A
Anonymous
Guest
Mimi ni Mkazi wa Zanzibar katika Mkoa wa Mjini Magharibi, Wilaya ya Mjini.
Kero yangu ni kwa Shirika la umeme Zanzibar (ZECO).
Wamekuwa na muendelezo wa kukata umeme mara kwa mara maeneo ya Kwahani, ikizingatiwa sehemu hiyo kuna Kituo cha Afya, Ziwani Police Health Center kinachotoa Huduma za jamii kwa wakazi wa maeneo hayo na kupelekea Huduma kusimama kwa muda mrefu na kuwaathiri wananchi.
Tunaliomba shirika la umeme ZECO wajitahidi kurekebisha miundombinu ya maeneo hayo ili huduma ziendelee kutolewa kwa jamii.
Pia soma ~ ZECO: Changamoto ya umeme Zanzibar inachangiwa na miundombinu ya kusafirisha umeme, kuna mpango wa kuweka njia kutoka Bara
Kero yangu ni kwa Shirika la umeme Zanzibar (ZECO).
Wamekuwa na muendelezo wa kukata umeme mara kwa mara maeneo ya Kwahani, ikizingatiwa sehemu hiyo kuna Kituo cha Afya, Ziwani Police Health Center kinachotoa Huduma za jamii kwa wakazi wa maeneo hayo na kupelekea Huduma kusimama kwa muda mrefu na kuwaathiri wananchi.
Tunaliomba shirika la umeme ZECO wajitahidi kurekebisha miundombinu ya maeneo hayo ili huduma ziendelee kutolewa kwa jamii.