Shibuda: CHADEMA nifukuzeni muone!

Shibuda: CHADEMA nifukuzeni muone!

Huyu dawa yake kumsakizia popo bawa,ahangaike naye wiki nzima angenyooka.
 
Hapana,

Ndioo, ndioo, ndioo ni mbiu ya CCM kumchagua Ally Mwinyi.

Tunataka watu wanaoweza kuleta migongano ya mawazo kwa nidhamu, ndani ya chama. Na wenye uungwana wa angalau kutokitukana chama kilichowapa ubunge hadharani kama watu wasio fadhila.

I mean ondoa siasa, Shibuda kakosa utu wa chini kabisa, na anaendekeza ubinafsi zaidi kuliko maslahi ya chama wala wananchi.

Hebu tuletee ushahidi wa tusi moja alilotukana Shibuda kwa Magwanda, hajawatukana CCM waliomwengua kwenye kura za chama.
 
It was a mistake they shouldn't have made in the first place. Kuna acceptable and unacceptable mistakes. Huyu walionywa sana juu yake. Ila kuona mvuke hawakutaka kuona kuwa sufuria ni la moto waka taka kuligusa wajionee wenyewe. This was simply a matter of politics 101.

kwani kuna mengine hawakufuata na wakafanyikiwa? Au mnakalia hili kwa vile halikuwa kama walivyotarajia?
Don’t blow this out of proportion! Kama ametofautiana na Chama na kamati itaamua hivyo, basi wamuondoe!
 
CDM, ni kikundi cha watu kipo kimaslahi zaidi wala akina dhamira ya dhati kuwakomboa Wananchi!
Kama akina Mbowe wangesikia wananchi wanasema hivyo dhidi ya Shibuda, ndipo wangepata ujasiri wa kusema wa kumfukuza Shibuda, CDM wanataka kila mbunge awe mateka wa chama, atii amri hata zile za zisizo na tija na faida kwa wapiga kura, kuna udikteta mkubwa ndani ya CDM
 
pure psycho case,..siku ya kwanza kumshuhudia ni siku cdm walipozindua kampeni zao pale jangwani,alipoanza kuzungumza niliangalia chini,..ila sababu nawaheshimu viongozi wa cdm nikajua labda ana kitu cha ziada ambacho wanakijua ambacho ni positive kuhusu huyu mwehu....looking back i realize that my mind didn't play tricks on me,.akapimwe akili..hivi huyu si ndiye aliyesababisha kizaazaa pale shy mpaka akafa mtu??
 
Chadema wajikite kwenye mambo ya maana .Shibuda mwacheni atamliza tu muda wake na anatemwa kwenye kupitisha majina arudi CCM au aenda UDP yaani anadhani ana nguvu kuliko wanachama ? Wamwache asiwayumbishe kwa sasa .
 
Duble Chris, kabla sijatoa maoni yangu kwanza nikushukuru kwa hoja yako. Kwa kweli mgongano wa mawazo ama kutofautiana na mawazo ya wengine ndani ya chama ni afya kwa chama na Taifa kwa ujumla. Huyu mzee wa Kisukuma (mtani wangu) ameonyesha ukomavu wa kisiasa kwa kusimamia kile anachoamini na siyo kuburuzwa na itikadi ama sera ambayo inakinzana na dhamiri yake. Mimi binafsi nampongeza kwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa. Ushauri wangu kwa Chadema ni kumwacha Shibuda aendelee kukikomaza Chama kwa faida ya Taifa letu. Wakimfukuza watakuwa wamekosea sana na itadhihirisha kwamba hawajakomaa kisiasa. Alichofanya Shibuda hakitoshi kumfanya kuwa mwasi kiasi cha kufukuzwa chama ama kupewa adhabu yoyote ile. Msimamo wa Shibuda (mzee wa mashairi na tenzi) kwa maoni yangu hauna athari yoyote kwa Chadema. Yeye ni mmoja na kama ni ushindi wabunge wa Chadema ndio wengi kuliko Shibuda sasa wamwache tu aamini anavyoamini. Tatizo la siasa za nchi changa ni kutokujua kwamba demokrasia siyo ya wengi tu. Ipo pia demokrasia ya mtu mmoja. Heshimuni msimamo wa Shibuda. Naomba sana uongozi wa Chadema watumie busara katika hili. Busara itumike na siyo sera ama ubabe wa namna yoyote ile
 
Huwa nikimuangalia anapoongea huwa najua tu kuwa kuna pumba nyingi zinakuja,huyu hakufaa kuwa mawanachama wa CDM kwani hana sifa kabisa na siku zake zinahesabika
 
sina hahika kama elimu uliyonayo (japo siijui) kama uliipata kihalali, unatarajia kuolewa lini?

Unanchekesha, Nna uhakika tena wa hali ya juu kabisa, kuwa uende urudi, upande ushuke, huna ubavu wa kuifikia elimu yangu. Ng'oo!
 
Mkuu huwezi juu. Siasa za public na behind the doors ni tofauti sana. Huwezi jua huyo Shibuda ana nini kinacho mpa kiburi. Jiulize kwa nini Chadema mpaka leo hawajamfukuza.

Mhh my understanding on this issue ni kuwa Chadema tayari walishamwandikia barua na kumtaka ajieleze kuhusiana na suala la kuwa na msimamo tofauti na msimamo wa chama juu ya suala la Posho ya vikao kwa wabunge wawapo bungeni. Katika barua hiyo pia wamempa muda (sikumbuki siku ngapi??) ili awe ameshajibu, ili kamati ikae na kuangalia nini cha kufanya. Hivyo sio sahihi saana kusema chadema inamwogopa Shibuda.
 
Wapendwa wanaJF

Chama chochote makini lazima kiwe na level of torelance kwa wanachama wake. Ni vema CDM mkaiga baadhi ya mambo mazuri toka kwa CCM japo mnakibeza kwa kila hali. CCM ina level of torelance ya juu sana kwa wanachama na hususani MAKADA wake. Ndiyo maana pamoja yote, CCM bado ni chama madhubuti......japo wengi hamkubaliani na ukweli huu. CCM hawakurupuki katika maamuzi yake.

RAI YANGU: Wapeni onyo Mh. Shibuda na Madiwani wa Arusha, na kisha fungeni ukurasa na mugange yajayo. Watanzania tuna imani kubwa sana na CDM, lakini mkiamua vinginevyo kwa hawa MAKADA wenzenu..........take it from me.........graph ya CDM itaporomoka sharply it may never regain! Siyo kwamba watanzania hawaoni na wala hawajui linaendelea.

Mkikurupuka na mkawatimua hawa MAKADA wenu WAZURI, UMMA utasympathyze na wao na CDM itaathirika vibaya sana!
 
Mbowe akiona anakaribia kuporwa ukwe wake na mtu yeyote kichwa ndani ya cdm tu anasema eti kwa kunususru chama anammuondoa huyo mtu, hapa nikubali tu kauli ya mtikila......
Zitto na shibuda na wengine wanaohoji wajiandae kufukuzwa kama sio kingine kuwakuta
 
CDM, ni kikundi cha watu kipo kimaslahi zaidi wala akina dhamira ya dhati kuwakomboa Wananchi!
Kama akina Mbowe wangesikia wananchi wanasema hivyo dhidi ya Shibuda, ndipo wangepata ujasiri wa kusema wa kumfukuza Shibuda, CDM wanataka kila mbunge awe mateka wa chama, atii amri hata zile za zisizo na tija na faida kwa wapiga kura, kuna udikteta mkubwa ndani ya CDM

Angalao umegundua kuwa CDM ni kikundi cha watu! CCM ni kikundi KUNDI la watu lililo na dhamira ya kuiangamiza nchi iitwayo Tanzania kwa masilahi yao na matumbo yao!
 
Shibuda usikubali kuwa mateka wa Mbowe na Dr Slaa, wanakunyanyasa sana sababu za Usukuma wako! Nakushauri nenda kawashitaki CDM kwa baraza la wazee wa Kisukuma wa kanda ya ziwa, kama ulivyomshitaki Wenje, wakagundua kuwa Wenje ni Mkenya walifanya makosa kumpa ubunge, wanasubiri kipindi chake kipite wamchague mwana Mwanza mwenzao, Mchagga mwenzao Selasini, alisifia serikali ya kikwete kuwa imekuza elimu kutokana na kujenga shule nyingi za kata, hawakusema kitu chochote
 
Itakuwa kosa kubwa sana kwa CHADEMA kuendelea kumlea huyu pandikizi ndani ya chama. Ni bora tu wamtolee uvivu na kumtimua mara moja na hili liwe ni fundisho kubwa kwa CHADEMA dhidi ya mapandikizi toka CCM ambao dhamira yao kubwa ni kuivuruga CHADEMA
 
Angalao umegundua kuwa CDM ni kikundi cha watu! CCM ni kikundi KUNDI la watu lililo na dhamira ya kuiangamiza nchi iitwayo Tanzania kwa masilahi yao na matumbo yao!
ID yako unaitwa Mangi wewe unadhani kina Mangi wapo chama gani!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom