Pole sana mkuu.
Ifike mahali kengele la adha ya kuishi kwenye nyumba za waswahili lilie ubongoni mwako, kama haukuwa na wazo la kuandaa mustakabali wako, basi hiyo ni fursa, lianzishe sasa, maana haujachelewa bado.
Umiliki wa kitu chochote huanza na wazo kwanza, kisha Mungu hufungua neema zake na hakuna kitu kilichowezwa na mwenziyo, wewe kukakushinda!
Kuna dharau ama manyanyaso mengine unaweza kuyapata mtu, yakawa ndiyo mwanzo wa mabadiliko ya mfumo mzima wa maisha yako.
Hiyo umeipata ni kiashiria sahihi cha tabia ya uswahilini.
Amekuwa ni baba yako mzazi huyo anayestahili kuamkiwa hata kwa kufunguzwa ili kumjulia hali?
Unaishi kwake kwa mkataba wa kulipana kodi, si vinginevyo na shikamoo yako haikupatii taafifu ya kodi.
Huyo anataka kukupandilia kisogoni umuabudu, kwa cheo cha baba mwenyenyumba ili aendelee kukunyanyasa!
Wewe fanya mambo yako kama kawaida, usimjali na wala asikukwaze ili mradi unamlipa kodi yake.
Fuata utaratibu uliojiwekea, namna ya kuamkia mtu kwa distance inayofaa kuwasiliana.
Usimuwekee kinyongo wala asikubadilishie mfumo wa uhuru wako na epuka naye mazoea.
Hizo 'shikamoo' kila mtu anaitafsiri kichwani mwake anavyotaka yeye.
Nikupe mfano, siku moja nikiwa mtumishi wa serikali kwa hadhi ya wilaya, alifika ofisini kwangu mbabu, anayenizidi kiumri kama miaka15hivi, akanitandika shikamoo!
Sikuvumilia nikamuuliza kwanini aninyenyekee kwa salamu hiyo, wakati aliyestahili kuamkiwa ni yeye anayenizidi umri?
Yule mzee wala hakumumunya maneno, akanieleza kuwa shikamoo aliyonipiga nayo usoni si ya umri bali ni ya ofisi na madaraka niliyonayo.
Akaongeza kuwa, vinginevyo nisingekuwa na cheo pamoja na ofisi, kamwe nisingelipata hicho kionjo toka kinywani mwake!
Nilishangaa sana na kugundua kuwa salaam ya shikamoo haina tafsiri moja yenye kueleweka kama watu wengi tunavyoichukulia!
Sent using
Jamii Forums mobile app