Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Shinyanga Mjini Vs Tabora Mjini

Msunguko wa pesa wa Urambo na Kaliua ni wa msimu, wanapouza tumbaku ndio hayo maeneo yanakuwa na pesa. Lakini Igunga na Nzega mzungukonwake ni mwaka mzima na mind you Igunga ni centre ya baishara ya mpunga kwa sasa, pamoja na dengu, pia uwepo wa machimbo ya dhahabu pale shelui unapainua sana igunga.

Wafabyabiashara wengi wadogo na wa kati wa Shinyanga wanakimbilia igunga, hii ni baada ya kahama kuwa mkoa wa kikodi hivyo shinyanga kujikuta ikihaha kukusanya mapato na kuwatoza wafanyabiashara kodi kubwa, kwa hiyo mzunguko wa pesa wa Igunga ni mkubwa sana, pengine kuliko hata wa Nzega, and in few yrs to come Igunga itaiovertake Nzega.
Ukiwa Igunga usiku huwezi kuamini kama pale ni igunga, pana starehe zote unazozijua, si vibaya kama huwa unapita hiyo njia ulabreak your journey pale, you ll never regret
Rudi kwenye kudesa upya mkuu,Wilaya zenye mzunguko mkubwa wa Pesa Tabora ni Urambo na Kaliua hizo nyingine zinafuatia,pitia tu takwimu za halmashauri husika uone makusanyo ya Ndani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hadithi za kufikirika,eti roho ya umaskini...nyie ndo mnaua albino..kwamba Tabora hakuna makazi yenye hadhi kama huko kwingine na kama yapo wanaojenga wametoa wapi pesa?
Wewe ungejibu hoja kwa hoja badala ya kupanic. Mimi miji miwili yote nimeishi na ninachokizungumza nina uhakika nacho. Ule mji wa Tabora unafaa kuishi wafanyakazi siyo wafanyabiashara. Sasa ni hiari yako kukubali au uendelee kuamini unachoamini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbuka pi sehemu za urambo na kariua zipo karibu sana na kahama
Kahama haizalishi chakula kwa kiwango unachotaka kusema hapa.

80% ya karanga zinazopatikana Kahama zinazalishwa Tabora na soko kubwa la Karanga za Tabora ni kahama.

Zao kubwa kahama inalozalisha ni Mpunga tu sasa utasemaje kuwa wanategemewa na Shinyanga ?

Mahindi unayoyaona sokoni hapo kahama yanatoka Tabora katika wilaya za Uyui, Kaliua na Urambo.

Kimsingi bila Tabora Shinyanga inaweza kuteketea kwa njaa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa mbona mnahama kutwa utafikiri wakimbizi mnakimbia nini?

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuhama ndugu yangu hakukwepeki kwa sababu idadi ya watu inaongezeka lakini ardhi haiongezeki, na Tabora, Shinyanga, Mwanza, Geita na Simiyu ni mikoa ndugu, hivyo akihama Simiyu akaenda Tabora ni kwamba yupo nyumbani tu wala hajawa mkimbizi bali ni kwao na mila na desturi zinafanana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kupika vizuri hawajui,usiku hakuna sehemu ya maana ya chakula hadi uwe mlevi ukale ugali nyama choma,ukuanza biashara hii ya chakula na ukafanya vizuri utawangiwa ili usiendelee.Ni wivu na ujinga tu
Shinyanga pa hovyo zaidi kuhusu msos..sijui kwanini jamani...unamweleza boda nipeleke sehem nzuri ya kula anakubwaga kwa mama ntilie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vichaa wengi huja kwa usafiri wa treni mkuu maana Tabora inahudumia karibia mikoa yote ya magharibi na Mwanza na mara hivyo Vichaa hupanda tu kwenye trains basi hujikuta wapo Tabora, na kwakuwa Tabora gari moshi huchelewa sana kuondoka (kwani hapa hufanyika kwanza shanting) hivyo abiria hulazimika kushuka kwanza na ndipo hapo hata vichaa hushuka na kuanza kulandalanda huku na huko.

