Shibuda: CHADEMA nifukuzeni muone!

professor safari huwa simuamini sana sijui kwa nini...au kwa vile namuona tbc mara kwa mara???
Wewe sema ukweli wa nafsi yako.........Haumuamini Prof. Safari kwan sababu ana jina la Kiislamu. Hata kwenye orodha yako ya watu wa kuaminiwa slaa, mbowe, mnyika, mdee, lissu wote ni WAKORINTHO!
 
CDM wamshachemsha na wanachotakwia kufanya sio kumfukuza. bali ni kuomndoa kwenye ngazi za kiuongozi na kiutendaji ndani ya chama. Abaki kuwa mwanachama wa kawaida na mbunge. Wamuache ajifukuze mwenyewe
Wewe lazima utakuwa umetumwa!!Jaribu kufikiria kidogo kabla yakupost thread:Huyu kinamchomsumbua ni Tamaa na uroho ndomana anapinga posho kuondolewa sasa ukimuachia ubunge aendelee kulamba hayo mavumba utakuwa umefanya nini?na wewe kwa akili yako unafikiri atajiondoa wakati anazitaka hizo chapaa.
 
Msiumize kichwa wana CHADEMA, SHIBUDA hana lolote, yaani na nyie mnaamini anaweza kuwa juu ya maamuzi ya kamati kuu? if the guy is to be fired he will be fired na hatafanya lolote. na hata akitishia kukimbiia mahakamani hakutamsaidia kitu badala yake atakutana na zomea zomea popote atakapopita na Peoples power!!! - maisha yake yatakuwa magumu sana akijaribu kikipeleka CHADEMA mahakamani.

He was born to be a looser, just ignore these kind of hopeless people. Cha msingi CDM watakuwa wamejifunza kwamba chama kinapo GROW milango inafunguka na watu kama kina SHIBUDA wanaingia ili kuleta negative challenges kama hizi ambazo at the end of day - CDM watakuwa wamejifunza kitu muhimu sana kwa ukomavu wa chama.


 
Chadema wanamuogopa Shibuda kwa kuwa wanahofia nyadhifa zao katika chama zilizokaa kikabila na kikanda. Shibuda ni zaidi yao wote kwa siasa, hawamuwezi.
Mambo vp shosti. Mzima weye? Ushakula urojo?
 
Na baada ya muda si mrefu, magwanda wataona kuwa Safari hawafai na pia wataona kuwa Lissu hawafai, wee ngoja tu. hapo ndipo watu watajua kuwa hiki ni chama cha kifamilia kwa maslahi ya wachache wanaokubaliana na mwenendo wa familia fulani fulani tu.
Lazima kuna mtu ulimpa akili akushikie!
 
Huu ni uzushi, Shibuda hajasema hayo uliyobandika hapo. Hata hiyo source uloweka hapo haina kitu.
Bill:nakuheshimu sana,nitafute nikupe copy ya hilo gazeti,kuna ubishi mwingine auna maana kabisa,nakama shibuda ajasema hayo maneno basi mhariri wa hilo gazeti atakuwa na ajenda zake za siri,sababu hiyo habari ipo kwenye front page,sasa kinachokufanya utoke povu jingi ni nini?
 
Wewe sema ukweli wa nafsi yako.........Haumuamini Prof. Safari kwan sababu ana jina la Kiislamu. Hata kwenye orodha yako ya watu wa kuaminiwa slaa, mbowe, mnyika, mdee, lissu wote ni WAKORINTHO!

Kumbe Safari ni jina la Kiislamu? Nilikua sijui. By the way kuna majina ya Kiislamu au Kiarabu? Maana kuna Waarabu Wakristo lakini wana hayo hayo majina unayo ita ya "Kiislamu".
 
Mimi sikuwa na uhakika sana na ujio wake CHADEMA, mi tangu mwanzo niliona kuwa alikuwa "CCM ndani ya CHADEMA" nafikiri CHADEMA walitakiwa kuliangalia hili kwa makini................ na hasa in future maana sio wote wana moyo wa kuwatetea wananchi ila MATUMBO yao
 
Msiumize kichwa wana CHADEMA, SHIBUDA hana lolote, yaani na nyie mnaamini anaweza kuwa juu ya maamuzi ya kamati kuu? if the guy is to be fired he will be fired na hatafanya lolote. na hata akitishia kukimbiia mahakamani hakutamsaidia kitu badala yake atakutana na zomea zomea popote atakapopita na Peoples power!!! - maisha yake yatakuwa magumu sana akijaribu kikipeleka CHADEMA mahakamani.

He was born to be a looser, just ignore these kind of hopeless people. Cha msingi CDM watakuwa wamejifunza kwamba chama kinapo GROW milango inafunguka na watu kama kina SHIBUDA wanaingia ili kuleta negative challenges kama hizi ambazo at the end of day - CDM watakuwa wamejifunza kitu muhimu sana kwa ukomavu wa chama.



Kichama Shibuda hana nguvu, anaweza kuwekewa mkakati, akafukuzwa uanachama na kupoteza hata ubunge.

