Sheria ya salamu ya "Shikamoo"

Sheria ya salamu ya "Shikamoo"

Paku hama hapo!!!! utakuta nyumba nyingine ndio balaa kabisa akina mama walio na umri mchanganyiko, wanapiga soga mlangoni mwako kelele vicheko na vijembe!! kwenda chooni hapaendeki ndio karibu na walipoweka kijiwe!!! ukisalimia ndio unabadilika kuwa topic ya mjadala ukiuchuna ndio balaa!!!! uswahili ni kazi
Yani hizi nyumba za kupanga tunapata tabu sana kwa kweli
 
Inategemeana na mda huo ni mda gani na unaelekea wapi? Wengine mishe mishe zetu zina depend sana time....ukichelewa sekunde tu unalala njaaa
Yap, Upo sahihi.

Jaribu kukwepesha macho yasikutane pengine inaweza kusaidia. Kama mkikutana na akikukumbusha hilo suala mwambie; " samahani mzee wangu ujana unasumbua, kuna mambo kidogo yalivuruga kichwa"
 
Yap, Upo sahihi.

Jaribu kukwepesha macho yasikutane pengine inaweza kusaidia. Kama mkikutana na akikukumbusha hilo suala mwambie; " samahani mzee wangu ujana unasumbua, kuna mambo kidogo yalivuruga kichwa"
sawa bhana
 
Achana nae huyooo, atakuwa mchawi🙊🙊🙊 usimsalimie tena lkn jiandae kuhama mkataba ukikaribia kuishaaa
 
Kumbe tupo wengi, niliazimia kutotumia hii salaam na nilianzia nyumbani kwa wazee nashukuru walinielewa
Umeamkaje
Umeshindaje
Habari etc
(Kutegemeana na mahusiano na rika)
Hizo ndo salamu hata kwa makabila yetu, bila kujali umri. Hii shikamoo binafsi sipendi kabisa kutumia. Nakumbuka mwalimu wangu wa Histori hakutaka kabisa kuisikia, akiwa na maana ilitokana na neno la Kiarabu ikiwa na tafsiri 'niko chini ya miguu yako' ilitumika kwa watwana kuomba wasamehewe kwa kushika miguu ya Bwanyenye ili wasamehewe. Mwenye kujua zaidi ataweka mambo sawa..
 
Ndugu yangu hivyo vi mia mbili mbili tafuta uwanja ujenge!
 
Huku tunavyoishi ni nadra kukuta mtu akusalimie bila kukuanbia assalam alayqum, nikajikuta mazoea yamejengeka kiasi sion maana ya shikamoo, lakin wengine usipowapa shikamoo ukawapa assalam alayqum wanaona huwaheshim na kuwadharau

Binafsi siwez kusalimia kwa mbali labda nipunge mkono mtu yule ajue nimepa ishara tu ya salam
Tatizo ni kwamba, mtu kutoa shikamoo haina maana katoa kwasababu anaheshima, wengine nidhamu ya woga ama mazoea tu.
 
Naamini mko poa humu ndani.

Leo mida ya asubuh wakati naelekea kwnye miangaiko yangu ya hapa na pale bhana, nikapita mita ya karibu na nyumba anayoishi Mzee wetu mwenye nyumba.

Sasa kikukweli alikua mbali sana kiasa cha distance ya kama mita 25 au thelathini tokea nipokua napita Mimi.

Nikaona hapa kama ni kutoa salam ili aiskie bs nipaze sauti sana ndo tuskilizane...basi nikaona sio kesi nikapita kikauzu

Sasa kumbe yeye kanichora tu.

Nimerudi sa hv geto nimemkuta nje ya nyumba yetu aliotupangisha anafanya Fanya usafi.........nikamsalimia...akanikaushia....nikarudia tena kumsalimia aiseee..

Nikashangaa Mzee kawaka "unanisalimia nin wakat asubuhi umenipita bila salam,, siku hz umekua na dharau sana, hvo vimiambili mia mbili vinakuchanganya"

Yani kwa kifupi aliongea kinoma....nikaona niingie zangu ndani tu, ile nimeshangaa sana,

Sasa sijui nyie watu wa humu ndani katika swala LA kutoa shikamoo mnakua mmejiwekea utaratibu gani.
Mana mim mtu akiwa mbali sana siwezaji kupaza sauti kumsalimia kama natangaza salam bhana.



Sent using Jamii Forums mobile app
Ulitakiwa kumsalimia kwa kusema " Mkuu kwema", au "Kiongozi kwema" hawa wadudu huwa wanafurahi kuitwa hivyo
 
Achana nae huyooo, atakuwa mchawi usimsalimie tena lkn jiandae kuhama mkataba ukikaribia kuishaaa
Hahahaaa hamna mkuu haka kanyumba ninako kaa kazuri bhana siami....ntakomaa nae tu
 
Hizo ndo salamu hata kwa makabila yetu, bila kujali umri. Hii shikamoo binafsi sipendi kabisa kutumia. Nakumbuka mwalimu wangu wa Histori hakutaka kabisa kuisikia, akiwa na maana ilitokana na neno la Kiarabu ikiwa na tafsiri 'niko chini ya miguu yako' ilitumika kwa watwana kuomba wasamehewe kwa kushika miguu ya Bwanyenye ili wasamehewe. Mwenye kujua zaidi ataweka mambo sawa..
Inasikitisha sana
 
Ulitakiwa kumsalimia kwa kusema " Mkuu kwema", au "Kiongozi kwema" hawa wadudu huwa wanafurahi kuitwa hivyo
Ni age sanaa hyu Mzee ana approach 70 aisee.....mbona sasa hyo mkuu kwema imekaa kishkaji kidgo
 
Hata Mimi ningekuwa upande Wa Mzee na notisi ningekutwanga.( nakuongezea kodi)

Baba mwenyenyumba ni sawa na mzazi wako, ulipaswa umpe umuhimu Wa salamu ya asubuhi sawa unavyompa mzazi wako.

Kwangu mm neno SHEMEJI silipendi kabisa au MTU kumuita mtoto Mdogo eti " mchumbake" sipendi kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom