nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Monday, 08 August 2011
NA HAMIS SHIMYE
Gazeti la Uhuru
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeitoza faini ya sh. milioni 100 CHADEMA, baada ya kubainika inakwepa kodi tangu ilipoanzishwa mwaka 1992. TRA pia imeanza kukata kodi mshahara wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa na watumishi wengine wa CHADEMA.
Habari za kuaminika kutoka ndani TRA zilisema ulipaji faini unaanza mara moja, baada ya uchunguzi kukamilika na kuonyesha chama hicho hakilipi kodi.
"Tumemaliza uchunguzi na kubaini CHADEMA hailipi kodi ya mishahara ya kila mwezi ya watumishi wake tangu ilipoanzishwa,'' kilisema chanzo chetu cha habari.
Imeelezwa kuwa, CHADEMA imekiuka sheria na kanuni za ulipaji kodi, zinazotaka mtu, kampuni au taasisi yoyote kulipa kodi TRA.
"Ijapokuwa tangu ilipoanzishwa ilikuwa hailipi kodi, katika uchunguzi tulipata taarifa za kuanzia mwaka 2000 hadi sasa zinazoonyesha hailipi kodi,'' kilisema chanzo hicho.
Kutokana na hilo, chama hicho kinapaswa kulipa faini ya sh. milioni 100 na kimeamriwa kulipa kodi ya mishahara ya watumishi wake kuanzia mwezi uliopita.
Chanzo hicho kilisema CHADEMA imeiandika barua TRA ikidai wanacholipana ni posho na si mishahara.
Hata hivyo, sheria ya kodi inaeleza kiwango chochote cha posho kinachozidi kima cha chini cha mshahara kinapaswa kukatwa kodi.
Watendaji ambao TRA imeanza kuwakata kodi ni Dk. Slaa, ambaye analipwa mshahara wa zaidi ya milioni 7.4, fedha ambazo ni nyingi kuliko mshahara wa mbunge.
Mshahara huo unatokana na mapendekezo ya Azimio la Kamati Kuu ya chama hicho iliyokutana Januari 29 na 30, mwaka huu, mjini Dar es Salaam, ambapo mshahara huo umegawanya katika sehemu sita.
Sehemu hizo ni posho ya mwezi, fedha za mafuta, majukumu, viburudisho, nyumba na utendaji kazi, ambapo mshahara wa mwezi ni sh. 2,300,000.
Fedha za mafuta ni sh. sh. 1,387,000 kwa wastani wa lita 750 kwa mwezi, huku fedha za majukumu zikiwa sh. 575,000, mawasiliano sh. 460,000 na nyumba sh. milioni moja.
Posho kwa ajili ya viburudisho sh. 462,500 na utendaji kazi sh. 989,000. Mshahara huo umefanywa maalumu kwa Dk. Slaa pekee na iwapo chama hicho kitapata katibu mkuu mwingine hawezi kulipwa mshahara kama huo.
( Monday, 08 August 2011 19:
CHADEMA yakiri kukwepa kodi
Tuesday, 09 August 2011 20:09
NA SULEIMAN JONGO[/B]
KATIBU Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibroad Slaa, amekiri kuwa chama chake kimetozwa faini na Mamlaka ya Mapato (TRA).
Hatua hiyo imetokana na chama hicho kudaiwa kukwepa kulipa kodi za mishahara na posho za watumishi wake kwa miaka kadhaa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, jana, Dk. Slaa alisema TRA imeitoza CHADEMA faini ya sh. milioni 94. "Ni kweli tumepigwa faini na TRA kulipa sh. milioni 94, kwa kutolipa mishahara ya watumishi wetu.
Tutalifikisha hilo katika vikao vya juu na tutalipa tu," alisema Dk. Slaa.
Alisema kuwa tayari wamepokea barua kutoka TRA inayowataka kulipa sh. milioni 94, kama adhabu ya kutolipa kodi za watumishi wake. Hata hivyo, katika hali ya kushangaza Dk. Slaa alisema kuwa CHADEMA haijalipa kodi tangu kuanzishwa mwaka 1992, haijalipa kodi za watumishi wake kwa kutofahamu.
Pia, alisema kuwa walikuwa hawafahamu mabadiliko ya Sheria za Kodi, ambayo huko nyuma mishahara ya watumishi inayotokana na fedha za ruzuku ya serikali.
Wakati huo huo, CHADEMA kimeshauri kutazamwa upya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) baada ya kukosa mwelekeo katika kutimiza majuku yake.
Dk. Slaa alisema mkanganyiko katika mbalimbali yanayotokea kwenye sekta ya nishati na maji yanatokana na ulegevu wa EWURA na kutotimiza majuku yake ipasavyo.
Alisema lengo la kuanzishwa EWURA ni kusimamia na kuratibu huduma mbalimbali zinzohusiana na maji na nishati ya mafuta na gesi, jambo ambalo linafanya kuwepo na haja ya kuitazama upya EWURA.
Kwa mara ya kwanza habari za CHADEMA kukwepa kodi ziliibuliwa na gazeti hili, ambapo baada ya TRA kufanya uchunguzi wake ilibaini ni kweli na sasa itavuna mamilioni ya shilingi kama adhabu, ambazo zitasaidia kutoa huduma kwa jamii.