Sent using Jamii Forums mobile app
wewe noma sana mkuu
 
Kahama ni habari nyingine, kwa mzunguko wa hela na per capital ni pakubwa kuliko wilaya nyinginza tanzania na pengine baadhi ya mikoa kama singida, rukwa, lindi na shintanga nyenyewe.
Ukiondoa Kahama, kwa ukanda huo, bariadi panaweza kufuatia, napo ni sabahu pamekuwa makao makuu ya mkoa, then Igunga, igunga inakua kwa kasi sana.
Ukuaji wa Nzega ni mdogo sana,
Maswa na Meatu wako nyuma sana, na kunakua taratibu sana,labda lami ya maswa bariadi ikiisha itaweka chachu ya maswa kukua, lakini hata hivyo panahitaji miaka mingi sana, kwa sababu Bariadi itaendelea kuimeza Maswa

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kujitekenya Bariadi panapanuka lakini siyo kwa kasi unayotaka tuamini. Hata Geita tu Bariadi haioni ndani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shinyanga mjini hovyo sana.

Hata ukitaka breakfast hakuna sehemu insyoeleweka ukanywa chai uka enjoy.

Chakula cha uhakika ni mchana tu tena sehemu moja tu ambayo wakati mwingine pia wanapika vibaya tu.

Ni sehemu ambayo bara bara ni chafu zimejaa udongo ijapokuwa ni za lami.

Usafiri wa tax ni wa shida,wafanya biashara hii wana nyodo na waongo.Unakubaliana nae unaamka mapema kuwahi basi,ikinyesha mvua tu anazima simu.

Biashara ni ngumu sana shinyanga,nadhani ni sehemu mojawapo ngumu Tanzania.

Maji ya ziwa yapo ila wanachanganya na maji ya bwawa chafu sana la ning"hwa na kuyafanya yawe ya chumvi na mabaya sana.

Bora Tabora sana utapata hata bookshop ya kueleweka,library nzuri,taasisi za mafunzo zinazoeleweka,na bara bara safi zisizo na mchanga

Sent using Jamii Forums mobile app
Ning'hwa dam aka chibe miaka ya 90 tumevua sana Hapo mafish
 
Well said,Shy ina hasara imeshamezwa na Mwanza,Kahama na Bariadi/Maswa yaani kitu pekee wamebaki nacho ni ardhi tambarare ya viwanda
Acheni uongo nyie watu....yaani bariadi na maswa iimeze shy...una akili kweli wewe.

Mwanza ndo unaipa changamoto shy...watu wa shy kwenda mwanza ni kitu cha kawaida kama kutoka bunju kwenda kariakoo.

Kahama geographical location yake ndo unaipa nguvu....iko kwenye njia kuu...junction

TANZANIA TUNA MIJI MIWILI TU TUNAWEZA ITA MIJI DASLAM, MWANZA ikifuatiwa na Arusha kidogo....Mbeya..

Miji mingine ni takataka tu....hakuna unsomzidi mwingine kiasi cha kuwa bora zaidi ya mwenzake......

Pili acheni kulinganisha miji kwa mahaba na ubinafsi..wekeni data tuone,
Ni wakati muafaka sasa serikali ianze kushindanisha hii miji kwa standard za kimataifa..mfano Uzalishaji wa ajira ( employment), services and products zinazozalishwa na mji husika (GDP ya kila mkoa), mchango wa mji au mkoa katika pato la taifa (National GDP) etc...

Sasa nyie mnajua kabisa...zaidi ya nusu ya pato la taifa linatoka Daslam...sehemu inayobaki inazalishwa na mikoa zaidi ya 20...hapo kuna cha kulinganisha kweli....

Wenye data ambazo ziko verified walete watu waone na sio sijui.kisa ulienda tabora au shinyanga ukaopoa demu basi unasem ndo kila kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom