Mkuu kizazi cha leo kimekuwa cha kulalamika tuu bila kuangalia tunatoa vipi solution za matatizo yanayotukabili.
Kwa mtu mwenye akili timamu huwezi kufurahia nchi kuwa omba omba. Ofcourse kuna mengi mkubwa anayafanya yanahitaji mjadala mpana. Lakini kwa ukaribu waTanzania tumekuwa walalamishi sana. Tukisahau kwamba kuna 80% ya waTanzania wenzetu wameishi haya maisha ya kupigika mwa miaka mingi tangu uhuru. Lakini kwa sababu walikuwa watu inconsequential hakuna aliytewahi kupaza sauti kwamba hawa watu wanastahili kuangaliwa.... I mean kuna maswali legit kabisa ambayo watu wanastahili kuuliza na kupatiwa majibu. Lakini huu ulalamishi hautusaidii. Na naamini kabisa hata Mkubwa anajua hizi kelele ni za elites (ambao ndo wanaisoma namba kwa sana-maana ndugu zetu wa vijijini walishazisoma kwa sana na kuzikariri). Elites hata siku ya kupiga kura hawaendi. Its sad but sad truth.
Ndo maana leo mtu bila aibu anaandika humu eti...JK ndo alisababisha yote haya kwa kutuletea Magufuli....(kwa kumkata Lowasa) wakisahau kwamba huyo huyo ambaye angekuwa mkombozi aligombea kwa upande wa pili! You and I know what happened.
Mkuu una hoja ambayo ni valid kwamba yapo aliyoyafanya yanayostahili pongezi na kwamba ulalamishi hausaidii pasipo kupata suluhisho.
Niseme tu kwamba, kiongozi anapofanya wajibu wake hastahili sifa kwasababu huo ndio wajibu wake na ni haki kwa raia wake kutendewa hiko anachotenda. Kiongozi hasipofanya matakwa ya wengi anakosa uhalali wa dhamana aliyopewa na hivyo malalamiko hayazuiliki. Watu wanalalamika kwa kile kisichofanywa kwa namna ya mategemeo yao, hawalalamiki kwa kile kinachofanywa ipasavyo.
Nakubali hoja yako kwamba 80% waliishi maisha magumu tangu mwanzo na hawakulalamika. Mimi nadhani hawakulalamika kwasababu bado walikuwa within a threshold ya umasikini ambao ulikuwa tolerable. Na asikudanganye yeyote hiyo 80% ndiyo inayolalamika zaidi na sio kweli kwamba elites na wapiga deal ndio wanaolalamika sio kweli. Kwenye mfumo wa kibebari wowote duniani, kuyumba kwa uchumi kunawamaliza zaidi watu wa chini wakiwamo masikini, watoto na akina mama kwasababu kipato chao kinategemea kipato cha mtu wa daraja la juu au kati.
Sio hivyo, hata viongozi wa ngazi zote wanalalamika, iwe wa chadema CCM au vyama vingine. Nchi inalalamika. Viongozi wanakosa sehemu ya kwenda kulalamikia lakini ukipata muda wakua karibu nao wakakueleza mitazamo yao naamini utajuwa kwamba we are in a full blown leadership and economic crisis.
Upo sahihi kwamba yapo mambo yanahitaji mjadala mpana. Tatizo linakuja mjadala huu unaletwa na kudhaminiwa na nani na kutekelezwa na nani kama wingu la woga limetanda pande zote za nchi? Demokrasia ndio inayotoa fursa ya mjadala mpana huku ikishikilia msingi wake wa majority rules while minority rights and interests considered. Sasa hivi leo Tz tuna demokrasia? Tuna uhuru wa kujieleza (labda kwenye mitandao tu kama hivi tufanyavyo na huku bado wanatuvizia)? Hivyo suluhisho la mjadala mpana haliwezi kufanyakazi kama mazingira ya mijadala yamejaa woga, ubabe, visasi na uadui.
Lakini yapo mambo ambayo wala hayahitaji mjadala ambayo kwa kweli yanaifanya hii serikali ichukiwe kila siku. Hivi hotuba za kiongozi wetu zinahitaji mjadala kuwa hotuba zinazovuta usikivu na kuliunganisha taifa? Tunahitaji mjadala kweli kwa kiongozi wetu kuonyesha human face kwenye matatizo yanayoikabili nchi? Tunahitaji mjadala kwa kiongozi wetu kujuwa kwamba njaa inainyemelea bara la Africa ikiwamo Tz yetu na hivyo kuwaambia wananchi nini wafanye na yeye kama kiongozi atafanyaje kuhakikisha wananchi wake wako salama? Tunahitaji mjadala kiongozi wetu ajuwe kwamba moja ya kazi tuliyompa ni kulinda usalama wetu ikiwamo usalama wetu nyakati za njaa, vita, au magonjwa? Kama haya yanahitaji mjadala basi mjadala wa kwanza ni kujiuliza kama tulimchagua kiongozi sahihi na kama tulikuwa sahihi kumchagua basi turudi kwenye kurekebisha sifa za kiongozi wetu kwenye katiba.
Hakuna nchi inayofurahia kuwa omba omba lakini ajabu ya dunia ni kwamba hakuna nchi isiyoomba duniani. Tunatofautiana tu namna ya kuomba na masharti ya mwombaji na mwombaji na viwango vya kuomba au kuombwa. Kama kusingekuwa na waombaji na waombwaji basi World Bank na IMF zingefia mbali tangu kuundwa kwakwe. Kwa nchi yetu kuomba ni aibu lakini ni LAZIMA, na tunachosema sisi ni kwamba kiongozi wetu alitakiwa ajuwe hili, kwamba kuomba aibu lakini lazima na hivyo basi hakutakiwa awakejeli nchi zilizokuwa zinatusaidia. Amezikejeli na sasa anaziomba kwa kuzipigia magoti na tayari deni letu ndani ya mwaka moja limeumuka andazi limesingiziwa. Juwa uwezo wako, juwa limitations za nguvu na uwezo wako then tengeneza mazingira ya kusaidiwa na kushaurika ili mambo yanapokuwa magumu unasaidiwe.
Nihitimishe kwa kusema kwamba, sio kweli kwamba wanaolalamika ni elites na wapiga deal, kwasababu mitikisiko wa uchumi unamtikisa kwanza mtu wa chini. Watu wa chini wanalalamika kwasababu wametikiswa kuliko ilivyokuwa kawaida, wanashindwa kustahimili tikisiko hili. Yapo mambo yanayohitaji mjadala mpana wakitaifa lakini kwa hilo kutokea lazima misingi ya demokrasia iheshimiwe na wingu la woga liondolewe. Hakuna anayependa kumvasha paka taruma. Lakini yapo mambo rahisi mno kuyasawazisha pasipo mjadala haya yakiwamo kauli, maamuzi yasiyofuatia utafiti, kulipiza visasi, na hotuba za kuligawa taifa. Ingawa kuomba ni aibu lakini Tz kamwe hatuwezi kukwepa na tayari tumeanza kukopa kwa spewed isiyowahi kutokea, basi tulitakiwa tujenge urafiki na mahusiano mazuri kwa hao tunaowaomba ili watulegezee masharti.