Kinachwapa watu maswali hapa ni, Shibuda anathubutu vipi kuwa na kiburi hiki? Je, kashajichukulia siri nzito za CHADEMA kiasi cha kuweza kubwabwaja bila kuogopa huku akijua kwamba inawawia vigumu CHADEMA kumfukuza kwa kuwa wanajua ana siri za uongozi wa juu wa chama?
 
ilikuwa ni sawa chadema kumkaribisha shibuda
wangejifunzia wapi??very good lesson

mkuu hakuna kujifunza kwenye haki na maisha ya watu.. CHADEMA kumkaribisha Shibuda ni janga...Intention ya Chadema katka uchaguzi kushika dola, watwale na kama wangefanikwa basi hata shibuda ungesikia ni waziri wa wizara furani may be.... kukosea na kijigamba ndio kijifunza ni fikra za mtu masikini wa uwelevu.... kama kiuosea ni kijifunza basi HATA TANESCO tusiwalaumu nawao tuseme wanajifunza........ hili ni anguko na wakishindwa kufanya maamuzi sahihi kwa wakati basi hata uwezo wa CHADEMA kama chama kushika dola ni mdogo kwani hawataweza kufanya maamuzi makubwa kwa maslahi ya nchi....... taratibu zifuatwe kwa haraka san kumadabisha huyu mamluki
 
mara nyingi nasema siri za chama wanatakiwa kuzijua watu wawili hadi waTANO ndani ya CDM,slaa,mbowe,mdee,mnyika na tundu lisu basi,waliobaki wote hawaaminiki sana..
Mbona kuna makamu wenyeviti na manaibu katibu hujawataja, nao hawatakiwi kujua siri cha chama kweli?
 
Chadema wanamuogopa Shibuda kwa kuwa wanahofia nyadhifa zao katika chama zilizokaa kikabila na kikanda. Shibuda ni zaidi yao wote kwa siasa, hawamuwezi.
hawamuwezi kumfanya nini! jivike akili japo kwa muda.
 
Wewe sema ukweli wa nafsi yako.........Haumuamini Prof. Safari kwan sababu ana jina la Kiislamu. Hata kwenye orodha yako ya watu wa kuaminiwa slaa, mbowe, mnyika, mdee, lissu wote ni WAKORINTHO!
wakorintho ndio nini tena?
 
Kwa hiyo mnataka watu wanomwitikia mbowe ndiooo, ndiooo.

Hapana,

Ndioo, ndioo, ndioo ni mbiu ya CCM kumchagua Ally Mwinyi.

Tunataka watu wanaoweza kuleta migongano ya mawazo kwa nidhamu, ndani ya chama. Na wenye uungwana wa angalau kutokitukana chama kilichowapa ubunge hadharani kama watu wasio fadhila.

I mean ondoa siasa, Shibuda kakosa utu wa chini kabisa, na anaendekeza ubinafsi zaidi kuliko maslahi ya chama wala wananchi.
 
.

Kile kile anachowafunza Chadema. waulize baraza kuu la Chadema watakwambia Nyanda jilili ni nini?

Ur still cryptic son.

Sihitaji baraza la CHADEMA kunieleza Nyanda Jilili ni nini, labda mimi naweza kufunza watu katika hilo baraza kuhusu siyo tu habari za Nyanda Jilili, bali pia hata habari za "Basumba Batale" na "Bafumo".

Tena unaleta mambo ya ukabila unnecessarily, which is a sign of being politically bankrupt. Wasukuma ni watu wenye akili na utulivu kushinda hizi petty tribalism antics and innuendos. Hata Shibuda kwanza kabisa alivyotaka urais alifikiri Wasukuma wataanguka kwa karata ya ukabila akawakuta hawaja respond, ndiyo maana aka withdraw bid yake. Kama Wasukuma wasingekuwa hivyo kanda ya ziwa ingekuwa nchi nyingine ile. Wangeweza kuwa na claim to statehood iliyo valid kuliko Zanzibar ambayo kwa population, area na resources haiifikii hata wilaya ya Kahama tu, but that is another ballgame.

Nimekuuliza swali rahisi tu, Shibuda ni mwanaume wa shoka kwa msingi gani? Umalaya wa kisiasa?

Mwanaume wa shoka anajua principle moja ya maisha, kwamba ukiwa ndani ya chama, hata kama hupendezwi na mambo ya chama, unayakemea mambo hayo ndani ya chama, sio kubwabwaja ovyo.

La sivyo, ukitaka kukishambulia chama publicly kwanza unajivua obligation ya "collective responsibility" kwa kujiuzulu nyadhifa zote za chama na kurudisha kadi kwa kujivua uanachama, then unaweza kubwabwaja unavyotaka kutoka nje ya chama.

Mwanaume wa shoka, akishaoa mke, hawezi kumsema mkewe vibaya pembeni. Mambo ya ndoa, pamoja na matatizo ya ndoa, yanamalizwa kwenye ndoa.

Shibuda ni kama mwanamme aliyeoa ( or more like mwanamke aliyeolewa) halafu anatangaza matatizo ya ndoa hadharani kabla ya kuyatafutia ufumbuzi ndani ya ndoa.

Mtu kama huyo unaweza kumwita mwanaume wa shoka? Habari za udhaifu wa mkeo ndani ya nyumba unaweza kuja kutuletea hapa JF kwa kumsuta kweli maalim ?
 
Back
Top Bottom