Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,899
Nipo na wewe Mkuu 100%! Yaani asipofukuzwa atajiona wa maana sana. Huyu alishaonyesha toka mwanzo yupo the magambaz
Kila mtu yuko na uhuru wa kutoa mawazo anavyotaka, lakini uhuru una mipaka yake. Hata wanyama pori huongozwa na sheria za za maumbile (silika) vinginevyo kila kitu kingekuwa kiholea tu.
Chama maana yeke ni watu waliokubaliana kuwa na misingi na itikati zinazofanana, na wanajiweka taratibu na kanuni za kuwaongoza. Lakini mwanachama anapokiuka taratibu na sheria za chama maana yake amesaliti chama na anatakiwa atengwe au kuachishwa.
Mbaya zaidi mwanachama anapojivunia kuvuruga chama akiwa bado mwanachama ni donda ndungu. Kazi yo yote ufanyayo na hata maisha binafsi kuna mtu unatakiwa uwe na unyenyekevu na kukubaliana na yale hata usiyoyapenda, vinginevyo utakorofishana na watu po pote unapolwenda.