NA HAMIS SHIMYE
Gazeti la Uhuru
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imeitoza faini ya sh. milioni 100 CHADEMA, baada ya kubainika inakwepa kodi tangu ilipoanzishwa mwaka 1992. TRA pia imeanza kukata kodi mshahara wa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa na watumishi wengine wa CHADEMA.
Habari za kuaminika kutoka ndani TRA zilisema ulipaji faini unaanza mara moja, baada ya uchunguzi kukamilika na kuonyesha chama hicho hakilipi kodi.
"Tumemaliza uchunguzi na kubaini CHADEMA hailipi kodi ya mishahara ya kila mwezi ya watumishi wake tangu ilipoanzishwa,'' kilisema chanzo chetu cha habari.
Imeelezwa kuwa, CHADEMA imekiuka sheria na kanuni za ulipaji kodi, zinazotaka mtu, kampuni au taasisi yoyote kulipa kodi TRA.
"Ijapokuwa tangu ilipoanzishwa ilikuwa hailipi kodi, katika uchunguzi tulipata taarifa za kuanzia mwaka 2000 hadi sasa zinazoonyesha hailipi kodi,'' kilisema chanzo hicho.
Kutokana na hilo, chama hicho kinapaswa kulipa faini ya sh. milioni 100 na kimeamriwa kulipa kodi ya mishahara ya watumishi wake kuanzia mwezi uliopita.
Chanzo hicho kilisema CHADEMA imeiandika barua TRA ikidai wanacholipana ni posho na si mishahara.
Hata hivyo, sheria ya kodi inaeleza kiwango chochote cha posho kinachozidi kima cha chini cha mshahara kinapaswa kukatwa kodi.
Watendaji ambao TRA imeanza kuwakata kodi ni Dk. Slaa, ambaye analipwa mshahara wa zaidi ya milioni 7.4, fedha ambazo ni nyingi kuliko mshahara wa mbunge.
Mshahara huo unatokana na mapendekezo ya Azimio la Kamati Kuu ya chama hicho iliyokutana Januari 29 na 30, mwaka huu, mjini Dar es Salaam, ambapo mshahara huo umegawanya katika sehemu sita.
Sehemu hizo ni posho ya mwezi, fedha za mafuta, majukumu, viburudisho, nyumba na utendaji kazi, ambapo mshahara wa mwezi ni sh. 2,300,000.
Fedha za mafuta ni sh. sh. 1,387,000 kwa wastani wa lita 750 kwa mwezi, huku fedha za majukumu zikiwa sh. 575,000, mawasiliano sh. 460,000 na nyumba sh. milioni moja.
Posho kwa ajili ya viburudisho sh. 462,500 na utendaji kazi sh. 989,000. Mshahara huo umefanywa maalumu kwa Dk. Slaa pekee na iwapo chama hicho kitapata katibu mkuu mwingine hawezi kulipwa mshahara kama huo.
( Monday, 08 August 2011 19:
CHADEMA yakiri kukwepa kodi
Tuesday, 09 August 2011 20:09
NA SULEIMAN JONGO[/B]
KATIBU Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibroad Slaa, amekiri kuwa chama chake kimetozwa faini na Mamlaka ya Mapato (TRA).
Hatua hiyo imetokana na chama hicho kudaiwa kukwepa kulipa kodi za mishahara na posho za watumishi wake kwa miaka kadhaa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, jana, Dk. Slaa alisema TRA imeitoza CHADEMA faini ya sh. milioni 94. "Ni kweli tumepigwa faini na TRA kulipa sh. milioni 94, kwa kutolipa mishahara ya watumishi wetu.
Tutalifikisha hilo katika vikao vya juu na tutalipa tu," alisema Dk. Slaa.
Alisema kuwa tayari wamepokea barua kutoka TRA inayowataka kulipa sh. milioni 94, kama adhabu ya kutolipa kodi za watumishi wake. Hata hivyo, katika hali ya kushangaza Dk. Slaa alisema kuwa CHADEMA haijalipa kodi tangu kuanzishwa mwaka 1992, haijalipa kodi za watumishi wake kwa kutofahamu.
Pia, alisema kuwa walikuwa hawafahamu mabadiliko ya Sheria za Kodi, ambayo huko nyuma mishahara ya watumishi inayotokana na fedha za ruzuku ya serikali.
Wakati huo huo, CHADEMA kimeshauri kutazamwa upya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) baada ya kukosa mwelekeo katika kutimiza majuku yake.
Dk. Slaa alisema mkanganyiko katika mbalimbali yanayotokea kwenye sekta ya nishati na maji yanatokana na ulegevu wa EWURA na kutotimiza majuku yake ipasavyo.
Alisema lengo la kuanzishwa EWURA ni kusimamia na kuratibu huduma mbalimbali zinzohusiana na maji na nishati ya mafuta na gesi, jambo ambalo linafanya kuwepo na haja ya kuitazama upya EWURA.
Kwa mara ya kwanza habari za CHADEMA kukwepa kodi ziliibuliwa na gazeti hili, ambapo baada ya TRA kufanya uchunguzi wake ilibaini ni kweli na sasa itavuna mamilioni ya shilingi kama adhabu, ambazo zitasaidia kutoa huduma kwa jamii.