sikumbuki kuchukua pesa na kupeleka TRA kwaajiri ya mshahara wangu ila huwa naona kila mwezi kwenye vikaratasi kuwa nimelipa kodi au hii likoje...
 
Hongera Kitilya kwa kuwatambua CDM:kev: kuwa ni wadaiwa sugu wa kodi. Hawa ni wapinzani wa maendeleo ya nchi yetu.

Miaka 50 ya UHURU hawajatambua umuhimu wa kulipa kodi. JK BIG UP kwa kumuongezea Kitilya muda wa miaka 2 kuongoza TRA
 
Lakini mwajiri ndiyo mwaenye jukumu hili ingawa inakatwa kwenye msharaha wa mfanyakaz mfano mimi sikumbuki kuchukua pesa na kupeleka TRA kwaajiri ya mshahara wangu ila huwa naona kila mwezi kwenye vikaratasi kuwa nimelipa kodi au hii likoje...

CDM ni mwajiri wa Dr. Slaa hivyo ni wajibu wao kumkata kiasi cha pesa kwa ajili ya KODI. Nyie mnakuwa wepesi kulalamika barabara mbovu; wakati hamlipi kodi. Zoezi hili litakuwa endelevu kwani mmezoea kutumia ruzuku kulipana posho ya MAANDAMANO.
 
Tukianza kuidai ccm, basi tuta attach mali zao zote maana ni wadaiwa sugu ambao hawamithiriki, uwanja wa maji maji songea wanadaiwa kodi ya majengo ya kufa mtu, hapo hujataja mwanza na arusha.
 
Cdm wanajukumu la kulipa kodi nao walijue, tunawaamin kwa sasa. Ccm tunawachukia kwa magumashi kama hayo, watch out cdm!
 
Wakuu,

Tuache politics hata kwenye mambo ya maana kwenye ustawi wa nchi yetu. Suala la kulipa kodi ni wajibu wa kila mtu na kila mwajiri kuhakikisha anafikisha kodi ya wafanyakazi wake TRA. Kitendo cha chama cha siasa chochote kile kutokulipa kodi ni cha kusikitisha sana. Inapotokea kwamba hata watu wanaotaka kuwa viongozi wa nchi yetu hawalipi kodi kwa visingizio vyovyote vile ni jambo la kusikitisha mno. Mimi namwelewa Dr. Slaa na mapambano yake dhidi ya ufisadi. Hata siku moja nisingetegemea Dr. Slaa apokee mshahara wake bila kulipa kodi. Ningetegemea awe na mjanja vyakutosha na kusema hapana, hapa kuna tatizo. Kwa sheria zet za kodi wenye kosa hapa ni CHADEMA maana kama mwajiri lazima uhakikishe kila mfanyakazi analipa kodi. Lakini pia mwajiriwa una hata moral responsibility ya kuzijulisha mamlaka husika pale unapoona jambo fulani haliko sawa.

Arguments nyingi tunazotoa hapa ni shallow mno kwa maana ya kwamba kujifanya hujui sheria si utetezi kwenye mambo ya sheria. Ninaamini CHADEMA, CCM na vyama vingine vina watu wenye elimu zao na ambao wanajua kwamba ni wajibu kwa kila raia mwenye kipato kulipa kodi.

TRA imeshindwa kazi na is not fit for purpose. Inakuwaje kwa miaka yote hii wameshindwa kujua kwamba vyama vya siasa vina mapato ya kutosha kwa wafanyakazi wao kulipa kodi? Inakuwaje miaka yote hii wameshindwa kukusanya hata senti tano kutoka CHADEMA? Je kuna vyama vingapi vingine ambavyo havilipi kodi? Kuna watu wangapi wengine ambao hawalipi kodi? Haya mambo yanafanyika wakati Machinga na wauza vitumbua mitaani wanalipishwa kodi kupitia leseni. Iweje hawa watu ambao wana mapato kidogo sana wanalipa kodi wakati wenye mamilioni hawalipi kitu? Huyo CEO wa TRA anaendelea kupewa muda wa kuongoza shirika kwa mafanikio gani wakati Watanzania wengi tu wenye mapato hawalipi kodi? TRA ni failure na kuna haja ya kuifanyia mabadiliko makubwa ili kodi ikusanywe hasa kutoka kwa matajiri mbalimbali ambo wanakwepa kulipa kodi.

Kule kwetu Kyela sisi tulipoanza biashara, moja ya majukumu niliyowapa vijana ilikuwa ni kuonana na TRA na kujadiliana nao juu ya nini tunatakiwa kufanya kwenye suala la kodi. Sisi tuna majengo pale tunakodisha vyumba vya biashara, mikataba yote tunaipeleka sisi wenyewe kwa hiari yetu TRA na kuhakikisha 10% withholding tax ya pango inapelekwa. Hata tulipoanza biashara zingine tumeenda kuwaona na wametupa ushauri mzuri tu na kutushukuru kwa kutambua umuhimu wa kulipa kodi. Kwa nilivyowaona mimi tungeweza kuendesha biashara zetu bila kulipa kodi kama tungelitaka. Lakini kama ni mfanybiashara ni muhimu kuwa na uhusiano mzuri na mamlaka ya kodi. Hata ukiwa na matatizo ni kuwaambia ili waone kama wanaweza kukusaidia. Kama umejenga uaminifu kwao nina uhakika hata kama una shida kuna nafasi kubwa ya kukuelewa na kukuruhusu kuchelewa kupeleka kodi au kulipa taratibu.

Ningependa kuona vyama vya siasa vyote vinatoka clean kwenye hili. Wahakikishe wafanyakazi wao wote pamoja na vifaa vyote vinavyonunuliwa kwamba vinalipiwa kodi. Vinginevyo wananchi tusahau kupata nafuu yoyote kutoka kwa hawa viongozi wetu. Binafsi ningependa TRA iunde tume ambayo ipite kwenye kila chama na kuhakisha wanakagua mahesabu yao yote na kuangalia wapi wanakwepa kodi. Adhabu ya 100m kwa kushindwa kulipa kodi kwa miaka 11 ni ndogo sana. Kuna haja ya kuwafilisi na kuwapeleka jela wale wanaoshindwa kulipa kodi kama wanavyofanya Wajerumani na hii ndio itafanya watu wawe waoga.

Mkuu mtanzania umeongea mambo ya maana sana lakini kama kweli TRA inataka kufanya reform kwenye tax ni upuuzi wa hali ya juu kuukomalia mshahara wa Dr. Slaa kama ndiyo mwanzo wa reforming. Wanachofanya TRA is politics pure an simple.

Mkuu hivi unaweza kuamini Waziri wa serikali mwenye mke ambaye ni kamisha au mkurugenzi wa wizara wanalipa kodi ndogo kuliko an individual anayelipwa 4.5 million kwa mwezi. Nna mfano halisi juu ya hili and that's why naona hawa TRA wanatuzingua tu!!!!
 
Mkuu mtanzania umeongea mambo ya maana sana lakini kama kweli TRA inataka kufanya reform kwenye tax ni upuuzi wa hali ya juu kuukomalia mshahara wa Dr. Slaa kama ndiyo mwanzo wa reforming. Wanachofanya TRA is politics pure an simple. Mkuu hivi unaweza kuamini Waziri wa serikali mwenye mke ambaye ni kamisha au mkurugenzi wa wizara wanalipa kodi ndogo kuliko an individual anayelipwa 4.5 million kwa mwezi. Nna mfano halisi juu ya hili and that's why naona hawa TRA wanatuzingua tu!!!!

Hizo nyumba za serikali walizouziwa wafanyakazi kule Masaki na O'bay kuna watu mpaka wanazipangisha kwa $10,000 tena hawa ni vigogo serikalini sasa uliza kodi wanalipa????? It is just a joke. Wakati ughaibuni maka kodi ya raisi au PM ni wazi uliza bongo JK analipa kodi kiasi gani, very likely none!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom