Shoka la TRA latua CHADEMA

Shoka la TRA latua CHADEMA

Hii itasaidia wakwepa kodi wengi wakubwa watajwe hadharani. Huu ndo uzuri wa mchezo wa kuvuta kamba ndo huu...
 
Ulitarajia nini baada ya dr. Slaa kumtataja mkurugenzi wa tra kuhusika na rushwa,ulitarajia nini katika nchi ya ovyohovyo na watendaji wake legelege katika kufanya hili,ccm iliingiza yale mapperushi ya uchaguzi mwaka 2010 je ilililipia kodi? Hata kama chadema hukulipa kodi wapi ccm imelipa katika transaction zake? Or right ni maagizo ya nape
 
Mkuu Mkandara,

Kwanza, nimeongelea ruzuku kama njia mojawapo ya mapato ya vyama vya siasa. Wana mapato yao mengine. Pia wana wafanyakazi ambao wameajiriwa na wanatakiwa kulipa kodi. Hiyo kodi ya wafanyakazi ndio haijawahi kupelekwa TRA. Sasa kama wewe unafaidika na ruzuku ambayo inatokana na kodi ya Watanzania, ningetegemea uwe wa kwanza kuelewa umuhimu wa kulipa kodi.

Pili, suala la mtu aliyeajiriwa, kodi yake hulipwa na mwajiri wake. Kwenye suala la Dr. Slaa ni kosa la CHADEMA kwamba hawajalipa kodi yake. Ingelikuwa amejiajiri hapo ndipo yeye mwenyewe angetakiwa kuhakikisha kodi yake inalipwa TRA. Lakini ukisema chama cha siasa hakilipi kodi, huwezi kuwaondoa viongozi wake wakuu katika lawama.

Tatu, Suala la viongozi kuwakilisha mali zao tume ya maadili, halina uhusiano na kodi au TRA. Hilo ni kwa lengo la kujua kama wamezipata hizo mali kihalali au la.

Nne, sijaona mahali popote wakisema Dr. Slaa alipokuwa mbunge hakuwahi kulipa kodi. Kodi ya mbunge inakusanywa na ofisi ya bunge au wizara ya fedha (sina uhakika nani analipa mishahara ya wabunge) na ndio wao wanaiwakilisha serikalini. Ambao hawajawahi kulipa kodi ni wafanyakazi wa CHADEMA. Dr. Slaa alikuwa hajalipa hiki kipindi cha hapa mwishoni ambacho mshahara wake sasa unalipwa na CHADEMA.


Hakuna kitu kama hiko!
Hawalipi Kodi hawa!
 
Swali:Chadema walikuwa wanalipa kodi?.....Huu ni ufisadi wa hali ya juu,kuweni mfano bora jamani dah!!!

Huwezi kuwa Kobelo yule wa gazeti la Sani enzi za John Kaduma,yule alikuwa mjanja sana sio kimeo kama wewe.TAHADHALI:Sheria ni Msumeno sawa!!,Wasiwasi wangu Siku CCM ikibainika walah itakuwa kuzaliwa kwa chama kipya kabisa Duniani maana Itakufa,inaweza daiwa zaidi ya zile Trillion za Kamanda Lt.Gen nakuhakikishia,na Chazaidi nyie tutawasugisia hadi Takukuru,CAG na kila kitu maana CCM ni majambazi ya huduma za Jamii,hizo mnazolipana Pension Mbilimbili mnazitoa wapi kama sio kukwepa KODI?Mola epusha mbali CCM isikumbwe na hili maana kabla haijafa tunatamani kuiona kama Chama cha Upinzani kwa kweli!!!!!
 
Ulitarajia nini baada ya dr. Slaa kumtataja mkurugenzi wa tra kuhusika na rushwa,ulitarajia nini katika nchi ya ovyohovyo na watendaji wake legelege katika kufanya hili,ccm iliingiza yale mapperushi ya uchaguzi mwaka 2010 je ilililipia kodi? Hata kama chadema hukulipa kodi wapi ccm imelipa katika transaction zake? Or right ni maagizo ya nape

Bosi achana na Hawa huwawezi Magamba majambazi hawa.Unajua huyu mkurugenzi wa TRA Mr.Harry KITILYA alibakisha miezi 3 tu astaafu kwa mujibu wa umri wake na sheria ya utumishi.

Haya ndio mazingaombwe ya Baba Riz,Amempa zawadi ya Kuiabisha na Kuidai kodi chadema, Wakati kuna Vijana Wasomi wanatafuta Kazi,Kamuongezea Muda jamaa Miaka MITATU(3) na Haya ndio malipo kwa Kazi nzuri ya Kuidai Kodi Chadema na ili aweke Kumbukumbu za CCM kutolipa Kodi.

A day will come,maana hata Hosn Mubarak hakutaraji wala hakuwahi ota kama yatamfika yaliyomfika, Wanacheza na Muda Tu Ze-Magambazi.

Na HII tayari ni Dalili ya Rushwa, Takukuru wamelala. Rais wa Nchi anatoa Rushwa!!!
 
Back
Top Bottom